Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Wednesday, November 27, 2013

Mkuki ni kwa Nguruwe-36


Nilishaanza kumshuku shemeji yangu kuwa anafahamu mengi, na siku ya leo niliona ndio siku pekee ninayoweza kumbana , na kusema ukweli wote, lakini sikutaka niongee naye peke yangu, nilishaongea na watu wa usalama, ambao nafahamiana nao,na niishawaeleza ni nini lengo langu, na nikaona niwaite watu waja wanisaidie, ...

Kwa hatu iliyofika, huruma ilikuwa haipo tena, nilishaona kuwa hawa watu nikawahurumia, wataniumiza, wao hawanijali tena, wanachojali ni masilahi yao ....ndio maana nikaamua kuwaita watu wa usalama.

Wakati nampigia simu, niliona kama shemeji yangu alitaka kuniambia jambo, kuwa yupo tayari kuniambia kila kitu, lakini nilishamfahamu kuwa anaweza akapoteza muda tu na asiniambie kitu, na hata kile nilichotaka kukipata nisikipate, na wakati huo nilishamuweka huyo askari kanzu hewani, sikutaka kurudi nyuma, nikamwambia aje...

Endelea na kisa chetu



WAZO LA LEO: Katika maisha yako jifunze kuwa mkweli, na jitahidi usimamie kwenye haki, hiyo itakuwa kinga yako kwa hali yoyote ile. Uwongo, hadaa, mwisho wake ni kuzalilika tu.

Ni mimi: emu-three

No comments :