Ni wakati magari sasa yanaanza kuondoka, na king’ora cha polisi kikaanza kulia ili masafara huo uweze kupita, mara simu ya Inspecta ikaita, alipoangalia mpigaji wa hiyo simu ni nani akaona hakukuwa na namba yoyote, hii iliashiria kuwa mpigaji hakutaka atambulikane, na mtu anayependa kupiga hivi kukiwa na hatari ni mmoja, Inspecta Maneno,..
Kwa mashaka akweka simu sikioni, huku akiwa kaweka kiwambo cha kunasia sauti, na kuiweka hewani
‘Ni nani mwenzangu?’ akauliza
‘Kwenye hilo gari la huyo mama kuna bomu…msimruhusu huyo mama aingie humo,..fanyeni juhudi..huyo mama akifa nitapambana na nyie, aaaah’ kukawa kimiya
'Hii sio sauti ya Inspecta Maneno, ni nani huyu...'akajiuliza
Inspecta Moto akaamrisha gari lao lisimame,akawa anataka kuwasiliana na mkuu wa msafara huo wa kuelekea huko makabaurini, lakini hata kabla hajaipiga namba ya mkuu wa msafara huo, kukasikika mlio mkubwa mbele yao …..
Endelea na kisa chetu....
Mlipuko
huo uliwashitua watu wengi, watu wakawa wanakimbia ovyo, kelele za vilio vya
tunakufa tunakufa vilisikia kwa wingi, na hata magari yakaanza kugongana kwani
madereva walishachanganyikiwa kila mmoja akiendesha kivyake na wengine hata
walikuwa hawajui wanaelekea wapi.....kwa
hali ile ya ghasia na watu kukimbia huku na kule,kusababisha ajali nyingine za
hapa na pale, ilichukua zaidi ya dakika kumi nzima hadi pale watu wa usalama walipoweza
kuituliza ile hali na wao kuweza kufanya kazi yao vyema.
Baada
ya hali ile kutulia watu majeruhi na
wengine walikuwa wamepoteza fahamu, ikawa kazi ya watu wahuduma ya kwanza
kufanya kazi yao, na kundi moja la watu waliokuwa wakihudumiwa karibu na
aliposimama Inspecta Moto likawa linaongea;
‘Mimi
nilijua yale mabomu ya Gongolamboto yamehamia hapa....’mmoja akasikika akisema
alipoambiwa hana tatizo na anaweza kuondoka.
‘Kwani
wewe huoni, ndio hay ohayo mabomu, angalia lile gari lipo wapi, kumebakia
vipande vipande utafikiri lile gari lilikuwa
limetengenezwa kwa vipande vya miti…jamani vita vibaya, kumbe wenzetu wa
gongolamboto ilikuwa hivi...’akasema mwingine
‘Mbona
hata sielewi ina maana ooh....hapana sio
lenyewe, kama ndio lenyewe, sizani kama kuna, kuna mtu kapona ….hivi imekuwaje,
ndio yale mambo ya magaidi nini…hawa watu wamehamia huku kwetu..?’ akauliza
mwingine.
‘Akipona
mtu pale huyo sio mtu.....sijui walikuwa watu wangapi mle ndani, wote watakuwa
maiti, na hata miili yao sizani kama inaweza kupatikana...’akasema mwingine na
mara kukasikika sauti za vilio, kuashiria kuwa kuna msiba.
‘Huu
sasa ni ugaidi, Osama kahamia huku tena, unakumbuka ile ya Ubalozi wa Marekani,
naona ndio hao tena...’akasema mwingine.
‘Mhh,
kila kitu Osama, magaidi si lazima Osama,….wanaweza wakawa wananchi wetu
wenyewe weney tamaa zao za utajiri…’akasema mwingine
‘Sasa
ni nani hao…..?’ akauliza mama mmoja akijaribu kusimama.
*******
Inspecta
Moto ambaye alishuhudia yote hayo kwa macho yake mwenyewe, alikuwa akihangaika
na mawasiliana na watu wake, na kwa muda huo huo, ndio akaweza kupokea simu
yake, maana mawasiliano yalikatika ghafla, akawa anawasiliana na mtu wake
aliyekuwa huko makaburini.
‘Mkuu,
mawasiliano yalikatika ghafla, huku kumtokea tatizo, kuna mlipuko mkubwa
umetokea eneo hili la makaburini…..’akaambiwa
‘What…?’
akauliza kwa mshangao kama haamini.
‘Ni
pale pale alipozikwa yule mtu aliyeletwa kipindi kile kwa ajili ya uchunguzi…’huyo
msemaji akaendelea kuongea akionyesha kuwa wasi wasi, na alikuwa kihema,kama
vile alikuwa akikimbia
‘Huo
mlipuko umetokeaje?’ akauliza Inspecta kwa mshangao, maana hapo alipokuwepo
kulimuhitajia na huko sasa kuna jambo limetokea anahitajika pia awepo, hapo
akamkumbuka rafiki yake Maneno, kwani angelikuwepo kazi hiyo angelifanyika kama
atakavyo.
‘Wakati
tumeamua kwenda kupachunguza pale mahali, kama ulivyotuagiza, kabla
hatujakaribia hilo eneo , mara ghafla mlipuko mkubwa ukatokea eneo hilo, na lile
kaburi likazama kabisa, na moto mkali ukawa unatokea hapo kwa ndani, tuliwaita
watu wa zima moto, na tunashukuru walifika haraka, na kikosi cha askari wa kazi
hizo, sasa hivi wapo wanafanya kazi yao, wakichunguza chanzo cha hilo bomu,
ndio hivyo mkuu,...
‘Imetoka
saa ngapi, na kwanini mawasiliano yakate ghafla, hawa watu wana uwezo gani wa
kufanya hivyo...?’ akauliza naalipotajiwa saa, akagundua kuwa ni muda ule ule
ambapo bomu la kwenye gari ulipotokea,
inaonekana ilipangwa itokee muda huo huo.
‘Mkuu
ulipotokea mlipuko, kila mmoja alitafuta usawa wake wa usalama, hata mimi kwa vile nilikuwa msitari wa mbele kuelekea
pale makaburini, ilibiai nilale chini na nilipoona naweza kusimama, nikatafuta
uelekeo salama, maana sikujua ni nini kitafuata baadaye, nilirudi sehemu hiyo
nikaona moto usio wa kawaida kutoka ardhini kwenye eneo hilo ambalo lilikuwa na
kaburi.
‘Cha
ajabu ndio hicho, nilipojaribu
kukupigia nikaona mawasiliano hakuna, hadi
ikapita dakika kumi hivi, ndio mawasiliano yakaanza kupatikana...’akasema
‘Nilikuwa
kwenye mihangaiko mingine, hata mimi nililiona hili, kwani nilikuwa najaribu
kuwasiliana na makao makuu, lakini kukawa hakuna mawasiliano....’akasema Moto.
‘Mkuu
ukifika hapa sasa hivi utakuta ni handaki la kwenda chini, na kwa vile moto
haujatulia vyema, hatujaweza kugundua kuna nini ndani yake, bado wanahangaika
kuweka mambo sawa, kwahiyo sikuweza kukuelezea vyema humo ndani kupoje, ila ni
handaki,..bomu hilo limechimba hasa....’akasema huyo mtu wake
‘Oh,
endeleeni kuangalia eneo lote hakikisheni hakuna mtu anayekimbia , angalieni
eneo lote kuzunguka ukuta wa makaburini, nahisi kuna sehemu ambapo hao watu wapo,
wapange vijana vyema, japokuwa kikosi cha mambo kama hayo wapo huko, lakini sis
tunahitajika kwa ajili ya kuwasaka hao watu, wasiwazui kufanya akzi yenu, ngoja
niwasiliane na makao makuu, tuone tutafanya nini,....’akasema
‘Sawa
mkuu, na sasa hivi ndio nimesikia huko nako kumetokea mlipuko, mpo salama kweli
mkuu, je kuna watu wamefariki?’ akauliza huyo askari
‘Ndio
mlipuko huo umetokea sambamba na huo wa huko, kwa muda ulionitajia ndio muda
ambao mlipuko kwenye gari ulitokea huku,...na hali ilivyo, hakuna uhai kwenye
hilo gari, hata sisi huku tunasubiri hali itulie, gari hilo limeungua kabisa, ni
gari ambalo kumetokea huo mlipuko, .....’akasema na muda huo alikuwa akisogelea
pale kwenye hilo gari akikagua kwa macho, lakini askari wa kazi hizo akawa
anamzuia.
‘Oh,
mkuu poleni sana, je muheshimiwa hakimu na watu wake wapo salama?’ akauliza
huyo askari wake
‘Wapo
salama, ...nyie endeleeni huko mniarifu kinachoendelea, maana siwezi kujigawa,
na makao makuu naona hawapatikani, sijui kuna nini huko, simpati mkuu wala
msaidizi wake…, toka jana imekuwa ni tatizo kumpata, sijui kapatwa na nini, sio
kawaida yake....’akasema akijaribu kumpigia kwa simu nyingine.
‘Hata
huku wanamtafuta hapatikani mkuu, huenda kapatwa na dharura, lakini nakumbuka
aliondoka akiuguliwa na mzazi wake, kwani alirudi....?.’akauliza
‘Nyie
endeleeni tu, nitaona jinsi ya kumpata, ila muwe makini maana hatujui lengo lao ni nini, na ionavyoonekana
wanataka kuhakikisha kuwa hakuna ushahdi wala mashahidi,...’akasema Moto, huku akiendelea kukagua kwa macho kwenye lile
gari, akatikisa kichwa na kusema;
‘Sawa
mkuu..’akasema huyo askari
Eneo
sasa likazungukwa na maaskari kuhakikisha hakuna janga jingine, na magari yote
yaliyokuwepo hapo yakachunguza kusije kukawa na bomu jingine, na kikosi cha
uchunguzi wa mabomu kikawa kinaendelea kufanya uchunguzi wake, na kwa taarifa
za haraka. walisema bomu hilo lilitegewa kwenye simu kinamna amabyo mtu huwezi
kugundua, na wote waliokuwemo kwenye gari hilo ni marehemu hata miili yao
haiwezi kutambulikana tena.
Taarifa
hiyo ilimfanya Inspecta Moto ambaye kwa muda huo alikuwa njiani kuelekea huko
makaburini, kuwaarifuu watu wa uchunguzi, ambao walikuwa wakichunguza simu
walizopelekewa, wawe makini na hizo simu.
‘Mkuu
tumehakikisha hakuna kitu kama hicho, hazina bomu kabisa ...’wakasema
‘Hao
watu ni wataalamu wa hali ya juu, wanaweza kuweka bomu kwa njia ya mitandao,
kinachotokea ni hali ya hewa na viundo-mbinu vya miozi, vilivyopandikizwa humo, ambavyo
husababisha mlipuko…huwezi kuviona, ni utaalamu wa aina yake…’akasema Moto
‘Mkuu
tunaendelea kuchunguza, kama kuna kitu kama hicho, naona ha watu wanatumia
ugaidi wa hali ya juu wa kupiga kwa kutumia setelaiti na mionzi ni
hatari,lakini tunao wataalamu hapa wanaendelea kuhakikisha kuwa kitu kama hicho
hakipo, na ishara ya mawasilioana
haionyeshi wapi mpiga au mtumaji wa yale mawasiliona yametokea wapi, kwa
jinsi ilivyoweza kupatikana lakini sio kwa uhakika, ni kutokea baharini,
muelekeo wa makaburi ya Msasani….
‘Baharini?’
akauliza kwa mshangao
‘Ndio
mkuu, ndio tumeweza kugundua hivyo, lakini hakuna uhakika zaidi….’akasema
Inspecta
akawa sasa amefika eneo la makaburini na kuanza uchunguzi wa kina, akawa yupo
na kundi la maaskari wengine wakikagua lile handaki ambalo mwanzoni lilikuwa ni
kaburi.
‘Mkuu
hapa palikuwa sio kaburi, mnaona huku, hili ni handaki, kuna njia ya kuelekea
nje ya huu ukuta, ila kwa vile kumebomoka, njia yote imezibwa, unaona huku
...’akasema mtu ambaye alikuwa chini pamoja na kikosi maalumu.
Ikabidi
Inspecta na baadhi ya watu watoke nje ya ule ukuta kukagua huko kulikuwa na
nyumba, na watu wamezunguka wakishangaa, kulikuwa na moshi unatokea kwenye hiyo
nyumba, kuashiria kuwa kuna moto unawake ndani, na wakati huo akili yake ilikuwa
ikifikiria kauli ya mtu wa uchunguzi kuwa mawasiliano yametokea baharini,
akatupa jicho kuangalia lile boti, akaliona bado lipo na kuna askari wapo
tayari kwa lolote.
‘Hii
nyumba ni ya nani?’ akauliza Inspecta, na wakati huoa moshi ulikuwa ukizidi
kuongezeaka kutoka kwenye hiyo nyumba
‘Ni ya jamaa mmoja mvuvi, huwa muda mwingi
hayupo, haonekani mara kwa mara humo, nyumba hii imekuwa kama imehamwa, ni mara
chache sana unasikia kuwepo na mtu humo ndani, sasa tunashangaa kuona huo
Moshi, na umeanza pale kuliposikika mlipuko wa huko makaburini, watu walikuwa
wamekimbia, sasa hivi ndio wamerudi na ndio tukaona hivyo...’akasema jirani wa
hiyo nyumba.
‘Huyu
mvuvi mnafahamu...?’ akaulizwa
‘Tunamfahamu
kwa kumuona , huwa haongei na watu, hufika na kuingia ndani, akiingia humo
hatoki, na anavyotoka huwezi kujua katka muda gani, kwani unaweza kumuona
akiingia lakini akitoka humuoni, huwezi kujua kaenda wapi, ...’akasema huyo
jirani.
‘Anafananaje?’
akaulizwa
‘Mhh,
ndugu yangu, mtu huyo muda wote kavaa mawani, na kofia pana, hata sura yake
siwezi kumfahamu ipoje, na wakati mwingine akiwa katokea baharini huwa na na
koti linalimfunika unaweza kuona kidogo usoni, ..labda ukawaulize wavuvi huenda
wanaweza kumtambua...’akasema huyo jirani akionyesha kuwa na wasiwasi
‘Sasa
umejuaje kuwa ni mvuvi?’ akaulizwa
‘Kwa
vile akiingia humo huwa kabeba matenga ya samaki, au vifaa vya uvuvi ndio
hivyo, lakini kuna kitu mimi kinanitia wasiwasi siku nyingi nimekuwa nikiwaambia
wenzangu,..’akasema huyo jirani
‘Kitu
gani hicho?’ akauliza
‘Huyu
mtu hafanani kuwa mvuvi….kwa jinsi anavyoonekana japokuwa kavalia hayo mavazi,
lakini wavuvi tunawafahamu hali zao,..huyu bwana hata….labda ndio hao wavuvi
matajiri, jana nilimuona akiwa katika hiyo hali, kavalia koti,akionekana na wasiwasi, akaingia humo ndani hajawahi kutoka…’akasema huyo mtu
Inspecta
aliposikia hivyo, akawa na hamasa ya kuonana na huyo mtu, hata hivyo, hali ya hiyo nyumba ilionekana kuwa hatarini, kulikuwa na kila dalili kuwa kuna moto ndani tena mkubwa,
'Tuvunje tuingie....'amari ikatolewa, na Moto akiwa na kikosi chake ikabidi wavunje hiyo nyumba, waingie ndani, kwani hali ilivyo ni tofauti na
jinsi watu walivyodai kuwa ni vipande vya bomu vilivyodondokea humo ndio vinaleta moshi....
Mlango
ulipovunjwa, tu, watu wakakaribishwa na mbaya, ilikuwa ni harufu ya gesi, na ghfla mlipuko mkubwa ukasikika…….
WAZO LA LEO: Moyo wa mwanadamu
ukishatawaliwa na dhuluma utu huondoka kabisa na kinachobakia ni chuki, huruma inakuwa haipo tena, na hapo ni bora
kukutana na mnyama hatari kuliko huyo mwanadamu. Ndio maana ni vyema mara kwa mara tunahitajika
kusaidiana kwa kukatazana mabaya, na kuelekezana mema. Kwani ubaya ukizidi,
amani haipo tena. Tujaribu hasa viongozi kuwa waadilifu, tuhakikishe haki na
ukweli vinakuwa ndio dira yetu.
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment