Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Monday, February 4, 2013

Uchungu wa mwana Ujuaye ni Mzazi-55




Bindamu tusingejaliwa kusahau, natumai nisingelijiingiza kwenye ushawishi wa mama mdogo,  kwa jinsi walivyonifanyia, ilifikia hatua nilitaka kukimbia na kwenda kuishi sehemu nyingine, lakini nlijiuliza nitakwenda kuishi wapi, na je huko nitakapokwenda nitapata usalama gani, na hali niliyokuwa nayo. Ilifikia mahali nilishaapa kama mambo ndiyo hayo, basi ni bora nirudi kijijini kwa mama yangu, lakini haikuwa rahisi hivyo….ikia hatia niliipa kulipiza kisasi, lakini kwa vipi, ……

``Siku hiyo nilikuwa nimechoka baada ya kazi za ndani, nilipata ujumbe kuwa tajiri amefika na anataka kuonana na mimi, kwanza nllizarau, lakini baadaye ukaja ujumbe ukisema kuwa tajiri anataka kunipa mikanda ya matendo yangu, ..’Maua akaendelea kuhadithia kisa hiki.

****
`Mkanda wa matendo yangu…..!?’ Maua akajiuliza huku akijaribu kuwaza, akaendelea kusoma ule ujumbe , sasa hivi akiwa na akili mbili, moja ikiendelea kusoma ule ujumbe , na akili nyingine aikijaribu kukumbuka hayo mtendo ni matendo gani.

‘Kila nikiangalia mkanda wako nashindwa kulala, sijawahi kufanyiwa hivyo kabla,….ulikuwa kama mwigiza picha aliyejitokeza toka kusikujulikana, na kuwa nyota wa picha….nimeshindwa kuvumilia, na naona nikufanye kweli uwe nyota ya maisha yangu….’ Ule ujumbe ukakatika na kuendelea kwenye sehemu nyingine.

‘Mkanda gani huo….’Maua akaendelea kujiuliza.

‘Najua wengi watasema na kukunyoshea kidole, wakitizama matendo yangu , umri wangu, ….lakini yote hayana maana kama kwani maisha, raha, …ni ukiwa na pesa, na mimi sijivuni, lakini pesa kwangu sio tatizo ,na mrembo kama wewe unahitaji mahali kama kwangu, ili uwe nyota ang’avu, nyota itakayongara katika moyo wangu, na kumulika maisha yangu mapya…..kwa ujumla nimechoka, na nahitaji kupumzika….’ule ujumbe ukakatika tena na kuendelea sehemu nyingine.

‘Na bado utachoka sana, kwa hili ulilonofanyia, nahakikisha na wewe yatakupata makubwa,….’akasema kwa sauti na huku akiendelea kusoma huo ujumbe

`Sasa nahitaji kutulia na kuwa mtu mwingine, na nimegundua mtu pekee ninayeweza kutulia naye, na kuituliza nafsi yangu , sio mwingine ni weye nyota, nuru, na ua la moyo wangu, na nakiri, aliyekupa jina hilo la Maua, hakukosea,…kweni wewe ni Ua,..uwa waridi….’ule ujumbe ukakatika tena.

‘Na kwa jili hiyo,.. sasa naona bora nisiwe na huu mkanda wako, na kuungalia kama picha, huku nikikuona kama nyota wa hiyo picha, nahitaji uwe kweli ndani ya maisha yangu…na kama haitawezekana, basi sina budi kuuza huu mkanda …ili nisifanye hivyo, nakuomba ufike ofisini , ili uje uharibu mwenyewe huu mkanda, kabla haujachukuliwa na watu wengine….’ujumbe ukakatika.

‘Mkanda gani huu?’ akajiuliza na kabla hajawaza vyema, ujumbe ukaingia tena, na alipofungua akakuta ni sehemu ndogo ya ujumbe ikimalizia na sehemu hii ilikiwa na maneno machache, ikasema;

‘Kama umesahau, mkanda ninaoxungumiza ndio ule uliokufanya utake kujiua…kwanini ulifikia uamuzi huo, wakati mimi nakupenda…usirudia tena upuuzi huo, na kwa kukujali, nitahakikisha naharibu mikanda yote, lakini nataka uje uiharibu mwenyewe…..’ukamalizika huu ujumbe.

‘Mikanda…?!...’akajikuta kihema kwa hasira, na kumbe ni ule upuuzi wenu mlionifanyia…ngoja nifike hapo, sijali kuwa wewe ni tajiri…..’akatoka nje na kwenda jikoni, kule akachukua kisu kidogo, akakinoa na kukiweka kwenye mkoba wake….

**********

Mama mdogo alipofika, alitulia kwanza , na alionakana mwingi wa mawazo, na kutokana na hli ngumu waliyokuwa wakikabiliana nayo, ilimfanya huyo mama aonekane mzee kabla ya umri wake. Akakaa kwa muda kwenye sofa bila kusema neno, na baadaye akasema….

‘Huyu jamaa yako kaja na anasema anataka kuonana na wewe haraka iwezekanavyo…na nahisi kuna jambo la muhimu kaja nalo, ni bora tu twende, kwani huyu jamaa akiamua jambo lake harudi nyuma, na ukumbuke  ni mtu mwenye kujulikana na kuheshimika kwa ajili ya utajiri wake…’akasema mama mdogo.

‘Kama utajiri ni wa kwake,….haunihusu kamwe…’kabla hajamaliza akasikia tumbo likumuuma….akahisi hali ambayo imeanza kujijenga mwilini. Hali ambayo hata mama yake mdogo alishaihisi na kumwambia wazi wazi….

‘Maua unaonekana una uja uzito, hebu niambie ukweli huo uja uzito ni wanani?’ akauliza mama yake siku hiyo alipomgundua…

‘Mama mimi sina uja uzito,…’akasema Maua.

‘Mimi sio mtoto mdogo, dalili zote zinajionyesha, ….sasa anona umelikoroga, sijui hata huo uanamitindo utaupata tena, …..umeharibu kila kitu, …ni mwanaume gani kafanya mambo hayo, maana sitaweza kulea kiumbe cha mtu, …’akasema mama.

‘Mimi sina mwanaume yoyote, na wala sijui…..nyie ndio mnajua zaidi yangu’akasema akikumbuka jana yake, baada ya kuendelea kujiskia vibaya aliamua kwenda kumuona dakitari,…lakini hata baada ya vipimo kumwambia hivyo, bado alikuwa hajaamini….

***********

 Maua alianza kujisikia vibaya, akawa anahid kuchoka, na hali isiyo ya kawaida mwilini, na akamwambia mama yake mdogo kuwa anajisikia vibaya…

‘Labda una malaria nenda ukapime, ….kwanza tangu uje hapa Dar, sijawahi kukusikia ukiumwa, na ni bora ukapime sasa hivi usijea uakzidiwa hapa nikahngaika usiku, …pesa ya kukodi taksi tutapata wapi.

 Maua akajiandaa na kuondoka kwenda kupima, na alipofika kwa docta, akajielezea na dakitari akamwambia akapime mkojo na damu, …na baada ya vipimo akafika tena kwa huyo dakitari waliyemwambia akapima mkojo na damu…

‘Vipimo vyako havionyeshi tatizo,..huna malaria, na huku kwenye mkojo, mmh, inonyesha una uja uzito..’
Maua alihisi kitu kimegonga kichwani, na akili ikawa haifanyi kazi kwa muda, akatulia na akili ilipokaa sawa, akawa kama anataka kusimama, na kumkodolea macho docta.

‘Eti nini?’ akauliza kwa hasira.

‘Huna tatizo kubwa, hii ni hali ya kawaida, …vipimo vyetu vinaonyesha una uja uzito…na ni vyema ukatu....’akaambiwa na dakitari, ambaye alikuwa anamwangalia kwa makini, kwani alishahisi huyo mwanadada, hakuwa tayari kupokea taarifa hiyo, na hata kabla hajamaliza kuelezea Maua akawa keshasimama

‘Uja uzito? ‘akauliza na kugeuka nyuma , kama vile anahisi kuwa aliyekuwa akipewa taarifa hiyo sio yeye, kuna mtu mwingine nyuma yake, na alipoona yupo yeye na dakitari, akishika kichwa, akasema kwa sauti isiyo ya kwake

‘Uja uzito huo kanipa nani?’ sasa akaguka kumwangali yule dakitari kwa hasira, na dakitari akaegemea kiti chake akimwangalia huyo binti kwa makini, …na alishangaa, kwani sauti aliyotoa yule binti, ilikuwa ya besi, ya mwanaume

‘Sijui..?’ dakitari akasema huku akionyesha uso wa kushangaa na mkono wake mwingine ukawa umebonyeza kitufe , ambacho hutoa ishara kwa wanausalama, waje kutoa msaada.

`Unasema nini…haiwezekani, haiwezekani, kiti wangu …umefanya nini…ni lazima uniambie hii mimba imetoka wapi….’sauti ya kiume nikatoka kwa yule binti, na akawa anamsogelea dakitari. Dakitari, akawa anainuka pale kwenye kiti,..lakini kabla hajainuka vyema akawa keshahikwa shati na koto lake la kidakitari, ….
‘Tulia…..tulia..wewe…..’akawa anajisema huku akizidi kubonyeza kitufe cha kutoa ishara, lakini hakuweza kufanya hivyo zaidi, kwani aliinuliwa kama mtu anayeinua mtoto na kubwaga chini..aliona vinyota vikitanda gizani, na kabla hajapotewa na fahamu mlango ukawa umefunguliwa.

‘Kuna tatizo gani dakitari…’wakauliza wale walinzi, na walipoona dakitari yupo chini, wakamgeukia yule mgonjwa, ambaye aliwaangalia kwa macho ya kutisha, na mlinzi mmoja akagundua hiyo hali, akatoa pingu, lakini hakuweza kufanya hivyo, …..alishikwa na kubwagwa chini…mwenzake alipoona hivyo, akapiga filimbi ya hatari.

Walifika walinzi wengine na madakitari, na chumba kikajaa watu, ….na dakika chake wengi, walitoka wakikimbia, hadi dakitari mmoja alipofanikiwa kumdunga sindano ya usingizi, huyo mgonjwa, na alipoishiwa nguvu, alidondoka chini, ….

Maua alipozindukana alijikuta yupo chumba maalumu akiwa kafungwa kamba, akashikwa na mshangao; akamuuliza mlinzi mmoja aliyekuwa kasimama mbali na yeye. Yule mlinzi alionekana akiwa na wasiwasi, na hakutaka kabisa kumsogelea.

‘Kwanini mumenifunga kamba?’ akauliza Maua.

‘Kwasababu umepandisha na unaleta fujo, wewe una mashetani, eeh?’ akauliza bado akiwa na amshaka.

‘Nina mashetani…mbona sikuelewi, mashetani hayo yametoka wapi?’ akauliza Maua, akiwa anashangaa.

‘Kama ulikuwa hujui, sas aujue kuwa una mashetani, na kama usipoyashughulikia yatakuharibu huo usichana wako’akasema huyo mlinzi.

‘Mikono yangu inauma, nifungueni hii kamba…’akasema Maua, na yule mlinzi alipoona kuwa huyo binti hana matatizo tena akamuita dakitari, na baadaye akafunguliwa na kupelekwa mbele ya dakitari,….dakitari huyo alikuwa mtaalamu wa mambo ya akili, akaanza kumhoji Maua kwa undani.

‘Hebu niambia binti una matatizo gani?’ akauliza

‘Mimi nilikuja kupima, maana hali yangu, imekuwa sio njema, najiskia kuchoka, kizunguzungu, na kichfu chefu,…na natamini kulala tu muda wote,…..na…’akawa anajielezea huku yule dakitari akiendelea kusoma kado yake aliyoandikiwa na dakitari mwenzake ambaye alishaondoka kwenda kupimzika, baada ya kutibiwa, ….kutokana na majeraha aliyoyapata.

Dakitari yule alimhoji kwa muda, na baadaye akaandika kwenye kadi yake, na kumwambia afike sehemu ya dawa akachukue dawa, na baada ya wiki arudi tena hapo hospitalini.

‘Kwani mimi nina matatizo gani?’ akauliza Maua

‘Tatizo lako linatokana na uja uzito…na mengine tutayajua baadaye, tukiendelea na uchunguzi, ila ningekushauri ukija safari nyingine ufike na mama yako, au mume wako…’akasema yule dakitari

‘Hapana dakitari, ……..kuna makosa yamefanyika, nahitaji kupima tena….’akasema na kabla docta hajasema kitu, akondoka, na hakurudi tena kupima, hadi leo alipopata taarifa hii kuwa anahitaji kuonana na huyo tajiri

***************

‘Eti sisi ndio tunajua, yaani wewe ufanye ufusuka wako, ubebeshwe mimba, halafu uje kutusakizia sisi, mimi nitajuaje mwanaume aliyekubebesha hiyo mimba….hebu niondolee upuuzi huo’akasema mama mdogo.

‘Nyie ndio mlionikamatisha na kufanya nibakwe siku ile…..kama ni mimba basi ndio nyie mlionipa…’akasema Maua huku akianza kulia. Na yule mama akainama chini, hakuweza kusema neno. Akainuka na kwenda kwenye shughuli zake.

Maua akibakia akiwaza, akawa anawa maisha yake yatakavyokuwa, na akikumbuka maisha ya mama yake, aliyowahi kumsimulia, alijiona mwenye bahati mbaya;

‘Ina maana hali iliyompata mama ndio imenipata na mimi..kwanini ….hapana haiwezekani, sikubali, kwanini…..’akawa analia huku akishika kichwa , maumivu yakaanza kumjia, na hali isiyo ya kawaida ikaanza kujijenga kichwani, akakumbuka dawa aliyopewa na mtaalmu mmoja, kuwa akijisikia hali kama hiyo ainuse.

Alipoinusa na kupiga chafya akajihisi ana mang’amung’amu ya usingizi na hapo taswira ya mwanamke asiyemfahamu ikawa umesimama mbele yake, mwanamke yule akawa anaongea, lakini hakuweza kusikia sauti yake, ilikuwa kama anawa ni nini huyo mwanamke anamwambia.

‘Mjukuu wangu, matatizo hayo uliyo nayo ni makubwa, yanahitaji urudi kwenu,….ufike msitu , sehemu ulipozaliwa, huko,….utaweza kumpata mtu atakaye kusaidia kuondoka hayo yaliyopo kichwani mwako, lakini hata hivyo…mzigo uli nao hautakuwezesha kuingia huo msitu, kwani ni nuksi….kwanza itabidi usubiri mpaka ujifungue…

‘Mpaka nijifungue, kwani mimi ni mja mzito?’ akauliza

‘Ndio,….ndio…..ndio…..lakini ni mkosi….oh, mkosi mkubwa’ile sauti ikawa inasema hivyo hivyo.

`Mkosi gani , na nani kanipa huu uja uzito?’ akauliza.

‘Unamfahamu sana…na hayo ndio matokea mabaya yanayokikabili kizazi kipya,….maisha yenu yamagubikwa na mitihani mingi, …ninawasikitikia sana, …..’ile sauti ilikuwa kama inafifia.

‘Lakini mbona sina makosa….’akalalamika Maua.

‘Najua huna makosa, ….lakini ni lazima hayo yatokee, …..siku ukirudi kwa mama yako utagundua yote, na poleni sana, kwa hayo yote, ..cha muhimu usikate tamaa…..kwaheri’ ila taswira ikaondoka na Maua akaamuka na mbele yake alikuwa kasimama mama yake mdogo.

‘Ina maana hujajiandaa?’ akauliza kwa hasira.

‘Kujiandaa kwenda wapi?’ akauliza Maua.

‘Hivi wewe una nini lakini,…hali uliyo nayo, siyo ya kukaa kimiya, kama huyo jamaa keshafika ni lazima twende kwake, na ukifika ujielezee, usifiche kitu, na najua atakupa ushirikiano, na akikataa tutamstishai kumshiktakia, najua haogopi…’akasema mama mdogo.

‘Mimi sitaki matatizo na mtu,….tutafute nauli, nitarudi nyumbani kwa mama yangu…’akasema Maua huku machozi yakimtanda usoni.

‘Kwa mama yako, kwani yeye ndiye aliyekupa huo uja uzito?’ akauliza mama mdogo.

‘Nasikitika sana, kwani ulinichukua ukimdanganya mama kuwa unanileta huku, kunisomesha na kuniwezesha, na kumbe nia na lengo lako lilikuwa hivi….nashukuru sana mama, na mungu atakulipa’akawa anasema huku akilia.

‘Acha utoto huo..maji yameshamwangika,..hapo hakuna jinsi, lazima tupambane, …najua utanilaumu kwa hilo, na mama yako atanilaumu sana, lakini lengo na nia yangu ilikuwa njema,…kupata mafanikio, unafikiri hili ni tatizo, mbona mimi haya nilishayapaat sana, mbona bado naishi….’akasema huku akionyesha kutojali.

‘Kwahiyo unawaambukiza wenzako…ili wafuate maisha yako, na unawafanyia watoto wa wenzako kwa vile huna uchungu nao, ….kama ingelikuwa ni mtoto wako ungelimfanyia hivi….mama, utanisamehe sana, lakini wewe ni ibilisi…sina jina jingine linalofaa kukuita wewe’akasema Maua.

‘Mimi ni ibilisi, sio…yaani kukutoa kule kijijini kuja kukutafutia maisha , leo hii nimekuwa ibilisi, nashukuru sana…hata hivyo, jiandae twende, huko ni lazima twende, hata kwa kama ni kukubeba nitakubeba, ni lazima tukamuone huyo jamaa…

Maua akasimama, na kabla hajainua mguu, akahisi mwili kuishiwa nguvu,….kizungu zungu, kikatanda usoni, na hapo hapo wakasikia mlio wa gari, na honi, na …Maua akapoteza fahamu.

********

NB: Sehemu hii nimeiandika kwa haraka asubuhi asubuhi, huenda hajakaa vyema, 

WAZO LA LEO: Tunapofanya mabaya, tusiwashawishi wengine wafanye hayo mabaya , eti ili na wao yawasibu hayo yaliyokukuta wewe. Ni vyema tukawa waalimu wazuri, na sio  kuwa walimu wabaya, na kuwa wa Ibilisi, wa kushawishi kufanya ubaya.
 


Ni mimi: emu-three

1 comment :

Anonymous said...

If you have had situation going your own home, some of our companies may well take you approximately the whole set of family home for their B . C . drivers license. The service plan is very little internet site monetary cost. Satisfy twenty-four hours a day you can ask some of our staff in touch you and me article. http://www.vancouverhomesrealestate.com/