Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Thursday, December 13, 2012

Uchungu wa mwana Aujuaye ni mzazi-38




Malikia aligeuka na kwamwangalia mumewe, ambaye alikuwa kihangaika kuweka  silaha yake kwenye chombo chake. Tabia ya mume wake imekuwa hivyo siku zote, kujituma kwenye kazi, hata zile kazi ambazo alitakiwa awaachie watu wafanye, bado alikuwa akizifanya yeye mwenyewe, haikuonyesha tofauti ya maisha yake kabla ya huo wadhifa  na sasa hivi akiwa mtu  mkubwa katika jamii yao. 

Malikia aliweka alisimama na kutaka kumsogelea mumewe pali alipokuwa akihangaika na silaha yake, lakini akasita , na baadaye akasema, huku akitabasamu.

‘Mume wangu hizo sio kazi zako kwa sasa unatakiwa uwaachie watu wako wazifanye, wewe ni mtu wa kutoa amri tu..na kupata muda wa kufikiria mambo mbali mbali ya jamii yako’akasema mke wake akijua kwa hakika kuwa mume wake hataweza kukubaliana na wazo hilo.

‘Mke wangu, kuwa kiongozi , sio kuwa bwana mkubwa …sio kuwafanya wenzako watwana, kama lipo la kufanya na ninaweza kulifanya siwezi kusubiri mpaka nifanyiwe, hiyo sio hulika yangu…na natumai hiyo sio hulka ya kiongozi bora anayehitajiwa kuwa mfano kwa jamii’akasema mume wake.

‘Lakini huoni kuwa watu wako watajisikia vibaya, na kujiona kuwa hawawezi kazi….walitarajia uwatume, na wewe hufanyi hivyo, kazi zao unafanya wewe…?’ akauliza malikia.

‘Hapana sio kazi zao ni kazi zetu…kila mmoja anatakiwa kuamini hivyo, kuwa kazi zote ni zetu, na kama ni zetu, basi tuwajibike kwa pamoja. Tukijenga hulka ya kutegeana kuwa mwenzangu atafanya kazi hii, hii kazi ni yake, sifanyi….’hapo akatulia kidogo akiwaza.

‘Kazi zitasimama, na kama ni makasia kwenye boti, boti litayumba, na mtazama…mimi nawakubali sana watu wangu, wana kazi nyingi sana, wakati mwingine nawaonea huruma, kwani wanahangaika kwa shughuli nyingi toka asubuhi, hadi usiku, ….’akatulia akihakikisha silaha yake kuwa ipo safi, halafu akasema;

‘Mimi kama binadamu, ambaye nimepitia mazingira ya shida, ya kuhangaika, na kuwajibika  nayajua hayo yote, jinsi gani mtu anavyoamuka asubuhi, akiwa hajui atakula nini, hajui atawalishaje watoto wake, na anadamka kwenda kibaruani kuwajibika, mwili hauna nguvu, maana hakupata cha muhimu jana yake, alitaabika, ..hapana, lazima niwaonee huruma wanajamii wenzangu’ akasema akionyesha uso wa uchungu.

‘Mke wangu tabia yangu na jinsi ninavyofanya, .usijali kabisa, kwani ndivyo nilivyozoea, na nataak niwe hivi wakati wote, hizi kazi ni kazi ndogo sana kwangu,…ninajua nina  kazi kubwa, tuna kazi kubwa mbele yetu,…hilo nalo linahitaji kutafakari, na linahitaji vichwa vya pamoja,…mimi peke yangu sitaweza kutimiza, au kuwaza kila jambo….lakini mwisho wa siku najua mimi, na wewe ni wazazi wa jamii yetu.’akasema huku akiining’iniza silaha yake vyema kwenye bega lake.

Mkewe akamwangalia na akaona katika kuiweka ile silaha, nguo zake zikawa zimejivuta kwa juu, akamsogelea na kuziweka zile nguo vyema, akazinyosha na kuiweka silaha vyema kwenye bega la mume wake, namkono wake akaupeleka kwenye shavu la mumewe, na kusema;

‘Sipendi mume wangu ujichoshe na kuuchosha mwili wako  kiasi kikubwa…..na najua kuwa kweli kama kiongozi kazi iliyopo mbele yetu ni kubwa sana, yenye lawama nyingi, lakini kazi nyingine za utawala ni za kushirikiana, wewe ni kama kiongozi,…kuongoza kuwa kazi zinakwenda kwa mujibu wa makubalionao, au sio?’ akamwangalia mumewe machoni.

Mume wake akawa kama anakwepa kumuangalia mkewe usoni moja kwa moja, alikuwa akitaka kutafakari jambo, lakini hakuweza kumwambia mkewe ampe nafasi hiyo, akijua huo muda ni wa kwake na famlia yake…

‘Mume wangu cha muhimu ni kugawana majukumu, ili utendaji uwe kwa haraka na uzito wa kutenda, kuwaza na kuwajibika uwe kwa wote, usijitwike mzigo usioweza kuubeba peke yako…utachoka kabla hujafika mbalio….’akatulia huku akiangalia mkono wa mume wake uliotuna kama mtu anayeinua vyuma, mkono unaosikia kwa kazi.

Mume wake ni mshindi katika mapigano, na hata anappambana na wenzake katika miereka , kulenga shabaha,…na hata kubeba mizigo mizito, wakati wote anakuwa wa kwanza, …pamoja na hayo akili yake ni nyepesi kuwaza jambo, lenye manufaa, na akiona jambo hilo linahitaji kufikiria, huwa hapendi kutoa maamuzi hapo hapo, huomba muda wa kulitafakari, na akija kutoa rai yake, inakuwa yenye tija.

Mume wake alipoona mkewe anakuwa karibu yake sana, na muda unakwenda, na anahitajika kuwahi kazini, akamsogelea mkewe na kumshika begani kwa mkono mmoja, wakawa wanatizamana moja kwa moja, hakusema kitu kwa muda, ….na mkewe akatabasamu, , yeye alibakai vile vile na uso wa kutafakari, halafu akasema;

‘Ni muhimu kuelewa hivyo, kuwa kazi zote ni zetu sio jukumu la kiongozi peke yake, lakini je wote wanaelewa hivyo, najua kama kiongozi mkuu, natakiwa nihakikishe kila kitu kinakwenda sawa, na ili hilo lifanyike natakiwa niwe mfano, kwani uelewi wa wengine unahitaji kuona unavyotenda, na wengine hujituma zaidi kiongozi wake akiwajibika…..nataka nifanye kila njia, kila namna ili kila mtu anielewe…’ akatulia na kuangalia nje.

‘Kwanza ni kweli nahitaji kuwa na watendaji wanaojituma na wenye uchungu na jamii yetu , lakini kinachonitia wasiwasi ni kuwa  wengi ninaowajua wanatoka kwenye ukoo wetu, na hili naliogopa kwani tukijaza viongozi wote kutoka kwenye ukoo wetu, wengine watatulaumu, na hapo ndipo ninapohisi kuwa kuna umuhimu wa kumtafuta kijana wa mzee hasimu, na viongozi wengine kwenye koo ndogo ndogo  ili ….tuwe pamoja…...’akatulia na kuwaza.

‘Sasa utampataje huyo kijana, na je atakubalina na ombi lako hilo kuwa unataka uongozi wa pamoja,….ukumbuke walishasema wao hawatshirikiana na sisi kwasababu huna sifa ya kuwa mfalme,….walikengeuka, na kusahau yote waliyotabiri huyo mtabiri waliyekuwa wakimsfikia. Utabiri huo walitaka uangukie kwao , kwa wengine wanaona sio sahihi….’akasema malikia.

‘Ndivyo ilivyo , kama binadamu inapofika kwenye masilahi, kwenye sehemu ambayo anaona atapata kile anachokihitaji, hutafuta kila mbinu , …na wengine huondoa kabisa ubinadamu,…..ubinafsi unatawala nyoyo,….lakini hatima ya yote ni matakwa ya wanjamii, …je ubinafsi huo utakuwepo mpaka lini, je hatuwaonee huruma wengine, kuwa na wao ni banadamu kama wengine….hapana hapo ndip ninapoona wenzetu wanakosea’akatulia kidogo.

‘Wanakosea ndio na wanajua hilo,….ndio maana walikuwa wakifanya kila mbinu hata kuzitumia sheria ili ziwafae wao, na kuzigeuza geuza kwa maslahi yao…sasa wanaogopa, maana sheria zile zitawaumiza wao, …ndio maana wamekimbia’akasema malikia.

Malikia akatulia na mawazo ya kumshukuru mungu yakamjia , akapeleka mikono yake mbele na viganja vya mikono vikawa vinaangalia juu, na yeye akaviangali vile viganya akawa anasema kimoyo moyo;

‘Ahsante mungu kwa kunipatia mwenza mwenye mawazo na hisia kama zangu, asente mungu kwa kunirejeshea mume wangu, ahsante mungu kwa kunikubalia maombi yangu, nakuomba uijalie ndoa yetu iwe ya fanaka na baraka…’akatabasamu na hapo akageuka na kumsogelea mume wake ambaye alikuwa akijiandaa kuondoka kwenda ofisini kwake.

Mume wake akageuka na kumwangalia mkewe akahisi kuna jambo zaidi linalimsumbua mkewe, na ilionekana kama anasita kumwambia, akasema;

‘Vipi mke wangu nakuona una jambo zaidi moyoni mwako, nakuomba mke wangu kama lipo jambo niambia mimi ni wewe na wewe ni mimi,…..je kuna tatizo?’ akauliza mfalme mtarajiwa.

‘Hakuna tatizo mume wangu, nilikuwa na mawazo mengi kichwani, lakini yote hayo yalifutika pale nilipokuangalia, namshukuru sana mungu, kwa kukurejesha , maana mengi yaliyopita huku yalishatukatisha tamaa, na hata kufikia kusema wewe umeliwa na mamba, na ukiliwa na mamba maana yake una dhambi…..hilo ndilo limenifanya nitulia na kumshukuru mungu wetu’akasema malikia.

Hapo mfalme mtarajiwa akatulia na ile haraka ya kuondoka ikatoweka kwa muda na kumuuliza mkewe

‘Ina maana hata wewe ulishaamini kuwa nimeliwa na mamba?’ akauliza.

‘Sikuamini   kabisa, na sijui ni nani alilikata kata lile ua…nilipoliona limesambaratika, kwa kweli nilishituka hadi kupoteza fahamu….lakini nilipotulia na kuanza kufuatilia tena na kugundua kuwa ua hilo halikuwa limenyauka, bali ni mtu alikuwaja akalifinyanga finyanga na mkono…nikajua hapo kuna jambo, nikajua bado upo hai,….’akatulia.

‘Binadamu ni mwerevu sana,…hapo unaona jinsi tulivyo, hakuna siri ….na ukiwaza hivi kuna wengine walishawaza, na wana kipaji cha kujua unawaza nini……mimi niliwahi kuambiwa na wazee wa kule makaoni kuwa ukisafiri safari yenye mashaka unahitajika kumpa mkeo ua,….ua hilo ni sihara ya upendo, na ili mkeo awe na hisia za upenzo, atatii yale uliyomuagiza na ua lile litasimama kama mwenzako….’akatulia.

‘Ni kweli pia hata babu aliniambia hivyo, kuwa katika imani zao, ua linasimama kama ishara ya upendo, na ukiliombea vyema, …litasimamia zile hisia zetu, na kama hisia zenu zipo pamoja, ua lile litaendelea kuchipua,…kunawiri, lakini hisia zikitengemana, basi ua hilo hunyauka,….na huenda mmoja wenu akawa hana uhai tena….’akatulia hapo.

‘Inawezekana ikawa sio uhai wa kuishi, lakini uhai wa kuwa pamoja….ingawaje wazee wetu waliniambia likinyauka ni kuwa maisha ya mmojawapo yamenyauka, lakini mimi sikuwa nimemini hivyo moja kwa moja….na kama ilifikia hadi wenzetu wakajua hio, basi imani hiyo ina nguvu, na hapo tumejiunza jambo, lakini nisingelipenda kutumia imani hiyo kwenye mapenzi yetu’akatulia kidogo.

Mkewe akamwangali kwa muda na kulikumbuka hilo swali la mumewe kuwa kama yeye kweli aliamini kuwa mumewe keshafariki kwa kuliwa na mamba, alitamani ile hali aliyokuwa nayo aipeleke kichwani kwa mumewe akumbuke jinsi gani alivyokuwa akiteseka, na jins gani alivyokuwa akipingana na mawazo hayo kuwa mumewe kshafariki….na…., hapo akasema;

‘Katika hali iliyokuwepo …. ungelifanyaje ….nilikuwa katikati ya watu na majukumu yao waliyojipangia, mimi kama mimi, nilishaamua kutokukubaliana nao, na hata huo umalikia sikuutaka tena kama ni lazima niolewe na mtu mwingina, nilishaamua  nikusubiri, lakini babu ndiye aliyenipa moyo, na kuniambia jukumu hilo halikimbiwi, na yakkuwa mimi sio mama wa ukoo wanu tu, ni mama wa koo zote…’akasema na huku akiangalia nje, alishaona kuwa anamchelewesha mumewe.

‘Mke wangu, najua jinsi ulivyokuwa kwenye wakati mgumu, nilihisi hivyo, lakini sikutegemea kuwa mambo yangelichukuliwa kwa haraka kiasi hicho, najiuliza je kama ningelichelewa ingelikuwaje, …kama ningelifika hapa nikute umeshaolewa na huyo kijana wa mzee hasimu ingelikuwaje? ‘ akauliza mfalme mtarajiwa.

‘Mume wangu kila kitu hupangwa na muumba, kama alipanga tuwe nawe, isingeliwezekana iwe hivyo, ndio maana imekuwa hivyo….hilo amini, na yote tunayofanya binadamu ni kutimiza wajibu tu,lakini mwisho wa siku ndio unaosema na hutendeka hivyo inavyotakiwa’akasema malikia huku akimwangali mumewe usoni. Na wakawa sasa wameangaliana.

‘Mkewe wangu sijui niseme nini, maana katika kutimiza majukumu yangu huenda nimetelekeza, na siina budi kukuomba msamaha, na naomba tuwe pamoja na tushirikiane kwa kila jambo, kama utaona nimeteleza, niambie,…na yaliyotokea huenda yalitokea ili niweze kutimiza majukumu yangu’

Mke wake akatulia na kumwangalia mumewe kwa makini alitaka kumuulizia kwanini afikie kuomba msamaha, kuna nini kikubwa alikitenda na kabla hawajaongea zaidi mara mlango ukagongwa, na ikabidi mazungumzo hayo yakatishwe.

Mfalme mtarajiwa alitoka na kuongea na mlinzi wake, baadaye akarejea na kumkuta mkewe akiwa kasimama akiangalia nje ,

‘Mke wangu inaonekana wahasimu wameshakusanya kikosi chao cha maaskari na inaaminika kuwa wapo kwenye ngome yao muhimu, hatujui wana maana gani, na kwa hilo inabidi tujiandae kwa lolote na hata ikibidi kuingia vitani kwa maslahi ya wanajamii….’akasema mfalme.

‘Vitani……?’ ‘akauliza malikia mtarajiwa akiomba hilo lipitie mbali.

NB: Inabidi tuishie hapa kwa leo.., tupo pamoja.

WAZO LA LEO: Upendo wa kweli ni ule unaojengwa na hisia za pamoja, na akili , mwili na matendo yakashabihiana kama mapacha. Na wengine hufikia kusema wanandoa hawo wanafanana kama mapacha. Hili linawezekana kama kila mmoja atajua kuwa yeye na mwenzake ni kitu kimoja. Mkifanya hivyo kwa upendo wa dhati, mungu huwabariki mkafanana hata kisura.

Ni mimi: emu-three

1 comment :

Unique said...

Ahsante sana kwa kuandika. Nilipotea mtandaoni kwa muda kiasi, leo ndio nimeianza hii story na kufika hapa ulipo, dah yani niliingia katika ulimwengu mwingine kabisa. Ni kisa cha kusisimua nawe ni mwandishi mzuri. Cheers!!