Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Saturday, May 3, 2014

BAADA YA DHIKI FARAJA-49


 Kesi ya mauaji ya mtoza ushuru ilianza kwa kasi waendesha mashitaka wakiwa wamejipanga vyema, wakiwa na ushahidi na vielelezo vyao, na muendesha mashitaka alitamba kuwa kesi itakiwsha mapema, kwani kila kitu kipo tayari, na hali ilivyojionyesha ni kuwa mlinzi huyo ndiye muuaji, japokuwa alikana shitaka hilo kuwa yeye hakuua.

Muendesha mashitaka akawa anamuita shahidi mmoja baada ya mwingine, wakifuatilia tukio lenyewe lilivyokuwa, na kila shahidi aliyesimamishwa kutoa maelezo yake ilionyesha wazi kuwa mlinzi wa mdada yupo hatiani. Hata ule usemi wa avumaye bahari papa, kumbe samaki wengine wapo ukasahaulika. ushuru

Wakati wa mapumziko nikapata muda wa kukaa na mpelelezi, ambaye mara nyingi alionekana akitoka na kuingia, kila simu yake ilipoita, kwa vile sikuwa mbali nay eye, niliweza kusikia mngurumo wa taratibu wa kuashiria kuwa kuna mtu anataka kuongea nay eye, kwa hali kama ile, sizani kama alipata muda mzuri wa kuifuatilia hiyo kesi, nilipokaa naye nikamuuliza

‘Kwa jinsi kesi ianvyokwenda, inaonyesha wazi kuwa kweli huyu mlinzi ndiye aliyemuua mtoza ushuru,au wewe unasemaje?’ nikamuuliza

‘Mengi yaliyotokea huko ndani imekuwa ni kazi kubwa sana kuupata ukweli wake,kwani wote waliokuwa huko ndani hawataki kusema ukweli,ukiwemo wewe mwenyewe, nah ii inanipa shaka kwua huenda haki isitendeke, ...’akasema

‘Kwa vipi, wewe mwenyewe umeona maelezo ya mashahidi na jinsi tukio lilivyokuwa, ukweli wote umeshatajwa, unataka mimi niseme nini tena....’nikalalamika.

‘Una uhakika na hilo, ...?’ akaniuliza

‘Uhakika kwa vipi, kwani wewe ulitaka niseme nini tena, ?’ nikamuuliza

‘Una uhakika kuwa hayo yaliyosemwa na hao mashahidi yana ukweli wote, sikatai kuwa waliyosema sio kweli..ni kweli maana mengi ya hayo niliyaona mwenyewe kwa amcho yangu, lakini bado kuna ukweli mkubwa haujasemwa,....’akasema

‘Kama upi?’ nikamuuliza

‘Hebu niambie huyo mtu aliyekuwa na ndevu ni nani, ...?’ akaniuliza

‘Unarudi kule kule,...nilishakuambia mimi huyu mtu simjui, huenda huyo mlinzi alitunga uwongo wake tu...’nikasema

‘Una uhakika na hilo?’ akaniuliza

‘Sasa kama wanasema alikuwepo mtu kama huyo kwanini huyo mtu asikamatwe kama muuaji,..?’ nikamuuliza

‘Hajaonekana...ndio maana nakutaka wewe uniambi ukweli, kwanini huniamini,...nataka kumaliza hii kesi, kabla hukumu haijatolewa...’akasema

‘Mimi nilishakuambia, hakuna mtu kama huyo, ..mimi sikumuona, hata huyo mlinzi mwenyewe sikumuona akiingia, kwahiyo kiukweli, mimi ni kama vile nilikuwa nje, kipigo cha mdada kilinipoteza akili, na huyo aliyenipiga nyundo kichwani ndiye akanimaliza kabisa, sikuona ...na akili hakuwa na utulivu wa kuona kilichokuwa kikiendelea...’nikasema

‘Kama unavyoona maelezo yote wanayotoa hao polisi, hawajauliza jinsi gani huyo mlinzi alivyoingia, hiyo imekuwa siri ya mlinzi na watu wake waliomtuma,...kama ningeliupata ukweli angalau kidogo ningeliweza kuyageuza haya mashitaka, na kuelezea mahakama kuwa mlinzi hajasema ukweli wote, lakini bado sijapata ushahidi wa kutosha….’akasema

‘Ina maana ungeliwaambia polisi kuwa huyo mlinzi alipitia dirishani, lakini wewe mwenyewe umesema hufanyi kazi na hao polisi, kwanini sasa unavunja miiko ya kazi yako…?’nikamuuliza

‘Mimi nafanya kazi kwa mtizamo wangu,..na sio kwamba sifanyi kazi na polisi, ila kwa tuklio hili, imabidi nijitenge, kwa jinsi ilivyokuwa, lakini mwisho wa siku nikishakamilika,natakiwa kuonana na hao hao waendesha mashitaka....’akasema

‘Kwa mtizamo wako, umesema  huenda haki isitendeke, kwa vipi una hisi mlinzi sio yeye aliyemuua mtoza ushuru?’ nikamuuliza

‘Tutaona huko mbele,…siwezi kusema lolote kwa sasa, ila bado kuna sintofahamu kwenye hii kesi, ...na nakupa nafasi ya mwisho ya kufikiri, uniambie ukweli wote kabla hukumu haijatolewa, ukumbuke, mlinzi sasa hivi yupo kubaya, atahukumiwa kwa mauji na huenda sio yeye muuaji, huoni huo ni unyama...’akasema na marasimu yake ikiita

‘Samahani kidogo niongee na hii simu,...’akasema  na akasogea pembeni na haikupita kidogo,muda wa mahakama ukawa umeshafika, na mashahidi mbali mbali waliendelea kuitwa, wakiwemo askari waliofika, ambao waliwahi kunikamata mimi, na muda ukawa umeisha kesi ikaahirishwa.

‘Jiandae mhasibu, nitakusimamisha kama shahidi...’ilikuwa sauto ya muendesha mashitaka akiwa anapita pale nilipokuwa nimesimama nikimsubiri mpelelezi,

‘Mimi hapana, kwanini....?’ nikauliza

‘Wewe na mdada zamu yenu imeshafikia, mjiandae , nitaongea na nyie baadaye ili kuyaweka mambo sawa...’akasema na kunikabidhi barua, na hakutaka kuongea na mimi kwa kirefu,akaondoka, nilibakia kama mtu aliyepigwa kofi la kushitukiziwa

‘Vipi, nasikia kesho kutwa kesi ikiendelea wewe na mdada huenda mkasimamishwa kutoa ushahidi?’ sauti ya mpelelezi ikanishitua toka kwenye lindi la mawazo, nikageuka kuangaliana naye, na akawa akiniangalia usoni, na mimi nikasema;.

‘Kaniambia hivyo muendesha mashitaka, na mimi sikupenda kusimamishwa kwasasa, japokuwa nafahamu kuwa muda wangu utafika na mimi nitoe ushahidi wangu, lakini hata hivyo naona kama sijajiandaa kwa hilo’nikasema.

‘Kujiandaa kwa vipi?’ akaniuliza

‘Hata sijui, najiona kama nipo njia panda, na sijui nitaulizwa nini, na je hayo nitakayoeleza hayataweza kuwaathiri, watu nisiopenda ...’nikatulia

‘Tatizo lako unajaribu kukwepa ukweli, kwa hivi sasa huna ujanja ukweli wote unatakiwa usemwe, ili haki itendeke, nilishakuuliza toka awali, uniambi ukweli, ili na mimi niwee kukushauri, lakini hujapenda kufanya hivyo, ngoja usimame kiziambani huenda ukazindukana...’akasema

‘Naona iwe hivyo, nikisimama kizimbani nitasema yale yanayostahili...nitajitahidi kufanya hivyo, lakini, sio kuwa hayo ninayofahamu mimi yataweza kubadili mstakabali mzima wa kesi hii, sizani maana kiukweli mimi sijui lolote, ..’nikasema huku nikijaribu kuwaza ni ukweli gani anaoutaka huyu mpelelezi.

‘Nikuambie ukweli, mauaji ya mtoza ushuru, ni sehemu ndogo tu ya tatizo lenyewe, kuna kundi haramu lililojianzishia himaya na sera za umimi, wao walishajiona ni watawala wa kudumu, wanaweza kufanya wapendavyo...hili kundi ni lazima ling’oke...’akasema

‘Kundi gani hilo?’ nikauliza

NB: Nawatakia wikiendi njema.


WAZO LA LEO:Kuua damu isiyo na hatia ni kosa kubwa sana, kumsingizia mtu ubaya asioutenda ni dhuluma kubwa sana, tuwe wakweli na pale tunapotoa shutuma tuwe na uhakika nayo, kwani huwezi kujua ni kwa jinsi gani unavyoweza kumuathiri mtu mwingine kwa kusingiziwa kosa asilolifanya.

Ni mimi: emu-three

No comments :