'Ndio twendeni nikawaonyeshe wapi alipo mwanangu,….ili na mimi nife kwa amani, …’akasema
huyo mama.
‘Twende
wapi mama,watu wamefika huko wanasema hakuna mahali ambapo mtoto wako aanweza kupatikana, ni wapi mtoto wako yupo, anawezaje
kuishi huko makaburini….?’ akaulizwa.
‘Mnaogopa
eeh, nilishawaambia sharti la mtu kufika hapo alipozikwa mtoto wangu ni moja
tu….hahaha. mumeanza kuogopa eeh....'akasema akitikisa kicha
'Lakini kwa sasa tuliache hilo, ...... muhimu ni nyie mfike huko mkutane na huyo
mnayemtafuta , au sio, na…na ..na tukichelewa, hatutamuona tena, na wote waliopo naye
huenda ikawa ndio mwisho wao wa kuonekana hapa duniani…..twendeni
haraka…..’akasema.
‘Ndugu
muheshimiwa hakimu, tunahitaji kibali chako, mahakama hii ihamie huko makaburini
ili tuone ukweli wa hili tukio…..’akasema muendesha mashitaka, lakini watetezi
wa hiyo kesi, wakakataa hilo ombi, na kusema hayo ni mambo ya kishirikina,
hakuna mtu anayeweza kuishi makaburini na huyo mama kacjhanganyikiwa hajui
anachokiongea…
Hakimu
akatulia kwa muda na baadaye akauliza;
‘Je
askari waliokwenda huko wanasema nini?’ akauliza
Akafika
Moto na kuteta na muendesha mashitaka, na waakti wanateta yula mama akasema kwa
hasira;
‘Twendeni
mbona mnachelewa,msije mkanifanya nife kifo kibaya,twendeni ili nife kwa amani,
twendeni haraka, mume wangu huyoo, anakuja kunichukua, twende askari wangu kabla muda haujaisha….’akasema na kugeuka huku na kule
akasema;
‘Askari
wangu yupo wapi jamani,....nataka mimi mwenyewe nitangulie mbele, kama nyie mnaogopa, mwaogopa kufa nyie eeh, ….'akasema huku askari wake akimuendesha kutoa nje ya mahakama.
Haya tuendelee na kisa chetu....
************
Kutokana na unyeti wa kesi yenyewe, watu walizuiwa
kuongozana na msafara uliokuwa ukielekea huko makaburini, hata hakimu mwenyewe
ilimchukua muda sana kukubaliana na
shauri hilo, la kuhamishia mahakama makaburini, lakini baadaye akasema;
‘Natumai waendesha mashitaka mnajua dhima mnayoibeba, hatutakubali kupoteza muda wetu bure, na muwe
na uhakika kuwa kweli huko tunapokwenda tutamuona huyo mtoto wa huyu mama…na
kweli mna uhakika kuwa mama huyu ana akili timamu kama mlivyosema...sitaki
kuwakumbusha kuhusu sheria, kuwa mtoa ushahidi ni lazima awe na akili timamu....’akasema
Muheshimiwa hakimu.
‘Muheshimiwa hakimu, pamoja na utu uzima wa huyu mama,
pamoja na kuchanganyikiwa kwake, lakini sio wakati wote anakuwa kachanganyikiwa, na haya anayoyaongea
kwasasa yana ukweli muheshimiwa...'akasema kutulia kidogo.
'Ndugu muheshimiwa hakimu sisi tuna imani kubwa sana kuwa huyu mama alichosema kinaweza
kutufikisha mwisho wa kundi hili haramu….’akasema muendesha mashitaka, na
watetezi wakasimama kuipinga hoja hiyo wakisema;
‘Ndugu muheshimiwa hakimu, sisi bado hatujakubaliana na
maamuzi ya waendesha mashitaka, kwa vile huyo mama kisheria anafahamika kuwa ni
mgonjwa wa akili, na sheria haimlazimshi mwenye matatizo ya akili kutoa
ushahidi mahakamani, lakini wenzetu wamamlazimisha huyo mama, lakini pia
kiukweli hebu tuliangalia hili jambo kwa makini, itakuwaje mtu aishi makaburini…muheshimiwa hakimu hawa watu wanataka kupoteza muda tu......’watetezi
wakahoji.
Muheshimiwa hakimu akageuka kumuangalia muendesha mashitaka, na watetezi wakawa wanaendelea kuongea;
‘Lakini pia muheshimiwa hakimu sheria na taratibu za
kimahakama zinaendana na kumbukumbu na ushahidi, hapa tuna kumbukumbu zote
zinazoonyesha kuwa huyo mtoto wa huyo mama alifariki na kuzikwa, na stakabadhi
zote tunazo, tunahitajia ushahidi gani mwingine, sisi tunaona ni upotezaji wa muda wanaotaka
kuutumia hawa wenzetu….’wakaongea upande wa utetezi na muendesha mashitaka
akajibu hoja hiyo kwa kusema;
‘Hizi ni mbinu za hili kundi, yote hayo yalifanyika
kiujanja ujanaj, ili mtu huyo aweze kufanya mambo yake bila kupatikana, sisi
tuna uhakika na tunachokifanya, kwahiyo tunaona ni vyema tukaenda huko ili tuhakikishe sote,
sioni kwanini kuwe na kigugumizi kwa hilo, labda na nyie mnaogopa kuwa ukweli
utajulikana….’wakaambiwa watetezi .
‘Hatuogopi lolote tunachohitajia sisi ni sheria
zifuatwe, ndio maana wakati wote tumekuwa tukidai kuhusu sheria zinasemaje
tusiwe wa kwanza kuzivunja sheria …hebu tujiulize,je sio kweli kuwa mtu aliye
na matatizo ya akili haruhusiwi kutoa ushahidi mahakamani, je huyo mama hana matatizo hayo, nab ado tunataka
kupoteza muda muhimu wa mahakama ...’ wakazidi kujitetea. watetezi.
‘Nani kawaambia nina matatizo ya akili, nyie watoto
mnafikia hatua ya kunitukuna mbele ya mahakama yenu, muishie hapo hapo, mimi
nina akili zangu timamu, na sitaki muendelee kunitukana, mimi sio mwenzawazimu,
uwendawazimu huo wamekuwa wakiniletea hawa watu kwa kundunga madawa yao ya
ulevi...sasa twendeni huko tuone ni nani mwendawazimu nyie au mimi...’akasema
huyo mama.
‘Muheshimiwa hakimu.....’watetezi wakawa hawajakata
tamaa,...
Hatimaye muhehimiwa hakimu akaongea na wasaidizi wake,
wakakubaliana mahakama ihamishiwe huko kwa muda, na safari ya kuelekea huko
mhakamani ikaanza, watu wanaostahili kwenda wakaanza kuingia kwenye magari
chini ya ulinzi mkali.
Yule mama akaingia kwenye gari lake na walinzi wake, na
Moto akaingia kwenye gari lake, lakini alihisi wasiwasi, hakupenda Yule mama
abakia na walinzi wake tu, lakini hakuwa na la kufanya kwa vile mambo yote
yalikuwa yanasimamiwa na mahakama.
Moto akiwa ndani ya gari lake tayari kwa safari ya
kuelekea huko mahakamani, akaanza kuwasiliana na watu;
‘Mambo yanakwendaje huko?’ akauliza Moto, kuwauliza
vijana wake.
‘Mpaka sasa hakuna jipya, …’akaambiwa.
‘Je zile simu za hao watu, bado mnazo?’ akauliza.
‘Ndio mkuu, lakini kuna kitu cha ajabu sana, kwenye hizi
simu….’akaambiwa
‘Kitu gani cha ajabu…?’ akauliza.
‘Ulituambia tuzizime na kuhakikisha hazifanyi kazi,
lakini tunaona kuna kitaa kidogo kwenye hizi simu, hakizimi kabisa…’akasema.
‘Hakikisha kuwa mumezizima kabisa, toeni mpaka betrii
yake…’akasema moto.
‘Sawa mkuu……’akatulia na baadaye akasema.
‘Tumezizima, na hata kutoa betrii, lakini kuna taaa
ndogo inaonekana kuwaka wakati wote….’akasema huyo askari.
‘Hakuna jinsi ya kuizima hiyo taa, kitakuwa kinawaka kwa
kutumia nguvu gani, hebu zichunguzeni vyema, Toani betri kabisa, na hakikisha
hiyo taa haiwaki kabisa….’akasema Moto, na ilichukua muda na baadaye akasikia
mtu wake huyo akiongea.
‘Ni ajabu kabisa, hata baada ya kutoa betrii, lakini bado
kitaa hicho kinawaka nahisi kinatumia
solar….’akasema.
‘Ziwekeni ndani ya mfuko wa palasti na mpeni askari
mmojawapo azipeleke chumba cha uchunguzi, nina wasiwasi na hizo simu, inaweza
ikawa ni chombo cha kunasia matukio…’akaambiwa namoyoni akasema;
‘Inawezekana
ikawa ni bomu…lakini sizani’ kukawa na ukimya Fulani baadaye akaambiwa;
‘Tumeshazitoa kwa kijana wetu aziwahishe huko ofisi ya
uchunguzi, lakini mtalaamu tuliye naye hapa anasema sio bomu, ila inawezekana
kabisa ikawa ni chombo cha kunasia matukio, kwahiyo inavyoonekana muda wote hao
watu walikuwa wakituona…’akasema
‘Kama mlikuwa naye kwanini hamkumuuliza mapema?’
akaambiwa
‘Ulituambia tusimuhusishe mtu yoyote mpaka utuambie
mkuu, tumefuata amri yako mkuu…’akajitetea huyo askari.
‘Halafu huyu mtaalamu wetu, kasema kwa kutumia hiyo
simu, wanaweza kutambua wapi walipoweka
vyombo vyao hivyo vya kunasia hayo matukio, na wameshaanza kufuatilia…’akasema
‘Sawa hilo lifanyike haraka sana, kwani hatuna muda wa
kupoteza tena…’akasema Moto.
Ni wakati magari sasa yanaanza kuondoka, na king’ora cha
polisi kikaanza kulia ili masafara huo uweze kupita, mara simu ya Inspecta
ikaita hakukuwa na namba yoyote kuashiria kuwa mpigaji hakutaka atambulikane,
Inspecta akaweka kiwambo cha kunasia sauti, na kuiweka hewani
‘Ni nani mwenzangu?’ akauliza
‘Kwenye hilo gari la huyo mama kuna bomu…msimruhusu mama
huyo aingie humo,..fanyeni juhudi..huyo mama akifa nitapambana na nyie, aaaah’
kukawa kimiya, na Inspecta Moto akaamrisha gari lao lisimame,akawa anataka
kuwasiliana na mkuu wa msafara, lakini hata
kabla hajamaliza kusema, kukasikika mlio mkubwa mbele yao …..
WAZO
LA LEO: Unapotoa kwa nia kusaidia, hakikisha unatoa kile kilicho
kizuri, kile unachokipenda wewe mwenyewe na usitoe kwa ria, kwa nia ya kujionyesha
kuwa unazo. Hili pia ni pamoja na pale unapofanya jambo kwa nia ya kuwasaidia
wenzako iwe jamii vikundi, au hata kwa
mtu mmoja, fanya hivyo kwa nia njema ya kusaidia.
Unajua, wakati mwingine
kujitangaza kuwa umesaidia watu au kundi, au mtu, unakuwa kama unawazalilisha wapokeaji, hujui wanajisikieja moyoni mwao, japokuwa ni kweli huenda hao watu , au kundi au mtu wanastahili kusaidiwa, swali hapa ni kwanini mpaka tujitangaze,
au kuwatangaza wanaosaidiwa….
Ni mimi:
emu-three
2 comments :
Jamani unatubania unaweka kiduchu sana, hata ivo twashukuru na hongera sana
Kwakweli Kisa kinazidi kunoga haswa,nasubiri muendelezo wa kesho,all the best
Post a Comment