Inspecta Maneno
aliitwa kwenye jopo maamulumu, jopo hilo ni la maadili na uwakajibikaji, humo
kuna wanasheria, na wakuu mbali mbali wenye dhamana. Inspecta aliambiwa aseme
ukweli wake, kuhusiana na kadhia ya kundi haramu, lakini hakuweza kusema ukweli
huo…..
Kama wakuu na
watendaji wanaojua kazi yao vyema, waliona ni vyema kujisafisha na kusafisha
idara yao, kwa kashifa zilizokuwa zinaendelea, kwani ili uwe sahihi kwa jambo
lolote, kwanza jichunguze kwanza wewe mwenyewe, chunguza familia yako, chunguza
watu wako unaofanya kazi nao kwanza….
Ndio maana mku huyo
akasema;
‘Ndio maana
nimekuita ndani ya chumba hiki, maalumu kwa kazi hiyo, mimi kama mkuu wakitengo hiki, nina mamlaka ya kusikiliza kesi
zote, na mwanzoni nilikutaka useme ukweli ili tujue jinsi gani ya kulitatua
hili tatizo, na kwa vile hukutaka kutoa ushirikiano, basi inabidi tupate
maelezo sahihi kutoka kwako, kwa utanguzi wa kesi, na hili linatakiwa lifanyike
sasa hivi…’akasema.
‘Lakini sikujiandaa
kwa hilo….’akajitetea.
‘Wewe ni askari,
askari popote anatakiwa awe tayari, kwa hilo huwezi kujitetea, ndio najua hayo
ni mambo ya kitaalamu zaidi, lakini kwa kuanza, ni lazima leo tusikilize ukweli
, …tunahitaji kusikia ukweli wote ili kuhakikisha kitengo hiki kinaondokana na
dhana ya kuwa hamfanyi kazi zenu vyema, na kama hilo lipo, …..’akasema na
Maneno akakatiza na kusema
‘Lakini mkuu unataka
ukweli gani kutoka kwangu, ina maana huamini taarifa yangu niliyokupa?’
akauliza
I
nspecta akachukua
simu na kumpigia mtendaji mwingine, akasema;
‘Mlete….’
*************
Inspecta
maneno akawa kaduwaa, hakujua ni nani aliyeitwa, na mara mlango ukafunguliwa, kwa
pale alipokaa manen asingeliweza kumuona moja kwa moja huyo aliyeingia, hadi
pale alipofika mbele ya meza ya huyo mkuu, alikuwa ni binti mmoja, akiwa
kavalia mawani, akayavua yale mawani, na wigi kubwa alilokuwa kalivaa kichwani
Akawa
sawa na usawa wa Maneno kumuona, na Inspecta Maneno akabakia mdomo wazi, na
hakuweza kuficha mshanga wake, akisema;
‘Mrembo
Jembe, umefuata nini hapa?’ akauliza kwa mshangao, na mrembo Jembe akatabasamu
kidogo, huku akiwa kasimama kiaskari…yule binti akasema;
‘Mkuu
nimekuja…’akasema kwa ule ukakamavu wa kiaskari, na kuendelea kumfanya Maneno
kushangaa zaidi, maana ile ishara na ule ukakamavu aliouonyesha huyo binti
unaonyesha wazi huyo binti hakuwa anaigiza ni kweli upo kwenye damu.
‘Detective Jembe, karibu ndani ya kikao,….nakutambulisha
kwa jopo kwa mara ya kwanza, sikupenda utambulike mapema, lakini kwa vile
unahitajika kwenda masomoni na ukirudi najua utakuwa mtu mwingine nimeona
nikuweke wazi kwa watendaji wengine…’akasema mkuu huyo.
‘Haiwezekani….’akasema
Maneno, na mkuu hakujali huo mshangao wake, akawa amemuangalia huyo binti,
akiendelea kusema;
‘Pole
sana kwa majukumu mazito, najua ni kazi ngumu na yenye kujitoa mhanga, na wakati
mwingine ilibidi ujizalilishe, ili mwisho wa siku tuweze kupata kile
kinachostahili…hilo mungu atakulipa, na serikali imethamini juhudi yako hiyo
ndio maana imeona ikupeleke ukasome zaidi, ili ukija uwe mkuu kama sisi…’akasema.
‘Ni
kweli kazi zetu hizi zina mitihani mingi, …mwanzoni kama isingelikuwa kipaji
hiki alichonipa mungu, ningewachukulia nyie wote, kuwa makosa mliyoyafanya ni
kutokana na utendaji wenu wa kazi, ni sehemu ile ya kujitoa mhanga,…ndio maana
nilitangulia kumsisitiza Maneno aseme ukweli wake,..wenyewe mumesikia
nikimsisitiza, lakini akakataa..nilijua hataweza kusema ukweli…’akasema.
‘Sasa
Inspecta Maneno unapewa nafasi ya mwisho, ya kuongea ukweli ulivyo…’akasema na
Maneno akainama chini akiwa hana la kuongea. Mkuu akageuka kuwaangalia waliopo
humo ndani, halafu akageuka tena kumuangalia Maneno na kusema;
‘Maneno
unajua katika kazi zetu hizi tunatakiwa tuwe waangalifu kila hatua, nilipowatuma
wewe na mwenzako kwenda kwenye hicho kituo niliwaamini sana, na ni kweli
mwanzoni ulikuwa mtendaji mzuri sana wa kazi, kwahiyo hakuna aliyeweza
kukutilia mashaka…ila mimi sikuwa nimekuamini kihivyo..’akatulia
‘Kutokana
na uzoefu na kipaji alichonipa mungu, cha kuwagundua watu walivyo, mimi
niliwahi kutamka kwa mkubwa wangu wa kazi kuwa wewe sio mwaminifu kama
unavyojionyesha, ni kama fisi ndani ya ngozi ya kondoo…’akasema.
‘Mkubwa
wangu huyo hakunikubalia kauli yangu hiyo, akijua wewe umeweza hata kwenda
kusoma nje, na kupata ujuzi, elimu iliyo bora, kwahiyo utakuwa ni hazina ya
serikali,..na kiukweli ulifaulu vizuri na kazi yako unaijua, una taaluma nzuri
elimu ya hali ya juu, lakini kuna udhaifu ulio nao, ambao ni tamaa, tamaa
imekuzidi…hilo unalijua mwenyewe ndani ya nafsi yako….’akasema.
‘Ni
kweli wakati mwingine kwenye kazi zetu hizi, unategeka inafikia hatua unasema
potelea mbali ngoja nifanye wanavyotaka wao, lakini mwisho wa siku unatakiw
ujirudi, ujue wajibu wako ni nini…nilitarajia na wewe utafanya hivyo, tumekupa
muda wa kutosha kufanya hivyo, lakini hata kama tungekupa miaka mia, hadi
unaingia kaburini, usingelibadilika….’akasema.
‘Na
sasa hivi ulikuwa mbioni kuandika barua ya kuacha kazi…ili upate muda wa
kufanya mambo yako vyema, hayo yote tunayajua, ..au unabisha hukuwa umeshaandaa
baru ya kuacha kazi?’ akaulizwa.
‘Mkuu…..’akataka
kusema lakini mkuu wake akaendelea kuongea;
‘Maneno,
hata hivyo kwa vile wewe ni mfanyakazi wetu, kiubinadamu tuliona bora tukupe
nafasi nyingine mbele ya jopo hili, ujirudi, kwani huenda, umetegeka, sana,
unaogopa ahadi uliyotoa kwa mabosi wako wa utajiri,ndio maana nimekupa nafasi a
kusema ukweli na kujitetea hapa, sisi kama watendaji , viongozi tuliopewa
dhamana tungejua ni nini cha kufanya..lakini hukuweza kufanya hivyo…je unaweza
kujitetea kivipi kwa hilo…’akasema
‘Labda
kwa muhutasari tu, ningelipenda, kuelezea kwa kifupi, kuhusu hili kundi haramu,
kutokana na utafiti uliofanyika hadi sasa, ni kuwa kweli kundi hilo lipo, na
limeweza kuwateka sehemu kubwa ya watendaji wazuri kutoka kwenye idara nyeti,
na nia yao ilikuwa hivyo, kuwapata wale watendaji wazuri, hasa wale wenye akili
ya ziada katika utendaji wako, ni kipaji chao….’akatulia
‘Kwahiyo
utaona kwa jinsi gani walivyokuwa wamejipanga, kila sehemu kila idara na kila
mahali ambao walijua kuna umuhimu kwako waliweza kuwapata watu wao, kutoka humo
au kuwapandikiza wengine kwa kuajiriwa sehemu hizi…’akatulia.
‘Tulihitajia
muda zaidi wa kulikamata hili kundi, kwani ni hatari na wamejipanga kikamlifu, wameenea
kila sehemu, na sio humu nchini tu, kundi hilo ni la kimataifa, hili lililopo
hapa nchini ni kundi dogo tu, ukilinganisha na mtandao wao ulioendea dunia
nzima…’akasema
‘Wameweza
kupenyeza watu wao kila mahali, na kila vurugu inayotokea ujue ni wao
wameichochea kupitia kwa watu wao waliowapandikiza, na wanafanya hivyo wakiwa
na malengo, kuhakikisha kuwa wanawavunja nguvu wale wanaoona ni maadui zao, na
pia ili waweze kupenyeza mambo yao….ni wajanja sana.
‘Maneno
angeweza kuthibitisha haya, kama angekuwa mkali, lakini naona aliona huko ni
bora kuliko nchi yake, ni bora kuliko wananchi wake, maana yanayotokea hapa ni
madhara kwa nani, ni madhara kwa raia, kwa wanachi ambao wanalipa kodi zao, ili
tuweze kupata mishahara yetu, ina maana wao ndio wametuajiri, sasa leo
unawageuka…ni dhambi kubwa sana…’akasema.
‘Utajiri
ni kitu cha muda, huwezi kuishi nao milele, utatumia, itafika muda utakufa utauacha,
lakini wema, uadilifu, haki na uwajibikaji kwa ajili ya dhamana uliyopewa ndio
hazina pekee utakayoondoka nayo, hiyo ni taji kwako, hata ukifa bado utabakia
nayo milele…..’akasema.
‘Katika
kazi zetu hizi, asilimia kubwa ni kujitolea muhanga, unakuwa tayari kufa kwa
ajili ya wenzako, na ni kweli hakuna
utakachoweza kulipwa kitosheleze hayo tunayofanya, kujitolea nafsi kuwa
mbele ya risasi kwa ajili ya kulilinda taifa lako, ni kazi kubwa sana…’akasema
na kugeuka kumuangalia yule binti.
‘Hebu
angalia binti mdogo kama huyu, aliwekwa mbele ya hatari, kujitolea kufanya hata
yale yasiyofaa, kwa ajili ya taifa lake,….anashida gani huyu binti, ni mzuri,
ana vipaji vingi tu, angetulia na kujifanyia shughuli zake na, angelikuwa mbali
sana, lakini kwa uzalendo wa nchi yake, utashi, wa taifa
lake, aliamua kujitolea, kufanya hata yale yasiyofaa ili kuhakikisha taifa lake
linakuwa katika amani,…hivi kweli mtamlipa nini huyu binti, kinacholingana na hiyo kazi aliyofanya….’akatulia.
‘Eti
Maneno, hivi kweli wewe ungelikuwa ni mkuu, ungelimpa nini huyu binti kwa hayo
aliyoyafanya kwa ajli ya taifa lake, ambayo wewe umeshindwa kuyafanya, hakuna thamani itakayolingana na hayo aliyoyatenda ni kujitoa mhanga tu kwa ajili ya taifa lako….’akatulia
‘Jembe
najua upo kwenye maandalizi ya safari yako, lakini tutakuhitajia kutoa ushahidi
muhimu kwenye kesi yetu hii, ikibidi,….hata hivyo, najua kwa sasa Maneno ana
mengi ya kusema, na yeye, atahitajika kulikabili hilo kundi lake, hadi mtu wa
mwisho…huo ni wajibu wake….’akasema.
‘Pamoja
kuwa yeye ni mhalifu lakini kwa dhamana aliyopewa, ajue kuwa ni deni, na hilo
deni ni lazima alilipe, na kwa kazi yetu hii, huwezi kusema naacha kazi, hili
halipo, wewe ni mtu wa usalama katika maisha yako yote…sasa basi…tunahitaji
ushirikiano wa kila mmoja wetu kuanzia sasa…’akatulia.
‘Maneno
tunakupa nafasi nyingine ya mwisho, kuliweka wazi hili jambo, tunahitaji
kusikia kila kitu unachojua kuhusu hili kundi, na unajau ni nini kitakacho
kupata ukisaliti nchi yako…’akaambiwa na Maneno akabakia kimiya akiwa hana
nguvu kabisa.
‘Pamoja
na wewe pia tuna nguvu nyingine ya kutosha, wapo watu wengii mtashirikiana nao,
kuhakikisha kundi hili linafyweka, na kila anayehusika, kufikishwa kwenye
vyombo vya sheria, kila kitu kipo tayari, cha muhimu ni mambo machache ambayo
tunayahitajia kutoka kwako …’akasema akimuangalia Maneno
‘Maneno
upo tayari kutoa ukweli wote….?’ Akaulizwa
‘Mkuu,
kwa hali kama hii unataka mimi niseme nini,….najua hamtanielewa, kwasababu
mumeshaniweka kwenye kundi hilo, lakini hamjui mitihani gani niliyokutana nayo
hadi kuweza kuingia huko…..ni vyema, ikabakia hivyo, na kama ulivyosema,
nahitajika kulipa deni la wananchi, ..nitafanya hivyo, na kiukweli sikuwa
nafurahia hayo yaliyotokea, ili kulihakikisha hilo nitafanya yote niwezayo
kuhakikisha hilo kundi linapatikana….’akasema
‘Kabla
ya hayo, tunahitaji ukweli wako, tunahitaji yote unayoyajua, na uliyoyafanya,
kuanzia kwa kifo cha muheshimiwa, hadi kifo cha mke wa Inspecta….maana hata
kauli yako bado ina mashaka, unakuwa kama huamini kuwa kundi hilo lipo…unaposema
linapatikana una maana gani…’akasema mkuu.
‘Mkuu
hayo si yanajulikana, …mimi sioni kwanini nioyaongee tena, …na kuhusu kundi
siwezi kukiri moja kwa moja kuwa lipo….’akasema
‘Nakuelewa
sana Maneno, najua ulivyo, lakini kumbuka utajiri sio mali kitu, na natumai umenielewa
vyema niliotaka kujua kutoka kwako, kama mkuu wako nahitaji uyaongee yote
ukweli wote….’akasema.
‘Sawa
mkuu nitafanya hivyo….’akasema
‘Kabla
hujaanza kusema ukweli, kiutaratibu wa kesi, kwanza heu tuambie, je ni kweli
mke wa Inspecta alijiua mwenyewe…?’ akaulizwa
‘Ni
kweli alijiua mwenyewe…’akasema kwa kujiamini
‘Je
Inspecta Moto yupo wapi…?’ akaulizwa
‘Hilo
mimi sijui, ndio tulikuwa tunamtafuta..’akasema
‘Kwa
ajili ya kumuaa au sio…?’ akaulizwa
‘Hayo
ni yao wao, lakini mimi nilikuwa na mbinu yangu ya kumuokoa, kama nigetaka
kufanya wanavyotaka wao, angelishakufa, ..lakini sikupenda itokee hivyo, na
nimefanya juhudi kadri ya uwezo wangu kumuokoa, hata yeye mwenyewe anajua hilo…’akasema
‘Hebu
tuambie ukweli kuhusu urafiki wako wewe na mke wa Inspecta…’akaambiwa
‘Hivi
hilo ni muhimu kuliongea hapa kwa sasa, hamuoni kuwa linapandikiza chuki,..na
mnajua fika hayo yalitokea kwa dhamira ya kunitega mimi ili niingie kwenye hilo
kundi…’akasema.
‘Hata
kabla ya hayo, hamkuwa na urafiki huo wa siri…?’ akaulizwa
‘Hakuna
kitu kama hicho, mimi nilimchukulia yeye kama shemeji yangu, na tulikuwa na
utaratibu mnzuri tu, mimi na Moto, hata Moto alikuwa akitoka na mke wangu
nilimuamini…’akasema.
‘Wewe
ulimuamini mwenzako na kiukweli yeye alikuwa muaminifu kwa mke wako, ila wewe
sio mwaminifu..sema ukweli wako, maana hapa ni sehemu ya kujitakasa…’akaambiwa
‘Hilo
halipo, sio kweli, tuliheshimiana sana na shemeji yangu,…hata kama mwenyewe
Inspecta Moto angelikuwepo angalibainisha hilo…’akasema
‘Sawa
labda tusipoteze muda, sasa naona ni bora tuianze hii kesi, kuhakikisha kuwa
kila kitu kinakuwa wazi, ukweli ubainike, na uwajibikaji uwepo, kisheria na nidhamu
za kijesho ziwepo, naona tufanye hivi…’akasema na kuchukua simu kupiga sehemu
nyingine akasema
‘Waambie
wote waingie chumba cha mashahidi na tutawaita mmoja mmoja….’akasema
WAZO LA LEO: Mara nyingi kwenye
ukweli uwongo hujitenga.
Kuna
watu wana tabia ya kuwa ndumilakuwili, wakifika kwa huyu wanasema hivi wakifika
kwa mwingine wanasema vile, nia na lengo ni kuchonganisha, watu hawa ni wabaya
sana, kwa tabia zao hizo, kwani mwisho wa siku ni kuleta uhasama. Ukiona tabia
ya namna hiyo ni vyema ukawaita wote wawili, mtoa taarifa na msemwa, ili ukweli
ubainike, na hapo uwongo utajitenga, na tabia hiyo itakoma.
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment