Watu wanne, wakiwa watu wa usalama, walifika hoteli ya Paradise, ambapo waliambiwa kuna sehemu anaishi mama wa mtoto ambaye anamiliki hoteli hiyo. Kuna tetesi kuwa huenda mmiliki wa hoteli ya Paradise, ana mafungamano na kundi haramu, linalosadikiwa kuwepo nchini, na huenda huyu mtoto alikuwa ndiye kinara wa kundi hilo haramu. Lakini kwa taarifa rasmi mtu huyu ni marehemu.
Walipofika
eneo hilo ambalo ni eneo la hoteli ya Paradise, wakajieleza na kueleeka eneo la
sehemu ambayo wameambiwa mama huyo anaishi, na walipofika hapo wakazuiwa na
mlinzi aliyekuwa mlangoni akiwa na silaha. Alipoelezwa kusudio la watu hao
kufika hapo, huyo mlinzi akasema;
‘Docta
kasema huyu mama hastahili kusumbuliwa kutokana na hali yake….’akasema
‘Tuliomba
kibali mapema, tukaambiwa tuje leo, na
hatuna nia ya kumsumbua, sisi ni watu wa usalama, …’akasema msemaje, na yule
mlinzi akazidi kusisitiza kuwa amri iliyowekwa hapo na dakitari wa huyo mama ni
kuwa asisumbuliwe mpaka mwenyewe awepo, au atoe kibali.
Maneno
ambaye alikuwa kimiya, akasema;
‘Usiwe
na wasiwasi hatapata usmbufu wowote, mwambie huyo aliyekuzuia kuwa mimi Maneno
nipo….’akasema Maneno, na yule mlinzi akachukua simu yake na kupiga namba, na
mara akamgeukia huyo Maneno na kumpa hiyo simu.
‘Ni
Maneno, nimekuja kuongea na mama kuna mambo ya kiusalama tunahitajika kuyaweka
sawa….’akasema na kusikiliza kwa muda, baadaye akasema.
‘Usitie
shaka tupo pamoja, …’akamrejeshea yule mlinzi, na yule mlinzi akaipokea na
kusikiliza, halafu akageuka na kwenda mlangoni, akabonyesha kitufe, na ukapita
muda, mlango ukafunguliwa.
Walipoingia
ndani, wakaelekezwa wapi waende na kukaa, na hapo wakaulizwa wanahitaji
vinywaji gani, na kila mmoja akataja kinywaji chake wakaletewa na kuanza
kunywa. Baadaye akaja mtu mmoja na kusema;
‘Mama
anakuja, lakini tunaomba muwe wastahimili, msimuulize sana maswali ya
kumchosha, na kawaida yake akitoa amri sisi tunahitajika kuitimiza…’akasema mtu
mmoja aliyekuwa na jambia, au panga kiuononi na upande mwingine bastola.
‘Hamna
shaka….’akasema Maneno, na kweli kukaonekana kigari cha kukokotwa na mikono…kilikuwa
kikijiendesha chenyewe, japokuwa kulikuwa na mtu nyuma yake, akiwa kavalia kama
yule mtu mwingine aliyewakaribisha, naye akiwa na jambia, kiuoni, na bastola
upande mwingine.
Kwenye
kile kigari, alikuwepo mama akiwa kakaa kwenye hicho kigari cha bei mbaya, na
kikawa kinasogea karibu na pale walipokaa hao watu wa usalama wa polisi, na kwa
heshima wakasimama.
‘Heshima
yako mama…’wakasema.
‘Heshima
zenu nyie watumwa wa watu wengine, niambieni mumefuata nini hapa, mnataka nini
hapa, kama mnamtaka mwanangu yupo kaburini, nendeni mkafukue mtamuona, mzima
kabisa…’akasema na wale maofisa wakawa wametulia na huyo mama akasema;
‘Mnasubiri
nini, mumeshawapa hawa wau damu ya shetani?’ akauliza
‘Ndio
mama…’akasema huyo aliyewapokea.
‘Sawa
kabisa, haya anzeni kuongea…’akasema.
‘Mama
tulikuja hapa kukuuliza kuhusu vitega uchumi vilivyokuwa vikimilikiwa na mtoto
wako, nasikia ulisema hutaki mwanao aondolewe kwenye orodha ya wamiliki, na
wakati hayupo hai, ni kwanini mama..?’ akaulizwa na mmoja wa maofisa.
‘Nani
kawaambia kuwa mwanangu hayupo hai, mumemuua nyie….niambie ni nani kamuua mtoto
wangu…?’ akauliza akiwaangalia maofisa hao akipepesa pepesa macho.
‘Mama
kama ulivyosema mtoto wako yupo kaburini, kuna mtu anaweza kupelekwa kaburini
kama hajafa?’ akaulizwa.
‘Sio
wote waliopo makaburini wamekufa,..hivi hamuoni, kwani mimi hapo nipo wapi, si nipo
kaburini , hamlioni hili kuwa ni kaburi, hebu angalieni tofauti ya hapa na huko
nje,…au na nyumba nyingine,…. Lakini mnanionaje mimi sijafa, ..na yeye
kapalekwa huko hajafa, tatizo ni lazima uwe vile uondokene na roho yako,
wanaita kufa, hebu niambieni kama engalikufa na kila kitu kingelikufa au sio.
Mumeliona
hilo jumba kuwa hapo nje, ni la nani, ni lake, mnaifahami miradi yake mingi,
inaongozwa na nani, mbona inaendelea kama kawaida…kuweni na akili nyie….wajinga
wakubwa nyie….’akasema na kukohoa mfulululizo.
‘Mama
tunaweza kupata picha ya mtoto wako?’ akasema mmoja wa maofisa.
‘Sihitaji
picha yake, mimi namfahamu mwanangu, kwanini niwe na picha yake,mwanangu yupo
hapa moyoni,…kama mnataka pasueni hapa moyoni mwangu kama hamtamuona…’akasema
akifunua kifuani kuonyesha.
‘Mama
samahani sana kwa usumbufu, lakini nikuulize swali mtoto wako alizikwa sehemu
gani, maana tumeuliza sana , hatujaweza kuonyesha kaburi la mtoto wako?’
akaulizwa
‘Mnataka
niwapeleke ehe, huko anatakiwa maiti, kwanza mfe ndio niwapeleke, askari wangu
upo….’akaita na yule mtu aliyekuwa akimuendesha kwenye kigari akaja na kusema;
‘Nimekuja
mama..unasemaje?’ akauliza yule askari akija kusimama mbele yake.
‘Una
jambia lako hapo tayari….?’ Akauliza na yule askari kwanza akatulia na
kuwaangalia wale, akawaonyesha ishara ya kuondoka,, halafu akasema;
‘Ninalo
mama…’akasema akishika mpini wa lile jambia lililopo kiuoni mwake.
‘Wewe
ni mtu wangu na unanitii au sio?’ akauliza
‘Ndio
mama, …’akasema huyo askari
‘Kila
ninalokuambia fanya unafanya…au sio?’ akauliza
‘Ndio
mama,…’akasema
‘Sasa
nataka hawa watu wakazuru kaburi la mwanangu, na msharti ya huko siunayajua?’
akaulizwa
‘Ndio
mama ninayajua…’akasema yule askari
‘Masharti
yake ni nini?’ akaulizwa
‘Ni
lazima mtu huyu awe ni marehemu, atengane na roho yake, awe na roho nyingine ya
ya kuzimu…’akasema huyo askari.
‘Anaipataje
hiyo roho ya kuzimu?’ akaulizwa
‘Ni
kwa kufa kwanza…..’akasema yula askari akiwa kama anataka kulitoa lile jambia
kiuoni
‘Sasa
hawa watu wanataka kwenda huko kuzimu, wanataka kumtembelea mtoto wangu, eti
mtoto wangu yupo wapi?’ akauliza.
‘Makaburini….’akasema.
‘Sasa,
waulizeni hawa watu je wapo tayari kwenda huko, na wapo tayari kwa msharti yake…’akasema
huyo mama.
Na
yule mlinzi akawaangalia wale maofisa akipepesa macho yaliyojaa ujasiri,
kuonyesha kuwa yupo tayari kwa lolote, na wale watu wa usalama japokuwa
walijitahidi kuwa wakakamavu, lakini kwa ile hali, walishaanza kuonyesha
wasiwasi.
‘Mumesikia
jamani, ..mpo tayari…’akasema huyo askari, na wakati huo mkono wake umeshikilia
mpini wajambia lililokuwa kiunoni.
‘Sikiliza
mama …sisi ni watu wa usalama, hatukuja hapa kwa shari, na nia yetu ni njema
kabisa, kama hutaweza kutusaidia kwa
hilo tunaondoka mama…’akasema
‘Aaah
subirini, hatujamalizana na nyie bado, msije kusema mama ni mkorofi, …mlichotaka
mtakipata, lakini masharti yake ndio hayo, toka alipofariki mwanangu nimekuwa
nikiwauliza watu kama kuna mtu anataka kuliona kaburi la mwanangu, na wakisema
sawa, nawapa hayo masharti, lakini wanaogopa..hivi kwanini mnaogopa kufa,
wakati ni lazima kila mtu atakufa…’akasema
‘Mama
tumemaliza tunaondoka…’akasema Maneno.
‘Na
wewe sio Maneno wewe?’ akauliza aliposikia sauti ya mmoja wa maofisa, akageuza
kichwa kumuangalia.
‘Ndio
mimi mama…’akasema.
‘Umeamua
kunisaliti au sio?’ akauliza
‘Hapana
mama…’akasema Maneno
‘Ole
wako,…..siku zako zinahesabika, karibuni utakwenda kulizuru kaburi la mwanangu,
hakuna anayeweza kumsaliti bibi Kikagula abakie hai, mimi ndilo jina
aliloniachia bibi yangu, Kikagula,nimerithi jina lake hahahaha…’akasema na
kujipiga kifuani.
‘Haya
kama hamna maswali mengine ondokeni na msirudi hapa tena…’akasema kwa sauti ya
hasira, na wale maofisa wakaanza kuondoka, na yule mama akasema.
‘Wewe
Maneno, umenisikia?’ akauliza
‘Ndio
mama…’akasema Maneno.
‘Mjinga
mkubwa wewe, unafikiri mali zinapatikana kirahisi hivi, hivi mimi nimekuzaa
wewe, mpaka nikulee kama mwanangu,ufaidi mali za bure bure…mjinga kweli kweli
wewe, mtoto huna shukurani wewe, kila kitu nimekupa, leo hii unanisaliti,
utakufa kama walivyokufa wengine mjinga mkubwa wewe…’akasema huyo mama
akionyesha sauti ya kukasirika.
‘Mama
nimekosa….’akasema Maneno
‘Waambie
na wenzako , mimi Ndiye Kikaguala, sifi…watakufa wao, mimi ninadunda tu,na
mwanagu ananiangalia huko alipo, ananiona..nyie hamumuoni, hahahahaha…wajinga
wakubwa nyie, mwanagu anaijua dunia, akaitengeneza ,kaiweka vizuri, na kila
anayetka kuwa naye, anafurahi tu, maisha mazuri, utajiri, lakini ole wake atakayemsaliti…..ni
lazima atafanya nini?’ akauliza na wale maofisa wakakaa kimia
‘Nimesema
nini nyie watu?’ akasema kwa ukali na Maneno akasema
‘Atakufa…’
‘Hahahaha,
hao wengine hawataki kujibu eehe, askari, unasubiri nini fanya kazi yako…wapanue
midomoo yao, ….’akasema akijaribu kujiinua kwenye kile kiti, na yule askari
akatoa panga, ambalo ni kama jambia.
Wale
watu wa usalama walipoona hivyo, wakaanza kutimua mbio kuondoka, na yule mama
akaanza kucheka na kutetemeshwa mwili mzima
‘Hahahahaha….mimi
kikaguala, hakuna anayeniweza mimi, na dunia yangu itazunguka itazunguka,
hahaha, na kila mmoja atatii amri moja, kama hutaki, wewe ni adui, ukikubali,
wewe ni rafiki, lakini hakuna rafiki wa kudumu, ukikiuka mashari wewe ni adui….’
Akatikisa kichwa kama kukubali, na ghafla akawa kama kshitulia na kuanza kupiga
ukulele
‘Oooh,ooh,
naumia, ooh, nihurumie, oooh, ..naumia….hapana, nisamehe mimi, mwanangu, …ooh,
alimuua, ndio,…alikosea mshemehe, nisamehe na mimi, ndio nili…ooh, nili….ooh,
naumia,….’alianza kulalamika, na haraka yule mlinzi akamsogelea na kutoa
sindani akamdunga begani, na haikuchukua muda yule mama akatulia na kuonyesha
kuwa amelalala.
Na
wakati huo huo mlango ukafunguliwa, akaingia docta akiwa kaandamana na jamaa
moja mwenye midevu…
WAZO LA LEO:Jitahidi sana
katika maisha yako kutokumdhulumu mtu jasho lake, uwe ni mwekezaji una
wafanyakazi wako walipe stahiki zao kwa haki, awe ni mfanyakazi wa ndani mlipe
ajira yake halali, na wafanyeni wafanyakazi wenu ni sehemu ya familia, ni
sehemu ya ile kazi…acheni kasumba ya ubosi na utwana. Hao waliopo chini yako sio
watuma wako.
Tukumbuke
tukifanya hivyo, kwa uadilifu na utawala bora, wanaoongozwa watajiona ni sehemu
ya hiyo kazi, watawajibika bila kusimamiwa. Na wewe uliyechini ya mamlaka, tii
sheria, wajibika kwenye sehemu yako ya kazi bila kutegea, kwani kwa kufanya
hivyo, riziki yako ya halali itakuwa na Baraka.
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment