Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Thursday, April 24, 2014

BAADA YA DHIKI FARAJA-44


‘Mimi hapo sielewi,nakuona unaongea tu, lakini sijakuelewa, hebu nieleze kwanini huyu mtu aliuwawa, na huyo muuaji aliwezaje kuingia, na kufanya hayo bila ya hata mimi kufahamu?’ nikauliza

‘Mlinzi....’akasema.

‘Mlinzi ana nini?’ nikauliza

Ukiangalia mandhari ya lile jengo, utaona kuwa jengo nzima, limezungukwa na ukuta mrefu,uliowekwa waya za umeme na nyaya za usalama...ina maana mtu akizigusa tu, sio tu atashikwa, au kurushwa na huo umeme, lakini pia kutatokea milio ya hatari....sijui kwanini mdada, alifanya hayo yote,...anajilinda sana....’akasema

‘Labda ni kutokana na pesa anazopata....’nikasema

‘Ukiangalai hilo huo ukuta kwanza nimrefu, na pili hata kama utakuwa na ujuzi wa kuziharibu hizo nyaya za umeme, ukapanda juu, ili uruke ndani, huko ndani nako kama ulivyoona unakutana na nyaya za seng’enge, zailizozungukwa na miti ya michongoma....

'Miba ya michongoma hiyo ni mikali sana, kwahiyo kwa yoyote yule, atakayejaribu kufanya hivyo, ni lazima awe amejiandaa, na kupajua sana,....sizani kuna mtu anaweza kufanya hivyo, utajiumiza bure, kwahiyo...uwezekano wa mtu kupanda ukuta haupo....’akasema.

‘Kwahiyo ina maana gani, kuwa hakuna mtu aliyeingia, au kama kaingia ni lazima kapitia kwa mlinzi, je mlinzi alikuwa wapi, alilala, au alitoka nje kidogo, au, hapo sieleai?’ nikauliza

‘Yule mlinzi ni mjuzi wa kazi yake, huwezi kupita pale bila ya yeye kukuona,na hata kama atapitiwa na usingizi, hisia zake ni kali sana, ni lazima atashituka, ...na asingeliweza kuondoka na kuliacha hilo lindo bila kumuarifu bosi wake ndani...namfahamu sana huyo mlinzi nimefuatilia utendaji wake wa kazi, ...hawezi kufanya uzembe wa namna hiyo...’akasema

‘Kwahiyo unataka kusema nini kuhusu huyo mlinzi?’ nikauliza nikiwa bado nimechanganyikiwa

‘Kuna maelezo kayaficha,na kunifanya nimuhisi huyu mlinzi vibaya, kuwa anahusika kwa namna moja au nyingine kulifanikisha zoezi zima la hicho kilichotokea hapo, japokuwa sina ushahidi wa moja kwa moja, na siwezi kusema yeye ndiye aliyemuua mtoza ushuru...’akasema

‘Una uhakika gani na hilo?’ nikamuuliza na yeye hakutaka kunijibu swali langu moja kwa moja akawa anaendelea kutoa maelezo

‘Kwa vyovyote vile, ni lazima mtu aliyeingia ndani aliwasialiana naye kabla au, hata kaam sio kabla, lakini kuna maongezi yalifanyia hadi kukubaliana, sijui labda ni kwa malipo fulani,au kuna ushirika kati ya mlinzi na mtu mwingine....siwezi kuamini moja kwa moja, kuwa mlinzi aliondoka pale kwa kuhadaiwa,....’akatulia kidogo.

‘Kuhadaiwa kwa vipi?’ nikamuuliza

‘Kuwa alifika mtu akamvunga vunga, na huenda akatokea mtu mwingine akapita kwa siri..hiyo inawezekana sana, lakini kwa jinsi mlinzi alivyofanya, inaonyesha wazi kuna mashikamano, kuna makubaliano, kati ya mlinzi na huyo mtu mwingine....kwani mlinzi aliondoka na kuacha lindo,akaingia ndani, na je alipoingia ndani alifanya nini, ?’ akawa kama anauliza

‘Sijakuelewa, wewe umesema huyo mlinzi hawezi kuacha lindo lake na kuondoka bila kuomba kibali kwa bosi wake, je huo muda alioondoka aliwasiliana na nani, na alimuacha nani lindo?’ nikamuuliza

‘Alipoondoka hapo lindoni, alihakikisha kuwa kuna mtu kamuachia hiyo kazi, , ...’akasema

‘Mbona unaongea kama vile ulikuwepo, alimuachia nani?’ nikamuuliza

‘Huyo mlinzi, alimuacha mtu hilo lindo, baada ya wawili hao kuongea kwa muda mfupi, na huyo mlinzi akaelekea ndani ya jengo, ....’akasema mpelelezi

‘Mhh, hapo sikuelewi, ....kufanya nini, au unazungumzia ule muda mlinzi aliokuja kuniarifu kuwa kuna mgeni kaja?’ nikamuuliza

‘Hayo yalitokea kipindi wewe upo ndani, na huyo marehemu,na ni kama walishafahamu kuwa ndani kuna tatizo, hapo sijapata uthibitisho wa moja kwa moja, bado kuna kitu hakijakaa sawa,...nakueleza haya nikiwa na uhakika nayo...’akasema

‘Una uhakika!...mmh, kwa vipi?’ nikauliza nikionyesha mshangao

‘Ilikuwa hivi,..wakati nyie mpo ndani, alifika mtu kuonana na mlinzi, huyo mtu alivaa kofia pana na miwani, waliongea kidogo na huyo mtu akawa anacheka kuashiria kufurahishwa na jambo, na ilivyoonyesha, mtu huyo anafahamiana na huyo mlinzi...’akatulia kidogo.

‘Kiukweli...waliongea kama marafiki wanaojuana, sasa sina uhakika kama walikuwa wanajuana kabla au ni ujanja wa huyo mtu,hapo sijawa na uhakika wa moja kwa moja, lakini kwa mtizamo wa haraka huyo mtu anafahamiana na na huyo mlinzi, kwani alivyofika na kuongea na yule mlinzi,walikubaliana kwa haraka sana...’akatulia

‘Kwahiyo, ninaweza kusema kuna kitu kati ya huyo mtu na huyo mlinzi, na mlinzi hakulisema hilo na hataki kusema hivyo, wao walipomaliza kuongea tu yule mlinzi akaondoka kwenye lindo lake na kuelekea ndani, nafikiri alitumwa kitu fulani na huyo mtu ...’akasema

‘Alitumwa kitu, kitu gani...?’ nikauliza

‘Huenda ndio hicho hicho alichokuwa akikitafuta marehemu, huenda kuna kitu kingine, hapo hakujafahamika vyema...’akasema

‘Sasa, hebu ...sijaelewa hapo, huyo mtu aliyefika na kuongea na mlinzi ni mtu gani,mbona humuelezi , ina maana huyo mtu hafahamiki, na ooh, ina maana hayo yote uliyapatia kutoka kwa nani, ni mlinzi, alikuelezea au...?’ nikauliza

‘Ninachotaka uelewe hapa ni kuwa huyu mlinzi ana mafungamano na huyo mtu, na nahisi wanajuana kabla, ndio maana alipofika tu, na kutoa maagizo huyo mlinzi hakupinga, akaondoka na kuingia na ndani, sasa yaliyotokea huko ndani ndio sina uhakika nayo...’akasema

‘Mlinzi...hakukuelezea, mbona mimi sikumuona...hapana sizani kama ni kweli....’nikasema

‘Kama sikweli, ni nani alikupiga na nyundo kichwani...ni lazima kuna mtua liingia, akaweza kufanya hayo...hebu fungua akili yako vyema....’akasema huyo mpelelezi.

‘Mimi ninachotaka kufahamu kwanza, ni jinsi gani ulivyoyafahamu hayo, ni mlinzi alikuelezea hivyo?’ nikamuuliza, na huyo mpelelezi bila kujibu swali langu moja kwa moja akaendelea kuongea;

‘Ninachotaka kufahamu zaidi, ni jinsi gani huyu mlinzi alivyomfahamu mdada,...hapo kuna kitu kingine muhimu sana,... kwani hajafanya kazi kwa huyo binti kwa muda mrefu wa kumfahamu mdada kihivyo, unaona hapo....,lakini inavyoonyesha, ni kuwa alikuwa anafahamu matatizo ya mdada, na jinsi gani ya kupambana naye, ndio yeye ni askari ana mbinu nyingi, lakini sio kwa jinsi ilivyotokea, hapo nahitajia kupaangalia...’akatulia

‘Bado mimi hapo sijakuelewa, kama mlinzi aliweza kukuelezea yote hayo, jinsi alivyoweza kuacha lindo la kuelekea ndani kutokana na maagizo ya huyo mtu usiyetaka kumtaja ni nani, basi angeliweza kukuelezea jinsi alivyomfahamu mdada, au sio?’ nikauliza.

‘Nimeshakuambia kuwa mlinzi ameweza kuongea , lakini kuna mambo anayaficha, hataki kuyaweka wazi, na ni kutokana na jinsi alivyoshibana na huyo mtu wake...nimeongea naye mara kadhaa na hata kutoa shinikizo la kumtisha, lakini hakuweza kunifafanulia zaidi,inaonyesha kuwa hapo alipokuwa kwa mdada, pia alikuwa kazini kwa ajili ya mtu fulani,....’akatulia

‘Kwa maelezo yako, ina maana huyo mlinzi anaweza kuhusika na mauaji ya mtoza ushuru?’ niamuuliza

‘Kwa maelezo yake binafsi,hahusiki, .....’akasema

‘Umemwamini ?’ nikamuuliza

‘Siwezi kumwamini moja kwa moja, ndio maana nataka ushirikiano wako, ...nikiweza kujua ukweli wa kilichotokea ndani, ninaweza kupata uhalisia wa tukio zima, na itaniwezesha mimi kuweza kukusanya ushahidi zaidi na kuimaliza hii kesi haraka iwezekanavyo....japokuwa  kwa hali ilivyo itakuwa vigumu sana kumshawishi hakimu.....’akasema

‘Mhh, hebu niambie ukweli, ...ni mlinzi aliyeweza kukuelezea yote hayo, na kwanini polisi hawajamkamata, ?’ nikauliza

‘Polisi wana namna yao ya utendaji wa kazi, kwa hivi sasa, kama nilivyokuelezea, wanafanya kutokana na maagizo waliyopewa, hata hivyo, huwezi kujua, ....huenda wanavuta muda, kuchukua hatua fulani, mimi nafanya kazi kwa namna yangu, siingiliani na hao watu....’akaangalia saa yake.

‘Hebu niambie mlinzi alivyokuelezea, kwa jinsi alivyoweza kushawishiwa na huyo mtu akaacha lindo na kuingia ndani kupambana na mdada,...?’ nikamuuliza

‘Elewa hivyo, mlinzi aliongea na huyo mtu akapewa maagizo, na mlinzi bila kupoteza muda, akaondoka na kuingia ndani, hakuingia ndani moja kwa moja, alikuwa akiangalia mara kwa mara kupitia dirishani, kuona ni kitu gani kinaendelea huko ndani, na alipoona kuna nafasi ya kufanya hivyo, akaingia ndani....’akatulia na kuniangalia

‘Ndio maana nakuambia kuwa huyu mlinzi alishamfahamu mdada, na alishajua ni wakati gani wa kuweza kupambana naye, ..ni mahesabu ya hali ya juu yaliyotumika...’akasema

‘Mimi ningelimuona huyo mlinzi akiingia, sizani, kama aliingia, na alipitia wapi....’nikasema

‘Kitu alichotumia kama silaha ni nyundo tu,...ile nyundo hata polisi hawakufanikiwa kuipata, kwani baada ya hilo tukio, ilipotea kabisa...., lakini hiyo nyundo ilikuwa ndani ya gari, na yeye ni kama alifahamu kuwa kuna kitu kama hicho kwenye hilo gari,....’akasema

‘Ina maana huyo mlinzi likwenda sehemu ya kuegesha gari, na akaweza kuiona hiyo nyundo, ni kutoka kwenye gari la nani?’ nikauliza maana siku hiyo ya tukio kulikuwa na magari mawili, moja la mdada, na jingine la marehemu.

‘Nyundo hiyo ilipatikana kutoka kwenye gari la mdada....’akasema

‘Oh, mbona sielewi....’nikasema

NB: Hata mimi sielewi,...ngoja tuone sehemu ijayo,...

WAO LA LEO: Ili kuwa na yakini na jambo lolote, ni muhimu kufanya utafiti kabla hujahitimisha kauli yako. Watu wengi wanaona kuwa, kuongea  vyema, kutoa propaganda, kushawishi hata kama ni ubishani ni namna ya kuonyesha kuwa unafahamu jambo,  hata kama halina ukweli, halina uhakika,lakini kwa vile lengo ni kufanikisha jambo kwa masilahi, basi upo tayari kutumia mdomo kushawishi watu wakubaliane nalo. Tusifanya hivyo, kwani hatima ya uongo ni kuja kuumbuka tu. 

1 comment :

Anonymous said...

Bravooh, i salute u friendo, kazi nzuri, ubarikiwe sana, tena sana