Nesi ambaye aikuwa kaduwaa akiendelea
kukumbuka jinsi ilivyokuwa, wakati huo madocta walikuwa wakitaka awape taarifa,
lakini mdomo wa nesi ulikuwa mgumu, kwani akili yake ilikuwa mbali, ilikuwa
ikijaribu kukumbuka ilivyokuwa, ili aweze kujitetea.
Na zaidi kilichomvunja
nguvu ni pale alipoanza kuelezea, na kabla hajamaliza docta bingwa akamkatiza,
alipoona kuwa yeye anapoteza muda, na kumkatiza kule kulimfanya ashindwe kuongea, akawa kama kagandishwa, na akilini akawa anakumbuka pale alipofika chumba cha mgonjwa akitokea kuchukua chupa ya
kumuongzea huyo mgonjwa maji….
Nesi alikumbuka kuwa, alipofika chumba
alichokuwa kalazwa yule mama, alifungua mlango, na mcho yake yakawa yametua
kitanda alichokuwa amelala yule mgonjwa. Alichokiona kilimfanya adondoshe hata
kile kisinia kidogo, ambacho aliwekea maji ya kumuwekea mgonjwa na dawa zake.
Macho
yalimtoka pima, kwa uwoga, alijikuta akitetemeka na kutamani akimbie, lakini
angekimbilia wapi,…akatamani apige yowe, lakini ingesaidia nini…akashikwa na
bumbuazi kwa dakika moja, huku akishindwa afanyeje…
Alijikuta amaichukua ile chupa ya maji na kuweka kwenye kile kisinia na kutoka mbio kuelekea kule walipokuwa madocta,....akijua huenda, wao ndio wamchuekua hata hatua hiyo..lakini haikuwa hivyo....
Tuendelee na kisa chetu
************
Madakitari walipoona nesi kaduwaa, hasemi kitu, hasa alipokatizwa
na docta bingwa, wakati anaanza kujieleza, akimuuliza mkuu, kuwa kumetokea
nini, ilikuwa kama kapigwa sindani ya gazi, akawa kimiya, huku mdomo
ukimtetemeka kutaka kusema jambo….
‘Wewe vipi….’ilikuwa kauli ya docta bingwa, ambaye alishahisi kuwa
huko alipotoka nesi kuna tatizo kubwa sana, docta bingwa akavuta hatua moja, mbili,
akamkaribia nesi, huku akisubiri kuwa labda nesi atasema lolote, lakini hakuna
kauli iliyotoka kwa nesi, zaidi ya kutetemesha mdomo
Docta bingwa naye kama
ilivyokuwa docta kijana hakusubiria tena, akampita nesi na kwa haraka akatoka
nje kukimbilia huko wodi aliyolazwa huyo mama, na akilini alijua tayari huyo
mama huenda keshakata roho, au vinginevyo kuna jambo jingine kubwa limetokea.
Madocta wengine na wao wakawa wanamfuatilia nyuma bosi wao, huku
kila mmoja akimpita nesi, anakuwa na shauku kuwa huenda nesi ataongea lolote
ili liwape fununu, lakini nesi hakuweza, mdomo ukawa mzito, basi wote wakawa
wanaelekea huko chumba cha mgonjwa wao.
Ikawa ni mbio mbio, kuelekea chumba hicho cha wagonjwa maalumu, na
chumba hicho kilikuwa chumba cha pili yake kutoka hapo, lakini wenyewe waliona
kama chumba hicho kipo mbali ajabu, walipofika mlangoni walishangaa, kwani
chumba hicho muda wote kinakuwa kimefungwa kwasababu ya kipoza hali ya hewa,
lakini muda huo chumba kilikuwa wazi, wakahisi huenda docta kijana ndiye
kakiacha wazi kwa dharura hiyo, au nesi
kasahau kuufunga ule mlango kwa kuchanganyikiwa.
Mbio, mbio wakisukumana kuingia mlangoni, kila mmoja akitaka
atangulie yeye kuingia. Na wa kwanza alikuwa docta bingwa, akiwa na lake
kichwani, kuwa sasa yule mama hauyupo tena duniani, anahitajika kuandika
taarifa, na sijui kama nesi alikumbuka muda huyo mama alipotulia kuonyesha kuwa
keshakata roho.
Weengine halikadhalika walikuwa na yao, kuwa huenda,…huenda…...
Waliyemkuta mle ndani alikuwa docta kijana, alikuwa kasimama
pembeni ya kitanda huku akiangalia mashine ya mapigo ya moyo, akiwa kashika
kidevu hakugeuka, alikuwa katulia kimiya…
*******
‘Vipi kuna nini kimetokea,…..?’ akauliza docta bingwa akiangalia kitandani,
lakini hakupata jibu. Docta bingwa akainua kichwa kumuangalai docta kijana, na docta
kijana, alikuwa kimia kaduwa, mtindo ule ule wa nesi, hakuwa na jibu.
Docta bingwa akamsogelea docta Kijana, na kuwa naye sambamba, na
yeye akawa anatizama ile mashine ya mapigo ya moyo, kama vile atapata jibu
sahihi, …na waliokuja nyuma yao walikuwa madocta wengine, wakiwa na swali lile
lile
‘Kwani kuna nini , kumetokea nini….?’ Wakauliza, na wao hawakupta
jibu, wakasogea pale waliposimama wenzao, na wao wakawa wanaangalia kule kule
walipokuwa wakiangalai wenzao. Mshine ilikuwa kimiya kama haianyi kazi!
Huku nyuma nesi alikuwa kaachwa peke yake, akiwa anatafakari jinsi gani ya kujitetea,
alikuwa kabakia mwenyewe kwenye chumba cha mapumziko cha hao hawo madakitari,
akiwaza, nini afanye, kwani mdocta wote walikuwa wameshakimbilia huko kwenye
tukio.
Nesi alikuwa kama ndio katoka usingizini, akashituka, na akili
ikaanza kufana kazi, mdomo uliokuwa mkavu, sasa ukawa na umajiumaji, tayari kwa
kuongea, lakini kwa muda huo angeliongea na nani, madocta, wakubwa wake wa kazi
walikuwa wameshaondoka, na kwa kukaa kwake kimia itakuwa imetafsriwa vingine,
kuwa hayupo makini, hawezi kutoa taarifa kukitokea tatizo, mzembe…hayo yote
yanaweza kumkosesha kazi,
‘Mungu wangu nimefanya nini, kwanini nilishindwa kujieleza…..’akawa
anajilaumu, lakini alikuwa ameshachelewa.
Nesi taratibu akageuka,
akavuta hatua kutoka nje, akawa anaelekea mlangoni, huku, moyoni akiwaza
mengi, na mwishowe akasema;
‘Ngoja na wao wenyewe wafike wajionee kama nilivyojionea mimi…,
najua baada hapo nitatakiwa kujibu maswali mengi, ambayo kiukweli sina majibu
sahihi, na labda nitaonekana mzembe, lakini watakuwa wamenionea, mmmh, najua
sasa nakosa kazi, sijui nitakuwa mgeni wa nani, …’akasema
huku akishika kichwa.
Nesi alipofika nje, akasimama, akijaribu kuwaza aende wapi,
alifahamu fika anatakiwa kwenda kujieleza, maana yeye ndiye aliyekabidhiwa
majukumu yote, kwahiyo anabeba lawama, anatakiwa kwenda kujieleza,…’
‘Nitawaeleza nini mimi…?’ akajiuliza, kwanza akasubiri kidogo ,
halafu kwa mwendo wa taratibu akaanza kutembea kuelekea huko walipokwenda hao madocta
akijua sasa anakwenda kujibu kesi, kesi ambao hana cha kujitetea, na hata hajui
kabisa atasema nini, akawa najilaumu
kwanini alipoteza muda kuongea na shiga yake.
‘Lakini sikukaa sana, niliongea kidogo tu, nikatoka,…sasa sijui
kuna nini kilitokea…’akawa anajiongelesha mwenyewe huku anatembea mwendo wa
kusua sua.
‘Ngoja niende huko huko…. Mungu atanipa njia….mungu naomba unipe
kauli maana hili sio fungu langu…’akawa ansema huku anatembea kulekea kile
chumba alichokuwa kalazwa huyo mama, kwenda kukutana na madocta…..
************
Katika kitongoji kimoja nje
ya mji, kulizuka sintofahamu, watu walisikia ghasia, na ghasia kitogo ikigusa
masikio ya watu, huvuta hisa za kutaka kujua kuna nini, basi watu wakatega
masikio, na pale masikio yaliposikia, lakini hayakutosheka, akili ikamtuma
macho aone ni nini kinaendelea.
Watu wakajikuta wakitoka majumbani mwao na kuangalia hicho
kinachoendelea huko barabarani, na mara sauti moja ikasikika, sauti nyembamba
ya kike, na sauti nyingine ya watoto wakimuegelezea huyo msemaji ikasikika
ikiitia.
Wanasemaje vile….akili ikajiuliza na kusikiliza zaidi, na sauti
ikarudia;
‘Nata-nata, nataka, mtoto wangu ….’ Ilikuwa sauti ya kike.
Waliobaatika kutoka haraka kabla kundi la watoto halijaongezeka,
wanasema aliyekuwa akighani hiyo saui alikuwa mwanamama aliyekuwa akipita
njiani, na watoto wakaanza kumfuata nyuma, wakimuigizia hiyo sauti, wakisema; `
Nata-nata, nataka, mtoto wangu’
Ilianza kama mchezo, watoto wawili, watatu, wanne, na mara kundi
kubwa la watoto, likawa linamfuatilia nyuma huyo mama. Watu wakawa wanashangaa,
ni nani huyo, na kwanini anaimba hivyo, na kwanini watoto wanamfuatilia nyuma
wakimuegelezea anavyoimba, au kutoa kauli hiyo.
Kuna muda sauti ya mwanamama huyo ilikuwa kama inakaripia, na
kuona ni kero, na kwa kufanya hivyo, watoto nao wakaona ni kama mdhaha, akisema
na wao wanamgeza, na huyo mama anatembea huku na kule, akigeuka kuwaangalia
watoto, watoto wanasimama, na yule mama anageuka kuendelea na safari yake, na watoto nao wanamfuata nyuma.
‘Nata-nata, nataka, mtoto wangu ….’ Anasema na watoto nao waniga,
` Nata-nata, nataka, mtoto wangu , …’ ikawa ni wimbo, hata akina mama majumbani
na wao wakawa wanageza, ` Nata-nata, nataka, mtoto wangu , ….’
Watu wakawa wanashangaa na kila mmoja akawa na hamu ya kumsikia
huyo anayeimbisha huo wimbo wa aina yake ni nani, na kitu gani kimewafanya watoto
wavutike naye…huku wazazi wengine hasa wenye watoto wakiingiwa na wasiwasi na
watoto wao wakiogopa asije ikawa ni mbinu ya kuwadhuru watoto wao.
‘Hivi mnamfahamu huyo mama?’ ilikuwa sauti ya mama mmoja aliyejitokea
kwa jirani yake akiwaangalia watoto waliokuwa wakizidi kuongezeaka kumfuatilia
huyo mama
‘Hata hafahamiki, sijawahi kumuona kabla, …kwanini anafanya hivyo, au kapungukiwa nini….’akasema
mwingine.
‘Jamani visa vya kupotea watoo vimezidi , mumesikia juzi kijiji
cha jirani watoto wawili wamepotea hivi hivi mpaka leo hawajulikani walipo,….’akasema
mama mmojawapo.
‘Pia kijiji kingine kuna mtoto alipotea na wkagundua mwili wake
ukiwa umenyofolewa sehemu za siri, sasa
isije ikawa ni mbinu ya huyu mama kuwateka watoto wetu…’mama mwingine akasema.
‘Ikishindikina inabidi tumuambie mjumbe, mama huyo akamatwe…’akasema
mwingine
Na kwa minajili hiyo kile
mwenye mtoto akawa anakimbilia barabarani kumtafuta mtoto wake, kwahiyo badala
ya watoto, sasa wakawa watu wazima na wao wapo kwenye kundi, na wengi wao wakiwa
ni akina mama, wakawa wanamfuatilia huyo mama, na wengine wakawa wanawaita
watoto wao majina.
Kwa jnsi ilivyo, ilikuwa vigumu kumuona huyo mama yupoje, kwani
watoto walimzunguka, na ilikuwa kama vurumai sasa, na kila mmoja alikuwa na hamu
ya kumuona huyo mama anayeimbisha watoto ni nani
Kundi la watu wakawa nawo wanamsogelea huyo mama, lakini kwa
tahadhari, na kila wakimkaribia, anakuwa kama anakimbia, watoto
wanamkimbilia, na yeye huanza kuimba, ‘Nata-nata,
nataka, mtoto wangu..’ watoto kwa furaha na kwa mdhaha na wao huimba, ` Nata-nata,
nataka, mtoto wangu’
Basi watoto wakawa
wanaongezeka kuwafuta watoto wenzao, na
wazazi wakawa wanawakimbilia watoto wao kuwarudisha nyumbani, na wazazi hawa
wakikutana na wenzao wanabakia kuulizana
‘Huyu ni nani, nasikia ni mama…?’ wakauliza.
‘Hata mimi sijamuona vyema,…’akasema mwingine
‘Nasikia ni mama tu, lakini hajulikani wapi alipotokea….’mwingine
akaongezea kusema.
‘Anafananaje?’ akauliza mwingine.
‘Hatujui, maana kazungukwa na watoto, kuna mtoto mmoja kasema mama
huyo kajifunika sehemu kubwa ya kichwa chake, na amevaa gauni kubwa, ambalo sio
la kawaida. Ni mwanamke mgeni sana hapa kijijini kwetu…
‘ Nata-nata, nataka, mtoto
wangu…’ sauti ikawa inaongezeka kila muda.
*************
Kwenye nyumba moja ya jirani na hapo barabarani, kulikuwa na mama
mmoja aliyekuwa kajipumzisha ndani ya nyumba yake, alikuwa kajilaza kitandani
baada ya shughuli za ndani, na pilika za hapa na pale, aliona ajipumzishe huku
akimsubiri mume wake, ambaye huja kula chakula mchana nyumbani, akawa kajisikia
kuchoka, na kausingizi kakawa kamempitia.
Akiwa katika usingizi wa mang’amu
ng’amu, mara akawa kama anaota, watu wanatafuta watoto, na watu hao wakawa wanapita
kila nyumba kuulizia mtoto aliyepotea. Na cha ajabu muulizaji akawa anauliza
kama vile anajua kuwa mtoto huyo yupo hapo anasema kwa sauti kali ya kigugumizi…
`Na-na-na taka mtoto wangu..’ huyu mama akiwa ndotoni, akamjibu
‘Mbona mimi sina mtoto wako…’akajitetea
‘Na-nataka mtoto wangu..?’ akaulizwa tena, kwa hasira, na
anayeuliza akawa na panga akitaka kumcharanga nalo, na huyo mama akasema;
‘Mimi mwenyewe nataka mtoto …’akasema.
Mara akakurupuka toka usingizini, na kusikia kelele nje, akainuka
na kuangalia dirishani baada ya kusikia kelele zikizidi.
Alipofunua pazia la dirisha na kutizama nje, aliwaona wale watoto
wakiwa wanaimba kwa sauti, na sauti ya kike ilikuwa kama ndio inaimbisha,
ikisema; ‘Nata-nata, nataka, mtoto wangu , ..’ na watoo nyuma hata baadhi ya akina
mama wengine wakawa na wao wanaigilizia, …` Nata-nata, nataka, mtoto wangu …..!
Yule mama akashangaa, hii ndoto ina maana gani, na kwanini iwe
sawa na tukio hilo linaloendelea huko nje,…! Ndoto za mchana mbaya, inakuwa
kama kweli.
Mama yule akapangusa pangusa uso na kuwaangalia wale watoto,
wanavyoimba kwa furaha, na kwa jinsi wanavyoruka ruka na kuimba kwa furaha, na
mama zao wakijaribu kuwashika mikono kuwarudisha nyuma, mama huyu akaingiwa na
mawazo ya huzuni.
Mawazo yalimrudisha nyuma, akawa anawaza kuwa kama naye angejaliwa
watoto, au hata mtoto mmoja tu, na yeye
angelikuwa miongoni mwa hao akina mama akimrudisha mtoto wake nyumbani,lakini
yeye hajajaliwa mtoto.
Yule mama alipokuwa akiwaza hivyo akajikuta machozi yanamlengalenga,
akawaza na kutikisa kichwa huku anasema moyoni;
‘Hivi mimi nina kasoro gani, mbona sipati mtoto, mwaka wa kumi
sasa, tangu tuoane na mume wangu, lakini hakuna cha mimba au mtoto, angalau
ningepata mimba, itoke, nione nina tatizo lakini la, hakuna hata dalili, au kweli nimelogwa…’akasema
‘Mmmmh mungu wangu, nisije nikawa…mmmh, hapana, kizazi ninacho hii
nina uhakaika, sasa tatizo ni nini…mume naye haeleweki, hanisikilizi…’akawa
anongea peke yake huku akiwaangalia watoto wanavyoruka ruka.
Akawaangalia wale watoto, huku machoni kukiwa na ukungu wa
machozi, yaliyoanza kububujika, …akainua kichwa juu kumuomba mungu kuwa amjuze
tatizo lake ni nini, kuwa yeye hatazaa tena, au kuna tatizo gani zaidi.
Alikumbuka jinsi gani akimwambia mume wake asivyotaka kusikiliza
kilio chake kuwa waende hospitli wakapime , ili wajue tatizo nini, lakini yeye
hakubali. Huishia kwa maneno mengi, utafikiri yeye ni mtaalamu wa vizazi…na
jana tu alisema;
‘Kwani wewe una tatizo gani, unaumwa, unajisikia vibaya, mtoto ni
kudura ya mungu, kama tutapata tutashukuru mungu, kama hatukupata, basi ndivyo
tulivyopangiwa, mimi sioni tatizo lipo wapi…’akasema
‘Mume wangu lakini tumesubiri sana….’akasema
‘Hivi kwanini, nakuona siku hizi unawaza saaana kuhusu mtoto,
mbona mwanzoni nilipokuambia swala hili ukalipuuza, sasa unajifanya kujisikia
uchungu…achilia mbali mawazo hayo…mtoto, mtoto, mtoto tutapata tu…’ hayo maneno
aliyasema mume wake jana, kabla hawajalala.
Ni kweli maneno hayo, kama ingelikuwa yeye na mume wake tu
asingelijali, kwani kupata mtoto ni kudura ya mungu, lakini kila wanapokuja
mawifi zake inakuwa ndio gumzo, kwanini wifi hupimi, kwanini wifi hampati
watoto…kwanini, kwanini…’mazungumzo kama hayo, yanakuwa hayampi raha.
Japokuwa mawifi zangu wananipenda, lakini itafika muda
watanichukia tu ..kwa jina la kukosa mtoto…’akajisemea moyoni.
Ni kweli, mawifi zake wanawmpenda kama anavyowapenda wao, hajaona
chuki yoyote kwao, lakini kibinadamu ,lazima watakuwa wanamjadili huko majumbani
kwao vinginevyo. Kwani, eti, nani asiyependa kuona ndugu yao, au mtoto wao ana
watoto…raha ya mzazi ni kupata mtoto, mtoto ni tunda na faraja ndani ya
familia…oh!
‘Mhh, namuonea sana huruma mama yake mume wangu, najihisi kama
mimi ndiyo yeye, nina mtoto wa kiume, kaoa, natamani mjukuu toka kwa mtoto
wangu lakini hapatikani…’akafuta machozi.
‘Mmmh, pia namkumbuka mama yangu, huenda huko alipo na yeye hana
raha, anajiuliza kuna tatizo gani kwa mtoto wake, sijui niende kwetu kwa mama,
nani kama mama, kila jambo ni yeye tu, sijui huko ulipo ananikumbukaje…’ alishika tama huku anazidi kuwaangalia
wale watoto wanaoendelea kuimba!
‘Nata-nata, namtaka, mtoto wangu..’ sauti hiyo ilikuwa inazidi
kusikia kwa nguvu na sasa walikuwa wakija eneo hilo alipo huyo mama, na kelele
ile sasa akaiona ni kama kero, na yeye akajikuta akiimba, `na mimi nataka mtoto
wangu..’
Akatokeza kichwa nje, na kusubiri huyo mama aimbe, na yeye akawa
anaitikia, ..na karibu na dirishs hilo,
akawasikia akina mama wakiteta, na mwanaume mmoja, na huyo mwanaume akasema;
‘Huyo ni mtu katumwa kutoka mbinguni, kuwakomboa akina mama wasio
na watoto, ndio maana anaimba hivyo, kuwa mwenye kutaka mtoto naye aimbe, ‘nataka
mtoto wangu..’akasema huy o mwanaume.
‘Nani kakuambia anhitaji mtoto, tulio nao wanatushinda, fujo
kelele, gharama za kuwasomesha, …wewe unataka watoto tena…’akasema
‘Wewe hutaki, lakini kuna wanaowataka, angalau mmoja tu hawampati….’akasema
mama mwingine.
‘Ndio hao wameletewa huyo mjumbe, akisema `nataka mtoto wangu…’ na
wewe unayetaka mtoto, unatakiwa uutikie, uombe, shida zako, ndio maana watu
wanamfuatilia huyo mama wakimuigizia…’akasema huyo mwanaume.
Ulikuwa umbea uliotungwa na mmbea mmoja, na umbea humea haraka na
kusambaa, umbea ukazaa matunda, watu wengine wakachukulia ni kweli, na baadhi
yaakina mama wenye shida zao, wengine za watoto, au wanajiona hawaelewani na
waume zai, wakatoka majumbani wakajua ni kweli, wakaanza kuitikia ili waipate hiyo baraka.
‘Nata-nata, nataka, mtoto wangu…’akisema huyo mama, na watoto na
wale waliosikia huko umbea, na wao huitikia, ‘nata-nata, nataka mtoto wangu
Huyu mama kusikia huo umbe akajiuliza nay eye atoke nini, lakini
aliogopa mume wake anaweza kurudi, akakuta hayupo, na ikawa ni kesi, lakini
akasema;
‘Ngoja nitoke mara moja, nikaitikea mara mbili mbili tatu, huenda
nikaipata hiyo Baraka,…’akasema na kutoka kulifuatilia hilo kundi, na yeye akawa
miongoni mwa wanaoitikia,
‘Nata-nata, nataka, mtoto wangu’
Huyu mama alipofika
barabarani, akajikuta anavutika sana kumuona huyo mama anayeimbisha huo wimbo
wa maneno ya aina yake, kwahiyo naye akasogea mbele, na kusukukumana na watoto
ili apite amuone huyo mama, na akina mama wengine wakawa wanasukumana ili
kuwaikia watoto wao wawarudishe nyumbani,
huyu mama akawa nay eye anaitikia
kiitikio ;
‘Nata-nata, nataka, mtoto wangu …..’aliitikia sijui kwa ajili ya
hiyo kauli ili apate hiyo Baraka au ni kuvutika tu kuimba nay eye huo wimbo,
akawa anaimba huku anasukumana na hao watoto ili amakaribie huyo mama amuone ni
nani huyo mama, akawa sasa anamkaribi..
NB: Ngoja nisiwachanganye, soma kwa makini sehemu hiyo
WAZO LA LEO: Kuna baadhi ya ndoa huvunjika kwa tatizo
la kukosa mtoto, na mara nyingi kunapokuwepo na
tatizo hili, anayetupiwa lawama ni mwanamke. Au ikatokea kupatikana
watoto wa kike tu, au wa kiume tu, halikadhalika, lawama anatupiwa mwanamke. Tunashau kuwa ndoa ni mke na mume. Tukumbuke
kuwa kwenye ndoa kuna mitihani yake, na hilo mlipokee kama moja ya mtihani, ya
kuwa ikitokea hivyo, kaeni chini
muongee, kwanza mkubali kuwa yote ni mapenzi ya mungu, pili kujitahidi katika
njia sahihi za kitaalamu, kama vile kwenda hospitalini kupimwa kama kuna tatizo
la kiafya. Na jithidini sana kuiweka imani yenu ya dini mbele , kuwa mungu
ndiye anayejua zaidi.
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment