‘Mkuu
unahitajika makao makuu haraka….’akasema huyo msaidizi wake
‘Kuna
nini tena…?’ akauliza inspecta Maneno kwa mashaka huku akifunga mlango wa nyumba ya Inspecta kwa nyuma yake.
‘Inspecta
Moto kapatikana….’akasema Inspecta mwenzake, ambaye kaletwa hivi karibuni kwenye kituo chao
‘Eti
nini….!’
Tuendelee na kisa chetu
*********
Lilikuwa
ni jopo la watu wa usalama, miongoni mwao alikuwepo Inspecta Maneno aliyefika
muda mfupi kutoka kituo chake cha utendaji, na alipofika, alikaribishwa kwenye
ofisi maalumu.
Kwanza
alitakiwa kutoa maelezo kuhusu kituo chake, na kuhusu tetesi zilioenea kuwa eneo
lao limeingiliwa na kundi haramu…kwanza alianza kwa kusema yeye alipoitwa hapo
hakuwa amearifiwa ni nini anachoitiwa kwahiyo hakuwa amejiandaa kihivyo, ila
kwa vile yeye ni askari, wakati wote yupo tayari, basi ataweza kutoa maelezo
hayo na kwa ushahidi, kwani kila kitu kipo kwenye mtandao wao wa usalama, …akaanza
kutoa maelezo yake na ushahidi
Maelezo yake yalipokwisha ilionekana kama hayatoshelezi, hasa aliposema kuwa maneno au tetesi zilizozagaa kuwa kuna hujuma ndani ya
kitengo chao ni mambo ya kisiasa na hayana ukweli wowote.
Jopo
hilo lilikuwa na mambo mengi ya kiutendaji, na yalihitajika kusikilizwa,
kwahiyo likaamua kuliweka hilo tatizo la pemneni kwanza, wakawa
wanajishughulisha na mambo mengine.
Kwa
hali ile ilimfanya Inspecta Maneno kujisikia vibaya, kwani hakujua ni kwanini
wanamfania hivyo, lakini kwa vile waliopo hapo ni wakuu wake, ikabidi atulie hadi
ikafika hata tena ya yeye kusikilizwa, na sasa akawa anahojiwa na mkuu wake wa
kazi.
‘Inspecta
Maneno tumekuita hapa ili utuambie ukweli ni nini kinachoendelea katika kituo
chako’ akaambiwa.
‘Nimeshaeleza
ukweli wote mkuu….’akasema
‘Hatujarizika
na maelezo yako, wewe kama kiongozi kuna zaidi ya hayo tunahitajika kuyafahamu,
maana hili hapa ni jopo, na linahitaji kuona kuwa kila kitu kipo sahihi na
maelezo yote yanafika kwao, …wamaone kuwa leo wapate taarifa moja kwa moja
kutoka kwako, je huo ndio ukweli wote….?’ akaulizwa
‘Sijaelewa
mkuu msingi wa swali lako, maana juzi tu uliniagiza nikupe maelezo ya uchunguzi
wangu na kazi kwa ujumla nikakupa, sasa hili swali ni kuhusu hiyo taarifa
nilitoa sasa hivi au jpo linahitaji nini zaidi…?’ akauliza.
‘Ni
kutokana na taarifa yako uliyonipa, ambayo inagongana na taarifa nyingine tulizozipokea
hivi karibuni kutoka kwa watendaji wenzako…’akasema.
‘Wenzangu
ni akina nani ambao wanaokiuka utaratibu wa kiutendaji, kwani wao walitakiwa
kufikisha hizo taarifa kwangu kwanza, ili nizifanyie kazi kabla hazijafika
kwako…’akasema.
‘Wamefanya
hivyo, baada ya kuona kuwa taarifa zao hazipewei kipaumbele, ni kama vile wewe
unazizarau taarifa zao, na wakati wao wamesema wana uhakika na hicho
walichokifanyia kazi,na wamewahi kukuambia ukasema hazina uzito, sio kweli, ni
siasa tu…’akaambiwa
‘Kwanza
hao watu ni akina nani,..kweli kiutendaji hilo lipo sahihi, wamekosea sana,
hata nyie mnajua hivyo, walitakiwa wanithibitishie, nipata uhakika, mimi kama
kiongozi wao siwezi kuleta taarifa zenye walakini…mnalifahamu hilo vyema kama
ningelifanya hivyo, nyie wenyewe mngekuwa wa kwanza kunilaumu…’akasema
‘Sikiliza
Maneno, kuna kundi haramu lipo katika maeneo yenu, kundi hili sio kundi dogo,
ni kundi la kimataifa, inavyosadikiwa ni kuwa kundi hili limeshaingiza hata
watu wa usalama, wanasisasa, wafanyabiashara na watu wa kila idara nyeti, kutokana
na mbinu zao za ushawishi, mimi nilikuamini sana wewe, ndio maana nikawa
nakutumia wewe kupata ukweli, je huo ndio ukweli wote….’akatulia
‘Ndio,
huo ndio ukweli wote, nimeshawafikishia kila kitu kutokana na uchunguzi wetu
mkuu…’akasema
‘Maneno,
hili jopo hapa ni la wataalamu mbali mbali wakiwepo wanasheria, mimi kama mkuu
wako wa kitengo, nakupa nafasi ya mwisho nataka kujua ukweli wa hicho
kinachoendelea huko, na ukweli huo nautaka sasa hivi...’akasema
‘Mkuu,
ukifanya hivyo, unaniweka katika mahali pabaya, maana kila kitu kina utaratibu
wake, kama ni taarifa ya hizo tetesi na mnahisi kuna zaidi ya hayo, basi labda
mnipe muda tena nilifania kazi…’akasema
‘Kwa
hali hiyo ya kuomba muda, ina maana
unakubali kuwa ukweli wote hujatupatia au sio?’ akaulizwa
‘Ukweli
wa tatizo ambalo tumekamlisha uchunguzi wake, ndio huo, kuna matatizo mengi
kwenye vitengo vyetu nab ado tunaufanyia kazi…sasa kuhusu kuwepo kwa kundi hilo
hararamu na kuwa kuna watendaji nyeti wameingizwa, mimi hilo sina ushahdi nao
ndio maana nahitaji muda, niweze kuandaa taarifa kitaalamu sizani kama hilo
litakuwa sahihi nikiongea tu.
‘Nataka
uongee hivyo hivyo, tupata maelezo yako….’akaambiwa.
‘Mkuu
lakini hivyo nitakuwa sitimizi wajibu wangu kitaalamu, wewe ni mkuu wangu sawa,
ukinilazimisha nikupe maneno tu, ninaweza,
hata bila vielelezo lakini je itasaidia nini,…mimi ni mtendaji na
mtaalamu, sitakiwi kufanya hivyo…’akasema kwa kujiamini
‘Nafahamu
wewe ni mmoja wa watu wetu tuliowafunza na kuwapeleka nje kusomea kazi
hizi,lakini utaalamu wako hauwezi kunifanya mimi nishindwe kutimiza wajibu
wangu, kwani hli ninalokuambia lina uthibitisho kuwa kuna walakini katika taarifa
zenu, kuna mgongano wa taarifa zenu,….kwahiyo kuanzia sasa nataka uniambie
ukweli ulivyo..’akasema huyo mkuu
‘Ukweli
upi mkuu, zaidi ya huo niliokuambia…?’ akauliza Inspecta Maneno
‘Inspecta
Moto yupo wapi?’ akaulizwa swali.
‘Ndio
tuliokuwa tunamtafuta mkuu, hadi napigiwa simu kuja huku, tulikuwa kwenye hizo
harakati, siwezi kuja kuongea maelezo yasiyojitosheleza dhidi yake, na kama ulivyosema, kuwa kuna tetesi kuwa kuna kundi
haramua, tena la kimataifa, tulihitaji uangalifu wa hali ya juu, kumtafuta
mwenzetu huyo ikizingatiwa kuwa karibuni alimpoteza mkewe, kwahiyo ilibid tuwe
makini sana, kwa usalama wake pia …’akasema
‘Mpaka
hapo mlipofikia mlishagundua nini?’ akaulizwa
‘Tulikuwa
hatujahitimisha, ukumbuke huyu mtu nilimdhamini mimi, kwenye kesi ya kifo cha
mkewe, kabla hatujagundua kuwa kweli mkewe alijiua mwenyewe, na kesi yake
ilitakiwa kesho au keshokutwa isikilizwe huko uraiani, mara akapotea, iliniweka
mimi sehemu mbaya,..kama mdhamini wake…lakini hilo lipo chini ya uwezi wetu
tutalitatua tu mkuu….’akatulia
‘Kwanini
ulimdhamini ukijua kuwa ana kosa, ..?’ akuliza
‘Mwanzoni
ilionekana hivyo, kuwa ana kosa, kuwa huenda ni yeye aliyemuua mkewe, lakini
baada ya uchunguzi wangu nikagundua tofauti, na kwa vile naamini kutokana na
upelelezi wangu kuwa yeye hakumuua mkewe, mkewe alijiua mwenyewe, nikaona kwanini
nisimdhamini mfanyakazi mwenzetu…’akasema.
‘Kutokana
na taarifa zako za nyuma, ilionekana kupishana sana na taarifa za mwenzako
huyo, ilikuwa kama mnashindana, je hiyo haiwezi kuwa sababu ya matatizo
yanayotokea ndani ya kitengo chenu…?’akaulizwa
‘Kitengo
chetu hakina matatizo, huo ulikuwa mtindo wetu wa kazi, pamoja na ushirikiano,
lakini pia tulitaka tufanye kazi kwa mashindano, ili kukuza utendaji wetu, na
kama mlivyoona, kazi zilikuwa zinakwenda haraka na kwa ufanisi….’akasema
‘Kundi
hili haramu, linasadikiwa kuea limeweza kuwaingiza watu wa usalama, na hilo lina
ushahidi, ni hatari kwa usalama na kashifa kwetu, wewe ni mmoja wa viongozi wa
ngazi nyeti katika idara zetu, una taarifa gani kuhusiana na hili….?’ Akaulizwa
‘Kivipi,
kuwa ni kweli au si kweli…?’ akauliza swali hili akijua kuna mtego ndani yake.
‘Umenielewa
vizuri sana swali langu Maneno, wewe ni mtendaji , mtaalamu nijibu swali langu…’akasema
huyo mkuu.
‘Tetesi
hizo zipo, lakini mimi kama mmoja wa viongozi , siwezi kulithibitisha tu kwa
maneno ya kusikia , mpaka nilifanyie kazi, nilishawahi kusikia hivyo kabla,
nikafanya uchunguzi, lakini nilikuja kugundua kuwa ni mambo ya kisiasa tu,
hayana ukweli….’akasema.
‘Maneno,
hili ni tatizo kubwa sana, na usiponipa maelezo ya kutosha sitasita kuchukua
hatua za kinidhamu, ..unajua utendaji wetu ulivyo, na kiongozi kama wewe
ulitakiwa unifahamishe hilo mapema, ili tuhakikishe idara yetu haina kashifa
zozote…’akasema mkuu
‘Lakini
mkuu unaposema hivyo, unakuwa kama unatuhuma dhidi ya utendaji wetu,….je kwanza
nielewe, nipo kama kama mtuhumiwa au kutoa taarifa…?’ akauliza
‘Yote
mawili,…..nikuambie ukweli, kuwa, kwa hatua iliyofikia, na kwa maeelzo
niliyoyapata, mimi kama kiongozi wetu, siwezi kuvumilia tena, kwahiyo kuanzia
sasa wewe utafanya kazi huku makaoni, kituo cheni kwa hivi sasa kitaongozwa na
Inspecta tuliyemtuma huko hivi karibuni….’akasema
‘Kwanini
mkuu…?’ akauliza
‘Uchunguzi
bado unaendelea, ulitakiwa urudi kituoni kwako kakabidhi kila kitu kwa
mwenzako, lakini kwa vile bado kuna mambo yanatakiwa kufanyiwa kazi, wewe kwa
hivi sasa utabakia hapo hadi taarifa nyingine zitakapotolewa…natumai
umenielewa, mengine yatafuata baadaye…’akaambiwa
‘Lakini
mkuu bado nilikuwa sijamaliza kazi yangu, na bado tunamtafuta mwenzetu hatujui
yupo wapi,…’akasema
‘Hili
linafanyiwa kazi, kama kawaida, hapa tunataka kuimaliza hii kesi…’akasema
‘Kesi
ya nani?’ akauliza kwa mshangao.
‘Kesi
ya mauaji ya mke wa Inspecta, hiyo ni kesi ndani ya idara zetu za usalama,
japokuwa uraiani imethibitishwa hivyo, kuwa kajiua mwenyewe, lakini ndani ya
idara zetu hilo halijathibitishwa hivyo, ..’akaambiwa
‘Kama
ni kesi huo ndio utaratibu wa kesi…?’ akauliza kwa mshangao.
‘Tunachotaka
kutoka kwako ni maelezo, kama kweli kajiua au hajajiua na kwanini akajiua, …hilo
ni lazima lifanyiwe kazi, kwani ni muhimu kusafisha kitengo chetu haraka
iwezekanavyo, na kama ni kuwajibishwa, hatutasita kufanya hivyo…’akasema
‘Na
kutokana na unyeti wa kesi hiyo, tumeona kesi hiyo ianze mara moja,kwa kupata
maelezo yako binafsi ….’akasema
‘Una
maana gani mkuu?’ akauliza
‘Ndio
maana nimekuita ndani ya chumba hiki, maalumu kwa kazi hiyo, mimi kama
mkuu wakitengo hiki, nina mamlaka ya
kusikiliza kesi zote, na mwanzoni nilikutaka useme ukweli ili tujue jinsi gani
ya kulitatua hili tatizo, na kwa vile hukutaka kutoa ushirikiano, basi inabidi
tupate maelezo sahihi kutoka kwako, kwa utanguzi wa kesi, na hili linatakiwa
lifanyike sasa hivi…’akasema
‘Lakini
sikujiandaa kwa hilo….’akajitetea
‘Wewe
ni askari, askari popote anatakiwa awe tayari, kwa hilo huwezi kujitetea, ndio
najua hayo ni mambo ya kitaalamu zaidi, lakini kwa kuanza, ni lazima leo
tusikilize ukweli , …
‘Ukweli
upi tena mkuu?’ akauliza
Inspecta
akachukua simu na kumpigia mtendaji mwingine, akasema;
‘Mleteni….’
NB:
Ni mambo ndani ua kitengo maalumu, tunagusia kidogo tu ilivyookea, lakini
wenzetu wamejipanga wao wana kila kitu ndani ya utendaji wao, tutaona baadaye
itakavyokuwa.
WAZO LA LEO: Kiongozi wa kweli
ni yule anayetafutwa na watu kuwa awe kiongozi wao, kutokana na sifa zake. Na
sio yule anayeutafuta uongozi kwa watu kwa kuwaomba watu kuwa yeye anafaa kuwa
kiongozi wao. Hatua iliyofikia kwa sasa ,kwa uongozi hasa wa kisiasa umekuwa ni
kuwa uongozi sasa ni uwekezaji, kwahiyo ule utashi,
ari, na wito wa uongozi unakuwa
haupo tena.
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment