Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Wednesday, February 13, 2013

Uchungu wa Mwana aujuaye ni mzazi-60





Maua alifuata njia aliyoelekezwa, na alijaribu kuwa mwangalifu asigundulikane kuwa yeye ni nani na anapokwenda ni wapi, na kila mara akili yake ilitekwa na kauli za kejeli za yule mwanadada;

‘Hahahahaha…huoni hata aibu, ..ninajua yote, na bahati nzuri, nilipata ushahidi, ….nikaona, jinsi ulivyokuwa ukifanya, ulivyo kuwa ukitingisha, unavua nguo mbele ya wanaume, wanakushika shika huku na kule….ni aibu mtoto wa kijijini kwetu kufanya uchafu kama huo, ….

Maneno hayo kila yakimjia akilini, alijiona akipandwa na hasira, na hapo alitakiwa kutuliza kichwa na kuifukuza hiyo hali, kwani alishaambiwa ili aweze kuishinda hiyo hali, ahakikishe anaidhibiti hasira yake, na kukiwazia kitu kwa muda mrefu….

‘Oh, ….kwanini nashindwa kuvumilia…’akawa anajilaumu pale kichwa kilipoanza kumuuma, akatafuta sehemu akasimama kwa muda huku akijaribu kutuliza akili, na alipoona hali haitulii, akaona ni bora ajipake yale mafuta yake haraka, ..akatoa kile kichupa na kuyanusa yale mafuta puani,….kichwa kikawa kama kimemwagiwa maji ya baridi, …akawa kama hana chocna baadaye akili ikatulia na hote kichwani, na karibu ashikwe na usingizi….

‘Hapana nina haraka sitakiwi kulala hapa….’akasema na kuendelea na safari yake.
Alipofika mitaa hiyo waliyoelekezwa, mitaa ambayo kuna nyumba kubwa kubwa za kifahari, huku akili yake ikijaribu kukumbuka yale maelekezo waliyopewa,..

‘Ukifika hapo, angalia mitaa yenye maduka mengi,…kwenye barabara kuu ya mabasi, angali kulia kwako, kuna nyumba moja ipo tofauti, wa jinsi ilivyopakwa rangi, imapakwa fito mbili za njano na kijani, unaweza kuiona kwambali, ukiikaribia huwezei kuona kwa ndani tena kwani vile imezungushiwa ukuta mkubwa,….ukifika hapo gonga kengele, …’huyo jamaa yao akawa anawaelekeza.

‘Kuna walinzi?’ akauliza mama mdogo.

‘Ndio wapo, tajiri kama huyo, asiwe na mlinzi,…japokuwa kawapunguza, lakini kwa sasa yupo mlinzi mmoja tu…..muda wote analala, hana cha kufanya…’akasema huyo jamaa yao.

‘Hawezi kutuzuia kuingia…..?’ wakauliza.

‘Hapo ni akili yenu wenyewe….maana mimi sina mazoea na hawo watu, …nilimuuliza jamaa mmoja aliwahi kufanya akzi humo, amesema ukifika hapo, unachotakiwa kusema ni kuwa wewe ni mfanyakazi wa Tajiri, umeleta mzigo wake,….’akatulia akiwaza jambo.

‘Na kwa vila nyie ni akina mama,…na inategemea mtaavyovaa..mvae kiheshima, ili msitiliwe mashaka,…nina imani atawaruhusu tu kuingia, na ukishaingia ndani, nenda kwa haraka hadi kwenye jengo, na ukigonga mlango unaweza kukutana na dakitari anayemuuguza huyo mzee, kwasababu nilisikia hali ya huyo mzee ilikuwa mbaya….’akatulia tena.

‘Kama hayupo huyo dakitari, utawakuta wafanyakazi wa ndani wao hawana lolote la kumzuia mtu…wewe ingia na unapoingia ndani ya hiyo nyumba, utajikuta kwenye ukumbi, kuna viti vya kifahari, maua, mapambo, ukiwa mgeni unaweza kuzubaa kuangalia jinis kulivyopendeza…’akageuka huku na huku kama anaangalia.

‘Wewe si umesema hujawahi kufika humo ndani…?’ akauliza Maua.

‘Hayo ni ya kuhadithiwa na huyo mlinzi aliyewahi kufanya kazi humo, anasema kuna pendeza sana, sasa kushoto, kuna varanda, inakwenda mbele,….unaifuata hadi mwisho wake, ambapo, utakuta mlango wa kushoto na kulia…fungua mlango wa kulia….sijui hapo mnanielewa…?’ akasema huyo jamaa.

‘Tunakuelewa…muhimu ni kuingi ndani…’akasema Maua.

‘Sawa….huo mlngo wa kulia, ukifungua unajikuta tena kwenye ukumbi, sio mkubwa sana…lakini nasikia hapo ndio kamaliza kila kitu , utafikiri upo peponi..na mara nyingi huyo mzee anajipumzisha hapo, kuna sofa lake kubwa …lipo kama bembea, karibu yake kuna bwawa…baridiii, na ndege wanaruka huku na kule,…samaki…yaani we acha tu….’akasema huyu jamaa utafikiri aliwahi kufika humo ndani.

‘Hana mke?’ akauliza Maua

‘Mke wake walikorofishana akarudi kwao,….hawa matajiri wana mambo wewe, unaweza ukawaona mitaani au mabarabarani na mgari yao ya kifahari, ukafikiri wana raha,..sio wote wenye bahati kama hiyo, yeye na mkewe walikuwa wakiishi kama paka na chui,hawana maelewano kabisa…wanawake wengine hawana maana, maana pale mungu akupe nini, lakini nasikia alikuwa hatosheki….kila mara sherehe, mara anataka kusafiri nje ya nchi…yaani alikuwa akimuendesha puta huyo mzee, ….hadi basi….’aksema huyo jamaa yao ambaye aliombwa kuwasaidia.

‘Kwahiyo kumbe, huwezi kuzuiwa kuingia, au hawo wafanyakazi hawawezi kumzuia mtu asionane na huyo mzee na watoto wake je, kwani hana watoto,…?’ akauliza.

‘Mara nyingi hakuna anayefika fika humo,…kutokana na tabia zao za kujiona,… na kebehi zao, wao wanadai wanaishi kizungu, na kwahiyo maisha yao ni ya upweke, …maana kama hutembelewi na ndugu, au jamaa zako, na eti ukitaka kwenda kwake mpaka uwe na ahadi naye, ni maisha gani hayo kama sio upweke,….’akawa kama anauliza.

‘Mungu sasa anamueleleza, watoto wote wapo ulaya, wanaishi huko, hawataki hata kurudi, japokuwa wamesikia baba yao anaumwa, kisa, kwa vile haishi vyema na mama yao…’akasema huyo jamaa.

‘Sasa unaona, hivi sasa anaumwa,…ndugu na jamaa hawana habari naye, kwani wanadai kuwa huyo jamaa alipokuwa mzima alikuwa hajali ndugu zake au jamaa….yeye alimjali mke wake, na watoto wake tu, kwahiyo awaite watoto wake, waje wamsaidie…’

‘Kwahiyo kwasasa ninani anayemuuguza?’ akauliza mama mdogo.

‘Ni huyu mwanamke aliyepagawa, na mjomba wake,….yaani huyo anayeitwa Tajiri, ….na hata hivyo huyo mwanamke, nasikia hana kauli nzuri na huyo mzee, hawaelewani, ….nasikia huyo mwanamke, anajipendekeza tu kwa huyo mzee, kujifanya anajali na kumuuguza, na anafanya hivyo ili tu apate mali, ili arithi mali ya huyo mzee, na zaidi alikuwa akishinikiza aolewe na huyo anayeitwa Tajiri…’akasema

‘Kwani huyo Tajiri sio ndio jina lake?’ akauliza Maua.

‘Ndivyo tunavyomjua hivyo kwa jina hilo, huenda ana jina jingine, lakini wengi tunamfahamu kwa jina hilo…la Tajiri, …nilimuuliza huyo mlinzi swali kama hilo akasema hata yeye hajui jina jingine….’akasema huyo jamaa yao.

‘Mimi nitaenda ….nina hamu sana ya kuonana na huyo mzee, …’akasema mama mdogo.

‘Hapana mama nitaenda mimi,kwa vile yote haya yananihusu mimi, na wewe ubakie hapa, ili wajue kuwa bado tupo humu ndani, na hata huyo Tajiri akija akukute  humu ndani’akasema Maua.

‘Acha mimi niende, nahisi huyo mzee ana pesa nyingi…lazima nikamtoe pesa kidogo…na huyo ni mzee, anahitaji kuonana na watu wazima, wanaojua taratibu ….na wewe huwezi kumtoa pesa,….’akasema mama mdogo.

‘Hapana mama ..huyo anahitaji kuonana na mimi, …wewe utabakia hapa, najua ukienda huko utakwenda kudai pesa, na kuleta aibu tu….mama hiyo tabia sio tabia njema watu wanatufikiri vibaya, ….’akalalamika Maua.

‘Wewe bado mdogo, kula kulalatu…..hujui tukirudi bongo, tunahitajiwa kodi ya nyumba..tunahitaji kuendeleza ile biashara yetu,kwa hivi sasa mtaji umeguduka,….unafikiria pesa tutapata wapi, kama sikutumia ujanja ujanja….’akasema mama mdogo.

‘Mimi hayo maisha siyawezi….huko kwa huyo mzee, nitakwenda mwenyewe, wewe bakia humu..’akasema Maua.

‘Tuahidiane, kuwa ukienda huko utakuja na pesa, na zote utanikabidhi mimi, kama ukikubali hilo, mimi sina shida….’akasema mama mdogo, akiigiza laafudhi za huko.

‘Mimi siendi kutafuta pesa, siendi kufanya kazi huko…utapataje pesa bila kuzifanyia kazi’akasema Maua.

‘Kwani unakwenda kufanya kazi au unachohitajiwa ni kutumia akili kidogo, wakati mwingine inabidi ufanye hivyo kwasababu utajiri wao mwingine umepitia kwenye migongo yetu, na walistahili wakipata huo utajiri, watuinue na sisi angalu kidogo, lakini hawataki…,’akasema mama mdogo.

‘Hayo ni mawazo yako..’akasema Maua.

‘Hivi wewe utajifunza lini akili ya kutafuta pesa…hakikisha ukija hapa una pesa…’akasema mama mdogo kwa hasira.

Maua alimwangalia mama yake mdogo kwa macho ya kutommaliza,  akachukua khanga moja na kujifunga kiunoni na nyingine, akajitanda kichwani na kubakiwa na sehemu ndogo ya uso, alionekana kama akina mama wa maeneo ya huko, ….na alipomwangalia mama yake mdogo, mama yake mdogo akamnyoshea kidole cha gumba, kumpongeza;

‘Hapo umefanya itakiwavyo, ole wako uvurunde, halafu uje bila pesa...’ Mama mdogo akasema , Maua hakusema kitu, akatoka na kuanza kufuatilia njia kama wavyoelekezwa.

NB: Muda umewisha tukijaliwa tena kesho

WAZO LA LEO: Raha, shida, huzuni, upweke, yote ni majaliwa ya mwanadamu. Sio matajiri wote wana raka, kama tunavyofikiria,…. unaweza ukawa tajiri na bado ukajikuta ukiwa huna raha, na unaweza ukawa masikini ukawa na raha kulio hata huyo tajiri. Cha muhimu, ni kurizika, kujipa moyo, kuwa na subira, ….na hali uliyojaliwa nayo.

Ni mimi: emu-three

No comments :