Docta alikuna kuna kichwa
huku akimuangalia nesi wake kama ataweza kumpa wazo la kumsaidia, lakini kwa
muda huo nesi naye alikuwa na mawazo
yake kichwani, akiwa kashikwa na wasiwasi kuhusu mabadiliko aliyoyaona
kwa bosi wake, akawa tu anamuangalia bosi wake kwa mshangao,
‘Huyu bosi ana nini leo
au ni hizi pombe alizokunywa leo,....’akawa anajiuliza kichwani kwani hii sio
kawaida yake anapotajiwa mteja mwenye sifa kama hizo alizomtajia ambazo kweli
sifa hizo anazo huyo mteja aliyekuja,...
Docta alipoona nesi wake
kaduwaa akimuangalia akajua hapo sasa hana jinsi , akageuka nyuma kuangalia
kama kuna sehemu ya kuweza kujificha au kutokea, akaona hakuna hutaamini, kwa
muda huo alishaisahau ofisi yake mwenyewe kuwa ina mlango mmoja tu wa kuingilia
na kutokea, ...
‘Hii sasa ninalo, sina
jinsi, huyu nesi hawezi kufanya lolote, keshaharibu toka awali, anganipigia
simu kwanza,...ooh, siwezi kumlaumu sana...’akawa anajisemesha kichwani huku
akiendelea kujikuna kichwani.
‘Huyu mdada kama ndio
yeye sizani kama ataweza kunisamehe, hata kama ni tajiri, lakini kwa hayo
niliyomtendea, mmh, sijui, na hawa akina dada, huwa hawasahau mabaya
waliyotendewa kwa urahisi...hili sasa ninalo, lakini.....’akajaribu kufikiria
njia ya kufanya
Wakati anawaza afanye
nini, ...akilini akaanza kukumbuka tukio lilisababisha haya yote, tukio ambalo
lilimtia doa, na alijua hataweza kulisafisha hilo doa, mpaka mtendewa mwenyewe
akiri kumsamehe,...na huenda angelifanya hivyo kama wangelikutana, je leo kaja
na kwa nia mbaya au ndio kaja kumfunga,....hapo akataka kumuuliza huyo nesi
kama hakuja na polisi,
‘Ni kimuuliza huyu nesi
nitazua maswali mengi....’akajisema na mara kichwani kumbukumbu ya yalitokea
kati yake na mwanadada huyo zikaanza kumjia kichwani, akaanza kukumbuka tukio
lenyewe, na kumbukumbu hizo zilimjia kwa haraka sana....
******
Siku hiyo akiwa ofisini
kwake ofisi isiyo rasmi, akiwa na chupa ya kinywaji chake akipendacho, alijilaza
kwenye kiti huku akiwa jinsi ya kupata pesa, kwani mshahara wake alishaukopa
wote, na ofisi yake ya vichochoroni hailipi, polisi wanamuandama.
Akainua chupa yake juu kuangalia nini kimebakia, akakuta ni kama robo
tu, akajifuta mdomo, akainama na kutulia, alihisi kama sauti inakuja mlangoni,
na kwa haraka akavuta droo ya meza na kuiweka chupa yake, baada ya kuhakikisha
kuwa ameifunga vyema mara , akasikia mlango ukigongwa.
‘Naomba huyo awe mteja...’akaomba kwa imani yake, na kuanza kujirekebisha
vyema, huku akisema
‘Mhh, kama ni mteja mmh...’akawa anahakikisha meza yake ipo makini
kwa ajili ya kupokea mgeni, akashika kipimio chake cha kidakitari akakivaa
shingoni,...pamoja na ulevi wake, lakini akilini alikuwa makini.
Pale alitamani aitoe chupa yake apige mafundo mengine mawili,
lakini akaona atafumwa, na hakupenda mteja wake amuone akinuka pombe, akavuat
droo nyingine akatoa chupa ya manukato ya kuondoa harufu akapuliza na
kujipulizia mdomoni..
‘Come in....’akasema,
Mara mlango ukafunguliwa, akaingia mdada mmoja mrembo, akili yake
ilisimama kwa muda, hakuamini, lakini kitu kilichomshangaza na kumfanya ile
hali yake ya kushangaa iwe ya namna nyingine ni ile hali ya yule mdada, pamoja
na urembo wake, lakini alikuwa analia
Hii ilionyesha wazi kuwa huyo mdada ana tatizo kubwa, docta akavuta
pumzi na kuzikaribisha hisia za maliwazo , alijua ni nini afanye kwa muda kama
huo, hiyo ilikuwa akzi rahisi kwake, lakini kuna kitu kingine kilishateka nafsi
yake,....tamaa.
Akijitahidi kusimama akayumba karibu adondoke, lakini akajishikiza
kwenye meza, akaona akisimama kwa muda huo ataumbuka, akarudi akakaa, na
kumkazia yule mdada macho, sura ya yule mdada ilionekana kama lulu machoni
mwake, akasema;
‘Kwaza tulia sitaki mtu kulia kwenye ofisi yangu, maana hapa ni
sehemu ya neema, sehemu ya kuondoa matatizo sio ya kulia, hebu niambie una
tatizo gani...?’ akauliza, na mdada akawa anafuta machozi
‘Kaa kwenye kiti, ....’akasema docta, na yule mdada akawa sasa
katulia, na akasogea kwenye kiti
Yule mdada kwanza alimuangalia yule docta, alishasikia sifa zake,
hakuona ajabu, alijua kabisa kalewa, lakini alishaambiwa kuwa huyo docta ili
afanye kazi yake vyema ni mpaka alewe, hiyo ndio tabia yake, kwa mashaka
akasogea kwenye kiti ni kukaa
‘Niambie mrembo una tatizo gani?’ akauliza
‘Nina mimba, na siitaki hii mimba, lakini.....’akasita na machoni
kukaanza kujawa machozi
‘Lakini nini... wewe sema usiogope, umekuja kwa mtaalamu
mwenyewe...’akasema docta huku akimkagua yule mdada kwa macho, hakuamini dada
mrembo kama huyo anaweza kukutwa na hayo aliyoyasikia, akataka kujua zaidi,
japokuwa kwake muhimu ilikuwa pesa, au vinginevyo....
‘Sina pesa kabisa,...nilikuwa nazo lakini nimeibiwa, ...na wazazi
wangu walishanifukuza nyumbani, na aliyenipa mimba kanikana kabisa...sijui hata
nifanye nini, ndio maana nimeona niitoe
hii mimba....’akasema huyo mdada
‘Oh, my God, ndio
kinakufanya ulie, ...hapana, labda kama kuna jambo jingine,..lakini usijali,
mimi nitakusaidia,unasikia mrembo, mimi nipo kwa ajili ya warembo kama
nyie..hapa umefika, ...’akasema docta
akisimama, sasa alikuwa kajiamini.
‘Kweli docta, nitashukuru sana, nakuhakikishia nitakuja kukulipa
pesa zako, ngoja mambo yangu yakae sawa, kwani kuna kazi nimepata, lakini....’akasita
tena kuongea akawa kama anataka kulia.
‘Usijali, ....umesema umepata kazi, ....okey, sasa kwanini unaweka
uwalakini...?’ akauliza
‘Ni kuhusu masharti ya hiyo kazi, wao hawataki mwanamke mja mzito,
au aliyezaa...kwahiyo sitaki nijulikane kabisa kuwa nilikuwa na mimba....’akasema
huyo binti.
‘Hahaha, hapa umefia, haina shaka kabisa nikuambie kitu, mimi
najua jinsi gani nitakufanyia, haiwezi kabisa kujulikana, na nitakuandikia
cheti cha kuthibitisha kwua wewe hujawahi kuzaaa, unasikia, ...’akasema docta
‘Lakini mimi sina pesa zakukulipa...’akasema huyo mdada
‘Nimeshakuambia pesa kwangu sio tatizo, kwanza kwanini utoe pesa,
...wewe mwenyewe ni pesa tosha kabisa, hahaha, wewe, ni mamilioni....’akasema
na yule mdada akabakia mdomo wazi, hakujua huyu docta ana maana gani, akauliza
‘Una maana gani kusema hivyo?’ akauliza
‘Mhh, jamani ina maana huelewi, wewe sio mtoto mdogo, maana mpaka
ukafikia kupata mimba, ina maana unajua kila kitu, sio lazima unilipe pesa,unaweza
kunilipa kwa njia nyingine,...nikuambie ukweli wewe dada ni mrembo
sana...’akasema na yule dada akashituka sasa akawa anataka kusimama ili aondoke.
‘Mmh, docta, hapana mimi sio kama unavyonifikiria, hata hiyo mimba
niliipata kwa bahati mbaya, sana, siku hiyo alitumia nguvu...docta mimi naahidi
nitakuja kukulipa pesa yako....’akasema
‘Mimi nimeshasema sitaki pesa yako, nitakusaidia, ila na wewe
unisaidie, ni kitu kidogo tu kwangu..unajua nikishapiga gilasi nikaona mrembo
kama wewe siwezi kabisa kuvumilia,...ni kidogo tu, tunamaliza tunaanza shughuli nyingine....’akasema docta sasa akimsogelea
yule mdada, na yule dada akawa keshasimama
na sasa akawa anarudi nyuma.
‘Sikiliza mrembo, kwani kipi cha ajabu kwako wewe, wewe umesema huna
pesa, lakini mwili wako unazidi pesa zozote utakazonilipa, kabla ya yote
tumalize hili sio kitu kigeni kwako au sio....’akasema docta.
`Wewe docta vipi, nimekuambia pesa sina mimi ni pesa kwa vipi una
maana gani wewe mbona sikuelewi....hebu niache, usinisogelee nitapiga
kelele....’ ubishi mkali ulizuka, na kwa muda huo mzuka wa uzinzi ulishampanda docta
huyo, hakuwa anajali kitu, pombe ilishamvuta hisia zake, na ibilisi akawa
anashabikia....
‘Kumbe ndio tabia zako..mimi sitaki tena,....’yule mdada akawa
kajitoa kwa docta na kumsukuma , na docta akapepesuka, lakini akajitulia na kujiweka
sawa, akasema;
‘Unajua wewe dada, mimi nimeshakupenda, usijali, mimi nipo tayari
kwa lolote lile uwe mpenzi wangu unaonaje, hata hiyo mimba mimi nitailea
mwenyewe, lakini kwanza unipe uhakika wa hapa hapa...’akasema
‘Sitaki mwanaume mimi, yaliyonikuta yanatosha ninachotaka ni
kuajiriwa niishi maisha yangu kivyangu....’akasema huyo binti na docta akaona
atashindwa kumshawishi huyu binti, na hata akitumia nguvu, anaweza akazidiwa,
lakini yeye ni docta ana mbinu nyingi tu.
Docta akajaribu kumuhadaa hivi na vile na alipoona binti
haeleweki, akaanza kutumia nguvu tena, na alipoona hata nguvu hazifanyi kazi,
akatumia dawa anazojua yeye mwenyewe na yule binti wa watu akapotewa na fahamu,
na hapo docta akatimiza adhima yake, ....
‘Alipomaliza zoezi la kwanza, kwa haraka, akafanya kazi ambayo
binti huyo aliijia, kabla binti hajazinduka jamaa akawa ameshaitoa ile mimba..ilikuwa
rahisi kwake, lakini kwa pupa, na kwa haraka alijikuta kafanya kosa ambalo
hakuwahi kulifanya kabla....
Binti akazindukana na kujikuta yupo kitandani, akasimama na kwa haraka
akahisi maumivu tumboni, akalishika tumbo lake, akahisi maumivu yakiendelea, na
mara docta akaja akiwa kashika dawa, akasema;
‘Maumivu ni kawaida, yatakwisha tu, tumia dawa hizi....’akasema
‘Umenifanya nini docta...?’ akauliza
‘Kwani wewe ulikuja kufanya nini hapa?’ akauliza
‘Mimi sikubali kwanza umenibaka, halafu ....mmmh,...’akawa amahisi
maumivu makali tumboni, akawa anajinyonga nyonga, na hapo docta akajua ni lile
kosa alilolifanya, akaanza kujijutia, kwanini hakutuliza kichwa chake..kwanini
imetokea hivyo, na hajawahi kufanya makosa kama hayo kabla..
Yule mdada akapoteza fahamu, na alipozindukana, alijikuta yupo
hospitali nyingine, akihudumiwa na docta mwanamke, na yule docta alipoona huyo
mdada kazindukana akaanza kumhoji
‘Hebu niambie ilikuwaje?’ akaulizwa
‘Mhh, nimefikaje hapa?’ akaulizwa
‘Umeokotwa barabarani karibu na mtaro, na ukafikishwa hapa, na
tulipokuchunguza tukagundua kuwa umetolewa mimba..lakini.....’akasita
‘Lakini vipi?’ akaulizwa
‘Aliyefanya hivyo alikosea, kakuharibu sana, inabidi tukusafishe,
na sijui...tutaona baadaye, naona aliyefanya hivyo, hakuanya kwa uangalifu,
...ni nani huyo?’ akaulizwa
‘Kwani kanifanyeje, mbina hata sijui alichofanya...?’ akauliza
akianza kulia
‘Kwanini kwanza ulifanya hivyo, hivi nyie mabinti mna akili gani,
kwanini ukakimbilia kutoa mimba, huoni balaa ulilokumbana nalo, umeshaharibu
kizazi..’akasema
‘Oh, mungu wangu,....’akasema na mwili mzima ukaishiwa na nguvu,
..
Kumbe kwa papara za yule
docta, aliitoa mimba na kumaribu binti wa watu kizazi, kiasi kwamba kupata
mtoto mwingine ingekuwa ni miujiza. Alitibiwa hapo hospitalini na akashauriwa,
kwenda polisi kumshitaki huyo dactari..
Na kweli huyo binti akiwa na ushahidi wa udakitari, akaenda
kushitai polisi na polisi walishasikia taarifa za huyo jamaa toka kwa watu
wengi, na walisubiria ushahidi kama huo;
‘Kwahiyo kakubaka, na kukutoa mimba bila rizaa yako...ushahidi upo
wazi, ngoja tukalisokomeze ndani, safari hili harina ujanja...’akasema askari
wa hicho kituo.
Polisi wakafika eneo alilokuwa akifanyia hizo shughuli huyo
dakitari, kama walivyoelekezwa na huyo mdada, maana huyo jamaa naye alikuwa
mjanja, kila siku alikuwa akibadilisha kituo cha shughuli zake, lakini hata
hivyo, polisi walipofika kwenye eneo wakakuta kweupe, alishakimbia, japokuwa
kulikuwa na mabaki mabaki ya ushahidi kuwa kulikuwa na dispensari isiyo rasm
kutoka kwa mwenye nyumba, na mwenye nyumba akakamatwa kuisaidia polisi, lakini
baadaye akaja kuachiwa na jamaa hakuonekana hata kazini kwake akawa haonekani.
Jamaa hakuwa na ofisi moja, hata hivyo aliona hali sio shwari
kwake, akahama jiji kwa muda na kwenda kujificha mikoani... aliishia mikoani
kwa muda, akitoa uzuru kazini kwake kuwa anauguliwa na baba yake, na baadaye
akaomba uhamisho wa muda kufanyia kazi hiyo ya udakitari huko mikoani, akakubaliwa...kwani
alikuwa na watu wakimsaidia huko kazini kwake, ...., alikaa huko mikoani karibu
mwaka mzima bila kujulikana.
Docta huyu aliporejea, ndio akaanza harakati nyingine za kupata
kipato cha ziada, ndio akajiingiza kwenye biashara ya madawa, na alijua jinsi
gani ya kupooza mambo, bongo hii ukiwa na pesa hakishindani kitu...akajitahidi
hadi akawa mmoja wa wakuu kwenye kitengo cha madawa, kwahiyo ikawa rahisi kwake
kufanya kile alichokianza.
Mitaani yule mdada akawa anahangaika, akifika polisi anaambiwa
bado wanamtafuta;
‘Mimi nimeambiwa karudi na kesharudi kazini kwake...’akasema
‘Sisi kila tukifika hatumuoni, usiwe na wasiwasi dada tutamkata
tu...’akaambiwa
Yule mdada akaona kuna kitu kimechezwa hapo, akaamua kwenda ngazi
za juu, na taarifa zake zikafika ofisini alipokuwa akifanyia kazi rasmi, kuwa
huyo jamaa ana kesi ya kujibu kwa kuendesha shughuli za utoaji mimba na hata
kubaka, na pale kazini waliposikia hivyo sasa wakaona hawawezi kumbeba tena
huyo jamaa.
Walichofanya wao, ni kumsimamisha kwa muda wakisema wanafanya
uchunguzi kujirizisha, kwani hata wao walishashuku hilo tatizo lakini walikuwa
hawana uhakika ni nani anafanya hiyo hujuma, na waliona ili uchunguzi uweze
kufanikiwa vyema, inabidi huyo docta apewe barua ya kusimamishwa kazi kwa muda...
Docta akasimamishwa kazi, kwa uchunguzi....
NB: Jembe na mtandao vinanipa shida, inabidi nimalizie hapa kwa leo....tupo pamoja
WAZO LA
LEO:
Udhalimu ukizidi, mioyo ya watu huota sugu, na hata ubaya ukitendeka watu
wanaona ni awaida tu, hasa wakitendewa wale wanaoona sio wenzao. Tukumbuke kuwa
dhuluma anayotendewa mwenzako kama wewe unaona na unafahamu kuwa ni dhuluma,
halafu ukakaa kimiya bila kukemea, au kufanya jitahada zozote basi na wewe ni dhalimu,
laana ya udhalimu huo itakuandama...na ipo siku utaulizwa.
Tuteeni haki, pale tunapoona wenzetu wasio na hatia wanadhulumiwa, tuache ushabiki usio na tija, ili dunia iwe ya amani na upendo. haki ikipotea, na dhuluma ikatawala, ujue ni swala la muda tu, leo ni kwao na kesho ni kwako
Ni mimi:
emu-three
No comments :
Post a Comment