‘Kakuambia
nini....’mume mtu akauliza kwa hasira
‘Kasema
kuwa yote hayo ya wewe kutokuzaa, anayafahamu....’akasema mke mdogo
‘Anayafahamu
kwa vipi?’ akauliza mume mtu kwa sauti ya juu.
‘Anafahamu
kuwa wewe huzai, na….na amefanya hivyo
kwa kiherehere chako cha kutaka kuoa mke mwingine...’akasema mke mdogo.
‘Mimi
sizai, ....nani kasema mimi sizai?’ akaulize mume kwa jaziba
‘Alianiambia
kakufanya wewe usizae,...kwa vile umetaka kuoa mke mwingine...kwa jinsi
alivyofanya ni kuwa wewe hutaweza kuzaa tena, ndio maana akaenda kutembea na
mume mwingine…’akasema mke mdogo bila kuogopa, na mume akawa kama kapigwa na
shoti ya umeme, akasema.
‘Na
hiyo ni siri ya yeye na rafiki yako.....kama utambana vizuri rafiki yako
atakuambia..kwani yeye kafanya kama kukusaidia, usiadhirike...’akazidi kusema.
‘Nini
amesema nini,....kakumbia hivyo huyu mwanamke...? ‘akauliza sasa akimgeukia
mama
‘Hebu
niambie wewe mwanamke unanitaka nini mimi, kumbe yote hayo sababu ni
wewe,.....na ndio maana ukakimbilia hospitalini ili kubadilisha ukweli,
ionekane kuwa tumevunja masharti...nimelewa....’akatikisa kichwa
‘Kwahiyo
sasa unaongea kwa kujiamini, unamsimulia mwenzako kwa vile una uhakika kuwa
wewe unazaa, wewe sio mgumba tena, na mimi umeshaniharibu, ili nisizae, eeh,
...hata nikikuacha huna hasara au sio…’akasema akimuangalia mke mkubwa kwa
hasira.
‘Mume
wangu, si-sio...’akawa anashindwa kuongea
‘Ndio
hayo aliyoniambia, ni kweli si kweli haya mwambia na mume wako, je hukuniambia
hivyo....?’ akauliza mke mdogo na mama alijikuta hawezi kutamka neno, ilikuwa
kama kapigwa sindano ya ganzi.
Mume
akawa anamwangalia mama asema neno, lakini mama akawa hawezi hata kutamka neno,
pumzi ilikuwa haitoki, alikuwa akisikia vibaya..., na kwa kukaa kwake kimia,
mume mtu akaamini ni kweli…’ na kabla mama hajarejewa na fahamu na kuanza kujitetea
baba akaingia ndani….
Mke
mdogo akamuangalia mwenzake kwa zarau, akasema;
‘Unaona
umelitaka mwenyewe kwa umbea wako...’akasema mke mdogo huku mama akiwa kashikwa
na butwaa, hasira, na akahisi kama mwili unamuishia nguvu, alikuwa akijisikia
vibaya...akasimama na kuanza kutoka nje....
Tuendelee na kisa chetu
**********
Mama anamfahamu sana mume wake
na alijua ni nini kitafuata baada ya hapo, hata hivyo hakuwa na la kufanya
maana kwa jinsi alivyokuwa akijisikia, hakujali kingine tena, akakusanya nguvu,
na kuinua mguu taratabu kutoka nje, kwani alihisi kama kutapika, kiuno
kinamuuma kweli, hata kuinua mguu ilikuwa shida...
Baadaye kidogo hali ikawa
nzuri, maumivu na ile hali mbaya ikampungua, akainua mguu, akaona unakubali ,
na kwa mwendo wa kunyata akatoka nje, huku mwenzake akimuangalia kwa kumsanifu,
aliona kama mke mwenzake anaigiza
‘Hahaha ndio mwendo wa
kichawi huo, unaanza kuwanga mchana…’mke mwenzake akasema huku akiendelea
kumuangalia kwa makini.
Mama alipofika nje akakaa
kwenye kigogo kilichopo hapo nje, huwa wanakitumia kama kiti, akatulia kidogo
maana pumzi ilikuwa nzito, alitulia kidogo hadi pumzi ilipomkaa vyema, akawa
sasa anaanza kufikiri la kuanya, hasa mume wake akitoka, aliwaza hivyo akiwa kainama….alijua
kwa vyovyote kuna kupigwa hapo, naolote kutokea, mara akahisi hayupo peke yake,
akainua kichwa kuangalia.
Mke mwenzake alikuwa
kasimama mbele yake huku kashika kiuno kwa nyodo, hakujali kuwa mwenzake yupo
katika hali gani, akaanza kuongea;
‘Hahaha nguvu zote z
kichwawi leo zimegonga mwamba, hahaha, ungejiona ulivyokuwa ukitembea utafikiri
roboti, ndivyo wachawi wanavyotembea hivyo ehe….’akasema na kucheka
Mama hakumjibu akawa
kimiya akiwaza yake, lakini moyoni alitamani amtapikie huyo mtu,…..
‘Mhh, nambie mbona
umekimbia, kwanini hukusubiri upambane na mume wako, wewe si unajifanya unajua
kuongea, wewe umeanza kwa kunichongea
kuwa mimi sifanyi kazi,eeh, vikapanda vikashuka, ...ulifikiri mimi nitashindwa
kujitetea, sasa umelikoroga mwenyewe....utakiona cha mtema kuni…’akasema huku
akichezesha chezesha kiuno kwa mapozi ya nyodo.
Mama aliendelea kukaa
kimiya hakumjibu, na mke wenza akaona hafaidi, maana kazoea kujibishana,
akamsogelea mama pale alipoinama, na akaongea kwa sauti ya chini.
‘Jamaa anakuja na bakora
na rungu, anakutafuta, alivyokasirika, sijawahi kuona,...sasa wewe si ulitaka
kuondoka,...huu ndio muda wa kuondoka maana akitoka hapa uchawi wako wote
utautoa, na huko ndani kwako alipoingia kagundua mambo yako mengine, kumbe kuna
mambo yako unaficha huko ndani ehee....’akasema mke mdogo.
‘Mambo gani,....?’ mama sasa
akainua kichwa na kumuangalia mke mwenza, na alishangaakuona mume hatoki, ni
muda kaingia huko ndani.
‘Ulifikiri hutagundulikana
eehe....’akasema mke mdogo, na mama akawa anamuangalia kwa macho yaliyochoka,
hakuwa na hata nguvu ya kujibishana.
‘Hivi wewe mwanamke
unanitaka nini mimi, nimekukaribisha kwa mikono yangu miwili kwa wema, nikijua utampatia mume kile
anachokitaka....mtoto, sasa...jamani hebu niacheni mngelijua hali niliyo nayo
mungenihurumia…’akasema mama kwa sauti ya kinyonge.
‘Hahaha, mtoto,… mtoto
eeh, wakati unafahamu fika kuwa umeshafunga njia ya mimi kupata mtoto na mume
wangu, umeichukua nyota yangu ukaimeza, ili wewe uzae, mimi ndiye niliyetakiwa
kuzaa, na kutokana na mimi ndio na wewe upate mimba, sasa....sasa unasema eti umenikaribisha,
ili nimpatie mume mtoto... acha unafiki wako wewe...’akasema mke mdogo.
Mama akawa anamuangalia
huyo mke mwenza kwa macho ya kushangaa, huku mwenzake akiwa kashika kiuno
akijichezesha kwa mikogo, mama akasema;
‘Hivi wewe kweli umekwenda
shule, nasikia ulisoma sekondari,..hivi kweli wewe una dini kweli wewe, nilisikia
mume akisema wewe ni mcha mungu, haaah, siamini...’akasema mama
‘Huamini nini, kusoma
kwangu, ucha mungu wangu haukuhusu,….muhimu ni uchawi wako….’akasema
‘Wewe mwanamke….ni nini
lengo lako, hebu niambia mara moja, ina maana gani kunifanyia hivi,
unanipakazia uwongo kuwa mimi ni mchawi, sijui nimekuloga usizae, sijui nimemloga
mume wangu asizae, kwanini unakuwa Mwongo kiasi hicho,...?’ akauliza mama
‘Kwani ni uwongo, kwani
wewe sio mchawi,...ngoja mume aje akuonyeshe ndumba zako, wewe ni mchawi hata
mganga alisema hivyo, usitake kujishaua hapa, sasa nataka nikuonyeshe kuwa mimi
ni nani,….mimi namtambua mchawi hata kama akijificha vipi, siri zako zote
nimeshazifahamu, huna ujanja tena, lakini kabla hujaondoka, nataka nikupe
vipande vyako .....’akasema
‘Vipande gani, matusi na
kashifa zako nimeshazisikia una mengine zaidi ya hayo…?’ akauliza mama.
‘Nataka uijue hii sura,
unijue kuwa mimi ni nani na hata ukikutana na mimi ujipange vyema, unasikia,
huyu binti sio waleee…..unaona eeeh, hebu iangalie hii shepu, mume kazimia
hapa, na hayo mengine usiombe, hahahaha….mwenamke ovyo….’akashika pua
‘Hivi wewe mwanamke nia na
lengo lako ni nini…kwakweli wewe sio binadamu, wewe ni shetani mchonganishi tu
umeolewa kwenye familia hii kuja kuangamiza ndoa za wenzako, nikuambie ukweli,
wewe ni wakala wa shetani.....’akasema mama sasa na yeye akipandisha hasira
‘Ndoa za wenzako!!,
kwanini mimi sio mwanandoa,huyo mume kanioa mimi baada ya kuona udhaifu wako,
kwanza hujui mapenzi...mke gani hata kujiremba hujui,hebu jiangalie.., pili
ulikuwa huzai, mume akaona achukue chomb kipya..mmh, kumbe kanichanganya na
mwanga…ukani…loga….’akasema kwa kusita aliposikia mlango ukifungulia.
‘Na jingine ambalo mume alikuwa
halijui ni kuwa wewe ni mchawi, halafu unaniita mimi shetani, wewe ndiye shetani mchawi mkubwa wewe’ akasema
kwa sauti.
‘Wewe binti, chunga ulimi
wako....’akasema mama akimnyoshea kidole
‘Wewe ndiye umetaka mimi
nisizae ili wewe uonekane zaidi, umeona mimi ni mzuri zaidi yako,basi unataka
nisiwe na maana, sasa utaikimbia hii ndoa, maana kwetu nimeaga bibi wewe, na
naweza kukufanya lolote na mume akanisikiliza mimi...’akasema mke mdogo
akipiganisha viganja vya mikono.
‘Yaani lengo lako ndio hilo,
kuleta fitina, umekwenda huko kwa mganga kawadanganya, binti mdogo kama wewe
unaendekeza ushirikina, badala ya kufikiria maendeleo, ni nani kakuambia wewe
huzai, ...angalia mimi walisema sizai, mbona nimezaa, hiyo ni mitihani tu,kwanini
usiende hospitalini ukajichunguza kwanza.....’akasema mama
‘Hospitali,…kumbe …aah,
ndio mliongozana na mzazi mwenza, ili kuhakikisha mambo yameiva, na unarudi
kumbambikia mume …hahaha, wenzko hayo tulishayaona mapema,…..’akasema
‘Mimi nakushauri kwa nia
njema, mume wetu hana matatizo, nenda ukapime uone tatizo liko wapi, achana na
ushirikina,….mbona mimi nimepata mimba, huoni kuwa hao waganga wamewadanganya…..’akasema
mama kwa shida, kuna hali ilikuwa aikimjia na kuondoka.
‘Wewe si umezaa kwa
kuzini, kwa kutembea na rafiki wa mume wako, unafikiri mimi sijui yote
mliyokuwa mkifanya na huyo mwanaume nilikuwa nayaona yote, siku ya zamu yangu
unamkaribisha hawara wako kwa siri kweli si kweli, yote hayo nilikuwa nayaona,...
sikutaka kumuambia mume wetu mapema, sasa yeye mwenyewe kajionea,....mwanamke
malaya wewe.....’akasema.na mama kusikia kauli hiyo hasira ikamjaa
‘Yaani wewe binti unazidi
kunichefua, siwezi kuvumilia hayo matusi yako tena, ....sasa kama umefikia hapo, sikubali, umeniita
mchawi , bado haitoshi, unaniita malaya, huo umalaya umejulia wapi kama sio
tabia yako....kama hujafundishwa adabu kwenu leo mimi nitakufundisha
adabu....’mama akasema kwa hasira alipoona hali imetangamaa, akasimama
‘Thubutu, hebu niguse
uone, wazazi wangu wenyewe hawajawahi kunipiga wewe ...hebu
niachie...nita.....’akawa anausukuma mkono wa mama huku akijifungwa kibwebwe
tayari kwa shari, inaonekana shari kwa huyu binti ndio fani yake.
Mama mtu hakuvumilia, akamshika yule binti
bila kujali hali yake wakaanza kupigana, yule binti ni kama alijiandaa, akaanza
kumpiga mama, kwa ngumi na mateke, na mateke yake aliyaelekeza tumboni kwa mama,
hakujali kuwa mwenzake ni mja mzito.
Baba akawa anatoka na
rungu lake na bakora mkononi, akakuta wanawake wameshikana, akaingilia kati, na
kuingilia kwake, hakuwa na nia ya kugombolezea, alikuwa na hasira zake
kichwani, akaanza kutembeza bakora
Cha ajabu yeye hakujali
anampiga nani akawa anazungusha bakora inampiga huyu au yule, na mwishowe
akalizungusha rungu hili bahati mbaya likamgonga mama kichwani, mama akayumba
kwa kizunguzungu na kabla hajakaa sawa mke mwenzake akamsukuma kwa nguvu zote,
msukumo ambao ulimfanya mama akose balansi na kudondokea kwenye kuni.
Kuni alizodondokea mama
alizikusanya mwenyewe kwa ajili ya banda la mifugo. Kuni hizo nyingi zilikuwa
za miba mikali kweli, zilikuwa maalumu kwa kujengea banda la mifugo, na miba
hiyo ikamuumiza sana mama usoni. Miba ile ilimchanachana sana mama, kama mtu
aliyetumuia wembe kurarua raua uso na sehemu nyingine za mwili .
Mke mwenza akaitumia ile
miba sasa kuzidi kumchana mama usoni, ilikuwa hali mbaya , mama uso wote
ukageuka damu….akawa anaguna tu kwa maumivu
Mume naye bado alikuwa na
hasira zake akaanza kumcharaza mama kwa hasira, wakishirikiana na mke mwenza,
walipiga bila kujali wapi wanapiga, hadi mama mtu alipopoteza fahamu….
Baba hasira zikapoa, akiwa
kashikilia kimfuko cheusi, akasema;
‘Huu ndio uchawi wako sio….sasa
utaenda kuwangia kuzimu na hiyo mimba yako utaenda kuizalia kaburini..’akasema
na mke mwenza akawa anakiangalia kile kimkoba, ni kimkoba kidogo kama pochi za
akina mama, cheusi,
‘Ohoo, kumbe…umeona eeh,
nilikuambia huyu mwanamke ni mwanga, unaona hiki kimkoba ndio urithi wa
kichawi, sijui kutoka kwa bibi zake…’akasema akiogopa kukishika.
Mume akamtupia mama na
kugeuka kutaka kuondoka, mama alikuwa kalala pale chini kapoteza fahamu, huku
damu nyingi zikimvuja, na kwa hali ile, walijua wameshaua na huenda kukazuka
vita vya kiukoo.
‘Mume wangu tumeua,
usiondoke…..’akasema mke mwenza.
‘Hajafa huyu wachawi
hawafi kirahisi hivyo….’akasema mume sasa na yeye akionyesha wasiwasi, akasogea
na kumuinua mama kichwa, akaona kalegea, uso ulikuwa hautambulikani ni kama
nyama nyama zimeraruliwa.
‘Mhh, nani kamchana hivi,
wewe..umemfanya nini mwenzako…’akasema mume mtu.
‘Nimemfanya nini,….tulikuwa
tunampiga wote, miiba hiyo, ….sasa mume wangu tufanyeje….?’ Akauliza mke
mwenza.
‘Hili sasa tatizo, ……’akasema
mume akionyesha wasiwasi.
‘Ni kuambie kitu, huyu
keshakufa, cha muhimu tukamtupe huko mabondeni, ataliwa na fisi …….’akasema mke
.
Mume bila kuikiri akaona
ni wazo zuri, na kwa vile giza lilishaanza kuingia hakukuwa na watu wakipita, wakambeba
kwa kushirikiana hadi eneo la bondeni,na kumtupa kama gunia.....
WAZO LA LEO: Mwanadamu akizidisha chuki, huwa
kama mnyama, na ni bora ukutane na mnyama kuliko huyo mwanadamu,..yote haya
husababishwa na kushindwa kujenga uvumilivu na subira kwenye mioyo yetu. Pupa,
tamaa husuda hutawala nasi zetu na matokea yake, nafsi hukutuma kufanya hata
yale yasiyofaa. Tujaribu kufikiri kabla ya kutenda, tujaribu kuwa na subira
pale tunapofikwa na masahibu yenye kuchochea ubaya.
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment