Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Saturday, November 9, 2013

Mkuki ni kwa Nguruwe-24


‘Nahisi rafiki yangu atakuwa mikononi mwa huyo wakili, kwani aliniambia mtoto wake, alitekwa nyara na watu wasiojulikana, na baadaye akapigiwa simu, kuwa ili ampate mtoto wake inabidi kusaini mkataba walioandaa hawo watu...

‘Kwasababu ya mtoto wangu sikuwa na hiari, nilikubali kusaini huo mkataba..’ hata mimi kama mzazi ningefanya hivyo, nikajisemea kimoyo moyo.

Ina maana huyo rafiki yangu, akasaini huo mkataba, na huyo rafiki yangu alikuja kugundua kuwa mkataba huo hakuwa na madhara sana kwake, zaidi ni dhuluma kwa watu wengine, ...lakini hakuwa hiari, akakubali, akasaini, na alitarajia kumpata mtoto wake...hakusema kuwa alimpata au la,na nafikiri hawo watu wamemzunguka, au...’ndivyo nilivyomwambia rafiki wa mume wangu, na huku nikiwaza mengine,

Kama kwaida ya rafiki wa mume, wangu, kupinga kila kitu, akawa ananiuliza maswali mengi,ambayo sikuwa na majibu nayo....kwani wakiti huo akili yangu ilishakuwa na mawazo mengine.

Wakati huo akili yangu ilishaona kuwa rafiki yangu huko alipo yupo matatani,hasa baada ya huyu rafiki wa mume wangu kuniambia kuwa Makabrsha ana ofisi huko uwanja wa ndege, na pia rafiki yangu aliniambia kuwa yupo huko uwanja wa ndege, na wakati anataka kunielezea zaidi simu yake ilikatika, mkatiko ambao uliashiria kuwa huko hakuna mema.

Kwangu mimi moyoni, nilihisi hawo watu waliomteka mtoto wake, wamemgeuka, na lolote linaweza kutokea, na mimi kama rafiki yake, ilibidi niende nikamsaidie, hata kama kuna hizo tetesi ambazo zinanichanganya, na mpaka sasa akili yangu ilikuwa hajaamini...

‘Ni lazima nifanye lolote, japokuwa nilikuwa nimechelewa....

Endelea na kisa chetu.....

********



WAO LA LEO:Kila kazi ina ujuzi wake na taratibu zake, ndio maana watu wanakwenda kuzisomea hizo kazi, tusijifanye kuwa tunafahamu kila kitu, eti kwa vile ulipitia pitia shuleni, kuna vitabu umesomasoma , hiyo peke yake haitoshi ...ndio maana kuna taaluma tofautitofauti, na kila taaluma, ina mabingwa, ina wataalamu wake, ina watu wanapewa madaraja na nyazifa mbalimbali, kuonyesha kuwa hizo ni fani zinazojitegemea, tusipende kujiingiza kwenye kazi za watu ambazo huenda ni za kitaalamu zaidi, na kujifanya tunaufahamu nazo, ilihali hatujazisomea, tujue kuwa  kuongea na kutenda ni vitu viwili tofauti,..tuweni makini na fani za watu.

Ni mimi: emu-three

2 comments :

Pam said...

Shukrani m3..

emuthree said...

Pam shukurani na ww pia kwa kuwa pamoja nami na wengine wote. TUPO PAMOJA