Inspecta Moto, akashika kitasa na kutaka kufungua, mara akasikia
kama mtu anakuja kwenye muelekeo wa varanda, akageuka kuangalia, akaona ni
mlinzi alikuwa kwenye mizunguko yake, na yule mlinzi alipomuona akasema;
‘Oh bosi, nilikuwa nafanya doria, mambo yanakwendaje?’ akauliza
‘Hamna shida, ...’akasema Inspecta
‘Samahani nikuuliza, nahisi nimewahi kukuona mahali...’akasema
‘Yawezekana maana dunia siku hzi ni kijiji, unafikiri uliwahi
kuniona wapi?’ akauliza Inspecta
‘Sikumbuki, lakini sura yako sio ngeni kwangu, wewe haupo kweney
safu ya wakubwa wa polisi?’ akauliza
‘Mhh, usijali, ...’akasema Inspecta na kuzungusha kitasa, na
mlango ukafunguka, akamuacha yule mlinzi akibakia kuwaza, hakutaka kumueleza
lolote, na mawazo yake sasa yakawa ni nani hao wanaongea huko ndani.
Kilikuwa chumba kikuwa kama studio ya picha, na komputa na dhana
za kisasa zilionekana mezani, na pembeni kabisa akamuona mtu kakaa, akiwa
kaangalia kwenye runinga iliyokuwa ikionyesha picha ya video, na jamaa huyo
alikuwa katulia kimiya hakugeuka.
Inspecta akatulia akichelea kusema neno maana aliingia kwenye
ofisi ya mtu bila kupiga hodi, akajiuliza arudi, au amuongeleshe huyo mtu, na
akaamua ageuke odnoke zaie lakini kabla hajachukua hatua huyo jamaa akasema;
‘Usipoteze muda, kwani muda ni mali, sogea hapa nikuonyeshe
kitu....’huyo jamaa akasema kwa sauti ya kilevi, na inspecta akajiuliza huyu
mtu anataka kunionyesha nini, na kwanini kalewa mapema hii.
Akasogea hadi pale alipokaa na macho yake yakawa yanaangalia
kwenye runinga, na alichokiona alitamani kuvunja vunja kiyoo kile lakini
akasubiri, na kusema;
‘Hiyo ndio kazi yenu sio, kwani wewe ni nani?’ akauliza akitafuta
njia ya kuona sura ya huyo mtu,
‘Usifikiri mimi napenda kuyafanya haya, na nijuavyo hukutakiwa
kuona, au kuniona, mimi sitakiwi kuonekana na watu wasiostahiki, na sijui
kwanini umeingia hapa, ila nimekuamini... na nahisi unaweza kunisaidia jambo,
je unanikumbuka mimi?’ akauliza na kugeuka, aligeuza kiti ambacho kilikuwa
kinazunguka.
‘Mimi siwezi kuwajua watu kama nyie, manachokfanya kitawatokea
puani...’akasema Inspecta .
‘Nakumbuka kama uliongea na ndugu yangu akakuambia nimepotea
kimaajabu, na y a kuwa wamapeleka taarifa polisi lakini hawajapata msaada
wowote...’akasema
‘Ni nani kakuambia maneno hayo?’ akauliza inspecta kwa mshangao
‘Tatizo lenu ni kuwa hamtaki kujifunza, hii dunia kuna watu
wameiweka mkononi, kila kinachotokea, wanakijua kama kima masilahi
kwao,....hebu angalia angalia hapa, toka umetoka nyumbani kwako hadi umefika
hapa, wenzako wanakuona...’akasema na kumuonyeshea alivyotoka nyumbani hadi
akafika hapo
‘Kwanini mnanifuatilia?’ akauliza
‘Kwasababu wewe ni tishio, wenzako wote wamekwa mkononi, lakini
wewe unajifanya hamnazo, lakini sasa huna ujanja , nakusihi, ni bora ufanye
watakavyo vinginevyo, ...’akatulia na sasa akawa anaonyesha yale yaliyotokea
kati yake na huyo msichana, na inspecta akataka kwenda kuzima ile kopmuta jamaa
akazunguka na kitu kama ngao kikaziba na Inspecta akajikuta akisukumwa na hiyo
ngao hadi akaanguka chini.
‘Usithubutu kufanya hivyo, watakuua hao jamaa,...mimi nakusaidia
kukupa taarifa ili uweze kujipanga, ...haina faida kwangu, ni kwa ajili yako
tu...’akasema
‘Kwani wewe ni nani?’ akauliza Inspecta
‘Kama hujanifahamu haina haja kukuambia, ila nataka usije kusema
uliniona, ni muhimu sana, mimi nakusaidia kukupa taarifa na wewe unisaidie
kunilinda,.....’akasema
‘Kwa vipi, mimi ni kulinde wakati wewe inaonyesha una ulinzi wa
kutosha...’akasema
‘Maana yangu ni hii, kwa hali niliyo nayo sitaki kuonekana na
ndugu zangu, kama unavyoniona madawa yameniharibu nipo kama sipo, na hapa
nikikosa madawa nakuwa kama goigio sijiwezi, hawa watu wameniharibia maisha
yangu,....’akasema
‘Sasa kwanini ukakubali kujiunga na kufanya hayo wanayotaka wao,
huoni umejiingiza wewe mwenyewe, kwanini usitoe taarifa polisi...?’ kaulizwa
‘Swali hilo utakuja kupaat jibu lako pindi...hakuna aliyetaka
kujiunga na hawa jamaa ila wao wakitaka ujiunge na wao utajiunga tu, na mimi
walichofanya ni kunidunga haya madawa,....nikawa kama zezeta, na sasa siwezi
kuishi bila haya madawa...’akasema
‘Ina maana walikulazimisha..?’ akaulizwa
‘Nahisi ndugu yangu aliwahi kukuelezea jinsi ilivyotokea, ...au?’ akauliza na
Inspecta akamuangalia tena kwa makini , akauliza;
‘Ina maana wewe ndiye.....ooh, nimekukumbuka,
nimekumbuka sura yako, kweli alinionyesha picha yako, japokuwa nakuona kama
umebadilika sana....’akasema Inspecta akimuangalia kwa makini.
‘Ndio lengo lao hilo, nibadilike kabisa hata nikitoka hapa, biwe
sio yule waliyekuwa wakimfahamu na hapo wameshaniosha kichwa na kuchukua kila
kilichokuwa kichwani mwangu, wanataka hata ndugu zangu wakiniona wasinitambue,...wanadai
watanisaidia baadaye nirejee kwenye hali yangu maana wana huyo mtaalamu wao,
dakitari bingwa....’akasema
‘Ni nani huyo...?’ akauliza
‘Simjui...’akasema
‘Kwahiyo mimi nitakusaidiaje ...?’ akauliza.
‘Cha kunisaidia kwa hivi sasa hakuna,hakuna...hakuna...hakuna
anayeweza kunisaidia mpaka wenyewe wapende...ninachokuomba kama unajijali,
kubali hayo watakayokuambia...kubali ndugu yangu, yasije kukupata yaliyonipata
mimi,...’akatulia akikunja uso kama akihisi maumivu
‘Hebu nikuulize tangu nipotee kumefanyika, hata ndugu wameshakata
tamaa, huku naumia, sio kwamba nimekaa tu,..unaona hapo, ina maana utatekwa,
utafanya lolote baya, wenzako watajaribu kukutafuta au kukusaidia siku ya kwanza
ya pili ya taatu wanaanza kukusahau....,mimi nilijaribu kuwa mbishi ,
walichonifanyia ndio hivi, najuta kwanini sikukubali nikaenda nao taratibu...
kama una mipango yako ni bora ukaisimamisha kwa muda hadi wakati muafaka, najua
kabisa dhuluma haidumu, ipo siku haki itakuja kuishinda dhuluma...’akatulia
kidogo.
‘Hebu fikiri hawa watu walivyo na mtandao mkubwa, walikuwa
wakikuchunguza nyendo zako kila siku, wanakufuatilia hatua ka hatua, wanakuona,
wanaweka kumbukumbu zako, unaona huo utaalamu, sasa utashindana na watu hawa,
wanaojua hata kile unachokula, ukiingia chooni wanakuona, hebu fikiria
hapo...kuwa makini...’akasema
‘Lakini kwanini tushirikiane , wewe umeliona hili na ni kweli ni
tatizo kubwa, lakini tukisaidiana mimi na wewe,tutawashinda, kwa mfano wewe
hapo unao ushahidi wa kutosha au sio,...hayo mambo unayofanya hapo yote ni
ushahidi wa kuwakamata hao wote wanashiriki kufanya uchafu huu...’akasema
Inspecta.
‘Nakuomba tena sana, na nakutahdharisha, hili jambo kwa hivi sasa
uliache kama lilivyo, hawa watu wamejipanga, kila kona wana watu wao, na watu
walionao sio watu wadogo, ndio wanashikilia maidara yote nyeti, hebu niambie
kwa hali hiyo utaenda wapi,...ok, tusema umeupta huo ushahidi halafu ....’akatulia
kwa makini kama anafikiri jambo
‘Hatua ya kwanza najua utakwenda kwa wakubwa zako, au ...wapi
mahakamani moja kwa moja, huwezi kwenda mahakamani moja kwa moja kuna taratibu
zake, sasa hizo ngazi za kupanda hadi kufikia mahakamani kuna watu wao
katikati, ushahidi unageuzwa, na itakuwa wewe unashitakiwa....hayo ynafanyika
itaalamu kabisa, na propaganda nyingi tu...wangapiw anasota rumande kwasababu
ya propaganda...
‘Sikiliza ndugu yangu, wewe kwa hivi sasa kula bata, kubali, fanya
watakalo, kama utapata mwanya, na uhakika, basi fanya hilo unalokusudia, lakini
natumai siku ukionja asali mwenyewe utachonga mzinga, wangapi
nimewaona..hahaha...mimi nakuambia ukweli ni mzalendo haswa,..lakini mmmh,
nimesalimu amri, japokuwa kiukweli wamefanya jitihada hadi za kunifanya hivi,
...sasa hivi aaah, nimechoka....’akasema na ujumbe ukaingia kwenye mitandao
yake.
‘Jiandae ...mtu wako anakuja....’akasema
‘Angalizo, ni kuwa wenzako walishafikiria kila hatu, kuwa kwa
mfano wamekufanyia hivyo, wana uchafu wako mwingi tu, kwanza ni kukuharibia
jina, hilo linafanyika kitaalmu kwa propaganda ya hali ya juu, pili wanaharibu
ajira yako, tatu wanaharibu afya yako, hapo utafanya nini...na nikuulize unajua
ni nani na yupo kwenye huo mtandao...’akawa kama anauliza huku akifanya vitu
kwenye komputa baada ya kupokea huo ujumbe.
‘Nikuembie ukweli hawa watu ni wajanja sana,...yeye alifanya
uchunguzi wa kina, akagundua kuwa viongozi wengi walijisahau wakawa wanakula
wanastarehe, wanafanya ufisadi...unaona hili, kumbe jamaa anawanakili,
akahifadhi shutuma zao...na pia wengine wameingizwa kimtego tu kama mimi, na
wengine wakategewa skendo...unaona alivyoijenga dunia yake huyu mtu....’akasema
‘Dunia yake..?’ akauliza Inspecta akikumbua kuona hayo maandishi
‘Sikiliza mtu wangu,sitaki kusema mengi kwa sasa, ...naona mtu
wako anakaribia, sio vyema akakukuta humu,....’akasema.
‘Mimi bado nakushauri, hujachelewa, shirikiana na mimi, tulimalize
hili tatizo, ili haki ipatikane, hawa watu waondolewe, sheria ichukue mkondo
wake....’akasema Inspecta
‘Ka hali ilivyo, na ndivyo ilivyo,haki dunia hii sasa haipo, kila
mtu anatafuta kwa juhudi zake, ubinafsi, ....ufisadi..ndio asili ya mwanadamu
au sio ndio maana wewe waitwa jina hili, wewe upo hivi, unaona, hakuna jina
moja kwa wote, hata vidole unavionaje....eeh, sasa kama hakuna haki,ni ubinafsi
kwa kwenda mbele, dhuluma inakuwa ni ujanja, ndio shule...unaonaeeh,..unafikiri
nini kitaendelea
‘Angali hali ilivyo, wengine sasa hivi wananeemeka kwa visingizio
mbali mbali, wengine wanadhulumiwa, mifano ipo hai ndugu yangu, hakuna haki
hapa duniani, hata hao viongozi wa dini, wanatumia dini kujitajirisha
tu,...kama si hivyo, ni kwanini kiongozi wa dini awe na majumba ya kifahari,
magari, wakati waumini wake ni masikini...hebu fungua akili hapo...dunia hii
hakuna haki..kila mtu akipata mwanya na yeye hata bila kupenda atafanya mabaya,
na yanaweza yakawa mabaya zaidi ya hayo ya waliotangulia, nenda ndugu yangu...’akatulia
‘Sasa nitakupataje..?’ akauliza Inspecta, na huyo jamaa akawa
anafanya kitu kwenye mtandao, akasema bila kujali swali la Inspecta
‘Hebu niambie ni nani hataki kuendelea kuwa madarakani, kuingiza
kipato, kuendelea kuneemeka,eeh, wewe si una watoto, je wewe hutaki watoto wako
wasome nje, au kwenye shule nzuri, angalia hao watoto wanaosifika kuwa
wamefaulu, wanatoka wapi,...ni kwenye shule za bei mbaya, sasa ni nani hapendi
watoto wake wasome huko,..kila mtu anapenda au sio, ni kwanini, ni ili baadaye
wawe kama yule au yule waweze kuendeleza mrija wa neema.....hahaha amuka ndugu
yangu
‘Hakuna aliyejipangia kuwa apate zaidi zaidi ya mwingine watu wote
wanayi haki ya kupata asu sio, sasa kwanini wengine wapate haki hiyo kuliko
wengine,...elimu mpo sawa, kazini unafanya zaidi yao, unalima, unafanya
biashara, lakini wengine wanakuwa juu, juu zaidi, ukiangalia kiukweli
hawajapitia njia ya haki,...hao ndio wanaonekana watukufu,...unaona hapo,..
hicho ndicho chanzo cha watu kama hawa kuibuka...’akasema na Inspecta akakunja
uso akiwaza.
‘Makundi mabaya yanatokana na kukithiri kwa dhuluma,haki ikipotea,
ni lazima watu wengine watabuni mbinu, hata zikiwa chafu, lakini na wao wanaona
ndio haki yao...bila hivyo, usemi wa aliyenacho atapata zaidi na atapata zaidi
kutoka wapi, ni kutoka kwenye kile chako kidogo ulicho nacho...unafikiri kwa
nini wanaunadi huo usemi, na je kweli huo usemi ulikuwa na maana hiyo, ...sio
kweli, wanacheza na maandiko na kujenga propaganda wapendavyo wao....natumai
imenielewa, kama hujanielewa, subiri watakufundisha wenyewe....’akasema,
akionyesha wasiwasi, nahisi alishahisi jambo.
‘Unaona hapa, mtaalamu wao ameshafanikiwa kupandikiza vimelea vya
ukimwi na magonjwa mbali mbali kwenye mtandao...wamenitumia niweke tayari kwa
majaribio, sasa sijui wanataka kujaribia kwako.....hahaha..hawa watu balaa....’akawa
kama anasoma jambo kwenye komuta
‘No..no, ...mkuu jiandae, wakishindwa kukushawishi kwa hizo skendo
zao, utakuwa majaribio ya hivi virusi, wameshaviingiza kwenye mtandao, nakuonea
huruma mkuu, kama hutafanya watakavyo watakupandikizia hivi virusi na utakufa
kifo ambacho kitaonekana ni kawaida tu....’akasema
‘Kwa vipi, kwenye mtandao..?’ akauliza Inspecta.
‘Usiniulize kwa vipi, ....ninachojua ni kuwa wanakuwekea kama
shoti ya umeme, na au kwenye chombo chochote utakachoshika kwenye maji, kwenye
aina yoyote ya kitu kinachoweza kukusambazia hivyo virusi,..wao wana mbinu za
kila namna, ila hii ya mtandao ni kubwa yake, ....’akatulia akawa anasoma maelezo.
‘Unaona na hapa, vyakula, madawa, watakuwa wanadhibiti wao....mmh,
unaona na hapa...eeh, hata haya mavukula ya kupandikiza, mime ya kupandikiza,
yanawekwa vitu, vya wenda kuharibu mfumo wa binadamu,...wanahisi watu weusi
wanazaa sana, na watu wa rangi, unaonaeeh, na wamebuni jinsi gani binadamu mume
anaweza kupata vimelea, awe kama mke, wanachotaka wao eti ni kujenga usawa,
dunia hii isiwe na tofauti ya mume au mke...no..no...hapana
this now is too much...’akawa
anaendelea kusoma.
Inspecta akasogelea akitaka kusoma, lakini jamaa akasogeza pembeni
na kusema,;
‘Wao..wenyewe watakuonyesha mfano halisi, mkuu, kubali
tu,...yaishe, hivi wewe kwenu una akili zako utakataa kufanya watakavyo ili
upate sifa tu, shujaa, sijui nani,..huku unakufa taratibu kwa magonjwa
yasiyotibika..unajua naanza kuamini kuwa haya magonjwa mabaya chanzo chake ni
watu kama hawa, nikuambie ukweli, hawa watu ni mashetani...i don’t know wanataka nini katika hii dunia, nahisi wanahitaji
dunia yao....’akasema
‘Hebu nikuulize hao watu ni akina nani...?’ akauliza Inspecta sasa
akianza kuhisi hatari inayomkabili.
‘Kwa hivi sasa mimi sijui, nimeshikwa, nimefungwa na nipo hivi
kama nilivyo, kazi yangu ni kuambiwa fanya hiki, fanya hiki,nikikataa napata
adhabu isiyovumilika....siwezi kuilezea, lakini wanajua kuumiza, sasa mimi nimeamua
kufanya watakavyo, kwanza nitakosa nini, kama wanaostahiki kunisaidia
wameshindwa, mimi nifanye nini, nifa wanililie, kama shujaa, hahaha, eti
alikuwa mtu mzuri, shujaa, hakuna kitu hapo wewe umeshakuwa mzoga, huna maana
tena....’akasema
Inspecta akawa hajakata tamaa akasema;
‘Lakini kwa vile wewe upo kwenye huo mtandao inamaana utakuwa
unawafahamu wote au sio, na yote wanayofanya unayo kwenye kumbukumbu zako,
huoni ndio wakati muafaka wa kujitoa , mimi nitakusaidia, tulimalize hili
tatizo,...ukumbuke familia yako wanakutafuta...nilitaka kujua kuhusu familia
yako ....’akasema Inspecta na kabla hajamaliza huyo jamaa akageuka na
kumuangalia akasema
‘Jamaa wajanja kweli, mimi ni mtaalamu wa mitandao, naweza kubuni
namba yako ya siri kwa ujanja ujanja, lakini hawa watu ni zaidi,....nashindwa
kujua ni nani anawasaidia,..wameniwekea mipaka ambayo siwezi kuona zaidi...wamenificha
mambo yao mengi, lakini nitawashika,....hilo naahidi, ila sijui lini na kwa
vipi....unajua, nimejaribu kwa uwezo wangu lakini sijaweza kuwafahamu ni nani
wahusika wote...’akasema
‘Ama kuhusu familia yangu, tafadhali sana, usije kunitaja kuwa
umeniona, mimi nimeshakufa, sitaki kabisa familia yangu waje kuniona katika hii
hali, ...’akasema na kushika kichwa kama anawaza jambo, halafu akasema;
‘Wakati mwingine akili ikinijia naumia sana nikijiona hivi
nilivyo, nilikuwa mtu wa maana nina kazi yangu, lakini utaalamu wangu , kipaji
changu ndio kimenipoza, sijui kama nitaweza kurudi hivyo, ,....unaona
walichonifanya madawa yakiisha mwilinini nahisi vibaya, ....unaona oooh,
imeanza taabu, ooh, balaa, dawa yangu ipo wapi....’akaanza kama kujikuna, na
hapo hapo akachukua kitu kama kiko na kuvuta puani, akatulia kimiya kama kalala
Inspecta alipoona hivyo, akataka kusogea pale kwenye hivyo vifaa
vilivyopo mbele yake, ili ajaribu kuona kama anaweza kupata chochote, lakini
mara akasikia sauti nje ya gari lipikipiga honi, akajua hao jamaa wameshaingia, na sasa anatakiwa kujiandaa kupambana nao, akatoka nje ya kile chumba kwa haraka.
WAZO LA LEO : Kila siku maisha
yanazidi kuwa magumu, na jinsi hali inavyozidi kuwa mbaya ndivyo watu
wanavyozidi kubuni njia mbali mbali za kupata kipato, na mara nyingi kipato
kikubwa hupatikana kwenye njia mbaya. Tusipoangalia yale yaliyosemwa kwenye
vitabu vitakatifu sisi tutafanya mara dufu yake, sisi tunafanya mabaya zaidi
yao, na yote haya ni sababu ya kutojali haki za watu, dhuluma imekuwa ndio
rasimali. Tujirudi, tuangalia haki inatendeka, tuache dhuluma...
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment