‘Unataka kwenda
wapi?’
‘Naondoka zangu
nyumbani, kama hutaki kuniambia ulichoniitia hapa mimi inabidi niondoke tu….…’
‘Uende wapi,
nyumbani kwako, kufanya nini, na wakai mkeo yupo anastereje na mpenzi wake wa
siku ya leo..’
‘Unasema nini,
usinidanganye na propaganda zenu,…Mke wangu yupo nyumbani hawezi kufika hapa,
na hapa hajawahi kufika, angefika ningelishafahamu…’akasema kwa hasira akitaka
kuondoka, na Yule binti akacheka na kusema;
‘Hahahaha, unasema
nini, eti mke wako yupo nyumbani una uhakika na hiyo kauli yako, hebu njoo huku
nikuonyesha wapi alipo mke wako…’yule binti akamshika Inspecta mkono na kunza
kumvuta waende huko anakopelekwa…
‘Wapi….’akalalamika
Tuendelee
na kisa chetu
**************
Inspecta
kwa kutaka kuhakiki, akachukua simu yake ya mkonoi, na kumpigia mke wake,
hakuweza kumpata mke wake, akapiga tena na tena, lakini simu haikupatikana,
akageuka kumuangalia binti, Jembe kwa macho ya hasira.
Muda
huo, binti Jembe alikuwa anasoma ujumbe kwenye simu yake, na alipohisi kuwa
Inspecta anamuangalia,akainua uso kumuangalia Inspecta na kwa macho ya kurembua
akasema;
‘Baby,
upo tayari twende, nakusubiria wewe, au bado una matumaini ya kumuona mke wako
nyumbani?’ akauliza
‘Twende
wapi sasa?’ akauliza Inspecta akimuangalia huyo binti, na macho yake
yalipokutana na kuna hali ikamnasa Inspecta,…siri ya maanani. Inspecta
akajaribu kukwepesha macho, lakini ibilisi alishateka nafsi yake.
‘Na
wewe bwana, kwani tuliondoka pale mezani kwa madhumuni gani,…wewe si umesema
unataka kwenda kuhakiki kauli yangu,….’akasema kwa sauti laini ya kumpagawisha
Inspecta, na inspecta japokuwa alikwepesha macho, lakini ibilisi akamcheza
shere, akamuambia hebu muangalie tena….Inspecta akafnya hivyo.
‘Sikiliza
wewe….nikaumbie kitu, usinione hivi, ukafikiri mimi ni hivyo mnavyofikiria nyie,
utajukuja kujuta kwa hiki mnachokifanya, nakuambia ukweli…’akasema
‘Usijali..yote
haya nayafanya kwa vile nakupenda,…yaani usipungue uzito kabisa, kwa maneno mengi, wewe
fanya kile unachoona ni sahihi,…ila ujue kuwa mimi nafanya haya kwa vile
nakupenda, sio utani, sio kwa ajili ya kazi, hili nakuambi kutoka moyoni,
kwahiyoukitaka kuniua,..niue, lakini …’akamsogelea inspecta na akawa kama
anamkumbatia, na kutaka kumbusu mdomoni, na Inspecta akamsukuma.
‘Jamani
baby, mbona hivi tena, kwani tumekubaliana nini tena…usitake na mimi
nibadilike, mimi sitatumia nguvu, natumia akili, mtandao chaaah, unaumia ..na
utaumia kweli, na hata ukitaka kunitafuta, hunipati ng’ooooh, hilo
nakuhakikishia, muda huo unafikiri takuwa wapi….’akasema
‘Usinitishe
kabisa, mimi sasa naondoka, …’akasema akitaka kuondoka, na Yule binti akasema;
‘Nenda
halafu utakutana na uchafu wako,…utakutana na yale tuliyoyafanya kulee,
unakumbuka sana,…mimi nimekuita leo niwe na wewe, nina mazungumzo nyeti na
wewe, pamoja na yote, nitakusaidia mambo mengi tu, …niamimini mimi,…ila muhimu
usivuruge utaratibu, usivunja mkataba au sio?’ akauliza
‘Mkataba
wetu ulikuwa usiihusishe familia yangu, naona nyie ndio mumetangulia kuvunja huo
mkataba…’akasema Inspecta
‘Nani
kaihusisha familia yako baby, nimekuambia mke wako kaja mwenyewe kwa hiari yake
mwenyewe, na kuja kwenye hii hoteli sio mara ya kwanza, hilo nakuambia , kama
unataka kuhakiki, twende nikakuonyeshe…’akasema na Inspecta akasita, na
taratibu akarudi kukaa kwenye kiti.
‘Mbona
unarudi kukaa kwenye kiti tena bosi,…mimi nataka twende chumbani.haya mambo na
mengine hayatakiwi hapa hadharani, au unataka tumeage radhi hapa hapa, unaona
wenzetu kule hapa ni kila mtu na wake, ni ruhusa tu…ni kwa wanachama
tu…unawaona wale kule..wapo huru kabisa….’akasema
‘Wewe
mwanamke wewe, unajua nilikuwa nakuheshimu, na sijui kwanini umenileta hapa,
hapa sio mahali pangu,..na huko chumbani unataka tukafanye nini, unataka kunitia
majaribuni tena…’akasema na mara simu yake ikatoa ujumbe, akautizama ule
ujumbe, haukuwa na namba, akaufungua ule ujumbe, haukuwa na maneno, ila kuna
alama ya kuashiria kuna kitu kama picha au kifurushi cha video, kwanza akasita
kukifungua, lakini baadaye akaona kwanini asifungue…
Kilipofungua
akamuona mkewe akiwa kakaa kwenye meza, na pembeni yake kuna mtu, mwanaume,
lakini huyo mtu mwanaume alionyweshwa sehemuu ya mgongoni tu, sura ilikuwa
haionekani, wakawa wanakunywa na kuongea, na mkewe alionekana mwenye furaha tu,
na ilionekana walikuwa wakiongea jambo lililokuwa likimfurahisha sana mkewe,na
sauti ya kiume ikauliza;
‘Je
upo tayari kuwa na mimi, …ujue mimi nakupenda sana….’sauti ya kiume ikasema
‘Unanipenda,
kwa vipi?’ akauliza mke wake
‘Acha
mzaha wako, ….ina maana hujui nakupenda kwa vipi, kama mume wako anavyompenda huyo
aliye naye huko alipo…’akasema
‘Unasema
nini?’ akauliza mkewe akionyesha hamaki, na hata ule uma aliokuwa nao ukiwa
umeshikilia kipande cha tunda ukamdondoka, kuonyesha jindi alivyo shituka.
‘Mumeo
sasa hivi ana msichana mrembo, anastarehe naye, ukitaka kuona
nitakuonyeshe…’akasikia
sauti ya kiume ikisema.
‘Hapana
najua siku hizi kuna mitandao ya uwongo, siwezi kukubaliana na hilo na sina
haja ya kuona hilo jambo, mimi naona nirudi nyumbani, maana umeshaniumiza
kichwa changu…’akasema mkewe
‘Hahaha.
Hivi unataka nikueleweshe vipi, hayo siku hizi ni mambo ya kawaida tu, na wewe
unatakiwa uyazoee, leo ukiwa na mwingine usiogope,kwa vile na yeye yupo na mtu,
na yeye atakuja kuyazoea, lakini ukikaa nyumbani ukasononeka, utakuja kufa, na
mwenzako atabakia na huyo anayestarehe naye…’sauti ikasema
‘Yaani
hata wewe unaniambia hivyo..ina maana hata wewe…..’sauti ikawa kama inakatika
katika, maneno mengine yalikuwa hayasikiki…’
‘Lakini
mipango yetu umekubaliana nayo, au sio?’ akauliza huyo mwanaume
‘Nitafikiria,
nahitaji kujua mengi kwanza, pia…’maneno yakakatishwa, na ideo hiyo haikuendelea
tena.
‘Ni
nani huyu alikuwa na mke wangu?’ akauliza Inspecta
‘Utamuuliza
mke wako wako, na mke wako anachofanya ni kama hicho unachokifanya wewe, sio
jambo geni au sio, usimulaumu sana, maana ukitenda ujue na wewe utatendewa,au
sio…?’ akawa kama anaulizwa
‘Kwani
mimi nimemtenda nani mke wangu, hebu niambie?’ akauliza
‘Hahaha,
hivi wewe hukuja kwangu kwa hiyari yako mwenyewe, na kuna ushahidi unaonyesha
jinsi ulivyokuwa ukiongea na mlinzi kuwa umenipenda, na unahitaji kunifuatilia,
ukafika sehemu ukabadili nguo, ili uonekane mtanashati, au sio, …je huo ni uwongo,
sema mwenyewe, hukunifuatilia,…?’ akaulizwa
‘Hizo
ni mbinu zenu, mimi nilipanga kuja kwako kutaka kupata taarifa, na hizo
zilikuwa mbinu zangu, hayo mengine mumeyapanga wenyewe kwa kuunganisha
unganisha habari ili ziendane na mnavyotaka nyie…’akasema
‘Yoyote
atakayeiona hio kanda ya video hatakuwa na mashaka, na hata ukipeleka kwa
wataalamu wa video wanaoweza kutambua kuwa video hiyo ni kuunga unga au ni ya
asili, watathibitisha hilo,….kauli, vitendo, na kila kitu ni asilia, hakuna
kuunganisha hapo,..kwanini nikusingizie baby, je kweli hukunifuata, je kweli
hatukustarehe na mimi siku ile, je hayo ni ya kuunga unga….?’ akauliza
‘Mliniliwesha
nikawa sijatambui…’akasema kwa sauti ya kukata tama.
‘Hahaha,
ukitaka nikuonyeshe hiyo video utaona mwenyewe, kama kweli ulikuwa umeleweshwa,
kila kitu kipo wazi, inaonekana kabisa ulilewa mahaba….ukanizimia, na ukawa
unatamka mwenyewe, kwa kauli yako pana, kuwa hujawahi kuona msichana mrembo
kama mimi, na hutaweza kuniacha kamwe..’akasema
‘Mimi!!?,
Mimi nilisema hivyo, haiwezekani?’ akauliza
‘Twende
chumbani ukaone mwenyewe…’akaambiwa akishikwa mkono.
‘Ina
maana hiyo kanda chafu unayo, unatembea nayo?’ akauliza Inspecta
‘Kuna
utaalamu baba, mimi nikitaka kuipata naipata, na sio wote wanaoweza kuipata,
na hata mimi naipata kwa kibali
maalumu…tunahakikisha siri zako zote zinachungwa hadi hapo utakapokiuka
mkataba….’akasema
Mara
ujumbe ukaingia kwenye simu ya Inspecta, ilikuwa ujumbe wa mtandao kuwa namba
ya mkewe,aliyokuwa akipiga, kwa sasa anapatikana. Inspecta alipoona ule ujumbe,
kwa haraka akampigia mkewe, na mkewe akapokea, na kila mmoja akauliza
‘Wewe
upo wapi…?’ kauli zikakutana
‘Mke
wangu upo wapi?’ akauliza Inspecta
‘Na
wewe mume wangu upo wapi?’ akauliza mkewe
‘Ina
maana tunashindana, hukunielewa kuwa nafanya haya kikazi…’akasema Inspecta
‘Kwani
mimi haya nafanya kimaigizo, hata mimi nafanya kikazi, ..’sauti ya mkewe,
ikasema na ilikuwa sauti ya kama mtu kalewa.
‘Kwani
upo wapi?’ akaulizwa
‘Niambie
kwanza na wewe upo wapi, na huyo mwanamke ni nani?’ akauliza mkewe.
‘Naomba
urudi nyumbani, tutaongea nikifika huko nyumbani, na ni nani kakuleta hapa,
umepajuaje hapa, …?’ akaulizwa
‘Kwani
wewe ulipajuaje hapa, ulivyopajua wewe ndivyo na mimi nilivyopajua, unachofanya
wewe na mimi ndicho ninachofanya tatizo lipo wapi..’ilikuwa sauti ya mkewe na
sasa haikujificha, kulikuwa na hali ya kulewa, kutokana na sauti ilivyokuwa ikitoka.
‘Ina
maana umelewa mke wangu, au umeleweshwa…?’ akauliza akionyesha sauti ya
kusikitika.
‘Nimekunywa
mwenyewe kwa hiari yangu, na wala sijalewa,kwani wewe hunywi, hapo ulipo
hujakunywa, japokuwa nimekunywa lakini hapa nilipo nina akili zangu timamu
kabisa..kabisa…nastarehe kwa raha zangu, kama unavyofanya wewe..halafu unasema
au nimeleweshwa, kwanini nileweshwe wakati mimi ni mtu mzima na nina akili
zangu hahaha utajijuuuh…’akasema mkewe na kucheka, na sauti nyingine ikaguna,
ilikuwa ni sauti ya kiume.
‘Upo
wapi huko wewe mwanamke, ninakuja huko na kitakachokupata usije kunilaumu
..utanitambua…?’ akauliza Inspecta mwili mzima ukimzizima kwa hasira
‘Hahaha
heeya,..njoo, nipi kwenye vyumba maalumu vya starehe, najua na wewe upo kwenye chumba
cha starehe na mwenzako, kwani kuna tatizo gani, siku moja moja sio mbaya,
hahaha, kama wewe umeshatosheka, nitakukuta nyumbani….’akasema na mara sauti ya
kiume ikiguna tena, Inspecta akazidi kuchemka kwa hasira na wivu, akageuka
kumuangalia binti Jembe na kusema;
‘Hii
maana yake nini?’ akauliza Inspecta akiwa katoa jicho la hasira
‘Kuhusu
nini?’ akauliza Binti mrembo
‘Haya
mumeyafanya nyie kwa makusudi , nauliza maana yake nini, mnataka nini kwangu…?’
akauliza akimsogelea binti Jembe na binti Jembe hakusogea nyuma akawa kasimama,
hadi pale mkono wa Inspecta uliposhika bega la Binti Jembe , na Binti Jembe
akahisi maumivu, akainua mkono wake na kuushika mkono wa Inspecta, akasema.
‘Sikiliza
baby,unaniumiza, hatuendi hivyo, mimi nikitaka kukuumiza nitakuumiza kweli, na
mimi nakuumiza moyoni, ondoa mkono, au ulegeze mwanamke hafanywi hivyo, nguvu
hazilipi kamwe…’akasema halafu akashika mdomo na kunyosha kidole kuelekea
kwenye simu ya Inspecta
Kumbe
simu ya Inspecta bado ilikuwa hewani, Inspecta hakuwa ameizima hiyo simu, na
kwenye simu akasikia mkewe naye akisema;
‘Nimesikia huko ukiitwa baby eeh, kumbe bado una na huyo baby wako, usijali na mimi nina baby wangu hapa,.... sogea
huku baby tumalize kazi yetu……’ilikuwa sauti ya kilevilevi …
Inspecta
akatoka pale kwa haraka akaelekea sehemu ya mapokezi, akaongea na Yule muhudumu
lakini walionekana hawaelewani, akatoa kitambulishi chake..
‘Inspecta
humu vitu kama hivyo haviruhusiwi, unataka kufanya nini, unakumbuka mashartii
ya kuingia humu, nilikuonyesha na ukayasoma, ….
Kuna
sehemu imeandikwa wazi, ..`hata kama
utaona mke wako au mume wako yumo humo na mtu mwingine, huruhusiwi kumuingilia,
maana kila mtu kaja kwa hiari yake mwenyewe… unakumbuka hayo maandishi,
uliyasoma na ukaweka sahihi yako,..’Ilikuwa sauti ya mdada ikasema kutoka nyuma
yake, na Inspecta akageuka kwa hasira kwa dhamira ya kutoa kipigo, lakini alipogeuka
akamuona mdada yupo na walinzi wawili huku na huku yeye yupo kati kati.
‘Kama
unataka nikupeleke alipo mke wako, kwanza twende chumbani, huko nitakuambia
wapi alipo mke wako, na ukitaka nitakupeleka, mguu kwa mguu umuone akiwa na
mpenzi wakeeeh, hehehhe…,Inspecta , Inspecta….’akasema huyo mdada kwa dharau,
na wale wapambe wake wakawa wanatunisha vifua vyao, …walionekana ni watu wa
kazi kweli.
‘Upo
tayari twende,… lakini kwanza utii masharti yangu,…’akasema Yule binti
akimuangalia Inspecta machoni, hakuonyesha wasiwasi, abasamu lilijaa tele
mdomoni.
‘Masharti
gani?’ akauliza Inspecta.
‘Unayafahamu
sana, sihitaji kuyarudia, ukumbuke usipoyatii, kwanza hutamuona mke wako, na
pili uchafu wako utazidi utasambazwa kila kona …, na safari hii utamfikia hata baba
na mama mkwe wako, unaihisije hiyoo, inauma lakini ndio ukweli ulivyo, mimi
natimiza wajibu wangu, pole Inspecta, I
love you baby….’akasema Binti Jembe, na Inspecta akawa katulia, akitetemeka
mwili mzima kwa hasira.
Yule
binti bila kuogopa akamsogelea Inspecta na kupitisha mikono yake laini kifuani
kwa huyu simba aliyejerushiwa, akapeleka kidole kwenye mdomo wa Inspecta,
akasema;
‘Twende
zetu baby, hizo hasira zina dawa yake wala usijiumize, ukistarehe na mimi
utasahau kila kitu….mimi ndiye dawa ya yote hayo…’akasema na kumshika mkono
Inspecta.
Inspecta,
hakuweza kusema neno akawaangalia wale mabaunsa wawili, akilini alitaka
kuwaonyesha kuwa yeye hawaogopi, na anaweza kupambana nao, lakini akachelea ,
akijua yupo sehemu ambayo vitu kaam hivyo havitakiwi…akanywea,
‘Baby
twende..hebu fikiria, kama mwenzako kaamua kukufanyia hivyo…yupo anastarehe na
mwenzake, wewe utapungukiwa na nini ukiwa na mrembo unayempenda, kwani
hunipendi, … mimi nakupenda sana baby, twende basiiiih….’akasema akimvuta mkono
Inspecta kuelekea huko chumbanii….
NB
Haya wapendwa mimi sisemi zaidi ndiyo mambo ya dunia yangu, mwenye akili
atatambua
WAZO LA LEO: Hadaa katika maisha
yetu imekuwa ni jambo la kawaida tu, mtu kumuhadaa mwenzake ili apate jambo,
atatutumia kila lugha za mapambio ili kitu chake au jambo lake lipokelewe, na
yeye kupata pesa au malipo ya hicho kitu au hili jambo, huku mtu huyo akijua
alichokisema sio kweli, hii ni dhuluma na huu ni wizi.
Wewe ukiona mwizi anapigwa kaiba, unachhekelea
tu, au wewe ukiibiwa unaumia sana, na unakuwa msitari wa mbele kumpiga huyo
mwizi na kumlani, lakini kila siku unaibia wenzako, kwenye biashara zako,
kwenye shughuli zako za kila siku unazozifanya kwa njia ya hadaa.
Tuweni
makini, kwenye kuzitafuta riziki zetu, tujishughulishe kwenye kupata kipato
halal , kwa kuwa wakweli kwa kufanya hivyo riziki na maisha yetu yatanyooka,
maana ukweli ni Baraka, na Baraka itakuza vipato vyetu.
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment