‘Unajua …kuna yule sister, …’akasema
rafiki wa dakitari kijana wakiongea.
‘Ssiter yupi..?’ akauliza
‘Yule nesi mkuu, …siku moja aliniambia
kuwa wewe unajifanya huna habari na akina dada hapa kazini…kwanza akatania na
kusema huenda..hahaha..’akacheka kwanza.
‘Huenda nini..?’ akauliza akiwa kakunja
uso
‘Haupo kamili..una madhaifu ..eti ya
kiume..’akasema mwenzake
‘Hayo ni mawazo yenu..na kama ninayo hayo
madhaifu, basi yangu mwenyewe,..ila mimi mwenyewe najua ni nini ninachokifanya,..’akasema akiwa
kakunja uso.
‘Sio mimi mkuu, ni yule sister…lakini
akasema anawajulia watu kama nyie, huwa mnajifanya hivyo kumbe mna yenu ya
siri…na ni kwa vile hujaondolewa tongo tongo usoni…hahaha…nakutania tu mkuu,
usikasirike…’akasema
‘Unafikiri mimi nayajali hayo,…najua ni
nini ninchokifanya hilo ndilo la muhimu..’akasema
‘Mhh..sasa ujue yule dada
anakufuatilia…siku ukifanya kosa na pengine likahusishwa na yule dada mnayefanya
kazi naye ujue unalo..nasikia mara kwa mra unamtetea huyo nesi hasa akifanya
kosa…’akasema
‘Eti nini!….lakini ni kawaida tu, maana
yule dada nipo naye kwenye kazi nyingi, sitafurahi mtu akimsingizia uwongo…,
unajua kuna makosa ya kibinadamu, eeh..sasa kwanini nisimtetee kama kakosea
kibinadamu tu, sio makusudio yake….?’
‘Ndio hivyo…yeye anataka kuonyesha kuwa
wewe una mahusiano na huyo dada..na wakati mwingine hamanyi kazi…, kwahiyo,
kuwa makini..na kaahidi kuwa ipo siku atakunasa, aufichue unafiki wako..’akasema
‘Unafiki wangu…! Ok, ninachoweza kukuambia
ni hivi, hawezi…mimi siogopi…kwanza mimi hapa nipo kwa muda tu…unajua, anapotea
muda wake bure …’akasema
‘Lakini uhakiki wa utendaji wako,ambao ndio utakufanya ufanikiwe huko mbele ukiharibiwa
je huoni kuwa hutafanikiwa kwenye ndoto zako, lakini pia utamuachia taabu huyo
nesi…, kwahiyo jichunge sana....uwe makini na huyo nesi..’mwenzake akamwambia.
‘Usijali, mimi sina mpango na nesi yoyote
hapa kazini hilo nakuhakikishia…’akasema
Leo anajikuta yupo na nesi..na walivyokuwa
wamesimama mtu yoyote atasema ni wapenzi…hakutaka kabisa ije kuonekane hivyo….na
wakati anaangalia huku na kule mara akamuona, yule dada ..nesi mkuu
akiwaangalia kwa mbali, na mkononi ana simu, simu inayoweza kuchukua picha kwa
mbali..
Je huyo dada alikuwepo kwa muda gani,na je
ana malengo gani,…
Tuendelee na kisa chetu
***********
Basi ile hali ya nesi kumkumbatia bila kutarajia ikamfanya
akumbuke ahadi yake,..kwanza ilibidi ashikwe na mshangao…hakutarajia hilo
kabisa , kwani alikuwa akimuona huyo nesi kama msichana mwenye aibu, na hawezi
kufanya hicho alichokifanya hapo, japokuwa alihisi kuwa nesi huyo kafanya hivyo
kwa nia tu ya kushukuru kwa kile alichofanyiwa....kiukweli hakulitajia hilo.
Lakini akakumbuka kule kwenye jengo la pili kwa juu yupo nesi mkuu, na kama
atakuwa kakiona hicho kitendo,..ni balaa,…
Dakitari kijana , kwanza kwa kujiamini, akamuangalia yule msichana
usoni , wakawa wanaangaliana, halafu akakunja uso kama kutahayari, alipoona
dalili za usoni kwa huyo msichana…akashangaa na kujiuliza ina maana kumbe kweli
msichana huyo kadhamiria hicho alichokifanya..na huenda sio kafanya hivyo…kwa
nia ya kumshukuru tu, akasema hapana..ni
kawaida tu ,…
Yeye kuonyesha msimamo wake, hakuinua kabisa mikono yake kuitikia hilo tendo, akatulia vile
vile kama alivyo kuwa awali, akazungusha macho hadi kule alipokuwa kasimama
yuel nesi, ..hakumuona pale alipokuwa mwanzoni…
Alitarajia huyo nesi ataondoa mikono yake kwa haraka, na alipoona
huyo nesi haondoi mikono yake kwa haraka, akapandisha mikono yake na kuiondoa
ile mikono ya huyo nesi,..huku anageuka huku na kule sasa akiwa kaingiwa na
wasiwasi, alichelea watu, alichelea yule nesi mnoko asije akamuharibia `sivii’ na msimamo wake.
Aakukumbuka kuwa yeye ndiye alimdhamini huyo dada na kumpigia
chapuo kwa huyo dada hana kosa..sasaa kionekana anafanya hivo na huyo dada
itaonekana dhahiri kuwa alifanya hivyo kwa vile yeye ni mpenzi wake.
‘Lakini huyu nesi mkuu kwanini ananiuatlia hivyo, ..ana lengo
gani, pili mimi simuamini..’akawa anajiuliza kichwani, akakumbuka katika
uchunguzi wa kupotea huyo mama, nesi mkuu alisema huyo nesi anayeshutumiwa kwa
uzembe alionekana akiwa kasimama chumba walichokuwa wakifania upasuaji,..kama
ni hivyo huyo nesi alikuwa wapi..je hakuona huyo mama akitoka kwenye hilo
jengo…
‘Huyu mama nahisi ana kitu..’akasema moyoni
‘Ipo siku nitamnasa nay eye, ni kwa vile tu naondoka, sitakaa sana
haap hospitalini, huyu dada, anaweza akawa pia anahusika na kupotea kwa huyo
mama,…mmh, lakini sina uhakika…’akasema kimoyo moyo.
Wakati anawaza hayo, alimshika yule msichana mikono yake na
kuiondoa mwilini mwake huku akijifanya kuwa ana haraka ya kuwahi jambo fulani.
Na alipofanya hivyo mikono ya yule dada ikawa kama inaendelea kuwepo, sasa
akataka kumsukuma na wakati anataka kufanya hivyo, alijikuta akiangaliana tena uso
kwa uso na huyu nesi uso-kwa-uso, na
hapo akajihisi kutahayari zaidi, na hisia za ujana zikataka kumtawala….akajikuta
anahema..na ilikuwa kidogo tu,… kama wasingelisikia mtu anakohoa nyuma
yao….bila kuangalia ni nani, akasema;
‘Unasikia sister, unatakiwa utafakari vyema hicho unachotaka
kukifanya…’akasema
‘Mhh kwanini docta…kwani kuna ubaya gani, hebu nikuulize docta
..mimi nipoje…?’akasema nesi, na yeye hakutaka kumpa nafasi akasema;
‘Unajua sister…wewe kwa hivi sasa una majukumu mazito mbele
yako..huu sio muda wa kufanya mambo mengine yatakayo kufanya usijisikie
mnyonge…na kushindwa kutuliza kichwa kwa jukumu hilo kubwa ulilo nalo..sijui
unanielewa…’akasema na nesi akiwa kama kaishiwa nguvu, akainama, na unyonge
fulani ukamuingia, kwani alichotarajia hapo hakikutokea, akahisi huenda huyo
dakitari kijana hampendi, kama alivyohisi yeye moyoni.
‘Mhh, haya bhana,…samahani kwa hili…bosi, ..najua hujapendezewa, na usione kuwa mimi nimuhuni,
hapana…imetokea tu…naomba tafadhali usije kunifikiria vibaya…nilitaka tu
kukushukuru kihivyo…’akasema nesi,
‘Kwani umefanya nini sister..ni kawaida tu….muhimu ni kuchunga
macho ya watu, macho ya watu yana tafsiri nyingi, hasa yakiona tendo lenye
kuvuta hisia..hata kama sio kweli, akili za wapiga domo, akili washambenga,
zitatafsiri kwa nia mbaya, ..unajua hilo. ..’akasema
‘Nikuambie kitu sister…, shati jeupe ni rahisi sana kuonekana
uchafu wake, kuliko shati jeusi au lenye rangi inayofanana na uchafu..na ndivyo
ilivyo kwa watenda wema, kwao wao wakifanya kosa dogo tu…itakuwa ni gumzo,propaganda,
uzushi utasambazwa..kwanini, kwa vile wenye wema wana mitihani mingi sana…kwahiyo
kuwa makini..’akasema dakitari.
‘Kwani…kuna nini kinachoendelea baada ya hiyo kesi..?’ akauliza nesia
akionyesha wasiwasi
‘Bado wanafanya uchunguzi kuhakiki, kama kweli kuna kosa, japokuwa
wamelinyamazisha kinamna..lakini kwa ufupi bado uchunguzi unafanyika, maana
huyo mama hajulikani wapi kaenda, na kama litatokea baya ujue hospitali itabeba
lawama..kwahiyo bado hali ni tete, na ni kuwa nesi mkuu, kapewa kazi ya
kufualia nyendo zako….’akasema.
‘Nesi mkuu,..nesi mkuu…. huyo dada simpendi..…lakini ipo siku
..nina imani hiyo sehemu yake ipo siku nitakuja kuishika mimi , hizo ndio ndoto
zangu…’akasema
‘Kila laheri…’akasema docta
‘Ahsante….’akasema na kujaribu kutabasamu.
‘Sasa sikiliza sister, pamoja na mengine ukumbuke kuwa huyo mtoto ni mtoto mchanga…anahitajia huduma za ziada,
sio kazi ndogo hiyo…na inahitajika uwe na maamuzi ya haraka, kuanzia sasa..’akasema
dakitari.
‘Ndio hivyo,…kiukweli nilishakata tamaa kabisa, na nilitarajia
kuwa utanisaidia kwa hilo, tukamlea huyo mtoto kwa pamoja..’akasema
‘Kumlea kwa pamoja mimi na wewe…!?’ akauliza docta kwa mshangao
‘Mhh…niliwazia hivyo tu..samahani kwa hilo..na uliposema
haiwezekani, nikajua sasa ninalo..’akasema
‘Hapana sitaweza hilo..ila..kiushauri tupo pamoja…’akasema
‘Lakini hata hivyo nimefurahi sana…hasa ulipolitoa hilo wazo, la
kama kuna nduguna ..wazo ambalo nilikuwa nimelisahau kabisa,..ukaniwezesha
kukumbuka kuwa dada yangu alikuwa akihitajia mtoto, hata wa kulea… ,’akatulia
akitabasamu.
‘Sawa haya ngoja mimi nikuache, maana tumesimama hapa kwa muda, na
..nilimuona yule nesi mkuu akituchunguza..’akasema
‘Wapi…., mungu wangu weeeh..’akasema nesi akiangalia huku na kule,
lakini dakitari kijana hakujali, akasema;
‘Usijali, hujafanya kosa lolote, niamini….wewe hukusikia mtu
akikohoa…alikuwa yeye, kaona kule mbali haitoshi kasogea karibu atakuwa maeneo
ya hapa karibua natusikiliza..lakini usijali…’akasema huku akiwa kajiegemeza
ukutani
‘Mhh, nashukuru bosi, nikiwa nawe najihisi salama..’akasema
‘Sawa usijali,ila… kuna kitu nataka kukuambia, samahani sana kama
nitakuwa nimekuuzi..’akasema dkitar kijana na nesi kusikia hivyo moyo ukalipuka
paah, akajua sasa huenda, dakitari anataka kusema lile la moyoni, ambalo
linaweza kufungua ukurasa anaoutaka yeye, akatabasamu na kuinama chini kwa
aibu.
‘Sister, kama nilivyokuambia, sio wote wanaokuchekea ukazani wana
nia njema na wewe…kicheko, tabsamu linaweza kuwa la wema au ubaya, furaha au
huzuni, au sio..yote yawezekana kwa binadamu, sasa…mimi , ningekushauri saaana,
ili kuwa salama,…tukiwa hapa kazini, jaribu sana usiwe na mimi karibu karibu
kama hivi…’akasema
‘Mhhhh..’akaguna nesi.
‘Unajua bado unafanyiwa uchunguzi…kama nilivyokuambia, na nesi
mkuu kapewa jukumu la kuchunguza nyendo zako…sasa utawala ukiona upo na mimi
kihali ya …kama hii, utanihisi vibaya kuwa mimi nimekusaidia kwa kuwa wewe ni
rafiki yangu…’akasema
‘Mhh..ni kweli..hata hivyo, …wewe ni rafiki yangu kikazi..au
sio…na sio mbaya sijui kama nimekosea..’akasema nesi.
‘Sister..sitaki kukuumiza, ..wewe unajua kabisa mimi na wewe
hatuna mahusiano yoyote…, zaidi ya kuwa wewe umetokea kuwa ni mwenza katika
kazi zetu.., na nataka iendelee kuwa hivyo na sio vinginevyo… naomba uelewe
hivyo, samahani sana..’akasema huyo docta..
‘Mhh..samaahni docta..nimeshindwa tu kuvumilia…lakini..sijafanya
vibaya, eti…kama nimekosea naomba unisamehe…nilishindwa kuvumilia, na
ningekushuruje…hata hivyo,…sijui..nisamhe tu docto’akasema nesi akiwa kainama
na sasa akitaka kuondoka.
‘Sikiliza sisiter, wala usijisikie vibaya…hujafanya vibaya…kuna
kitu kingine nataka tu kukuambia…’akasema docta huyo sasa wakiwa wapo mbali
mbali, na nesi akawa hasikii vyema, akageuka na wakaangaliana, na machozi
yalishaanza kumtoka yule dada
Docta akanyosha mkono wake, na kumfuta yule dada yale machozi,
wakawa wamesimama, japokuwa sio kwa karibu sana.. docta akatulia akilini akiwa
anajiskia vibaya,a kihisi huenda kaongea jambo lililo muumiza huyo dada,
hakupenda kabisa kumuumiza mtu ..hasa akina dada, akina mama, kwake yeye,
anawaona kama watu wanaohitajia upendo wa hali ya juu, akawa najiuliza afanye
nini kumliwaza huyo dada.
Bila kuogopa sasa akamsogelea huyo dada, akanyosha mikono na
kumshika sister kwenye mabega kwa mikono yake miwili…, ni kwa mbali, hakuwa
kama wamekumbatiana, wakawa wanaangaliana usoni, akasema;
‘Kwanza naona usisononeke…sio kwamba nimesema hivyo kwa vile
labda,…sikupendi..hapana..nikuambie ukweli, wewe ni msichana wa peke yake hapa
kazini, na mwanaume atakaye kupata wewe , atakuwa na bahati kubwa,..’akasema na
kutabasamu.
‘Ahsante..’akasema nesi.
‘Mimi siwezi kukudanganya, bado nina safari ndefu ya
masomo…sijataka kutulia na kujiingiza kwenye mahusiano na yoyote yule..muda ukifika
hali itasema lakini kwa hivi sasa..hapana,…sitaki nije kumuumiza yoyote
yule…’akasema
‘Hamna shida nimekuelewa…’akasema sister huku akiumia kimoyomoyo.
‘Sasa sikiliza…unajua ..kuna kitu nilikiwaza kabla, nataka
nikuambie ...’akaanza kusema doctor, na
nesi moyoni nesi akawa anaombea dakitari huyo atamke neno tu la kumliwaza hasa
la kimapenzi..ambalo litaonyesha kuwa huyo docta anampenda...japo..hata kwa
baadaye.
‘Mhh…kitu gani… wewe sema tu, nakusikiliza wewe bosi wangu…’akasema
nesi akimuangalia doctor sasa kwa macho yenye kuonesha huruma .
‘Ni kuhusu huyo mtoto na mama yake…’akasema.
‘Huyu mtoto...! sawa, lakini mama yake mhh, maana hayupo, kuanzia
sasa mama yake ndio mimi, au sio?’
akasema nesi kwa sauti ya unyonge na kukata tamaa.
‘Mhh…mimi nazungumiza mama yake wa asili, mama mzazi…unajua,
nikuambie ukweli wa kutoka moyoni,… kama kuna kitu kinanigusa moyoni ni hali
kama hiyo…’akasema akiangalia mbele, alikuwa hamtizami huyo nesi…
‘Mhhh..hali ipi…?’akaguna na kusema hivyo huyo nesi.
