‘Msiniue, mimi sio mwanga, mimi sio
mchawi… jamani…nimewakosea nini walimwengu…kwanini mnataka kuniua…..mimi
namtaka mtotow angu tu……nataka mtoto wangu..msiniue msiniue….’ akaanza kupiga
ukelele mara mbili, halafu akatulia kimia..
Haikupita muda, yule mama akatikisika
mguuni, na akawa kama unajivuta, na miguu ikatikisika mara moja mbili na ya tatu akawa kimia..ni
kama vile mtu anakata roho..
‘Oh, amekufa…’alisema baba mwenye nyumba
akiwa kaduwaa..
Baba mwenye nyumba kuona vile akapanua
macho kama haamini akashika kichwa , halafu akachuchuma na kumshika mwili wa
huyo mama akise kwa masikitiko,
‘Hapana, usife…nataka kuwa na
uhakika..nataka kukujua, ..nataka kujue kuwa kweli ni wewe, nataka kukujua wewe
ni nani, na kama ni wewe..ooh, ..’akawa anasema na kuinama huku akihangaika,
akitafuta sehemu ya kushika, akitafuta, la kufanya, mikono ikawa inacheza cheza
hewani, na akashituka anashikwa begani, alishituka na kusimama …akitaka
kukimbia.
********
‘Mkuu huo moto sio wa bahati mbaya…
‘Nilishahisi hivyo..’akasema
‘Watu wa uchunguzi fanyeni kazi yenu, ila
kwanza nataka kuiona sura ya huyu marehemu…’akasema akisogea pale alipolzwa
huyo mwanamama.
‘Na kwanini wamefunga hivi, wasije wakawa
wamemkata kichwa…hebu mfungue tuone kichwa na sura yake…’akasema huyo askari
kiongozi wao.
‘Hajafungwa na mtu huyo…ndivyo alivyokuwa
toka awali..ndio maana nawaambia kachanganyikiwa huyo..mnapoteza muda wenu
bure…’akasema mjumbe aliyekuwa akichungulia kwa mbali.
‘Hebu mfunue kabisa eneo la kichwani, kuna
shida kufunua hapo,…ooh, ‘akasema huyo askari kiongozi alipoona mwwenzake
akiangaika kuifungua ile nguo.
‘Na kwanini kajifunga hivyo, ok,..’akasema
na aliposkia mjumbe anasema kuwa wanapoteza muda bure, yeye kwanza akawa kama
hmjalia lakini baadaye akasema;
‘Mjumbe sisi kufanya hivi hatupoezi muda
hapa…hii ni kazi yetu, tunatakiwa kufanya uchunguzi kujua ukweli, hatuangalii
huyo mtu yupoje, hata kama kachanganyikiwa lakini yeye kama binadamu ana haki
ya kuishi….’akasema huyo askari na yeye akisaidia kufungua ile nguo iliyofungwa
shingoni.
‘Sijasema kuwa hana haki hiyo, ila naona
mwisho wa siku mtagundua kuwa hakuna lolote baya lilifanywa, ni …..kwa vile
kachanganyikiwa,..nyie hamuoni mtu akajifungaje hivyo kama
anajinyonga….’akasema mjumbe.
‘Na kuna jingine, watu walipoona huyo mama
anajiunika hivyo, wakais kuna tatizo,kwahiyo wakatafuta njia ya kumfunua,
kilichowapata watakuambia….ina maana haitakiw huyo mama kufunuliwa..mtakuja
kuniambia….’akasema mjumbe.
Askari huyo kiongozi akamuangalia mjumbe,
huku mwenzake akiendelea kufungua sehemu ya mwisho ya hiyo nguo iliyozungushiwa
shingoni, ..huyu mkuu akatabasamu alivyoskia mjumbe akiema hivyo, akasema;
‘Yaonekana na wewe mjumbe unaamini sana
mambo ya kishirikina…sisi askari hatuogopi hayo, ulishawahi askari
amelogwa…hatulogeki sisi…..’akasema na kumgeukia mwenzake aliyekuwa sasa
anavuta sehemu nyingine ya nguo.
Yule polisi akawa anamfungua uso yule
mama, na akawa sasa anataka kuvuta ile sehemu ya juu, iliyomfunika yule mama
kichwani,.. ili uso wa huyo mama uonekane…mara kwa nje, kulitokea upepo mkali…watu
wakawa wanakohoa, hata huyo muu alizidiwa kwa kukohoa…
Baadaye ule upepo ukaisha, na kulipotulia,
yule mkuu akasema;
‘Haya endelea kumfungua…’akasema huyo mkuu
akijifuta futa mavumbi.
`Koho koho…koho…’ ilikuwa
kikohozi..kikohozi kilichomfanya polisi kuachia ile nguo na kurudi hatua moja
nyuma,…akagongana na mkuu wake, aliyekuwa kasimama nyuma yake, wakajikuta
wanataka kudondokeana,….wote wakabakia midomo wazi….
Tuendelee na kisa chetu
***************
Mkuu wa askari hao, akiwa ameshikana na askari mwenzake kujuzuia
wasianguke, huku wakiwa wametizamana, na kila mmoja akawa anachezesha mdomo
kutaka kusema neno, lakini hakuna aliyetamka hata kauli moja, kwa sekunde kadhaa….
Baadae yule mkuu akasema;
‘Ni wewe umekohoa?’ akauliza
‘Sio mimi mkuu…sssi-sijui..sina uhakika..mi-mi –oh, mkuu siamini…au
ni wew eumekohoa mkuu, kunitisha..’akasema askari mwenzake.
‘Hapana, …ni wewe umekohoa..haiwezekani…nimekusikia
kabisa..haiwezekni, kwanini unafanya hivyo…’akasema sasa akitizama kwa wasiwasi
, hakutaka kutizama pale alipolazwa huyo mama, alitazama upande kwa askari
mwenzake , upande kwa mjumbe, mjumbe kwa muda huo yeye alikuwa kwa mbali akiwa
anaonyesa uso wa kushangaa, akauliza;
‘Kwani kuna nini tena huko mbona kama mnashikana?’akauliza
‘Mjumbe mna uhakika …?’ akauliza huyo askari
‘Uhakika wa nini tena kila kitu nimeshawaambia?’ akauliza mjumbe
‘Ulisemaje kuwa huyu mama yupoje, kwanini tusimfunue tukaona sura
yake?’ akauliza huyo mkuu
‘Kwa ushauri wangu, huyu mama akiwa hai alikuwa hapendi kabisa kufunuliwa
uso wake, sasa nyie mnachukua jukumu la kumfunua,…sawa nyie ni askari labda mna
nguvu za ziada,…endeleeni..msije mkasema sikuwaambia..maumeona huo upepo, upepo
kama huo wazee wetu wangelikutafsiria..sio bure…’akasema mjumbe.
‘Lakini mjumbe, kwani tukimfunua kuna nini , maana ni muhimu
tumjue sura yake ikibid tumuweke kwenye magazeti ili mwenye huyu ndugu
ajitokeze, hapo kuna ubaya gani, ..lakini pia huyu aanokena kakatwa na mapanga…je
ni wapi na wapi, labda huko usoni kuna majeraha pia…, ni muhumi tukamilishe
uchunguzi wetu…’akasema huyo askari wakiwa sasa wamesimama wakimuangalia huyo
mama.
‘Nyie watu, mkumbuke kuna waliojaribu kumfunua sasa hivi
hawajiwezi…mimi nawapa kama angalizo, sio kwamba naingilia kazi yenu..hapaan
hapaan msije mkasema mjumbe alisema hivi…mmmh, sitaki,!’ akasema akigeuza uso
upande wa pili..
‘Niuhasuri wako, ..hauna ubaya, lakini ni lazima tufanye kazi
yetu..;akasema askari huyo.
‘Ndio..anyeni..mbona mnasita…, ingelikuwa mimi, aaah, huyo
tungelishazika zamani ..maana hatujui ya mbeleni, huenda kweli ni mwanga,
huenda kweli….ka-katokea kuzimu na ukimfanyia asilolitaka, anakugeukia,
atakujia usiku kama jinni, au kibwengo, atakutisha,..…’akasema na kuwafanya
wale askari wawili kuangaliana.
‘Mimi siwatishi…lakini hayo nimeshayasikia, kwa umri wangu huu,
nimeyasiki na mengine kuyaona..si ndio hayo..watu wapo kitndani
hawajiwezi..sasa..sijui,..nyi askari mnaojifanya hamlogeiki, haya endeleeni mbona mumeacha..kwasababu ya vumbi,
naona vikohozi vimewazidi...au ndio huko kuogopa?’akasema mjumbe
‘Tunaendelea mjumbe sisi hayo hayatutishi…’akasema huyo mkuu
akimuangalia mwenzeke akasema;
‘Endelee kumfunua, ila acha tabia ya kunitishia…tuache kabisa,
nitakufanga.ohooo, kama ni wewe umekohoa halau unaniishia mimi,..ok, endelea
kumfunua…’akasema huyo mkuu akimuangalai mwenzake, ambaye sasa lionekana kuwa
na wasiwasi, akawa anasita kuendelea kumfunua huyo mama.
Akasogea na kwa mkno sasa ulioonyesha kutetemeka, akawa anaanza
kuvuta ile nguo ya juu ili uso ubakiwa wazi..akavuta..nguo hatoki, akavuta….hiyo
ikaanza kutoka….
******
Baba mwenye nyumba ambaye alikuwa kwa nje, akataka kuingia kuona
ni kitu gani kinachoendelea, lakini kulikuwa na watu wamesimama mlangoni, na
hawakutaka kuachia nafasi ili aweze kupita, kila mmoja alikuwa akihangaiak
kupata upenyo wa kuangalia ni kitu gani kinachoendelea huko ndani, baada ya
upepo huo mkali kupita.
‘Huo upepo unaashiria nini mzee mwenzangu..?’ wazee wawili wakawa
wanaongea.
‘Ingelikuwa enzi za mababu zetu, huo upepo ni ishara ya kitu…onyo..au
kumetokea jambo lisilo la halali…’akasema mwenzake.
‘Mhh, hata mimi nakumbuka kitu kama hicho ndio maana nikataka kuwa
na uhakika..sasa kwa hili huoni kuwa inawezekana…kuna onyo hapa, kuna ishara
hapa tnapewa, lakini nani atakusikiliza..’akasema huyo mzee.
‘Aaah, mzee mwenzangu hayo yalikuwa ya enzi hizo,..maana hata
ujana wetu tulishaanza kupuuzia puuzia ya wazee wetu..kila karne inakuja na
mambo yake..’akasema
‘Na kweli na karne hizi mmh, tunashuhudia mengi…sijui…’akasema
mwenzake.
‘Mzee mwenzangu, kwa sasa tuache waendelee na sera zao, ukiongea
hapo utaambiwa wewe umepitwa na wakati umesikia wale vijana walivyokuwa
wakisema muda ule..’akasema mwenzake.
‘Waliesemaje?’ akauliza
‘Wenyewe wameshaanza kutuita sisi wazeee ni wanga,…sisi wazee ni
wachawi,… eti kwasababu ya macho yetu..macho yataacha kubadilika rangi na hali
yenyewe ilivyo, hakuna chakula bora, tunishi kwa shida,..ndani hakuna taa,
mnatumia kibatali..moshi metanda…ufukuto, macho yataacha kubadlika rangi kweli,
hili hawalioni na usomi wao..ooh, jamani natamani nijiondokee, nikapumzike huko
tusipopajua…’akasema mzee mwenzake.
‘Usije ukatamani kurudi, na ujue ukienda huko hakuna kurudi..unasikia
mzee mwenzangu,.. ukienda huko hakuna kurudi, uliwahi kuona, au kusiki kuna mtu
kaenda huko akarudi,kamweeh, ukifa ndio bye
bye..sasa acha kauli zako hizo za kutamani uamauti ..uamuti hautamaniwi,
siku ikifika imefika, mtoa roho hafanyi makosa…nikuambia kiu mzee mwenzangu, ilimradi
unapumua, hata kama unapata taau lakini una nafasi ya kupumua, mshukuru mungu
wako, ..’akasema
‘Kwkweli tunaongea tu..hapa nilipo tumbo linasokota kwa njaa, …mmh
mzee mwenzangu, kufa hatufi ila cha moto tutakiona…’akasema mzee mwenzake.
‘Sasa kuhusu huo upepo…’akaanza kuongea mzee mwingine aliyekuwa
kimia wakati wote…
Lakini kabala hajaongea akakatishwa pale alipoona mwenye nyumba
akikatisha kuelekea mlango wa kuingia huko walipo hao maaskari wakifanya
uchunguzi kwenye mwili wa huyo mama. Na mzee kama ada alitaka kumpa huyo mwenye
nyumba mkono wa pole..
Na ndio kipindi kile upoepp umetulia, na watu wengi sasa
wanahangaika kutaka kujua kinachoendelea huko ndani na mwenye nyumba naye kama
wengine akawa anahangaika kupata nafasi ya kuangalia huko ndani , akawa
kasimama mlangoni huku akiangalia kile kinachoendelea pale alipowekwa huyo
mama, japokuwa kichwani alikuwa na mawazo mengi.
Mawazo yake yalizidi kuchanganywa hasa aliposiki hayo mazungumzo
ya hao wazee wawili, kuwa upepo kama huo ni ishara ya onyo, au kuna jambo
limefanyika lisilo la kawaida, sio jambo sahihi….akasema kimoyo moyo,
‘Huenda wamejaribu kumfunua..kuangalia uso wake…watabakia
kushangaa kama nilivyoshangaa mimi na huenda yakawakuta yaliyowakuta haoo
wengine waliojaribu kufanya hivyo..mmh hata simwambii mtu nilichokiona kwa huyo
mama..’akabenua mdomo akiabsamu.
‘Hahaha, sio kwamba naogopa kufa,..kuwa nikisema nitakufa, …mmmh
hapana..ila ile sura haielezeki, sijui ndio hayo mapanga, sijui..lakini hata
hivyo, kuna jambo kwenye sura ya huyo mama, sio sura yake ya kawaida, mmm na
yake macho..’akasema
‘Yale macho mmh yananikumbusha mbali, hata hivyo,sio yeye...hapana,
sio yeye..’akawa anarudia rudi hayo maneno, huku akitikisa kichwa kukataa.
Na kwa namna nyingine huyo mwenye nyumba alijawa na huzuni sio tu kamkosa mtu ambaye
anahisi ana jambo, ana mswali mengi yanyohitaji majibu kutokwa kwake,.na pia ana
hasira, ana chuki…ana kisasi…, lakini ni mtu ambaye alishaweza kuibadili hali
ya maisha yao.
Maisha yake yalianza kubadilika pindi huyo mama alipohamia hapo
kwake, kipato kikaongezeka, mahitaji ya ndani hayakuwa ni tatizo tena kwake,
akaanza kukarabati nyumba yake, akaweza kukitengeneza vyema hicho chumba cha
uwani na alishaanza kufyatua matofali kwa ajili ya kuongezea chumba kingine..
Huko kwa mkewe biashara ikapanuka, na wakawa na wasaidizi zaidi ya
mmoja wa kusaidia kwenye biashara yao huko sokoni…oh, yote hiyo ni kutokana na
baraka za huyo mama..sasa ndio huyo keshakufa…sasa..oh jamani…akajikuta machozi
yakitaka kumtoka
‘Mhh, kama ni kufanana,..lakini hapana...sio yeye, haiwezekani,..sio
yeye...kama ni yeye kwanini afe….kwanini afe , kwanini hakusubiria kunipa
majibu ya maswali yangu…’akawa anongea mwenyewe, hakujua kuwa kaongea kwa sauti
na yule aliyekuwa karibu yake akasema;
‘Mhh, huyo mama, kweli kila mtu alikuwa na maswali mengi ya
kumuuliza…sasa wamemuua..mimi sijui wanadamu wengine wana mawazo gani…, sijui
waliomuua sasa wamepata nini kwake, eti ni mwanga, eti ni mchawi, mtu mwenyewe
kachanganyikiwa atamloga nani..’akasema huyo aliyekuwa jirani yake
‘We acha tu…aheri wasingelimuua…unajua kafa mikononi mwangu…,
namuona hivi hivi..yaani inasikitisha sana, sijui kwanini walifanya
hivyo,..hata hivyo, …wakati mwingine nawaza mbali..nawaza ingelikuwa mimi
niifanye hiyo kazi..’akasema
‘Uifanye hiyo kazi, kazi gani…?’ akauliza mwenzake huku
akimsogelea huyo mwenye nyumba kusikia kauli yake..lakini mwenye nyumba akawa
anajisogeza mbali na huyo mtu akitafuta upenyo wa kupita, hakuna aliyemjali
kuwa ni mwenye nyumba,..
‘Hivi kwanini hawaendelei na akzi yao, ..nasiki awalikuwa wanataka
kumfunua, nyie mnaoweza kuangalia huko ndani hebu tupeni taarifa…maana
nilisikia sasa wanataka kuiona sura yake, mara kukatokea upepo mkali… si
walitaka kuiona sura yake, hata mimi nina hamu ya kuiona, mbona wamesitisha
hilo zoezi?’ akauliza baba mwenye nyumba
‘Hata naelewa…hawa askari wapo
‘slow’ sana.. si sijui ndio mambo ya
kisasa maana kila hatua wanataka kuchukua picha..nahisi ni kwa ajili ya ushaidi
mahakamani, siku hizi njia hizi za utandwazi zimerahisha mambo…, na kwa vile
wameona kuwa huyo mama ana majeraha, basi wameshachkulia kuwa hiyo ni kesi ya
mauji, kwahiyo wanataka kuwa waangalifu kila hatua..’akasema mwingine.
‘Mhh, nimesikia mjumbe akiwaonya kuwa huyo mama hatakiwi
kufunuliwa hata kama hayupo duniani, ..mimi naona ni sawa, watu wakumuangalia
ni watu wake wa karibu..sasa hao polisi wanataka nini kwa huyo mama?’ akauliza
mtu mwingine.
‘Wansema huenda kuna majeraha usoni, huenda wa wamemchinja na kukiunga kichwa vile ili
kusionekane..lakini pia wanataka kuitambua sura yake, wapige pichana ikibid
wamtoe kwenye vyomba vya habari kama kuna mtu wake aliyepotolewa na ndugu basi
watamuona…’akasema mwingine.
‘Lakini kwa hali halisi, kama angelikuwa hai,angelikubali kufanyiwa
hivyo…habu tuweni wakweli,kama mtu mwenyewe hakupenda sura yake ionekane akiwa
hai kwanini sasa kafa wanang’ang’ania kutaka kumuona, wakimuona ndio
watamrejesha duniani, na hata hao ndugu zao,..muda wote huo mbona hawakuhai
kujitokeza,..hana ndugu huyu mama..mama nahisi ..sio mama wa kawaida…nyie
mnalionaje hilo?’ akauliza mwenzake, na mara kukazuka vurumai,..watu
waliokuwepo pale mlangoni wakageuka, kutaka kutoka nje..
‘Kuna nini tena huko ndani, mliambiwa hamuhusiki sasa manakimbia
nini..?’ akauliza baba mwenye nyumba
‘Hata hatujui..mimi nimeshitukai tu namuona askari mmoja yupo
chini, na mwenzake anataka kukimbia…’akasema na mwingine akadakia.
‘Ohh, kweli yule mama hatakiwi kufungulia, hata akiwa mfu …hutaamini
yule askari aliyekuwa akimfunua kala mwereka,..kadondoka chini na mwenzake
akageuka kukimbia..’akasema mtu mmoja aliyekuwa mlangoni akichungulia, na baada
ya kusema hivyo, kila mtu akakimbilia pale mlangoni kutizama ndani, na wale
waliokuwepo ndani ambao walikaidi amri ya askari kuwa wasiingie ndani lakini
baadaye wakaingia, wakawa sasa wanataka kutoka nje, ikawa sasa ni mgongano pale
mlangoni.
‘Tupisheni tupite…hili sasa ni balaa..’wakawa wanasema
‘Kwani kumetokea nini?’ wakauliza waliokuwepo nje, na baba mwenye
nyumba ambaye pale aliposimama hakuweza kuone vyema, akawa anahangaika kuchungulia
lakini hakuona kinachotokea zaidi ya askari mmoja kuwa yupo sakafuni, na
mwenzake akiwa kasimama huku akiwa anaangalia pale alipolazwa huyo mama.
Mjumbe alikuwa ameshafika mlangoni, akiwa anataka kutoka nje, na
watu wakambana kwa maswali
‘Mjumbe tuambie kumetoeka nini huko ndani mbona watu wanakimbia
kutoka nje..?’ akaulizwa
‘Hapana niacheni,..mimi niliwaambia hawakutaka kuniskia, nasikia
hata hata hao washukiwa…waliotenda hicho kitendo, hali zao ni mbaya…wanaweweseka
ovyo…’akasema mjumbe
‘Ina maana unawafahamu hao wtu mjumbe..?’ akaulizwa
‘Hapana nimesikia watu wakisema..oh, jamani niacheni maana nina
haja….nataka kwenda haja…nipisheni jamani, waliyoyataka wameyapata…nipisheni
nitawakojolea..’akasema mjumbe huku akiharakisha kutoka nje, na alipopata
upenyo, mbio akatokomea upande wa pili ambapo haonekani.
NB Kuna nini kimetokea, watu wanakimbia, askari wanadondoka,
kulikoni
WAZO LA LEO: Tuweni na tabia ya kusamehe mauzi
tunayotendewa, kwani kama binadamu walivyo na wingi wao, mauzi hayakosekani,
kuna watu hawajui kauli nzuri, kuna watu wana tabia zisizo njema kwa majirani
zao..lakini wapo miongoni mwetu, tutafanya nini, inabidi kuvumiliana, ..Hata
hivyo kiuungwana tujifunze kukatazana kutenda maovu, ili kujenga jamii yenye
amani. ..na zaidi tuelekezane kutenda yaliyo mema, ili tujenge upendo ulio
sahihi. Huko ndio kufunzu kuliko na ukweli.
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment