‘Kuna taarifa za kutatanisha kuhusu huyo
mama, lakini mimi siwezi kukuambia nitaarifa gani….’ Aliambiwa na nesi mkuu
Sasa leo karudi toka kijijini mara
kakutana na shoga yake na kupewa taarifa kuwa kuna jambo, lakini kama alivyo
nesi, naye shoga yake hakutaka kumuambia ukweli
‘Hivi umesikia kilichotokea..?’ akaulizwa
shoga yake na nesi akamuangalia shoga yake wa zamani kutaka kusikia zaidi,
akauliza;
‘Kuhusu nini?’ akauliza
‘Ina maana hujui,…?!’ akaulizwa shoga wake
kwa mshangao, na hata alivyojaribu kuadadisi zaidi hakupata jibu kuwa kuna kitu
gani kimetokea….`
Hata hivyo nesi hakutilia maanani kwani
alijua huyo ni mmoja wa wapinzani wake…na kicghwani alishajaa mawimbi, kuhusu
kuondoka kwa dakitari kijana bila kumpa taarifa….huyoo, moja kwa moja…,akaelekea
ofisi anapofanyia kazi, na kukutana na mmoja wa wafanyakazi wenzake, na hapo
akaambiwa…
‘Ulikuwa unahitajiwa kwa mkuu wa
hospitali…’
‘Una maana kwa Dakitari mkuu wa hospitali,
kuna nini tena huko..?’ akauliza
‘Mhh, najua..hapa hospitalini siku hizi
kuna mambo ya siri-siri, na kila mmoja anaogopa maana huyo nesi mkuu na sikio
la utawala, ukijifanya uan mdomo mrefu…mmmh, ngoja hata nisiongee mengi..’akasema
‘Lakini najiuliza mbona ndio nimefika tu,
halafu naitwa, na inaonekana kuna jambo limetokea lakini wenzangu hamtaki
kuniambia..’akasema
‘Mimi sijui, ila tu uwe makini na huyo
dakitari mkuu….anapenda dodgo dogo…aijui mke wake hamtoshelezi..’akasema
‘Mhh….unanitisha…’akasema na kabla
hajatulia vyema, mara, akaja mfanyakazi ambaye kazi yake ni kutumwa huku na
kule(tarishi wa ofisini) akamwambia;
‘Nesi unaitwa ofisini kwa dakitari mkuu,
haraka…’….
Hiyo kauli ilimfanya nesi ashutuke, kwani
ni amri, na mtoaji hiyo kauli sio mtu wa
kutoa amri kihivyo, ila kawaida yeye ni mjumbe tu, kwahiyo kaitamka,kama
ilivyo, na inaonyesha ina msisitizo.
Tuendelee na kisa chetu.
**************
‘Kwani kuna nini?’nesi akamuulize yule mjumbe
‘Mhh, sister wangu… hata sijui,..kazi yangu ni kufikisha ujumbe, …
nimeitwa na mkuu, kufika ofisini kwake akanipa huo ujumbe….ila kwa kukutonya, …sio
umbea, nakuambia wewe kwa vile ni sister wangu,
naona pale ofisini kwake kuna mgeni au….wageni.. .’akasema
‘Kuna mgeni, au wageni gani?’ akauliza nesi
‘Niliyemuona kwa uwazi, ni huyo mmoja,…yule pale..niiii, naona ni
ofisa usalama japokuwa hajavaa mavazi yake rasmi,..nasikia siku hizi ndiye mkuu
wa kituo, kazi ipo, … hata kama hajavaa yale manguo yao, mimi
namatambua…’akasema
‘Ofisa usalama! Mkuu wa kituo! Mhh ni yule jamaa watu wanasema ana
roho mbaya..mmmh, sasa kuna kitu gani tena jamani…’akasema nesi
‘Bora nenda sister wangu mungu yupo pamoja na wewe, kwa hivi sasa
nakushauri, usijitwike mzigo kabla
haujatua kichwani..’ akasema huyo mjumbe, na kuondoka zake.
Nesi akapitia maliwatoni,(washroom),
akajiweka sawa, na kwaharaka akatoka na kuanza kutembea kuelekea ofisi ya dakitari
mkuu, na wafanyakazi wa hapo wanajua ukienda hiyo ofisi kuna mawili, kupewa
barua ya majukuu mapya, au kufukuzwa kazi…
*************
Nesi akiendelea kukumbuka
tukio hilo ambalo hakupenda lijirudie tena kichwani kwa jinsi lilivyo, akageuka
kuwaangalia, mabosi wake ambao walikuwa wakiendelea na kazi nyingine wakisubiria
yeye atoe melezo waliyoyataka, na akaona asiwapotezee muda wao, akasema;
‘Bosi zangu, mimi naomba mnipe muda niweze kulifikiria hili tukio
vyema, maana kipindi hicho sikuwepo peke yangu, walikuwepo wakubwa zangu wa
kazi na kipindi hicho mimi nilikuwa nesi wa kawaida tu…., na kama ni hilo tukio
la huyo mama, ambaye nina imani sio huyu, basi ni jukumu ambalo lipo juu ya
uwezo wangu….’akasema nesi
‘Lakini ukisema hivyo, ina maanisha nini, kuwa ni jambo ambalo
wewe ulipewa maagizo tu na hukuwa na hiari nalo..na unaogopa nini kutuambia,
maana sisi ni wakubwa wako hapa na tuypo tayari kubeba hilo jukumu, kwani
livyokuwa, ilikuwa sio kikazi, yaani lilitokea kibinafsi zaidi, au kuna nini?’
akaulizwa
‘Tafadhali wakubwa zangu, kwa hilo naombeni sana mniwie radhi,
sitaweza kusema lolote mpaka nijirizishe kutoka kwao…’akasema nesi na wale
madakitari wakaangaliana na halafu wote wakamgeukia nesi na dakitari bingwa
akauliza;
‘Unahitajia siku ngapi..maana hapa tunapambana na muda, sio kwamba
nakushurutisha kusema ...hapana lakini ni muhimu kwetu…mgonjwa anahitajia
huduma, na moja ya huduma ni kujaribu kuangalia yale anayoyahitajia, kama yana
uzito basi ni muhimu tumtimizie….pili ana toa shutuma kwako…’akasema dakitari
huyo.
‘Lakini shutuma zake sio za kweli….’akajitetea nesi
‘Na tatu, kutokana na kazi yangu, kama jambo lina utata,
tunahitajia kufanya uchunguzi, kwa lengo la kumsaidia mgonjwa ili aweze
kukumbuka vyema ..na hili linaonekana lina utata…’akasema
‘Mimi naona ni kuchanganyikiwa tu akiwa sawa, hilo tatizo
litaisha..’akasema nesi.
‘Nesi unayeongea naye ni dakitari bingwa wa maswala hayo,…mimi
najua kabisa kuna kitu kilitokea kwa huyu mama,…na ukumbuke kuwa mgonjwa bado
anadai kuwa wewe ndiye uliyemchkua mtoto wake,..sasa tuchukulie kaona hayo
madai ni kweli akiamua kwenda kushitaki polisi sisi tutajiteteaje…’akasema huyo
dakitari.
‘Sasa mnataka mimi nifanye nini, maana nimejaribu kuwafahamisha
halai halisi…mimi ninachowamboa, kwa nia njema tufanye tufanyalo… ili tuvute
muda, mimi nitajitahidi kuwasiliana na wakubwa waliokuwepo, kipindi hicho, wote
hata sijui wapo wapi hivi sasa…’akatulia na wale madakitari wakaangaliana tena.
‘Lakini nitaulizia watu wanaowafahamu… na ili na mimi nipate …kujirizisha
mwenyewe, kiukweli huyu mama ana lake jambo sio bure, …kama ni hilo tukio huyo mama
sio huyu, huyu ni mwingine kabisa,…hyule mama alikufa, sasa huyu katoka wapi’akazidi
kusisistiza na dakitari bingwa ajkatabasamu na kugeuka kuangalia dirishani,
huku akisema.
‘Wewe unasema huyo mama alikufa akazikwa na unadai kuwa kuna
mfanyakazi, alikuwepo, ambaye alihudhuria hayo mazishi, huyo mfanyakazi bado
yupo hapa?’ akaulizwa
‘Hapana, hayupo,…’akasema
‘Na hatuna jinsi ya kumpata…?’ akaulizwa
‘Hata sijui yupo wapi siku
hizi…nitajaribu kutafuta kama kuna mtu anafahamu wapi alipo, lakini ni mtu aliyekuwa
akiaminika, ..’akasema
‘Kwa vipi?’ akaulizwa na huyo dakitari mwingine
‘Alikuwa ndiye nesi mkuu kipindi hicho…’akasema
‘Mhhh, naona manesi wakuu, mna kazi kubwa
hapa, kuficha siri eeh….sasa tusipoteze muda wewe jitahidi leo …eeeh, au…eeh...kesho..mmmh,
utaweza kutupatia hiyo taarifa lini hivi…?’ akaulizwa
‘Kesho nitawaambia kama naweza kuelezea
ilivyokuwa nikikumbuka kila kitu…., kama nitashindwa, basi nitawaunganisha na hao
wakubwa waliokuwepo muongee nao wenyewe, maana nisibebe jukumu ambalo sina
uwezo nao…’akasema
‘Kwanini usituunganishie tukaongea nao hao
waliokuwepo kwenye hilo tukio moja kwa moja…kwani kipindi hicho dakitari mkuu
alikuwa nani..?’ akauliza dakitari bingwa
‘Bosi,..tafadhali..naona unataka kucheza
mchezo wa askari kanzu..nieleweni jamani, hilo hata nyie mngelikuwepo,
mngajikuta hivyo hivyo….., sio jambo la kujitakia, lakini ilibidi ifanyike
hivyo, sasa msinibebeshe lawama…na bado nashindwa kujua kwanini mnalivalia
njuga wakati nimeshawaelewesha kuwa huyo mama alishafariki….’akasema akiona
kama kukerwa, lakini kwa vile hao ni mabosi wake, akawa haongei sauti ya
hasira.
‘Ok tumekuelewa nesi…., haya nenda
kafuatilie…na, kesho nahitajia taarifa ya kwamba imewezekana au la…basi kama
haiwezekani..huna budu…. itabidi utusimulie kisa chote ili sisi tujue ni nini
cha kufanya…vinginevyo, tutamwambia huyo mama ashitaki kwa utawala, au aende
polisi…..’akasema na nesi akatoka hapo ofisini akiwa hata hajui aanzie wapi na
hapo akakumbuka tahadhari ya aliyekuwa mkuu wa hospitali hiyo kipindi hicho;
‘Hata itokee vipi, usije kusema lolote, au
kunitaja mimi au mkuu wa kituo…hili liwe kama halikuwahi kutokea,…. maana hii inawezeza
kuchukuliwa kama kesi ya kuua bila kukusudia, au sio mkuu, na imetokana na
uzembe wako…’
Na hapo kumbukumbu za siku
ile zikaanza kurejea kichwani,..na kuanza kukumbuka pale alipoambiwa na mjumbe
aliyetumwa kuwa anahitajika kwa dakitari mkuu kwa haraka, ….
************
Nesi kwa haraka akaelekea huko kwa dakitari mkuu, …ambaye ndiye
kiongozi mku wa hiyo hospitali, na alipofika kwa adabu akagonga mlango, …alipogonga
mara tatu bila kusikia sauti ya karibu, yeye akafungua mlango….., akaingia
ndani na hata kabla hajasalimiana na hao waliokuwepo, akaambiwa;
‘Nesi karibu na funga huo mlango….’ilikuwa sauti ya dakitari mkuu,
na alipogeuza macho pembeni akamuona jamaa mmoja kashikili gazeti, likiwa
limemziba kabisa uso wake, ila aliposikia hiyo karibu, akashuka lile gazeti na
kumtumpia macho huyo nesi, halafu akendelea kusoma lile gazeti sasa akiwa
kalishusha na kuweka sehemu ya uso wake wazi...huku akishika shika kikombe cha chai
Nesi kwa haraka akamtambua ni nina huyo jamaa…, akamkumbuka,
alikuwa afisa usalama wa kituo cha hapo kwao, na baadaye wakasikia kuwa kawa
mkuu wa hicho kituo, Huyu ofisa, wengi wanamuogopa…anajulikana kwa roho mbaya,
mara nyingi kesi ikienda kwake ujue wewe umefungwa.
‘Huyu ni mkuu wa
kituo..wengi hawajalifahamu hilo, bado wakimuona wanamtambua kama ofisa
usalama, sasa hivi ndiye mkuu wa kituo, baada ya yule wa mwanzo kustaafu…’akasema
na nesi akasogea na kunyosha mkono kumsalimia na yule ofisa akasimama na
kuupokea huko mkono,
‘Haya kaa hapo kwenye kiti maana hili tunalotaka kuliongelea hapa
ni muhimu sana..ofisa …ooh, mkuu, samahani, mkuu wa kituo…kaja na
taarifa…taarifa hiyo ni nzito sana..’akaanza kuongea dakitari mkuu.
‘Kiujumla tukio lile,
nikisema hivyo natumai umenielewa, tukio lililokupeleka kijijini, ..la huyo
mama aliyepotea lilipotokea tulijaribu kufuata taratibu zote…..’akasema
dakitari mkuu akigeuka kumuangalia huyo mkuu wa kituo, halafu tena anageuka kumuangalia
nesi.
‘Ikiwa ni pamoja na kutoa taarifa kituoni,na uzuri aliyefikishiwa
taarifa hizo ni huyu rafiki yangu, ..ni rafiki yangu, tumesoma naye huko shule
ya msingi mwenzangu akajiunga na usalama, na mimi kwenye utabibu..lakini hapa
hatuzungumzii urafiki tena..’akasema akimkazia nesi macho.
‘Sasa ni hivi…, baada ya lile tukio, askari wa usalama wakafanya
uchunguzi, lakini huyo mama hakupatikana, ikawekwa kama tahadhari kuwa atakayemuona
au kuona dalili za wapi huyo mama kaelekea taarifa zifike kwa walengwa…yaani
polisi…lakini huyo mama hakupatikana kwa siku …mbili eeh..kitu kama hicho…’akasema
‘Wakati hayo yanaendelea sisi kama utawala, tukapata wazo,…hasa
kuhusu huyo mtoto mchanga…atakwenda wapi , ni nani wa kumlea..tukaongea tukaona
wazo hilo tulilolifanya linafaa…mimi nikamfahamisha ofisa usalama..ambaye
alifikisha ujumbe kwa mkuu wake …, akasema kwa hali ilivyo, huyo mtoto ni wetu,
tufanye kile tunachoona kinafaa…, maana mtoto yule angechukuliwa na nani…unaona
ilivyo…’akasema dakitari mkuu akimwangalia huyo mkuu, halafu nesi.
‘Sasa taarifa zimefika, huyo mama kaokotwa njiani, bondeni,
kafariki…’akasema
‘Ohh, mungu wangu, mama wa watu jamani….mungu nisamehe jamani...sikufanya
makusudi…najuata kwanini niliondoka kufuata hizo dawa…..isingelitokea hayo…’nesi
akaanza kulia.
‘Mhhh, hatutaki kilio hapa..unasikia, imeshatokea, na ni uzembe
wako…, lakini tutafanyaje, na tumeongea na mwenzangu hapa tukaona, kifo
kimeshatokea, na..hata tufanyeje,..haitasaidia kitu..sasa tufanyeje..sisi
tukaoana tuendelee kubeba hili jukumu…kinamna tuonavyo ni sahihi…’akatulia
‘Maana ilivyo ilitakiwa wewe ukalale rumande, huku uchunguzi
unafanyika, lakini tukaona mtoto mrembo kama wewe..hapana, na pia tumekwisha
kupa jukumu la kulea huyo mtoto..hatujui hilo kuwa umempa dada yako..maana
tukisema hivyo ina maana kumbe wewe unaweza kwenda jela kwa uzembe wako…tunajua
wewe huyo mtoto unaye, na ukienda jela mtoto atalelewa na nani’akasema
‘Lakini tujiulize kwa hali kama hiyo, je isingliweza kutokea kwa
yoyote yule kama angelikuwa kwenye nafasi yako…ni makosa ndio, ni uzembe ndio…lakini..inatokea,…kiujumla
mimi kama unavyonifahamu sitaki uzembe...lakini kwa nia ya kumsaidia
mtoto,…tuendelee kulinyamazia hili kuwa mtoto hayupo…’akasema huku akigeuka
kumuangalia huyo ofisa ambaye alikuwa kaangalia nje kwa kupitia dirishani.
‘Imebidi tufanye tufanyalo…ni hatari kiutendaji, usione tunaamua
kubeba hili jukumu tu, na kwa namna nyingine pia ni gharama..watu wanaojua wote
wanatakiwa kunyamazishwa..sasa ni ..anyway
…ni hatari…’akatulia halafu akasema
‘Sasa usikie nesi, sisi kwa kukujali wewe, tukaona tubebe hilo
jukumu…utasema kwanini…sikiliza huyo mtoto anahitajia huduma, na familia anayotoka
huyo mama ni masikini,masikini kweli..….ina maana kama tutaamua kumpeleka huyo
mtoto huko na kusema mtoto wenu huyu…sijui kama ataishi, wanaweza hata kumuua…’akasema
‘Unajua..nesi mambo mengine inabidi yafanyike kihivyo…ndio maana
nimekuita hapa usikie vyema..sasa…hili tumelifanya kama siri, ndio maana
nikakuita wewe, na sikutaka mtu mwingine, kiujumla huyo mtoto hakuzaliwa hai…unasikia,
huyo mtoto hakufanya nini..?’ akaulizwa
‘Lakini..’nesi akaanza kujitetea.
‘Kama hutaki, basi ongozana na huyo mtu wa usalama mkaandikishane,
ukiri wewe mwenyewe kuwa wewe ndiye uliyefanya huo uzembe…basi wao watajua ni
nini la kufanya, mimi sipo tena….’akatulia
‘Na..sio vizuri wewe kuwekwa jela…unajua kituo chao kilivyo,kuna
wanaume wenye laana…sijui ukitoka hapo utakuwaje..nimelifikiria hilo,… samahani
mkuu kusema hivyo, …sijakusudia kuharibu jina la kituo chako,….ila nataka huyu
nesi aelewe kwanini sisi tukaona tumsaidie…’akasema akimuangalia huyo mkuu, na
huyo mkuu akawa kama hayupo anafungua fungua gazeti.
‘Kwanza ujue…, nimefanya
hili kwa vile nakujali…mimi kiukweli nakupenda, sitaki upate shida…naongea
mbele ya rafiki yangu hapa maana tunajuana..usione kwanini naongea hivyo..usiwe
na shaka naye…’akasema huyo dakitari akimgeukia mwenzake, na mwenzake alikuwa
kama vile hasikilizi.
Neno nakupenda lilimshitua sana huyo nesi, kwani ni kweli dakiatri
huyo amekuwa akimtongoza,..mwanzaoni alijua ni utani wa kikakazi…lakini baadaye
akajua kuwa mwenzake kazamiria…nesi akajitahidi kuweka msimamo wake, akijua
kuwa huyo dakitari ana mke na familia yake,…
Huyu mkuu alipoona nesi haelekei, akawa hamfuati fuati tena, ila
alimpa onyo kuwa ajitahidi asifanye kosa,kwani kosa dogo itabidi alilipe kwa
namna yake…. sasa kauli hiyo ya `nakupenda’ inaweza ikawa na maana hiyo, ..lakini akatulia
asikie ni nini kitakachofutia.
‘Sasa nesi kwanza ni wewe kuonyesha upo tayari, hatua ya pili,
ambayo sio shida sana, ni kubadili kila kitu…ionekane huyo mtoto hakuzaliwa
hai, ..na dada yako ndiye mama halali wa huyo mtoto, basi…je upo tayari?’
akaulizwa
‘Nipo tayar i kwa vipi?’ akauliza nesi akiwa kama haelewi, lakini
akilini alikuwa kalenga mambo mawili, kwanza je akikubali kuna nini cha kulipa,
pili, yupo tayari kwa kufanya nini…huenda kuna m zigo ambaoa ataubeba
usiobebeka, kwahiyo akaona awe na tahadhari.
‘Kubeba hilo jukumu na kuhakikisha siri hii inakaa moyoni mwako,
maana ikijulikana umeniharibia kazi na mwenzangu hapa, sisi tumefanya haya kwa
ajili yako na dada yako,… vinginevyo unahitajika ukafungwe, na mtoto aende
kwenye maisha yasiyo na matarijio…unaona huruma yetu inavyotuponza….sasa
tuambie je hilo tulilofanya sio jambo jema..?’akasema kama anauliza.
‘Ni jambo jema,..ila nina shaka ..nitajiona nimekosa sitaishi kwa
raha…hata hivyo nashukuruni sana…mimi kwa hilo la kuweka siri, nitajithidi
maana najua mtoto keshafika sehemu sahihi, ..lakini kama kuna jingine..hapana
sipo tayari...’akasema
‘Hahaha, kama kuna jambo jingine….anyway, Usijali, mengine, tupo pamoja,..muhimu ni hilo,…. hakikisha
hata iweje, usije kuliongelea hili, ni kama vile halikuwepo, na wala usije
kunitaja kwa namana yoyote ile kuwa mimi nilikushauri..tukafanya hili na lile…,
au kumtaja mwenzangu, ..unasikia…kama haupo tayari basi..tuanze michakato
mingine..’akasema na kumgeukia huyo ofisa usalama.
Ofisa usalama au mkuu wa kitu alipoona anaangaliwa akagundua kuwa
kaulizwa swali akaweka gazeti mezani,
akamtizama kwanza nesi, halafu akageuka kumtizama dakitari mkuu, akasema;
‘Mimi sioni kama kuna tatizo hapa, maana kilichotokea ..ndio ni
uzembe, lakini ni jambo ambalo lingeliweza kutokea hata kwa yoyote,…kitu
kikubwa ni kuwa tunahitajia huyo mtoto aishi sehemu apate yote
yanayostahiki….maana hali ya ile familia ni mbaya, mimi naifahamu sana ile
familia....pale ni ulevi, kupigana..hakuna amani, inaonekana hata huyo mama
alikimbia hayo maisha, na mwisho wake uka ndio hivyo…’akasema.
‘Ni kweli kafariki, na..tulikuwa na kumbukumbu za kutoroka kwake
hospitalini, na kakutwa kafariki, akiwa na sare za hapa…kwahiyo ni wajibu wetu
kuja kuulizia tena hapa, ..na kama wanandugu watashinikiza kutafuta ukweli,
basi tutaona la kufanya kitu ambacho naona hakipo…’akasema
‘Huyo mama unamfahamu vyema kwa sura…tabia?’ akauliza nesi.
‘Unajua ni siku nyingi mimi niliondoka huko., sikumbuki vyema…hata
sura siikumbuki vyema…lakini ile familia yenyewe naifahamu, kuna muda
nilitembelea huko nikakutana kesi ya ndugu wa hiyo familia wamekatana mapanga,
kisa ni wivu tu…sasa hata ukiangalia yale maisha yao ni ya hatari.
‘Na…na mmojawapo wa huyo aliyepigana ndiye mume wa huyo mke, …kakimbia
hayupo hapo kijijini muda hajulikana wapi alipo…sasa huyo mtoto utakwenda kumpa
nani…wakati wanafamilia wenyewe wana visasi…’akasema
‘Kwahiyo ndugu zake wanajua kuwa mke wa ndugu yao alikuwa mja
mzito na alitarajia kujifunguao?’ akauliza nesi na huyo mkuu wa kituo
akamgeukia dakitari mkuu, inaonekana hakutaka kulijibu hilo swali yeye na
dakitari mkuu akasema;
‘Hutaamini hakuna aliyewahi kuuliza hilo, ..aliyeongea kwa niaba yetu,
ni nesi aliyehudhuria hayo mazishi maana yeye anaishi huko…., na yeye tulishamwambia
asiongee lolote kuhusu mtoto, na alifanya hivyo, kwahiyo huyo naye ujue kabeba
siri yako,siri yetu..yeye sina shaka naye...umuheshimu sana huyo mdada, na
umtii…’akasema.
‘Yah,,..ni bosi wangu namtii na kumuheshimu, na
sivinginevyo..’akasema nesi na yule mkuu wa kituo akamtupia jicho la mara moja halafu
akaendelea kusoma gazeti, nesi alikumbuka kuwa kuna siku nesi mkuu alimwambia
mkuu huyo anamtaka, na kwahiyo yeye anataka kuweka njia ya wao kukutana mara
kwa mara kwa siri, na nesi akakataa.
‘Na mtu mwingine aliyejifanya anakupenda sana..akajitolea
kukutetea ni yule dakitari kijana,mmh,
napenda dhamira yake na juhudi zake kikazi…lakini kimaisha bado kijana,
hajaiva, madakitari bingwa waamsifia sana..lakini ndio hivyo hajatulia..…unaona
alivyo, katoa ushauri, halafu yeye huyo kaenda zake ulaya hivi ulikuwa unajua
kuwa anakwenda kusoma Ulaya, je alikuaga?’ akauliza dakitari mkuu.
‘Wala sikuwa nafahamu hilo…na hakuniaga, maana alisema hana
uhakika kama atakwenda lini kusoma, ..na hakugusia kusoma nje ya nchi..’akasema
nesi akionyesha masikitiko. Na kwa muda ule alikuwa kakasirika, na alione kweli
alichofanya dakitari kijana sio sahihi, kwanini hakumgusia, lakini hakufikia
kumchukia.
‘Unaona ndio vijana walivyo kudanganyana…sasa huyo achana naye, na hakuna hata haja ya kuwasiliana naye, kama
kuna lolote nione mimi…na kama tutahitajia mambo ya usalama nitaongea na
mwenzangu hapa, huyu ni mtu wangu hana matatizo labda ukiuke sheria, …’akasema
na yule mtu wa usalama akatikisa kichwa na kusema;
‘Mimi naona tumemaliza..muhimu docta…. , ule mzigo…’akasema
akimkazia macho mwenzake na dakitari
mkuu wa hospitali akatabasamu, na kusema;
‘Usijali…hilo ni mimi na wewe….wewe weka sehemu safi, mzigo
utafika, ….haya mambo yapo kwa mwenyewe…’akasema na kumgeukia nesi, akisema;
‘Nesi nilichokuitia ndio hicho kama una swali..uliza, au unaweza
kuja baadaye tukaongea vyema, au sio, kwaheri, ….tutaonana kazini,..nakuahidi
hutapata shida, ilimradi mimi nipo..na ili usiwe na mashaka sana kuna nafasi za
kusoma…mimi nitakutupa huko ukasome,..au unasemaje?’ akamuuliza nesi
Kama kuna kitu ambacho alikuwa akikihitajia hapo kazini, basi
kimojawapo kikubwa ni kwenda kusoma,na aliposikia hivyo, akajikuta akitabasamu
na kwa furaha akasema;
‘Nashukuru sana mkuu, kama itakwua hivy nitafurahi sana,
..’akasema.
‘Najua..ukienda kusoma, utakuwa akili yako kwenye masomo…na huko
hutakutana na watu wa kukuulizia kuhusu mtoto, nani…siunajua, na..ukirudi
..basi wewe utashika nafasi nzuri tu nakuahidi hilo….unaona ninavyokujali, ni wewe
tu sasa…’akasema na kusimama maana yule mkuu wa kituo naye alishasimama
kuondoka, nesi hakutaka hata kusubiria maana alishaona dalili za huyo dakitari
wao mkuu za kumsogelea, yeye kwa haraka akasimama na kwa haraka akatoka mbio
mbio..
‘Mhhh..’alisikia mguno wa huyo mkuu, na mwenzake akasema
‘Huyo ni wako…’
Nesi alitoka pale kichwa kikikuwa kina mawingu, ina maana pamoja
na hayo kuna mambo mengine yamefanyika, kwa ajili ya kufanikisha hilo…je yeye
atabebeshwa mzigo gani…maana hajambiwa atoee pesa…na kauli hiyo ya `huyo ni
wako ina maana gani
WAZO LA LEO: Cheo ni dhamana kamwe usipende kukitumia cheo chako kwa
masilahi binafsi ..ukumbuke kuwa cheo
hicho mwingine anaweza kuja kukishika na akafanya zaidi yako, kwahiyo hicho sio
cheo chako, bali ni dhima, ni jukumu, na ni dhamana.
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment