‘Mhh, ina maana huyo mama ni mtu gani, na
kwanini watu wachanganyikiwe wakimuangalia.au wakitaka kumuangalia sura yake…?
‘Lakini docta bingwa kaweza kumuhudumia na
ili kufanya hivyo yeye ilibidi kuiona sura yake, mbona hajachanganykiwa..?’
Hayo yalikuwa maswali ya nesi akitembea
kuelekea huko kwa docta aliyemuita ambaye ndiye anayeshughulika na huyo mama.
Tuendelee na kisa chetu
*************
‘Nesi mkuu tumekuita hapa, maana kuna kazi kubwa, sio kazi kubwa
sana kama tutazingatia taaluma yetu…’akasema docta mkuu wakiwa kwenye jopo
maalumu, ofisini kwa docta bingwa….
‘Huyu mama kaletwa hapa kwa matibabu, na kiujumla hatujui sana historia
yake, kwani waliomleta hapa hawakuweza kutuelezea vyema, walisema watarudi tena
lakini hawajawahi kufanya hivyo….kwanza mkumbuke walipomleta hapa, walimleta
kama maiti na haya ya kuwa mama huyu bado yupo hai, wamechukulia kama huyu mama
kafufuka..’akaanza kuelezea docta mkuu.
‘Mimi siku ile …nikiwa nakabidhiwa na mwenzangu…tulipata taarifa
kuwa kuna maiti imeletwa na mgonjwa mmoja….kwahiyo kama ni maiti
hatukuchukuliwa uharaka sana, tukawa tunatibia walwe wenye dharura…nilishawaambia
hilo.
‘Na kama mlivyosikia….’akasema na kucheka kidogo kuonyesha kuwa ni
kichekesho.
‘Nilipofika kumkagua huyo mama, badala ya maiti mimi nikakuta yupo hai…na muda huo alikuwepo mtu
mmoja ambaye nilijua ni ndugu yake, na nilipogeuka kumuangalia nikakuta huyo
mtu keshaondoka,..sijui ni kwasababu ya kuogopa maana kama walileta maiti, ..na
sasa mtu yupo hai, unajua tena,…’akasema docta.
‘Na kwa muda ule sikuwa na haja ya kufuatilia sana, nikijua ndugu
zake wapo…na zaidi ningelipata taarifa yoyote kutoka kwa hao askari waliomleta,
maana aliletwa na maaskari…’akaendelea kuongea docta.
‘Sasa huyu mama kama mnavyoona hataki kabisa kufunuliwa hiyo nguo
aliyojifunika usoni mimi nimetii matakwa na utashi wake, na ni emfanya hivyo
hivyo…mimi ili niweze kumtibia…nilimuomba samahani,… kuwa mimi ni docta bingwa,
na nina haki ya kumuangalia usoni kwa dharura kwa ajili ya kumtibia, ni hekima
ndogo tu kwa watu kama hao, wanaelewa….nilimuomba sana na kumuahidi kuwa
sitatoa siri yake..kama kuna siri kutokana na yaliyopo usoni mwake, au kama ni
kutokana na imani yake….’akasema docta.
‘Ilichukua muda kukubali….na nilipoanza kumfunua hakuleta
pingamizi nikafanya yale yanayostahiki, na nikamwambia wazi kuwa nitajitahidi
kutokusema yale ambayo hakutaka yaonekane kwa watu….kiufupi ni hivyo…na nyie
mnatakiwa kuyafahamu hivyo…ila kiukweli huyo mama kajeruhiwa usoni…kakatwa
katwa na mapanga, lakini yale majeraha hayakuingia ndani kugusa mfupa wa kichwa,
..ila yameharibu wajihi wa usoni…’akatulia
‘Sina uhakika sana kuwa mama huyu ..labda ni imani yake kufanya hivyo….na sijui
kwakweli kuwa hali hiyo alikuwa nayo toka zamani , au ameamua kujifunika hivyo
kutokana na majeraha aliyo nayo…’akasema docta
‘Toka zamani alikuwa akijunika hivyo..’akasema nesi na kumfanya
docta amgeukie nesi huyo kwa hamasa,
akasema;
‘Kwahiyo ni kweli wewe unamfahamu vyema huyu mama?’ akauliza
docta.
‘Kidogo…kuna kipindi nilikwenda huko kijijini nikakutana naye
akipita mabarabarani akiimba, ni hivyo tu kumfahamu kwangu na kipindi hicho ni
muda, kabla hata hajavamiwa na watu na kujeruhiwa hivyo…kwahiyo mimi sizani
kuwa anajifunika hivyo kwasababu ya kuharibiwa sura na mapanga…nahisi kuna
sababu nyingine…’akasema nesi.
‘Oh sasa kama unamfahamu japo kidogo tutapata nafuu…na je huenda
kama ulijaribu kumfuatilia..na kumjua zaidi…mimi ningelipenda kujua je huko
kijijini alikuwa akiishi na nani , au alikuwa kitembea tembea tu?’ akaulizwa
nesi.
‘Ina maana hamjaongea na polisi, akawaelezea ilivyo, nakumbuka
ulisema kuwa utaongea na polisi wanaochunguza hilo tukio….maana mimi kumjua
kwangu ndio huko kumuone akipita barabarani ….sijui zaidi docta’ akasema nesi
akijaribu kuficha ukweli .Hakutaka kujihusisha zaidi na huyo mama kutokana na
yanaoongewa na watu.
‘Hutaamini..yule askari aliyemleta huyo mama, nasikia naye anaumwa
sana, kichwa, halafu…nasikia kama kama kachanganyikiwa…na zaidi yule mwenzake ambaye
alikuwa ni dakitari wa kundi lao…kachanganyikiwa kabisa, …’akasema docta
akitabasamu kidogo.
‘Mhh imekuwa hayo..mbona balaaa..’akasema nesi mwingije aliyeitwa
kwenye hilo jopo.
‘Yaani ukihadithiwa ….hili tukio, sijalipaat vyema, lakini kidogo
nilichokipata utaona ni kitu cha ajabu..lakini..ni …hali halisi ya eneo
hilo..watu hawanielewi nikisema..haya mabangi, na ufinyu wa elimu…nah ii tabia
ya kuuana uana, damu za watu zanamwagwa tu kiholela…unajua kitaalamu yana
atahari zake…sasa huyo askari mwingine imebidi wamrudishe kijijini kwao
wakashughulikie kienyeji…sijui....’akasema docta.
‘Mungu wangu kwanini…ni kwasababu ya huyu mama?’ akauliza nesi.
‘Sizani,….mimi sina uhakika sana kuwa ni kwasababu ya huyo mama,…huyu
mama kwa vile imeangukia kwake, anachukuliw akama kigezo,…na unajua mwanadamu
akishindwa hoja…akawa hana njia nyingine atatafuta upenyo tu..hata kama ni kwa
kusingizia..ilimradi afanikiwe kile anachokitaka…sasa huyu mama wanamtumia tu… kwani huyu mama ana nini cha kuwafanya wao
wachanganyikiwe..?’ akauliza docta.
‘Si wanasema hataki watu wamuangalia usoni…’akasema nesi.
‘Unajau kuna kitu tukiangalie kwa makini,..ni kweli kuna imani na
kuna utashi wa mtu…kila mwanadamua na utashi wake, mimi naweza kusema sitaki
miguu yangu ionekane, nikawa najifunika hivyo…haitakiwi mtu kuja kuniingilia, …sasa
ingia ndani kabisa kwenye imani za watu ambazo zinagusa hisia ya ndani…,’akasema
docta.
‘Lakini kwa huyo mama…docta sizani kama anafanya hivyo kwa
iamni..kachanganyikiwa tu..’akasema nesi.
‘Una uhakika…?’ akauliza docta na kabla hajajibiwa akasema;
‘Kiukweli kuna watu wana imani zao…hawataki kuangaliwa baadhi ya
sehemu za miili yao, kwao ni aibu..ni fedheha, ni dhambi… na imani hizo zikakita
ndani kabisa ya miyo yao… sio kwa unafiki, anafanya vile kwa dhamira moja…ukimlazimisha
mtu kama huyo..lolote linaweza kukutokea....tunatakiwa tuheshimu utashi wao….’akasema
docta.
‘Lakini docta twende mbele na kurudi nyuma, maana wewe mwenyewe
kila siku unasema kwanza vipimo, mengine baadaye, lakini kauli yako hiyo
inapinga msimamo wako..sasa huyu mama kaja hapa kutibiwa, ina maana tusimfunua
tumkatibia,….hata hapa hospitalini?’ akauliza nesi.
‘Inategemea….. je kweli unataka kumtibia au kumuangalia…maana hata
sisi na utaalamu weu bado tuna madhaifu ya kibiandamu, lengo linaweza lisiwe
kumtibia…je ni kweli lengo letu lilikuwa hivyo….?’ akauliza docta.
‘Docta kwani sisi hapa tunafanya nini,…tumeajiriwa kufanya
tiba..na ili tufanya kazi yetu vyema, wagonjwa wnastahiki kujiweka wazi, ikiwa
ni pamoja na mauongo yao yale yanayostahiki kutibiwa… tunataka kutibia ndio
maana tunamwambia ajifunue..’akasema nesi.
‘Je ni kweli…kuwa nia yako ni hiyo tu..?’ akauliza docta.
‘Docta hata sikuelewi….ina maana unaamini kuwa sisi nia yetu ni kumuangalia
tu….sawa basi wewe unayeoona hilo utamtibia mwenyewe..’akasema nesi akionyesha
kukerwa.
‘Mimi najaribu kuingia kwenye kichwa cha huyo mama, na kujaribu
kuona kwanini hataki kuwaruhusu watu wengine, hata sisi ambao tunawajibu wa
kuanya hivyo…sio kwamba nawaona kuwa hamfai au mna malengo mengine…najaribu
kuona …msimamo wa huyo mama,….anyway….sasa
hebu niambie wewe nesi mkuu wewe ulisikia nini kuhusu huyu mama?’ akaulizwa
nesi mkuu.
‘Kusikia nini..docta mimi nimekuambia kuwa nilimuona tu njiani..’akasema
nesi na kama kashtuka jambo akatulia.
‘Nasikia kuna watu walikuja kutaka kumuona na …ni ndugu zako au
nimekosea?’ akauliza docta na nesi akakumbuka kuwa kumbe kuna ndugu zake
walifika na huenda walishaongea na waliokutana nao na wakajitambulisha kama ni
ndugu zake, na taarifa zimeshafika kwa huyo docta…, akaona hana ujanja akasema;
‘Mhh, ni kweli, kuna ile siku walikuja ndugu zangu, ndugu zangu
walibahatiska kuishi na huyu mama , kama kumsaidia, mimi nilikuwa siyajui hayo
kuwa huyo mama alikuaj akaishi na ndugu zangu hao…wanasema ni kweli huyu mama
hapendi kufunuliwa usoni, kama alivyojifunika na kila aliyejaribu kufanya
hivyo, bila ridhaa yake yanamkuta makubwa..kuchanganyikiwa na kitu kama
hicho….’akasema nesi
‘Na hata wao hawajawahi kumuona sura yake..mhh yawezekana kweli,
mtu muishi pamoja kwa muda..isitokee hata mara moja?’ akauliza docta mwingine.
‘Hawajawahi kumuona kabisa…hata wao wenyewe hawakuwahi kumuona sura yake yaani ndivyo ilivyo....’akasema
huyo nesi
‘Je hao waliowahi kumuona au kutaka kumuona ndio hao
wanaochanganyikiwa..?’ akauliza huyo docta mwingine, na kabla hajajibiwa docta
bingwa akasema.
‘Mbona mimi sijachanganyikiwa, na nimemuona…mimi naona tusiweke
hoja hiyo au ulitaka kusema nini docta?’ akauliza docta bingwa
‘Mimi naona ni kwasababu kakubali wewe ufanye hivyo,na kwa vile
wewe ni docta bingwa akaona hana jinsi, na kwa vile anahitajia matibabu…’akasema
nesi
‘Mhh…umeona eeh, kwa vile kaona kuwa nia yangu ni njema kwake…’akasema
docta bingwa.
‘Unajua mambo mengi hayaingilii akilini…sasa tufanyeje..maana kama
ilivyo huyo mama hataki mtu mwingine kumuhudumia hadi zaidi yako wewe,..na wewe
una safari, sas auanondoka unafikiri
atakubalia nani mwingine amuangalia,..amtibie hayo majeraha….’akasema docta
mwingine.
‘Kiukweli kwa hivi sasa ilivyo huko usoni hakuhitaji matibabu ya zaidi…vile
vidonda vimeshajifunga..ila …anahitaji utaratibu mnzuri tu…mimi naona tiini
utashi wake, msije mkapatwa na mengine mkasingizia kuwa ni huyo mama..maana
naona mioyo ya ya wengi hapa imeshaathirika kwa wasiwasi..’akasema huyo docta.
‘Kwani yupoje,..si mwanadamu kama sisi…?’ akuliza nesi mwingine
aliyekuwepo hapo.
‘Mhh,..ni binadamu, aminini hivyo hana tofauti…msije mkazua ya
kuzua, mimi ninachowaomba ni kuwa huyo mama, anahitajia utulivu…anahitajia
ushauri…na taratibu atapona...huko baadaye, …kwa hali aliyo nayo,..japokuwa sikuweza
kumshona..kwani majeraha yalishajifunga….kiujumla uso wake umeharibika…waliyomfanyia
hivyo sio watu wema…wamehakikisha uso unakatwa katwa na mapanga….aah, lakini
hana shida sana…’akasema docta.
‘Kwahiyo unataka kusema nini..?’ akauliza nesi mkuu akiwa na wasi
wasi.
‘Unajua.niliposikia kuwa kuna ndugu zako walikuja kumuona huyu
mgonjwa, nilitaka kujua kama unamfahamu zaidi..hata hivyo mimi napendekeza kuwa
ufuatilie kujua huyu mama ni nani, na….ili tuweze kupata historia yake, maana
tukianza matibabu yake ya akili…ndio sehemu yetu ya pili itafuata huko…,
tunatakiwa kujua historia yake kwa ujumla,….inavyoonekana kaathirika kisaikolojia,..lakini sizani kama ana …mtindio
wa ubongo ..hapana hilo…ok, tutaona huko baadaye.., …’akasema docta bingwa
‘Mhh, docta kwahiyo unataka mimi nifanye nini….maana nona huo ni
mtihani kwangu…’akauliza nesi
‘Mtihani gani?’ akauliza docta msaidizi.
‘Kwanza..ukiangalia hayo yaliyowakuta wengine ni sababu hizo hizo
za kutaka kumchimba huyo mama…kumfunua na kuona yupoje…’akasema
‘Mhh..nia yetu iwe njema, sio kumchimba,..au kumfunua kutokana na
hizo tetesi… bali tufanye hivyo tukiwa nalengo jema la kumtibia…hilo liwe akilini
kwenu, mkiwa hivyo, ..tutaweza kumsaidia huyu mama..huyu mama ana matatizo
makubwa..angalia walivyomfanya, hivi wewe ufanyiwe hivyo, bado uzingiziwe mambo
yasiyostahiki..kiukweli utaathirika kisaikolojia utaona kama hutakiw hapao
duniani..hasa kwa akina mama, ambao wengi miyo yao, haina utahabiti wa
kuhimili..….’akasema docta.
‘Unajua docta hata ndugu zangu waliokuwa wakiishi naye wameshaanza
kuogopa…maana watu wamechoma hadi nyumba ya ndugu zangu kwa ajili ya huyu mama,
watu hao waliofanya hivyo wanadai huyu mama ni mchawi…’akasema nesi.
‘Je na wewe unaamini hivyo..au na hao ndugu zako wanaamini hivy,
waliwahi kuona dalili kama hizo za kiuchawi…?’ akauliza docta
‘Hapana docta..mimi siamini hao kuwa mama kama huyu anawezaje kuwa
mchawi, hata ndugu zangu hawaamini hivyo…..isitoshe kumbe huyu mama alikuwa
akiwasidia watu kuwa..tibia matatizo ya watoto wao…wema wake huo haukuangaliwa,
waliona kama anafaiadi…nahisi hivyo wakaona wamuharibie…’akasema nesi
‘Kuwatibia kwa vipi?’ akauliza docta akimuangalia huyo nesi
machoni, na huyo nesi akawa kama kainama …kuonyesha anaongea na bosi wake,
akasema;
‘Wanasema huyu mama ana karama…mtoto akiwa analia…au anaweweseka…na
vitu kama hivyo huyu mama akimuwekea mkono wake kwenye hicho kichwa cha mtoto,
ananyamaza na yale matatizo yanakwisha..’akasema nesi
‘Hahahaha…mmmh,..unjajua hata mimi nimewahi kusikia kuwa kuna watu
wenye karama kama hizo, sikatai…lakini jinsi gani ya kuthibitisha hayo kitaalamu
ni ngumu kidogo..sisi kama docta tunasimamia kwenye vipimo..sikatai kuwa hayo
hayapo yapo..mimi na ani yangu hii nimekutana nayo nayafahamu,…lakini…..’akasema
docta na kusita kumalizia.
‘Aaah, docta sio kwamba nimeyaona hayo kwa macho yangu au
kuyaamini, ila mimi nasema wanavyodai watu wa huko kijijini waliwahi kumuona….sio
mimi docta..’akasema nesi na docta akamuangalia kukatulia kidogo na docta
akasema;
‘Sasa tufanyeje…?’ akauliza akigeuka kumuangalia msaidizi wake,
halafu akasgeuka kumuangalai nesi akasema;
‘Mmmh, hebu nikuulize,..lini hao ndugu zako watakuja tena
kumtembelea mgonjwa…, maana mimi sitakuwepo kesho, au kesho kutwa, ..ina maana
hiyo kazi nakuachia wewe na..docta …eeeh….,wakija muwahoji , muongee nao, mjue
histora ya huyo mama vyema… ‘akasema huyo docta akimgeukiwa docta mwenzake.
‘Sawa..’akasema docta mwenzake akitikisa kichwa kukubali.
‘Japokuwa kama mnavyoona tatizo la huyu mama ni kuwa hataki mtu
mwingine hata docta mwenzangu hapa alikataliwa kumfunua uso wake…unaona
ilivyo…sasa..anyway..kama kutakuwa na
dharura mtajua la kufanya..’akasema
huyo docta bingwa
‘Sawa docta, lakini..huo sasa ni mtihani…sijui kwa dcta yeye
atajua la kufanya lkini mimi mmmmh, nahisi huo ni mtihani…’akasema nesi.
‘Yah..ni mtihani….lakini ndio kazi zetu zilivyo…wakati mwingine
changamoto kama hizi hutokea, na inabidi kutafuta njia ya kupambana nazo…ila
msimlazimishe kama hataki jambo fulani lifanyike…hilo nataka nilifanyie kazi
mwenyewe nikirudi….nina imani kuna jambo kwa huyo mama..anahitajia uchunguzi wa
tarataibu …nitaona nikirudi…..’akasema huyo docta na wakatawanyika, na nesi
akataka kupitia kue alipo huyo mama kumuangalia tena, akiwa na mengi ya
kujiuliza
**********
Matibabu ya yule mama yaliendelea,..kuna muda alikuwa akazidiwa
hadi kupoteza fahamu inakuwa akzi ya kukimbizan huku na kule..lakini hali hiyo
ikaanza kupungua..ikabakia ile hali a kushituka shituka na kutaka kukimbi,a na
hiyo hali nayo ikaanza kupungua kidogo kidogo…
Mama huyu akaanza kuwa nah alia yenye mategemei na akaanza kuinuka na siku hiyo alipoweza
kuinuka, alikuwa kazungukwa na madakitari, wakikabidhiana, yeye aliinuka kama
kawaida na alipotizama ile hali ya watu kumzunguka, alitulia kwa muda akawa
kama anashngaa anaangalia huku na kule…na mara akakurupuka, na kuanza kukimbia,
…
Siku hiyo ikawa mshike mshike tena, na madakitari kwa utaalamu wao
wakamuweka sawa, nafikiri kukimbio huko kulitokana na hio tukio la kupigwa na
kukatwa mapanga, kwahiyo bado alikuwa akihisi watu hao waliomzunguka wanataka
kumfanyio hivyo tena! Lakini baadaye hiyo hali ilitulia.
Siku ya pili yake akawa na
nafuu, na akaweza kuinuka na kwenda kujisaidia mwenyewe, ila akiwa katika
uangalizi wa karibukaribu. Na siku hiyo mdogo wa dada mtu akawa yupo zamu, na
alipofika kwa huyu mama akaanza kumuulizia hali yake. Yule mama alikuwa akijibu
kimkatomkato, hakuwa anaongea sana, na maswali mengine akiulizwa alikuwa
akishangaa, hata jina alikuwa hajui kuwa yeye ni nani…
‘Naomba uondoe hiyo nguo uliojifunika usoni, kwani huko kwenye uso
kuna majeraha, yanahitaji hewa na kusafishwa…’ akamuomba yule mama
ajifunue. Dakitari wake alikuwa akimsafisha
kwa siri hakuna aliyetakiwa kuwa karibu naye na nesi alikuwa akijaribu
kumshawishi ili abadilike….
Yule mama alipoambiwa hivyo kuwa aondoe ile nguo aliyjifunika nayo
kichwani na usoni, akaangalia huku na kule, alisita kujifunua akabakia kimiaya
hakusema kitu au kufanya lolote, na nesi akaona hakuna haja ya kumlazimisha
akaangalia yale yanayofaa kuangaliwa halafu akataka kuondoka.
‘Mtoto wangu yupo wapi..?’ nesi akasikia sauti kutoka kwa huy
mama, akageuka kumuangalia, halafu akasema
‘Mtoto gani unayemtaka, ..?’ akauliza
‘Nataka mtoto wangu..’akasema huyo mama
Yule nesi alimwangalia….akawa anawaza amuambia nini huyo mama,
akilini alikuwa akiwaza meng, hasa aliposikia kuwa askari waliofika kufanya
uchunguzi siku ho ya tukio wamekabailiwa an magonjwa yasiyofahamika, kisa watu
wanasema walilazimisha kutaka kuuangalai huyo mama uso wake..shemeji ake naye
kawa kama mtualiyechanganyikia, anaongea peke yake…
‘Kwanini unawatesa watu?’ akasema huyo nesi bila kufikiria kauli
yake hiyo na huyo mama akawa kimia tu.
‘Watu wote waiojaribu kukutizama au kuataka kukutizama usoni
wamechanganyikiwa, …ina maana gani, kuwa wewe hutakiwi kuangaliwa uso wako, au …’akasema
na kukatiza kile alichotaka kukisema.
‘Mimi mwenyewe sijui uso wangu upoje…kwanini watu wengine watke
kuuangalia…mimi sijui waulize waliotaka niwe hivyo…’huyo mama akasema
‘Akina nani…?’ akamuuliza
‘Sijui…’akasema
‘Kwani wewe umetokea wapi?’ akamuuliza
‘Sijui..labda mbinguni, kwanini wewe unajua umetokea wapi?’
akauliza huyo mama, na naesi akawa kimia
‘Ina maana hata mimi nikitaka kukuangalia kwa nguvu,
nitachanganyikiwa?’ akamuuliza.
‘Hivi na mimi nikitaka kukufunua ukabakia uchi nikuangalia
utakubali?’ akauliza huyo mama.
‘Lakini tunachotaka kukuangalia ni uso wako..sio sehemu nyingine ya
mwili..’akasema.
‘Na mimi nataka kuakuangalia uchi wako sio sehemu nyingine ya
mwili..’akasema huyo mama, na nesi kwanza akawa kama kashituka kwa ile
kauli,..akatulia huku akiwazia ile kauli…halafu akageuka kuondoka na kabla
hajainua hatua ya tatu, mara sauti ya yule mama ikasikika ikisema kwa hasira;
‘Umenisikia,nataka mtoto wangu…’ilikuwa sauti kali ya kuonyesha
kukasirika, na nesi akahisi uwoga, hakutaka hata kugeuka kumuangalua yule mama,
alihis kama yupo nyuma kwake anataka kumzuru…, akakimbia kuelekea ofisi ya dakitari wake ,
WAZO LA LEO: Tuheshimuni utashi na imani za watu
wengine..kuna watu kutokana na imani zao, wana taratibu zao za maisha, iwe ni
mavazi..kufanya ibada, au vyakula na jinsi gani ya kuishi …kutokana na imani
zai wanafahamu zaidi kwanini wanafanya hivyo, …wewe kama unaona wanavyofanya
hivyo sio sahihi,..au kutokana na imani zako inakizana na imani hizo…usiwe
kikwazo kwako ukazuia…, muhimu ni kujenga uvumilivu, na kuheshimu imani hizo
ili kuwe na mahusiano mema. Tabia ya kuzarau imani nyingine na kubeza, ndio
chanzo cha mifarakano kwenye jamii, kama kuna mijadala ya kufahamu kwanini,…au
kutangaza imani kwa kulinganisha basi ifanyeni kiuungwana na kwa hekima.
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment