Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Wednesday, August 6, 2014

DUNIA YANGU-12



‘Nawataka wataalamu wa kila fani, wa mashine hadi wa siasa ...Niwe na nguvu, niogopewe.....’ 

‘Hahaha hao wataalam wa kila aina ya fani,  ndio wataniwezesha, nifanye kile nilichokitaka. Nahitaji mikono mingi ya wataalamu...yah, hili ndio wazo langu...’


`Nikifanikiwa hilo, basi nitakuwa na dunia ninayoitaka mimi, dunia ambayo naimiliki mimi kina mna yangu,...hahaha...'

'Ukiwa na akili na pesa, bhwana, dunia unaweza kuiweka mikononi mwako,...lakini kwanza ni lazima nipate mikono ya wataalamu mbali mbali, ambao watakuwa wakifuata amri yangu, hawa watasaidia kuijenga dunia niitakayo mimi...’

`Dunia yangu...'


Tuendelee na kisa chetu
  
                          ***********

 Simu iliendelea kulia na kushiria kuwa mupigaji ana jambo muhimu sana, Inspekta Moto akiwa bado usingizini, aliinua mkono hadi alipoiweka simu yake ya mkononi, na wakati anataka kuishika ikawa imeshakatwa.

Akashukuru na kulivuta shuka vizuri, baada ya kuangalia saa ukutani na kumuonyesha kuwa bado ni bado ni alfajiri, na alikuwa na saa nzima la kulala kabla hajaamuka kuanza shughuli zake za siku hiyo, lakini kabla hajatuliza kichwa simu sasa ya mezani ikaanza kuita, na mlio wa simu ya mezani ni mkubwa kiasi kwamba hata iweje utaamuka tu kuipokea.

‘Hivi hawa watu hawataki na mimi leo nipumzike kidogo, huyu ni nani asubuhi ya leo na leo ni siku ya mapumziko...’akawa analalamika

Akasimama kwa uvuvi akiomba na hiyo simu ikatike, lakini haikuonyesha dalili, kwani ilikatika na kuanza tena kulia, akawa sasa ameshafika kwenye meza ndogo haikuwa mbali na kitandani, akasogea karibu yake akizidi kupoteza muda ili simu hiyo ikatike, lakini haikuwa hivyo, akaishika na kuiinua akaweka sikioni, na akilini alishahisi kuna jambo, mara nyingi simu za namna hii huwa zina jambo zito. Akaiweka sikioni na kusikiliza , na mpigaji akawa kama anahema kabla hajasema neno

Inspecta alisubiri mpigaji aanza kujitambulisha, lakini alipoona yupo kimiya akasema yeye;

‘Inspecta Moto,oooh, hapa nikusaidie nini’ Alipiga miayo miwili mfululizo, na wa pili ulikatishwa na sauti ya Inspekta mwenzake.

‘Mimi ni Inspekta Majuto anaongea, nipo Maeneo ya Mbezi Beach, nyumbani kwa Muheshimiwa Shingo, kama unakumbuka vyema muheshimiwa huyo pia ndiye mmiliki wa makampuni ya `Private Telecommunication’. Kwa uhakika sasa hivi ni marehemu, ingawaje madakitari hawajafika na kupima, na kutoa taarifa yao…’

‘Ok, kwahiyo unahisi ni.....’kama hajamaliza, akasikia kama mlio wa kuguna kutoka huko kwa mwenzake, lakini ulikuwa sio sauti ya mpigaji wa simu, na kukawa kimiya, na Inspecta ,Moto akasema;

‘ Ok basi nakuja sasa hivi, endelea kuchukua taarifa muhimu..’ Inspekta Moto alikata simu na kukimbilia bafuni, akiwa anaoga kichwani alikuwa na mawazo mengi kumuhusu huyo marehemu, kwani jana tu walitoka kuongea naye, na walikuwa na miadi ya kukutana leo, na alikumbuka marehemu alisema kuna jambo nzito ambalo alihitaji msaada na alisema maneno `ushauri wa kiusalama’.

Na Inspecta akamuuliza

‘Una mashaka gani muheshimiwa?’ alikumbuka kumuuliza hivyo

‘Ni maswala nyeti kidogo nahitajia tuongee faragha mimi na wewe tu, kwenye simu haitapendeza...’akasema huyo muheshimiwa, na sauti yake kwenye simu haikuonyesha wasiwasi, aliongea kwa kujiamini tu, kwahiyo hata Inspecta alijua ni mambo ya kawaida tu, ila alipomuuliza swali jingine;

‘Kwahiyo tukutane wapi?’ akamuuliza, na muheshimiwa hakujibu moja kwa moja kwanza alitulia kwa muda kidogo kama anawaza jambo, na baadaye akasema

‘Nitakuambia nikiwa tayari, maana yote ni tahadhari, ...nitakupigia au kukupa ujumbe, kama hatutakutana hapa na pale, lakini sitaki tuongee juu kwa juu ...’akasema na kukata simu.

Kauli hii ya mwisho ilamfanya Inspecta kuwazia jambo, kuwa huenda muheshimiwa huyu ana tatizo, lakini hata hivyo hakuweza kumuuliza zaidi kwani simu ilishakatika, akaacha kama yalivyo, akijua wakikutana wataongea kwa mapana, na mara nyingi wanakutana, ila hawajawahi kuongea maswala mazito ya kutia wasiwasi.

Baadaye usiku akapokea ujumbe kutoka kwa muheshimiwa huyo kuwa wakutane nyumbani kwake, huko Mbezi alipo na makazi yake mapya. Inspecta alishawahi kufika nyumbani kwake kabla, ni makazi mapya, maeneo ya Mbezi,  kwahiyo anapafahamu vyema. Yeye na muheshimiwa huyu wanafahamiana sana, na mara kwa mara wanakutana. Makazi ya muheshimiwa huyu mwanzoni yalikuwa Msasani.

Inspecta japokuwa alikuwa na kazi nyingine siku hiyo, lakini alilichukulia swala la muheshimiwa huyo kwa uzito mkubwa, kwahiyo kwenye ratiba zake za siku aliweka miadi hiyo, sasa leo anasikia ameshafariki, je kuna mahusiano na kukutana kwake na hicho kifo au imetokea tu kwa bahati mbaya...

Akawa anajiuliza huku akiingia kwenye gari kuelekea huko nyumbani kwa marehemu. Na kwa vile siku hiyo ni siku ya mapumziko, na kwa vile ni asubuhi, wananchi wengi bado wapo majumbani, na hakuna magari mengi barabarani, kwa hiyo Inspekta Moto aliendesha gari lake kwa kasi kidogo akielekea eneo la tukio .

Njiani alijaribu kumuwaza muheshimiwa huyu ambaye pamoja na kujiunga na mambo ya siasa, lakini alikuwa ana vitega uchumi vyake vingi, vikiwemo makapuni ya mawasiliano na baadhi ya viwanda. Alikuwa mtu anayependa sana kusaidia wanyonge na mara nyingi utasikia amejitolea kiasi kadha, au kujenga mahospitali na mambo mengine.

Katika ulingo wa siasa anajulikana kama mtu mwenye msimamo akiamua kitu huwa hatetereki. Na kuingia kwenye ulingo wa siasa kulitokana na wananchi wenyewe kumtaka awe mmoja wa wabunge wao kwa jinsi moyo alivyokuwa na upendo wa watu na kusaidia watu kwa hali na mali, kwa hali hiyo matajiri wenzake walikuwa hampendi, ndivyo dunia ilivyo, watu wanaopenda jamii, kusaidia watu kwa moyo wa upendo, anakuwa hapendwi na wale wasio na tabia hiyo

‘ Je kifo chake ni katika ulingo wa kisiasa au biashara au ni kifo cha kawaida tu..’akawa anendelea kujiuliza, na alipoona anawaza jambo ambalo hana uhakika nalo sana, akasema;

‘ Well, Nitajulia hukohuko......’akasema kwa sauti na kufungulia redio ya kwenye gari kusikia kama kuna tangazo lolote kuhusiana na kifo chake, lakini kwa ajabu kabisa hakusikia lolote, hata kwenye vyombo vyake vya habari, hawakusema kitu

‘Kwanini mbona ...labda kifo chake hakijajulikana...’akasema

‘Lakini kwanini wamuue mtu kama huyu, mtu ambaye hana kinyongo na watu,..na watu wazuri kama hawa ni wachache sana, wengi na utajiri wao hawapendi kabisa kusaidia watu, mungu amulaze mahali pema peponi’...akasema wakati anaingia maeneo ya makazi ya muheshimiwa huyo.

Alifika eneo la makazi ya Mheshimiwa huyu, eneo lake ni kubwa na ukiingia kwenye geti utakutana na walinzi wa Group Four, na hapo utakaguliwa gari lako , na kuna mwendo kutoka hapo getini hadi nyumba ya familia ilipo, napo kuna geti dogo, kwahiyo kwa maana ya ulizi jamaa huyu alijitahidi na huenda ni kwasababu ya shughuli zake ndio maana alijihami hivyo.

Alipofika kwenye nyumba ya familia aliwakuta askari wakifanya kazi yao ya usalama kuhakikisha kuwa hakuna kitu kinachoharibika, na kuhakikisha kuwa ushahidi wote upo, na wakati huo huo madakitari wa uchunguzi wakawa nao wanaingia. Lakini hawakuanza kazi yao mara moja, hadi Inspekta kwanza aone tukio lilivyo.

Inspecta alipoingia akakagua kwa haraka haraka kwa macho kwa kuangalia eneo zima la chumba, kilikuwa ni chumba kidogo cha maongezi, na kwa pembeni yake walikuwepo wanafamilia wakilia, na Inspecta Majuto alikuwa akiteta na mmjoa wa wanafamilia, Inspecta mwenzake alikuwa bado akiwahoji baadhi ya wanafamili, lakini alipomuona mwenzake akasimama kuwahoji wanafamilia na kumsogelea mwenzake, akasema;

‘Karibu Inspekta Moto, twende huko ulipo mwili wa marehemu, na hakuna mtu ambaye amegusa kitu tangu nifike…ni makitaba yake’ Aliongea na inspecta Moto, akawatupia macho ya haraka wanafamilia, na baadaye kamfuata Inspecta mwenzake, kwenye chumba kinachoitwa makitaba, ni chumba ambacho ni kikubwa na kina kila kitu kama ofisi.

Wakaingia kwenye hicho chumba kinachoitwa makitaba, na hali ya hewa ya hapo ndani ya chumba ilikuwa ni ya ubaridi sana, inaonekana kipozea hali ya hewa kilikuwa kinafanya kazi toka muda mrefu. Na inspecta alikagua kwa haraharaka kwa macho na hali aliyoiona haikuonyesha uvamizi, mapigano , kulikuwa kuna ushwari, kwani kila kitu kilionekana kipo katika mahala pake, kwani sio mara ya kwanza kwa inspecta huyu kufika kwenye hiyo maktaba.

Aliangalia pembeni kwenye makabati makubwa, yaliyojaa vitabu, na makabrasha mbali mbali, kuonyesha kuwa mtu huyu alikuwa msomi, na kila kitu kilipangwa vyema kabisa, na picha za viongozi wa siasa zilikuwepo pia ukutani, kuashiria kuwa huyo jamaa pia ni mkereketwa wa siasa ya nchi yake.

Akatupa macho kwenye meza iliyopo karibu na dirisha, ni meza ya kiofisi, na juu yake kuna simu ya mezani ya kisasa, kuna kitabu kilichofungulia nusu kuashiria kuwa kilikuwa kinasomwa, kulikuwa na mafaili mawili yapo mezani, na maandishi makubwa yalionekana, `AJENDA ZA VIKAO...’ kulikuwa na makabrasha mengine, kuashiria kuwa huyo mtu alikuwa anafanya kazi fulani, pia kulikuwa na komputa ndogo `laptop’ ,iliyokuwa imefunguliwa

Akazidi kusogeza macho yake na sasa akafikia kwenye kiti, aina ya sofa, hapo kulionekana mtu kakaa , mkao usio wa kawaida, mdomo umefungua nusu, kuashiria kuwa huyo mtu ama amelala, au ndio hivyo tena, mmh, kwa dalili ile, iliashiria kabisa hakuna uhai, alikuwa huyo marehemu.

Akamkagua kwa macho kwa haraka haraka, na kwa mtizamo wa kawaida, inaonyesha marehemu hakufa kifo cha kuhangaika, maana alikuwa katulia kwenye kiti, na kichwa tu ndio kilionekana kuwa upande.

Inspecta akausogelea ule mwili, na kwasababu alishaambiwa, alijua sasa anakabiliana na maiti, alikuwa ameshavaa kinga za mikononi, lakini bado alijaribu kuwa makini asiguze kitu, akaangalia mandhari ya pale alipokaa huyo marehemu.

Marehemu, mkono wake mmoja ulikuwa karibu kabisa na simu ya mkononi, simu hiyo ilikuwa mezani ikiguswa kidogo na vidole, ilionyesha kuwa marehemu alikutwa na umauti, wakati akiongea na simu, au akitaka kuongea na simu. Na inspecta alipohakikisha kuwa kaona kila kitu muhimu, na kwa vile hakutaka kugusa kitu kabla taratibu nyingine hazijafanyika akasema;

‘Mumeshachukua picha na kila kitu humu ndani...?’ akauliza na kabla haajjibiwa, akasema
‘Kama bado picha zichukuliwe, na docta aingie .....’akasema na mwenzake akatoka kuwaita wapiga picha na wataalamu wa alama za vidole, wafanye kazi yao.

Na wakati mwenzake anatoka, Inspecta akamsogelea marehemu na kwa haraka akipitisha mkono kwenye mifuko ya koti la marehemu na akatoa karatasi na nyaraka mbali mbali zilizokuwa kwenye mifuko, akaziweka hizo nyaraka kwenye mfuko wake na nailoni, alihakikisha hakuna kitu kimbebakia kwenye mifuko hiyo ya marehemu, na mara watu wakaingia kufanya zoezi lililohitajika na kwa utaratibu unaotakiwa.

Walipomaliza kazi yao Inspecta akasogea pale mezani na kuchukua simu ya mkononi,  na kuikagua vyema, ilionyesha imezimika, sijui kwa kuisha chaji, au ilijizima yenyewe. Akaandia kwanza kwenye kijitabu chake, na kuchukua picha ya video, akaiwasha...wakati inawaka akawa anaendelea kukagua pale mezani huku simu yake ikichukua kila tendo analolifanya.

Simu ikawa imeshawaka, na ilionyesha kujaa chaji, sasa kwanini ilizimwa, ni kitu kingine kilimtia mashaka huyu Inspecta, akaanza kukagua miito ya karibuni,  cha ajabu kulikuwa hakuna kumbukumbu ya miito ya karibuni, hii ilimpa wasiwasi sana Inspekta, kwasababu kwa taaswira ilionyesha alikuwa akiongea na simu, je iweje kumbukumbu zifutwe, alizifuta mwenyewe au kuna mtu alifika hapo baada ya tukio, au ndio alikuwa akitaka kuongea na mtu...haiwezekani awe alifuta kumbukumbu kabla....

Alimkagua marehemu, na hakuonyesha dalili zozote za majeraha, kama alivyosema dakitari,na hii ilionyesha kifo chake kinaweza kuwa na matatizo ya ndani ya mwili na huenda ikawa shinikizo la damu. Lakini hayo yatasubiri maelezo ya dakitari wake, ambaye alishamaliza kuchukua kumbukumbu za haraka, na alihitajia marehemu kufikishwa hospitalini kwa uchungiz zaidi.

‘Hajaumia, au kuumizwa mahali popote, na kwa hali hii siwezi kujua tatizo ni nini mpaka tumfikishe hospitalini kwa uchunguzi zaidi...’akasema huyo docta

Inspecta alipohakikisha kuwa amekagua mambo yote muhimu aliwaomba wataalamu wa uchunguzi na dakitari wamalizie kazi zao zilizobaki na mwili wa marehemu ufikishwe hospitalini kwa uchunguzi zaidi.

Wakati Inspecta anatoka akaona kitu kama kijijarida, au kadi, ambacho ilikuwa imedondokea pembeni mwa meza ya kiyoo, kilikuwa kimejificha sana, na aliichukua muda kukitoa sehemu hiyo.

‘Kuna nini Inspecta...?’ akauliza mwenzake

‘Kuna kitu kama kijarida, au kadi, mmmh, ok..inaonyesha ni kadi ya mualiko....’akasema

‘Kadi ya mualiko, oh, ngoja nikusaidie kukitoa?’ akasema mwenzake na kusogea ili kutoa msaada, lakini Inspecta alishaitoa hiyo kadi, na kuipitisha jicho la haraka, halafu akaitumbukiza kwenye mfuko wa plastiki aliokuwa nao mkononi.
‘Kadi ya mualiko,wa harusi au kikazi?’ akauliza mwenzake

‘Hapana haionyeshi hivyo, naona alialikwa kwenda kwenye kikao maalumu, mmmh,inaonyesha alialikwa kwenda hoteli ya Paradise....’akasema Inspecta Moto

‘Mhh, Paradise,........’akasema mwenzake akionyesha mshangao kidogo

‘Hivi umafahamu mumiliki wa hiyo hoteli?’ akauliza huyu Inspecta Moto

‘Mhh, hapana namsikia tu, na kwa hadhi ya muheshimiwa, kualikuwa huko sio jambo la ajabu, au sio?’ akasema Inspecta mwenzake akionyesha kutafakari jambo.

‘Yah...ni kweli, lakini kila kitu kinaweza kuwa sababu...ni muhimu kujua ikiwezekana kila kitu, je kwanini alialikwa, kuna nini huko, na kwanini na kwanini itatupa jibu, nahisi hiki sio kifo cha kawaida....’akasema Insepecta

‘Nitaifanya hiyo kazi, usijali....’akasema inspecta mwenzake na kwa haraka akatoka kwenye kile chumba na kumuacha Inspecta akiendelea kukagua mle ndani na safari hii kwa makini zaidi, na moyoni akahisi kuna jambo kubwa kuhusiana na hicho kifo, hasa akikumbuka mawasiliano yake na marahemu, ....

NB: Sehemu hizi ni nyeti kidogo, kwahiyo inabidi niwe makini kuziandika, lakini natumai tupo pamoja

WAZO LA LEO: Halahala na jirani, jirani ni mtu muhimu sana kwako. Jirani, anaweza akawa jirani wa sehemu yoyote unapoishi, iwe kazini, majumbani au  kinamna yoyote ile, ambayo inakufanya wewe na yeye muwe majirani, kuna ujirani hata wa kiimani , kikabila nk. Jirani ana haki zake muhimu, na usipokuwa makini na jirani yako, inaweza ikawa sababu ya fitina, uadui na uvunjifu wa amani.

 Cha muhimu ni kuwa makini sana kwa kila tunachokifanya, tuangalie kisimkwaze jirani yako, tukumbuke kuwa kosa dogo tu linaweza kuzua uhasama, chuki, na uvunjifu wa amani, ndio maana tunaambiwa mpende jirani kama unavyojipenda wewe mwenyewe, hata ikibidi zaidi ya hapo.


 Ili kulifanikisha hili, kama una uwezo, toa msaada wa hali na mali,kam ni bosi toa haki stahili, hakikisha unashirikiana na jirani yako kwa shida na raha, kwa kufanya hivyo, unajenga udugu, unajenga mahusiano mema, na jirani na jirani kunazaliwa mtaa, au kijiji,au ofisi, kampuni nk, kama wote mtafanya hivyo nina imani, amani na upendo vitakuwepo daima. 

Ni mimi: emu-three

No comments :