‘Lakini mimi bado najiuliza kwani wewe
shida yako ni nini hasa kwani huyo mama kashitaki, kwani kumetokea nini zaidi, ni
huko kwa mgonjwa kuwa ana mtoto, huyo kachanganyikiwa, ni kawaida tu, akipona itakwisha wasiwasi wako ni nini…?’ akasema
dakitari yule wa zamani.
‘Docta, siwezi kukuelezea kila kitu kwa
hivi sasa, ila ni muhimu sana, …’ akasema nesi maana alijua hiyo ilikuwa ni
siri, na jinsi anavyoongea na watu ndivyo maswali yanavyokuwa mengi..akaona
hatapata kitu kwa huyo dakitari akaelelea kwa mtunza store na huko hakuambulia
kitu, kumbukumbu za huyo mama zimapotea…
Sasa atafanyaje..sasa atajiteteaje kwa
wakubwa zake
Tuendelee na kisa chetu
Nesi alipotoka kwenye store ya zamani akiwa kakata tamaa ya kupata
kumbukumbu za huyo mama wa zamani alifululiza moja kwa moja hadi kile chumba
alicholazwa huyo mama, ulikuwa sio muda wake wa kumtembelea huyo mama maana
kulikuwa na nesi anashughulikia,… lakini kama nesi mkuu anawajibu wa
kuhakikisha kuwa wagonjwa wanahudmiwa vyema, akaona atumie mwanya huo kumuona
huyo mama.
Kitu cha ajabu cha huyo mama, ipo siku moja yeye mwenye alitaka
kumpima huyo mama, kwani huko kijijini walikuwa wakidai kuwa huyo mama kila
akiona mwenye mtoto anadai huyo mtoto ni wakwake, basi akamuita nesi mmoja,
akamwambia amchukua mtoto mdogo, apite karibu ya huyo mama ili waone itakuwaje..
Yule nesi akafanya hivyo,na huyo mama alichofanya siku ni
kuwaangalia tu, huyo nesi na mtoto wake, utafikiri alijua kuwa wanampima akili
yake,…lakini huyo mama alionekana kama anawaza jambo, lakini hakudai kuwa huyo
ni mtoto wake kama ilivyokuwa huko kijijini, ikaonekana kuwa huyo mama sasa
anaanza kupona…na nesi akamuendea na kumuuliza
‘Yule mtoto sio wa kwako..?’ akamuuliza na huyo mama akamuangalia
tu bila kusema neno, na baadaye nesi akaondoka,..maana ilionekana huyo mama
hataki kabisa kuongea., toka siku ile akawa anapita kwa huyo mama anamsalimia,
na huyo mama kuna mda anaitikia na kuna muda mwingina akakuwa kimia kabisa..
Leo nesi akaona aende kuonana naye tu….akilini alishaona
anahitajia kuongea na huyo mama na takachomuuliza hata hakijui, lakini ni
lazima aongee naye…
Kuna kitu kilimsukuma kwenda kumuona huyo mama tu, lakini hakuwa
na sababu ya msingi..alihisi anataka kumuona…, akili na mwili vikamtuma kufanya
hivyo huku akijiona kama anaulizwa, na
bosi wake wamefikia wapi, nay eye hana la kusema…sasa nitasema nini, akawa
anajiuliza .
‘Huyu mama mbona anipa shida…’akasema
‘Hata siwezi kuvumilia tena, leo ni lazima niongee naye nijue kwanini
ananishuku mimi kuwa nimechukua mtoto wake, …wakati sio kweli, kwanini
ananifanya niwe na wakati mgumu..kwanini, kwanini…ni lazima nikaonane naye
leo..’akasema kwa sauti sasa
‘Kwanza yeye …hafanani na yule mama kabisa, yule mama alishakufa…
iweje tena huyu mama, sijui ni nani, anakuja an madai ya ajabu ajabu ya kutaka
mtoto..’akasema na akilini akawaza, huenda inawezekana huyu mama anadai mtoto wake
ambaye hayupo hapa..ambaye labda yupo kwa ndugu zake….labda, lakini kwanini
wakubwa zake wanamshinikiza na mambo yaliyopita,….mmh, lakini hili nimejitakia
mwenyewe kwanini niliwaambia kuna tukio kama hilo…’akawa anajisema mwenyewe,
Nesi hakujua kuwa anaongea peke yake tena akionyesha vitendo vya
mikono, akawa anakaribia mlango, na huku anasema;
‘Mtu alishakufa, na ikathibitishwa na yule nesi…hapana..hawa
wanataka kunipotezea muda wangu bure,…..eti mzuka uje kulipiza kisasi
haiwezekani, huyu ni mama mwingine tu…mimi siamini mambo hayo…hapana…’akawa
anaongea kwa sauti na kuonyesha msisitizo wa mikono.
Akawa ameshafika mlangoni, akafungua mlango, na hakwenda moja kwa
moja kwenye kitanda, ..humo ndani kulikuwa na vitanda viwili na vyote sasa vina
wagonjwa….alichofanya yeye,…., kwanza akaenda sehemu ya kuhifadhia vifaa vya
kusafishia vidonda kama geresha, ili tu aonekane alikuwa na dhamira ya kumkagua
huyo mama vidonda na ikibidi kumsafisha.
Akatoka na sinia akiwa kaweka mkasi, pamba, na dawa za kusafishia,
….
Alipofika kwenye kitanda cha huyo mama anayemtaka yeye,….alimkuta
huyo mama kalala, inaonekana alishapewa dawa ambazo akizinywa mgonjwa, hupatwa
na usingizi.
‘Mhh, sasa naweza kulifanya zoezi langu bila wasiwasi….’akasema
moyoni.
Taratibu akamsogelea yule mama pale alipolala kitandani, wakati
anamsogelea akawa anamtizama kwa makini, kama kuna lolote analoweza kuliona la
kumkumbusha siku za nyuma kuwa ndio yule mama wa wakati ule au anamfananisha
tu, lakini haikuwa rahisi, kwasababu huyo mama kalala, na kajifunika shuka,
toka miguuni hadi shingoni, na kuacha sehemu ya kichwa tu. Na kichwa kavaa kile
kitambaa cheusi…kama vijana wa mitaani wapendavyo kuita `ki-ninja’ kavaa kininja
Kuna mtu alimletea huyo mama kitambaa kizuri tu cha kujifunika
kichwani, ambacho kinamuwezesha kupata hewa bila shida,…nesi alipokumbuka hilo
neno la `ninja’ akacheka, kweli huyu mama anaonekana kava kama ninja-mwafrika….na
hafanani kuwa kavaa hivyo kwasababu ya imani ya kidini, anakumbuka aliwahi
kumuuliza na huyo mama, alisema anavaa tu maana ndivyo wanawake wanatakiwa
kuvaa hivyo.
‘Ni kutokana na imani yako ya dini au?’ akamuuliza
‘Kila mwanamke anatakiwa kuvaa hivi, na kuvaa hizi sio swala la imani peke yake…kwanza kwanini
unapenda kuniuliza uliza maswali kuhusu mavazi yangu..’akasema kwa ukali na
toka siku hiyo nesi hakupenda kumuuliza uliza tena maswali ya namna hiyo..
‘Lakini kama ni kwa ajili ya imani yake ya dini, mbona sijawahi
kumuona akiswali,…au kwa vile ni mgonjwa..sijui,..labda ni imani yake,..lakini
nahisi kuna kitu anaficha huko usoni, lazima nikione hicho anachokificha……mmh
naogoapa kumuuliza tena maswali maana siku ile alinijibu kwa hasira…ngoja leo
nijione mwenyewe….’akawa anajisema akimsogelea karibu.
Alipofika pale kitandani, akasita kidogo, nia yake ilikuwa amfunue
kile kitambaa alichojifunika usoni…lakini kuna mawazo yakawa yamsuta,
akikumbuka wale waliowahi kufanya hivyo, walivyokuja kupata taabu,…hata hivyo
akaona ajaribu tu…yeye haamini hayo mambo , kwanza yeye ni nesi mkuu, anatakiwa
kuhakikisha mgonjwa yupo salama…
Taratibu akausogeza mkono wake….taratibu hadi ukafikia ncha ya
kila kitambaa, kilikuwa cheusi cha kama hariri, sehemu ya macho pua..ni nyepesi
zaidi..na sehemu nyingine kichwani kipo kama kofia, na mahususi kwa wale
wanawake wenye imani yao ya dini…lakin nesi hakuwa na uhakika kama kweli huyo
mama anavaa hivyo kwa ajili ya imani ya dini. Akakumbuka yule aliyemletea hilo
vazi, alivyosema;
‘Nimemuona yule mama anapenda kuvaa ‘nikabu’ naona ana imani
thabiti na dini yake..’akasema mama mmoja,
‘Mhh, hata hatujui, na hapendi kuondoa ile nguo yake aliyojifunika
…’akasema huyo nesi
‘Basi mimi nitamletea vazi sahihi, linaitwa ‘nikabu…’ asijifunge
ile nguo..naona imeshachakaa, imeungua ungua..…na haipo sahihi….’akasema huyo
mama na kweli siku ya pili akamleta huyo mama hilo vazi, na yule mama
akalipokea, na hakubadili hapo hapo, alikuja kubadili kwa wakati wake.
Basi nesi mkono wake uliposhika sehemu ya lile vazi,ili alivute
kwa juu, akashangaa kuona mkono wake unatetemeka,…sijui kwa woga…au, na hakujua
kwanini mkono unamtetemeka vile wakati hiyo ndio moja ya kazi zake. Na pia moyo
ulikuwa mzito kufanya alichotaka kukifanya,k wani moyoni alikuwa akijisuta kuwa
anachotaka kukifanya pale sio taratibu zake za kikazi,…
Taratibu zake za kikazi, ilitakiwa kumwamsha mgonjwa kwanza…amueelzee
ni nini anachotaka kukifanya…, akakumbuka jinsi wagonjwa wanavyolalamika kuwa
hawatendewi haki, ..na yeye ni kiongozi anatakiwa kuhakikisha haki za wagonjwa
zinatimilizwa,..na akionekana na yeye anakiuka hizo haki na ikafika kwa wakubwa
si ndio atazidi kujiaharibia kazi na kuonekana kumbe kweli yeye alifanya hicho
anachodai huyo mama,kitu ambacho sio kweli…
‘Aaah, nitajua la kujitetea, kwanza mimi ni nesi mkuu, nina wajibu
wa kuhakikisha utendaji wa manesi upo sahihi….ngoja nimtizame kidogo..’akasema
huku, akakivuta ile sehemu ya vazi kwa juu, akaona inavutika, taratibu,
halafu….
Alishituka ghafla mkono wake umedakwa, na kabla hajasema neno,
ukaachiwa mara moja…!
Alishangaa sana, jinsi huyu mama alivyokuwa mwepesi kuulinda uso
wake, utafikiri hilo vazi la kitambaa, ni shemu ya mwili wake. Nesi alishituka
karibu adondoshe vile vyombo alivyokuwa amebeba vya kusafishia vidonda.Na
akajikuta anayatizama macho ya yule mama, ambaye naye alikuwa kamkodolea macho.
Kwa ukaribu ule aliweza kuona yale macho, maana sehemu ya mcho
kuna uwazi ..na akayaona macho ya yule mama yakipepesa…macho….
‘Mhh huyu mama kumbe ana macho mazuri hivi…sijui sura yake ipoje…’akajikuta
akisema kimoyo moyo…
‘Mcho yake kama ya wazungu, yana rangi ya kibuluuu, makubwa, na
nyusi nyingi…..mmh, ningekuwa na macho yenye mvuto kama haya, …’ akajikuta
akijisemea moyoni, huku akitamani kuyatizama yale macho.
‘Kwani unataka kufanya nini..?’ mgonjwa akauliza
‘Oooh, samahani, upo macho, mimi nilidhania umelala…dawa
hazijafanya akzi yake nini…?’ akasema nesi.
‘Nilipitwa na usingizi, mmmmh, mimi naona nimepona huku usoni,
hakuna haja ya kunisafisha tena, sipendi watu kuniangalia uso wangu…’ akasema
yule mama.
‘Hebu nikuulize tena mpendwa wangu…., kwanini unaficha huu uso
wako, …ni imani au,…kama ni kwa ajili ya imani yako, sawa, …nijuavyo mimi,
sijui kama nakosea, hapa upo ndani ya hospitali na hii ni wodi ya wanawake
watupu, unaogopa nini…ndivyo imani yakoo inavyokuagiza hivyo kweli..?’ nesi
akaona aanze kutafuta ugomvi tena.
‘Mhhh, naona mara ya pili
unanidadisi kama sikosei au sio wewe…aah, kumbukumbu haziji, sijui kwanini..,
na…na..sio imani kufanya hivi, jana mwenzako karibu anikimbie nilipofunua uso
wangu…sipendi kuwatisha watu kwa uso wangu ulivyoharibika kwa kuungua na moto,
na wamenichana na mapanga…’ akasema huku akijifunika vizuri.
`Ina maana unafanya hivyo kwasababu ya kuogopa hayo majeraha au…kwani
moto uliunguza uso pia…, au kuna jingine lilitokea…?’ nesi akamsogelea ili asikie
vyema.
‘Mhh, …sikumbuki vyema, ..lakini nahisi…nilipokuwa nakimbia nguo
ilinitoka nikadondokewa na kitu chenya moto, kikaniungza usoni…kwenye majeraha
waliyonikata na mapanga…sikumbuki vyema…sijui ndio hivyo…’akasema
Nesi alishangaa kumsikia huyu mama akiongea kwa utaratibu mnzuri
sio kama siku zilivyopita…, kwani alivyofika hapa mara ya kwanza huyu mama
alikuwa haongei sana, na madakitari walishauri asisimbuliwe na maswali mengi,
kwani anaweza akaathirika kisaikolojia…kuna muda akiona watu wanamshangaa
kuhusu uso wake alivyojifunga, basi anatafuta jinsi ya kujificha hata
kujifunika gubi gubi na shuka…!
`Inaonyesha sasa unaanza kupona, maana mara ya kwanza ulikuwa
huongei sana ukiulizwa wakati mwingine unakuwa mklai sana…’ akasema nesi
‘Kweli kabisa, na nahisi kama vile nimefufuka kutoka kwa wafu..’akasema
na nkauli hiyo ikamfanya nesi ashituka
‘Kafufuka kutoka kwa wafu…’ akawa anayarudia yale maneno akilini
‘Yaani hapa najiona kama, akili ilizibwa, kama mtu alikuwa ndani
ya maji, maji yakaingia msikioni.. unasikia ndiiiii, akilii inakuwa kama ina
giza, na kila mara kunakuja kitu kama kinataka kuzibua ganda lililoganda
ndani..sijui nikuelezeje…’akasema
‘Usijali hayo ni maendeleo mazuri, naona sasa unapona..’akasema
nesi.
‘Na…na, na sijui kuwa nilikuwa wapi, na nipo wapi…mmh, umesema,
aah, hapa ni hospitali eeh, …hivi hapa ndio hospitali ehe, wapi, hapa panaitwaje?’
akauliza yule mama. Nesi hapo akamuangalai tena yule mama, sasa akianza
kuingiwa na wasiwasi, maana mwanzoni alikuwa akienda vyema, lakini hii kauli ya
sasa inatia mashaka…akasema;
`Hii ni hospitali ya mkoa, na uliletwa hapa ukiwa umeungua na
moto…na majeraha ya kukatwa katwa na mapanga’ akasema nesi.
Kwenye hicho chumba kulikuwa na mgonjwa mwingine, mgonjwa huyo
naye alikuwa kaunguza sana..sasa alishaanza kupona. Na yule mngonjwa mwingine
akawa anawaangalia wanavyoongea nesi na huyo mama.
Yule mama mwingine,akahisi yule mama kama anafuatilia yale
anayoongea na huyo mama,…mpaka nesi akashuku jambo, ikabidi amtizame vyema yule
mama, na yule akashituka na kugeuza kichwa chake kuangalia juu, sasa akawa
kachukua simu yake akionekana kama anabonyeza bonyeza
Nesi akawa kashuku kitu, kwa huyo mama mwingine, akawa haongei
tena na huyu mama aliyekuwa na matatizo naye, akawa anamchunguza yule mama
mwingine na kila akimchunguza yule mama mwingine, moyo akamuona kama
anafanana-fanana na yule mama aliyeletwa kipindi kile, umbo, na sura…na yeya
alinguza karibu mwili mzima..uso umebadilika,…yeye hajifuniki, anaachia uso
wake kama ulivyo….
‘Yule mama kama angedai kuwa ndiye yule mama aliyekuja kipindi
kile ningehisi vinginevyo maana ninavyokumbuka yule mama alifanana vile vile…’akawa
anasema kimoyo moyo moyo.
Nikimalizana na huyu nitakwenda kumuulizia, maana anafanana sawa
kwa sawa…huenda akawa ni ndugu yake yule mama ….ngoja nimalize na huyu hapa!
Akagutuka toka kumtizama yule mgonjwa mwingine, aliposikia huyu mama akimuuliza
swali, kama vile anatoka usingizini…!
‘Unasema niliungua na moto, niliungua na moto, wapi nilipoungulia,
sikumbuki…sikumbuki…kichwa kinaniuma,…kwanini kinauma hivi…, ilikuwaje mpaka
nikaungua…?’ akauliza huku anashika kichwani, kuonyesha kuwa ana maumivu
makali. Na nesi akachukua dawa za kutuliza maumivu na kumpa.
‘Kunywa hizi hapa dawa, ulikuwa hujapewa dawa zako za maumivu ….’akasema
alipona kumbe kweli dawa za maumivi hajapewa.
Na yule mgonjwa alipomaliza
kumeza zile dawa , akawa kama anataka kujifunua kile kitambaa, lakini akasita…baadaya
akawa kimia.
‘Umelala..?’ nesi akamuuliza, na hakupata jibu nesi akajua huyo
mgonjwa ameshalala, akaona ajiondokee zake
Nesi…akapanga atakuja kumuhoji huyo mama mwingine wakati mwingine,
aliona muda huo sio wakati muafaka wa kumhoji zaidi, lakini alihisi kuwa huyu
mama hafanani kabisa na yule mama aliyekuwa na mtoto akafariki, aheri
angelisema yule mama mwingine
Akageuka kumtizama huyo mama vyema alivyojilaza pale kitandani, na
moyo wa huruma ukamwingia akifikiria unyama wa wanadamu, kama kweli alivyosikia
ni kweli basi wanadamu sio wema, wanadiriki kumteketeza mama wa watu kwa imani
za kishirikina! Wanamkata kata na mapanga halafu bado hawakutosheka,
wakamuunguza na moto…hata huyo mama mwingine aliyeletwahapo alikuwa na masahibu
hayo hayo….kweli dunia …kweli wanadamu hawana huruma tena..imani tu, hisia tu…mmh
ni hatari.
Wakati anageuka kuondoka, mara akasikia huyu mama akisema maneno
yaliyomshitua kidogo …
‘Jana niliota ndoto ya ajabu sana… , na sijui inamaanisha nini,
…nahisi kuna mtoto, nina mtoto…nahisi niliwahi kuwa na mtoto, nahisi yupo mtoto… hata
nikigusa tumboni langu upande huu… naona kama..nilifanyiwa upasuaji..eeeh,…sasa
mtoto wangu yupo wapi…’akawa kama anauliza
‘Hiyo ni ndoto tu mpendwa…wewe lala dawa ifanye kazi…’akasema nesi
baada ya kitambo kidogo.
‘Mhh, natamani sana niiote tena hiyo ndoto, maana naona kama
inanionyesha njia, na kunifunulia jambo lililojificha…kama nina mtoto yupo
wapi, mimi ni lazima nimpate..’akasema
‘Oh, nesi, naomba uniache nilale…., kwani kichwa hakinipi raha,
kinakuwa kama kina mawingu, kinazibuka na kuziba, nakuwa kama nakumbuka mambo
emngi kwa wakati mmoja, hata sijui nipo wapi…, au sijui…aaah..ngoja…ni-la-le…’
akalalamika halafu akatulia. Na yule nesi akachukua vifaa vyake na kuanza kuondoka
huku akiwaza alichosikia kwa huyo mama.
‘Amesema , nahisi `kuna
mtoto’ sio `anahisi kuwa ana mtoto’ au sikusikia vizuri…akaongezea maneno
kuwa `nahisi yupo..’Huyu mama
kachanganyikiwa, lakini kama kweli ana alama ya upasuaji huenda aliwahi kuwa na
mtoto, sasa sijui huyo mtoto wake yupo wapi…mimi nahisi huyo mtoto atakuwa kwa
ndugu zake, au…alishakufa…sijui…kwa hali kama hiyo sizani kama ndugu
watakubalia abakia na mtoto…’nesi akawa anawaza.
‘Mhh, naona …akili zake zinamrudia na kumvuruga kabisa, inabidi
nimuambia docta kuhus haya ambadiliko…na mimi nataka akili yake ikiwa sawa,
nikae naye nimdadisi vyema, ataweza kunisaidia kuondokana na hizi shutuma za
hawa mabosi ambao wanataak niongee yale nisiyotakiwa kuyaongea
‘Mhh, mungu wangu nisaidia, maana hayo yalishapita….’akasema huku
akikunja uso kwa huzuni.
‘Mungu wangu…usiniache nikaabika…sio kuaibiak tu, naweza kuishia
jela..aheri wahusika wangelikuwepo…sasa hawa mabosi wangu wananishuku vibaya…wanataak
niongee iliyokuwa siri…hapana, hata iweje siwezi kuiongea hayo
yaliyopita..siwezi kamwe….’akasema akiondoka kwenye hiyo wodi maalumu.
Akiwa anatembea kuelekea kwa docta, akasimama akashiak kichwa
‘Nahisi kichwa kinauma ghafala…labda ni uchomvu…aah, nahis ni
kuchoka, ngoja nikapumzike nyumbani…!’ akasema na kugeuka hakutaka kwenda tena
kwa huyo dakitari.
‘Mhh, hata hivyo nilitakiwa kufuatilia yale maswala ya kumbukumbu
za yule mama aliyekuwa na mtoto…’akasema
‘Mhh, na huyu mama mgonjwa naona mabadilio yake yananipa mashaka
mengine..sasa hanidai mimi mtoto, anadai alikuwa na mtoto…. kutoka kudai mtoto
na kusema mtoto wake atakuwa mahali fulani, sasa hivi hamnyoshei yeye kidole…anaongea
ongea yasiyoyoeleweka….naona sasa haitakuwa na haja sana ya kuumiza kichwa
kuhusu kumbukumbu za yule mama, za nini kwanza, huyu mama atakuja kujielezea mwenyewe
mtoto wake kamuacha wapia…!’akawa anaongea peke yake. Na mara akasikia akiitwa
‘Sister, simu yako inaita huku njoo haraka…’ akasikia mwenzake
akimuita na akakumbuka kuwa aliiacha simu yake kwenye chaji na hakuizima,
akakurupuka mbio akijua simu hiyo inaweza ikawa ya muhimu sana. Huenda inatoka
kijijini na hajaongea na ndugu zake wa huko kijijini kwa muda mrefu..na alitaka
kujua maendelea ya mtoto na wazazi wake.
Alipofika sehemu ilipo simu
yake, akaikuta imeshakatika, akatizama ile namba akaona ni namba ya nchi za
nje..
‘Daaaah...nani huyu kanipigia toka nchi za nje…nani ,jamani,
naomba apige tena, …’ akatizama salio lililopo kwenye simu lilikuwa halitoshi
kabisa kupiga simu ya nje, akaangalia pochi yake na kukumbuka kuwa hana pesa za
kutosha kununulia vocha ya kuongea nchi za nje.
‘Mhh tarehe mbaya hizi..pesa hakuna..’akalalamika
‘Maisha haya, mshahara hautoshi ….hata sijui nitawatumia nini huko
kijijini, sasa ningelikuwa naishi na huyo mtoto sijui ningefanyaje, aheri ndugu
zangu wamemchukua…’akawa anaongea peke yake huku akichukua simu yake kwenye
chaji.
‘Na hii namba ni ya nani…mhh, hata sijui….’akasema huku
akiiangalia kwa makini.
‘Basi tena kama ni mtu muhimu atanipigia…sina jinsi nifanyeje…’
akairudisha simu yake tena kwenye chaji..maana aliona haijajaa..lakini
akakumbuka kuwa anataka akajipumzishe nyumbani kidogo, nyumbani kwake sio mbali
sana na hapo hospitalini,
Akainama kiuchukua ile simu na mara akakumbuka jambo…akaitizama
ile namba tena, akatabasamu, ….
‘Mhh atakuwa ni yeye nini….hapana, hii namba ni ya nchi gani..’akawa
anajiuliza
‘Ni lazima nitafute pesa hata kukopa nipige hii namba hata nisikie
tu ni nani, halafu hata ikikatika najua huyo mtu atanipigia…’akasema na
kuichukua simu yake na kutoka nayo nje…
WAZO LA LEO:
shida zinapotushika, matatizo ya kiuchumi, maisha kutuelemea, tusikate tamaa,
tuzidi kujibidisha katika shughuli zetu za kutuapatia riziki iwe ni sehemu zetu
za kazi, au biashara au shambani…na kamwe tusiingiwe na tamaa ya kufanya
yasiyostahili kama kuiba ,kugushi na
mambo mabaya ysiyostahiki, …tukumbuke kuwa shida na matatizo ndio ngazi ya
kutupeleka juu, ndio chachizo la kutufanya tufanye bidii au kutafuta njia
mbadala au nama nyingine ya kupata maendeleo, lakini hala hala njia hizo ziwe
za halali..pambana kihalali, na utapata faida yenye manufaa. Wito, Tusikate
tamaa, tutafanikiwa tu…
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment