‘Mama alipoulizwa nesi aliyemuona kwenye ndoto ni nani kwanza akaonyesha kama dalili ya kutaka kuinuka na madocta wakamsihi, na kumshauri kuwa aendelee kulala,….
‘Wewe ongea tu huna haja ya kuinuka,..au umechoka kuongea kama umechoka tunaweza kukuacha upumzika halafu tutakuja kuongea baadaye, utumalizie hiyo ndoto
yako.....’akaamabiwa
‘Hapana sijachoka, hasira zilipanda, ….’akasema
‘Kwanini?’ akaulizwa
‘Kuhusu huyo nesi, mimi nilimuona kwa macho yangu, maana alijifunua, sijui
alijisikiaje mapaka akajifunua,...au ndio mungu alipanga nimuone ili baadaye uwe ni ushahidi,…kwahiyo
sio kwamba namsingizia..mimi nilimuona huyo nesi kwa sura ….na huyo docta
mwingine sijui yupo wapi…’akasema
‘Lakini hayo unasema umeyaona kwenye ndoto au sio?’ akaulizwa
‘Ni ndoto ndio…lakini ni ndoto inayonionyesha yaliyotokea, na
kutokana na ndoto hiyo ndio nikakumbuka yaliyotokea… na ndivyo ilivyokuwa,….’akasema
huyo mama
‘Ehe hebu endelea unasema kulipatikana kiumbe cha ajabu ambaye
unahisi alikuwa ni mtoto wako, na hicho kiumbe cha ajabu akapewa jitu mwanamke
kutokana na ndoto yako halafu ikawaje….?’ Akaulizwa
‘Ndoto …naona kama hamuaniamini…’akasema
‘Mama unajua sisi tunataka kukusaidia…na mwenzangu hapa ni
mtaalamu wa mambo hayo anajua ni nini unachokiongea,….maelezo yako ndiyo
yatamsaidia kubainisha ukweli,..mimi ni mtaalamu pia, lakini siwezi kuamua
tu..ni lazima kuwepo na mtu mwingine ili niweze kufikia maamuzi yaliyo sahihi…’akasema
‘Nimekuelewa….’akasema
‘Ehe…tuendelee au umechoka…?’ akaulizwa
‘Baadaye wale watu-mijitu wakawa `wameshiba’....huo ni mtizamo
wangu kuwa kwa vile walikuwa wanakula nyama zangu, sasa wametosheka, na kwahiyo
wameshashiba, na mwili wangu utakuwa umebakia gofu tu…’akaendelea kusimulia
huyo mama
‘Uliona wakila hizo nyama?’ akaulizwa na hapo akabakia kimia kwa
muda, halafu akasema.
‘Kiukweli sikumbuki kuona wakila hizo nyama,…ni hisia tu kuwa
walifanya hivyo…maana kutokana na maumbo yao huwezi kuwaona mwili wote, ila
yule aliyekuwa kainama ndio niliweza kumuona kwa uzuri, japokuwa
alikuwakajifunika uso…nikawa najiuliza kwanini wajifunike uso kama sio watu
wenye nia mbaya kwangu…’akasema
‘Waliposhiba kwa uoni wako, kwenye hiyo ndoto, hao watu-mijitu
walifanya nini, waliondoka?’ akaulizwa
Nilimuomba mungu wasiniache pale nikabebwa na mwewe au midege
yenye uchu, au fisi maana kwa hisia zangu tulikuwa porini, pori nene lenye miti
mikubwa, na mwanga mkali, na baridi kali haliwezi kukosa wanyama wakali…nikawa
najaribu kulia , lakini machozi yakawa hayatoki, nikajua kwa vile damu
imeshakauka basi hata machozi yameshakauka pia. Nimeshakufa…
‘Umeshakufa,..kwahiyo kwenye hiyo ndoto ulijua kuwa umeshakufa,….?’
akaulizwa
`Niliona ajabu pale walipochukua kitu kama kamba…zilikuwa nene ,
na zinametameta na kama vile kamba hizo zina maji yanapita ndani yake,
wakanifunga mkononi…’akasema na kutokujali hilo swali aliloulizwa, akaendelea
kuongea.
`Niliona hiyo kamba ikishikanishwa na kitu huko ..nahis ilikuwa ni
mkononi au mwilini, hapo sikuona, ila nikahisi hali kwenye mishipa ya damu,
kwahiyo nikajau ni njia ya kuninyonya damu yangu…nikawaza hivyo.. na ikawa kama
kumbukumbu zimepotea kwa muda, ni kama nimelala siwezi kuwaza tena…’akasema
`Baadaye kabisa, nikahisi nabebwa hewani hewani au kitu kama gari
linanibeba…wananipeleka wapi hawa watu-mijitu, au ndio wanaenda kunitupa, kwani
nimebakia mifupa, au gofu la mtu? Nilihisi kama naelelea hivi,...
Baadaye nikajua kuwa
nimehamishwa, nimetolewa pale nilipokuwepo na kupelekwa pori jingine, na zile
kamba zikawa zimefungwa kwenye michuma mikubwa iliyotokea huko juu, nisipopaona
vyema. Nikawa najiuliza nipo wapie sehemuyanye michuma mikubwa namna hiyo…ubaridi,
utulivu ulikuwa vile vile…nipo wapi hapa jamani, nikajaribu kufunua mdomo
lakini, ilikuwa kama vile sina mdomo …!
Baadaye wakaondoka , …nakahisi nipo peke yangu, nikajiuliza hapo
nilipo ni porini au ni wapi, na mbona kamba niliyofungiwa imefungwa kwenye
chuma, ni pori gani hili lina vyuma. Nikajaribu kugeuza macho, yakawa
hayageuziki, ina maana hata macho sina, ikawa ni kuhisi tu!
Mara nikaona mtu-jitu akinikaribia,…aaah, ni yule yule mwanamke
aliyemchukua mtoto-jitu wangu kutoka tumboni mwangu, alikuwa bado kavaa kitu
usoni... kuzuia sura yake isionekane..nilihisi hivyo, nilitaka kumwambia hata
ukijificha uso wako mimi nimeshakuona…lakini sikuweza kutamka neno.
Baadaye kwa mshangao…akakiondoa kile kitambaa usoni, …..mungu
wangu, nilitamani niinuke nikimbie, macho ya huyu mtu-jitu yalikuwa makubwa
kama mpira wa miguu,meno yalikuwa makubwa kama majembe ya trekta kubwa sana, na
aliptabasamu kuyaonyesha hayo meno yalitisha sana..meupee, makubwa..!
‘Woga, wasiwasi vikanizidi…nilihisi kuwa huyu sasa katumwa kuja
kunimalizia, huenda yeye alikwenda kumla mtoto wangu…akili iliwaza hivyo,
kuwa huyo waliyemchukua `ni mtoto wangu’ maana walimtoa tumboni mwangu…japokuwa
alikuwa mkubwa kama wao...lakini kwa namna fulani nikajua ni mtoto
wangu..kwahiyo ni lazima nifanye kitu…ni lazima nijitetee hata kama kuna mabaki
ya mtoto wangu niyapate…lakini kwa vipi?
‘Kila mara huyo mwanamke-jitu, alikuwa akija karibu yangu na
nilihisi kama alikuwa akiniongelesha jambo..lakini, sikuelewa anaongea, nini,
…lakini nilisikia maneno yakipaa kama mwangwi...nahisi kuna neno kama
mtoto....halafu baadaye yule jitu
mwanamke akaondoka . Nilitamani nipige kelele kuwa anirudishie angalau mabaki
ya mtoto wangu, lakini sikuweza.
‘Baadaye huyo mwanamke-jitu akarudi akiwa na kitu, nikataka kutoa
kauli , kumuulizia kuwa kampelekea wapi mtoto wangu, lakini sikuweza.
‘Alikuja hadi pale nilipolala, sijui ni kwenye nini,…akashika ile
kamba nene iliyotoka nahis ni mkononi mwangu na kufanya kitu nisichokielewa,
akawa amashika kitu kama gunia , yeye kwake kwasababu ni jitu kashika kama
kapaketi ….sijui hata kuelezea, kwani
akili hukumbuka itakavyo…lakini kile kitu, ambacho mimi nilikiona kama gunia la
plastiki, lilikuwa limejaa maji ndani yake, akalitundika kwenye chuma na …sijui
alikuwa analitoboa ili maji yanimwagikiea u vipi, lakini maji niliyoyaona mle
ndani hayakumwagika!
Yule mtu-jitu mwanamke akasogeza kiti na kukaa karibu na nilipolala
mimi, akawa ameshika karatasi kubwa kama shuka linalojaa eneo lote nililoweza
kuliona, kama vile limejaa chumba kizima,kulikuwa na maandishi makubwa ajabu
nafikiri alikuwa akisoma kitu! Nikajiuliza. Huenda anasoma, kwa vile ni mijitu
mikubwa lazima hata vitabu vyao vitakuwa vikubwa. Muda ukawa unapita tu,
siwaoni wale wengine na huyu haondoki hapo alipokuwa kakaa pembeni yangu!
‘Nilihisi kama kusubiri kukubwa tu,..sasa subira ikawa inanishinda,
niliomba mungu wangu wasinimalizie sehemu iliyobakia, angalau yabakie mabaki
ili ndugu zangu waweze kunizika. Na pia yaweze kupatikana mabaki ya mtoto wangu…Nikaomba
sana, na kila mara nikitulia na kumwangalia yule mtu-jitu mwanamke , namuona
habandui macho yake kunitizama mimi, na macho yake ni makubwa yanatisha,
naogopa hata kumuangalia.
‘Kuna muda alikuja yule mtu jitu amabye alikuwa mgawa nyama yangu…,
nilijua ni yule aliyekuwa akinikata nyama, yule aliyetoa mtoto wa ajabu tumboni
mwangu, alikuja akawa anaongea na huyo mwanamke....alipofika alijifunua uso
nikamuona vyema uso wake ...baaaye alikuja kunikagua, maumbile yake ni yale
yale...macho makubwa....meno makubwa, yaani kila kitu chake ni kikubwa cha
kutisha...alifanya kama ananikagua akaleta kidole chake kikubwa na kufanya kitu
kwenye jicho langu..baadaye akaondoka na kumuacha huyo mwanamke-jitu...
‘Akili ikiwa imechoka kufikiri na kitu kama usingizi kikawa kinaninyemelea
na hatimaye nikahisi kulala maana akili ilikuwa kama imeingiwa na giza,sikuweza
kufikiri tena.
‘Baaaye ile hali ya kichwa kutokufikiri tena kama mtu umelala
ikaisha na, akili ile ya kuwaza ikanirejea tenaa...ni kama kulala na kuamuka,
lakini kwa hisia tu...
‘Kwa mbali nilimuoana yule mtu-jitu –mwanamke akishika ile kamba
nene na kufanya kitu fulani, halafu akainuka na kunitizama machoni, alileta
kidole chake kwenye jicho langu kama alivyofanya yule mwanamume-jitu mwanzoni,…sijui
walikuwa wakifanya nini kwenye jicho langu..nahisi walikuwa wakilifunua. Halafu
nikamuona akiondoka.
‘Anakwenda wapi tena…au ndio anakwenda kuwaita wenzake waje
kunimalizia…? ‘ nikawa nawaza hivyo…
‘Hapa, hapa, ndipo pakutorokea, hapa hapa, jitahidi mwanamke,
jitahidi utoroke, kabla hawajarudi tena….’ Nikahisi sauti ikitoka sijui wapi,
sijui ni akilini au nihisia zinaniamurisha hivyo, ila kuna sauti ilikuwa
ikiniamrisha hivyo.
‘Sijui ilikuwaje, nilihisi hali ya kupata nguvu…,nikahisi nguvu za
ajabu zikinijia, nikaweza kuinua mabaki ya mwili wangu na nikajitutumua na kuweza
kukaa, nilihis nimekaa sehemu ya juu, na mbaki ya mwili wangu umening’inia
chini,..nikaona kuna kitu kinanizuia, nikakumbuka ile kamba yenye maji ndani
yake,…nilitumia nguvu kutoa ule mnyororo au kamba niliyofungwa mwilini mwangu.
Ulikuwa kama huo mnyororo umezamishwa ndani ya mwili wangu, kwani
kila ulipokuwa ukitoka nilihisi mwili mzima ukihisi maumivu ya aina yake, na
nahisi ulikuwa umeanzia kwenye moyo….., lakini sikujali hatimaye
ukatoka…nikajitutumua na kujiondoa iel
sehemu niliyokuwa nimelala, na kukaa,sasa nikawa nahis nimekanyaga chini.
Nilijaribu kuinama kutizama mabaki ya mwili wangu yaliyobakia kwa
chini, lakini kichwa kilikuwa hakiwezi hata kuinama, mwili hauwezi hata
kujipnda, ni kama jitu limenyooka tu…nilikuwa kama roboti. Kichwa kinaangalia
mbele tu…!
Nikasema hivyo hivyo,
lazima nitoroke hapa kabla hawajaja kunimaliza…
Nikatoka pale nilipokuwa nikajikongoja na niliona sehemu kama
upenyo wenye mwanga, ni kama upenyo mkubwa kama mlango, lakini ni mkubwa sana…nikauendea
na kuona upande huo mwingine kuna mwanga mkali…
Nikauendea huo mwanga, nikijua kuwa huko ndio kwenye uzima,….nikawa
natembea, kuna muda nilihisi kitu, sijui ilikuwaje, nikainua kumbe ni mkono
angu, ooh, mkono ulikuwa mkubwa….
Ooooh...kumbe....hata mimi ni jitu..., ina maana hata mimi ni jitu
–mtu…nikacheka, kumbe naweza kupambana na hawa-watu –mijitu…nikawaantembea
kuelekea huko kwenye mwanga mkali, ulioenea kote…mwili wangu ulikuwa kama
umetoka kwenye barafu na kuingia kwenye moto…
‘Bora nikafie kwenye huu moto kuliko kuliwa na haya
majitu-watu…bora…bora…lakini nakumbuka walitoa kitu mwilini mwangu kama
mtoto-jitu…wamekiweka wapi! Nikawaza, nikaanza kusogea huku naangaza macho huku
na kule mithili ya roboti, linageuka mzima-mzima…’mtoto wangu yupo wapi....mtoto
wangu yupo wapi…’nikawa najiuliza
Baadaye nikawa najiona kama napaa, au natembea, lakini mwendo wa
kiroboti. Hadi nikafika mahala kuna nguo zimeanikwa, nguo ni kubwa ajabu…nani
anavaa nguo kama hizi, lazima ni hii mijitu watu. Nikaona kitu kama kitambaa,
kimeshonwa nikakisogelea na kuona kinaweza kunisaidia kuficha macho uso wangu
usiungue na mwanga huu mkali na kujikinga na joto. Nikakivaa, bahati nzuri,
kilifunika kichwa chote na kuweza kuacha sehemu ya macho tu…
‘Safii kabisa, haya majitu-watu hayataniona kamwe, nikaingiwa na
nguvu nakuanza kutembea kwenye eneo lilojaa mwanga mkali unao-unguza. Nilihisi
kuona watu-mijitu wakitemebea, lakini walikuwa hawaji ninapotembea mimi,
ilikuwa kama kila mtu-jitu ana njia yake. Nikaongeza mwendo, nikawa naondoka
nisipopajua….joto, ..joto…likawa kero, lakini nashukuru usoni pamefunikwa!
Unajua natembea kama roboti, lakini mwendo ni wa kupaa, kuna mtu
kama unavushwa waaaaah, kama unapaa vile na kujikuta sehemu nyingine kabisa….
Sasa sijui ilikuwaje kwani wakati natembea nihisi kitu kimenigonga
na kujikuta nikielea hewani juu kwa juu kama mtu anayepaa juu kwa juu..na
mwisho nilijikuta nikidondokea kwenye vitu kama matakataka, kunatoa harufu
mbaya…!
‘Umeua, umeua…’ nikasikia sauti kama mwangwi ikisema
hivyo…Nilijaribu kuinuka pale nilipodondokea, sikuweza.
‘Ina maana mimi wameshaniuaa…?’ Nikawa nawaza hivyo… kama
nimekufa, mtu anakufa mara ngapi!...maana ile hali niliyokuwa nayo awali
nilihis kama mfu sasa hapo imakuewaje
tena..
Mara kelele zikasikika toka
mbali zikisema `hajafa bado mzima, …’
‘Ina maana kumbe mimi
sijafa bado, haiwezekani, nikajitutumua na kujiinua na nilipogeuka kama roboti,
niliona watu….au niseme mijitu watu imejaa kwa mbele, lakini ilikuwa kama
kilima, mimi nipo chini wao wapo juu. Kila walipofunua meno ya ilikuwa
inatisha, nikaona hapo hakuna heri nikimbie tu..
Wale watu wakanisogelea wakanishika sijui ilikuwaje maana nilihisi
tupo kwenye kitu tunakwenda kama tunapaa baadaye nikajua hawa watu wana nia
mbaya na mimi, nikainua mkono sijui ilikuwaje, nilihisi napaa na kudondokea
sehemu nyingine…nikawa nimetulia sikuona watu tena…nikasikia sauti
‘Karuka kwenye gari…hayupo, twendeni zetu….’nikasikia hivyo
Mimi nikatulia kidogo na baadaye nilipoona kimia nikajau hapa
hakuna amani watakuja tena hao majitu watu…nikajitutumua kama roboto inayopaa,
nikaanza kukimbia kiroboti….
Hali hiyo iliendelea hivyo
kukimbia kutokea sehemu sehemu…na baadaye nikawa kama mtu amezama ndani ya giza
nene, sikuweza kufikiri tena! Nikawa kama nimelala , akili haikumbuki, haijui,
imetulia kimia..ni kama umelala bika kuota ndoto…
Nilipoamuka kwenye huko
kulala, nikasimama, na mbele yangu kukawa kunakuja mtu jitu, kajifunika kama
mimi, ni mwanamke..alioniona akawa kama ananiogopa,akanisemesha...mimi nikaona
nifunua uso wangu nimuone vyema vyema labda kule kujifunika ndio kunaleta hiyo
hali….mamamamama...
‘Yule mwanamke jitu alipoona uso wangu sijui ilikuwaje....aligeuka
kutaka kukimbia, hakujua nyuma yake kuna kitu kinakuja kinatoa mngurumo….akilini
hapo sikujua ni nini, hkitu hicho kikubwa kikamgonga huyo mama, na kudonoka
chini.....akawa katulia kimia, ...
Baadaye kulipokuwa kimia, mimi nikamsogelea huyo mama aliyegongwa
na kitu nisichokielewa kinachotoa mngurumo,...nilimuona katulia kimia...nikajaribu
kumchunguza mapigo yake ya moyo…alikuwa amekufa....oh jitu mwanamke alikuwa
amekufa nitaambiwa mimi ndio nimemuua …nikakumbuka kuwa hata mimi ni jitu
kwahiyo…hahaha, nikajikagua mkono…ulikuwa mkubwa, nikajua hata mimi huenda nipo
hivyo hivyo.
Sijui kwanini nilifanya hivyo....ila niliona nguo nilizovaa sio
stahiki yangu….ni nguo zitakazonionyesha kuwa mimi ni nani…, nikija kutafutwa
na mijitu ile iliyokuwa ikitaka kunila nyama yangu itanigundua haraka nikiwa na
nguo zile zile..nikajiwa na wazo, kama huyu jitu mwanamke kafa, hana haja n
nguo zake ....nikamvua nguo zake na mimi nikavua nguo zangu, nikavaa zile nguo
zake, nikamvalisha zile nguo zangu...
Sikusahau kujifunika usoni maana mwanga ulikuwa ni mkubwa kwangu
Nikaanza kutembea,...natembea kama roboti lakini nahisi kama ni
mwendo wa kupaa….nilitembea hadi nikachoka, mwili unauma,…nahisi tumbo linuma,
sina nguvu… nina kiu...natafuta maji siyapati hadi nikafika sehemu nikaona maji
nikayanywa, ....na nilipokunya hayo maji ilikuwa kama dawa ya kunipa usingizi
nikalala usingizi....akili ikawa haifikirii tena.
Ilikuwa kama vile nililala kwa muda, nilipoamuka, nikajikuta
nimetokea sehemu kama dunia nyingine
vile....
Yaani ile hali ya kuona vitu kwa ukubwa ikawa imeondoka kidogo
kidogo, mpaka ikafikia mahali sasa naona hali ya kawaida,..na hali hiyo
ilitokea kwenye hiyo dunia nyingine… lakini akili inakuwa gizani bado,..ni kama
umaingia dunia nyingine ya vitu vya kawaida.
Cha ajabu kwenye hiyo dunia nyingine hukumbuki huko ulipotoka
akili haijui imetoka wapi au inakwenda wapi…nikafikia sehemu sasa sikumbuki
yote ya nyuma...sikumbuki ilikuwaje mimi ni nani, yaani unakumbuka hicho
unachokiona mbele yako tu.... yaani sijui nielezeje….ohooo kichwa kinauma..’huyo
mama akasema
‘Unahitajika kupumzika mama umeongea vya kutosha, …chukua dawa hii
kunywa itakusaidia..’akasema docta na kumpa huyo mama dawa, na baadaye
wakaondoka, Nesi akawafuata nyuma, na ilionyesha wazi kuwa huyo mama ameshikwa
na usingizi
‘Nesi umesikia,…?’ aliyeuliza ni docta wakati wameshaondoka eneo
hilo wakiwa wanaingia ofisini kwa mkuu wa hiyo hospitali, nesi hakusema kitu
kwani alikuwa amezama kwenye mawazo.
‘Ina maana huyu mama ndiye yule mama……hapana mimi sijaamini ,
mbona alikufa, akazikwa, na nesi mkuu wa kipindi kile alithibitisha hayo…haiwezekani,
basi mimi sijaamini…huenda haya kayatunga tu akilini mwake,..ngoja tumsikie
akiendelea na uwongo wake, nitamtega,..’akasema kimawazo hakujua mabosi wake
wanamuuliza nini
‘Nesi nesi, kweli upo nasi…’ akaulizwa
‘Ndio bosi nahitaji kupumzika ila nahitajia pia kumsikia huyo mama
akiendelea kutoa uwongo wake..’akasema
‘Uwongo wake…hayo anayoongea ndiyo yaliyotokea huko nyuma, ila ni
hali ya ubongo inavyoweza kurudisha kumbukumbu, inakuwa kama njozi, lakini
ikionyesha yale yaliyotokea, huo sio uwongo…’akasema docta
‘Kwahiyo mnataka kusema nini, kuwa mimi ni muongo…’akasema
‘Hautajafikia huko,…muhimu kwa vile wapo watu wa usalama, na wao
watatusaidia kwa hilo, kamaikibidi, ila tunakuomba kama mwenzetu ushirikiane
nasi, kwani kuna kitu gani kibaya kilitokea unachoogopa kuwa ukisema ukweli
utapata matatizo…?’ akaulizwa
‘Ndio maana nawashangaa nyie, kwanini niwafiche, mimi
ninayemtambua aliyekuwa siku hiyo ni marehemu, huyu ni mwongo..mwizi na mwanga…si
mliona wenyewe pale nilipomkemea, mungu akamzalilisha….’akasema
‘Sikiliza nesi tutarudi tena kwa huyo mama, lakini hatutaki huyo
mama akuone ..najua akikuona moto utawaka..na itakuwa mwisho wa kupata habari
za hiyo ndoto yake, ni muhimu sana kuisikia yote..’akasema
‘Sawa lakini kwangu hakitabadilika kitu….’akasema
‘Na huyo mtoto uliyemchukua ulimpeleka wapi,…alikufa, au ilikuwaje…?’
akaulizwa na docta bingwa wa mambo ya kili
Nb….tuishie hapa kwa muda
WAZO LA LEO: Haki ya mtu ni lazima ifike kwa mlengwa,
hata kama huyo mlengwa hajui,..na wewe una dhamana na hiyo haki usitumie ujanja kuifisidi hiyo haki ya watu.
Sasa hivi kuna ujanja wa wale waliopewa dhamana ambao wana elimu, wanawadhulumu
wale wasiokuwa na ufahamu wa sheria, au haki hiyo, hii ni dhuluma, huu ni
ufisadi, huu ni wizi,….
Ni mimi:
emu-three
1 comment :
cialis for impotence [url=http://tadalafilfor.com]canadian pharmacy mall[/url] cialis for everyday usehow long does it take for levitra to work [url=http://fastshiplevitra.com]is it safe to buy levitra on line[/url] levitra high heart ratepropecia results months pictures [url=http://healthcarerxusa.com]Buy Finasteride[/url] subaction showcomments propecia smile olderpropecia and pregnancy [url=http://acheterpropeciafrance.com]propecia prix 2008[/url] can you take cialis and propeciadoes cialis 5mg daily work [url=http://cialisfor.com]Buy Cialis[/url] cialis ed dosage
Post a Comment