‘
'DUNIA
YANGU’
‘What,..dunia
yangu..ana maana gani ?’ .....akakumbuka hiyo nembo aliiona wapi, kule kwa mdada, na kwenye CD, aliyoichukue kule kwa mtaalamu wa komputa kwa uficho...akajikuta akijiuliza mara nyingi,...
‘Hii
ina maana gani?’
mara akasikia mlango ukisukumwa akageuka
kuangalia ni nani alyeingia asubuhi hiyio, na kujikuta akiangaliana na Inspecta mwenzake ....
Tuendelee na kisa chetu...
************
‘Umeshapona mkuu...?’ ilikuwa sauti ya Insecta Maneno, akiwa kashikilia mikono kifuani kuonyesha kuwa hana
wasiwasi, lakini macho yake yalikuwa uakiangalia komputa yake ya mezani,
Inapecta alimuangalia rafiki yangu, akaona jinsi mwenzakew alivyobadilika, afya
yake na usoni alionekana mtu mwenye kurizika, tofauti na ilivyokuwa siku za
nyuma, sijui karizika na nini.
‘Oh,
unajua leo nimeona ajabu sana, nimefika hapa asubuhi na kushangaa kusikia na
wewe siku hizi unafika asubuhi na mapema, vipi kuna dharura gani?’ akauliza
Inspecta
‘Wewe
ulikuwa haupo, na unavyojua wewe na mimi ndio tuna kazi nyingi kwenye kikosi
chetu, ..kwahiyo inabidi niwajibike, sikutaka ufike ukute mlundikano wa kazi,
hata hivyo, ..nimerudi kidogo kuna kitu nilisahau...’akasema
‘Ulisahau
kuzima komputa yako au sio?’ akauliza na Inspecta kwa haraka akaelekea kwenye
komputa yake na kusema;
‘Oh,
Mbona imezimika!?’ akasema kwa mshangao
‘Nilifika
na kuikuta kama ipo haijazimwa, maana kitaa cha kuashiria kuwa haijazimwa
kilikuwa kinawaka, na wakati nataka kuhakiki, ndio ukatokea,...’akasema
‘Ok,
hamna shida, naona imeshajizima, ilichelewa kuzimika yenyewe, niliacha ikiwa
inaendelea kuzima, nikaharakisha kwenye dharura zangu, mambo ya kifamilia, si
unaelewa tena....’akasema
‘Kwani
shemeji karudi?’ akauliza
‘Bado
ana vikao vyao huko kwao, mke wangu ni mtu wa shughuli, na hapendi kuwa mbali
na shughuli, kila shughuli yumo, sasa imenijia akili, kama anapenda shughuli,
inabidi nibuni miradi ya kumshughulisha....’akasema na huku anawasha komputa
yake tena.
‘Kama
ipi..?’ akauliza mwenzake.
‘Yeye
si mama shughuli, na mimi naanzisha mrdai wa shughuli, namuanzishia mradi ambao
yeye atausimamia, nikitafuta na akina mama wengine majembe wa kumsaidia,...unajua
mkuu, tusikalie kuwazia ajira tu, hiiz ajira zetu zina mwisho wake, na mwisho
wa sisi tuliobobea kwenye ajira mara nyingi inakuwa ni mbaya, unaacha kazi huna
cha kukuendeleza, unakuwa kama unaanza maisha mengine upya...’akasema
‘Ok,..sasa
tufanyeje...?’ akauliza na hilo swali likamfanya mwenzake amuangalie Inspecta
kwa macho ya udadisi, maana siku zote akianza kuongea mazungumzo kama hayo mwenzake
anakuwa kwenye kupinga tu.
‘La
kufanya ndio hilo, tuwaanzishie wake zetu miradi, tunachotakiwa kuangalia ni je
mke wako ana kipaji gani, kama ni msusi, muanzishie mradi unafanana na hivyo,
kama ni mama shughuli kama mke wangu, unamuanzishia mradi wa shughuli,
unamjengea mazingara ya shughuli, kama ni ukumbi au ofisi, unaangalia ni kitu
kinahitajika kwenye shughuli, unatafuta mtaji, unamuanzishia, cha muhimu kwanza
ni kumuelismisha hata ikibidi kumpeleka shule...’akasema
‘Ni
wazo zuri, siwezi kukukatalia, lakini je ataelewa, maana unaweza ukatumbukiza
sukari baharini, unatategemea nini hapo...mimi hilo la shule kwanza nakuunga
mkono, ili ajua ni kitu gani anakifanya, sio kujaribu, .....eeh, au...?’ akasema
na kuuliza na Inspecta Maneno akaona mwenzake anakuja kwenye anga zake,
akasema,
‘Ndio
hapo nikasema ikibidi unampeleka shule, kuna semina za kuwekeza, kuna shule za
kuwekeza pia, zipo nyingi tu siku hizi, ni pesa yako tu,....kwa mfano nikuambie
kuna huyu tajiri mmoja eeh,...sijui kama
unamfahamu, yeye keshabuni hilo wazo, kaanzisha shule za namna nyingi, na
anatoa semina na wakati mwingine bure, akilenga vipaji vya watu....’akasema
‘Tajiri
yupi huyo?’ akauliza Inspecta kwa mashaka, lakini akijifanya anataka kujua
‘Huyu..eeeh,
bwana Diamu, huyu jamaa kichwa, kabuni miradi mingi kutegemeana na vipaji vya
watu, ukimuona navyofanya utazani anapoteza pesa zake bure kumbe ana malengo
mapana, anaanzisha mradi huu, anawafundisha watu, ....kwa malengo maalumu,
ambayo mwisho wa siku ana[ata nay eye chochote humo...’akasema
‘Umesema
tajiri gani?’ akaulizwa
‘Diamu....ushamsikia?’
akaulia
‘Namsikia
tu, sijawahi kumuona, kweli yupo hapa nchini?’ akauliza
‘Ana
watu wake, yeye ni muelekezaji tu, ana vichwa vingi vyenye vipaji, watu hao kwa
vipaji vyao, wanatumia mikono yao wanazalisha...kwa kupitia wao, ananeemeka, na
wao wananeemeka, ndio kujiajiri huko, ukikalia hizi kazi za mshahara usiokidhi
mahitaji , utakufa masikini....’akasema
‘Sawa
sasa hebu niambie wewe utawezaje kuelekeza nguvu zako kwenye miradi huku
unatakiwa kuwajibika ofisini, utagawaje muda wako...?’ akaulizwa
‘Hilo
mbona linawezekana,...mfano ndio hivi nawahi ofisini mapema, najipanga , najua
mwenyewe jinsi ya kufanya, kiasi kwamba siharibu kazi za watu...’akasema
‘Kwa
ufupi haiwezekani, unachofanya ni kuiba muda wa watu wa kazi, kwa manufaa yako,
au sio?’ akaulizwa
‘Sasa
hebu niambie utafanyaje, kama ni hivyo, ili usifanye haya yote, watoe mshahara
wa kukidhi mtakwa ya wafanyakazi wao,...kama wangekuwa na haki, wasingelitoa
marupurupu mengi kwa watu wachache, wangatoa kiasi na kiasi kingine wakaelekeza
kwenye kipato cha wafanyakazi wa chini..hili halipo, kwa vile wao wanajifikiria
wao wenyewe....’akasema.
‘Haya
bwana, sasa niambie kwa jinsi gani utamuwekea hiyo miradi mkeo, au unamtegemea
huyo huyo tajiri ?’ akaulizwa, na hapo Inspecta akakukunja uso kidogo,
inaonekana kauli ya mwenzake hakuipenda, ila hakuvunjika moyo akasema;
‘Sio
kumtegemea huyo tajiri, yeye ametoa fursa, watu wajifunze, sasa utajifunza
bure, ni lazima umlipe kwa vile kawekeza, ni ujanja wake...mengine yanayofuata
ni wewe mwenyewe, sijui unanielewa...’akasema.
‘Sawa
nauliza hivi utamuwekezeaje mkeo, utampeleka shule, au ulishamuandaa , na lini
maana nijuavyo, yupo kwao, au,...hapo nataka kujua ili na mimi nifahamu...au na
wewe unataka ulipwe ndio unielekeze na mimi...’akauliza na kucheka kama mdhaha,
lakini inspecta sasa hivi hakuonyesha lile tabasamu lake la awali akasema;
‘Mimi
namfahamu sana mke wangu, na nimeshampima, nikisema kwa hivi sasa nimpeleke
shule hatutaelewana, yeye na shule ni kama maji na mafuta, mke wangu hapendi
kusoma,...niliwahi kumshauri awalia akakataa...’akasema
‘Kwahiyo...?’
akauliza na kabla hajamalizia swali lake Maneno akasema
‘Japokuwa
mke wangu hapendi shule, lakini ana akili ya kuzaliwa, ana kipaji cha kuongea, kwahiyo
nitaelekeza nguvu zangu huko huko, ninachotaka kufanya kwa sasa ...nikumtafutia
majembe, yaani akina mama wengine vichwa, ambao watashirikiana naye, kwa vile
mimi natoa mtaji, na wazo na kila ...ofisi nk, basi yeye atakuwa msimamizi,
kiongozi wao,...wewe mwenyewe utaona...’akasema
‘Na
hao akina mama wengine utawapataje, maana nionavyo, unachotaka kufanya hapo ni
ujanja ujanja utumie nguvu za wengine a,bazo unaziita vipaji kwa manufaa yako,
na ukumbuke kiongozi ni lazima ajue elimu ya kuongoza, awe na hekima ya
maamuzi, ili kuhakikisha haki inakuwepo, huoni kuwa ukimfanya mke wako
kiongozi, wakati hana ufahamu wa huo uongozi, utasababisha kutokuelewana na
wenzake, atakuwa anatumia nguvu kuliko hekima na akili?’ akaulizwa
‘Wewe
utaona tu,..hiyo kazi ndogo, nimeshapata shule ya maana ya jinsi ya kuwekeza,na
kuwaelekeza watu wa namna hiyo, mimi nitakuwa mwalimu wake,na mwalimu wao pia,
ni kazi ndogo tu..’akatulia kidogo kama anawaza jambo.
‘Kidogo
kidogo mwenyewe atakubali, ni njia ya kusaidiana, nitaona kama inawezekana,
kigharama, wengine nitawapeleka semina au shule,...hilo nitalifanyia kazi,na
njia mojawapo ya kuwavuta wadhamini,..unapata misaada kwa njia hiyo, ilimradi
uwe na ushawishi, na ushawishi mkubwa kwa sasa ni kuona unawasaidia akina mama,
wewe mwenywe utakuja kunivulia kofia...’akasema
‘Mimi
bado nina mashaka, japokuwa nakuunga mkono na akili hiyo, lakini najiuliza
jinsi gani ya kuwapata hao watu, ikizingatiwa kuwa ni wake za watu au sio,
umesema wake, ina maana ni wake za watu, hujasema lolote kuhusu waume zao,
usije kuleta mifarakano, uwe makini na hilo...’akaambiwa
‘Hahaha,
unajua mkuu, unajifanya kama huelewi, hao akina mama wenyewe watajileta...tatizo
unashindwa kunisifia tu, si unakumbuka tabia yangu, nikitaka jambo ni lazima
nilpate, na wazo hili ni lazima nilifanyie kazi na nitafanikiwa tu, anyway,, ...samahani kuna jambo jingine
nimefuatilia hapa naona muda umekwenda, inabidi niharakishe kabla kazi
hazijaanza, unaonaje tukija kuliongelea hili swala kwa nafasi yake,
....’akasema akisogelea komputa yake, na inspecta akaelewa kwanini mwenzake
anasema hivyo
‘Hamna
shida mimi nipo ofisini kwangu, ukimaliza tutaongea, hata mimi nina mambo muhimu
nataka kuongea na wewe,...’akasema Inspecta Moto
‘Mmabo
gani tena hayo, ya kikazi au ni haya haya tuliyokuwa tukiyaongelea...?’
akauliza Maneno kwa wasiwasi, akimuangalia Inspecta mwenzake.
‘Mimi
nilikuwa sipo,...siku mbili hizo, sasa nitajuaje umefikia wapi...’akasema Moto
‘Ok,
ok, nimekuelewa, nilifikiri kuna jambo jingine maana na wewe bwana huachi
kujilimbikizia kazi hata sizizo na maana, ...kama ni hivyo, nitakupa muhutasari
wa niliyofanya na nimeishia wapi....’akasema akiendelea kufanya analolifanya.
‘Sio
kweli kuwa najilimbikizia kazi zisizo na muhimu, hizo kazi ni wajibu wetu, ila
tunapenda kuziacha mpaka zipate msukumo fulani, sio vyema, mimi sipendi
hivyo...’akasema
‘Nikuambie
kitu, achana na tabia hiyo, utajizeesha muda si wako, angalia mbele, maisha
yalivyo, ...maisha ni mafupi, muda wa kufanya mambo hautoshi,sasa hivi utafikia
muda una majukumu mengi, huna miradi, huna akiba, watoto wanahitaji ada,
majukumu ya kifamilia, ya kijamii, yanaongezeka, mshahara ni ule ule mwisho
wake ni nini kama sio kufa kwa shinikizo la damu, fanya kazi kwa wasaa, jipe
muda wa kutafakari mambo yako...’akasema
‘Unasema
kufa kwa shinikizo la damu, mmmh, kama alivyokufa muheshimiwa au sio...?’
akauliza Inspecta
‘Hilo
umesema wewe, ..’akasema akionyesha kutaka muda wa kufanya mambo yake.Na
Inspecta Moto akawa anataka kuondoka, lakini kabla hajasogea mwenzake
akamuuliza swali;
‘Kwa
vile umegusia swala la muheshimiwa, hebu niambie vipi mipangilio yako maana
kwenye kikao na wakubwa mimi niliwaelezea hali halisi...’akasema Maneno
‘Hali
halisi ipi, maana nikumbukavyo, bado tulikuwa kwenye kukusanya ushahidi...na
sijapitia hayo maelezo uliyopeleka kwa wakubwa...’akasema Moto.
‘Ushahidi
upi zaidi ya huo wa madakitari, kuwa kweli muheshimiwa alikufa kwa shinikizo la
damu, na ndivyo nilivyopeleka taarifa yetu, na nimesema tumekubaliana hivyo,
mimi na wewe, utaona taarifa yangu, fupi, na yenye umakini wa kitaalamu...hakukuwa
na zaidi, na wao wakasema sawa,...’akasema Maneno
‘Wakasema
sawa, kirahisi hivyo, hawakutilia mashaka, maana kwa hali ilivyo, hata mimi
ningelitilia mashaka, kama kweli unamfahamu huyo muheshimiwa...walikubali
kirahisi hivyo?’ akauliza Inspecta kwa mshangao
‘Kwani
wangelisema nini, wakati vitu vipi wazi, je wewe unapingana na taarifa ya
madakitari, je wewe unapingana na familia husika, mashahidi
tuliowahoji,....hebu niambie kama familia husika wanahisi mtu wao kafa kifo cha
utata wangelileta malalamiko kwetu, je walifanya hivyo, ina maana wao wamerizika
na kifo cha jamaa yao kuwa kafa kifo cha kawaida, sasa wewe unataka kufanya
nini, tusiendelee na malumbano yale yale,...oka, nona uniache, nina kazi nataka
kufanya...’akasema
‘Wewe
ndio umeanzisha hiyo hoja...nilikuwa sijajipanga kuliongelea hilo, na kwa vile
umeligusia ni vyema tukawekana sawa, ninachosigishana na wewe ni ile kusema
tumekubaliana, hatukuwahi kukubaliana kwa hilo,....’akasema Inspecta Moto.
‘Nimefanya
hivyo , kwa nia njema kabisa...kuweza wewe kutuliza kichwa na kuangalia mambo
mengine kwa nia njema kabisa kwako wewe na kwa majukumu yetu pia, kuna mambo
mengi ya kufanya, kwanini tupoteze muda kwa kitu ambacho kipo wazi, ina maana
mimi nimefanya vibaya, ?’ akauliza akionyesha mshangao
‘Siwezi
kusema umefanya vibaya au vizuri, tatizo hapo ni kuwa hukunishirikisha kwenye
hiyo taarifa, mimi ningekushauri nionavyo mimi, wewe ulichofanya ni kukimbilia
kutoa hitimisho lako binafsi na kunishikirisha na mimi, ...hilo ndilo
tatizo...’akasema
‘Ok,
sasa unataka kusema nini?’ akashika vidole viwili karibu na shavu, huku
akimuangalia Inspecta mwenzake.
‘Umeshapeleka
hiyo taarifa kwa wakubwa na mumekubaliana iwe hivyo,mimi nitasema nini hapo,....na
hali ilivyo, yaonekana inatakiwa iwe hivyo, mimi inaniuma sana kuona haki na
ukweli unapindishwa...’akasema
‘Haki
ipi na ukweli upi uliopindishwa mkuu,...hebu nipe ufafanuzi wa kitaalamu, maana
wewe ni mkufunzi, na unajue vyema ni kitu gani kiwepo, ili kushinikiza hoja,
haya nipe hoja yako ya kitaalamu...’akasema
‘Unajua
mimi mpaka kesho sikubaliani na hiyo kuwa muheshimiwa amekufa kifo cha kawaida,
kuna hujuma zipo, na zimetengenezwa kitaalamu, ili iwe hivyo,na watengenezaji
walijua hizo hoja zitalindwa vipi.....sasa mimi nilitaka hili tulifanyia kazi
ili hali hiyo isije kujirudia tena...’akasema
‘Una
uhakika na hiyo kauli yako, maana usiseme tu, nipe uhakika wako na ushahidi
wako wa kitaalamu,....ili nikuelewe’akasema Maneno
‘Ndio
nilitaka kulifanyia kazi hilo, siku mbili hizi nimejikuta nashindwa kulifanya
hilo
kwasababu zilizokuwa nje ya uwezi wangu....’akatulia
‘Sababu
za kuumwa sio, au kuna jingine lililokuzuia,...?’ akauliza Maneno
‘Unajua
mimi sikupendezewa kwa wewe kupeleka hitimisho hilo kwa wakubwa, mimi na wewe
tulitakiwa tuwe kitu kimoja, unakumbuka tumetoka mbali, sasa iweje ifike mahali
tuanza kuachana njia panda...hebu niambia tatizo hapo ni nini, unakumbuka kiapo
chetu, kuwa tupo tayari kufa kwa ajili ya kusaidia watu...kiapo hicho
kimepotelea wapi...’akasema Moto
‘Sijakuelewa
unataka kusema nini hapo...’akasema Maneno akiwa hamuangalii Moto, akawa
anafanya jambo kwenye komputa.
‘Huwezi
kunielewa kwasababu wewe umeshaamua, na hatua uliyofikia, umesharizika nayo,
huwezi kuona tena uchungu,...lakini kumbuka mwenye kovu usidhani kapoa, kumbuka
dhuluma haidumu, kumbuka,kiapo ni ahadi...’kabla hajamaliza, Inspecta akasimama
na kusema;
‘Unajua
sikuelewi, kwani unanishuku nini mimi...?’ akauliza kwa hasira
‘Sijakushuku chochote usijihami,
ila nakutahadharisha, ...unakumbuka siku zetu za mwanzo, hilo la kuambiana
ukweli ndio ilikuwa msimamo wetu, mwenzako akitetereka unamuonya hapo hapo, ili
tuwe na msimamo mmoja, je upo kwenye kile kiapo au kuna namna nyingin
inakusukuma ufanye vinginevyo...’akasema
‘Kama
vipi nimefanya vinginevyo, nionyeshe kosa langu lipo , ni huko kupeleka taarifa
ambayo wewe unaona haijakamlika, au kuna jingine unanishuku?’ akauliza kwa
sauti ya juu kidogo.
‘Bwana
wewe endelea na kazi yako tutakuja kuongea ukiwa umetulia, ...’akasema Inspecta
na kuondoka, na Inspecta mwenzake akabakia amesimama akimuangalia mwenzake
akiondoka, akawa kama anawaza jambo, akashika simu yake na kupiga namba..
******
‘Mume
wangu, leo ujitahidi kufika nyumbani mapema...’ilikuwa sauti ya mke wa Inspecta
Moto.
‘Oh,
mke wangu, unajua ndio nimefika kazini na siku mbili nilikuwa na hiyo mitihani
ya kufuatilia jambo, sasa nimejikuta nina kazi nyingi za kufuatilia hapa
ofisini, sizani kama nitaweza kuwahi kwani kuna nini cha zaidi?’ akauliza
‘Unasema
una siku mbili hujafika kazini,...ulikuwa wapi, mimi najua ni hiyo siku moja?’
akauliza mkewe kwa wasiwasi.
‘Siku
hiyo nyingine nilikuwa kwenya kufuatilia jambo, sikuwaeleza wenzangu, hayo ni
maswala yetu ya kazini wewe niachie mwenyewe, niambie kuna kitu gani muhimu
unachohitajia mimi kuwahi?’ akauliza
‘Kuna
kitu gani muhimu?!, yaani mimi mkeo nakuomba uwahi unauliza kuna kitu gani
muhimu!, na nakuomba muda ambao sio wa kazi, ..mume wangu mbona unabadilika hivyo
kuna nini kinachoendelea, ....?’akauliza mkewe
‘Ni
maswala ya kazini tu, nitakuja kukuambia kwa wakati muafaka...ila nahisi
sitaweza kuwahi kufika nyumbani labda kama kuna swala muhimu sana...’akasema
‘Sasa
ni hivi, mwenzako kanialika kutembelea miradi yake, nia ni kunivutia na mimi
niweze kuwekeza, sasa hivi akina mama wana miradi yao, wanasaidiana na waume
zao, nimeona ni jambo jema tukiongozana na wewe ukajionee mwenyewe ....’akasema
‘Mwenzangu
yupi?’ akauliza kuonyesha mshangao, na akilini akajua ni yale yale ya Inspecta
mwenzake.
‘Mwenzako
yupi tena, si Inspecta rafiki yako....’akasema mkewe
‘Lakini
mkewe si hayupo, atakualikaje wewe bila mimi kunihusisha, mbona nipo na yeye
hapa ofisini hajaniambia kuwa atakualika wewe,....?’ akauliza
‘Mangapi,mumekuwa
mkifanyiana kama ndugu na tulikuwa tunaitana uwepo au usiwepo, wewe unatoka na
mkewe na mimi natoka naye tukiaminiana kabisa leo mbona unauliza hivyo, ile hali
ya kuaminiana imeishia wapi, mbona mimi sielewi, kuna nini kimetokea....’akasema
mkewe
‘Lakini
tulikuwa tunambizana mimi na mwenzangu, sizani kama ilikuwa inatokea tu, bila
kujulishana kinachoendelea, je uliwahi kuitwa au kwenda naye mahali bila mimi
na yeye kuliongelea kabla, hili naliona kama
lina ajenda ya siri..’akasema
‘Kama
ni ajenda ya siri umeianzisha wewe mwenyewe, maana leo unasema utachelewa
kikazi, lakini sio kweli, kuna sehemu unakwenda kukutana na mtu, na nahisi mtu
mwenyewe ni mwanamke ni kweli si kweli, na huyo simuamini kabisa, je tuliwahi
kukubaliana hilo ....’akasema mkewe kwa sauti ya kulalamika
‘Nani
kakuambia hayo, nani kakumbia huo uwongo, toka lini ukanitilia mashaka katika
maswala yangu ya kazini, umeanza lini hiyo tabia mbaya, sasa nasema hivi huko unapotaka
kwenda usiende, mpaka nitakapo-ongea na huyo, mwenzangu, kama kweli ana nia
njema na wewe....’akasema
‘Hahaha
mume wangu, naona huo sasa ni wivu, halafu unamuonea wivu rafiki yako kipenzi,
au urafiki wenu umekwisha lini,..mimi hapo mahisi kuna jambo, na mara nyingi
mtenda anaogopa sana kutendewa, nahisi kuna kitu kinaendelea,..sasa ufanyavyo
wewe unahisi hata wewe utafanyiwa....’akasema
‘Una
maana gani kusema hivyo?’ akauliza Inspecta kwa sauti ya hasira.
‘Unaelewa
sana, ...ukikutana na huyo mnayeenda kukutana naye utalijua hili ya kuwa nina
maana gani,...ukumbuke hilo tu, na ujue vyema mara nyingi mtenda akitenda,
huishi kwa mashaka, na kila mara anahisi na yeye anatendewa hivyo hivyo....;akatulia
‘Mke
wangu ina maana huniamini, mimi ninayofanya ni sehemu ya kazi yangu, naweza
kukutana na watu wa aina tofauti, lakini mara zote nachunga mipaka ya ndoa
yangu, hebu niambie ni nani kakutumbukizia hzio fitina...?’ akaulizwa
‘Fitina!,
hakuna cha fitina hapo bali ni ukweli ninaousema, si zaidi....’akasema na
kutulia
‘Mke
wangu, haya yameanza lini , mbona sio mara ya kwanza kuchelewa au kukutana na watu tofauti, na haya yote nayafanya
kutokana na kazi yangu ilivyo, siwezi nikakuambia kila kitu, maana kazi yetu
ina mitihani mingi....’akasema
‘Usitumie
kisingizio cha kazi yako, nyie wanaume mnapenda kujiendekeza, unadai kazi kumbe
una mambo yako, ila nakuambia ukweli ipo siku utaumbuka,....’aasema wa hasira
mkewe, na kabla mumewe hajasema kitu, akasema
‘Kila
laheri, sina zaidi, utanijulisha mkielewana na mwenzako,kuwa niende au
nisiende..kama sitakwenda basi mimi nitakuja huko huko unapokwenda kukutana na
huyo aliyekuita....’akasema na simu ikawa haipo hewani.
‘Kuja...kufanya
nini....?’ akauliza lakini kumbe mkewe hakuwepo kwenye mawasiliano, simu
ilishakatwa na Inspecta akainua kichwa na kuanalia mlangoni, akamuona Inspecta
mwenzake kasimama, kwa msimamo wake ule ule akimuangalia,na tabasamu la dharau
mdomoni ...
WAZO LA LEO: Dharau na kiburi
sio tabia njema, ikitokea wewe unacho, au unaweza, zaidi ya wenzako, basi
mshukuru mola wako, na waone wenzako kwa jicho la huruma, wasaidie kadri ya
uwezo wako, lakini usijenge tabia ya kuwadharau na kuwakebehi wenzako, na hata
kuwaona wao eti ni wazembe, hicho ni kiburi, na kiburi sio uungwa mwema, maana
aliyekupa wewe ndiye aliyewanyima wao, yeye huyo huyo aliyekujalia, ukapata,
ndiye huyo huyo anayeweza kukunyanganya ulicho nacho na kuwapa hao
unaowadharau. Mifano ipo hai chunguza utaona, na mwenye akili ataelewa.
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment