Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Friday, January 23, 2015

NANI KAMA MAMA-23


  Mara akasikia simu yake ikiita, iliita kwa mara ya kwanza, nay eye hakuwa na haraka ya kuipokea akijua huenda ni watu wanapiga tu hawana la umuhimu, ikatulia, haikuchukua muda ikaanza kuita tena, hapo akajua mpigaji ana jambo muhimu, akaipokea simu yake na akagundua kuwa ni mdogo wake anayefanyia kazi hospitali ya rufaa mjini.

Wakasalamiana kama ada, lakini mdogo mtu akaanza kulia na kulia huko kuliashiria tatizo, dada mtu kihekima hakutaka kulichukuli jambo hilo kihofu zaidi, lakini moyoni alijua kuwa kuna tatizo kubwa, dada mtu akauliza ;

‘Vipi habari za huko..?’ akaulizi akijaribu kujipa moyo , alihisi sauti ya mdogo wake, japo anajitahidi lakini yupo katika wakati mgumu, kuna jambo baya limetokea huko anakofanyia kazi, au kuna taaarifa ya msiba. Lakini hakutakiwa kuipokea kwa pupa, ndio maana akamuuliza kama vile ni jambo la kawaida. Mdogo mtu naye akajikaza na kusema;

‘Dada habari za huku sio nzuri ….kuna matatizo…..’akasema na kilichofuata hapo ni kilio, mdogo mtu ikimashinda akawa analia badala ya kuongea.

‘Unasema kuna matatizo, tatizo gani , kwani  imekuwaje, sema basi mbona unaanza kulia kwanza, mimi unanitisha, kuna msiba au kumetokea nini…’ akauliza dada mtu na kusubiria jibu kwa mdogo wake, lakini simu ikakatika.  Kukawa hakuna mawasiliano, dada mtu akaitoa simu sikioni na kuikagua simu yake kwa macho
Alipoangalia akakuta simu yake imezima, kumbe  haina chaji, akakumbuka kuwa alisahau kuichaji usiku, kwasababu umeme ulikatika, Akakimbilia kuichaji, lakini akakuta umeme haujarudi…tatizo la umeme….

Alihangaika huku na huku mpaka akaamua kwenda kwa jirani kuomba simu, lakini hata jirani naye hakuwepo, akarudi nyumbani kutauta fikira nyingine huku akiomba mume wake arudi haraka,….

Wakati ameshakata tamaa, mara mlango ukagongwa, na mgongaji naye alimtia wasiwasi, kwani sio kawaida yake kugonga hivyo, akajua ehee, ni yale yale ya mdogo wake kupiga simu analia huenda taarifa ndio zinaanza kuja, akilini akawa anajiuliza ni nani kafa….

Hebu tuendee na kisa chetu…

*************

Mama huyu akauendea mlango huku mkono ukitetemeka mwili umeisha nguvu, akajitahidi hivyo hivyo na kushika kitasa kuufungua mlango. Mlango ulipofunguka akamuona mumewe kasimama huku kashika mizigo miwili huku na huku, yeye akaenda kumpokea, na mumewe akampa mziogo mmoja mwingine akbakai nao.

‘Vipi mbona nagonga mlango mara mbili lakini hakuna majibu, au ndio unazifanyia kazi hizo baraka za huyo mtu wako, na huenda zimeanza kufanya kazi?’ akauliza lakini hakusikia kauli ya mkewe.

Tofauti na ilivyokuwa siku nyingine mkewe akimpkea kuna bashabasha fulani, tabasamu,..lakini leo kuna utoauti, au mkewe keshagundua…huenda kuna watu wameshampaka majungu..akawa anawaza.

Mawazo hayo ya kuwa mkewe kapewa majungu yamejitokeza leo kwa vila tu ana jambo la kutaka kumuambia, jambo ambalo anachelea kabisa kuliongelea, lakini kwa vile imekuwa ni kero akaona kuna umhimu wa kuliongelea, lakini je ataanzaje.

Akamtupia jicho mkewe la haraka, ile fuaraha ya mchana haikuwepo usoni kwa mkewe…na mkewe alipompokea mzigo hakusema neno, na hata hapo alipomuulizia, kwanini hakufungua mlango mapema mkewe hakusema neno, alichofanya mkewe ni kumpkea mzigo na kuingia ndo ndani na yeye akamuatia nyuma.

‘Hapa leo pagumu, sizani kama nitaweza kuliongelea hili…’mume mtu akawa anawaza na huku mkewe akawa anawaza jambo jingine kabsa jambo la kupkea taarifa mbaya.

Mume wake aliingia ndani akiwa na mzigo mwingine, akajipweteka kwenye sofa, alionyesha kuchoka, akageuka huku na kule, na mkewe akarudi na kuchukua huo mzigo mwingine akaiuniza sehemu wanapoweka mizigo kama hiyo kabla hajaiunguliwa.

Mkewe aakaelekea sehemu wanapoweka maji ya kunywa, akayajaza kwenye jagi kubwa, halafu akarudi nayo pale alipokaa mumewe,  akamimina yale maji kwenye chombo maalumu cha mumewe, maana mumewe ana chombo chake kikubwa ambacho anataka awekewe, maji ya kutosha, na mume wake akayapokea na kuyabugia kama ana kiu ya siku mbili.

‘Ohuuu, mke wangu, mmh nimechoka kweli, mwili na akili pia…, yaani hayo maji yamepita kama sijanywa, lakini ngoja nipumzike kwanza kabla sijanywa mengine…’akasema huku akijinyosha, akahisi kuna kitu mkewe kakisahau, na hilo likampa mawazo kuwa mkewe hayupo sawa,..

‘Hapa hapaongeliki hili swala…’akasema kimoo moyo, kumbe mkewe naye akagundua kuwa kuna jambo hajalianya kwa mumewe, na akili yake ikamjenga kuwa ni kwa vile kuna taaarifa mbaya inakuja.

Mke wake alipoligundua hilo akaja na kukaa karibu ya mume wake, akamsogelea mume wake na taratibu akawa anamvua mumewe koti,kwani mume wake anapenda sana kuvaa koti, tai utafikiri ni mkurugenzi fulani.. zamani alikuwa akifanya kazi ofisini na tabia ile ya ofisini akawa nayo hata akiwa huku kijijini.

‘Mke wangu japokuwa sina kazi nimepunguzwa kazi sio,….wamenionea tu, lakini usijali, yote maisha,… , lakini mimi napenda kuvaa vyema, hata nikiwa sina kazi, ila napenda kuvaa hivi hata hizi kazi za vibarua zisizostahiki hadhi ya kuvaa koti na tai, mimi sitajivunga, utanashati ni hadhi , ukiwa nayo, unathaminiwa….’siku hiyo akamwambia mkewe.

Na kweli kila akienda huko kwenye vibarua vyake, ni lazima avae kitanashati, suti safi, au shati na tai…na mkewe anajua hivyo, kwahiyo huwa anamnyoshea nguo zake sai kabisa, na akirudi haraka anamvua koti , tai na shati, halafu anamkanda kanda mabegani na mgongoni, mumewe anapenda sana kufanyiwa hivyo.

‘Mke wangu ukinifanyia hivyo, nafurahi sana, nahisi mapenzi ya hali ya juu, ….’akamwambia

‘Mhh, mume wangu, hata hivi tu….’akasema

‘Yaani ni zaidi na unavyofikiria, wewe hutaki kufanyiwa hivyo sijui kwanini, …wewe wapenda nikufanyie nini?’ akamuuliza

‘Unitahimini tu kama mke wako….unijali, ni kuniheshimu…..’akasema mkewe, basi mume wake akawa anajitahidi sana kuchunga heshima ya mkewe, na akirudi aghalabu, hakosi kuwa na zawadi hii na ile kwa mkewe.

 Basi mkewe alipokumbuka kuwa kasahau jambo muhimu, akamsogelea mumewe na kumvua koti lake…..alipomaliza kumvua mavazi ya juu, akawa anamkanda kanda mabegani, kwa mikono yake, kwa hali ile mke akawa anawaza huku akisubiria hiyo taarifa,  moyoni akawa anavuta pumzi, akijua kurudi haraka kwa mume wake ni lazima kaja na hiyo taarifa.

‘Mdogo wangu alitaka kunipa taarifa mbaya..na nahis ni msiba tu, aisngeliweza kulia vile kwenye simu…’akawa anajismea moyoni.

‘Najua mume wangu hawezi kuniambia mapema, ni kawaida, ngoja nivute subira, atulie ataniambia,…namshukuru sana mungu kwa nkunipa mume mwema anayenijali, na mimi nitajitahidi kuwa mke wake mwema, kwani kwa hali kama hii, wangelikuwa wanaume wengine wangelishakimbilia kuoa mke mwingine …’akawa anawaza.

‘Mke wangu….’mumewe akasema na mkewe akashituka akajua ehee, taarifa hiyo inakuja. Moyo ukaanza kumuenda mbio, akili ikawa anajaribu kuhisi ni jambo gani, msiba …na kama ni msiba ni wa nani….au ….

‘Labeka mume wangu….’mkewe akasema sasa akijisogeza karibu na mume wake,…bila kujijua akawa anamimina maji mengine kwenye kile chombo alichompa maji mumewe mara ya kwanza kutoka kwenye jagi la maji,  na huku akuvuta pumzi, ili kama akisikia taarifa mbaya sana asidondoke mbali na mume wake.

Mumewe alimwangalia mkewe bila kusema neno, huku naye akiwaza yale yale kuwa mola kamjalia kupata mke mwema, na yeye kama mume , atajitahidi kadri ya uwezo wake kuhakikisha wanaishi kwa amani hata kama wana mtihani huo wa kutokupta mtoto. Na ikibid hilo la kuoa mke mwingine kama mkewe hapendi basi hatafanya hivyo, sasa je ataanzaje kuliongelea hilo…

Akawa anakumbuka jinsi alivyoitwa na familia yao kuhusu hilo jambo la kutokupata mtoto, walimdadisi kujua yeye ana mtizamo gani, au wao wamefuatilia kwa vipimo wakagundua kuna tatizo lolote, na yeye aliwaambia yeye hana mtizamo mwingine zaidi ya kuvuta subira.

‘Subira mpaka mzeeke, vipi wewe bwana au hujioni kuwa umri umekwenda?’ akaulizwa.

‘Au kuna tatizo kama kuna tatizo ongea tuone jinsi gani ya kukusaidia…’akasema shangazi yake

‘Mimi siwaelezi, kwa hli kama hii nyinyi mnataka nifanye nini?’ akawauliza

‘Kama una uhakika kuwa huna tatizo…basi kuna njia moja tu ambayo hata wewe unaiahamu..’akasema mjomba

‘Njia ipi mjomba?’ akauliza

‘Uoe mke mwingine…’akasema shangazi.

‘Yaani hata wewe shngazi unasema hivyo, nilijua wewe utamtetea mwenzako,hebu niambie kama mimi nikiamua kufanya hivyo, na wakati huo huo tumegundua kuwa sote hatuna matiatizo, na mwenzako naye akaolewe kwingine au maana naye anahitaji mtoto….’akasema.

‘Hivi wewe unataka tukuambie nini…mwenye maamuzi hapo ni mwanaume, kuhusu mke, hilo ni jambo jingine, na huenda ukio make mwingine inaweza kuwa ni baraka..’akasema baba yake.

‘Mimi nawauliza mwenzangu naye hana tatizo hilo tumehakikisha, Je na yeye naye afanye nini, …maana naye pia anataka mtoto, na yeye akamtafute kwa nani, jamani tuangalia kote kote,msiniangalia mimi tu, hili ni mtihani kwenye ndoa , mimi na mwenzangu tunarizika, tumemuachia mungu, na kuoa mke wa pili kunahitaji maandalizi,..uadilifu na…je mwenzangu atalikubali, isije ikawa ni vita …’akasema.

‘Wewe jifanya huelewi, lakini hili tunalokushauri ni muhimu kwako,…umri unakwenda , utazaa huku unaitwa na mtoto wako babu, shauri lako…’akaambiwa

Kwakweli kikao hicho hakikumrizisha wakatawanyika bila kuafikiana, na hauwahi kumsimulia mkewe kuhusu kikao hicho, ilikuwa siri yake.

Hata hivyo pamoja na changamoto hilo, moyoni alijisifia kuwa kweli kamapata mke mwema, na anampenda sana, hakutaka kabisa kumuuzi, kwani licha yeye kuwa chaguo lake, lakini hata wazazi na familia yao wanampenda sana mke wake huyu, ila sasa tatizo ni hilo, la kutokupa mtoto. Tatizo hilo hata yeye sasa limeanza kumkera, maana kila akikutana na ndugu ni hilo hilo, na hata mkewe sasa keshaanza kuliongelea.

Sasa kama hata mkewe analiongea, na wakati mwingine wanabishana kuhus hilo mpaka wanaishia kununiana, …. basi umuhimu wake umekuwa mkubwa, kwake imekuwa ni kero,  sasa yeye afanyeje…basi kwake ikawa ni adhabu ya mawazo.

‘Hivi kumbe swala la kupata mtoto ni swala nyeti sana kiasi hiki…’ akasema siku hiyo alipokuwa akongea na raiki yake.

‘Oooh, ndio maana nilitaka kuongea na wewe kuhus hilo jambo, mimi kama raiki yako ni lazima nikushauri jambo muhimu, …’akawa kachokoza

‘Jambo gani na wewe usiwe kama wazee wangu maana wanachonishauri ni ubinafasi mupu, wananiangalia mimi tu, hawamjali mkewe wangu….’akasema.

‘Mimi nakushauri kwa nia njema , tafuta mke mwingine uone…’akasema rafiki yake na akilini akasema ‘ni yale yale…’

Rafiki yake huyo alimshawishi aoe mke wa pili ili ajaribu bahati huenda akapata mtoto. Lakini yeye alipinga kabisa swala hili, akamwambi kuwa yeye na mkewe wanapendana sana na huenda akioa mke wa pili, itakuwa chanzo cha wao kukosana.

‘Sasa wewe umeoa ili iweje, mkae tu mpaka uzeeni, na nani ataiendeleza familia yako, ukifa, na mali yako atairithi nani..wewe hulioni hilo..’ akamuuliza rafiki yake

‘Mimi nina mali gani ya kuritiwa hicho kibanda cha matope…aah, kama mungu atapenda iwe hivyo, siwezi kukalifisha nafsi..unakumbuka mtume Ibrahim, alikaa miaka mingapi bila mtoto…nyie watoto mnaona ndio kila kitu’ akasema

‘Sasa wewe unajilinganisha na mitume, wao walipewa umri mrefu, sisi kama umejitahidi sana utafikia miaka themanini, tisini, ..hapo umeshakuwa kizee, huna uweze tena wa kuzaa, sisi unatakiwa uzae mapema, ukichelewa sana isizidi miaka thelethini na saba..’akaambiwa,

‘Rafiki yangu  hilo wazo la kuoa mke mwingine, hapana, mimi mapenzi kwa mke wangu niliye naye ndio muhimu sana, ilimradi tunapendana na mke wangu, sioni sababu ya kukosana naye kwasababu ya watoto…kama tutapata tutapata tu…’ akasema akionyesha kukerwa na hilo jambo, kwani haya mazunguzmo yamekuwa kero, kila akikutana na jamaa yake yoyote ndio gumzo.

Akaona akaliongelee vyena na mke wake, kama atakubali basi atafanya hivyo, lakini iwe kwa ridhaa ya mke wake, akaona apitie sokoni anunue vitu vizuri, amnunulie mkewe zawadi nzuri, ili wakiongea mke wake ajue kuwa anampenda, na hataki kufanya hivyo kwa tamaa …

Aliponunua vitu hivyo akaharakisha kurudi nyumbani, akagonga mlango kwa mbwembwe ili mkewe aje kumpokea, lakini hali aliyoiona kwa mkewe alipofungua mlango na kuja kumpokea, ilikuwa sio ile hali ya siku zote, ile hali ilimtia mashaka, na hata lile wazo la kuongea naye kuhusu hoja ya kuoa mke wa pili ikamtoka, kwanza alijiuliza atamuanzaje mkewe, maana mwanzo wa jambo ni kianzio chema.

‘Vipi mume wangu umeniita , kama una jambo, lakini umebakia kimia unaniweka roho juu..’akasema. mkewe huku akimuangalia machoni, yeye kwa kuliona lile jambo alilotaka kumuambia ni kama la aibu, akakwepesha macho yake kuangalia na mkewe na mkewe kuona hivyo akajua lazima mume wake ana jambo kubwa, na hilo lawezekana ni msiba.

‘Aaah we acha tu mke wangu , kazi hii ninayofanya sasa inachosha, nimechoka sana leo, nikaona leo nirudi mapema, maana uliniambia leo alikuja huyo mama, mleta baraka , sasa huenda barakahizo ni za kweli, tuzifanyie kazi…’akasema mume wake akijaribu kuvuta hisia za mkewe aili akianza kuliongelea hilo jamb lisiwe ni jambo gumu .

‘Mume wangu naye, ina maana umetoka kazini mapema kwa hilo au kuna jingine, nahisi kuna jambo jjingine hutaki kuniambia kwa haraka, kwanini huaniambii hilo jambo, …’akasema na mume wake akashangaa, ina maana mkewe keshahisi kuwa yeye ana jambo anataka kumuambia akakohoa kama kusafisha koo, na kusema;

‘Mke wangu ina maana unahisi kuwa nina jambo nataka kukuambia, kwanini umesema hivyo, usiwe na wasiwasi mke wangu, mimi nakupenda sana, ndio maana nataka tuongee…’akasema na mkewe akaona ehee, hiyo ndiyo kauli ya waume wakitaka kutoa taaria mbaya kwa mkewe, sasa ngoja asubirie kusikia hiyo taarifa mbaya, alikumbuka jinsi baba yake alivyokuwa akifanya akitaka kumuambia mama taarifa ya huzuni, alikuwa akifanya hivyo hivyo

‘Haya niambie mume wangu maana hapa nilipo sina amani, kuna nini kimetokea…’akasema na mumewe akawa katulia hakusema kitu, alikuwa akitafakari jinsi y akuanza, na mkewe alipona hivyo akasema;

‘Mume wangu, niambie kuna taarifa gani, mimi siwezi kusbiria tena….’akasema sasa akishika kichwa

‘Taarifa, taarifa gani mke wangu, mimi nilikuwa nataka tu tuongee, mambo yetu , hasa nilipofika mchana ukasema wewe upo tayari kufuatili jambo lolote linalohusu kupata mtoto,…sasa mke wangu, hivi hakuna njia nyingine tunaweza kupata watoto….’akasema na mkewe akabakia kaduwaa, na muemwe kuona vile akahis keshaanza kumuuzi mke wake akaona huenda kaanza vibaya, akasema;

‘Mke wangu lakini hili umelitaka wewe, na kila mara nikija ni wewe unaniuliza kuhusu hili, ndio maana nimerudi mapema, ..wewe unasema kuhusu taarifa, taarifa kutoka kwa nani, ..au umepokea simu kutoka kwa mdogo wako au…?’akasema

Mkewe akaanza kuhisi mwili unamtetemeka, pale aliposikia taarifa kutoka kwa mdogo wake, moyoni akajua sasa mume wake anataka kumuambia hilo jambo.

‘Ndio …niambie kuna nini kimetokea…ndio nimepokea simu kutoka kwake, lakini…haya niambia kuna nini kimetokea?’ akauliza mkewe sasa akionyesha hamasa

‘Mke wangu…..ndio nimepokea simu kutoka kwa mdogo wako , na kiukweli …’akatulia maana kweli alisahau kuhusu hiyo simu kutoka kwa shemeji yake, yeye alililiona hilo kama swala la kuongea baadaye tu,  na kilichomfanya hata asahau ni kutoka na mazunguzmo yake na rafiki yake, kimachanganya akaona leo akifika cha muhimu ni hilo tatizo la siku nyingi, na hilo la shemeji yake akaliweka sehemu ya pili ya mazungumzo yake na mkewe.

Alipokumbuka hivyo akatahayari, hakutaka kusema alisahau,  akaona akisema alisahau ataonekana hana mapenzi na ndugu za mkewe, akatulia kidogo. Kwa kutulia vile hakujau ndio kunampa mkewe wasiwasi na mashaka mwenzake akijua kuwa kuna jambo kubwa anafichwa, labda akiambiwa litamshitua

‘Kuna nini kimetokea, naona unanizungusha tu kwanini usiniambie ukweli,  au yule mgonjwa ameshafariki….au kuna msiba mwingine, niambie mume wangu usiogope nipo tayari kupokea taarifa hiyo…’akasema sasa akikaa vyema.

`Mke wangu,….yule mgonjwa, mgonjwa yupi huyo,….?’ Mume we akauliza akijaribu kutafakari na kabla mkewe hajasema neno akaendelea kusema;

‘Mke wangu  ni kweli nilipokea simu kutoka kwa mdogo wako, na ndio nilikuwa najipanaga kukuambia…, lakini naona mwenzangu una fikira nyingine  kabisa, tulia mke wangu, nina mazungumzo mengine mazuri, muhimu sana, nataka tuyaongee kwanza….’akasema. Na mkewe akamtolea macho na kusema;

‘Mume wangu una nini leo….ina maana hilo la mdogo wangu, na taarifa hiyo sio muhimu …hivi unajua najisikiaje hapa nilipo, .., au unataka kupoteza muda tu, kwa vile unaogopa nitazimia,..hapana  mimi sasa ni mtu mzima, akili imepevuka, wewe niambie , tena haraka, mdogo wangu alipokupigia simu kasemaje…au kuna nini…niambie haraka..’akasema sasa akionyesha kukerwa.

‘Mke wangu ni kweli, shameji kanipigia simu, kwanza alisema alikupigia wewe simu, lakini simu yako ikakatika kabla hajakuambia…’akaanza kumuelezea.

NB: Naona niishie hapa kwa leo,


WAZO LA LEO: Kuna vitu vidogo tukiviboresha kwenye ndoa zetu vinaleta tija , furaha na baraka, kwani ndoa ni raha na furaha,lakini vitu hivyo tunavidharau. Kwasababu mumeshaoana basi vitu hivyo havina umuhimu , kwa pande zote mke na mume. Vitu kama kupeana zawadi za kushitukiza, kupokeana mizigo, kusalimiana na bashasha, na mume au mke akitoka kazini kukaa na kunyoshana viungo(massage), ni tendo litaonekana dogo lakini moyoni linavuta hisia kuwa mwenzangu ananijali, ananipenda. Tujitahidi kuboresha matendo mazuri katika ndoa zetu .
Ni mimi: emu-three

No comments :