Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Thursday, October 18, 2012

Ndugu wakigombana chukua jembe ukalime....



Nilishangaa nilipokutana na `school mate’(yaani jamaa tuliyesoma naye) mitaa ya Kariakoo, akiwa kabeba vifaa vyake vya biashara, akaniambia anakwenda kwenye duka lake. Nikajiuliza kichwanii huenda katoroka kazini , na kwenda kuangalia duka lake mara moja, lakini alivyo , yaani nguo na muonekano wake ulikuwa sio wa kiofisini, kama nilivyokuwa namjua awali.

‘Kwani kazini vipi?’ nikamuuliza.

‘Kazini wapi vipi bwana, mimii siku hizi nimejiajiri,nimeacha kazi za kuajiriwa muda mrefu mbona, baada ya wao kutangaza kuwa anayetaka kupunguzwa ajiorozeshe,mimi nikaona ndio nafasi yangu, ili angalau nipate msingi, msingi ambao kwa kwelii umenisaidia, ingawaje ulikuwa mdogo, lakini niliweza kufungua duka langu,na nashukuru mungu, watoto wanakwenda choo’akasema huku akitabasamu.

Nilimuangalia jamaa yangu huyu, na kukumbuka maisha yetu ya shuleni, kwani darasani alikuwa ni wale wenye kipaji maalumu, alikuwa akifanya vizuri sana hata mtihani wa mwisho, alikuwa mmoja wa waliofanya vyema kitaifa, na kuchaguliwa kwenda chuo kikuu.

Yeye alipomaliza chuo kikuu, ndio akaajiriwa kwenye kampuni hiyo kubwa hapa nchini, na nikajua kuwa hatachukua muda, kwa jinsi alivyo na akili, atateuliwa kuwa bosi ,au kupelekwa nje kusoma zaidi,maana akili aliyo nayo sio ya mchezo. Leo hii nakutana naye mitaa ya Kariakoo, kavaa kimitaani, sikuamini.

‘Ndugu yangu nilichoka na maisha ya ofisini, niliona napoteza muda wangu, na akili yangu bure na mwisho wa siku naishia kuchanganyikiwa, maana juhudi, akili na kujituma kwangu kote mwisho wa siku unapata eti kinachoitwa mshahara, mshahara wa siku thelathini, mimi huo naweza kuupata kwa siku mbili, katika biashara zangu….hebu angalia ningelijua hilo mapema ningelikuwa wapi,lakini bado sijachelewa..’akasema akiangalia saa yake.

‘Ina maana biashara yako ni kubwa sana?’ nikamuuliza.

‘Sio kubwa ya kutisha, ni ya kawaida tu, mimi sio mwizi,mimi sio fisadi ndio maana nimeamua kutafuta chumo halali, na kiukweli mimi sifanyi biashara ya kilanguzi, nafuata sheria, kwahiyo faida yanguu ni ya kawaida tu, ninachotumia ni akili yangu na elimu yangu tu’akasema.
‘Sasa niembie kwanini uliacha kazi,maana mimi naona unapoteza hazina, elimu uliyo nayo ni hazina kwa taifa, ulitakiwa uitumie vyema ofisini, kama ulivyosomea?’ nikamuuliza.

‘Sizani kama serikali inanihitaji mtu kama mimi, mimi ni mtoto wa mkulima, masikini, ambaye hana usemi mbele ya watoto wa wakubwa, sikupenda kuacha kazi, wakati nimesoma, nimetumia muda mwingi shuleni hadi chuo kikuu, lakini niliona kama nitaendelea kuwa kazini, nitaishia kubaya, ningeliweza kufa kwa kihoro, au kupatwa na ugonjwa wa moyo, au kiharusi.

‘Kazini,sisi watoto wa wakulima,mshahara wetu unajulikana, sio sawa na watoto wa wenzetu, waliosoma nje, …hili liliniuma sana.Hayo ni madogo tu, lakini kuna mambo yalikuwa yakitendeka humo ndani, mimi sikuyapenda,…uhujumu wa mali, ubinfasi wa wakubwa, na utendaji mbovu, ulinifanya nifikirie mara mbili. Usione mashirika yetu hayo, yaliyokuwa yakiitwa ya Uma yamekufa, yaliuliwa na sisi wenyewe,kwa mpango maalumu, …inaniuma sana.

‘Mimi akili yangu sio ya kutapeli, sio ya kufanya ujanja ujanja ili nipate kipato kisicho halali, akili yangu ni kufanya kile nilichokisomea, ili mwisho wa siku nione manufaa yake, kifamilia, kiofisi na kitaifa, lakini sivyo ilivyokuwa. Na sikuweza kupewa nafasi hiyo, na nilionekana kama `kipingamizi’ fulani…

‘Wenzangu wakifika ofisini wapo na juhusi ya kutafuta `dili’ wanatafuta masoko, ambayo yatawapatia `teni parcent’ yatawaingizia kitu,angalau kwa siku wasikose chochote,na kuna safari ambazo kila mtu alikuwa akizipigania, watu wasafiri, ili wapate marupurupu, humo kuna madudu yanafanyika, maana mtu anapewa fungu,lakini halifanyi kazi iliyotakiwa, ili akirudi awe na akiba…, kuna spea bandia zinanunuliwa, zinaandikiwa kuwa ni spea mpya….aaah, mimi nilishindwa, kwani sikukosomea hayo..

‘Rafiki yangu, aliye nacho anacho, sisi huenda tulitakiwa tuwe wasindikizaji tu, huenda tulipata nafasi ya kusoma ili ijulikane kuwa kila mtu kapewa nafasi hiyo, lakini kiukweli, wapo wanaotakiwa kufaidi, wapo walioandaliwa, na ndio hawo wanaoshika madaraka,kila kukicha,…mimi niliiona hiyo hali nikasema,ngoja nisije nikaja kuujutia umri wangu bure, nikajitoa mapemaaa.

‘Nilichofanya ni kubuni aina ya biashara, nikitumia elimu yangu, nikagundua kuwa nguvu zangu hazitapotea bure, kwa kuanzia ilikuwa sio kazi rahisi, maana ili upate leseni, inabidi uende maofisini tena, kuna makodi yasiohesabika,…lakini ilibidi iwe hivyo, na sasa sijutii uamuzi wangu huo, na hata siku moja hutaniona nikikatisha maofisini eti ninatafuta kazi, nitaenda kwamambo mengine...

'Mimi nimesoma na vyeti vyangu vipo, vizuri tu, lakini elimu yangu sio vyeti, elimu yangu ipo hapa kichwani,...'akashika kichwa chake kwa kidole. Lakini vyeti, au kutahiniwa, sijui `interview' kwangu hiyo elimu, ni kutafutana ni nani mwenzetu. Nasema hivi,hivyo vyeti vyangu watakuja kuvisoma watoto wangu, ili wasije kusema baba hakusoma. Wao nawasomesha nataka wafike mbali zaidi, najuaa huko mbele huenda mambo yakabadilika, sijui lini.....

Mara daladala likaja akaingia na kuondoka zake na kuniacha mimi nikiwa nimeduwaa, sikuamini, lakini ndivyo ilivyo. Nilibakia pale nikjiuliza hivi kweli ndivyo ilivyo, kuwa kuna watu ambao hatuna nafasi, tupo kama wasindikizaji tu, hata tufanye nini, tutaishia kumeza mate huku wenzetuu wameshika uma na kijiko,mezani kuku, pembeni kuna gari sijui linaitwaje….

Haya ndiyo maisha yetu, na ndio hali halisi ya maisha yetu, inabidi tukubali kuwa, kila mtu ana maisha yake, na ana mtizamo wake, lakini tukumbuke (angalizo) kuwa, kila linalotokea usilichukulie juu juu  tu, lina sababu. Na wenzetu wanalijua hilo, na wanajua kuwa wengi wetu tutayachukua kama yalivyotokea, na kuishia kubishana, kunyosheana vidole, hata kupigana…na ndio lengo lao, wakati nyie mnabishana, wao wanasonga mbele.

Nikakumbuka huo msemo kuwa `ndugu wakigombana chukua jembe ukalime, na siku wakipatana,(kamakweli watapatana) maana dunia hii sijui kama kuna kupatana tena, wewe chukua kapu ukavune!

Tupo pamoja daima.


Ni mimi: emu-three

13 comments :

Anonymous said...

Heу theгe! Тhis pοst coulԁ not be wrіtten any
bеtter! Reаdіng this pоѕt
remindѕ me of mу olԁ room mate!
He always kеpt chatting about this. I will fοrward this
ωrite-up to him. Fairly certain he will have a good read.
Mаnу thanks fοr shаring!
My site ; allergy rash pictures

Anonymous said...

Hii imenikumbusha mbali kweli, visa vyako ni vuzuri vina mafundisho, ingeliwezekana ukawa anatunga vitabu kwa ajili ya wanafunzi , hasa wa nje ambao wanahitaji kujifunza kiswahili. Hapa nchini wengi hawapendi kusoma vitabu

Anonymous said...

It was excited to come across your site a short while ago. I arrived here today hoping to learn interesting things. I was not upset. Your well thought out ideas with new strategies on this subject matter were enlightening and a great help to me. Thank you for making time to create these things and for sharing your mind.

Anonymous said...

bear grylls messer
my site - bear grylls messer

Anonymous said...

Plеaѕe let me know if уοu're looking for a writer for your weblog. You have some really great articles and I feel I would be a good asset. If you ever want to take some of the load off, I'd аbsοlutеlу lοvе
to ωrite some articles fοr youг blog in exchangе fοr a lіnk back tο mіne.
Ρlеаѕе ѕend mе аn e-maіl if interested.
Regardѕ!
My site ; payday loan

Anonymous said...

I am sure this paragraph has touched all the internet viewers, its really really nice paragraph on building up new
blog.

My web site; fortitude
My web site: curve

Anonymous said...

This site was... how do you say it? Relevant!! Finally
I have found something that helped me. Thank you!


Feel free to surf to my blog post oases
My site: cardiac

Anonymous said...

Howdy! I know this is kinda off topic nevertheless I'd figured I'd ask.
Would you be interested in trading links or maybe guest authoring a blog
post or vice-versa? My blog goes over a lot of the same subjects as yours and I feel we could greatly benefit
from each other. If you are interested feel free to send me an e-mail.
I look forward to hearing from you! Superb blog by the way!



Feel free to visit my webpage - pasteurize

Anonymous said...

Very nice post. I just stumbled upon your blog and wanted to
say that I've really enjoyed browsing your blog posts. In any case I'll be subscribing to your rss feed and I hope you write
again soon!

my blog - valuables

Anonymous said...

que la fabrication du pain, viagra effet secondaire, citerons ici les principaux, y mas atras en el Colectivo cialis 5 mg, organizacion de una nueva sociedad. Stylobates morchellacformis Fr. vendita viagra italia, tanto in esemplari conservati in alcool od mit Blei ausgefutterte Bottiche abgelassen und cialis erfahrungen, der Forderung arsenhaltiger Erze und beim,

Anonymous said...

Infections by virus', worms, adware and spyware may go unnoticed, you may not even know you are infected. You can also try out a variety of anti-spyware programs for free and then decide to take your pick and buy the one which, according to you, gives the best service. These sorts of things are impeccable to stay secret and private.

my homepage: computer virus books

Anonymous said...

Infections by virus', worms, adware and spyware may go unnoticed, you may not even know you are infected. In a previous article about Spyware Doctor update failure, I described some solutions to fix updating issues for the antivirus program by PC Tools:. Because of this, you really too need a malware remover that updates itself frequently.

my blog: how to uninstall ms removal tool

Anonymous said...

bph cialis [url=http://tadalafilfor.com]Cialis[/url] cialis professional cheappropecia 1mg [url=http://healthcarerxusa.com]Buy Finasteride[/url] generic for finasteridegeneric viagra side effects [url=http://viagradoseusa.com]viagra for men for sale[/url] china viagrawatermelon rind viagra [url=http://comprarviagraspain.com]viagra efectos secundarios[/url] viagra and infertilityfollistim clomid success [url=http://usfastmed.com]Buy Clomiphene[/url] early period clomid