Inspekta Moto, aligeuka kumwangalia mwenzake inspekta Majuto, hali
aliyomuona nayo, ilimpamashaka, mwenzake alionekana mwingi wa mawazo, na mara
nyingi alikuwa akisimama kama ana wasiwasi na jambo,halafu hurudi kukaa tena, na
kabla hajamuuliza kitu, mara simu yake ya mkononi ikiita, akaangalia mpigaji,
na kwa haraka anachepuka nje , na haikupita muda akarudi, na safari hii
alionekana kabisa kuchukia, hakuwa na raha usoni.
Inspecta Moto, akashindwa kuvumilia, ikabidi amuulize mwenzake
kulikoni,kwani ni karibu siku ya tatu mwenzake huyo haonekani kutulia na huenda
kuna jambo ambalo wangeliweza kusaidiana,likaisha;.
‘Haya ni maswala yangu binafsi, usijali, nitayatatua pindi….kuna
mambo hayajakaa sawa…’ hili lilikuwa jibu lake na alipenda kulirudia kila
akiulizwa swali linalofanana na hilo.
Inspekta moto alihisi kuna tatizo zaidi ya mwenzake anavyoelezea,
lakini aliona si vyema kuingilia maswala ambayo huenda yataleta kutokuelewana
ndani ya kazi, kwahiyo alijifanya hafuatilii tena maswala ya mwenzake. Mara
simu ya mezani ikaita, na aliyehitajiwa kwenye simu ni Inspekta Majuto, ya
kwamba kuna mgeni wake nje anamuhitaji..
‘Huyo mgeni yukoje?’ aliuliza Inspecta Majuto.
‘Ni binti, ambaye anasema anamiliki kampuni ya warembo , anasema
unamiadi na yeye…’ sauti ilisema
‘Miadi na mimi, ngoja nakuja mwambie anisubiri chumba cha wageni’
alisema inspekta huku akionyesha kuchanganyikiwa zaidi. Mawazo ya wiki nzima
yalizidi kumchanganya kichwa. Alihisi huyu binti atakuwa amekuja na tatizo jingine
kubwa, na hakutaka matatizo mengine kichwani mwake.
Inspecta Moto akawa anafuatilia yale mazungumzo na mwishowe
akilini mwake akavutika amuone huyo binti ni nani, akajifanya anafuatilia
mafaili yaliyopo ndani ya chumba cha wageni, naamu, huyo binti alikuwa binti
kweli, na amjuavyo Insekta Majuto sio mtu wa mabinti, yeye ni mpenzi wa pombe,
na sigara., lakini tabia ya mabinti hakuwa nayo! Je huyo binti kaja na
maswalagani.
Na kipindi anaingia chumba cha wageni, aliona yule binti
akimkabidhi Inspecta kadi, ilikuwa kadi iliyonakishiwa vyema, na yule binti
alionekana kumwangalia inspecta yule kwa macho ya udadisi zaidi, sio ya mahaba,
kuashiria kuwa swala hilo halihusiani kabisa na mapenzi.
Inspecta alisita kuipokea pale alipoona mwenzake akiingia,akajibaragua,
na yule binti akatabsamu, na kumshikisha yule askari ile kadi, na hapo hapo
akasimama kuondoka,na inspecta yule akaichukua ile kadi na kwa haraka akaificha
kwenye mafaili yaliyokuwepo pale mezani,na kitendo kile kilimfanya yule binti
kutabasamu.
Na yule binti akiwa alisimama kwa madaha na kuelekea mlangoni.
Aligeuza shingo kimadaha na kusema;
‘Usikose, ukikosa utamkosea bosi wako, na unajua nini matokeo
yake..’ alisema kwa kujiamini.
‘Bosi wake?, ni nani huyo bosi wake,…?’ Inspecta Moto alijiuiliza
bila kupata majibu, ina maana mwenzetu ana mabosi wengine ambao hawajulikani.
Alijifanya kuchukua mafaili na kujifanya faili analotafuta halionekani.
‘Inspecta Majuto faili maalumu la wale watuhumiwa namba moja la
ile kesi ya mauaji,umeliona wapi?’ Aliuliza akiwa na uhakika kuwa ndio lile
lililokuwepo pale mezani. Inspecta majuto akajibaragua na kuliinua lile faili
na wakati huohuo ile kadi iliyopo kwenye bahasha ikadondoka chini. Na yeye
akajifanya kama haioni
‘Naona kama kuna kitu kimedondoka,…..’akasema inspecta akitaka
kuinama kukiokota lakini inspecta akawahi kuinama na kuichukua ile kadi, lakini
inspecta moto alishaona kile alichotaka kukiona.
Kwa jicho la haraka, inspecta akaona nembo na jina kubwa
likionyesha mualiko kwenye hoteli moja kubwa sana, `Paradise…’.
‘Oh, kumbe….’akasema kimoyo moyo, akikumbuka hiyo hoteli,
inayomilikiwa na tajiro mmoja ambaye hajulikani anaishi wapi.
Hakutaka kupoteza muda akalichukua lile file kutoka kwa mwenzake
na kugeuka kuondoka, alitaka amuwahi huyo binti hapo nje, lakini alipotoka
hakumuona tena, na akaona haina haja alichotaka kukijua kwa sasa kimetosha.
‘Ni lazima nifuatilie huko kuna nini , na kwanini mwenzangu
anaonekana kutokuwa na amani ….’akasema kimoyo moyo
**********
Wakati haya yakiendelea kichwani mwa Inspecta majuto kulikuwa na
mambo mengi na kila hatua alijiona akiiingia kwenye mitihani mikubwa, na
kutokana na misongo ya mawazo isyokwisha, akahisi maumivu makali upande wa
mkono wa kushoto,maumivu hayo hayakuwepo kabla.
Kichwani alihisi kuna tatizo, mwanzoni alijua labda ni zile pombe
alizokunywa jana, lakini alihisi zaidi ni mawazo ya kazi ambayo alielekezwa
kuifanya na jamaa wamuitaye bosi. Huyu
bosi ni nani…akawa anajiuliza
Hakupenda hii hali ya
kuwa na mabosi wa uraiani yeye ana mabosi wake wa kazini, lakini kuwa na mabosi
wa uraiani,hakutegemea, na hakupenda iwe hivyo, hata hivyo kwa jinsi ilivyo
ilimlazimu kufanya hivyo ili kufanikisha maisha yake na mkewe, ili kuficha aibu
kubwa ambayo haijawahi kutokea katika maisha yake.
Alipokumbuka kuhusu mkewe, kwa haraka akajizoa zoa, akikumbuka
ahadi aliyompa mkewe kuwa leo hatachelewa, wanatakiwa kwenda kutafuta nguo
mpya, toleo jipya….
‘Huyu mwanamke atanitoa nyongo….’akasema
Mke wake ni mpenda anasa, na kama akihitaji kitu ni lazima akipate,
asipokipata ndani hakukaliki. Hali hii ilimfanya Inspecta kubuni ajira za
pembeni, na aliyemsaidia kufanikiwa hili ni tajiri mmoja mwenye makampuni mengi
ambaye hajawahi kumuona kwa sura na mara moja aliyoonana naye alikuwa kavaa
mawani meusi, na ilionekana hakutaka kabisa kuonekana sura yake.
Na walipoonana naye akamuahidi kazi maalumu, iliyokuja baada ya
yeye kupitia mafunzo maalumu, mafunzo yaliyokuja kumbadili, hata hivyo akilini,
na kazi yake alijiona anafanya makosa, hakuwa na raha, hata hivyo, hakuwa na la
kufanya.
Alikumbuka jinsi alivyokutana na huyo aitwaye bosi...
*******
ilikuwa ni kwenye sherehe ya wakubwa, matajiri wa nchi hii, na
mualiko ulikuja kupitia kwa mkewe. Na hiyo kadi ya mualiko haikuja kwake moja
kwa moja, hiyo kadi ya mualiko alipewa mkewe, hata alipoambiwa na mkewe kuhusu
huo mualiko, hakupendezewa, kwani licha ya kazi aliyokuwa nayo mbele yake, hata
yeye mwenyewe hakupenda kujumuika kwenye hizo sherehe kutokana na kazi yake
ilivyo, lakini mkewe akalazimisha kuwa wamealikwa mke na mume,na yeye kaalikwa
ni lazima aende na mume wake.
‘Kama hutaki kwenda huko kwenye huu mualiko, ambao ni muhimu
kwangu, kwa biashara zangu, basi nitafutie mume wa kwenda naye, nataka umtafute
mwenyewe ili usije kusema nimevuka mipaka ya ndoa…’akasema
‘Mke wangu unafahamu fika kuhusu kazi yangu…sehemu kama hizo mimi
sitakiwi kufika, labda iwe ni shughuli ya kikazi…isitoshe nina kazi za watu
zipo mbele yangu...’akasema
‘Ifanye hiyo ni shughuli ya kikazi…..tafadhali mume wangu ,
tafadhali usiniharibie siku….’akasema
‘Unaweza kwenda peke yako mke wangu nimekuruhusu kwa leo...,sio
lazima uongazane na mwanaume, mimi nina kazi muhimu ya kazini, nahitajika kesho
kuonana na mkuu, kutoa taarifa ya kesi niliyokuwa naichunguza…’akasema
‘Unasema nini, hebu angalia hiyo kadi imeandikwa nini, MR, and MRS,sasa nitafutie huyo MR,
nakuambia ukweli, usipotaka kuondoka na mimi huyo Mr, atatafutwa, ..usije kunilaumu, unakumbuka baba yangu
alivyokuambia, mtoto wangu hana matatizo, matatizo labda uanzishe wewe, na haya
unayotaka niyaanzishe ni wewe..’akasema
Inspekta akakumbuka kuhusu baba mkwe wake huyo, akakumbuka jinsi
alivyomuoa huyo mwanamke kwenye ushindani mkubwa, na yeye alishinda kwa
kutetewa na baba mkwe wake huyo, na siku alipofungishwa ndoa, aliambiwa;
‘Umempata binti yangu, binti yangu alikuwa na nafasi ya kuolewa na
matajiri, lakini nimewakataa kwa ajili yako, kutokana na nafasi yako, kutokana
na kukuamini, sasa usije ukaniharibia binti yangu,binti yangu nampenda
sana….’akasema baba mkwe
‘Nashukuru sana mkuu wangu, mimi nakuahidi nitamlinda kama
ninavyolinda mboni yangu ya jicho...’akasema kwa kujiamini
‘Huyu binti kalelewa vyema…hana dosari, ukija kumharibu, akija
kuharibikia kwako, nitahakikisha hicho cheo chako,hiyo kazi yako unaisahau, na
nitahakikisha unakwenda kusota jela…’akasema mzee huyo ambaye alikuwa
muheshimiwa mkubwa, na kweli akitaka kumharibia angeliweza kutokana na wadhifa
wake, na kutokana na kumuoa huyo binti vyeo vikapanda haraka haraka hadi
kufikia hiyo ngazi aliyo nayo kwa sasa.
Kutokana na msisitizo wa mke wake, hakuwa na lakufanya, ikabidi
akubali,akakubali kuongozana na mkewe kwenye mualiko huo, na alipofika kwenye
huo ukumbi uliosheheni wageni mashuhuri, matajiri wa makampuni, wafanya
biashara,...akaona ili kuondoa wasiwasi ni bora kuzibugia pombe kwa wingi, na
kweli alikunywa kupita kiasi, alitaka alewe ili waondoke mapema, hakutaka
kuonekana na mtu.
Kutokana na kunywa kwa pupa akazidiwa, kuna muda alitaka kwenda
kujisaidia,ili apunguze akainuka kwenye kiti na kumuambia mkewe;
‘Nataka kupata hewa, napitia shotozi,nikitoka hapo nitatoka nje
kidogo, kupata upepo….’akasema
‘Ukichelewa mimi utanikuta nyumbani, na ukichelewa kurudi
nitampigia simu baba yangu aje kukufuata mwenyewe,…’akasema mkewe akiendelea
kunywa kinywaji akipendacho huku akichezesha mkono wake uliojaa vito vya
thamani.
‘Siwezi kuchelewa mke wangu siunafahamu mambo yetu ya kiaskari ni
chapu chapu.., wewe nisubiri…’akasema na kutembea kwenda kujisaidia na kwa vile
alikuwa kabanwa sana, alipofika eneo la chooni, hakuangalia juu, akajikuta
kaingia …
Alipoingia, akawa keshafungua fifungua vya suruali yake, na kabla hajaanza kukojoa kwa pembeni akamuona
mwanamama, bonge la mwanamama, wale akina mama waliofungasha,kama
wamepandikiza, lakini ndivyo alivyo.
Cha ajbu kabisa mwanamama huyo alikuwa na chupi tu, chupi zenyewe,
zile za vipande, na alikuwa kakaa kwenye kiti na kufanya sehemu kubwa ya
makalio yake kukuzidi kile kiti, huyo mwanamama hakuhangaika kujifunika,
alipoona huyo jamaa kaingia, aliendelea na mambo yake,alikuwa akijipodoa,…
‘Oh nimekosea nini,lakini juu niliona kumeandikwa
choo….’akasema,kwani mwanamamahuyo alikuwa akipodoa,na mbele yake kulikuwa na
kiyoo kikubwa, ambacho aliweza kumuona mtu akiingia mlangoni.
Huenda huo ulikuwa ni mpango, au jamaa alikosea, akaingia chumba
kisichostahili, labda chumba hicho kilikuwa maalumu kwa akina mama
kujipambia,…akawa anawaza yule askari, wakati huo alishaanza kuachia mkojo
ukutani, hakuwa na la kufanya.
‘Wewe…nani kakuambia huku ni chooni….’akasema yule Shangingi
‘Oh,lakini nimeona mlangoni kumeandikwa Toilet…..’akasema Inspecta
‘Umesoma maneno yote yaliyoandikwa juu ya mlango, au ulipitiwa
kidogo, uliponioa nimeingia humu, wanaume wengi wanajigonga kwangu, huu mwili
umekuwa ni tatizo, lakini sio mbaya...juu ya mlango kumeandikiwa kuwa , hii ni toilet ya akina mama ya kujirembea, sasa
wewe umeingia na mkwaju wako na kuanza kutuharibia chumba,….’akasema huyo
mwanamama.
‘Sahamani sana…’akasema mkuu akimalizia kumwanga mkojo wake
‘Hahaha, samahani eeh, ili nikusamehe,inabidi ufanye nitakavyo
mimi, unaniona nilivyo, wanaume wanautafuta huu mwili kama wanavyotafuta
almasi, sasa wewe umepata bahati ya kuuona mwili huu nikiwa hivi, fully naked, inabidi uwajibike…’akasema
‘Unataka nifanye nini…..acha upuuzi wako huo, unanifahamu mimi ni
nani?’ akauliza na wakati huo yule mwanamama akawa kasimama kwenye kile kiti
alichokuwa amekaaa, akamsogelea mkuu huyu kwa madaha,akijirembua, na mkuu huyu,
akataka kugeuka kukimbia lakini alichelewa, akawa keshaingia mikononi mwa
mwanadada huyu.
‘Hahaha ni mara ya kwanza kukutana na mwanaume anayekimbia
mwanamke na mwanamke mwenyewe kama mimi, hahaha, hivi wewe kweli wewe ni
mwanaume ajabu kabisa....hahahaha….usiniangushe,….’akasema huyo mwanamama akiwa
keshaanza kazi yake, na mkuu huyu akawa anajiuliza hili limetokea kwa bahati
mbaya au ilipangwa
‘Oh, samahani wewe mwanamke, …mimi sio kama unavyonifikiria,…..’akasema
Inspecta, akigeuka kutoka kuondoka na kusogelea mlangoni, alisahau kuwa
alishafungua suruwali yake, na yule mwanamke alishavita mkanda, kwahiyo ikawa
inamvuka..., akashika kitasa kufungua huo mlango kwa mkono mmoja huku mkono
mwingine ukishikilia ile suruwali yake..., lakini mlango ukawa haufunguki, kumbe
ulikuwa umefungwa kwa nje.
‘Nani kaufunga huu mlango tena, nataka kutoka haraka, waambie
wafungue huu mlango kwa haraka, kabla sijauvunja, mnanielewa mimi ni nani…’akasema
Inspekta
‘Nakufahamu sana, wewe ni Inspekta wa polisi, na mara nyingi
askari mnapenda sana wanawake, au sio..., na ndio maana nipo hapa kwa ajili
yako, kukuondolea kile unachokikosa kwa mke wako…..’akasema na Inspecta akaona
sasa hilo ni tatizo, akageuka akijiandaa kutumia umaarufu wake ili atoke humo
ndani kwa haraka, alimkumbuka mkewe, hakutaka kabisa kumsaliti.
Wakati anataka kugeuka, alihisi kama mkono umetoka kwa nyuma,
ukashika pua yake, na alichoweza kuhisi kwa muda ule ni kujiona kama anaelea
hewani, na hakujitambua tena, hadi alipoamuka asubuhi…,
‘Samahani bosi nimeambiwa nikuletee nguo zako hizi hapa uwahi
kazini…?’ ilikuwa sauti ya mwanadada, mwanzoni mkuu huyu alijua ni mfanyakazi
wake wa ndani, lakini macho yalipozoea mwanga, akamuona sio huyo mfanyakazi
wake, alikuwa muhudumu wa hoteli,kutokana na mavazi yake.
‘Nimefikaje humu ndani, na ni nani kakupa nguo zangu hizi za
kazini?’ akauliza akiziangalia kwa makini , ni kweli zilikuwa ni nguo zake
hakuwa na shaka nazo.
‘Nimepewa na bosi wangu?’ akasema
‘Bosi wako…bosi wako ni nani?’ akauliza
‘Vaa nguo zako utaonana naye pindi…..’akasema na Inspecta
akajiinua kitandani na kujiona kweli yupo uchi kama alivyozaliwa, na hapo
akakumbuka tukio la jana, akageuka kumuangalia yule binti, akauliza;
‘Yule, yule...yupo wapi huyo malaya,...yupo..yupo wapi?’ akauliza
‘Mimi sijui maana nimeingia asubuhi ya leo, sikuwepo jana, lakini …nimesikia
uliingia chumba hiki na shangingi….yule mwanamama mwenye mwili mkubwa na umbo
la nane…’akasema
‘Shangingi! Shangingi ni nani, na yupo wapi maana nikimpata ni
lazima akalale jela, hawezikunifanyia hivi?’ akauliza huku akionyesha hasira
‘Mhh, mbona wanaume wengi wanamfahamu sana kwa umbile lake, na
wengi wanamtaka sioni ajabu kwako ….’akasema na huyo mkuu akamkatisha kwa
hasira na kusema.
‘Mimi ni mume wa mtu siwezi kumtaka mwanamke yoyote zaidi ya mke
wangu, yupo wapi, maana anastahili kuadhibiwa, hawezi kunizalilisha kiasi
hiki....’akasema kwa hasira
‘Mhh, naona ajabu kweli, hata hivyo aliondoka asubuhi hii hii, saa
hizi yupo kwenye ndege, kasafiri kwenda Ulaya kwenye mafunzo na maonyesho ya
mavazi,akirudi hapa atarudi na mwanadada mmoja, ambaye yupo huko huko….’akasema
huyo muhudumu
‘Oh, mmh, kuna nini kimetokea,..’akajiuliza kichwani,na kabla
hajapata jibu akasikia saa yake ikitoa mlio wa ishara kuwa anahitajika kuwa
kazini, akamuangalia yule mwanadada, na yule mwanadada akaweka nguo pembeni ya
kitanda na kuanza kuondoka.
Inspecta, akasimama na
akajiona hajisikii vyema, akatoka na kuingia bafuni, akitaka kujimwagia maji
huku akijiuliza maswali mengi kichwani,na kujaribu kukumbuka yaliyotokea jana,
lakini akili ilikuwa haifanyi kazi kabisa, akawa hakumbuki, anachokumbuka ni
kuingia choo cha kina mama kwa bahati mbaya, na baada ya hapo hakumbuki kitu…..
Akamaliza kuoga, na kurudi chumbani, na kuzichukua zile nguo,
zilikuwa nguo zake, anazifahamu sana, kwani jana asubuhi zilivyoshwa vyema na mfanyakazi
wake wa nyumbani, na aakazichukua mwenyewe na kuziweka kwenye kabati lake, na
ndizo alitarajia kuzivaa leo akiingia kazini, sasa zimefikaje hapo...akazidi
kuchanganyikiwa.
Akaziinua zile nguo akijiandaa kuzivaa, na mara kukadondoka kitu,
akakifuatilia kwa macho,akaona ni bahasha inayoonyesha kuwa kuna kitu kizito
ndani yake,akainama na kukiokota, na kabla hajaifungua ile bahasha simu yake
ikaita, alipoangalia akakuta ni mkewe,hakuipokea kwa haraka akavaa zile nguo,
huku simu ikiendelea kuita.
‘Oh sasa nitamuambia nini huyu mwanamke….’akasema na ile bahasha aliyokuwa
nayo mkononi, ikamdondoka,na kutoka kwenye ile bahasha kukatoka picha kadhaa na
kusambaa sakafuni…
‘Picha,...’akasema kwa mshangao, hakumbuki kuweka picha kwenye
hizo nguo zake, akaina kuziangalia zile picha.
Picha iliyokuwa juu ni picha ambayo ilimfanya mapigo ya moyo
yasimame kwa muda, akahisi kichwa kikiuma, akahisi pumzi ikimuishia, akafumba
macho na kukaa kitandani, alipofumbua, akahisi hayupo peke yake, na aliona mtu
kasimama mlengoni.
‘Wewe ni nani?’ akauliza kwa sauti nzito ya kiaskari
‘Haina haja kuniuliza mimi ni nani, …lakini kama unataka
kunifahamu basi fuata nitakayokuambia..’akasema huyo jamaa.
‘We-we-we ndio umefanya haya yote…?’ akauliza akitaka kuangalia
chini, lakini aliona aibu, na alitamani aifiche ile picha isionekane
‘Mhh sina uhakika unaongelea nini, naona hapo chini kuna bahasha,
na pembeni kuna picha, ndio hilo unaloongelea au... ooh, mungu hebu angalia
hiyo picha,..ooh, hivi kweli mtu na wadhifa wako unaweza kufanya huo uchafu,
ma-ma-ma, mmh ni aibu mkuu mzima kama wewe unatembea na ..ni nani huyo?’
akauliza akichungulia chini.
Mkuu akitumia mguu wake azisogeza zile picha kwa mguu kama
kuzificha, lakini ndio akawa kasababisha picha nyingine zitoke kwenye hiyo
bahasha, na yule jamaa akawa anacheka, huku akiwa kashikilia kanda ya Cd’s
mkononi, akasema;
‘Usijali mkuu, hiyo ni kazi ndogo kuisawazisha, mtu kama wewe
huhitajiki kuaibika, mimi nitakulinda kwa nguvu zangu zote nawafahamu hawa watu
waliokufanyia hivyo, hata mimi wamenitumia hii Cd’s niinunue kwa milioni
kadhaa, nimeiona kidogo, nikaona kweli thamani yake inalipa, lakini, sio vyema
kumuabisha mkuu kama wewe.....’akatulia na huyo mkuu akasema;
‘Sikuelewi unasema nini, kwanza nimeshachelewa kazini, sasa hivi
wewe na wenzako mpo chini ya ulinzi ni lazima niwafishe nyote kituoni….’akasema
kwa hasira
‘Usijali mkuu tumeshaongea na mkuu wako wa kazi, na anajua kuwa
umepitiwa kidogo na pombe ulizokunywa jana, ila hajui ulichokifanya, na nahisi
akikijua sizani kama utadumu kwenye kazi yako, hebu angalia hizo picha vyema,
halafu ndio ufikirie kufanya hiyo kazi yako ya kutuweka chini ya ulinzi, nahisi
wewe ndio unatakiwa kuwa chini ya ulinzi, na mimi nitakuwekea dhamana,
unasemaje….’akasema huyo jamaa akitabasamu kwa dharau.
‘Oh, ….’akasema huyo mkuu sasa akiinama kuziokota zile picha, kila
picha iliyofika mkononi mwake,ilikuwa mbaya, mbaya hajawahi kuuona, aliwahi
kuziona picha kama hzio kwenye mapicha mabaya yanayoonyeshwa kwenye video chafu,
na alikuwa akizilaani sana, sasa anachoona yeye ni tofauti, kwani muhusika mkuu
kwenye hizo picha ni yeye na yule mwanamke...
‘Huyu mwanamke nikikutana naye tena, sijui nitamfanya
nini....’akawa anaapiza kichwani, akawa anajiuliza jina lake ni nani, na huyo
muhudumu kasema anaitwa shangingi, hakuwa kabisa kufkiria katika maisha yake
kuwa angelikifanya kitendo kama hicho.
‘Mungu wangu..’akasema akibadilika sura, hasira, chuki,….lakini
kikubwa kuzidi yote ni aibu, aibu kuwa hizo picha zikionekana kwa hao watu wa
udaku, atakuwa kaumbuka, na uso wake atauweka wapi, hiyo ni aibu ya mwaka, akamuangalia yule mtu
aliyesimama mbele yake...huyu mtu, alikuwa kavaaa mawani makubwa,na ndevu
zinazoonekana ni za bandia kwa uzoefu wake alijua kabisa huyo mtu hana ndevu za
namna hiyo, japokuwa hamfahamu ni nani. Kwa hasira akasema
‘Nyie watu nawahakikishia nitawafunga,na nitahakikisha hamtoki, mtaozea jela ….’akasema
‘Mhh,hilo sio muhimu sana kwetu, sizani kama una haja ya kupoteza
pumzi zako kwa hilo, kopi kama hizo zipo mbioni kumfikia mke wako, na nyingine
kwa nani yule ehe, nimewaambia wazipeleke kwa baba mkwe wako, au unasemaje na
nyingine zipelekwe kwa mkuu wako wa kazi, hapo tutaona ni nani ataozea jela….’akasema
na kucheka kwa kicheko cha dharau.
‘Hahaha, mkuu, inspecta mzima wa polisi unatembea na machangudoa,
unamfahamu huyo mwanamke, wanamuita shangingi...kajazia, kaumbika umbo la nane,
mkuu kama wewe ukashindwa kuvumilia...hahahaha...mke akiziona hizo picha sijui
kama kutakalika...hahaha...’akacheka kwa dharau
‘Hivi mnataka nini kwangu?’ akauliza sasa akiwa kasawajika.
‘Hapo sasa umesema neno….utapata ujumbe pindi, leo au kesho, cha
muhimu ni kuitikia huo ujumbe,na kufika huko utakapoelekezwa…mengine utayasikia
huko huko….ukumbuke hizo ni picha, bado kuna CD’s zake zitakuwepo madukani pindi ukijiafnya wewe ni
mjanja....’akasema huyo mtu
‘Mkuu sisi, hatuna nia mbaya na wewe, ila tunachotaka ni wewe
uishi maisha ya raha na mkeo, mkeo anapenda starehe, ni mtoto wa watu hajazoea
shida, sasa kwanini upate vidonda vya kichwa wakati njia ya kupata pesa ipo,
kama utakuwa mtu mwema ukawa mtu wetu, hizi picha na Cd’s tutazizuia, sizizagae
mitaani….’akasema.
‘Mtu wenu…mimi niwe mtu wenu na mambo haya machafu mnayoyafanya,
mna akili kweli...?’ akauliza.
‘Ni nani kafanya mambo machafu ni sisi au ni wewe, mkuu hebu
angalia hizo picha vyema, ni aibu, mkuu kama wewe kufanya mambo machafu kama
hayo,..lakini nikuambie ukweli, mwenyewe utafurahia, ….nakuambia usipate taabu,
nchi na maisha yako utayaona mazuri tu, eti nikuulize kwanini uje kufa
masikini, wakati kuna njia za kutajirika, hebu funguka kiakili, uone mbali,
....’akasema huyo jamaa, na mkuu huyu akawa kimiya
‘Mimi nakuhakikishia kwa mikakatii niliyo nayo, ukiwa na nami,
hutakufa masikini, utakuwa tajiri, cha muhimu kwanza ufike kwenye mafunzo
maalumu, kuna chuo chetu cha watu kama wewe, na ikiwezekana, utakwenda nje
kidogo,…..’akasema
‘Nje kufanya nini?’ akauliza
‘Kazi yako hiyo inahitajia utaalamu fulani, mwenyewe utaona, sio
lazima uende nje, ila ikibidi , nimefanya mpango, kuna mtaalamu fulani atakuja
hapa nchini, huyo mtakutana naye na mafunzo atakayokupa, hutaamini, hutakuwa
wewe tena, ...kuna utaalamu wa kisasa unatakiwa ujifunze...’akaambiwa
‘Utaalamu huo wa nini, ...?’ akauliza
‘Hayo maswali sio ya kuniuliza kwa sasa, kwanza fuata hayo
ninayokuelezea, kuanzia sasa mimi ndiye bosi wako....’akaambiwa
‘Bosi wangu!?’ akauliza kwa mshangao na mara simu ikalia, akaichukua simu yake
kuangalia mpigaji wa hiyo simu ni nani, akakuta anayepiga ni baba mkwe wake….
‘Huyo ni baba mkwe wako sio…sasa uamuzi ni wako...hizo picha anazo
mtu wa kupeleka vifurushi, anasubiri kibali changu, unasemaje mkuu?’ akauliza
Mkuu huyu akainama na kumbukumbu za hizo picha zilivyo, zikamfanya
ashindwe hata kupokea simu ya baba mkwe wake, akamuangalia huyo mtu mbele yake,
na moyoni akawa kajawa na wimbi la hasira, lakini angelifanya nini kwa muda
huo, akasema;
‘Nitafika kama utakavyo, ila nakuonya, leo umeshinda wewe
lakini.....’akasema na kukatishwa na simu alikuwa baba mkwe wake apiga tena,
akajua huenda mke wake kapeleka mashitaka kwa baba yake kuwa haonekani.
‘Usijali, viitisho, hasira jaziba vyote vitayeyuka pale utakapoona
mshahara wako wa kwanza, ulishawahi kupata dola elifu tatu hadi tano kwa
mwezi,...na kila kitu kitu unapata,....?’ akauliza na Inspecta kwa haraka akawa
anazibadili hizo pesa kwa pesa za kibongo
‘Eti nini?’ akauliza
‘Huo utakuwa mshahara wako wa kuanzia, nafikiri matatizo madogo
madogo ya shemeji yatakwisha, hutapata shida ya kuumiza kichwa tena, unakosa
nini hapo, ....fikiria kwa makini yote hayo....’akaambiwa
‘Pokea simu ya baba mkwe wako huyo, ujue anahitajia nini, maana
hizo picha atazipata pindi utakapokwenda kinyume na makubaliano yetu, na ukijifanya
mjanja simu kama hiyo akikupigia safari nyingine ujue ni nini atakuambia, nakutakia
kazi njema…’akasema na kufumba na kufumbua jamaa akawa haonekani, ni kama vile
kayeyuka…..
Inspecta akaiweka simu na kumsikiliza baba mkwe wake, huku akili
yake ikiendelea kuwazia zile dola elifu tatu hadi tano.....
NB: Haya mmoja mmoja akawa anaingia kwenye dunia ya bwana Diamu,
tuone ni nani atafuata au ni nini kitafuata.
WAZO LA
LEO:
Uwajibikaji wa kazi ni pamoja na kujiamini, na kujiamini hakuji bila ya kuwa na
uhakika na hicho unachokifanya, na ili uwe na uhakika na unachokifanya unahitajika
kusoma, kufanya utafiti. Tuwe na tabia ya kusoma na kufanya utafiti katika
mambo yetu, badala ya kuongea tu, kuzua, na propaganda...
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment