Kesi
ikaanza na cha ajabu kabisa kilichotokea ni kuwa mashitakiwa ambaye alitakiwa
kusimama pale mbele, kama mshukuwa wa mauji, hakuwepo, na hata wakili
alipoulizwa mshitakiwa yupo alichosema ni kuwa;
‘Mshitakiwa
hayupo hapa kwa sababu za kiusalama lakini muda utafika atakuwepo…’akasema
‘Kama
hayupo ni kwanini kesi hii inaendelea?’ akaulizwa
‘Kwasababu
mume wa marehemu anataka iendelee, ..’akasema
‘Lakini
mume wa marehemu si ndiye huyo anayeshukuwa kuwa ndiye aliyemuua?’ akauliza
‘Ndio
ilivyo , yeye anataka haki itendeke….’akasema
‘Anataka
haki itendeke ya kuwa yeye hakumuua, au mkewe kauwawa, lakini sio yeye?’
akaulizwa.
‘Yeye
hakumuua mkewe, hilo ni moja, lakini jingine la muhimu, ni kuhakikisha huyo
aliyemuua mkewe ambaye hajajulikana akamatwe,..’akasema.
‘Ina
maana sio kweli kuwa mkewe alijiua?’ akaulizwa.
‘Inawezekana
kweli alijiua, lakini kwanini alijiua, ….’akasema
‘Kwanini
alijiua?’ akaulizwa
‘Ndio
maana tunahitaji mahakama hii tukufu itafute ukweli, kama kweli alijiua, au
aliuliwa, na kama alijiua mwenyewe ni lazima kuna sababu,…’akasema
‘Je
upande wa mashitaka unasemaje?’ akauliza hakimu
‘Sisi
kwa upande wetu leo tulikuja kumaliza hii kesi , kwasababu ushahidi
uliopatikana unaonyesha kuwa marehemu alijiua mwenyewe…’akasema
‘Mnao
ushahidi wa kutosheleza hiyo hoja?’ wakaulizwa
‘Ndio
tunao ushahidi….’wakasema
‘Kwahiyo
mshitakiwa mliyemlta hapa mahakamani hana kosa, hakuua, kama mlivyowakilisha
sitaja lenu….?’ Wakaulizwa
‘Ndio
mshitakiwa hana kosa, kesi dhidi yake tunaomba iondolewe…’wakasema
‘Basi
tunataka muonyeshe huo ushahidi ili mahakama iweze kuamua….’ wakaambiwa
************
Wakati
kesi ikiendelea, mkuu wa idara ya usalama alikuwa kiteta na watu wake kuhusu
harakati za kulisambaratisha hilo kundi haramu, na mmoja wa watu wake akasema;
‘Mkuu,
tumejitahidi sana kumpata mumiliki halali wa jengo la hiyo hoteli ya Paradise
lakini imekuwa kama kitendawili, wanavyodai mtu huyo hayupo tena…’wakasema
‘Una
maana gani, kusema hayupo tena….?’ Akaulizwa
‘Huyu
mtu amefariki, alikufa kwa shinikiza la damu, na inadadakiwa alikufa kutokana
na kuchanganyikiwa, ….’akasema
‘Kuchanganyikiwa….!?’
‘Ndio
inavyoonekana kuna mambo ylitokea ndani ya familia yao, ambayo yalimchanganya
huyo mwenye hiyo hoteli, wanasema mtu huyo alikuwa akiweweseka na kupiga
kelele, akisema, wananiua, wanataka kuniua…, basi ikafika siku moja akadondoka,
na wlipompima wakaona shinikizo la damu lipo juu, na hiyo ikawa ni chanzo cha
kifo chake…’akasema
‘Sasa
ni nani wanaomiliki hiyo hoteli kwa sasa?’ wakauliza
‘Kulikuwa
na wanahisa…ambao waliungana naye kabla, akiwa yupo hai, na ukiangalia waraka
wa umiliki wa huo mradi, au kitega uchumi hicho utaona kuwa yeye alikuwa
akimiliki hisa hamsini na moja, na zilizobakia zilikuwa zikimilikiwa na
wanahisa wengine..’akasema
‘Kisheria
mtu baada ya kufa, kunakuwa na mrithi wake, je ni nani anayerithi hizo mali?’
wakauliza
‘Ni
mama yake, lakini mama yake alisema hataki jina la mtoto wake liondolewe, na
akasema nyaraka hiyo ya umiliki ibakie kama ilivyo…’akasema
‘Huyo
mama yake yupo wapi?’ akaulizwa
‘Tatizo
kubwa alilo nalo huyo mama ni kuwa kachanganyikiwa,…hayupo sawa kiakili, halafu
kapooza upande mmoja…’akasema
‘Mhh,
sasa hayo ya kusema mama huyo alisema utaratibu wote wa umiliki ubakie kuwa
hivyo, aliutoa vipi kama unasema yupo kama kachanganyikiwa….?’ Akaulizwa
‘Hayo
aliyatoa kipindi mtoto wake alipofariki, na muda huo alikuwa na akili zake
timamu, wanasema kifo cha mtoto wake ndicho kilichomchanganya….’akasema
‘Huyo
mama yupo wapi, anaishi wapi?’ akaulizwa
‘Kwenye
ile hoteli, kwa chini kuna sehemu kuna nyumba iliyotengenezwa vizuri sana,
ukifika utaona sehemu imejitokeza, huyo mama anaishi hapo, na wafanyakazi
wanaomuhudumia, ukiingia humo kulivyotengenezwa huwezi kusikia lolote
linalotokea nje, imentengenezwa kiasi kwamba, hakuna sauti inayoweza kupenya
ndani au kutoka nje….’wakasema.
‘Ni
nani dakitari wake anayemuhudumia?’ akaulizwa
‘Kuna
docta mmoja mtaalamu sana, alisomea nje, akaja hapa nchini na kuanzisha
hospitali yake, wengi wanamfahamu, ni bingwa kweli,…..anaitwa Docta Chiza…’akasema
‘Docta
Chiza…?’ akauliza mkuu
‘Ndio
mkuu….’akasema
***********
Ilikuwa
ndani ya hospitali moja kubwa inayosifika sana kwa matibabu mbali mbali. Ni
hospitali ya gharama kubwa sana, hata ukifika utaona kila kitu chake ni cha
hali ya juu, viti vya kusubiria wagonjwa ni masofa ya bei mbaya, kuna kiyoyozi,
na kila aina ya vitu vya kumfana mgonjwa asijisikie yupo kwenye ofisi, na sio
hopsitali.
Kwenye
mlango mmoja ulioandikwa, `dakitari mkuu..’ kulikuwa na jamaa mmoja kakaa
kwenye sofa la kusubiria zamu yake ya kuingia, alikuwa kashika gazeti akisoma, na
mara akaja msimamizi wa eneo hilo na kumuomba kadi yake.
‘Kadi
yako tafadhali…’ akaulizwa
‘Hii
hapa….’akasema ule mtu na yule msimamizi akaichukua na kuikagua, akamtupia
jicho yule mtu, na walipoaangaliana akainama kwa haraka na kuangalia chini, halafu
akasema
‘Kwa
vile tatizo lako sio kubwa sana, unaonaje ukienda kumuona msaidizi wake..’akasema
yule mhudumu, akiendelea kuiangalia ile kadi
‘Hii ni mara ta tatu nafika hapa na kuambiwa hivyo
hivyo, nataka kumuona docta mwenyewe,….ndio maana nimelipia hivyo….’akasema
yule mgonjwa
‘Hamna
shida utamuona tu….ni ushauri wangu , maana huyo docta sasa hivi anaongea na
simu, kuna mgonjwa mwingine anahitajika kutoka, kwenda kumuona..lakini ngoja
tuone kama anaweza kukuhudumia,….’akasema huyo msamamizi.
‘Leo
sitoki hapa mpaka nimuone….’akasema huyo mgonjwa.
Yule
msimamizi akaingia ndani, na baadaye akatoka,na kusema ingia, na yule mtu
akaingia kumuona docta. Na yule mtu alipoingia akamkuta yule docta akiendelea
kuongea na simu, yeye akakaa kwenye kiti kama sofa kilichopo hapo, akatulia
kumsubiria docta amalizie kuongea na simu yake.
‘Ni
nani anataka kumuona huyo mama?’ akauliza docta akiongea na simu
‘Watu
wa usalama!?Kwani hao watu hawajui kuwa huyo mama kachanganyikiwa, waambie mimi
kama docta wake, nimesema huyo mama harushusiwi kuongea na mtu, kutokana na
hali yake ilivyo…’akasema
‘Wanataka
kuniona na mimi pia, kuhusu nini?’ akauliza
‘Sawa
wapange muda wao nikiwa na nafasi nitakutana nao wafike ofisini watakutana na
katibu muhutasi wangu atawapangia siku na saa lakini sio leo…., sitaki
waniingilie kwenye kazi zangu, …mimi ni mtaalamu na bingwa,najua nini
ninachokifanya….’akatulia
‘Eti
nini, wanauliza kuhusu mtoto wa huyo mama?’ akauliza kwa mshangao, na akainua
uso kumuangalia huyo mgonjwa aliyeingia na kukaa kwenye kiti.
