‘Unaona hapa nimetumiwa
huu ujumbe na majaribio ya mtaalamu wako, wanasema wao wameshafanikiwa
kupandikiza vimelea vya ukimwi na magonjwa mbali mbali kwenye mtandao...unaona
huu ujumbe wao....’akasema akisogea pembeni kumpa nafasi Inspecta kusoma,
Inspecta alisoma kidogo, akataka kusogea zaidi lakini jamaa akasema;
‘Mkuu jiandae,
wakishindwa kukushawishi kwa hizo skendo zao, utakuwa majaribio ya hivi virusi,
wameshaviingiza kwenye mtandao, nakuonea huruma mkuu, kama hutafanya watakavyo
watakupandikizia hivi virusi na utakufa kifo ambacho kitaonekana ni kawaida
tu....
‘Usiniulize kwa vipi,
....ninachojua ni kuwa wanakuwekea kama shoti ya umeme, na au kwenye chombo
chochote utakachoshika kwenye maji, kwenye aina yoyote ya kitu kinachoweza
kukusambazia hivyo virusi,..wao wana mbinu za kila namna, ila hii ya mtandao ni
kubwa yake, ....wanakutumia ujumbe, na kwa vile siku hizi tunatumia sana
vidole, ukijaribu kuufungua huo ujumbe inakuja kitu kama shoti ya umeme kwenye
kidole....papu,...vimelea vimeshapenya mwilini.....’
‘Unaona na hapa, vingine
wataviweka kwenye vyakula, kwenye madawa,
na ukumbuke huko kwenye madawa wana watu wao, watakuwa wanadhibiti wao. wenyewe...mmh,
‘Mmmh, unaona na hapa...eeh,
hata haya madawa ya kurutubisha mimea, kuna vitu vyao wameweka ili kuharibu
mfumo wa binadamu,...wanahisi watu weusi wanazaa sana, na watu wa rangi,
unaonaeeh, kama wachina na wahindi, unaonaeeh, ...kwahiyo kwa kupitia hivyo
vimelea wataharibu uzazi, nguza za kiume na kike,....
‘Unaona hapa na pia wamebuni
jinsi gani binadamu mume anaweza kupadilika katika maumbile na hisia zake, mke
awe kama mume na mume awe kama mke kihisia, wanataka kuleta dunia isiyo na
utofauti...hahahaha, wanasema wanataka hizo haki za kila mtu kuwa sawa ziwe za
kiukweli mke asiwe tofauto na mume kimaumbile wawe na maumbile yao tu,
lakini....haya soma mwenyewe hapa...
‘Wanadai wao wanapigania
haki za binadamu vimelea hivi ni silaha yao, wanachotaka wao eti ni kujenga
usawa, dunia hii isiwe na tofauti ya mume au mke...no..no...hapana this now is
too much...’akawa anaendelea kusoma....
Hii ndio dunia inaliyojengwa
na huyu jamaa,...je hayo hayapo au bado... tuendelee na kisa chetu....
************
Inspecta alifika nyumbani kwake muda wa saa
sita na kumkuta mkewe hayupo, akaingia ndani na kupumzika kwenye sofa, mara
simu yake ikaita, alikuwa ni Inpecta mwenzake;
‘Vipi hali yako,...?’ akauliza Inspecta
mwenzake
‘Sijambo, nipo sawa hakuna shaka.....’akasema
‘Nafahamu kuwa kweli hujambo...dawa na tiba
uliyopata ni lazima utapona tu, pumzika tu. je kuna lolote umepata hadi sasa, najaua
kuumwa kwako sio bure kuna jambo ulikuwa unafukuzia..?’ akauliza inspecta
mwenzake
Kauli za mwezake zikawa zinamchnganya, lakini
hakutaka kumuuliza zaidi, hakutaka kuongeza msongo wa mawazo zaidi maana hapo
alipo alikuwa ameshazidiwa, pale alipo alitamani kwenda kuoga na kuondoa uchafu
wote uliopo mwilini na kwenye akili, lakini alijua hata aoge vipi hataweza
kuondoa huo uchafu, hasa ulioganda akilini. Akamjibu Inspecta wake kifupi fupi.
‘So far, hakuna, ..ni yale yale ya mzunguko tu
wa hapa na pale.....’akasema
‘Yah, nilijua tu, ...je kesho utaweza kuja
kazini, maana kuna kikao kwa wakubwa huko, ulisikia eeh?’ akauliza mwenzake
‘Utaniwakilisha tu, siwezi kufika...’akasema
akipiga miayo,na akaangalia saa yake, huku akijiuliza mkewe kaenda wapi,
hakutaka kumpigia simu, akaona asubiri tu.
‘Sawa nimeona Sick sheet yako, ugua pole...’akasema na kukata simu, Inspecta
akashikwa na mshanga maana hakuwahi kupeleke hiyo sick sheet, akakumbuka wakati
aanongea na yule binti alimuelezea kitu kama hicho.
Pale alipokaa alijikuta akimuwaza sana huyo
binti na hata pale alipojaribu kufikiria mambo mengine, alijikuta akitawaliwa
na sura iya huyo binti, akili ikawa hautulii ni huyo binti tu, ilikuwa kama
kapewa kitu kipiya kwenye ubongo ambacho hakikuwepo, uzoefu mpya ambao hajawahi
kuupata, ...akasimama na kukimbilia bafuni, akaoga na kujisikia afadhali kidogo.
Mara mlango ukafunguliwa na mkewe akaingia,
akiwa na mfuko wenye vifaa vya nyumbani, akasalimiana naye, na mkewe akasema;
‘Vipi kulikoni, maana nimesikia unaumwa,
lakini nyumbani huonekani, ulikuwa wapi?’ akaulizwa.
‘Aaah, haya mambo yetu yaache kama yalivyo,
unaweza ukaumwa nab ado ukawa kazini, na kazi zetu zilivyo, unaweza ukajikuta
kwenye matatizo, ukashindwa hata kurudi nyumbani, muhimu nione nipo
salama....’akasema
‘Mimi ndio maana nilishakuambia achana na hizi
kazi, kwanini unang’ang’ania hizi kazi, ona mwenzako sasa ana mipango ya kuacha
kazi, na kaanzisha miradi mingi tu...’akasema.
‘Mwenzangu yupo?’ akauliza.
‘Huyo unayefanya kazi naye, mwenzako mjanja
anauma huku anakupiliza, mkewe anamuendesha puta, lakini kwa manufaa ya
familia, umeshaona miradi yao?’ akaulizwa
‘Miradi gani hiyo?’ akaulizwa
‘Wewe endelea kulala, endelea kujituma tu ni
utaifa wako uone utafikia wapi, ...’akasema
‘Huyo mke wake ulionana naye wapi?’ akauliza
‘Kanipigia simu tukaongea kwa marefu, na mara
mume wake akaja kuniarifu kuwa anaumea, nikamwambia nataka kununu vifaa vya
ndani maana naona kumekauka, hakuna vyukala hakuna chochote akasema
atanipeleka, na ndipo akanipeleka kwenye miradi yao....mmh, wenzako wapo
mbali....’akasema
‘Kwahiyo muda wote ulikuwa na huyo unaiyemuita
mwenzangu?’ akauliza Inspecta kwa sauti ya wivu.
‘Hahaha, ndio waona wivu sio, umesahau kuwa
wewe ulilala nje, na huko nje ulilala na nani, au nyie wanaume ndio wakuona
wivu tu....’akasema
‘Sasa una maana gani kusema hivyo, kuwa kwa
vile nililala nje na wewe unalipiza, au?’ akauliza
‘Mimi sijasema hivyo, na hata siku moja siwezi
kufanya uchafu huo, ..ni wewe umeanza kwa kusema kauli zenye utata wa
wivu....haya niambie hizo picha ulizosema utanitumia zipo wapi?’ akauliza
‘Picha gani?’ akauliza Inspecta kwa mshangao na
mara mkewe akaenda kwenye kabati na kutafuta kitu, ..lakini hakukiona, akauliza
kwa sauti ya ukali
‘Ile karatasi yenye ujumbe wako kuwa haupo na
chini yake kulikuwa na maelezo ukasema kuna picha zako...mbona siioni, na mimi
niliweka hapa, ilikuwa juu juu, na sizani huyu mfanyakazi wa ndani kaingia na
kupekua huku kabatoni, hawezi kufanya hivyo ni wewe meichukua,?’ akauliza
‘Mbona mimi sikuelewi, sijaweka ujumbe wowote
humu ndani na wala sijui chochote kuhusu hizo picha, naona huyo mwenzangu
kakulewesha mpaka unaongea mambo ambao hayapo ...’akasema kama mdhaha,
alishamjulia mkewe akikasirika ujaribu kumtania.
Inspecta kichwani akakumbuka kuwa wakati alipokuwa
anaagana na yule binti , yule binti alimwambia;
‘Mpenzi kwa vile sasa tupo pamoja na umekubali
kuwa sambamba na mimi kila kitu kitakuwa shwari, nitahakikisha kila aina ya
fitina inaondolewa, ili mradi na wewe utimize wajibu,...hakuna kufuatana
fuatana ..achana na mambo ya watu, usichunguze chunguze saaana, huu ni muda
wako wa kujijenga...angalia wenzakoo wanavyoneemeka...’akasema.
‘Sawa akaitikia kwa shingo upande...’akiwa
kama hayupo, alikuwepo kimwili lakini kiroho alikuwa akiwaza mbali, na
kujiuliza je alichofanya ni sahihi, na kama si sahihi angelifanya nini, akawa
anajijutia.....
‘Na ukumbuke mimi ni mpenzi wako, ili mambo
yaende sawa, na hao jamaa waone kuwa upo kweli sambamba na wao, ni lazima niwe
mke wako...unaelewa....’akaambiwa na hapo akashituka na kusema
‘Itakuwaje wewe uwe mke wangu, wakati nina mke
wangu...huko sasa mnakwenda mbali...’akasema na kusimama kuonyesha kuwa anataka
kuondoka.
‘Mmm una mke wako tayari, eeh, naona mke wako
ni kikwazo, au tufanye hivi, wao wamuondoe huyo mke wako kabisa, ndivyo
unavyotaka, au...., ?’ akauliza na Inspecta akamuangalia huyo binti kwa
mshangao
‘Unasema nini?’ akauliza
‘Hebu niambie wewe unataka nini...ungelijua
haya ni kwa faida yako, usingelikataa kabisa muhimu ni kufanya wanavyotaka wao,
toa ushirikiano...unajua nyie watu mnajifanya wachapa kazi, lakini moyoni
mnaumia....’akasema
‘Sisi tunatimiza wajibu wetu kwasababu tuna
kiapo cha uaminifu,pia tunamuogopa mungu, haya yanayoendelea hapa ni
ushetani....’akasema
‘Hahaha eti ni ushetani, mbona ulikuwa
unafurahia, hebu nambie hayo tuliyofanya wanafanya akina nani, wewe si mcha
mungu au sivyo mnavyojiita kinafiki, kuwa nyie ni wacha mungu,...’akasema kwa
dharau
‘Hivi kweli mcha mungu anaweza kutembea na
mwanamke ambaye sio mke wake, hapa tumefanya nini, bado unajiita mcha mungu
hahaha...hahaha, kwahiyo ili kwelu uwepo ucha mungu wako, kuanzia sasa mimi ni
nani kwako..?’ akamuuliza akimkazia macho, na Inspecta akageuka kutaka kuondoka
na yule bint akamsogelea na kumzuia akasimama mbele yake, kwa kujiamini.
‘Kwanini unanifanyia hivyo, hivi kama wewe
ungelikuwa mke wangu akaja mwanamke mwingine akafanya kama unavyonifanyia ungelijisikiaje?’
akauliza
‘Ni mimi nimekufanyia au wewe ndiye
uliyenifanyia, ni nani alitoka nyumbani kwake akamfuata mwenzake,..ushahidi upo
wazi, kila ulipopita umeacha ushahidi, au unataka nikuonyeshe, kila kitu kipo
wazi, huwezi kumdanganya yoyote, ..kwa kauli yako mwenyewe umetamka
unanitaka..nikuonyeshe ushahidi....’akasema akiangalia zile CD mezani...
‘Ok, niambie mnataka nini, au umetumwa kufanya
hivyo kwa madhumuni gani?’ akauliza na yule binti akashika kichwa na kugeuka,
akasema;
‘Sijatumwa, ..ondoa huo usemi, nimekuuliza ni
nani aliyemfuata mwenzake,...kama ningelitumwa ningelikuja kwako,...umekuja
hapa kwa hiari yako mwenyewe kunitaka, kwahiyo hiyo kauli yako sio kweli, na
huenda umebadili mawazo, kinafiki, kwa vile mke wako amekuja..nimekuuliza je
mke wako ni kikwazo, kama ni kikwazo niambie , wenyewe watajua jinsi gani ya
kufanya, ila...usije ukalalamika....’akasema na kugeuka kumuangalia Inspecta
‘Acheni familia yangu, kama mnataka vita na
mimi ingilieni familia yangu, kama mna shida na mimi nifanyeni mtakavyo,
....mke wangu anawahusu nini, kwanini kila mara unamtaja mke wangu....?’
akauliza
‘Hahaha, mke wako, ukumbuke hata mimi ni
mchumba wa mtu, au nilikuwa sijakuambia, lakini wewe ukaanza kunitafuta, au
hujanitafuta...sema mwenyewe , hujanitafuta, ...hapo ulipo mwenyewe akili yote
ipo kwangu, ..umekipata kile ambacho hujawahi kukipata kwa mke-,o ni kweli si
kweli?’ akauliza akimsogelea na kuanza kumshiak shika.
‘Tafadhali narudia tena kama unataka
tuelewane, mke wangu asihusike kwa lolote lile, acheni kumsumbua, vinginevyo,
sitajali cha kashifa au nini, nitachukua hatua mikononi mwangu, nitawatafuta
chini hadi juu, na nawahakikishia nitawapata mmoja mmoja, na mnajua nini
kitakachofuata...’akasema akikunja uso wa hasira hadi yule binti akaogopa,
akarudi nyuma na kusema
‘Usinitishe,..hahaha, tatizo ni kuwa nyie watu
mna hasira, mna miguvu, lakini hamtumii akili, ...sisi tunatumia akili na zana
za kisasa, kwahiyo unajisumbua,....cha muhimu ni mapenzi tu, ...mimi na
wewe,..huku ukiwa mbali na mambo ya watu,ni hilo mpenzi, usijali, ....mimi
nitatimiza wajibu wangu, nitahakikisha mkeo haguswi, ila ......na wewe utimize
wajibu, kila nikikutaka uwepo,....sawa?’ akauliza
‘Huwezi kuniambia hivyo, maana ujue kuwa mke
wangu yupo, na yeye anastahiki haki zake, ...huwezi kuniambia nije kwako kwa
muda utakao, ....hilo ulifahamu....’akasema
‘Nalijua hilo sana, na nitahakikisha nachukua
tahadhari,...kwa vile nakupenda, amini hilo, sijui kwanini nimetokea kukupenda
hivyo, .....i love you...’akasema na kumsogelea kumbusu...Inspecta akajaribu
kumkwepa, lakini akawa keshawahiwa, kilichofuata hapo, kilimfanya aishiwe na
nguvu.
‘Unaona eeh, mkeo anaweza kufanya
hivyo....hahaha hiyo ni salamu tu, na mengine yapo pale kwenye CD, utachukua
nakala yako, utaangalia ukiwa peke yako ....hakikisha ukiwa peke yako, sisi
tutahakikisha hakuna anayeipata hiyo kazi, ni mimi na wewe tu...nimehakikisha
hakuna udurufu, ni live...utaona mwenyewe, ..hahaha ni ya hali juu, nimeipenda
sijawahi ....mmmh, baby, usiondoke....’akasema pale alipoona Inspecta
anaondoka.
‘Nakuapia, ...i will finish this myself, ..mtaona....’akasema
‘Mhh, baby,
ukumbuke mimi ni mpenzi wako, hilo likukakae kichwani vinginevyo.. hiyo CD ikifika
kwa mke, nakuapia, atajiua...si unampenda sana mkeo, sasa chunga hicho kitu
asikione, achilia mbali baba mkwe au kazini kwako...kumejaa raha za dunia humo,
hahaha, mke hawezi, ooh, samahani nafuta usemi, ulishasema tusimuhusishe mkeo,
..’akaweka mkono kuziba mdomo.
Inspecta alijikuta akitetemeka kwa hasira,
akasogea pale kwenye zile CD, akaziweka sakafuni na kuzikanyaga kwa hasira
kuhakikisha zimepasuka vipande vipande....’halafu akageuka kumuangalia yule
binti, akuwa kabadilika sura kwa hasira, na yule binti akatabsamu, kwa dharau
na kuanza kucheka,....
‘Unaona eeh, hivyo ndivyo nataka,yaani
mwanaume akiwa hivyo, nahisi mwili mzima unasisimuka..mmh...mpenzi usijali haya
yote yatakwisha, kuna watu walikuwa hivyo, huwezi amini, sasa wana majumba yao,
miradi yao, wanakuja kunishukuru, wananitaka tena, wengine wapo tayari kuwaacha
wake zao,...lakini nishamaliza kazi nao, ..na sasa nakupenda wewe tu, sitaki
mwingine.....’akasema
‘Narudia tena, haya hayataisha hivi hivi, na
kama mnataka vita visivyo isha, gueni familia yangu, ..mtaona kama mimi ni
nani, msione nipo kimia, msione nafanya hivi kama mjinga, lakini
hamnijui...waambie wenzako hapa wamechozea moto...hili jina sio bure, mtaona...’akasema
akianza kuondoka na yule binti akaanza kucheke kwa dharau akisema...
‘Hahaha, unalo hilo.....hiyo ni onja onja tu,
kazi bado kabisa...nisalimie mke mwenzangu, kwa nia njema, na ni bora ukifika
jaribu kutabasamu maana ulivyobadilika na hizo hasira unatisha, tupo pamoja well
come to our world bby.
WAZO
LEO: Fitina ni mbaya
sana, mfitinishaji anakuwa ni wakala wa shetani, ambaye kazi yake kubwa ni
kufarakanisha kati ya ndugu na ndugu yake mke na mumewe, jamii kwa jamii. Dunia
sasa hivi imegubikwa na fitina, kinachoendelea sasa hivi ni propaganda za kufitinisha
watu, jamii , nchi zifarakane, zipigane, ziuane, kwa manufaa ya matajiri...
Hao ni mawakala wa mashetani wanaofanya kazi
hiyo, hawa ni wachawi wa kisasa, na kazi ya wachawi ndiyo hiyo ya kumuwakilisha
shetani. Jamani tutafakari tuangalie mambo kihekima zaidi, tujaribu kuwa makini
kwa kila tukio linalotokea, kwani hicho kinachoendelea duniani hivi sasa, sivyo kilivyo, bali ni
mipango ya ubeberu na ukoloni mamboleo, mwenye macho aone, mwenye masikio
asikie na mwenye akili atafakari.
1 comment :
Lakini kumbuka pia mengi Mungu huangalia na kulipa haha hapa duniani. Kazi nzuri tupo pamoja.
Post a Comment