‘Kuna nini tena huko ndani, mliambiwa
hamuhusiki sasa mnakimbia nini..?’ akauliza baba mwenye nyumba naye akijaribu
kutafuta upenyo wa kuona ni nini kinachotkea huko ndani, walipo polisi na huyo
mama wanayemchunguza
Mara mmoja wapo aliyekuwa pale mlangoni,
ndani akatokeza na kumwambia baba mwenyenyumba;
‘Huko ndani naona hakukaliki, ...mimi
naona nijiondokee zangu..’akasema
‘Kwani wewe umeona nini?’ akauliza baba
mwenye nyumba
‘Hata sikuona vyema, maana nilipopata
upenyo wakuangalia...nikamuona askari mmoja yupo chini, na mwenzake anataka
kukimbia…’akasema na mwingine akadakia.
‘Asari anakimbia....! hapana, sio kweli,
labda hukuona vyema, mimi nasikia askari hawaogopi uchawi..’akasema mtu
mwingine.
‘Kwani ilikuwaje?’ akauliza baba mwenye
nyumba
‘Ohh, kweli yule mama hatakiwi kufungulia,
hata akiwa mfu …hutaamini yule askari aliyekuwa akimfunua kala
mwereka,..kadondoka chini na mwenzake ....mimi nimeona kwa macho yangu
mwenyewe...’akatokea mwingine akiongea huku akionyesha hamasa.
‘Yule askari aliyekuwa akitoa amri, kuona
mwenzake kala mwereka...akageuka kukimbia..’akasema huyo aliyetokea ndani.
Baada ya huyo mtu kusema hivyo, kila mtu
akakimbilia pale mlangoni kutizama ndani, na wale waliokuwepo ndani ambao
walikaidi amri ya askari kuwa wasiingie ndani lakini baadaye wakaingia kwa uchu
wa kujua kinachoendelea, wakawa sasa wanataka kutoka nje, wakionyesha wasiwasi,
na kwa hali hiyo ikawa sasa ni mgongano pale mlangoni, wanaotaa kutoka, na
wanatotaka kuingia kuona kilichotokea.
‘Tupisheni tupite…hili sasa ni
balaa..’wakawa wanasema waliokuwepo huko ndani
‘Kwani kumetokea nini?’ wakauliza
waliokuwepo nje, na baba mwenye nyumba ambaye pale aliposimama hakuweza kuone
vyema, akawa anahangaika kuchungulia lakini hakuona kinachotokea zaidi ya
askari mmoja kuwa yupo sakafuni, na mwenzake akiwa kasimama huku akiwa
anaangalia pale alipolazwa huyo mama.
Haikupita muda akatokea mjumbe mlangoni,
mjumbe alikuwa ndani na sasa anataka kutoka nje, na wale waliokuwepo nje
walipomuona mjumbe wakaona ndiyo nafasi yao ya kujua kilichotokea huko ndani,
wakambana kwa maswali;
‘Ehee mjumbe wewe umetokea ndani, kwanza
tuambie kwanini unatoka mbio mbo kama unakimbia...?’ akauliza mtu mmoja
‘Mjumbe tuambie kumetoeka nini huko ndani
mbona watu wanakimbia kutoka nje..?’ akauliza mtu mwingine
‘Ohooo, sina muda wa kujibu maswali yenu,
kwanza niacheni nipite,..mimi niliwaambia hawakutaka kunisikia...yule mama sio
wa kawaida, wakaona mimi ni naamini ushirikina...sasa unaona....wenyewe
wamathibitisha..’akasema
‘Eheee..ona eeeh, sasa mjumbe tupe picha
kamili....imetokea nini....maana haya mambo uyaone mwenyewe..’akasema mtu
wmingine.
‘Hawakutaka kuamini yamekuwa kama yale
yale .....ya hao walioambiwa hakutaak kusikia,..., nasikia hata hao washukiwawa
humo moto japokuwa jawajakamatwa… hali zao ni mbaya…wanaweweseka ovyo…’akasema
mjumbe na aligeuka upande wa pili akamuona baba mwenye nyumba akashituka na
kugeuka upande mwingine akitafuta sehemu ya kupita, huku jamaa mmpja akiendelea
kumhoji mjumbe
‘Ina maana unawafahamu hao watu
mjumbe..hao washukiwa wa moto, kumbe kweli kuna watu walifanya hujuma, mjumbe
unawafahamu ni akina nani?’ akaulizwa
‘Hapana nimesikia watu wakisema tu..oh,
jamani niacheni maana nina haja….nataka kwenda haja…nipisheni jamani,
waliyoyataka wameyapata…nipisheni nitawakojolea..’akasema mjumbe huku
akiharakisha kutoka nje, na alipopata upenyo, mbio akatokomea upande wa pili
ambapo haonekani.
Tuendeele na kisa chetu
‘Ina maana ni kweli kuwa kuna hujuma zilifanyika, na mjumbe
anafahamu hili,…wamechoma nyumba yangu kwa …aaah, …hapana ?’ alikuwa baba
mwenye nyumba ambaye aliweza kumsikia mjumbe pale aliposema;
‘’….nasikia hata hao washukiwawa huo moto
japokuwa hawajakamatwa… baadhi yao hali zao ni mbaya sana…wanaweweseka ovyo…’’
Na jinsi alivyoshituka alipomuona baba mwenye nyumba inaonyesha
dhahiri alitaka kuongea mengi, ila alikatisha tu alipomuona baba mwenye nyumba,..
Baba mweny nyumba akageuka kuangalia upande ule alipoelekea huyo
mjumbe hakumuona, …alishatokomea upande wa pili wa nyumba, ambapo hakuna choo,
sasa sijui alikuwa anakwenda haja ipi, yaonyesha kabisa mjumbe alikuwa na nia
ya kuondoka hapo.
Baba mwenye nyumba akaamua kumfuata , akijia huenda atamkuta hapo
nje, au au kama kaamua kuondoka atamkuta akiwa hajafika mbali, ..akatafuta
upenyo na kutoka nje, akaangalia huku na kule hakuona dalili za mjumbe,
akajaribu kuwauliza watu walikuwa wanakuja hapo kama walimuona mjumbe, na watu
hao wakasema hawajamuona.
‘Atakuwa kaenda wapi..?’ akajiuliza na alipohakikisha kuwa kweli
mjumbe keshakimbia, hayupo sehemu ya kuonekana akaamua kurudi ndani tu.
Akilini mwake, hata yeye alishahisi huenda moto huo si wa ajali,
lakini hakutaka kuweka tetesi za uvumi kichwani mwake, akajipa moyo kuwa
akikutana na mjumbe atamdadisi ili ajue vyema, akakumbuka jinsi mke wake
alivyoongea walipokutana baada ya kutoka kule kwenye jengo lililoungua….
‘Mume wangu una hatari kweli, sasa ni nini kilikupeleka huko, na
hali moto bado ulikuwa haujazimika vyema..angalia ulivyounguza hiyo shati…na
mbona una damu..?’ mkewe akamuuliza na alipogundua hilo, akakimilia ndani na
kubadili shati, akatoka na kukutanana mkewe.
‘Mke wangu sasa tutafanyaje,…maana sasa huu ni msiba na upo haa[a
nyumbani, inabidi utoe akiba yao, kuwahudumia watu…’akasema mume mtu.
‘Kwani wanasemaje,..ulihahakikisha wewe mwenyewe kuwa amekufa..?’
akauliza mkewe.
‘Ina maana hmjaamini kuwa kafariki…nimemshuhudia mwenyewe akikata
roho..muhimu kwa sasa ni kuona tutajipangaje…tukijua huu msiba ni wa hapa,
labda watokee ndugu zake…’akasema mume mtu.
‘Haya sisi tunawasikiliza nyie.. ujue pamoja na yote huenda huyu
mtu ana ndugu zake, hatuwezi kutangaza msiba huo kama wetu, wakati ndugu zake
wapo..inabidi kuangazwe kama kuna mtu anamfahamu, au ana tetesi zozote wapo
anapotokea..’akasema mke wake.
‘Tumekaa naye hapa, hakuwahi kusema ana ndugu, hajui ..na sina
uhakika kama anaficha…mimi nahisi hataki au hakuwa anaelewana na ndugu zake…sina
uhakika..’akasema mume wake.
‘Yote hayo hayatasaidia kitu…mimi naona tujipange tu, kuwa msiba
ni wetu…’akasema mama mwenye nyumba.
‘Basi ngoja niongee na mjumbe nitarudi baadaye, tatizo mjumbe yupo
na askari, wanamuhoji,..’akasema
‘Lakini mumewangu kuna kitu nataka kukuambia…’akasema na kumshika
mume wake, wakasogea mbali kabsa na watu, akasema;
‘Mume wangu unasikia watu wanavyosema..eti moto huu umewashwa na
watu wakikusudia kumuua huyo mama, wanadai huyo mama ni mchawi, kwahiyo watu wakaamua
wamchome moto…’akasema mke wake.
‘Maneno hayo umeyasikia kutoka kwanani, usiwasikilize watu, najua
yatasemwa mengi ..sisi kwa hivi sasa tuchukulie ni ajali tu…maana tukitaka
kudadisi sana, tutazidi kuumia, na hasara tumeshapata hata aikijulikana kuwa
kuna watu wamefanya hivyo, unafiri tutajengewa, hiyo imekula kwetu....’akasema
mume wake.
‘Mimi nakuambia nilivyosikia kwa watu,..hata mimi sikutaka kuamini
mambo yao, lakini kuna wanawake watatu wanasema waliona kwa macho yao wakiwa
wametokea mjini …’akasema
‘Wanawake gani hao, na wameonaje?’ akauliza mume mtu akiwa na
hamasa, mke mtu akageuka huku na kule kuhakikisha hakuna mtu anayewaona au
kuwasikiliza wanachoongea, alipoona kuna uhakika wa kutokusikiwa akasema;
‘Mume wangu…hao akina mama ni wenyeji wa hapa,..ni mabinti
wanaofanya akzi mjini, mimi naona wewe huna haja ya kuwajua,maana wanawake
wenyewe hawajatulia, ukikutana nao, nikujuavyo..mmh,...’akasema
‘Mke wangu ina maana huniamini, hilo limetokea wapi tena,..yaani
bado tu..aah, kama mambo yenyewe ni hayo haina haja ya kuniambia, wewe rudi kwa
akina mama muendelee na mipangilio….’akasema mume mtu.
‘S.ilaio kwambasikuamini….ila sizipendi tabia zao , nilishawahi
kuongea nao…sasa wao wakati wanatokea mjini, wakati wanapita, wakaona kundi la
vijana,…kama watano hivi au zaidi, ilikuwa ni usikuwa giza..hakuna mbalamwezi,…walimuona
mmojawapo akiwa na galoni , hizi za mafuta ya taa..’akasema.
‘Hao wanawake usiku wote huo walikuwa wanatokea wapi?’ akauliza
mume mtu.
‘Hao wanawake wanafanya kazi mjini, inavyoonekana walikuwa
wamekuja likizo, wao walisema, gari lao liliharibika walipofika maeneo ya huku
kwetu ni mbali …, walisubiria sana gari hilo litengenezwe, lakini halikutengemaa,
ikabidi waanza kutafuta njia za kufika huku, kwa mgu ni mbali sana,…wakahangaika
mpaka kukatokea gari moja ndipo wakaweza kuletwa hadi hapo njia panda, na
wakawa wanatembea kwenda majumbani mwao..
‘Sasa walipofika eneo karibu na nyumbani kwetu, kwanza wakahisi
harufu ya petrol, wakawa wanaulizana, harufu hiyo imetokea wapi…mara wakawaona
watu wakitembea kuzunguka eneo la nyumba yetu..wakasikia mmoja akisema;.
‘Lazima yupo humo ndani…hakuan sehemu nyingine ya kutokea..’mmojawao
akasema, na ara wakaonekana hao mabinti, na hakukuwa na njia nyingine ya
kujificha
‘Wanadai kuwa wale vijana walipowaona hao mabinti wakaanza kuwakimbiza
hao wasichana,hao wasichana wakatimua mbio, kila mmoja kivyake…walikimbizwa
hadi wakafika mbali na baadaye hao vijana wakarudi, inaonekana hawakutaka
kuendelea kuwafukuza hao wasicahana. Baadaye wale wasichana wakakutana na
kwenda kulala sehemu moja kwa mmoja wao.
Wale vijana wakarudi wakijua wana kazi ya kufanya..’akasema
‘Kwahiyo hawakuthibitisha kwa kuona huo moto ukiwashwa na hao vijana
…?’ akauliza mume mtu.
‘Hilo hawakuthibitisha, ila waliona hao vijana wakiwa na
galoni,..na harufu ilisikika wazi kuwa ni ya petrol , kwahiyo hiyo harufu
ilikuwa na maana gani, ina maana walishamwaga hiyo petrol..’akasema.
‘Walimwaga wapi, nani aliwaona wakimwaga..polisi watakuhoji sana
ukitoe taarifa za tetesi…je waliona dalili kuwa petrol hiyo ilimwagwa wapi?’
akauliza mume mtu.
‘Ina maana hunielewi,..hao wasichana hawakuona maana wao walipofika
hapo, na kuonekana tu, walikimbizwa..na walisikia hiyo harufu wakati wanapita
wakawa wanaulizana kuhusu hiyo harufu ndipo wakawaona hao vijana mmoja akiwa na
galoni..sasa wangejuaje hiyo petrol ilimwagwa wapi..’akasema mama mwenye nyumba
‘Kwahiyo kwa kifupi ni kuwa hawakuona wapi wapomwaga hiyo petrol,
na hawakuona moto ukiwashwa...ila walihisi harufu tu…na kuwaona hao vijana…hawa
ushahidi kuwa ndio wao waliwasha huo moto…’akasema.
‘Ndio hivyo….’akasema mke mtu
‘Huo ushahidi hautoshi mahakamani....maana hao vijana wakikamatwa
watadai kuwa kweli walikuwa na galoni ya petrol, na huenda hiyo petrol ilimwagika
kwa bahati mbaya wakati wanakwenda kwenye shughulizi zao..je hao wasichana
hawawezi kuongea na polisi?’ akaulizwa.
‘Hao wasichana hawapo, ..’akasema mke mtu
‘Hawapo! si umesema walitokea mjini, wamekuja likizo au
kuwatembelea ndugu zao au sio..sasa iweje waondoke haraka kihivyo? Akauliza
baba mwenye nyumba
‘Ndivyo ilivyokuwa,…kuwa wamekuja likizo, au mapumziko ya siku
kadhaa,… lakini wanadai walipata taarifa usiku huo huko, taarifa za vitisho
kuwa wakionekana hapa kijijini watauwawa, kwahiyo asubuhi na mapema, wakaondoka
kwa haraka na hawajulikani kama wamerudi mjini au wameelekea wapi, wanawake
wenyewe hawajatulia…’akasema.
‘Sasa wewe nani kakupa hizo taarifa..ni isiwe na wao wanahusika
ndio maana wamekimbia?’ akaulizwa.
‘Unajua masikio hayana pazia, wakati nipo kwenye mihangaiko ya
kuangalia watu wakae vipi, nikawafuma akina hao akina mama wawili wakiongea..mama
mmoja ni mama wa kati ya hao mabinti…’akasema
‘Ehee ukamuuliza?’ akauliza baba mwenye nyumba
‘Mama huyo hakukubali kuniambia ukweli….’akasema
‘Sasa yote hayo uliyapataje…?’ akaulizwa
‘Niliwasikia wakiongea na shiga yake , hawakujua kuwa mimi nipo
nyuma yao ….’akasema
‘Kwahiyo wewe uliwasikia wakiongea nini haswa kitakachosaidia…?’
akaulizwa
‘Kama hivyo nilivyokuambia kuwa hao wasichana walitokea mjini,
wakafika eneo hilo, wakasikia harufu, wakakimizwa…..huyo mama mmoja ndio
alikuwa akimsimulia mwenzake, na waliponiona wakanyamaza,na yule aliyekuwa
akimuhadithia mwenzake akawa anaondoka, nikaona nimfuate kumuulizia, nikamfuatilia
hadi nje, …, nikamuuliza, akakataa kata kata kuniambia ukweli, akasema yeye
hajui lolote…’akasema.
‘Haya mambo sitaki kuyakuza sana maana kama ni hasara tumeshapata
, muhimu ni kutoa ushirikiano na polisi ikibidi…nasema ikibidi, …lakini
tusiongee lolote kuhusu fununu au kusikia, hayo wao wenyewe watajua jinsi gani
ya kufanya, ukijianya unajua sana, siji umesikia, utaingia matatani...’akasema
mume mtu.
‘Mume wangu, mimi nawaogopa sana polisi maana wakianza kukuhoji
unaweza kujikuta umetegewa, ukaongea hata yale uliyokuw a hukukusudia
kuwaambia,… na hao vijana wamesikiwa wakisema atakayewataja watahakikisha
wanamuua…wapo tayari kufa, kwani kufa kwao ni kitu cha kawaida tu…’akasema.
‘Sikiliza mke wangu, hata mimi siwezi kusema lolote kwa hivi sasa,
maana hapa nilipo kichwa changu hakipo sawa…nahitajia muda wa kuliwazia hilo,
najua polisi watatuita kutuhoji, ninachokuomba ni kutokuongea hayo ya kusikia,
waachie polisi wenyewe wagundue hilo…najua watafikia huko na watagundua ukweli…’akasema.
‘Hata mimi nilikuwa na wazo hilo hilo...na jingine nimeonana na
mke wa mjumbe na yeye akawa ananimbia yake…’akasema.
‘Mhh, mjumbe, mkewe…ehe,…na yeye kasemaje, yeye uliongea naye,
..hukumsikia.. niambie maana huyu mjumbe mimi simuamini sana, anaongea
kupitiliza..’akasema mume mtu.
‘Mkewe anasema , mume wake wakati anatoka usiku kufuatilia…’akasema
‘Kufuatilia nini usiku?’ akadaikia muem wake.
‘Si baada ya kusikia ukelele wa huo moto, …sasa wakati mume wake
anaamuka kutoka nje, akasema huenda hao wapinzani wake wameamua kumfanyizia…’akasema.
‘Kwa vipi?’ akaulizwa
‘Anadai wamekuwa wakitafuta upenyo wa kuonyesha kuwa kijiji hiki
hakina amani, hakina mjumbe anayefaa, na yakuwa mjumbe hajui wajibu wake,
anawakaribisha watu wasiofaa akiwemo huyo mama …’akasema mkewe.
‘Mhh, najua yatasemwa mengi, …na hasa kama limegusishwa na kisiasa,
basi sisi tusubiri ..tutasikia mengi…lakini bado sijaelewa, unasema mke wa
mjumbe alimsikia mume wake akisema… anawakaribisha watu wasiofaa akiwemo huyo
mama sasa,..walijuaje kuwa moto huo umetokea kwa huyo mama…?’akasema mume
mtu na kuuliza.
‘Aaah, mimi sijui…hebu na wewe nikuulize ulipofika huko
alipokuwepo huyo mama, ulimkutaje..watu wanadai hawezi kufa maana ni mama
kutoka mbinguni…na hata huo moto hauwezi kumuunguza…ati ni kweli hajaungua
kabisa?’ akaulizwa
‘Hajaungua sana na moto, ni majeraha machache, sana sana..miguuni
na mikononi lakini sio saana…kwenye mwili hajaungua maana angelikuwa kaungua
nguo alizovaa zingekuwa zimengua, nimekuta na nguo zake kama kawaida…’akasema
na kuongezea;
‘Kiukweli kama ni kufa, labda kafa kwa kukosa hewa, ..na pia jinsi
alivyojifunga,..moshi hakuweza kumuathiri sana, labda huko kukosa hewa…sasa
sijui ..sina uhakika ,..ila ana mjeraha ya mapanga,..sasa hapo ndio nahisi kuwa
huenda kafa kwa kupoteza damu nyingi…’akasema
‘Uliona damu hapo alipokuwepo?’ akaulizwa.
‘Ndio hapo nashindwa kuelewa, hakukuwa na damu pale ardhini, ..sikuona damu zaidi ya matone kidogo tu…,
niliangalia kote sikuona sehemu kuna damu nyingi ardhini, maana hayo majeraha
ni makubwa,.damu itakuwa imetoka kwa wingi...’akasema.
‘Ina maana gani sasa mume wangu..?’ akauliza.
‘Nahisi atakuwa katendewa hivyo, kakatwa na mapanga nje ya chumba,
na huenda alikimbilia hapo ndani, na..kuingia mvunguni kujificha…wakawa wanamfuatilia,
walipofika hapo nyumbani hawakumkuta, na kwa vile wana uhakika kuwa aliingia
hapo ndani,ndio wakaona wachome nyumba moto…’akasema mume mtu.
‘Duuh, unaona eeh,…kwa vile
ni mama kutoka mbinguni, hana damu…na nikuambie kitu mume wangu..huyo mama
yawezekana hajafa..mwenyewe utaona…hapo anatafuta upenyo, watu wakizubaa
tu..huyoo, anapaa anaondoka zake…’akasema mkewe
‘Mke wangu hebu acha hizo imani haba….mtu yupo kalala pale mfu…unasema
hajafa, ina maana sisi ni wajinga..’akasema mume wake.
‘Haya, sasa mwili wake si unatakiwa upelekwe hospitali, maana kama
ni majeraha namna hiyo akiendelea kukaa hapo, mwili utaoza haraka, …?’ akauliza
mke mtu.
‘Ndio polisi wanamchunguza huko ndani…ngoja niingie nisikie
kinachoendelea nitakuja kukuambia la kufanya, jipangeni tu , …’akasema mume mtu
na kuondoka upande huo walipokuwepo akina mama.
*************
Kwa upande mwingine kulikuwepo na kikosi kingine ambacho kilipewa
kazi ya kuchunguza sehemu ya moto na pia kati yao kulipokuwepo na askari wawili
waliokuwa wakikusanya maelzo ya watu.
Kikosi kile cha kuangalai moto ulivyowaka, kama ni wa kawaida au
ni hujuma, kiliweza kwenda mbali zaidi, na kugundua baadhi ya vitu vinavyoweza
kusadikiwa kuwa ni vifaa vilivyotumika kuwashia huo moto, lakini havikiwa na
nguvu sana, kilipatikana kibiriti, na njiti zake na kitambaa kilichoungua nusu,
chenye harufu ya petrol
‘Bado hatujapata kitu cha uhakika..lakini harufu iliyoenea huku,
hasa hapa kwenye majani aonekana ni ya petrol…’akasema mwenzake.
‘Na huu moto ulianzia pale….’.akasogea hadi hapo anapohis moto
ulianzia,..
‘Huu moto waonekana ulianzia hapa…ukazunguka,…mmh, unaona…kuna
galani hapa mkuu, hebu njoo uione…’akasema mwingine na mwenzake akasogea hadi
hapo ilipo hiyo galoni
‘Mkuu..unaona huu moto umeanzishwa na watu kwa makusudi..unaona
hata hii galani haijateketea kabisa..haijaungua sana..’akasema na akiwa kavalia
kinga akasogea kutaka kuichukua.
‘Subiri…ngoja nikamuite mkuu, aje aone mwenyewe..nilijua tu..huu
moto umeanzishwa na watu..’akasema na kuelekea huko kwa mkuu wake, na baadaye
akarudi.
‘Nimekuja na huyu mpiga picha, ngoja achukue matukio,..na mkuu
kasema tuendelee, sasa cha muhimu kabla hatujaingia ndani kabisa, kwenye mabaki
mabaki naona tuzunguke kote kwa nyuma…’akasema
Kabla ya hapo, kundi hili lilikuwa na watu zaidi, ila waliamua
kugawana majukumu, wawili wakabakia kutafuta chanzo cha moto,na kukusanya
ushahidi, na wengine wakaenda kuwahoji watu walioshuhudia huo moto…na kundi la
kuangalia chanzo cha moto likiwa linaendelea kwa upande mwingine kulikuwa na
kundi la kuwahoji watu…
*************
‘Nataka kuongea na baba mwenye nyumba yupo wapi?’ akauliza askari
wa kundi la kuwahoji watu, na wakati huo baba mwenye nyumba ndio alikuwa katoka
kumfuatilia mjumbe, aliporudi tu akakutana na huyo askari kanzu.
‘Mimi ni askari na kazi yangu ni kutafuta ukweli kuhusiana na huo
moto..kwanza nikupe pole kwa maafa hayo..najua ni hasara na ikizngatia kuwa
huku kijijini hatuna huduma za bima, kwahiyo ni hasara isiyo na marejesho, au
sio…’akasema
‘Tumeshapoa…’akasema baba mwenye nyumba.
‘Muhimu ni kujua ukweli..hata kama kuna hasara lakini je haara hii
ni ajali a kawaida au ni ya watu wameamua kufanya hujuma..’akasema askari
mwingine
‘Na ukweli huo hatuwezi kuupata kama hatutpata ushiriakino kutoka
kwenu..na ni vyema mkatuelezea kila kitu, ili tuweze kuchanganua wenyewe, maana
kuna kusikia, kuna kuona, na kuna kudhani..yote sisi tunahitaji..’akasema na
mwenzake akaongezea kwa kusema.
‘Ila mara nyingi ukifika mahakamani wao sana sana wanahitajia
ulivyoona wewe…unaona, lakini sisi
tunataka yote, kama uliona, itakuwa ni bora zaidi..lakini hukuona umesikia,..tunahitaji
hilo pia, litatusaidia kufuatulia, au unavyodhani, unavyofikiria wewe hata hilo
tunalihatajia ili tuweze kukamilisha uchunguzi wetu…’akasema askari mpelelezi.
Baba mwenye nyumba akawa katulia akiwaza ni nini akiseme na ni
nini asikiseme maana ya kusikia ni mengi na hayo ya kusikia yanaweza kumtia mtu
hatiani , ….alpwaza hivyo moyini akasema ‘hapa natakiwa kuwa makini.
Akilini akawa anamuwaza huyo mama,…ambaye sasa anajulikana ni
marehemu pamoja na mengi, pamoja na kumbukumu zake, lakini moyoni aliona
hakustahili kufa kifo cha namna hiyo…walivyomkata kata na mapanga, ni
unyama….hata hivyo hakupenda kujiingiza zaidi, akaona akijiingiza zaidi anaweza
kujitia matatani.
NB: Haya kwa leo inatosha
WAZO LA LEO: Usiwe mwepesi kukubali taarifa za
kusikia, kwani nyingine zinaweza kuwa uchonganishi tu, na unaposikia taarifa
kama hizo kama zina umuhimi kwako zifanyie uchunguzi kwanza kabla ya kuziamini
au kuzitangaza kwa watu wengine.
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment