Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Wednesday, June 26, 2013

WEMA HAUOZI-25


 Wakati nipo nyumbani nimejipumzisha , tukisubiria siku ya hukumu, mara akaja mwanasheria wa hiyo familia ya marehemu mume wangu, alifika akiwa mnyonge na alionekana mwingi wa huzuni, na alipofika alinisalimia kwa upole na adabu, nikamkaribisha kiti kukaa, na hakufanya hiyana akakaa kwenye sofa na kutulia kidogo. 

Akawa anamwangaia mtoto wangu akiwa anacheza sakafuni, …nikamwambia mtoto akacheze nje, nikijua haya mazungumzo aliyokuja nayo huyu jamaa yanaweza yasimstahii mtoto kusikia.

‘Mtoto anakuwa haraka, natamani ningekuwa na mtoto…’akasema,

‘Muda muafaak utafika utakuwa naye, kwani wewe na mchumba wako hamjaafikiana lolote?’ nikamuuliza nikimwangalia kwa macho ya huruma.

‘Baada ya ile kesi, aliondoka, …unajua hakufika hata kuniaga,….’akasema

‘Lakini alisema ana haraka, ….kuna kesi aikuwa akiifuatilia…’nikasema

‘Najua aliona kuwa akifika nyumbani kwetu, na wakati kaka yangu keshakasirika, hakutakuwa na amani, nahisi keshanitoa kwenye moyo wake..’akasema.

‘Hiyo sio kweli, mwanadada anakupenda sana,….wewe tu hujajituliza kwake, …’nikasema.

‘Ttaizo kupenda kwake ni kwa masharti, na mimi nijuavyo, ukipenda hata chongo utaliita kengeza, huangalii lolote zaidi ya kupenda, sasa yeye keshaona mambo ambayo yamemkwaza, na sijui kama atakubaliana tena na uchumba wetu…’akasema.

‘Masharti ni kawaida kwenye mahusiano, na hayavunji upendo, cha muhimu ni kukaa pamoja na kuyaangalia hayo masharti , na kama kweli mnapendana mtakubaliana, …sioni kama kuna shida, …’nikasema.

‘Unajua shemeji, pamoja na hayo, hata mimi moyo wangu unaanza kuingia doa, na…na…..’akasita kuongea.

‘Kwanini uingie doa,…kwani wewe humpendi?’ nikamuuliza.

‘Nampenda…ni mtu tuliyezoeana, na kiukweli tumetoka naye mbali, lakini bado nina majukumu,…na kiukweli, najikuta kwenye njia panda,….pamoja na majukumu hayo, pia hata moyo wangu unahisi kupenda….’akasema.

‘Majukumu gani hayo shemu?’ nikamuuliza nikianza kuhisi jambo.

‘Shemeji nilishakuambai toka awali, kuwa pamoja na kuwa kaka yangu, aliniachia wewe nikutunze na mtoto, lakini  pia moyo wangu ulishakupenda…yaani hiyo ni kweli kabisa….sizungumzi I kwa ajili ya haya majukumu, nazungumiza kutoka ndani ya moyo wangu,….shemeji nakuomba tafadhali kubali nichukue nafasii ya kaka yangu….’akasema na mimi hapo nikakunja uso, nilitamani nimfukuze, lakini nikaona nitumie busara.

‘Shameji yangu huko sio kupenda, huko ni kutamani, wewe ulishapenda mtu, hadi kufikia kufunga uchumba,…na kama ulivyosema mumetoka mbali na mchumba wako, …jiweke wewe kwenye nafasi yake, ungelijiskiaje kama ungelifanyiwa hayo unayotaka kumfanyia…shemeji kumbuka mlipotoka, rejesha moyo wako nyuma, nina imani kuwa mtaendeleza upendo wenu…’nikamwambia.

‘Kwani shemeji, hata kama nikumuoa yeye, na wewe ukawa mke wangu wa pili kuna ubaya gani?’ akauliza.

‘Kwa mila zetuu hakuna ubaya…lakini kwa hali halisi , hasa ukizingatia maamuzi yangu mimi mwenyewe hilo halitawezekana, hata kama ingelikuwa huan mchumba mwingine, kwangu mimi nimeshaamua, kuishi kivyangu…..mwenzangu ameondoka, na sitaki kumsaliti….’nikasema.

‘Hapo una kufuru, ndoa inakufa pale mmoja anaptangulia ahera, hayo ni mapenzi ya mungu, na hatuwezi kuyakana, na ukisema hivyo kuwa hutaki kuolewa tena, ina maana unapinga mapenz I ya mungu…maisha ndivyo yalivyo,….’akasema.

‘Hilo nalifahamu kabisa,..kuwa hayo ni mapenzi ya mungu, kuwa mpende umpendaye ipo siku mtatengana naye, ..na kweli tumeshatengana naye, sina jinsi ya kumrejesha,…..hata hivyo, mimi sijatulia, na uamuzi wangu ni huo huo…..ninaona kuwa nitaweza kuishi bila kuwa na mume….huo ndio uamuzi wangu, ilimradi nisivuke mipaka…’nikasema.

‘Shemu kibiandamu, hilo haliwezekani, hutaweza kukaa peke yako usiingiwe na vishawishi….na kwanini ukufuru…ni lazima uwe na mwenzako, kwanza mtoto atajihis mpweke, hana baba…hulioni hilo?’ akauliza.

‘Mtoto ataelewa, na keshaanza kuelewa, hilo nitalifanyia kazi, ninachohitajia ni kumjenga kimaadili, na kumjenga apende kazai kama babu na bibi yake, maisha niliyolelewa mimi ya kupenda kazi kujituma na kutokupenda kutegea, ndiyo nitakayomfundisha mwanangu,…na elimu, itakuwa ndio taa ya maisha yake, hatapata shida…’nikasema.

‘Nakuomba sana shemeji, ….jana tu nimeota, marehemu akinikumbusha ahadi yetu, kuwa sitakuacha uteseke,..sitamuacha mtoto ateseke…sasa nifanyeje…shemeji naomba usinitese, nasema tena, mimi nafanya haya kwa vile nakupenda, sio kwa…vile….’mara simu yangu ikaita…

‘Unaona mchumba wako huyu ananipigia…..samahani nakwenda kuipokea, maana sijui ananipigia kwa maswala gani, na huenda asingelipenda asikie tunachokizungumza…..’nikasema.

‘Sawa …mimi ngoja nikacheze nje na mtoto, mkimaliza kuongea utaniita…’akasema na kutoka nje

********

Nilipomaliza kuongea na wakili mwanadada, nikatoka nje na kumkuta shemeji yangu akicheza na mtoto, kwakweli ilionekana wameivana, na nilipokuwa namuangalia kumbukumbu za mume wangu zikatanda kichwani, ….hawakuwa na tofauti sana, sura maumbile…..kasoro tabia kidogo, kwa vile huyu ni msomi, na marehemu mume wangu aliishia kidato cha nne, akawa hakufauu , kwenda mbele, kuna mambo wanatofautiana sana…

Hapo niliposimama nilihisi machozi yakinitoka, nikiwa, hali ya kibinadamu, huwezi kuamini, unaona kama jana tu, nilikuwa na mume wangu, tunapendana, na tulikuwa na mipango mingi ya pamoja, lakini leo nipo peke yangu, mjane, na mtoto…..oh, yote ni mapenzi ya mungu, lakini kwa ujumla inauma sana,…usiombe kufiwa na mume…

'Shemeji, mtoto ananiuliza lini nitakuja niishi hapa na yeye….’akasema.

‘Usianze hayo tena..nafikiri umenielewa,....na usimtumie mtoto kama kisingizio,ninachokuomba kwako wewe ni kujitahidi sana kuongea na mchumba wako,...mimi nimechunguza sana, jinsi gani anavyokuangalia, anavyoongea akizungumza kuhusu wewe, kwa ujumla anakupenda sana…’nikasema.

‘Ina maana mnaongea kuhusu mimi, mnapokutana, na hata sasa hivi kwenye simu mlikuwa mkiniongelea mimi...manaongea nini kuhusu mimi...?’ akaniuliza akiniangalia kwa makini.

‘Hapana sio kwamba tunakuongea kwa nia ya uchumba wenu, ila anapokugusia wewe kwa namna moja au nyingine, hisia zake usoni, zinaonyesha hivyo…na leo kwenye simu hatujaongea kuhusu wewe, na wala hajui kuwa upo hapa, yeye kaongelea mambo ya kesi yetu, na amesema atakuja kwenye hukumu…..alikuwa akiniambia kuwa nisimuone yupo kimiya, kuna mambo mengine anayafuatilia…ni hivyo tu shemeji, ila sauti yake inaonyesha unyonge fulani...’nikamwambia.

Anyway..shemeji,  najua kabia kama wanafamilia, mlitajia kuwa mmoja wetu atafika hapa, na mimi niliona hilo, kwani kesi ni haki ya kila mtu, kesi sio kujenga uadui, kesi ni sehemu ya kutafuta haki pale unapoona kuwa haki hiyo haikuweza kupatikana katika njia nyingine...kwahiyo ujio wangu huu, ni wa heri, ni wa kutafuta muafaka.....’akasema.

‘Shameji mimi na wazazi wangu, hatukuwa na mawazo hayo kuwa mtakuja kwa heri.....maana kama yako alivyofanya pale mahakamani, ilionyesha wazi kuwa mnatafuta shari,....hata hivyo hukumu haijatoka, na nyie mlishajiwekea uhakika wa kushinda, sijui baada ya huo ushahidi mnatarajia nini tena…’nikasema.

‘Baada ya huo ushahidi , kwangu mimi, kama nilivyoahidi sina jinsi , bali ni kutimiza ahadi yangu, japokuwa kaka kapinga kabisa na hakubaliani na huo ushahidi, na amesema yeye atapinga hadi hatua ya mwisho….’akasema.

‘Kwahiyo mnatarajia kukata rufaa mkishindwa?’ nikauliza.

‘Rufaa ya nini, huko ni kuzidi kujizalilisha, maana kauli yetu ilisikika mahakamani, na ukitenda kinyume chake inaonyesha kuwa umezamiria uhasama, na sisi ni watu wazima tunastahiki kuwa hekima za kiutu uzima, …mimi sina zaidi …nimeshasalimu amri, na nisingelingojea hiyo hukumu,kama isingelikuwa kaka yangu…’akasema.

‘Ulitaka ufanye nini na kesi ipo mahakamani, na huenda mkashinda..’nikasema.

‘Hamna cha kushinda pale, ushahidi muhimu ulikuwa ni hiyo stakabadhi, …ile ni karata ya ushindi, na inadhihirisha wazi kuwa kweli ulishinda hiyo bahati …na fedha ulizojenga hii nyumba na duka inatokana na hiyo bahati, kwasababu ndugu yetu alisema kuwa pesa yake iliibiwa…na nani, hilo ndilo halijawahi kujulikana…’akasema.

‘Labda mimi ndio nilimuibia hizo pesa zake,…si ndivyo nyie mlivyodai, …’nikasema.

‘Hapana …mimi nimeshakuamini,…sina shaka na maneno yako tena, kazi kubwa kwangu ni kumshawishi kaka, ambaye bado ana kesi mbili zinamuandama, badala ya kutulia na kuangalia jinsi gani atapambana na hizo kesi yeye kahamaki kwanini nikakubaliana na kushindwa kwa hii kesi…’akasema.

‘Kwahiyo sasa ni nini uamuzi wenu, …..kukata rufaa, au kusambaratika kwa familia, maana kama nyie hamkubaliani na kaka yenu, kiongozi wa familia, ni nini kitafuta hapo?’ nikamuliza.

‘Familia haiwezi kusambaratika, kwasababu ya mtizamo wa mtu mmoja, nay eye kuwa kiongozi wa familia sio kwamba ni yeye ni kila kitu, yeye kama binadamu huwa anaweza kukosea, na anatakiwa kukubali kukosolewa, na nimemwambia wazi kama yeye atakuwa hakubaliani na ukweli akawa anang’ang’ania sera zake za ubabe, uongozi hatahuweza, na hali kama hiyo inaweza ikamfunga…’akasema.

‘Yeye akasemaje..?’ nikauliza.

‘Amesema yeye kama kiongozi wa familia hawezi kukubali kushindwa kirahisi na,mna hiyo, na hasa ikizingatiwa kuwa aliokuwa akishindana nao ni wanawake, ….alisema wazi wazi , kuwa mwanamke hawezi kumshinda mwanaume, na ukiona mwanaume umeshindwa, basi hujakamilika….’akasema.

‘Kwahiyo kushindwa kwenu inaonyesha hamjakamilika kwa mtizamo wa kaka yako....hiyo sio kweli, huko ni kutokubali ukweli, ….hivi kweli  haoni kuwa anajizalilisha, kwanza kutaka kuficha ukweli, pili kudhulumu na sasa kujitia ubabe na kutokutimiza ahadi, nakumbuka aliahidi na yeye hivyo hivyo kuwa ushahidi ukipatikana hatakuwa na kipingamizi…sasa anataka nini…?’ akauliza na mara mtoto akaingia ndani kwa haraka.

‘Unakimbia nini..unaogpa nini?’ akauiliza.

‘Baba mkubwa anakuja…’akasema .

‘Baba mkubwa, baba mkubwa gani huyo?’ nikauliza.

‘Atakuwa kaka huenda kaja kunifuata,…

‘Au kuleta vurugu…’nikasema nikijiandaa kwa lolote lile.

Na mara mlango ukagongwa…………

NB: Sio mbaya tukiishia hapa, maana duuh, kazi ipo...lakini yote maisha


WAZO LA LEO: Mpende umpendaye, ipo siku mtatengana naye, penda ukipendacho ipo siku utakiacha, fanya ufanyalo ipo siku utaondoka na itabakia ni historia, cha muhimu ni kujua kuwa hapa duniani tupo safarini, sisi ni marehemu watarajiwa, je wewe umejiandaaje na  safari yako hiyo. Tenda matendo mema, ishi kwa amani na upendo, saidia wasiojiweza mayatima kama una uwezo wasomeshe mayatima,wasaidie wajane,… kwani hayo ndio masurufu ya safari yetu hii, tukiwa hapa kwenye kituo cha duniani.
Ni mimi: emu-three

3 comments :

Unknown said...

Hana jipya hiyo na mda maji haachi kutapatapa, hongera zako dada

Unknown said...

Hana jipya hiyo na mda maji haachi kutapatapa, hongera zako dada

emuthree said...

Ndugu yangu Nancy, tupo pamoja, nashukuru sana, kwa hongera zako.na wengine wote wa kimiya kimiya, tupo pamoja.