Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Friday, December 21, 2012

Uchungu wa mwana aujuaye ni mzazi-41




YALIYOPITA: `Ugeni huo kutoka makaoni….mbona wamewahi hivi…,?’ akauliza mfalme mtarajiwa.

Hapana huo ni ugeni wa mzee hasimu na kijana wake na wazee wenzake’ akasema huyo mlinzi
Hapo yule mfalme mtarajiwa akageuka kushoto kwake , ambapo ndipo wageni wanaposubiria na  kule aliona kundi la watu, na miongoni mwake akiwemo Mzee hasimu na kijana wake, walikuwa wote wamekunja uso kwa hasira.

Je ugeni huo ulikuwa kwa heri au kwa shari, hebu tuendelee tuone ni nini kilitokea …..

****
Wapendwa lengo la sehemu hizi katika kisa hiki ni kuona jinsi gani watawala wenye uchu wanavyopenda madaraka, hasa pale wanapoonja `utamu’ wa madaraka hayo kwa vile kwao wao wapo hapo kama `ajira’. Na wanashindwa kuelewa kuwa madaraka hayo ni kwa ajili ya wananchi,baada ya kupata kibali hicho kutoka kwa hawo wananchi,….
****
Kikao maalumu cha dharura kwa ajili ya kuwasilikiza wageni waliofika kilikamilika , wageni hawo sio wengine ni mzee Hasimu na kijana wake, wakiongozana na wafuasi wao. Wenyeji, walipomaliza kuongea na kuwekana sawa, wakatoka kwenye cha maongozi, ikabidi muhusika wa kukaribisha wageni atoke na kuelekea kule walipo wageni, ili apate kuwakakaribisha kwenye ukumbi huo maalumu.

Wageni hawo walikuwa wengi, walikuwepo viongozi waliokuwepo madarakani kipindi kilichopita, na pamoja nao kulikuwepo maaskari. Na kwa utaratibu wao ulivyo kikao kama hicho kilitakiwa kifanyike kwenye chumba maalumuho maalumu hakina uwezo wa kuwaingiza hawo wageni wote na wajumbe wa wenyeji.

Kutokana na hilo mkuu wa vikao,  ikabidi awaombe wageni hawo kuwa wengine wabakie nje. Waingie wawakilishi tu, ambao wanaweza kutoa hoja za wote, hasa viongozi wakuu, na wasaidizi wake wachache. Taarifa hiyo haikuwapendeza wahasimu, wao wakai kuwa wote wamekuja na hoja na wote wanatakiwa kushiriki kuhakikisha kuwa hoja yao inapita.

‘Lakini mzee wetu muheshimiwa, wewe mwenyewe unaifahamu sehemu hiyo ya kikao ilivyo, haitawezekana nyie wote muingie humo, na wengine watashindwa kuingia, je kikao hicho ni chenu peke yenu….?’ Akauliza mkuu wa wageni.

‘Hilo mtajua weneywe, cha muhimu ni kuwa lazima wote niliokuja nao waingie kwenye hicho kikao..’akasema huyo mzee.

‘Mzee, hatutaweza kuwaingiza wajumbe wote, wajumbe wako mlioongozana nao ni wengi kupita uwezo wa chumba chetu cha mikutano maalumu, chagua wawikilishi wachache …’akaambiwa.

‘Kwanini nichague wajumbe wachache, kwanza niwaambieni, kuwa tumekuja hapa kukutana na huyo mnayemuita mfalme wenu mtarajiwa na wawakilishi wake wachache, hatuhitaji watu wenu wengi, kwanza wa nini,… na madai yetu ni kwa huyo mtu wenu mliyemlazimishia kuwa ni mfalme mtarajiwa…nyie wengine hatuwahitaji…’akasema mzee kwa hasira.

‘Sawa mzee tumekusikiliza hoja yako, kama nia yako ni kuhakikisha watu wako wote uliokuja nao wanashiriki, basi, hicho kikao itabidi kikafanyikie sehemu nyingine na sio sehemu hii maalumu ya vikao vya kukutana na mfalme….na labda tukakifanyie kwenye uwanja wa mapambano’akaambiwa.

‘Haiwezekani, kikao kama hiki kinahitaji huo ukumbi si vinginevyo….sisi tunahitaji kuongea na huyo mtu, na kama mnataka tukaongelee uwanja wa mapambano, kwanza ajivue huo ufalme mliomvika isivyo halali, kwahiyo tukue tunaongea na mtu ambaye sio mfalme mtarajiwa….’akasema mzee huyo akiwaangalia watu wake ambao walimuunga mkono, kila mmoja akionyesha kuwa yupo pamoja na mzee wao.

‘Mzee  wewe ni mtu tunayekuheshimu sana,…na tunashangaa kushinikiza jambo ambalo unaona kabisa halitawezekana, hatutaweza kuingia wajumbe wote kwenye chumba hicho, sisi tunakuambia kuwa, chagua wawakilishii wako wachache  na wengine wasubiri nje’, ‘akaambiwa na yeye akawasogelea watu wake na kuteta nao, na ghafla wakaanza kuingia kwenye huo ukumbi, wote kama walivyokuja, na ukumbi ukawa umejaa, kama vile kikao hicho kilikuwa ni cha kwao peke yao…

Mfalme mtarajiwa alipoambiwa hilo,  hakujali, akamuita babu yake na wazee wachache na wawikilishi wake wawili, wakaingia kwenye hicho kikao, na alipoingia wale wageni wakaanza kuzomea kwa kuonyesha kuwa hawamtambui huyo mfalme , …

Mfalme mtarajiwa hakujali, akakaa kwenye kiti chake, na mzee mmoja mzungumzaji mkuu akaanza kukifungua kikao, alianza kwa kutoa salamu,na wageni wale wengine wakaitikia wengine wakawa wanaendelea kuzomea,…yule mzungumzaji akaanza kuongea kwa kusema;

‘Wazee wanasema, hekima ni ukomo wa elimu, ukikosa hekima hata kama una elimu kiasi gani, hujaelimika, ukikosa hekima hata kama utakuwa kiongozi mwenye nguvu kiasi gani hujawa kiongozi bora, hekima ndiyo inayokuendesha wewe kujua lipi ni jema na lipi baya na lipi lifanyike kwa wakati gani, na kwa watu gani, na ni vipi uishi na wenzako..

Ndugu zanguni,poleni na safari na tunaomba samhani kwa kuwasubirisha kidogo, na tunashukuru kuwa mumemkubali kiongozi wetu , ndio maana mkashinikiza kikao hiki kifanyikie hapa, na wote mkawa na hamu ya kuongea naye…’ akakatishwa na kuzomewa.

‘Ndugu zanguni, …ukweli unauma,….na ukweli upo, hata kama utaupiga chenga, ….hali halisi inajionyesha na ipo zahiri, ..ila kama nilivyotangulia kusema, nawaombeni sana tujitahidi kuwa na hekima, kwa kuheshimi kikao muhimu kama hiki, na sehemu muhimu kama hii…..’akasema mzungumzaji akinama kidogo kuonyesha heshima ya kuwaomba, na wale watu wakatulia kumsikiliza.

‘Baada ya kuanza kusema hayo, ninaomba nikifungue kikao hiki kwanza kwa kuwaomba wageni wetu ajenda zenu, maana mumesema ajenda hizo mtazitoa ndani ya kikao, na hatuwezi kuendesha kikao bila mpangilio maalumu, je mnayo ajenda gani muhimu?’ akauliza.
Akasimama mmmoja wao, aliyekuwa mpambe wa mzee hasimu anayejulikana kwa kuongea, akasema;

‘Ili tusipoteze muda, mimi namkaribisha kiongozi wetu wa siku nyingi, mtawala aliyeendesha jamii yetu kwa muda mrefu, na mnfahamu kwa kazi yake nzuri, ndio maana leo mpo hapa, karibu mzee wtu mkuu, mzee Hasimu;

Mzee hasimu kwanza akasimama, na baadaye akakaa, hakuinamisha kichwa kuonyesha heshima, akaanza kwa kusema;

‘Ajenda yetu namba moja ni kuwa huyo mnayemuita mfalme mtarajiwa aondoke kwenye kiti alichokalia maana hakubaliki na hana sifa ya kukikalia hicho kiti, vinginevyo, tutakuwa tunavunja hadhi ya hicho kiti, na ajenda yetu ya pili ni kumtafuta mfalme mtarajiwa , ambaye ana hiyo hadhi, …’wenzake wakashagilia.

‘Na ajenda yetu ya tatu, ni kufuata sheria kama zilivyotuagiza kuwa kama kutakuwa na tatizo kama hili la kulazimisha uongozi, huyo aliye lazimisha ni sawa na mvamizi, …….wa nchi na baya zaidi anaingia sehemu takatifu na kukalia kiti kitukufu,…’ Mzee huyo akawa anaongea na wenzake wakawa wanamshangilia.

Alipomaliza kuongea, Mzee mteula akasogea pale alipokaa mfalme mtarajiwa baada ya kumuona kama anataka kuinuka kuondoka kwenye kile kiti kama alivyosikia katika moja ya ajenda, kwa jinsi anavyomjua mjukuu wake, angeliweza kufanya hivyo, ili kuleta amani,na huenda, akatii yote yaliyosemwa na wahasimu, yeye akasogea pale na kumshika mjuu wake kwenye bega.

‘Wazee wenzangu na wajumbe wengine , mimi nisingelipenda kuliingilia hili, ila nilikuwa nataka niwarejeshe nyuma, kipindi ambacho alifika yule mtabiri, wazee wenzangu mnakumbuka vyema siku ile, alivyosema…’
 Watu wakaguna  na kusema;`mmmmmmh, kaanza huyo…’

‘Narejea maneno ya huyo mtabiri, ambaye wote tulimuheshimu na kuheshimu maneno yake kuwa ni muhimu na yana nguvu, mnakumbuka alisema nini…..’akatulia hapo kidogo na kuigiza sauti nzito, na huyo mtabiri;

‘Siku ikifika atatokea mtu, kutokea machweo ya jua,…na miali ya jua itakuwa inamchoma yeye kwa nyuma, huku akiwa kapanda kipando maalumu, huku akiwa kaongozana na kundi la watu, waliosalimu amri kwake…yeye atakuwa hajui kuwa ndiye mfalme mtarajiwa, ….

Hapo akatulia hapo na kuongea sauti yake ya kawaida kwa kusema;

`Mimi nitataja baadhi ya sifa ambazo alizitaja huyo mtabiri, moja ya sifa hiyo ni kuwa ,mtu huyo atakuwa,…, atakuwa ni jasiri….atakuwa na hekima, atakuwa mtu wa watu anayejali watu bila kubagua,….atakuwa ndiye mume wa malikia…..’aliposema hivyo, wakazomea na mmoja akasema

‘Ni mbinu zenu hizo, mlimteka malikia ili aolewe na kijana wenu, hizo ni minu zenu, hatkubali hilo….’wakasema.

‘Hebu tuanalieni kiukweli, …kama alivyosema mwenzangu katika utanguzi wake kuwa ukikosa hekima huna elimu, hata uweje, unaweza ukatumia elimu yako bila kujali madhara ya baadaye, na kwa manufaa yako binafsi, hiyo haitakuwa ni elimu,…na halikadhalika ukiwa kiongozi ukakosa hekima hutaweza kuwaongoza watu wako kwa busara, utaweka masilahi yako mbele…’watu wakacheka na kukebehi.

‘Hili linajionyesha hadi hapa,….nyie ni viongozi wa jamii, nyie ndio vichwa vya wale mnaowaongoza, mumeaminika kwa kila kitu, je hii mnayoionyesha hapa ni nini….? Hamuoni kuwa mnakosa hekima , hata ya kikao muhimu kama hiki…jamani tuangalienei mbele, tusijali ubinafsi wetu, hatutaki uongozi kwa ajili ya sifa,…

‘Uongozi ni kwa ajili ya wananchi na wale unaowaongoza, kama wewe ni kiongozi ukawa kwanza unajali maslahi yako, unataka kila kitu kikubwa kiwe chako,….una kasoro…na ninaweza kusema hukustahili kuwa kiongozi, …kiongozi bora ni yule kwanza anayewajali watu wake, na ikibidi kama ni njaa, kama ni maslahi, kwanza uhakikishe watu wako wameshiba, kabla hujaweka tonge mdomono kwako..’watu wakecheka kwa dharau.

‘Ni nani kati yenu aliwahi kufanya hivyo….kuhakikisha kuwa wananchi wanapewa kipaumbele, kabla ya kujali maslahi yake….ni nani aliyehakikisha kuwa wananchi wanasikilizwa hoja zao, matatizo yao…njaa yao, kabla hajalitizama tumbo lake. Ni nanli aliyekuwa tayari hata kupoteza maisha yake kwa ajili ya wananchi wake? ….’akawaangalia na hapo walikaa kimiya.

‘Sisi kama wazee ambao tumepitia wakati mgumu, tumeshuhudia umwagaji damu wa hali ya juu, ndugu wa damu, tumeuana kama wanyama,…na baada ya hapo ni chuki , visasi, ….ubinafsi, nah ii yote ni mdahara ya umwagaji damu, unapoua usifikiri ndio mwisho wa yote, damu ya mtu itakuandama….

‘Sisi nduguzanguni, naombeni tujaribu kukumbuka tulipotoka, tujaribu kuangalia mambo kwa upeo wa mbali, kwasabbu uongozi sio ajira, ukiweka mbele kuwa kiongozi upo hapo kwa ajili ya tumbo lako, ukasahahu hekima nzima kuwa wewe upo kwa ajili ya watu, hutakuwa umetenda vyema…

‘Sipendi niongee mengi, maana kuongea sana, hakusaidii, kinachohitajika hapa ni hekima, …na ili tufanikiwe hili, nafikiri ni vyema tukaangalia sifa za huyo kiongozi aliyetabiriwa, je haendani sawa na huyo kiongozi aliyejitokeza siku hiyo, kama haziendani nay eye  ni nani  mwingine, ambaye anazo hizo sifa na ina maana kama ni hivyo, siku hiyo haikuwa na umuhimu kwetu…

‘Kama tulikubali kuwa siku hiyo ndiyo siku iliyotabiriwa, na siku hiyo ndiyo huyo kiongozi atatokea, na akatokea, lakini sisi tunaona siyo yeye, je ni lini atatokea, na huenda mndai alitokea ikafanyika hujuma, je ina maana yule mtabiri alisema uongo, kwani kama mnavyokumbuka, alisema siku hiyo hata ifanyike vipi, huyo kiongozi atajitokeza.

‘Na hata hivyo, waamuzi wakubwa ni wananchi, je wananchi wanasemaje kuhusu huyo kiongozi, wanamkubali au hawamkubali, na kama yupo mwingine ambaye kafanyiwa hujuma, je wananchi wanamkubali….hayo ndiyo ya muhimu, hata kama tutakimbilia kumuondoa huyo ambaye hamumkubali kwa sababu zenu, bado tunahitaji rizaa ya wananchi wote...

‘Hatumkubali, …’wakasema kwa sauti….

‘Nyie I sehemu ndogo sana ya wananchi, na ka ingeliwezekana kuzifungua nafsi zenu, wote hapo mlipo mnamkubali , lakini kutokana na shinikiozo na propaganda potofu, sasa hivi mnapinga, lakini mkumbuke kuwa hicho mnachokifanya kitakuja kuwashitaki baadaye, kwasababu mnahini ahadi na utabiri …..’ kabla hajamaliza mara akaingia askari, na kumng’oneza Mzee Hasimu sikioni.

Mzee hasimu akamshika mfalme mtarajiwa bega, na kuinama kumng’oneza, wakaangaliana, na mzee akawageukia watu na kusema;

‘Kwa bahati nzuri, wenzetu wa makaoni wametumwa wajumbe, ambao watasimamia hiki kikao kwa ajili ya kupata suluhu, ….kwahiyo tuwe watulivu wakiingia na wao wataendesha shughuli yote ya kuhakikisha kuwa tunafikia muafaka..narudia tena, sisi ni ndugu, na udugu wetu ni wa damu, hatuoni kwanini turejee tena kwenye umwagaji damu, …..’akasema na wajumbe wale wakawa wanaingia.

Wajumbe walipokaa, na mzungumzaji kuwakaribisha, …ndipo kiongozi wa msfara huo akasema;

‘Nakumbuka mlisema aliwahi kuja mtabiri, ambaye amewaatbiria wengi, na waliofuta hayo waliyotabiriwa wameneemeka ,na waliopinga wamekuwa kwenye uhasama wa kudumu, na wanajutia kwanini walipinga….sasa niwaulize swali, japokuwa nimewambiwa wengi ya waliopo humu ni wale wanaompimga kiongozi  huyo mpya.

Lakini hiyo haijalishi kitu, kwani tukitoka hapa tutakwenda kukutana na wanachi ambao nimesikia wameanza kujikusanya kwenye uwanjwa mkuu, ….sehemu yenu ya kihistoria ambapo mliuana kama sio ndugu, na hili hatutaki litokee tena, na kwa minajili hiyo, ni bora kama hakutakuwa na muafaka , itatubidi tuchukue uamuzi mgumu…..ili kutokukaribisha tena hiyo hali…

‘Kwanza kabisa, inabidi tule kiapo, kiapo hichoo ni cha kuhakikisha kuwa makubaliano yote yanapitishwa, na yakipitishwa hapa atakayeyapinga, mnajua ni nini kitampata, lakini hata hivyo, inabidi tule amini ya kukubali au kupinga yale aliyowatabiria mtabiri wenu, kuwa je yalikuwa ni kweli, na kama ni kweli mnayakubali, na kama mnayakubali, na matokea yake yametokea, je kuna nini kimtendeka hadi tusiyakubali tena….

‘Pia huyo kiongozi zliyejitokeza anakubali kuwa kweli hajafanya hujuma yoyote, na kama anakubali na kula hiyo amini, je ni nani mwingine ambaye anahisi alihiniwa, na kumbe ndio yeye alitakiwa kutokea hapo, …akazuiwa ,…kama yupo na anakubali kuwa kweli ndio yeye, na yeye anatakuwa kula hiyo amini, na wenyewe mnajua madhara ya hiyo amini ukiwa unaongea uwongo…

‘Na nyie mnaomuunga mkono mnatakiwa mle hiyo amini kuwa mnakubalina na hilo, na ya kuwa mnamuunga mkono huyo kiongozi wenu mnayekubali kuwa ndiye yeye na kafanyiwa uhaini,..tukimaliza hilo….tutakwenda kwa wananchi, na wao watathibitisha kuwa kweli ni nani kiongozi wao….’akasema huyo muwakilishi na kazi ya kugawa hayo maji ya yamini ikaanza kugawanywa…

‘Vuramai ikaanza,….baadhi ya wajumbe wakaanza kukataa kuyapokea hayo maji…

‘Naomba kila mtu aliyekuwepo hapa ndani aaypokee haya maji, kwani nyie ndio wajumbe mnaowakilisha wenzenu,..na kuyapokea na kuyanywa, sio kwamba umeingia moja kwa moja kwenye kibano cha ahadi, wewe baada ya kunywa utatakiwa kukubali au kukataa hayo utakayoulizwa;

‘Maswali utakayoulizwa ni kuwa je unamkubali huyo kiongozi aliyejitokeza siku hiyo kuwa ndiye aliyetabiriwa, kama unamkubali utasema unamkubali, kama humkubali utasema humkubali, na kama huna jibu, utakaa kimiya…..maana kuna ambao hawana jibu kwa sasa, huenda wanaogopa…

‘Kama unamuogopa kiongozi wako, lakini huigopi imani yako,….unaweza ukakaa kimiya, lakini ki imaniz etu mtu kama wewe hutaweza kupata baraka katika amali zako,hili sihitaji kukufundisha maana nyote hapa sio watoto wadogo, na nyote mnajua madhara ya kiapo majanga yake hayapimiki,…yakianza hutamtemea kiongozi wako kuwa atakuja kukusaidia , hapi ni wewe na familia yako…,

‘Sasa basi, kama umeingia humu ndani, na umekuja kuwakilisha wenzao ni lazima ukubaliane na matakwa ya kikao, kama unahisi hutaweza kuhimili majukumu na msharti ya kikao, ikiwemo hili la kula imini, na kumtetea kiongozi unayemuona kuwa kweli ndiye mfalme mtarajiwa ni bora uinuke na utoke nje…..’ hapo akatulia kwani kabla hajamaliza huo usemi wake, mzee hasimu aligeuza kichwa na kuwaangalia watu wake kwa macho ya kuwatisha

Lakini hata hivyo hutaamini…..hakuna aliyejali macho ya huyo mzee, karibu nusu ya wajumbe wake walinuka na kuanza kutoka nje wakiwemo wazee wake watiifu,……na hata pale mzee hasimu alipowalazimisha wasitoke, hakuna aliyemsikiliza, na baada ya nusu saa wakabakia wajumbe wachache tu ambao walionekana kuwa ni ndugu wa karibu sana wa mzee hasimu, na hapo yule msuluhishi akamgeukia mzungumzaji wa kikao, akasema;

‘Naona wajumbe wamepungua sana, na kikao kama hiki kinahitaji wajumbe nusu kwa nusu, ili tuwe na muafaka kamili, ….tunaomba muwakaribishe wajumbe wengine waliopo nje, kama wapo tayari kwa hili tunaloendelea nalo waingie, kama hakuna ambaye yupo tayari kukubalina na hayo tuliyoongea basi inabid mliopo humu ndani tuendelee na tukimaliza hape tutaanza zoezi jingine…

Alipoamliza hivyo wajumbe wengine wa mzee hasimu wakaanza kutoka, na hatimaye walibakia wajumbe watano tu, mzee hasimu na kijana wake, na wasaidizi wa karibu wa mzee hasimu, …..

‘Mzee, hasimu, naona wajumbe wako wamekukimbia je unalo la kusema …..?’ akauliza mzee hasimu, na mzee hasimu akageuka nyuma hakuamini macho yake, akamwangalia kijana wake na kijana wake alikuwa kainama chini,….

Mzee Hasimu akakohoa na kusema; `hawo ni waoga, na katika vita hutakiwi uwe muwoga, sisi tuliobakia tupo tayari kwa hilo…’akasema na wenzake wakamwangalia kwa macho ya wasiwasi, hata kijana wake alionekana wazi akiwa na wasiwasi, na mzee akamshika bega kumtuliza.

‘Sawa mzee, tunashukuru kwa hilo, na naomba mgawaji wa hayo maji awapelekee hawo wajumbe, na wote waliopo humu ndani,…..je nyie wengine mpo tayari kwa zoezi hilo?’ akauliza huyo muwakilishi, na hata kabla hajamaliza watu wate walisema kwa sauati

‘Tupo tayari…tuna amini kabisa kuwa mfalme huyo hapo mbele ndiye yule mfalme mtarajiwa…’
Mzee hasimu akakunja uso kwa hasira, na wakati huo alikuwa kashika kiriba cha maji aliyoletewa, akionyesha ukakamavu kuwa yeye haamini, na akawaangalai wenzake kwa macho ya ya kuwapa moyo, …kijana wake, alionyesha wazi kuwa ana wasiwasi, na hata yale maji aliyopewa alikuwa kayashikilia kwa mbali kabisa …

‘Kijana wa mzee Hasimu , wewe nasikia ndiye uliyependekezwa an kundi lako kuwa ndiye mfalme mtaarjiwa, ….wewe ndiye unatakiwa uwe mfano, kwa vile unauhakika kuwa wewe ndiye mfalme mtarajiwa, …tunakuomba usisite kuyanywa hayo maji, kama kweli ni haki yako, kama kweli upo kwa ajili ya wananchi, na kama kweli ulidhulumiwa nafasi yako, basi wakati wa kuonyesha hili ndio sasa,…je upo tayari..

Kijana mtarajiwa akageuka kumwangalia mzee wake, ….mzee wake alikuwa kamkazia jicho, akageuka upande wa msaidizi wake, na mshauri wake mkuu, huyo alikuwa kainama chini, na hakutaka kabisa kumwangalia, akamgeukia jemedari wake wa majeshi, ambaye yupo tayari kufa na yeye, na kwa mara ya kwanza ali,muona huyo jemedari kaangalia chini….

Akilini akakumbuka madhara ya maji hayo ya kiapo, ambayo aliwahi kusimuliwa na huyo huyo mzee wake, kuwa kama utayanywa na ukasema uwongo, ….haipiti hata nusu saa, ….mwili mzima unaweza ukaanza kuharibika kama mtu aliyemwagiwa tindikali, au maji ya moto, au unaweza ukapoteza uwezo wa kuona, hapo hapo, au unaweza ukavimba tumbo,…kama mtu aliyepuliziwa upepo hadi lipasuke…..

‘Mjukuu wangu katu hata siku moja usije ukakubali kunywa maji ya yamini kama unajua kuwa yamini hiyo ni kweli na wewe unasema uwongo…ni bora usinywe, babu yangu aliwahi kuyanywa hayo maji ya yamini akijua kuwa ni mzaha,…..alipomaliza kunywa tu, mwili wake ulianza kubadilika kama vile kamwagiwa maji ya moto…

‘Hili nililishuhudia kwa macho yangu mwenyewe…alipiga ukulele, kwani maumivu yake ni makili sana,lakini hakuna aliyemsaidia, kwani ukimsaidia na kumuonea huruma na wewe yanakukuta hay ohayo….kwahiyo aliachwa na baada ya nusu saa, walikuwa mtu kaiva kama nyama iliyobanikwa,…lakini kufa hafi…na anaita watu wamuue, ili asiendelee kuteseka na mates ohayo…

‘Dawa yake hapo ni yeye kukubali ukweli, kuwa alikosea, na ….hapo atakata roho, na mwili wake unatupiwa mamba……’akamwambia babu yake. Na alishangaa kumuona leo akimshinikiza akubali uwongo….akatikisa kichwa,..

‘Haya ni wakati wa kuyanywa hayo maji, tunaanza kwa mfalme mtarajiwa, wewe ndiye unayetetea ufalme wako, upo tayari kuyanywa hayo maji?’ akaulizwa mfalme mtarajiwa,..na mfalme mtarajiwa akapokea kile kiriba cha maji na kusema;

‘Nipo tayari muheshimiwa,…..’

‘Haya kunywa hayo maji, …ukijua kama ni uwongo, basi hayo maji yatafanya kazi yake na kama ni ukweli, hayo maji yatakuongezea ujasiri, ….hekima na uwezo wa kuitawala nchi hii kwa amani na upendo, na hakuna atakayewea kukudhuru, kwani uma wa wananchi waliokusubiria miaka mingi watakuwa nyuma yako…haya kunywa hayo maji…na wale wote wanaomuamini, ambao wapo nyuma yake, wanywe hayo maji.

Mfalme mtarajiwa akainua kiriba juu na hapo hapo akaanza kuyanywa yale maji, na watu wake wakafuatia na kuyanywa mwaji waliogawiwa….na wengine nje wakaingia kila mmoja akitaka kuyanywa hayo maji, …na hata watu wa mzee hasimu wakajiunga kuyanywa maji kwa kiapo kuwa wanamkubali huyo mfalme kuwa ndiye mtarajiwa….na baada ya kuhakikisha kuwa wote wale wanaomkubali huyo mfalme wamekunywa hayo maji, ikabakia zamu yam zee hasimu na kijana wake…

‘Haya ni zamu yako mzee, na kijana wako….naona hata wasaidizi wako wamekukimbia…’akasema huyo mzungumzaji kwani kweli,. Kwa muda huo walibakia mzee hasimu na kijana wake. Mzee hasimu akamgeukia kijana wake na kusema;

‘Kijana wangu,…hivi ni vita, na unapokuwa kwenye vita unatakiwa uwe jasiri, unatakiwa upiganie kile unachoona ni haki na halali yako, mimi nimekuwa nyuma yako, na ,mimi ndiye mwalimu wako..na sitaweza kurudi nyuma kwa hili, kama upon na mimi basi kunywa haya maji…’ yule mzee akainua kiriba cha maji na kuanza kuyanywa…..

Kijana yule alipomuona mzee wake anafanya hivyo, na yeye akiwa anatetemeka mkono akainua maji na kuanza kuyanywa, kwanza alianza kwa fundo dogo, baadaye akaongeza, na lipoona yananyweka akaanza kuyanywa kwa kasi kama alivyofanya mzee wake…..na alipomaliza, kugeuka kumwangalia mzee wake, macho yakamtoka kwa pima….akaanza kutetemeka…..

NB Je ni kweli kula amini kuna madhara, kama yapo kulitokea nini katika kisa chetu hiki, hebu tuwe pamoja kwenye sehemu hii muhimu, nawatakia wikiendi njema

WAZO LA LEO: Katika maisha yako, katika shughuli zako, na kwa kila jambo unalotaka kulifanya jenga tabia ya kuwa mkweli na jitahidi kutenda haki. Ukiwa mkweli na ukasimamia kwenye haki, katu hutashindwa kwa lolote lile, katu hutayumba katika maisha yako, baraka amani na upendo, vitakuwa ndio maisha yako. 

Twawatakia IJUMAA NJEMA


Ni mimi: emu-three

8 comments :

Anonymous said...

Good answer back in return of this matter with firm arguments and telling all concerning that.
Take a look at my web page ; satilik daireler ankara

Anonymous said...

bear grylls messer
Feel free to visit my website bear grylls messer

Unique said...

Mh hapo hata mimi natetemeka... I wish hata huyo kijana wa mzee Hasimu angekataa maana anajua fika ni uwongo uliotengenezwa. thanks for writing, weekend njema kwako pia

Anonymous said...

I’m not that much of a online reader to be honest but your sites really nice,
keep it up! I'll go ahead and bookmark your site to come back down the road. All the best
Feel free to visit my web page ; panota.com

Anonymous said...

Simply want to say your article is as astounding.
The clearness in your post is just great and i could assume you're an expert on this subject. Well with your permission let me to grab your feed to keep up to date with forthcoming post. Thanks a million and please continue the gratifying work.
Also visit my weblog : cleaning house

Anonymous said...

I almost never write comments, however I browsed some of the remarks on "Uchungu wa mwana aujuaye ni mzazi-41".
I actually do have a couple of questions for you if you don't mind. Is it only me or does it appear like a few of the comments come across like they are left by brain dead visitors? :-P And, if you are writing on other online social sites, I would like to follow you. Would you list of every one of your public sites like your Facebook page, twitter feed, or linkedin profile?
My blog :: lacustomfinish.com

Anonymous said...

kaka mbona kimya kunani.

Anonymous said...

[url=http://buyallopurinol.download/]buy allopurinol[/url] [url=http://clomid.click/]clomid[/url] [url=http://colchicine.pro/]colchicine[/url]