‘Hali hiyo ambayo inafikia hatua….mama ana ujauzito, na labda
ujauzito wenyewe ni wa taabu na mashaka…na mungu bariki, anapata huyo mtoto kwa
shida…, huku hana uwezo hata wa kumlea,..ukirudi nyuma kwenye maisha yake
huenda…alikuwa akiishi kwa shida, majanga…na yote hayo, huenda ni kutokana na ndoa.., ‘akatulia.
‘Tunasoma tunaenda shule, tunajifunza mengi tu…, ili iweje..ili
tupate mkate tu wa kila siku ..hapana…tunahitajika kufanya jambo..maana kuna
mambo yanahitajika kubadilishwa..dini zimesaidia sana…, lakini cha ajabu hivi
sasa dini zinapigwa vita..sasa hizi, mila , desturi za ajabu ajabu zitaondokaje,
maana kuna desturi za zamani, na kuna nyingine zinajitokeza mbaya zaidi, ni
nani wa kuzikemea, maana zinaletwa na watu wenye uwezo, ni nani…’akawa kama
anaulizwa.
‘Nikuambie ukweli nimefanya tafiti nyingi…akina mama wananyanyasika
sana…hasa ndani ya ndoa….sijui kwanini, kwanini watu hawataki kuelewa ni nini
maana ya ndoa…ndoa sasa hivi ni sanaa tu, inakuwa kama watu wanaigiza tu…’akasema
dakitari kijana, na nesi akatabasamu….
‘Mhh, wewe unaelewaje maana ya ndoa maana hujaoa na umesema hutaki
kuliwazia hilo…kwasasa maana muda wake bado?’akasema nesi kama anauliza na
mdomo ukaonyesha tabasamu la mbali.
‘Mimi ni mtoto wa mkulima..nimesoma kwa shida sana usione hivi,
isingelikuwa ni juhudi za wafadhili na kipaji changu cha darasani…sijui
ingekuwaje…’akatulia
‘Wengi wakiniona hivi wanahisi natoka kwenye familia yenye
uwezo..hapana…mimi nikuambie ukweli…, nimeishi kwenye familia zetu za
kimasikini…, nimeona taabu za akina mama, kutoka kwa waume zao…mume muda wote
ni hasira, kakunja uso utafikiri kaona nini…ajabu kabisa’akatabasamu kidogo
lakini uso ukionyesha uchungu.
‘Mume na mke, wanaishi kama maadui…hata kitu kidogo tu, mume anamjibu
mkewe kwa hasira…mke anajaraibu kujishusha, kunyenyekea, oooh, ndio utafikiri
kapasha moto kwa mume…haya ni maisha gani…sivyo hivyo ndoa ilivyo.., hawa watu
wameoana, ili `kuwe na raha…kwa hali hiyo raha ipo wapi…ni taabu kweli kweli.’ ‘akasema
maneno hay kwa mapozi.
‘Umeonaeeh..’akasema nesi
‘Unajua mimi nijuavyo hata kwenye dini,..maana usionione hivi mimi
nasoma kila kitabu, nasoma vitabu vyote vya dini zote…ili nijue yaliyomo…hasa
kwenye fani yetu hii ni muhimu kuyaahamu hayo…nijuavo mimi , dini inasema, ndoa ni
raha..au sio..’akawa kama anauliza
‘Kwahiyo mke na mume hata wakiongea waonyeshe ile tabasamu…kuonyesha
wapo kwenye raa, upendo wa dhati…maana ukifanya kinyume chake wewe huijui ndoa,
unaikosea ndoa, na ni dhambi, kweli si kweli?’ akawa kama anauliza na hakusuiri
jibu akasema
‘Unajua….mkiwa ndani hata nje mke na mume mnatakiwa muonyeshe upendo
halisi,maana mumeshapewa ruhusa, nyi mpo uwanjani wengine ni watazamaji tu,
sasa kwanini muihini ndoa…kiukweli, hapo ndipo pa kumaliza lile tabasamu la
mwisho…unaniona….eeh..chuki haitakiwi kabisa, anayefanya hivyo hajui maana ya
ndoa…’ akasema kiamwangalia nesi kwa kujiiba pale alipomuona nesi akitabasamu.
‘Unajua… mimi muda wote napenda kutabsamu, najaribu kujifunza
nitakavyo tabasamu kwa mke wangu…lile tabasamu la mke wangu bado lipo
sandukuni….hahaha..... yah, ndio hivyo…akasema
‘Ni kweli… hilo usemalo ni sahihi kabisa, ndoa, inatakiwa kuwe ni
sehemu ya amani, na hata kaam umechoka ukirudi mkikutana na mke wako yale
machomvu yote yaishe,..je yanaanika hayo, …na kiujumla wanawake
wanajitahidi..lakini waume wanakuwa wagumu kuelewa, wanaona kuwa ukali, kukunja
uso…kukaripia ndio njia ya kuwa kiongozi wa familia….kiujumla wanawake tunapata
taabu sana..’akasema nesi.
‘Yah..ndio hivyo…nikutokuelewa..kwa mfano tu… hebu angalia huyu
mama, …sijui kwanini kafanyiwa hivyo,..ukiangalia alivyo…yaani kaharibiwa uso....yaonekana
kabisa kuna jambo baya lilimtokea…na aliyemfanyia hivyo aliataka kabisa
kuharibu sura yake, …sasa baya zaidi, siji watu hao wana roho gani, hawakujali
kabisa kuwa huyo mama ana kiumbe tumboni,
yaani namuonea huruma sana huyo mama, I wish, ningelipenda…nije niongee na huyo mama nijue chanzo cha
hayo yote ninini…haiwezekani….’akasema wka uchungu.
‘Mhh..jamani..unanihamasisha,…docta, lakini acha tu..endelea
kuongea..’akasema nesi.
‘Unajua pale nilipoambiwa tunamfanyia huyo mama upasuaji, na tunatakiwa kuchagua, mama au mtoto, nilihisi
machozi..yaani pale kabla sijaanza kazi, nikamuomba mungu kuwa mikono aliyonipa
na kipaji alichonipa kisije kuishia kwenye kutenda ya kuua, …sio kwamba tunaua,…
maana inafikia mahali unaambiwa hivyo, jitahidi umuokoe mtoto, mama achana naye
au jitahidi umuokoe mama, mtoto achana naye, hapo kwangu naona kama ni kuua,…
sikupenda na sitopenda ije itokee hivyo kwangu..ndio maana nikawa anjifunza
zaidi mishipa ya ndani yenye kusaidia…ni uchunguzi mgumu na unahitajia imani
zaidi..’akasema dakitari.
‘Kweli wewe ni dakitari mwenye moyo wa huruma, na ….sijui kwanini
watu kaam nyie ni wmungu …lakini wewe hujaoa na unasema hutarajii kuchache sana
hapa duniani…lakini mimi najiuliza wewe hujaoa, lakini unavyoongea utafikiri
mtu mzima anayejua au aliyewahi kuishi kwenye ndoa…, umejifunzia wapi mambo
hayo ya ndoa…na sijui mkeo atakuwaje…’akasema nesi.
‘Ni kweli, sijaoa..lakini kutokana na kazi yetu, unajikuta unasoma mambo mengi
tu maana kazi yetu kiujumla ni utashi..ni moy, ni kutuma zaidi wanasema ni
wito…kwahiyo ili uifanye kwa moyo mmoja, unahitajika, kunajifunza mengi…’akageuka
kushoto na kulia , halafu akasema;
‘Unatakiwa kujiunza mengi na
hata kupitiliza..mimi napenda kuwa dakitari bingwa wa akina mama, uzazi na
matatizo yao tu, upasuaji, na saikolojia nzima ya ndoa..kwa hivi sasa
nimejikita kuwa, Gynecologia..’akatulia kidogo.
Lakini
sijajitosheleza..nataka nijiunze kwa undani zaidi..ili niweze kujitosheleza,
yaani mambo yote ya` Obstetrics and Gynecology’…hayo..ndio fani
yangu..lakini sitaishia hapo, nataka kuangalia na matatizo ya ndoa, yaani
saikolojia nzima ya mke na mume, mpaka wanazaa, matatizo yao…ni ndoto lakini
inawezekana..’akatulia.
‘Lakini mimi naona
umeshahitimu tayari, tena kwa vitendo..’akasema nesi.
‘Bado sana..bado nina
safari ndefu…nataka nitakapokaa kuwa dakitari nifenya miujiza..nataka akinamama
muwe na raha…unajua…nilipokuona unatoa amchozi nilikumbuka mbalia sana,
namkumbuka mama…oh, nani kama mama jamani….ndio maana sitaki kuona
machozi….hasa yanayotoka kwa akinamama, nataka nione tabasamu na furaha usoni
mwao…hiyo ndio ndoto yangu…’akasema na alionekana kuonyesha dhamira ya kweli
usoni.
‘Mhh, jamani ukisema hivyo
ndio unazidi kuniumiza..’akasema
‘Kwanini..?’ akauliza
docta akimuangalai nesi kwa mshangao
‘Natamani niwe na mume wa
namna yako, ..ndio maana sijaolewa mpaka sasa, wengi wanaonitaka kunioa hawana
sifa nizitakazo mimi..naogopa sana ndoa na matatizo yake..nimeona machungu
mengi wanayopitia akina mama,hasa kupitia kwenye ndoa zao…akikosa kuzaa lawama
kwa mama, akizaa, lawama kwa mama, unazaa sana,au unazaa wanawake watupu..mtoto
akiharibika tabia lawama kwa mama…nikifikiria hayo mmh, yaani naogopa.. sijui
kama nitaolewa tena..’akasema
‘Usiseme hivyo..kuwa hujui
kama utaolewa… muda ndio utakaosema,..nikuambie kitu muda wa kuolewa au kuoa
ukifika, ..hakuna majadala, utajikuta umeolewa,au kuoa, na huenda ukaoa au
kuolewa na hata mtu usiyemtarajia kabisa…kabisa, na hapo unaweza kufanya makosa
ya uchaguzi…lakini yote ni heri muhimu ni wanandoa kufahamu nini maana ya ndoa,
wengi hawafahamu hilo…’akasema docta
‘Sasa kwanini inakuwa
hivyo docta…?’ akauliza nesi.
‘Ndivyo ilivyo..wenzetu
wanaita `destiny’…kiujumla ni mungu
mwenyewe kapanga iwe hivyo…na wengi wanakuwa na ndoto zao..hizoooh..mmm,lakini
mwisho wa siku , muda ukifika, ..inatokea tofauti..japokuwa ni muhimu kujipanga
na kuwa na malengo,na malengo ni dhamira ya kutoka moyoni na matendo…’akapiga
piga miguu chini, halafu akasema.
‘Kiukweli, huwezi kusema
nataka mume mwema, au mke mwema, wakati wewe mwenyewe haupo hivyo, sasa
utamlaumu nani eeh, lakini pia kabla ya ndoa ni muhimu kwanza kuweka msingi wa
maisha…maana ndoa bila kujiwekeza, ukajua mtaishije,..nayo ni mtihani…ndio hapo
ukasikia mimi nikisema hilo la ndoa bado sijawa tayari…’akawa kama anatabasamu.
‘Lakini pia ni kujibidisha
kwa kujifunza ndoa ni kitu gani, ni nini ndoa…hili ni tatizo…watu hawajui,
yaani hilo nimejifunza, na ni kweli,..hebu nikuulize, hivi uliona watu wakienda
shule kabla ya kuoa, kuwa wanasomea kuhusu ndoa…hakuna..watu wanachukulia
uzoefu kutoka…kwa baba na mama..na hapo ndio nikagundua jambo muhimu
sana..’akasema an kutulia.
‘Sister..nadharaia nzima
ya ndoa…ina mapungufu mengi…lakini ngoja nimalize `project yangu’…kwa hivi sasa
ninachoweza kusema ni kuwa...mungu anatufahamu kuliko tunavyojidanganya wenyewe…’akatulia
kama anawaza jambo halafu akasema;
‘Wengi tunafahamu hivyo
kuwa msingi wa maisha hujengeka kwenye elimu,…sasa najiuliza ni nani alikwenda
shule kufahamu nini maana ya ndoa kabla hajafunga ndoa…nikachunguza nikaona
hakuna…muda ukifika aah, mtarajiwa, aaah, keshaoa, ..mara ngumi, mara
…kuachana…kosa lipo wapi hapo…na kuna kitu kinakosewa hapa…, kwa sisi, hasa
waafrika, na sio waafrika walio wengi…tunakuja kujifunza kuwa kumbe msingi wa
maisha ya mwandamu, ..elimu ya msingi..ya maisha ya mwanadamu, inatokana na
maisha ya baba na mama,…’akatulia.
‘Hapa watu wengi hawajui
hilo.. elimu inakuja baadaye ukishapevuka, na elimu hiyo ya kitabu, darasani,
…unakuja tu kukupanua fikira zako na kukuwezesha ujue fani gani utakuwa nayo
kama mimi nimechagua kuwa docta..unaona eeh..’akamuangalia nesi.
‘lakini msingi mama,…ni
kutokana na jinsi baba na mama wanavyoishi, wakiwa na upendo..wanatarajia
familia yenye upendo na furaha…na kinyume chake ni ndio hivyo, wakiwa na
mihasira, kukemeana, mume ni kama simba..yaani taabu …basi watoto wanakuwa
hivyo hivyo…’hilo ndilo asilia.
‘Sasa sehemu ukilichunguza
hilo ukaona aaha, kumbe…baba na mama ndio msingi wa maisha…basi hapo hapo
utagundua umuhimu wa kuchangua mwenza,..na ile nadharia ya mke mwema na mume
mwema ndipo inakuja hapo..lakini hapa napo kuna walakini wake…’akatulia tena.
‘Unajua , wengi
hawalichunguzi hili kwa makini..na kwa vile umepevuka, umeshajitoa kwa baba na
mama, hebu basi chunguza mapungu yao na wewe uyaboreshe kwako, yale ya
asili..ukali, eeh, udume, ok, haat ujike chuja na ujipange kivingine, na
itawezekan basi kwa hata kulisomea hil..jifunze , chunguza…, ni nani mume mwema,
na ni nani mke mwema…hapa kuna tatizo, na ndio chanzo cha majanga duniani…’akahema.
‘Unaona vita…watu
wanauwana…watu wanachukiana, ni nani aliweza kuchunguza zaidi chanzo cha haya
yote…, akagundua ni nini asili ya hayo yote, hebu niambia wewe ukiulizwa chanzo
hasa cha uhasama, chuki hadi vita.. ni nini..’akamwangalia nesi.
‘Kiukweli…watu hawalisemi
hilo, chanzo na huku nyuma ,…jinsi gani wawili waliishi, wakajenga kizazi
chema, chenye maadili..jinsi gani ndoa ilichukuliwa kwa uzito wake, ndoa ikawa
ni raha, upendo, na matokea ni kuzaa watoto wenye upendo , furaha, na kizazi
kinakua hivyo..lakini duuuh..watu wakaifanya ndoa ni ndoana…sasa ndio hayo
mnazaa watoto vichwa maji,..unafikiri itakuwaje, chuki , visasi….mihasira watu
kuana wanaona kaamni raha tu…hawalisemi hilo…matokea yake wanaanza kuanzihs
mambo ya ajabu, …eti wanavunja uasilia wa mwanadamu, watu wenye jinsia moja
kuoana…hili litakuja kuigharikisha dunia…mtaona ..yatazuka magonjwa…mimi
naogopa…dunia inapokwenda ni kubaya, maana tumeshataka kuiharibu asilia…ya baba
na mama..’akatulia na kuangalia saa.
‘Ulisema unataka kuniambia
nini, maana naona unaangalia saa, na kiukweli docta, natamani kuwa nawe kwa karibu
sana, nikirudi kutoka kijijini naomba tukutane…naomba sana,please..tafadhali....’akasema
nesi na dakitari akaabasamu hakusema neno na nesi akaendelea kusema
‘Mhh.. sasa hivi, mmh, huenda
ukaitwa,na mimi, nataka kwenda kumuangalia huyo mtoto na kuona taratibu za
kumchukua, hata leo, au kesho..naona tukizidi kuongea hapa…unazidi kuniumiza
moyo wangu, lakini natamani nikae na wewe tuongee zaidi..kama hutojali lakini..’akasema
nesi
‘Ehee..nilitaka tu
nikuweke sawa…lakini ninachotaka kusema ni hiki….’akasema na nesi akatulia
kumsikiliza
‘Sasa ni hivi, kuna kitu wanasema
watu wenye hekima…, kitu bila kumbukumbu hupotea hewani, au sio….mimi haya yote
nayafanya katika kutimiza lengo langu na nahitaji kuweka kumbukumbu kila hatua
ya kazi zangu, nimeanza zamani….’akasema
‘Sasa kwa hili tukio la huyu mama, ..mmh, ..kutokana na hiyo hali,
nikijua kuwa huenda mama akafariki,…nikawa najiuliza kama atafariki na mtoto
anaishi bila mama, itakuwaje…najua huenda, ipo siku mmojawapo, atahitajia
kumbukumbu za mwenzake ama mtoto ama mama, ..nikaona nifungue kabrasha moja,
kwa ajili ya kumbukumbu za huyo mama na mtoto wake....’akasema
‘Lakini docta, hayo si yapo tu..lipo kabrasa lake la
kumbukumbu yapo mafaili kwa ajili ya
wagonjwa..’akasema nesi
‘Mhh, sio kama hizo kumbukumbu za kiutawala…hapana..nilichofanya
nikuchukua vipimo vyote vya huyo mtoto na mama yake, na maelezo yake…nilitaka
nijue zaidi historia yake..na kila kitu, hata picha yake..unajua, na kila kitu…,
ili vije kumsaidia huyo mtoto au mama yake huko baaadaye..’akasema dakitari.
‘Mhh, hata sijui umuhimu wake …naona dakitari wewe upo `too ambitions…’akasema nesi,
‘Mimi najua..hayo, nasoma vitabu vya hadithi, naangalia movie,
sisomi au kuangalia tu..naangalia na kati kat ya mistari..maisha katika
uhalisia wake… nimesoma na kusikia,…watoto waliokulia hivyo, wanavyohangaika
kutafuta wapi walipotokea, mara nyingi hakuna jinsi ya kuweka hizi kumbukumbu
za vizalia..na historia angalia kwa uchache…., hili ni kosa, kwa vile watu
wnafanya yale wanayoona yanawashibisha tu, hawafikirii kizazi kijacho…’akasema
‘Najua itafika muda utachoka tu…kwa nchi….wapo walikuwa hivyo, na
sasa wamejikalia tu…nina wasiwasi huo’akasema nesi.
‘Najua sana hilo, lakini kabla sijachoka niwe nimefanya jambo....’akasema
na kuangalia saa yake.
‘Sasa ni hivi…huyo mtoto huenda baadaye akataka kujua wazazi wake
ni nani,..na ni kitu gani kilitokea…unaona ilivyo,..mimi najaribu kujiweka sehemu
ya huyo mtoto na kujiuliza maswali kama hayo..na majibu yake nimeshawaweka
tayari… sasa ni vyema kumbukumbu kama hizo ziwepo mahali maalumu..’akasema
‘Sawa kweli..kama usemavyo..huenda akaja mmojawapo akaja kuzitafuta
lakini kwa hali ya nchi yetu ilivyo mmh, hata sijui…maana mtoto atakulia wapi,
maisha yenyewe yalivyo..au mzazi..mmh, wakitoka hapa wametoka, sijaona mtu
akija kuulizia kihivyo..labda tu akija hapa kakwama kuhusu angazo la uzazi kwa
ajili ya cheti cha kuzaliwa, lakini kudadisi, ilikuwaje…sijawahi kuona....’akasema
nesi.
‘Ndio hivyo, ndio maisha yetu yalivyo..lakini lazima mmoja afanye
jambo ili kueleta mabadiliko..lazima mmoja ajaribu kitu…Sasa mimi nimeanya
hivyo, kwanza kwa huyu mama, nimechukua kumbukumbu zote zake na kuzihifadhi
katika faili hilo hilo la mtoto…ni kitu tu kimenijia..na nimeona kwa vile hata
mimi nafanya kitu kama `project’…basin
a iwe hivyo’akatulia kwanza
‘Project ya nini..?’ akauliza nesi.
‘Ndio kama nilivyokuambia, nataka kusomea na maisha halisia,
napenda kuita saikolojia ya ndoa, ambayo inakwenda hadi kwenye uzazi,..na kila
kitu chake..unaonaeeh…’akasema na kuangalia saa tena.
‘Sasa nimeona pia nifungue mtandao maalumu kwa mambo hayo.., ukiingia kwenye komputa yangu utaona nimeweka
kumbukumbu nyingi tu, na huyu mama ipo pia….na nataka kulifuatilia hilo kwa
karibu sana..hata nikiondoka hapa najua wewe utanisaidia kunipa taarifa
zake..maana nimeshafungua `file endelevu’ maalumu kwa huyo mama na mtoto wake…’akasema
‘Mhh, na muda huo unao docta..naona utajichosha tu…maana mimi
nikitoka kazini mambo ya kazini nataka niyasahau kabisa…sasa nianze kukaa
kwenye komputa kuandika ..mmh, nakupa hongera…’akasema nesi
‘Nimekuambia tu wewe, kama itatokea, basi jaribu kukumbuka hivyo
kuwa kumbukumbu hizo unaweza kuzipata zilipo…, maana mimi nipo kwa muda tu
hapa…nimehifadhi hizo kumbukumbu kwenye
kabati namba 5, hili ni maalumu kwa kumbukumbu nyeti za kwetu kama madakitari,
sitarajii kuwa hap zitaharibiwa....’akasema dakitari kijana, akiwa sasa anageuka
kama kutaka kuondoka, lakini bado akawa kasimama hapo hapo.
Yule nesi mawazo yake kwa muda ule hayakuwepo hapo kabisa, alikuwa
akimuwaza sana huyo dakitari kijana, alikuwa akijaribu kuhisi jinsi
alivyojisikia pale alivyomkumbatia, na jinsi alivyo na ndoto zake ambazo,
aliomba aje kuishi naye ili wasaidiane, ziweze kutimia…, akawa anaombea kupata
mume wa namna hiyo….oh
‘Oh, jamani kama ingelikuwa hivyo kila siku ..niwe naye karibu
tu..tuongee hivi na ikiwezekana, tuwe mke na mume mmmh, labda anaogopa umri,
lakini, kiumri mbona hatujapitana,..yeye
kanidi kama mwaka au mika miwili…sina uhakika…..na ..sema kwa mwanaume ni lazima
yeye aonekane kijana zaidi….mmmh’akawa anajiongelesha kichwani kimawzo.
‘Mhh, jamani, kwanini hanikubalii niwe mpendwa wake, nifanyeje ili
anielewe..?’ akawa anazidi kujiuliza..akiwa kasahau kabisa kuwa bado yupo
matatizoni…
‘Umesema wazazi wako wanaweza kukusaidia..?’ akauliza huyo
dakitari sasa akigonga gonga kiatu sakafuni, kama anataka kuondoka, na nesi
akawa kimia, kwa vile bado alikuwa akiwaza mengine , na dakitari huyo akasema;
‘Lakini naomba unielewe kitu sister..usijipe mawazo sana…muhimu
kama ulivyosema,, kama unawaamini hawo ndugu wako kama ulivyosema, basi
wasiliana nao kwanza kwa simu..usije kumbeba mtoto hadi huko…ukakuta mengine..’akasema
‘Kiukweli mimi nisingelipenda kiumbe hicho kije kupata taabu…na
pia mimi ningeshauri hivi, ok, hata kama simu hazipatikani basi…wewe nenda moja
kwa moja kwa hao wazazi wako kaongee nao na kama wanahitaji kuandikisha kama
wazazi wa huyo mtoto, basi itakuwa ni vyema zaidi…
‘Mhh..ni kweli …yaani
ungelijua jinsi gani dada yangu anavyotafuta mtoto..hata wa kumlea, yaani kama
hivi aambiwe huyu sasa ni wako..sijui atafurahije…japokuwa kiukweli anataka
mtoto wake wa kuzaa..lakini bahati haijapafika kwao…sasa akipata huyu mtoto
..mmmh, sijui..’akasema nesi.
‘Na kama ni hivyo mimi naona hata kabla hujaondoka, basi wasiliana
na utawala watakusaidia kwa hilo kisheria..…, lakini mhh..sijajua sheria za
hapa hospitalii vyema,..kwahiyo…mmmh hilo la kummilikisha huyo mtoto moja kwa
moja, naona lisiende kwa haraka sana. Huwezi jua, mama akapatikana, huwezi jua..’akasema
‘Ina maana wewe watarajia kuondoka lini..?’ akauliza
‘Sijui…bado nasubiria kitu..’akasema.
‘Oh..poa…lakini ombi langu lipo pale pale, nahitaji kuongea na
wewe zaidi…ni ushauri tu…najua utanisaidia sana…’akasema nesi
‘Hamna shida…kama utaondoka leo mimi naona ni bora zaidi..ili
ukutane na hao ndugu zako..’ akasema dakitari kijana huku sasa akianza kutembea
kuondoka, akawa kama kakumbuka kitu
‘Kwani wewe ulikuwa unataka kuongea na mimi kuhusu nini, ni kuhusu
huyo mtoto au…au kuna jingine zaidi?’ akauliza dakitari...lakini kwa ule umbali
nesi hakusikia vyema, na docta akaona asipoteze muda, akafanya haraka kuondoka,
na wakati huo huo nesi akawa anaongea akijua dakitari badi yupo akasema;
‘Mh, mimi nakusikiliza wewe tu…na kuhusu hilo la mtoto mimi
nimekuelewa..docta, lakini..hata kama tunaweza kukuna kabla sijaondoka sio
mbaya, tukaongea zaidi, kama marafiki..’akasema nesi, na wakati anaongea akawa
kainama chini akichora chora na mguu, hakujua dakitari hayupo..lakini alijua
yupo kwani alihisi kuwepo kwa mtu. ..
‘Na kwani wewe watarajia kuondoka lini huko masomoni sijui wapi…mimi
kwenda kijijini, sijui nindoke kesho…eeh, kwani, wewe huwezi kufika
kwangu..tuongee au wasemaje kwa hilo…?’
alikuwa akongea akiwa kainamisha kichwa akichezesha mguu chini,..
Alipohisi ukimiya…hasikii sauti ya docta,… akainua kichwa, na kuangalia pale alipokuwa kasimama dakitari,
hakumona yeye na aliyekuwa kasimama hapo si mwingine..ni mkuu , bosi wake, nesi
mkuu…na uso wa kejeli ukiwa unemeta meta…..
WAZO LA LEO: Katika hali ya kimaisha wanadamu wote hatulingani, kuna
wengine wamejaliwa kuwa na kipato na cha ziada, na wengine wanakuwa hawana
kabisa, pia kuna matatizo yanatokea wengine hujikuta hawana jinsi ila kuomba, au
kukopa nk kwa hali ilivyo …
Kwa tamaa, kuna wengine
wanatumia fursa hiyo kupata ziada kwa hao wenye shida, wanatoza kitu kinachoitwa `riba’..anamkopesha
mwenzake akijua kabisa kakopa hiyo pesa kwa shida, ana matatizo makubwa,
…anamwambia ukirudisha unipe na ziada, `riba’…huyu kwa vile ana shida inabidi
akubali tu,…Huyu mtu hakopi kwa raha, kwa biashara,anakopa kwa matatizo wewe
unazidi kumlundikia matatizo, ..jamani huu sio uungwana..huu sio ubinadamu,
riba ni dhuluma…tukumbuke tutakuja kuhukumiwa kwa hilo !
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment