Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Tuesday, July 23, 2013

WEMA HAUOZI-39





Upande wa mshitakiwa mkuu, hali haikuwa shwari, kwani mshitakiwa huyo kabla hajatulia kwa mshituko wa mwanzo wa kuitwa shahidi ambaye kwa mtizamo wake, huyu mtu alikuwa keshafariki, na sio yeye tu, watu wengi wanaomfahamu huyo mtu, walikuwa wakijua ni marehemu. Sasa kuonekana kwake hapo, kulimfanya mshitakiwa mkuu akose amani, japokuwa wakili wake alimthibitishie kuwa atamsambaratisha huyu shahidi kama alivyokuwa akiwafanyia mashahidi wote waliotangulia.

Kabla mshituko huo haujatulia, ukaongezeka mshituko mwingine, wa kutokea kwa  mwanadada, ambaye alijua kabisa hataweza kuwepo . Akamgeukiwa wakili wake, kama anataka kumuuliza, lakini alimkuta wakili wake naye akiwa katika mshangao, na mshituko…na wakili wake, alipogundua hilo akajifanya kama hakuna lolote kwake,  tambo zake zilikuwa pale pale, na hata pale aliposikia mteja wake akisema;

‘Oh, huyu mtu kapona..mbona sielewi…nakumbuka ulisema….’akasema huyo mshitakiwa na wakili wake akajifanya kutabsamu kwa dharau, na kusema.

‘Mmmh, naona kapona, au sijui…lakini usitie shaka nipatambana naye, leo nitakuwa na furaha ya kupambana na huyu mwanadada, maana nilikuwa nikimsikia tu, sijawahi kukutana naye kwenye kesi….’akasema wakili huyu huku akimtizama huyo wakili mwanadada kwa macho ya hamasa.

Kwa muda huo, wakili mwanadada alikuwa akitembea kuelekea  sehemu yake, ambapo kundi la mmawakili au waendesha amshitaka walikuwa wamekaa, akapita hadi sehemu yake na kukaa, na alipotulia na kuweka vitu vyake sawa akamgeukia muedesha mashitakai mwenzake aliyekuwa akiongoza hiyo kesi wakateta kidogo.

Baadaye akageuka upande ule wa washitakiwa na macho yake yakagongana moja kwa moja na mshitakiwa mkuu, na wakili mwanadada, akatikisa kichwa kama anakubali jambo, na mjumbe,ambaye alikuwa bado kajawa na uso wa mshangao na mshtuko, akamgeukiwa wakili wake, na kusema;

‘Sasa uwe makini, ….huyu mwanadada ni mwerevu sana,…nataka leo tuwahakikishie kuwa huyu dada si chochote, fanya ufanyalo, …pambana naye, najua unajua ni nini cha kufanya…..’akasema huyo mshitakiwa mkuu, na  kukatizwa na sauti ya waendesha mashitaa.

‘Ndugu muheshimiwa hakimu, kwa vile mwenzangu ameshafika, na tulikuwa tumempanga yeye kama kiongozi wa leo, nitampisha yeye aendelee na kesi yetu,…’akasema na hakimu akatikisa kichwa kwani mwanzo aliwahi kuuliza yupo wapi wakili ambaye aliandikwa kuwa ndiye ataongoza hiyo kesi , akajibiwa kuwa yupo  anakuja..

Kwa kipindi kile, alipokuwa akiuliza muheshimiwa hakimu, kuwaauliza kambo hiyo ya waongoza mashitaka, wengi walikuwa hawakufahamu hakimu alikuwa na maana gani, kwa kwa taarifa za mitaani za uvumi, zilizokuja kuenezwa siku hiyo, ni kuwa wakili mwanadada, hali yake sio nzuri, anahitajika kusafirishwa nje kwa ajili ya upasuaji wa ubongo, kwani ile ajali ilimuathiri kwenye kichwa…ndio maana haajonekana na hataonekana tena kwenye kesi hiyo.

Wakili mwanadada akasogea na kumwangalia huyo kijana na kumpa moyo, halafu akageuka kuangalia kambi ya utetezi, na macho yake yakatua kwa mshitakiwa mkuu, akamkazi a macho mshitakiwa huyo kama vile anamsoma kwenye mawazo yake, halafu akageuka kumwangalia wakili, akatabasamu, lakini wakili yule wa kambi ya utetezi, alikuwa kakunja uso, ….hakujibu lile tabasamu, bali,alibenua mdomo kidogo kuashiria dharau

‘Kijana, ….tuambie, wewe ulikuwa unafanya kazi gani kwenye kijiji?’ akaulizwa.

‘Kazi yangu kubwa ilikuwa ni ulinzi shirikishi…’akasema.

‘Ni nani aliyekuwa akiwasimamia kwenye kazi yenu hiyo?’ akaulizwa.

‘Ni Jemedairi, ambaye sasa ni marahemu…’akasema.

‘Jemedari alikuwa na mamlaka gani kwenye kijiji…?’ akaulizwa.

‘Yeye alikuwa kiongozi wa walinzi shirikishi,..’akasema.

‘Kwahiyo yeye aliteuliwa tu kama kiongozi, ila kuna mkubwa zaidi yake, au sio?’ akaulizwa.

‘Mhh, tunaweza kusema, hivyo, maana kwenye kijijini kuna makundi mbali mbali ya kufanya shuguli mbali mbali, a kila kundi kunateuliwa kiongozi wake, kwahiyo wenye kundi letu la ulinzi shirikishi , Jemedari ndiye aliyekuwa kiongozi wetu.

‘Hiki kikundi cha walinzi shirikishi kwanini kilianzishwa?’ akaulizwa.

‘Ni baada ya kuona kuwa kuna matukio mengi ya uhalifu, basi likatokea pendekezo kuwa kuwe na kundi kama hilo….’akasema.

‘Kwahiyo kundi hili, lilianzishwa na huyu jemedari, au jemdari alichaguliwa kama mkuu wa hilo kundi?’ akaulizwa.

‘Jemedari alichagulia kama mkuu wa hilo kundi, …..labda nikuelezee zaidi ni kuwa kijiji kina mkuu wake ambaye ni mjumbe, na huyo mjumbe ana halimashauri zake, au makundi mbali mbali ya utekelezaji, na halimashauri hizo zina viongozi ambao hupokea amri kutoka mjumbe..’akasema.

‘Kwahiyo mjume ndiye kiongozi wa juu wa hilo kundi na ndiye mwenye mamlaka ya mwisho ya kijijini au sio?’ akaulizwa

‘Ndiyo…’akasema.

‘Kwahiyo mjumbe alikuwa na mamlaka ya kuliamrisha hilo kundi, hata kama kiongozi wake hayupo?’ akaulizwa

‘Ndiyo…’akasema

‘Sasa turudi nyumba kidogo, katika maelezo yako ulisema wewe umewahi kulitumikia hilo kundi lenu la ulinzi shirikishi,toka lilipoanzishwa na ulikuwa mdogo kuliko wote, na karibu kila kazi uliwahi kuhudhuria, je unaweza kutkumbusha kidogo, ni kazi ipi ambayo ulihudhuria, ambayo kiongozi wenu wa kundi hakuwepo, na akawa msimamizi ni mjumbe….? akaulizwa.

‘Mbona zipo nyingi sana….mojawapo ilikuwa ya kwenda kwenye nyumba ya mwanamama, na kumtoa kwa nguvu, baba wa kufikia wa mwanamama huyo…..’akasema.

‘Ni nani huyo mwanamama..?’ akaulizwa.

‘Ni yule Mwanamama, ambaye ambaye alifungua kesi ya kuwa kadhukumiwa mali yake…’akasema.

‘Kwanini mliambiwa muende kumtoa?’ akaulizwa.

‘Tuliambiwa alikiuka amri iliyomtaka atoke na kuicha hiyo nyumba ili iwe mikonono mwa wahusika…..’akasema.

‘Je ni nini kilitokea?’ akaulizwa.

‘Tuliambiwa tutumie nguvu kumtoa, maana alikaid amri halali ya mkuu wakijiji…’akasema.

‘Mliambiwa mtumie nguvu gani?’ akaulizwa.

‘Tuliambiwa tumfunze adabu….na tukiambiwa hivyo, sisi wenyewe tunajua ni nini la kufanya, …’akasema.

‘Ni nini la kufanya , una maana gani kusema hivyo?’ akaulizwa.

‘Tulishawahi kufanya kazi kama hizo, na mkuu huyo alishatuambia kuwa akisema kufunza adabu mtu mnahakikisha huyu mtu hawezi hata kutembea….’akasema.

‘Kwanini kiongozi mkuu wa kijiji alifikia kusema hivyo, ina maana hamkuwa na tabia hiyo ya kufunza adabu kabla, mpaka ikafika wakati  kiongozi huyo mkubwa wa kijiji  kuwalaumu,…..?’ akaulizwa.

‘Kwakweli tukiwa na kiongozi wa kundi, Jemedari, huwa yeye hakubali kabisa mtu yoyote kupigwa, hasa kumtoa mtu damu, hapendi kabisa, japokuwa yeye mwenyewe ana ahsira sana…’akasema

‘Je kwanini siku hiyo mliyokwenda kumtoa huyo mzee kwa nguvu,hamkuandamana na Jemedari? Akaulizwa.

‘Nakumbuka ni kipindi ambacho Jemedari alikuwa amefiwa na mdogo wake,….yeye alikuwa kwenye msiba….’akasema.

‘Kwahiyo mlipoambiwa mmfunze adabu huyo mzee, mlijua ni nini cha kufanya,kama alivyowahi kuwaambia mfanye kama anavyotaka yeye huyo kiongozi wa kijiji …?’akaulizwa na hapo mshitakiwa akamgeukia wakili wake na kusema;

‘Mbona huweki pingamizi huoni ….’akalalamika na wakili yake akaweka pingamzi lakini hakimu akataka swhali hilo lijibiwe.

‘Unaona,..mimi najua ni swali gani linahitajika kuwekewa pingamizi , huyo mwanadada ni mjanja sana haulizi swali tu kwa nia ya kuuliza, anajua ni nini anachokifanya, lakini hata hivyo mimi ninajua zadi yake, subiri muda wangu ukifika uone ni nini nitakachokifanya….’akasema huyo wakili.

‘Ndio tulijua ana maana gani, na tukafanya kama alivyotarajia..’akasema.

‘Kwahiyo mkafanya nini…?’ akauliza na wakili mwanadada alikuwa kama anaista akijua huenda swali hilo lingeliwekewa pingamizi lakini haikutokea hivyo, akamsikiliza shahidi akiongea

‘Ndio hivyo….tulianza kumvunja nguvu za miguu, kwa kumpiga na virungu, na wengine wakimchapa vibogo, na hata kumpiga virungu mabegani, na kwa vile huyo mzee, alianza kupambana na sisi, ilibidi tutumie nguvu ya ziada, na kwakweli wengi walimpiga mzee huyo bila huruma, mimi sikukubaliana na hilo, na hata ukimuuliza mwenyewe mzee, atakuhakikishia kuwa mimi nilikuwa nikiwazuia wenzangu wasizidishe …kipigo…’akasema huku akitupa jicho kuangalia kule alipokaa huyo mzee.

‘Ina maana nyie kundi la watu….mlikuwa wangapi?’ akaulizwa.

‘Tulikuwa watano…vijana mashababi…’akasema huyo shahidi na watu wakaguna kwa huruma.

‘Vijana watano wenye nguvu mkaanza kumpiga huyo mzee, bila huruma..na nini kilitokea baada ya hapo, ….?’ Akaulizwa.

‘Kwa vile mzee huyo alikuwa sio lele mama, ilichukua muda, na tukamzidi nguvu, na alipozidiwa nguvu wenzangu ambao labda waliumizwa, walichukua nafasi hiyo kulipiza kisasi,wakawa wanapiga kama wanataka kuua…’akasema.

‘Una uhakika kupiga huko, sio kwa jinsi alivyoagiza huyo kiongozi…?’ akauliza na wakili mtetezi akaweka pingamizi na hakimu akakubali hilo pingamizi.

‘Sawa je kuna kazi gani, zaidi ya hiyo ambayo mkuu wa kijiji, alishiriki yeye mwenyewe…kwa kuwatuma,bila ya kushirikishwa huyo kiongozi wetu, wa karibu?’ akaulizwa.

‘Kuna kazi maalumu, tulipewa na vijana wenzangu, hiyo ilikuwa kazi ya siri, hata mimi mwenyewe sikujua ni kazi gani, hadi tulipofika kwenye eneo,…’akasema.

‘Ulipofika kwenye eneo uliambiwa ni kazi gani?’ akaulizwa.

‘Mimi nilichoambiwa ni kumwangaia mafuta nyumba yam zee wa kijiji, huyo baba wa kufikia wa Mwanamama, na nilipouliza ni kwanini, nikaambiwa nifanye nilivyoagizwa, na nikimaliza niondoke….’akasema.
‘Je ulifanya hivyo, kama livyoagizwa?’ akaulizwa.

‘Ndio, maana moja ya mafunzo yetu, tuliyopewa ni kuwa ukiamrishwa na kiongozi, hutakiwi kukataa, amri moja, piga, au fanya, unafanya kama ulivyoamrishwa, ukisita, wewe utapigwa, au hata kuuwawa..kwani hiyo ni amri kama mpo vitani….’akasema.

‘Ina maana mlikuwa mkipitia mafunzo ya jinsi gani ya kufanya kwenye kazi zenu?’ akaulizwa.

‘Kila mara tunakuwa na mafuzo, na kuna mafunzo ama hayo, ya jinsi gani ya kupambana na mhalifu…’akasema.

‘Ukisema kama haya, ina maana hata hayo ya kumpiga huyo mzee, na kuchoma nyumba yalikuwa moja ya mafunzo yenu…’hapo pingamizi likawekwa..na hakimu akakubali

‘Kwahiyo ukagundua ni kazi gani mliyotakiwa kufanya siku ile?’ akaulizwa.

‘Ndio nikagundua, ….’akasema.

‘Kwahiyo unaweza kuiambia mahakama hii ni kazi gani hiyo ambayo kikosi chenu kilitumwa kuifanya, ..?’ akaulizwa, na pingamizi likawekwa na hapo hakimu akasita kidogo, na baadaye akasema pingamizi limakataliwa shahidi ajibu swali.

‘Ni kazi ya kwenda kuchoma nyumba ya….’kabla mshitakiwa akasema kwa sauti;

‘Mwongo huyo….’akasema na watu wakashikwa na mshangao, na hakimu akagonga rungu yake kwenye meza na kusema ;

‘Futateni taratibu za mahakama, na wewe wakili wa utetezi mzuie mtu wako asivunje taratibu za mahakama…’

Na wakili wa utetezi akaomba msamaha, na kusema kosa hilo halitarejewa tena halafu akamgeukiwa mteja wake, na kumnong’onezea kitu, lakini mteja wake, akaonekana kukasirika, na ilionyesha kama vile hana amani tena na huyo wakili wake

NB: Je ni nini kitafuata..

WAZO LA HEKIMA: dhuluma na ukatili, hauna heri, na mtendaji wa mambo hayo, hana amani , na kila mara hujishuku au kuwashuku wenzake vibaya. Kwanini uwe na maisha yasiyo na amani, kwanini ujitese kwa kutenda dhuluma wakati unafahamu athahri zake,…kumbuka kuwa dhuluma katu haina mwisho mwem
Ni mimi: emu-three

2 comments :

Yasinta Ngonyani said...

Hakika hapa ni bonge la shule kila uingiapo hapa ni kukusanya elimu tu. Pia wazo la leo ni funzo zuri sana...PAMOJA DAIMA.

Unknown said...

Mmmh, haya ndugu wa mm,