'Hivi ni kwanini madocta wa nesi wamamkazania nesi awasimulie kisa cha tukio ambalo nesi hakutaka kukihadithia kwa vile kina siri kubwa kwake...na kuna siri gani katika macho, mbona macho, macho...'
Tuendee na kisa hiki tuweze kuligundua hilo
***************
Nesi alipofika kwa yule mama, alimkuta kalala, na invyoonekana
hakuwa katika hali nzuri, akapewa dawa za maumivu na usingizi,..kwahiyo
akashindwa tena kuongea naye, hata docta alipokuja alishauri kuwa huyo mama
hatakiwi kusumbuliwa kwa hali aliyo nayo;
‘Huyu sasa kumbukumbu zinaanza kumrejea kwa kasi, kwahiyo anakuwa
na mambo mengi kwa wakati mmoja, muache apumzike, ….kwani ulikuwa na jambo
naye..?’ akauliza docta
‘Hapana ni katika majukumu yangu ya kazi tu….’akasema nesi na
docta akawa anamkagua kwa macho huyo nesi, na nesi alipoona docta anamuangalia
sana akageuka kutaka kuondoka na docta akasema;
‘Umependeza sana leo,….hata hivyo nilitaka tuongee, lakini kwa
bahati mbaya kuna dharura, kuna mgonjwa kaletwa huko anahitajia upasuaji wa
haraka…., nikimaliza hiyo kazi mapema nataka tukae tuongee, mimi na wewe
tu..’akasema
‘Kuhusu nini?’ akauliza nesi akionyesha wasiwasi na mshangao,
akilini akawa akijiuliza mengi, akahisi ni yale yale ya bosi wa zamani nini….
‘Sana sana ni kuhusu huyo mgonjwa, huyo mama, kidogo nimepata muda
wa kuongea naye kwa mapana..na muda huo alikuwa kidogo anaanza kukumbuka mambo..na
inavyoonekana hayo aliyonielezea yana ukweli….sitaki kuhakiki sana, lakini mimi
kama docta naweza kubaini kuwa kauli hiyo ni sahihi au imetokana na
kuchanganyikiwa tu…’akatulia akimuangalia nesi na nesi akawa kakunja uso
kuashiria kutokupendezewa na hicho anachoongea docta
‘Kitu ambacho kimenitia mashaka zaidi ni kuwa huyu mama bado
anazidi kukumbushia dai lake,..’akasema na nesi akamkatishia kwa kuulizia
‘Dai gani…?’ akauliza nesi kwa hasira, na docta akiwa anaongea kwa
sauti ya pole pole kama baba anayeongea na binti yake akasema;
‘Huyu mama tangu mwanzo amekuwa akidai kuwa mtoto wake
alichukuliwa hapa hospitalini, …na anasema ni kipindi cha nyuma, alifika hapa
hajitambui akafanyiwa upasuaji,..lakini mtoto wake alichukuliwa..’akasema
‘Na nani na ni muda gani maana ukumbuke kuwa muda fulani
nilikwenda chuoni kusoma, sasa isje ikawa ndio huo muda..’akasema nesi
‘Yawezekana mimi sikatai…lakini kwanini aseme ni wewe uliyemchukua
huyo mtoto..’akasema
‘Karudia kusema hivyo?’ akauliza nesi
‘Safari hii hakukutaja wewe moja kwa moja, safari hii kasema ni
nesi aliyekuwa akimuhudumia,..alipewa kazi ya kuwa karibu naye, ….’akasema
‘Bado haiwezekani ukasema ni mimi, ni kwa vile mwanzoni alisema
hivyo, ndio maana bado unashikilia kuwa ni mimi, ..docta nikuulize kwanini mimi
nimchukue mtoto wake?’ akauliza nesi
‘Sijui..labda kwa vile alichanganyikiwa mkaona hataweza kumlea huyo mtoto..siwezi kukisia
kwanini, ndio maana nilitaka tuongee, nijue hilo tukio ulilosema wewe
lilikuwaje,….’akasema
‘Docta..’nesi akataka kuingilia sasa akiwa kakasirika lakini
dakitari yule akaanza kuondoka akisema
‘Tutaongea tu usijali,…nina mambo ambayo yanaonyesha kuwa huenda
tukio hilo linamuhusu huyu mama, sasa sijui kwa vipi kama huyo mama alikufa
kwanini kuwe na sababu, na dalili za huyu mama kufanana na huyo mama mnyesema
alikufa..’akasema
‘Sababu na dalili zipi?’ akauliza nesi
‘Hebu kwanza nikuulize huyo mama marehemu alikuwaje,..macho yake…?’
akauliza na nesi aliposikia hivyo akashituka…akajikuta akiuliza
‘Macho yake..macho yake yana nini?’ akauliza
‘Na huyo mama alipokuja hapa alikuwaje usoni?’ akaulizwa
‘Mhh, hapo unanichanganya,..kwanza umesema macho, haalafu usoni
alikuwaje,…mimi nilikuwa nesi tu..na huyu mama alifika hapa akiwa hajitambui,
ina maana macho yalikuwa yamefumba, ningayaonaje..?’ akauliza
‘Na uso wake ulikuwaje?’ akaulizwa
‘Nakumbuka aliharibiwa na kitu kama ….kuchanwa chanwa na na kitu
kama miba, au seng’eng’e..’akasema
‘Yap…you’r right..’akasema huyo docta halafu hakufafanua zaidi
akasema;
‘Inabidi tuongee, …. ngoja ni muwahi huyo mgonjwa…inabidi tuongee
la sivyo, ohoo…’akawa keshaondoka na nesi akabakia peke yake na mgonjwa.
Nesi alijikuta mwili hauna nguvu akaogopa hata kugeuka kumuangalia
huyo mama, alihis akilini kama vile huyo mama ni mzuka,..au kibwengo,…au mfu
aliyefufuka, taratibu akageuza kicha kumuangalia huyo mama.
‘Haiwezekani sio yeye….hapana, docta ana lake jambo….’akasema na
wakati huo huo akageuka kile kitanda kingine, akawa anashangaa kuona yule
mgonjwa mwingine harudi kitandani kwake, kwani alikuwa na maongezi naye…akaona
akaulize kwa nesi aliyekuwepo hapo toka asubuhi…akaenda kwenye ofisi yao ndogo
wanapokaa wakisubiria kuwahudumia wagonjwa.
‘Nesi hivi yule mgonjwa wa kile kitanda kahamishwa maana..?’
akauliza
‘Yule mgonjwa kesharuhusiwa mbona…, hukuona kwenye hiyo ripoti
yangu,…?’ akauliza huyo nesi
‘Yaani hata sijaipitia hiyo ripoti yako, kwani nimefika hapa
nikiwa na hamasa ya kuongea na huyu mgonjwa, nilikutana naye hapo nje, nikajua
ataingia ndani ili nipate kuongea anye….oh kumbe kesharuhusiwa. Sasa na huyu
mama hapa mbona ananichanganya...’akasema
‘Kwa vipi nesi..?’ akauliza
‘We acha tu, …na huyu aliyeruhusiwa unajua wapi anaishi?’ akauliza
‘Yule mama anakaa kijiji cha mbali sana, ….na cha ajabu hakuna
ndugu yake aliyefika kumfuata angalau wakamsaidia,..hana haat pesa ya nauli…kosa
kalifanya mume wake, na ndugu wa mume wanasema kuwa yeye ndiye kumuunguza ndugu
yao, kwahiyo na wao wameenda mahakamani kudai kuwa huyu mwanamke ni mkosaji…..’akasema
‘Duuh, ndio imekuwa hayo..kumbe kuna mambo mazito nyuma ya pazia
kwa huyo mama,…..sasa kama ni hivyo,… badala ya kulisawazisha hilo jambo,
inawezekana kukazuka mgongano wa familia hizo mbili, wasiohusika wanaweza
wakasababisha ndoa hiyo kuvunjika..’akasema nesi.
‘Na ndivyo inavyoelekea huko, kitu nilichokiona hapa, mke
kajitahidi sana kuwa karibu na mume wake..yeye alishamsamehe mume wake kuwa
aliyafanya hayo kwa sababu ya ulevi…, maana hata hapa japokuwa wote ni wagonjwa
lakini mke alikuwa akienda kumsalimia mumewe kumujulia hali,..tatizo sasa ni
ndugu, maana hata mume alionekana kuongea na mkewe..’akasema.
‘Mhh maswala ya ndoa hayo…nayaogopa kweli kweli, wapendane wengine
wapambe ndio wawe washabiki,…ushabiki mbaya…na kiukweli kwa hali hiyo, hao
wanandoa wasipokuwa makini wataachana…kisa kujali matakwa ya wanafamilia’akasema
nesi
‘Ni bora tu waachane ,..kwangu mimi, ningeona bora iwe hivyo, maana
kama wamefikia kuunguzana na maji ya moto, si baadaye watachomana visu au
kutiliana sumu….mhh, lakini mke anaonekana kupenda sana….’akasema mwenzake.
‘Hebu nikuulize huyo mama uliwahi kumdadisi vyema wapi anapotoka,
kijini gani cha mbali..je ana ndugu yake
wanaofanana…?’ akauliza nesi
‘Nimekuwa nikiongea naye sana, nikitaka kujua ilikuwaje, siunajua
mimi ni mdadisi sana…ndio maana unaniita visinipite....mhh, ni kweli aliniambia
kuwa kuna ndugu yake kwa baba mwingine, wanafanana sana nay eye hata walifikia
kuonekana kama mapacha… lakini ndugu yake huyo ni marehemu kwa sasa...’akasema.
‘Eti nini ni marehemu eheee, ilikuwaje, alikufa kufaje?’ akauliza
nesi akionyesha hamasa hadi mwenzake akabaki kuduwaa na kushangaa, na baadaye
akasema;
‘Yaani we acha akikuhadithia maisha yao utamsikitikia, maana anasema
ni kama balaa kwake na familia yake hasa upande wa mama, …anasema ndugu yake
huyo kwanza waliivana sana kwa vile wanafana, jpokuwa hawakuzaliwa tumbo moja,
baadaye ikatokea wakampenda mume mmoja, basi ikawa ni vurugu,…wivu uhasama, na
urafiki na udugu ukavunjika, kisa ni kugombea mume, baadaye ndugu yake huyo akaolewa yeye na huyo
mume,…’akatulia
‘Ehe, lete mambo sister visinipite..’akasema nesi
‘Huyu yeye akakubali yaishe,..mara yule ndugu yake aliyeolewa huko
akaanza kuumwa, kama kuchanganyikiwa, ..wakasema huyu kamloga mwenzake kwa vile
kamkosa mume, wakati huo huyu alishaolewa na huyo mume mwingine ….huyo cha
pombe, …unaonaeeh..’akasema.
‘Acha lugha yako hiyo akikusikia je..’akasema nesi
‘Sasa hali ile ya kuchanganyikiwa ikawa haiponi, …akaanza hata
kutembea ovyo barabarani, kukimbia na hata kupotea, na ndio mara ya mwisho
wakamuokota akiwa amekufa…’akasema
‘Ina maana kufa kwake ilitokea kuwa kapotea,…sio kwamba alitokea
hospitalini?’ akaulizwa.
‘Ilivyo ni kuwa wengine wanadai, alipelekwa hospitalini, …na
kipindi hicho alikuwa mja mnzito…., akajifungulia huko alipopotelea…na watu
hawana uhakika na mtoto wake, wengine wanasema huenda mtoto alikufa…sasa hapo
ndio hata sielewi, maana huyo mama alikuwa akiongea na kuchanganya mada akilia
maana inasikitisha kweli....’akasema.
‘Mungu wangu, atakuwa ndio huyo..sijui nimpataje..unasema kijijini
gani?’ akauliza sasa akiandaa kuondoka.
‘Mhh, alisema kijiji cha mbali kweli..hata jina silikumbuki vyema…,
kwani vipi?’ akaulizwa
‘Atakuwa ndio yeye…ni ndugu yake, sasa
nimepata ufumbuzi, lakini mpaka nimuone huyo mama….sasa sasa..nitampataje…oh’akasema
nesi
‘Sikuelewi..’akasema mwenzake na nesi akageuka kuondoka, akitaka
ikibidi aombe ruhusa asafiri hadi hicho kijiji cha huyo mama, na wakati anatoka
akasikia simu yake ikiita;
Akaangalia akaona ni simu ya kutoka nje
‘Halloh, …dakitari ehe..’akaita
‘Ile komputa yangu inaweza kutengenezeka nimefurhi kweli ipo kwa
fundi,…ila nilitaka kujua taarifa za yule mama, mbona nimesikia kuwa alikufa..
ni kweli?’ akauliza
‘Ndio kwani ulikuwa hujui?’ akauliza nesi kwa mshangao
‘Nilikuwa sijui, mimi nilijua tu kapotea….nimepiga simu yenu ya
mezani na nilipokuwa naomba kama wamebahatika kupata hizo kumbukumbu zangu ndio,
nikaongea na yule rafiki yako, ndio akaniambia kuwa huyo mama alikufa..oh hata
siamini,, ilikuwaje?’ akauliza
‘Alikutwaa amekufa… na sasa nimempta ndugu yake kabisa, wanafanana
sana..’akasema
‘Hata macho..?’ akauliza
‘Macho…mmh, sijui, ..oh macho, ….sina uhakika sanai..’akasema nesi
kwani Alishahisi vibaya baadaya ya kusikia kuwa dakitari huyo aliongea na
rafiki yake.
‘Mhh jamani mama huyo…..niliyapenda sana macho yake….’akasema
dakitari na kutuli alionyesha kuhuzunika, na baadaye akasema;
‘Hebu nambie unamkumbukaje huyo mama, alikuwaje, anafananaje..na
hayo macho yalikuwaje?’ akauliza nesi
‘Zaidi eeh, alikuwa na macho mazuri sana ya aina yake….nyusi
ndefu, nyeusi..macho makubwa…na kingine usoni, aliharibika sana, alichanwa
chanwa na kitu kama miba au waya kali… usoni ulikuwa hautamaniki, …nilikuwa na
picha yake kwenye hizo kumbukumbu, na kama komputa yangu itapona nitaweza
kumuona vyema....’akasema
‘Oh, macho ya aina yake yapoje hayo….,
ndio siku ile ulitaka kuniambia hivyo..ulisema kitu kama hicho nikajua
unaniongelea mimi?’ akauliza nesi
‘Mimi, mmmh, labda ,…nilikuwa nakusifia wewe, kuwa hata wewe macho
yako ni mazuri kama ya huyo mama…macho makubwa, nyusi eeh…’akasema huyo docta na
nesi akatabasamu.
‘Kama ya huyo mama!!..?’ akauliza na simu ikakatika….
Nesi akajaribu kuipiga ile simu mara kadhaa, lakini ikawa haipatikani,
akasikitika kuwa amekosa kitu cha muhimu sana, akasema kimoyomoyo, nitakuja kumpigia tena, nione kama komputa
yake imepona...najua huko kuna kumbukumbu za kuweza kusaidia….
`Najua hata yeye anahangaika kunitafuta huko,.. ngoja nisubiri
kidogo’ akasema huku akitembea kuelekea wodi nyingine!
‘Macho yako ni mazuri kama ya huyo mama’…alikuwa ana maanisha nini, kwani machi
yangu ni mazuri, ina maana macho yangu yapoje, …au alikuwa ana maana gani,
akayakariri haya maeneo mara mbili na huku akitafakari haya maneno mapya kutoka
kwa huyo dakitari kijana ambayo sasa yanafana na yale ya dakitari bosi wake.
Cha ajabu alichofanya, ni kwenda chooni, na kujiangalia kwenye
kiyoo kikubwa kilichopo kwenye choo chao cha staff..Akiwa anajiangalia macho yake kwenye kiyoo, huku
akitabasamu, alijaribu kumkumbuka docta kijana, siku ile ya mwisho,..lakini
mbona hakuwahi kumsifia kitu kama hicho…macho macho..
Mara akakumbuka kitu..kuwa dada yake alisema mtoto ana macho
mazuri…mmh, kuna nini kwenye macho macho,…..’akawa anarudia hilo neno macho
macho..macho..mapaka akahisi kichwa kinamuuma.
Siku hiyo ikapita hivyo….
**************
Kesho yake akawahi wodini akiwa na nia ya kuongea na huyo
mama wa mitaani akiwa na uhakika atakuwa keshatulia na huenda kumbukumbu
zitakuwa safi..
Alipofika alimkuta akiwa kakaa kitandani, lakini alionekana kuwa
na mawazo sana, akamuuliza hali yake, akamuonyeshea kwa vitendo kuwa kichwa
kinamuuma
Nesi akakagua kumbukumbu zake, akaona keshapewa dawa, na kwahiyo
hakuwa na la kufanya, akamuangalia huyo mama, na huyo mama alionekana
kumuangalia nesi, japokuwa kajifunika vile vile ..lakini nesi alihisi huyo mama
anamuangalia yeye bila kupepesa macho, nesi akahisi mwili ukimsismuka
‘Mhh, sasa hata namugopa huyu mama..’akasema kimoyo moyo, hata
hivyo alijikaza asionekane hisia zake akasema.
‘Kama kichwa kinauma lala, kitapoa,..’akasema nesi na kuanza
kuondoka, kabla hajafika mbali, akasikia kitu kama kinadondoka, alipogeuka
akaona yule mama yupo sakafuni akajinyonga nyonga..
‘Oh sasa hili balaa..’akasema akiogopa hata kumsogelea, akaguka
kule kwenye chumba cha manesi na kumuita mwenzake.
‘Nesi mpigie simu docta , huyu mama kazidiwa..’akasema na kusogea
pale alipolala huyo mama.
Akainama kutaka kumshika, lakini alihis mikono ikigoma
kufanya hivyo,..hakujua kwanini kaingiwa nauwoga wa ghafla wakati yeye hana
tabia hiyo, akajipa moyo, na kujitahidi tu, akamshika yule mama pale sakafuni asizidi
kujinyonga nyonga huku akiuliza huyo mama anajisikiaje..yule mama akawa anaweweseka
na kuwa kama anataabika…na kitu alichosikia ni kauli ile ile, kuwa anataka
mtoto wake, ..
Na mara dakitari akafika na huyo mama akabebwa na kuwekwa
kitandani.
Dakitari akaagiza huyo mama awekewe dripu yenye dawa, na
haikuchukua muda yule mama akawa kalala..katulia..
Nesi katika ile hali ya purukushani alibahatika kujiiba na kuvuta
ile nguo ya usoni, katikati ya macho, haikuweza kuvuka na aliogopa asije
kuonekana anataka kumuangalia huyo mama..kwenye matundu ya macho…alichoona ni
kuwa yule mama kweli ana nyusi ndefu…nyeusi…mmh huyu mama anaonekana kuwa na macho
mazuri, angeyaweka wazi tuyaone..’akawa anawaza nesi, na mara akakumbuka kauli ya dakitari kijana
‘Macho yako ni mazuri kama
ya huyo mama….’
Na alipokumbuka hivyo yeye kwanza akawa anjiuliza kama kweli yeye
macho yake ni mazuri kihivyo, ni kweli kuwa hata yeye ana nyuzi ndefu na macho
makubwa,….lakini sio ndefu kama za huyo mama,…
‘Macho…’akajikuta anarudia hayo maneno, na alitaka kama docta
ataondoka atamfunua huyo mama aone macho yake yapoje…lakini atakuwa kayafumba
hayo macho, nitawezaje kuyaona..macho ya
aina yake..yapoje hayo
Mara akahisi sauti ikitokea kwa huyo mama, nesi akageuka
kumuangalia, kwa kipindi hicho docta alikuwa kasimama kitanda kingine
akimuhudmia maam aliyeletwa hapo karibuni,
nesi akahisi huyo mama anaota, au anahisi maumivu mahala fulani , lakini
kwa muda ule hakujua ni wapi, na wakati anamsogelea akiwa na nia ya kumshika
aone kuwa ana joto au kumkagua vyema..na ikiwezekana achukue nafasi hiyo
kumuondoa kile kitamba usoni.
Mara akasikia sauti nyuma yake ilikuwa ya huyo dakitari.
‘Vipi kuna tatizo?’ akauliza yule dakitari wake
‘Huyu mama naona anagugumia kama anaota,…’ akasem yule nesi
Yule dakiatri akamsogelea yule mama na kuweka mkono shingoni
mwa yule mama, aliuondoa mkono wake haraka na kumtizama yule mama halafu
akamtizama nesi
‘Ana joto kali sana….’ Akasema dakitari sasa akiweka kipimo cha
joto kwapani kwa huyo mama. Baadaye alikitoa na kusema;
‘Joto ni lile lile..’akasema akiangalia kadi ya huyo mama, halafu
akachukua kipimo cha shinikizo la damu, akampima na baadaye akachukua katarasi
na kuandika maelekezo.
‘Huyu sasa mtambadilishia dawa, baadaye kama nusu saa hivi mpe hii
dawa, nitakuja kumuona baadaye ngoja nikahudimie wagonjwa wengine..’akasema
docta
‘Na nakumbuka hatujaongea..’akasema docta akigeuka kumtizama huyo nesi
‘Ndio hatujaongea, na mimi bado sijakamilisha uchunguzi wangu..’akasema
nesi
‘Uchunguzi wako…!?’ akauliza docta kwa kuonyesha mshangao
‘Si niliwaambi a kuwa kuna mambo nataka kujirizisha nayo kwanza…ikiwemo
kuwasiliana na wale madakitari waliokuwepo kipindi hicho..’akasema
‘Nimeshawasiliana nao..’akasema huyo docta
‘Oh, umewaambia nini..?’ akauliza nesi akionyesha kushtuka
‘Kuhusu huyu mgonjwa...huyo mama’akasema docta
‘Waka-ka-semaje….?’ Nesi akawa hatulii akionyesha wasiwasi mwingi
‘Unajua nahisi kuna jambo lilitokea,…na sijui kwanini, maana hata
wao hawakutaka kuniambia ilikuwaje…., na wamesema hawajui lolote au kukumbuka
chochote kuhusu mama ..kwani eti kulikuwa na wagonjwa wengiwa namna hiyo…basi
yaonyesha kabisa kuna jambo kubwa lilitokea na mkapanga kulificha…’akasema
‘Sasa kama wao wameshidwa kutoa ushirikiano kwanini unanishinikiza
mimi?’ akauliza
‘Kwasababu wamesema kama wewe ulisema kulikuwan na tukio basi wewe
utakuwa unakumbuka vyema…. kama kuna kitu nimekisema basi tukubane wewe, na
uwajibike mwenyewe…maana wao hawakumbuki vyema ni mama gani huyo..’akasema
‘Mungu wangu ndio wanasema hivyo?’ akauliza.
‘Ndio maana nataka tushirikiane, mimi pamoja na kuletwa hapa
nikuambie ukweli, ni pamoja na kuhakikisha uchafu wote wa nyuma unazolewa, na
kama kuna masalia,..na kama kuna watu walizembea, na kusababisha mabilioni ya
pesa za hapa kupotea basi inabidi wafikishwe mbele ya sheria…sasa kama wewe
hutashirikiana na mimi basi itabidi uwe kwenye hilo kundi,..nakupa tu kama
dondoo..’akasema huyo docta
‘Ina maana wewe umeletwa hapa kuchunguza?’ akaulizwa
‘Nimeletwa hapa kama kiongozi, ..na kuhakikisha kuwa hii hospitali
inarejea katika hali yake iliyokuwepo kabla…, unajua hapa tulikuwa tunapata
wahisani wengi, wahisani wakakata misaada yao baada ya kugundua kuwa kuna
ubadhirifu kuna rushwa…kuna uzembe na ufisadi…na hata wagonjwa wakafikia kulalamika..sasa
na hilo la kupotea watoto lipo kwenye kumbukumbu..’akasema
‘Kupotea watoto , mbona haijawahi kutokea?’ akauliza nesi kwa mshangao
‘Ipo kwenye kumbukumbu za madai ya watu, na ushahid ni kama huo kutoka
kwa huyu mama, kama atathibitisha hilo ..nesi utakuwa hatarini, ni bora
ukaniambia ukweli nikajua jinsi gani ya kukutetea, kama itawezekana kufanya
hivyo..’akasema.
Nesi akabakia kimia hakujua
hata aseme nini..akakumbuka kauli ya bibi yake, kuwa kama huna uhakika na la
kuongea ni bora ukae kimia..lakini baadaye, akasema;
‘Ngoja nitaongea na mwenzangu nijua atanishauri vipi..’akasema
‘Na mwenzako!?, mwenzako nani?’ akauliza docta kwa mshangao
‘Si ndio hao madakitari…’akasema kwa hasira.
‘Ok..lakini nimeshaongea nao, labda….kupeana mikakati zaidi..ila
nesi, usije ukasema sikukutahadharisha..’akasema dakitari na kuondoka.
‘lakini mimi nina kosa gani?’ akauliza nesi kwa sauti ya
kusikitika.
‘La kuficha ukweli… na pind hivi unaweza kujikuta unaitwa au
kukutana na askari usalama’akasema docta
‘Askari usalama kwa nini..?’ nesi akasema kwa wasiwasi akikumbuka
kuwa kuna muda alimsikia huyo docta akiongea na mtu, na akawa anataja neno
afande,…na kusema ‘atakuwa anafahamu kitu huyu nesi, uje uonane naye..umbane
atajkuambia ukweli..’
‘Ina maana umeshanishitakia?’ akauliza nesi
‘Siwezi kufanya hivyo…watakaofnya hivyo ni hao waliokosewa kama
huyo mama..’akasema na nesi akageuka kuangalia pale alipokuwa kalala huyo mama,
na kumuona kasimama, akageuka kumuangalia docta na kusema
‘Docta….’akiashiria docta kuangalia kule alipokuwa huyo mama huku
akionyesha uso wa wasiwasi na kama kutaka kukimbia.
NB: Haya kwa leo ndio hayo
WAZO LA LEO: Japokuwa umasikini ni mtihani, na ukiwa
huna kitu unazalilika, unaonekana huna maana, lakini isiwe ndio tija ya wewe kufanya
yasiyofaa, ukageuka kuwa omba omba, au ukaiba..au ukajizalilisha. Umasikini kwa
mungu unathamani kubwa sana, kwani yeye anafahamu kwanini akakufanya hivyo,
huenda ungelikuwa tajiri ungetakabari na kuwa mtu mbaya sana…Muhimu, rizika na
kile ulichojaliwa nacho, huku ukifanya bidii kupata pato lako la halali, kwani
riziki ya halali ipo tu kama utajituma na kusimamia kwenye kutenda yaliyo haki na ukweli…
mimi:
emu-three
1 comment :
Good way оf explaining, and nice piece օf writing to obtain information about my presentation topic, which i am going
to delіѵer in academy.
Hɑve a look at my page temp2
Post a Comment