‘Hao
watu hawajui walifanyalo, huyo mtoto wa huyo mama amefariki siku nyingi, kama
wanahitajia vithibitsho vya kidakitari vipo, tutawaonyesha, au kama wanataka
kuliona kaburi la huyo marehemu wapelekwe walione, shida ipo wapi hapo,
wanataka nini zaidi, maelezo gani wanahitajia kutoka kwangu, kuhusu huyo mama…unasema
kuhusu vitega uchumi vyake…aaah, kila kitu kipo sahihi bwana….wasiwababaishe
hao watu, kwani ni ofisa gani huyo….?’akasema kwa dharau na kuuliza
‘Haya
ngoja nimalizane na huyu mgonjwa mmoja , ninakuja huko tuliongee hili, maana
naona kuna tatizo, lakini sio tatizo kubwa sana, tutalimaza tu,..na waambie
wengine, wajipange vyema…..’akasema na kukata simu
Akainua
uso na kumuangalia mgonjwa aliyekaa kwenye kiti mbele yake, kwanza akakunja uso
kuonyesha kutokufurahishwa na kitu , halafu akatabsamu na kuuliza
‘Kwanini
umefuga ndevu nyingi hivyo, huoni zitakusumbua, na kiusafi ningekushauri
angalau uzipunguze, ni ushauri tu kama docta, sio kwamba nakuingilia mambo yako…’akasema
‘Hilo
sio kusudio langu la kufika hapa…’akasema huyo mtu, na Docta akatulia kusoma
maelezo kwenye ile kadi ya huyo mgonjwa.
‘Na
mbona umeandika jina moja tu, hujaweka ubini wako, kwa kumbukumbu za kiofisi
ulitakiwa uandike kile kitu, na….kila kitu kipo sahihi, huna tatizo, moyo, damu….ok,
samahani kwa kukushauri kuhusu hizo ndvu, najua kuna watu wana imani hizo za
kufuga ndevu, lakini zako zimezidi hazikusumbui…?’ akauliza akitabasamu,
alionyesha kweli ni mtaalamu na anafhamu vipi kumweka mgonjwa sawa, ajisikie
yupo nyumbani.
‘Hazinisumbui,
na kama zingenisumbua ningezinyoa….’akasema huyo mgonjwa na huyo docta akawa
kama kahisi jambo, akamuangalia yule mgonjwa kwa makini, akauliza
‘Ni
nini shida yako…?’ akauliza
‘Shida
yangu ni kubwa ni kutaka kuongea na wewe..’akasema huyo mgonjwa
‘Eti
nini…..?’ akauliza huyo docta kwa mshangao, halafu akaangalia kwenye komputa
yake iliyopo mbele yake, halafu akashika kidevu, kumuangalia huyo mgonjwa,
akaangalia saa yake na kusema;
‘Umakuja
kutibiwa au kuongea na mimi…?’ akauliza
‘Nataka
kuongea na wewe kuhusu huyo mtoto wa huyo mama, na mahusiano yake na wewe……’akasema
huyo mtu, akito kitu mfukoni, kilikuwa ni kitambulisho caha kuonyesha yeye ni
nani , na huyo docta hakutaka kabisa kukiangalia,akasema;
‘Hapa
nipo kazini siwezi kufanya hayo, nahitajia kuwahudumia wagonjwa kwanza…’akasema
akionyesha kutokujali, na tabasamu la kuigiza likajaaa mdomoni.
‘Najua
hilo…, lakini kwa akuli yako mwenyewe hapo kwenye simu, umesema kuwa mimi ni
mgonjwa wa mwisho kuhudumia na wewe, mimi nikitoka, wewe unakwenda kuonana na
watu wako kuongelea swala la mtoto wa huyo mama aliyechanganyikiwa, mtoto wake
ambaye anamiliki miradi mingi ikiwemo mradi wa hoteli hiyo kubwa ya Paradise au
sio….?’akasema huyo mtu na kumfanya docta akaonyeshe uso wa kutahayari kidogo,
lakini akatabasamu na kusema;
‘Lakini
hayo yanakuhusu nini wewe, kuna kosa nimefanya, na je huu ndio utaratibu
unaotakiwa kufuatwa, twende mbele turudi nyuma, au…?’ akauliza
‘Yananihusu
sana, ndio maana nataka kuongea na wewe, na nafanya hili kwa nia njema tu, …’akasema
huyo mgonjwa.
‘Haya
niambie unataka tuongee nini….?’ Akauliza huyo docta akitulia kumsikiliza huyo
mgonjwa, na simu ya mkononi ya huyo docta ikalia kuashiria ujumbe, na
alipousoma huo ujumbe, akakunja uso…
WAZO LA LEO: Hakuna usafi
mnzuri kama usafi wa moyo, ukiwa msafi wa moyo, huwi na wasiwasi, na mara nyingi,
tabia zetu na matendo yetu yatakuwa ni mazuri. Wengi wetu tunajali usafi wa
mwili, nguo, na unadhifu n.k, lakini mioyo yetu ni michafu, zaidi ya mtu aliyejipaka
kinyesi.
Tunakuwa na roho mbaya, ubinafsi, wizi, na kila aina ya matendo
mabaya. Huo ni uchafu mkubwa sana, lakini hatuuoni, na mwilini tunajifanya
kuvaa kinadhifu. Tunaoga kupindukia, na harufu nzuri za manukato, lakini
tunanuka rohoni.
Ni
muhimu sana, tukajisafisha mioyo yetu kwanza, ili kweli tuonekane wanadhifu.
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment