Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Tuesday, October 30, 2012

Uchungu wa mwana aujuaye ni mzazi-16



Binti Kis kama walivyokuwa wakimuita, akiwa keshafika ndani ya jengo takatifu, ghafla woga ukaanza kuiteka nafsi yake, akihis sura nyingi za watu zikimtizama, na moja wapo ilikuwa ya yule mzee anayetisha, na huku akikumbuka maelezo mengi yanayosimulia kuhusu mahali hapo,  mwanzoni alikuwa haogopi, lakini pale mguu wake ulipokanyaga eneo jeupe la aradhi ya sehemu hiyo akili mwili ulilegea.

Akawa kaam sio yeye, akawa anatembea kwa uwoga, na ile hali ilimfanya awe kama mgonjwa anayejikokota kufika kituo cha matibabu, na huku akili yake ikianza kukumbuka yale aliyowahi kusimuliwa na bibi yake kuhusu eneo hilo, na sauti ya bibi yake iliposikika kwenye ubongo wake,akahisi ageuka na kuanza kukimbia kutoka eneo hilo.

Lakini cha ajabu hakuweza, miguu yake ikiwa imeisha nguvu, akwa anajikongoka kuelekea sehemu kulipojengwa jengo, na humo ndani kuna mahadaki mengi, ambayo humilikiwa na koo mbali mbali kama ofisi zao, na sauti ya bibi yake ikaanza kumjia akilini ikimuelezea kwanini eneo hilo likaitwa mahali patakatifu;

‘Mjukuu wangu enzi zetu tulipohamia hapa nilikuwa bado mbichi, mwali ambaye alikuja kula fungate na mume wangu mpenzi, nilikuwa nampenda sana, kama alivyonipenda mimi,, huyo ndiye babu yako ambaye aliponioa tu, ikaja taarifa hiyo kuwa baadhi tunahamia makao mapya, yalibashiriwa, na mimi niliipokea taarifa hiyo kwa furaha.

‘Ina maana ulifurahia kuwaacha wazazi wako na kwenda kuishi sehemu ngeni?’ akauliza mjukuu.

‘Unapoolewa ujue utamuacha mama na baba yako, hata kama unawapenda vipi, na hili tulishaambiwa na mashangazi, na walimuw ajadi, kuwa mume wako sasa ndiye atakayekuwa mzazi wako wa pili, yeye na wewe mnakuwa kitu kimoja.

‘Ndio kuna ilehali ya kuhisia hivyo, kwa vile wazazi ni wazazi, hawawezi kuwa mtu mwingine,na uchungu wa mwana aujuaye ni mzazi,lakini lazima ndoa iwepo, lazima mume na mke wawepo, ili kujenga kizazi kipya, na vyema yake ni kukipaat hicho kizazi mkiwa wawili, mke na mume...

Mimi kwa usichana wangu na kazi nyingi zanyumbani, nilikuwa najiona nachoka sana,nikajua kuwa anenda kuolewa na nitapata muda wa kuwa na mume wangu ambaye kila mara nilikuwa nikfokwa pindi ninapotaka kwenda kuongea na yeye, sasa nitakuwa huru,kwanu  keshanioa, na tunakwenda kuanz maisha ya raha, maana kuolewa wengi tunajua hivyo, kuwa umeshampata mwenzako unayempenda, basi mtaishi kwa raha…’

‘Siku babu yako aliponiambia kuwa tunekwenda eneo jipya, ili tuweze kuwa huru zaidi, nilimwambia, kokote unapotaka kwenda mimi nipo na wewe na nipo tayari kwenda, kwani mimi ni mkeo wako nipo tayari kwa ajili yako, na nitatii kila utakachonielekeza nikifanye, najua yote uliyopanga ni kwa ajili yetu sote’,

‘Lakini huko tunapokwenda koo nyingi zimepanga kwenda huko, huenda tukaanza kugombana wenyewe kwa wenyewe, kwahiyo ujiandae kwenda kuishi maisha ya vita’akaniambia, na mimi nikakubali sikujua lolote kuhusu vita, maana nilichukuliwa kwenye mikono ya wazazi wangu nikiwa nalelewa kama mtoto, licha ya kuwa vita vilikuwepo vya hapa na pale,lakini sisi watoto tulichungwa sana, tulilindwa kuhakikisha kuwa akili zetu hazitekwi na mambo ya kivita.

‘Mimi na babu yako tukaanza maisha, lakini siku zote yeye alikuwa msituni, wakipigana, na wakati mwingine anarudi akiwa kaumia , ana majeraha kila sehemu ya mwili,  mimi ndiye nahangaika kumtibia, na ingawaje ujuzi wa matibabu niliupata toka huko kwetu, lakini uzoefu zaidi wa kutibia watu walijeruhiwa kwenye vita niliupatia kwenye eneo hilo takatifu.

Kila mume wangu aliporudi na kumtibia akapona haraka ndivyo taarifa za ujuzi wangu zilivyozidi kuzagaa, na hata kutolewa kwenda mstari wa mbele wa vita kuwatibia majeruhi. Nikawa sasa naishi vitani, natabia watu walioumia, na wakati mwingine naitwa majumbani kama kuna wakina mama wanaotaka kujifungua, au watoto wagonjwa nikawa tibabu wa eneo lote hili.

‘Eneo hilo takatifu  ndipo babu yako alipofarikia, akiwa akimtetea mfalme, kiongozi wa kwanza ambaye tulihama naye, alijitoa nafsi yake kuhakikisha kuwa kiongozi huyo haumizwi, na alikufa kifo cha kishujaa..’akasema bibi.

‘Kifo gani hicho, cha kishujaa,mbona sisi hatupo kwenye eneo takatifu na kutambulikana kama wafamilia ya watu mashuhuru, hata kuolewa nimekataliwa eti sisi sio familia mashuhuri?’ akaulizwa bibi.

‘Eneo hio kila mmoja likuwa akiligombea, kwani ndilo walilotabiriwa kuwa ni eneo takatifu, na kila ukoo ulitaka ulimilki , kwahiyo kila kiongozi wa ukoo, alifika hapo na jeshil lake, kukawa na mapigano ya huku na kule, kila mmoja akipigana na mwenzake.. wakati mwingine ni vita vya kuviziana, huyu akimuone mwenzake ni ukoo wa mwingine anajitahidi amuue, ....

Babu yako yeye alikuwa mlinzi wa kiongozi wa ukoo wetu, na katika vita hivyo, ikatokea tukazidiwa na kiongozi wetu akazingirwa, babu yako akawa anapigana nao, na kuna muda wenzao maadui walitupa mishale, babu yako akajiweka mbele ya kiongozi wake, na mishale ile ikazama mwilini mwake, ….’akasema bibi kwa uchungu.

‘Na huyo kiongozi ikawaje?’ akauliza.

Yule kiongozi alipiga magozi akawa anamlilia babu yako, huku akiwa haamini, na hutaamini wengi wa viongozi wakafanya hivyo wakapiga magoti, kila mmoja akimlilia mlinzi wake, maana maaskari wengi walishafariki, waliobakia ni majeruhi tu.

Na kumbe huku tulipotoka walishafikia uamuzi watume jeshi kubwa kuja kudhibiti hiyo hali, jeshi lilipofika ndio likakuta hiyo hali imeshakuw ambaya, waliobakia ni viongozi wa ukoo, na mjeruhu wengi,wakavamia na kuwaweka wote chini ya ulinzi, na amri ikatolewa kuwa hakuna kupigana tena, kwani mizumu na mababu waliozikwa eneo hilo wamekasirika.



‘Mtamwaga damu zenu mpaka lini, hamjui nyie ni ndugu, mkirudi kinyumenyume kimaisha babu zetu walikuwa ndugu baba na mama mmoja, wakazaliwa hadi mkafikia kizazi chenu nyie, leo hii mnawakata matumbo wazee wenu,maana kuuana ni sawa ni kuwakata wazee wenu matumbo yao…

‘Sasa basi,amri moja, sitisheni vita na toka leo eneo hili litakuwa takatifu, sheri mtapewa kutoka huko mlipokuwa awali, kuwa eneo hili halitakiwi madhambi tena, kila mmoja ni lazima afuate sheria hizo na yule atakayekiuka adhabu kali itamuandama, na ikithibitishwa kuwa yeye ndiye mkosaji, atatoswa kwenye mto,huo mto umejaa mamba waliokuwa wakifungwa na wazee waliokuwa wakiishi hapa awali,..mamba hao ni wakurithi, wana baraka zake,kazi yao ni kula miili iliyotenda dahambiili hizo dhambi zipotee kabisa, ….

‘Sasa toka leo yule mkosaji atatupwa kwenye huo mto,..’ ikatolewa amri na kiongozi mpya akachaguliwa, na viongozi wengine wa kila koo, sisi hatukupa nafasi hiyo, maana watoto wangu walikuwa bado wadogo, walikuwa kwenye jeshi jipya. Na tangu siki hiyo ikawa sheria msimeno kile mkosaji hakuonewa huruma, akawa anatoswa ziwani, mpaka watu wakaanza kuogopa. Ilifikia muda mtu akifanya dhambi kwa siri, anajikuta kafichuliwa bila hata kujua ni nani aliyefichua hiyo siri, watu wakaanza kuogopa, na sheri ikaanza kufuatwa…

‘Kwahiyo mjuu wangu ukifika kwenye eneo hilo takatifi usije ukajidanganya kuwa hauonekani, wapo watu waliokufa hapo kwenye vita wanakuona, roho zao kila mara zinapita kupalinda hapo mahali,na mwenyewe ukifika mhali hapo, kama ni mkosaji utajihisi kweli wewe ni mkosaji, uatahisi watu wanakuangalia, wanakupigia makelele, na unaweza ukadondoka na kupoteza fahamu….’maneno ya bibi yake, yalimfanya ahisi kuwa yeye ni mkosaji,na alipohisi mwili ukisha nguvu, akajua muda wowote anaweza akadondoka na kupoteza fahamu, na alichowaza ni kugeuka nyuma na kurudi huko alipotoka.


‘Usiwe na wasiwasi, wewe ndiye mke halali wa yule mwanaume unayempenda,pigania kwa nguvu zote, huoni kila anateyka kukuoa anashidwa, usiogoe, sisi tupo nyuma yako…’akakumbuka yale maneno aliyoambiwa na mume wangu…na mara akasikia mtu akiwa nyuma yake, aliogopa kugeuka, akijua sasa anambuliwa, kumbe alikuwa mmoja wa walinzi ambaye alimwambia aendelee mbele,..

‘Hapa sasa hakuna kurudi nyuma..’akasema kimoyo moyo, na kusonga mbele, licha ya kuwa  mwili mzima ulikuwa ukisisimukwa kuashiri awoga na kuhisi kuwa hizo roho zinamuona kwa hicho anachotaka kukifanya,lakini baadaye akasema kimoyomoyo;

‘Mimi sifanyi haya kwa nia mbaya,nafanya haya kwa ajili ya mtu ninayempenda, na nina nia safi ya kuwa mke mwema kumtumikia yeye vyovyote iwavyo, tatizo ni kuwa wengi hawanijui kuwa mimi ni mke mwema….’ akasema kimoyomoyo huku akijitahidi kutembea akiigiza vile vile anavyotembea bibi yake, na wale maaskari vijana walionekana kutokumtilia mashaka, waliinama kwa adabu na yeye akapita kwa mwendo ule ule wa kibibi-kibibi.

Alishukuru sana mzaha wake aliokuwa akimfanyia bibi yake, kwani mara kwa mara alizoea kumuigiza bibi yake anavyotembea na akifanya hivyo bibi yake humkimbiza kwa fimbo. Siku moja alivaa nguo za bibi yake, na kujifunika kama anavyovaa bibi yake. Bibi yake huwa anavaa na kujifunika mwili mzima na kuacha sehemu ya macho,kwani sehemu hiyo takatifu hawafiki wanawake bila kazi maalumu na kuna sehemu ambayo anakaa malikia, ndipo hapo wanawake wanaweza kufika,

Siku hiyo alivaa kama anavyovaa bibi yake akawa anatembea kama anavyotembea bibi yake, na kupita mbele ya baba yake,. Baba yake alijua kabisa ni mama yake anayepita, akainuka na kuinama kwa adabu, baadaye akaanza kucheka.

‘Wewe binti, yaani umefikia kumchezea mama yangu, nitakupiga kipigo ambacho hutakisahau, wewe hujui thamani ya bibi yako, bibi yako ni mama mtakatifu, tibabu wa eneo hili, anaheshimik,a akipita kila mmoja huiana chini. Yeye alistahili kuwa malikia wa eneo hili, ila watu wabaya walimfanyai fitina’akasema baba yake.

‘Usimpige mjukuu wangu, huoni kuwa ananirithi, hata nikifa najua nina mtu anayelandana na mimi, na hata hivyo sikuhitaji kuwa malikia, kwani ningeliolewa tena, na mimi sikutaka kuolewa,tena, baba yako alikuwa ndiye mume wangu pekee, alipofariki, na mimi nilitaka nimfuete, ….nilitaka kujiua, na hilo tendo likaniondolea sifa ya kuwa malikia wa eneo letu’akasema.

Leo hii hakuwa anagiza, alitakiwa afanye kweli, kama alivyokuwa akifanya bibii yake, kuvaa kutembea, na kila kitu, vinginevyo akijulikana atakuwa chakula cha mamba na atamkosa yule aliyempenda,na kuwaaingiza wengine kwenye matatizo makubwa akaona kumbe kabeba dhamana kubwa, na ni lazima aitekeleze.

Akawa anawaza jinsi gani alivyofamyia bibi yake, na ilibidi afanye hivyo,kwani bibi yake asingelikubaliana na hayo anayotaka kuyafanya, akawa ana wasiwasi, akiogopa kuwa huenda dawa aliyompulizia bibi yake inaweza ikwa nyingi, tofauti na walivyoagizwa na kama ni nyingi inaweza kumuua kabisa bibi yake, kitu ambacho asingeliweza kukivumilia, kwani kama bibi yake atakufa na yeye itabidi ajiue.

‘Umpulizie kidogo tu bibi yako kwa mbali asiokuone, na akilala, chukua nguo zake, na mengine ni kama nilivyokuagiza’akakumbuka alivyoelekezwa, na hayo hakutaka kuelekezwa zaidi kwani yeye ni mtaalamu wa kuigiza, kama angelipewa nafasi hiyo angelikuwa muigizaji wa kimtaifa.

Akaingia ndani ya lile jengo na yule jemedari akainama na kumruhusu apite, hakuamini kwani sifa za huyo jemedari ni kuwa anaweza kunusa kuwa huyu ni adui, …lakini aliona ajabu ya huyo jemedari kuinama na kumuheshimu akijua kuwa huyu ni mama tibabu, bibi yake. Yeye akapita na kuingia ndani ya jengo hilo. Alipoingia huyo jemedari alikuwa nyuma yake, akachungulia mara moja kuhakikisha kila kitu kipo tayari, halafu akasema;

‘Kama unahitaji msaada wowote niite nipo hapo nje’akasema huyo jemedari , na yeye akatikisa kichwa huku akijifanya yupo kazini, kwa kuushika shika ule mwili, hadi alipohakikisha kuwa yule jemedari katoka nje. Akashisha pumzi kwa nguvu huku akimshukuru mungu wake!

Aliushika ule mwili na kuanza kuuvua nguo zote, akaupaka dawa ya kulainisha ngozi kama alivyoagizwa, halafu akazivua nguo zake na kuuvalisha ule mwili, na yeye wakati huo ameshavaa nguo za ule mwili, na alipohakikisha kuwa kila kitu kipo tayari, akauchukua ule mwili na kuulaza chini, huku akiwa kaufunika uso, na kuhakikisha kuwa hakuna atakaye gundua haraka ni nani huyo binti. Kawaida mwanamke anajifunika mwili mzima, na nguo zao maalumu za ngozi za wanyama laini.

Alipohakikisha kila kitu kipo tayari, akapanda kitandani, na kuchukua dawa kiasi kwenye kidole chake ile nyingine akawa kaificha ndani ya nguo zake akalala na kujifunika uso kama ulivyokuwa ule mwili, akaivuta ile dawa puani, na huku akapiga ukelele….akazama kwenye giza.

*******

Huku nje mume wangu alikuwa keshafika na vijana wenzake wakiwa wamejificha sehemu maalumu na kuvaa mavazi wanayotumia maadui zao, kwani kila ukoo ulikuwa na uvaaji wake,wakawa wanasubiri sihara, ishara ambayo ni kilio,..

Babu alikuwa na kikao maalumu na wazee wenzake kweye shemu maalumu, sehemu ambayo haingiliki ovyo, na hata watu wakipiga kelele huko nje huwa hawasikii, na kuna vijana wakuleta taarifa kama kuna lolote limetokea, wao walikuwa kwenye mazungumzo maalumu na wazee wenzake;

‘Jamani mimi niewaita, maana siku moja niliwauliza kwanini mwenzetu anatayarisha jeshi msituni, nyie mkasema ni jeshi la ukoo, sasa wakati umefika wa kumuuliza kuwa je hilo jeshi kama ni la koo zote mbona hawachukui vijana wa ukoo nyingine’akasema.

‘Kwani tuna wasiwasi gani, kama anataka kuleta fujo sisi tuna vijana wetu, na swala la kuwaita na kuwaandaa, na hilo haliwezi kutokea maana tuna kiapo kikuu, akikiuka wenzetu watakuja atashikwa na vijana wake watatupiwa mamba’akasema mzee mmoja.

‘Muwe na akili yakufikiri, hivi akishavamia na vijana wake, akahakikisha amechukua madaraka, na kutumaliza sisi wazee wote, akapata kura za wazee wenzake, ni nani atapata muda wa kwenda kutoa taarifa, na hata hawo wakifika huko hamuoni kuwa atakuwa keshajipanga na uwongo mwingine’akasema babu.

‘Tukuulize wewe mzee mwenzetu una lengo gani kusema hivyo, una wasiwasi gani au umekuja na hoja gani?’ akaulizwa.

‘Mimi hoja yangu ni kuwa na kikosi chetu kama hicho, na tukiulizwa majibu yetu yatakuwa kama wao, na vijana wetu wapo tayari muda wowote, ni kiasi cha kuwapa maelekezo’

‘Hilo ni wazo jema sana, na hata mimi nilikuwa nikiwaza hivyo hivyo..’akasema mzee mwingine.

‘Jingine ni kuhusu huo mwili waliouchukua kama ushahidi, ….nahitaji msaada wenu, hapo muda ukifika,kuna jambo nalifuatilia kwanza, hilo sitawaambia kwa sasa.Nafanya hivyo kwasababu tunahisi wenzetu wana lengo kubwa, na lengo lao ni kuhakikihs kuwa ukoo wetu hauna nafasi ya madakara, kwahiyo tunachohitaji ni kuhakiksiha kuwa huo mwili unarudi mikononi mwetu’akasema babu.

‘Kwa vipi naye kaushikilia na kuulinda kwa nguvu zote…na kwanini tuhangaika na maiti,?’akaulizwa.
Hilo nitakuja kuwaambia baadaye ni kwa maslahi yetu sote, vijana wetu wapo, wataifanya hiyo kazi, ila lolote litakalotokea naomba tuwe pamoja’akasema babu.

‘Tupo pamoja mkuu wetu’wakaitikia na mara akaingia kijana mmoja akihema

‘Vipi kuna nini huko?’ akaulizwa.

‘Kuna ukelele umetokea upande ule wa maadui, na huenda kuna tatizo, ..’akasema huyo kijana mtoa taarifa.
Wale wazee wakainuka na kutoka mle ndani na kuelekea huko ulipotokea huo ukelele.

WAZO LA LEO:Sio vyema ukitenda kosa kumsingizia mwenzako, kama umeona umetenda kosa ni vyema ukakiri kuwa umekosea ili kusahihiswa, unapolisukumia hilo kosa kwa mtu mwingine unakuwa umetenda kosa mara mbili, kosa la awali ulilolitenda na kosa la kumsingizia mwenzako, huo ubaya ni roho mbaya, kumbuka kutenda kosa sio kosa, bali kurudia kosa ndio kosa.


Ni mimi: emu-three

5 comments :

Anonymous said...

Nimelipenda sana wazo la leo, KUTENDA KOSA SIO KOSA KOSA KURUDIA KOSA

Anonymous said...

HONGERA KAKA

Anonymous said...

I drop a сomment eаch time I liκе a article
on а blog or I have something to vаluable to contribute to the cοnversation.

Usuallу it's caused by the sincerness communicated in the article I browsed. And on this post "Uchungu wa mwana aujuaye ni mzazi-16". I was actually moved enough to drop a thought ;-) I do have 2 questions for you if it's okay.
Could it be only mе or does it loοk aѕ if liκе some of theѕе
responses арреar liκe left by bгain ԁead
people? :-P And, іf you are wrіting at aԁditional οnline sіtes,
I'd like to keep up with everything fresh you have to post. Could you make a list every one of your communal sites like your linkedin profile, Facebook page or twitter feed?
Check out my web page - Money

Anonymous said...

Can I use some of the content from your site on mine? I will make sure to link back to it :)

Anonymous said...

First of all to see the quality [url=http://www.blackuggs4boots.com]black ugg boots[/url] of a fabric is shoes, if appear, chemical fiber, blending materials made [url=http://www.blackuggs4boots.com]UGG boots black[/url], it must is false; UGG in foreign countries is down the price also is in one thousand yuan associated with above, with hundreds of yuan extremely affordable prices for sale to be careful is fake. Genuine Uggs workmanship, especially the villi distribution denseness and length of villi are constant, watching from the work also compares is [url=http://www.blackuggs4boots.com]black uggs[/url] fine, light foot wear will be very comfortable, will not have a stiff feather firm feet feeling, and shoes self-respect is very light, no weight sensation.



---------------------------------------------------------
[url=http://www.blackuggs4boots.com]black uggs[/url] [url=http://www.blackuggs4boots.com]black uggs[/url]