Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Thursday, September 4, 2014

DUNIA YANGU-27


Inspecta alishituka kutoka kwenye usingizi mnzito ulioandamana na ndoto za kutisha, alipofungua macho alihisi kuchoka sana na akili hakiuwa sawa, hakujitambua kwa mara moja kuwa yupo wapi…akahisi kichwa kinamuuma…

Akashikilia kichwa na kupiga miayo, halafu akajitutumua na kukaa, akageuka kutafuta wapi maji yapo, mara nyingi akiwa nyumbani kwake ni lazima anakuwa na jagi la maji kwenye kimeza cha kitanda, kwahiyo kwa vile akili haikuwa sawa,a akujua maji yapo, akanyosha mkono kupapasa, lakini kulikuwa hakuna jagi la maji

Akainuka ili kutafuta maji, mara akahisi mkono laini ukimpapasa mgongoni, kwanza akajua ni mke wake, akageuka kumuangalia na sauti ya kutoka usingizini ikasema;

‘Baby wataka kwenda wapi saa hizi…..’sauti hiyo ilimfanya ashituka na usingizi wote na machomvi, yakaisha, akakurupuka na kutoka kitandani,  akasimama haraka na kuangalia huku na kule, alijikuta yupo uchi…oh, kumbe hakuwa nyumbani kwake, na alipogundua hivyo, akaanza kuhangaika kutafuta nguo zake.

‘Baby unafanya nini, mimi nasikia baridi…njoo bwana bado mapem.’sauti ile ikaendela kusema;

‘What, ooh, my God, hivi tumefanya nini…mungu wangu…’akasema na hakuweza kuona nguo zake, akasimama bila kujua la kufanya baadaye akauliza;

‘Nguo zangu zipo wapi?’ akauliza

‘Nguo za nini bwana, mbona hivi,..unajua saa hizi saa ngapi?’ akauliza huyo mrembo, na kujiinua pale alipokuwa amelala, akakaa kitandani, akiwa kama alivyozaliwa.

‘Siamini…’akasema Inspecta akimtupia macho kwa aibu, sasa akawa haulii, akawa anahangaika huku na kule kutafuta nguo zake, na wakati huu akawa anamuwaza mke wake, akijua atakuwa sehemu…

‘Hahaha heeya,..njoo, nipo kwenye vyumba maalumu  vya starehe, najua na wewe upo kwenye chumba cha starehe na mwenzako, kwani kuna tatizo gani, siku moja moja sio mbaya, hahaha, kama wewe umeshatosheka, nitakukuta nyumbani….

Alipokumbuka hayo maneno akashika kichwa, akageuka kumuangalia huyo mwanamke kitandani na jinsi alivyokaa mkao wa kihasara, akageuza kichwa haraka na kuanza kuendelea kutafuta nguo zake.

‘Huamini nini tena, …wewe sio mtoto mdogo, kama ni mke wako usiwe na wasiwasi yupo na mpenzi wake wanakula raha, kumbe mke wako ni mkali kiasi hicho, …’akasema na aliposikia hivyo akashituka na kugeuka kumuangalia huyo binti, na kusema

‘Unasema nini?’ akauliza na sasa akiwa katulia akijaribu kusikiliza sauti, kama vile anatafuta sauti ya mkewe itatokea wapi, na yule binti akalala kitumbo tumbo, na huku akisema;

‘Mhh, siamini..unajua hawa wanawake wengine bwana huwa wanajifanya wacha mungu kweli, lakini moyoni sio hivyo, wanakuwa hivyo pale wakiwa kwenye matatizo, lakini  wakipata mwanya mdogo tu, wanakuwa kama ngombe aliyekuwa zizini,… unajua kilichotokea…’akawa anajichezesha chezesha makalio yake na kumfanya Inspecta akeguke kuangalia kwingine.

‘Mkeo bwana, anakunywa, hivi ni mnywaji wa pombe hivyo, mimi nilijua ni mcha mungu wa kweli…, alikunywa sana, ikafika muda hata kusimama hawezi, mwenzake akaona hiyo imezidi kiasi, akamshauri waondoke,..lakini wapi, akawa anadai mengine…’akasema

‘Anadai mengine ana anadai nini….mwenzake nani huyo…?’ akauliza Inspecta kwa hamaki.

‘Alikuja na mwenzake mmoja, na walipoanza kunywa wakaja jamaa wawili watanashati, wakajiunga nao, ikawa kila mmoja na mwenzake, unaona hapo, kukawa hakutulii, kila mmoja anataka kumuonyesha mwenzake anajua ….’akakatiza.

‘Anajua nini…una maana gani, sio kweli,…haki ya mungu , nitaua mtu,…nguo zangu zipo wapi…’ akasema kwa hasira

‘Mkeo alipoulizwa na mwenzake kuwa kweli ana nia ya kufanya anachotaka kukifanya, maana alishavuka mpaka, na alikuwa akimtaka huyo mwenzake watoke, waende vyumba maalumu, akasema na yeye anafanya kama unavyofanya wewe…’akasema

‘Kama ninavyofanya mimi, kwani mimi nimefanya nini?’ akauliza kwa mshangao, na kabla hajajibiwa akaongeza

‘Kwani mimi nilifanya nini…?’ akauliza huku akijiangalia na mrembo akacheka na kusema;

‘Hahahaha , wanaume bwana, kwani wewe umefanya nini, hukumbuki eeh, haha eti kwani wewe ulifanya nini, …, hahaha, nyie wanaume bwana, mbona mna ubinafsi sana, wewe ulichofanya hukioni, unaona cha mke wako tu,…ningelikuwa mimi wewe, wala nisingelijali,..’akasema

‘Tatizo lako hujaolewa kwahiyo huna hisia za kindoa, ukiolewa utaona uchungu wa kuibiwa… nikimuona huyo mwanamke atanitambua, nitamuua, atajuta kuolewa na mimi, wewe utasikia hanijui mimi eeeh, na ole wako iwe ni uwongo,..ngoja, nguo zangu zipo wapi, niambie haraka, .’akasema

‘Unasema utamuua, acha mihasira hiyo…utafungwa…’akasema

‘Nitamuua, …yaani yeye kaamua kuwa kahaba,..hajui yeye ni mke wa mtu, anafanya kama nyie wanawake wahuni msioolewa, ….ngoja,..labda iwe sio kweli, nitamfanya kitu mbaya , hatakisahau maishani, nitamuulia mbali…’akasema kwa hasira.

‘Hahaha, niolewe mara ngapi wewe…tatizo lako unajifanya huelewi, anyway, tuongee kibiashara, maana naona unataka kuondoka….’akasema na kujigeuza akalala chali, hakuhangaika kujifunika, na hapo akamuona Inspecta akifungua kabati, na kuona nguo zake, akajua mtu wake sasa anaondoka.

‘Tuongee nini , kibiashara , biashara gani…?’ akauliza Inspecta akivaa nguo zake, na huku akikosea kufunga vifungo

‘Nakumbuka nilishakuambia kuhusu kuacha kufuatilia mambo yasiyokuhusu…’akasema

‘Mambo gani yasiyonihusu, kama yapi….?’ Akauliza Inspecta akitulia kumuangalia huyo mwanamke, kwa ule mlalo…na ibilisi akawa anafanya kazi yake…hasira ,mara tama kidogo, na akili ya ulevi ulevi, vikamchanganya mzee mzima…

‘Wewe huwa unajifanya unachunguza sana mambo ya watu, kiasi kwamba unawakera watu, unajua hii nchi yetu kila mtu ana mipangilio yake ya kupata riziki, na mingine ni ya kimabumashi, ….unaonaeeh, sasa kunaweza kutokea kutokuelewana, hapa na pale, …hapo nyie mnaingiza pua zenu bila kujua chanzo ni nini…’akasema

‘Bado sijakuelewa, ongea unachotaka kuongea mimi ninataka kuwahi nyumbani,…sijui kumetokea nini huko, sijihisi vyema…’akasema akipitisha ulimi kulainisha mdomo, akageuka kuangalia mlangoni.

‘Kwani kumetokea nini bwana, wasiwasi wako tu…mbona jana usiku hukuliona hilo…ulikuwa umeniganda kama ruba, hahaha mwanaume wewe, halafu wajifanya kumuonea wivu mwenzako, ukila vya wenzako na vya kwako ni lazima viliwe, titi for tati…au sio…hahahaheeeya…njoo baby, tuondoe hizo hasira….’akasema na kucheka huku akijichezesha kitandani.

Inspecta akageuka kumuangalia, halafu akageuka kuangalia mlangoni, na akilini akasikia sauti aliyosikia kwa mkewe akiwa kwenye ndoto, na kwenye ndoto hiyo alimuona mkewe kwa mbali akiwa kasimama , kachanganyikiwa, analia kwa kujuta huku akisema;

Mume wangu kwa lolote litakalotokea ujue nakupenda sana, ujua haya yote umeyataka wewe mwenyewe,usimlaumu mtu kwa lolote litakalotokea ujilaumu wewe mwenyewe…kwaheri….’ Sauti hiyo ikamfanya aanza kutembea kuelekea mlangoni na Yule msichana akasema;

‘Ukiondoka na kuniacha hivi, utakutana na uchafu wako kwa mkeo, na mwingine nautuma kwa baba ya mke wako……na unajua nini kitafuta baadaye,…’
Inspecta akasimama,na huki kichwani anasikia sauti ya mkewe akitoa maneno yale yale..

`Lolote litakalotokea ujilaumu wewe mwenyewe….’

Aliposikia sauti hiyo ya mkewe, hakusubiri, akatoka mle ndani na huku nyuma mdada akawa anatoa lugha ya kulaani na kuapiza kuwa atamfanya kitu mbaya, kwa kumtekeleza, hakujali, akatoka mle hadi sehemu ya mapokezi, akajaribu kumuuliza Yule mtu wa mapokezi ambaye alikuwa akijiandaa kuondoka , kumpisha mtu mwingine

‘Samhani ndugu yangu naomba masaada wako.’akasema

‘Msaada gani bosi, mimi nimeshamaliza muda wangu ndio naondoka hivyo…’akasema

‘Jana kulikuwa na mwanamke, alikuwa sehemu hizi,…akalewa na kuanza kuleta fujo, unamkumbuka….’akasema

‘Oh, Yule anaonekana ni mgeni sana, na sijui aliwezake kuingia, ..huku hakutakiwi mambo kama yale,…lakini hakuleta fujo, ila alilewa sana, na mwenzake akataka waondoke, lakini akawa hakubali, akawa anamlazimisha mwanamke aliyekuwa naye waingie kwenye vyumba vya wageni, wakati yeye ni mualikwa tu..’akasema

‘Alialikwa nani?’ akaulizwa

‘Na huyo rafiki yake…’akasema

‘Rafiki yake yupi?’ akauliza

‘Siwezi kukuambia, siruhusiwi….’akasema

‘Sasa huyo mwanamke yupo wapi?’ akauliza

‘Unajua bosi mimi kutoa siri haza za mwanachama, ila kama ni huyo mwanamke ameshaondoka kwenda nyumbani….’akasema

‘Kaondoka na nani,…saa ngapi?’ akauliza

‘Ni usiku huo huo, alikuja jamaa, tukasikia huyo mwanamke akisema;…’

‘Shemeji, shemeji…sasa .sijui ni shemeji yake kwa vipi....’akasema

‘Oh, nahisi ni Inspecta eeeh, yupoje, na alikuja baadaye au alikuwepo muda wote?’ akauliza akionyesha kutaka kuondoka.

‘Huyo shemeji yake ….aah, unajua siruhusiwei kuongea zaidi, ila ndio alikuja baadaye, na alipoona hiyo hali, akamshawishi huyo mwanamke, na baadaye akakubali wakaondoka naye…’akasema

‘Mke wangu muda huo alikuwa wapii chumbani au hapo nje…?’ akauliza

‘Tafadhali bosi,..nimekuambia vya kutosha…ukiwa hapa na ukiwa na mwanachama, kila sehemu ni hiari yako,….kama huna zaidi naomba uondoke…’akasema akigeuka kuangalia huku na kule, ilionyesha huyo mtu wa mapokezi alikuwa na wasiwasi kuongea zaidi.

‘Oh…sijui ….sijui…hii sasa ni kashfa, siwezi, haki ya mungu, nitaua mtu, huyu mwanamke atanitambua,….na huyu rafiki yangu nikikutana naye ama zangu ama zake, ina maana hata yeye ananifanyia hivyo…’akasema

‘Huyo aliyekuja baadaye ni rafiki yako, ehe, lakini, mbona yeye, hakuwepo,…alikuja badaye.’akasema

‘Hakuwepo alijuaje kuwa mke wangu yupo hapo..ina maana aliitwa na mtu , na huyo aliyemuita ni nani, huo ni ujanja wao…kwanini wasingeniita mimi, wakati mimi ni mume wake…’akasema kwa hasira

‘Mimi haya sijui zaidi,…..kwaheri, ’akasema huyo muhudumu na mara Yule muhudumu akasikia simu yake ikiingiza ujumbe, akawa anausome, halafu akamtupia jicho Inspecta, akasema;

‘Tafadhali uondoke…….hutakiwi humu ndani, vinginevyo urudi kwa mwenyeji wako…’akasema

‘Naondoka……lakini kabla ya yote nataka kuonana na muhusika wa humu ndani…’akasema

‘Unatakiwa uondoke, au urudi kwa mwenyeji wako…’ilikuwa sauti kali kutoka nyuma, alikuwa mlinzi akiwa na silaha yake,…akawa anamsogelea Inspecta, na Inspecta alipoona hivyo, akageuka kuondoka.

Inspecta alifika nyumbani kwake, ilikua ni alifajiri sana, kulikuwa kumeulia, akaingia na gari lake, na kulisimamisha, haraka akatoka na kukimbilia ndani, akazungusha kitasa cha mlango, mlango haukuwa umefungwa na ufunguo, akafungua na kuingia ndani
Mwili ukawa unamsisimuka, sio kwa hasira, sasa alihisi uwoga, alihisi hali isiyo ya kawaida,…akawa anaomba mungu kusiwe na tatizo, akaelekea moja kwa moja chumbani, akafungua mlango..

Kitandani kulikuwa hakuna mtu, ila shuka, lilikuwa limetupwa chini , kuonyesha kuwa kuna mtu alikua kalala hapo, akasogea hadi pale kitandani na kukaa huku akilini akitafakari yote yaliyotokea, alijua , na alijipa moyo huo kuwa mkewe atakuwa bafuni, au chooni,akasubiri, akaona kimia, akashindwa kuvumilia, akatoka taratibu hadi bafuni…

Macho yake yakatua kwenye beseni al kuogea,…mkewe alikuwa kalala ndani ya maji,, upande, kaegemea, mdomo upo wazi, macho yamemtoka….maji yamebadilika rangi, wekendu ..damu....

NB: Hicho kipande kidogo, japokuwa nimeandika kihivyo, tuwiane radhi kwa hilo


WAZO LA LEO: Katika maisha yetu magumu, tunahitajika kuhurumiana, na kusameheana, hasa mmoja anapokosea, kwani kuna kukosea kwingine kwa bahati mbaya, au kumetokea kwa kuzidiwa na mafungamano ya kimaisha,..hakuna kitu kibaya kama ufukara, ufukara unaweza kumtuma mtu akafanya mambo mabaya sana, ibilisi hapo hachezi mbali,..Lakini yote ni maisha cha muhimu sana ni kujitahidi kuwa na subira na kutenda mema…tukumbuke,mungu ni mja wa wote.
Ni mimi: emu-three

No comments :