Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Tuesday, October 22, 2013

Mkuki ni kwa Nguruwe-14


 Moyoni nikawa kama nawashwa washwa, nataka kujikuna , hasira na msongo wa mawazo vikanijaa sikuweza kuvumilia, nikasema kimoyomoyo,kwanini niteseke wakati muhusika yupo, na muhusika si mwingine ni mume wangu, ....nikaamua kwenda kukabiliana naye.

‘....Ila kumbuka usimuulize maswali mengi ya kumuumiza kichwa...’sauti ya docta ikawa ananireja kichwani, lakini hapo hapo sauti nyingine ikawa inasema;

‘Huenda hayo yanayomtokea mume wako yanahusiana na hilo, ....’

‘Yanahusiana na nini,....?’

‘Ina maana mume wangu kanisaliti, ina maana ata hiyo ajali imetokana na huo uzembe, na hiyo dhambi, ambayo tuliahidiana isije ikatendeka kwenye ndoa yetu...haiwezekani, ..sio mume wangu huyo ninayemjua, hapo ni lazima kuna kitu...’nikajiulizana kugeuka kumwangalia docta ambaye alikuwa kashikilia simu akiongea na watu wake, na ilionyesha kuwa hana habari na mimi kwa muda huo nay eye ndiye agenisaidia kujibu baadhi ya hayo maswali, nikasema kimoyo moyo;

‘Kwanini niume kichwa wakati muhusika mkuu yupo....’nikageuka tena kumwangalia huyo rafiki wa mume wangu ambaye aligeuka kidogo kuniangalia akaonyesha ishara ya dakika tano...ina maana nimsubiri, ....kwa dakika tano, haiwezekani...

‘Hilo siwezi kuvumilia tena ni lazima nikamuulize muhisika mwenyewe...’nikasema na kumbe docta alinisikia, akageuka kuniangalia kwa mashaka, na mimi moyoni nikaendelea kuwaza kuhusu uamuaiz wangu huo, na kusema kimoyo moyo;

‘Hata kama ni kuvunja miiko ya docta...kwani wao ni nani, ....kwani nikimuuliza ndio itakuwaje, atashindwa kujibu, ataathirika, kwa nini aathirike wakati ni dhambi zake mwenyewe..’nikawaza na kujikuta nikiongea tena kwa sauti;

‘Sitaweza kuvumilia hili ni lazima nikamuulize..’ nikasema kwa sauti kubwa, na hapo rafiki wa mume wangu akanigeukia, na kunitizama kwa macho ya mshangao, na mimi sikumjali nikaharakisha kwenda huko kwa mgonjwa, na yeye akawa ananifuatilia kwa nyuma huku akiendelea kuongea na simu, laini nilikuwa nimemuacha umbali kidogo, ...

Nilipofikakwenye  mlango wa kuingia kwenye chumba hicho alicholazwa mgonjwa, niligeuka nyuma, kumwangalia huyo rafiki wa mume wangu, ambaye nilimuona akija nyuma yangu kwa haraka, alionekana kama anaharakisha kunikimbilia ili kunizuia nisiingie, ...na nilipogauke kumwangalia akawa ananonyoshea kwa ishara ya mikono kuwa nisubiri kwanza, na wakati huo hataki kuachia simu, ikiwa karibu na mdomo,inaonyesha alikuwa akiongea jambo muhimu na huyo anayeonega naye, na hakutaka kulikatiza...

Mimi...sikumsubiria nikafungua mlango na kuingia ndani kukabiliana na mume wangu...

Endelea na kisa chetu......

**********


Ni mimi: emu-three

3 comments :

Unknown said...

Endeleaaa ndugu wa mm story nzuri Sana.

Unknown said...

Endeleaaa ndugu wa mm story nzuri Sana.

Unknown said...

Endelea ndugu story nzuri sn.