Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Thursday, September 27, 2012

Mbio za Sakafuni Huishia Ukingoni-Hitimisho




‘Je ulipotoka bafuni ulifika pale kitandani na kushika chochote?’ akaulizwa.

‘Hapana, nilipotoka pale na kuangalia pale kitandani na kumuona yule mwanamke alivyokuwa kalala, na kifuani kunavuja damu,sikutaka hata kumsogelea’akasema.

‘Sasa ulijuaje kuwa amekufa?’ akaulizwa.

‘Kwa jinsi alivyokuwa katoa macho, na ulimi umetokeza nje, ilikuwa dalili kwangu kuwa keshakufa’akasema.

‘Uliposikia mlio ulichukua muda gani hadi kutoka bafuni?’ akaulizwa.

‘Niliposikia huoo mlio cha kwanza nilitulia nikiwaza ni kitu gani, ndioakili yangu ilinituma kabisa kuwa ni mlio wa bunduki, lakini umetokwa wapi, …na baaadaye nikachukua taulo na kujifuta maji, kwani nilikwuanimeshamaliza kuoga, na kutoka nje haraka, na wakati natoka’hapo akatulia.

‘Ongea, wakati unatoka ilikwuaje?’ akaulizwa.

‘Nakumbuka kulikuwa na mhudumu ambaye nilimwambai anisubiri ,kama nikihitaji kitu, nilihisi ndio yeye, ingawaje sina uhakika, alifungua mlangi akitoka na kufunga’akasema.

‘Mlango upi?’ akaulizwa.

‘Pale hotelini chumba nilichokuwepo kina sehemu ya mapumziko na chumba cha kulala, sasa yule binti alikuwa chumba cha mapumziko, na ukitoka bafuni, unaweza ukapitia mlango wa kuingia chumba cha mapumziko au ukatokea chumbani. Mimi nilitokea chumba cha mapumziko kwakuchanganyikiwa’akasema.

‘Huyu muhudumu, wakati anatoka, alikuwa kashika nini?’akaulizwa.

‘Sikuweza kumwangali vyema , lakini kwa kumbukumbu zangu, alikuwa kashikilia lile sinia la vinywaji, na alikuwa naye kachanganyikwia, nahisi ni kwasababu ya kusikia mlio wa bunduki’akasema.

‘Je ukiwa bafuni huwezi kusikia sauti za watu wakiongea nje, chumbani au sehemu ya kupumzikia?’ akaulizwa.

‘Unaweza kusikia,na kwa muda huo kulikuwa na sauti ya runinga, ambayo ilikuwa bado haijazimwa, alikuwa akiangalai yule mhudumu, na kwa ndani chumbani halikadhalika, kulikuwa na sauti ya runinga alikwua akiangalia huyo mwenzangu, kwahiyo sauti zilikuwa nyingi, sio rahisi kugundua kuwa ni nani anaongea na anaongea kitu gani’akasema.

‘Sauti ya runinga na sauti za watu zipo tofauti, …’akasema mwanadada.

‘Kwa vile sikuwa na mawazoo ya kusikiliza nini kinaongewa kwa muda huo, kwanza nilikuwa na mawazo ya familia yangu, pili hizo sauti ni nyingi, na tatu mambo ya kisiasa ylikuwa yakipita kichwani, kwahiyo nisingelikuwa na mawazo mengine, hata kama kulikuwa na watu wanaongea’akasema.

‘Hukusikia mlangoo ukifungwa na kufunguliwa ?’ akaulizwa.

‘Hilo nakumbuka nilisikia,nakumbuka sana, na ulikuwa mlango wa nje, ambao ulikuwa ukiufungua au kufunga hutoa sauti tofauti na mlango wa kuingia chumbani.’kasema.
Mwanadada alipomuhoji mke wa muheshimiwa alibakia mdomo wazi kwa muda, hakuamini;

‘Ina maana wewe ulikuwepo siku hiyo ya tukio, na mumeo hajui?’ akaulizwa.

‘Ndio mimi nilikuwepo hapo, na …nilifikahapo nikiwa sijijui kwasababu ya ulevi, na zaidi nilikuwa nimechukau bastola, ya rafiki yangu,’akasema.

‘Mamamamaaa….ok, je hiyo bastola anayo bado huyo rafiki yako?’ akaulizwa.

‘Sina uhakika huo?’ akasema.

Mwanadada alipofuatilia kumbukumbu za polisi aligundua kuwa bastola iliyomua huyo marehemu sio hiyo anayomiliki huyo mke wa adui wa muheshimiwa, na hapo akawa na ahueni kuwa mke wa muheshimiwa sio yeye aliyeua.

‘Naomba tafadhali usije kumwambia mume wangu kuwa mimi nilikuwepo siku hiyo, yalipotokea hayo mauaji,’akasema mke wamuheshimiwa’

‘Kwanini,?’ akaulizwa.

‘Mimi katikamaisha yangu sijawahi kufanya kitu kama hicho,naheshimu sana ndoa yangu,nilifanya hivyo kwasababu ya shinikizo la huyo rafiki yangu…na jinsi nilivyoona kule na kushuhudia mwenyewe kuwa kweli mume wangu ana nyumba ndogo, mimi sioni umuhimu wa kuwa mke wake, nasubiri akipona tu, naomba talaka yangu…’akasema.‘

‘Hapana hilo sio jambo jema,kwanza tumalizane ni hili, ili tuone jinsi gani ya kuwasafisha na tukio hili,na ikibidi kufika mhakamani, hatuna jinsi,inabidi ijulikane tu kuwa ulikuwepo’akasema wakili mwanadada,

‘Lakini nitajitahidi kama huhitaji kujulikana, ….’akasema huku akiwaza jinsi gani ya kufanya ili kweli huyo mwanamke asijulikane kuwa alikuwepo huko.

Wakili mwanadada baada ya kusikiliza maelezo ya wanafamilia hawa kila mmoja kwa wakati wake, alifika ofisini kwake na kuanza kufikiri jinsi gani ya kuwaokoa hawa watu, kwani sio tu mambo ya kisiasa, lakinii kuna maswala ya ndoa, ambayo imeshaingai doa.

Kila siku anapopata kazi mpya ambayo mara nyingi inahusiana na ndoa za watu, anakuta ndani yake kuna mauaji, na mauaji yenyewe yameweka kinamna ambayo sio rahisi kumgundua muuaji, na yule ambaya anashikiliwa na polisi utakuta hahusiki kabisa na mauaji hayo.

Alimuwaza huyu mwanaume ambaya kwa sasa hali yake bado sioo nzuri, na ameshauriwa na dakitari asimuulize maswali ambayo yanaweza kumtia wasiwasi mgonjwa. Lakini maelezo machache aliyopata yamemfanya agundue kuwa kinachoendelea hapo na mambo ya mlungula, kuwa ili mambo yaishe akubalaine na matakwa yao.

*********

‘Mimi nii wakili wa familia ya muheshimiwa, nimekuja hapa kwa maswali machache yanayohisiana na watejawangu’akasema wakili mwanadada.

‘Maswali gani hayo, mimi sina mahusiano na hiyo familia?’ mke wa jamaa akauliza kwa wasiwasi.

‘Ndio , najua huna mahusiano na hawa watu,na mumeo ni adui mkubwa wa hiyo familia, hata hivyo, ni vyema tukajua kuwa sisi wanawake ndio tunaotakiwa kuwajenga waume zetu wawe na roho nzuri.Uadui na chuki sio silka njema ya maisha, kwani adui yako wa leo anaweza akawa msaada kwako kesho’akasema wakili mwanadada na yule mwanamke akawa ktulia.

‘Kwa kukumbusha tu, Unakumbuka siku ile ulipomchukua mke wa muheshimiwa, na kwenda naye huko Dodoma, kwa minajili ya wewe kutaka kumuonyesha ushahidi kuwa mume wake ana nyumba ndogo, na kwenye safari ile kulitokea mauaji…?.’akauliza wakili mwanadada.

‘Mimi, …hapana, labda umekosea,  sijawahi kuondoka na huyo mwanamke. Hivi mimi nitoke na mtu wa familia hiyo hadi huko Dodoma, unafikiriaje, wale ni maadui wetu wakubwa. Ndio, nakumbuka kuwa nilikutana na huyo mwanamke  nikampa liftil kiubinadamu tu, lakini kuondoka naye, hilo silijui’akasema yule mwanamke akionyesha wasiwasi.

‘Usiharakishe kukana, najua kwanini unasema hivyo, lakini kama nilivyokwisha kukutambushakuwa mimi ni wakili wao, na walishakufahamisha hilo nasikia ukakata simu,…ukweli ni kuwa mlikuwa naye, na wewe ndiye uliyemshawishi, hili usilikatae, ninachoka hapa ni mimi na wewe tusaidiane, ili kulimaliza hili tatizo,…’akasema wakili mwanadada.

‘Mimi nimekuambia sihusiki, kama unahitaji lolote nenda polisi, wao wanajua zaidi, lakini mimi sihusiki kwa lolote, na sitasema lolote, natumai umenielewa, maana hivi sasa ninasafari zangu, siwezi kukaa hapa kusikiliza tuhuma ambazo hazina tija kwangu’akasema.

‘Ushahidi upo, kuwa mliondoka naye, na gari mlilokodi linajulikana na hawo mliowakodi wameshathibitisha hilo, sasa mimi sioni kwanini ukatae, na kwenda polisi sio hoja, wao watakuja kwa wakati wao, maana hiyo kesi imefufuliwa upya.

Yule mwanamke akashituka kidogo na kuangalia chini, kama anawaza jambo, lakini hakusema kitu.

‘Mimi ninachotaka ni kuwasaida nyie, hasa akina mama.Najua hayo yalitokea kwasababu ya nia njema, ya kuwalinda waume zenu, na mlihitaji ushahidi, na katika kufanya hilo ndio mkajikuta mumeingia kwenye mataizo, sasa naomba tusaidiane hili swala muondakane na huu mzigo.

‘Mimi sijahitaji msaada wako, kwanza nina wakili wangu, kama ni maswala ya kisheria , basi nitapanga siku mkutane naye, ‘akasema.

‘Hilo halina shida, tutakutaka ikibidi, lakini kwanini twende kote huko, mimi nimekuja kwa kuomba msaada wako uli kuliweka hili swala vyema, unakumbuka siku ile usiku , siku ambayo mauaji hayo yalitokea, unamkumbuka yule binti wa tajiri wa ile hoteli ambaye ndiye unayemtumia kupata taarifa za mumeo, alikuambia nini? Akaulizwa.

‘Binti gani huyo, ?’ akauliza kwa haraka na kuonyesha wasiwasi.

‘Hakukuambia kuwa kuna mtu anataka kumkomesha, na ukamwambia  utamsaidia, je ulimsaida vipi, ?’ akaulizwa.

‘Wewe tatizo lako unasikiliza maneno ya watu, lakini hayana nafasi kisheria’akasema.

‘Yalikifika mahakamani yana nafasi, hebu kumbuka vyema siku ile , yule mwanamke alivyokuwa, jinsi alivyokunywa kupitiliza na wewe ukawa unamsaidia, je alipotokapale alikwenda wapi,na unakumbuka yale maneno aliyosema hadi mkaanza kuzozana, hebu kumbuke vyema’akasema wakili mwanadada.

Yule mwanamke akakunja uso akiwa kama anawaza jambo ndipo akakumbuka tukio lile ambalo yeye hakuwa amelitilia manani, kumbe…..

********

‘Rafiki yangu naomba msaada wako, ?’ akakumbuka siku ile walipokuwa wakiongea na huyo binti ambaye ni mmoja wa viongozi wa hiyo hoteli.

‘Msaada gani, wewe niambie mimi nitakusaidia kama inawezekana’akasema.

‘Kuna malaya mmoja anajifanya yeye anaweza kutembea na kila mwanaume, sasa hivi kanichukulia mtu wangu, ambaye nilishajua ndiye kitega uchumi changu, na baya zaidi anaongea mbele za watu kuwa kanizidi ujanja’akasema.

‘Malaya gani huyo, achane naye, wanaume wapo wengi, kwani wewe shida yako ni nini, pesa unazo, maisha mazuri unayo, unataka nini zaidi?’ akaulizwa.

‘Kanizalilisha, kutangaza kuwa mimi silolote kwake, na kwanini aingilie anga zangu, na hili sio mara ya kwanza, halafu nikuambia ukweli huyu nii mmoja wa wshikaji wa mumeo’akasema

‘Ni yupi huyo?’akauliza.

‘Yule mwalimu wa kule juu, yule ambaye alikuja wakati tunajaribu zile nguo akaanza kuongea kiingereza chake kibovu, akasema na y eye anahitaji nguo kwa ajili ya harusi yake, nikakubonyeza kwa kukuambia achana naye,umemkumbuka?’ akasema huyo binti.

‘Sasa yule naye anakubabaisha, kwanza ni rafiki yako, na siuliniambai kuwa ndiye anatembea na muheshimiwa adui wa mume wangu’akasema.

‘Huyo huyo, …ni mshikaji wa mume, anakula huku na huku’akasema.

‘Sasa unataka tumfanye vipi?’ akaulizwa . Yule binti akapitisha kidole shingoni, kuashiria kuwa anataka kumuua

‘Hayo achana nayo kwa sasa muda utafika wa kuchukua hatua, watakuja kujimaliza wenyewe, usiwe na papara’akamwambia huyo mwanadada.

‘Muda bado, wakati ananizalilisha, kanichukulia mtu wangu, na bado ananifuata fuata kwenye maisha yangu, ngoja …leo nikitoka hapa, nitamuonyesha jambo, kuwa mimi ni askari alikimbia jeshi,…ngoja kuna kitu nakifuatilia, kikikamlika tu, basi sijui kesho itamkuta…’akasema na wakawa wanaendelea kunywa, baadaye huyo mwanadada akaondoka, na kuwaacha waoo wakiendela kunywa.

Kesho yake hakumuona huyo binti hadi anaondokahapo Makaoni.

*********

Baada ya ushawishi mkubwa huyu manamama akakubali kutoa ushirikiano, na waaksafiri hadi makaoni na huko ukweli ukagundulikana kumbe mauaji yalipangwa na rafiki wa huyo marehemu, kwasaabbu ya wivu wa kimapenzi akishirikiana na kundi la adui wa muhehimiwa.

Ilikuja kugundulika kuwa bastola iliyotumika ilikuwa ikimilikiwa na mwenye hiyo hoteli. Hoteli hiyo ilikuwa na vyombo vya kunasa matukio yanatokea ndani ya vyumba, na ilipofuatiliwa ikagundulikana  kuwa mwanamke aliyefanya mauaji hayo, alikuwa mpenzi wa mwanzo wa muheshimiwa, lakini hawakudumu naye, baada ya kutokea huyo marehemu.

Mwanamke huyu alikuja kukutana baadaye na adui wa muhehimiwa, ambaye alikuwa katika mipango ya kumfuatilia muheshimiwa, wakaungana, na kwa vile walishachoka na huyo marehemu kuwa anavuja siri zao, wakaona huo ndio wakati muafaka.

Walichofanya ni kumtumia huyo mwanadada ambaye alikuwa mtu wa karibu wa mwenye hoteli hiyo kwa upande wa usalama, na akaweza kuiba bastola ya tajiri wa hiyo hoteli, na siku hiyo ya tukio, mwenye hoteli alikuwa kasafiri nje ya nchi.

Yule mwanamke kwa vile alikuwa upande wa usalama na anajua siri zote za hiyo hoteli, na mitambo inavyovyofanya kazi, na siku hiyo akaingia kwenye hiyo mitambo, na kufuatilia matukio yote hadi alipopata nafasi hiyo akaitumia. Alichofanya yeye ni kukaa kwenye ile mitambo akawa anamuelekeza  mtu , kutoka kwenye kundi la maadui wa muheshimiwa ambaye, alitumwa kwenda kumaliza kazi.

Siku mwenye hoteli hiyo aliporudi, akakuta mitambo hiyo haifani kazi, alipoita fundi na kuangalia tatizo limetokea wapi, ndipo wakagundua kuwa kuna mtu aliiharibu, na mtu wa mwisho kuonekana ikawa ndio huyo muuaji aliyetumwa na maadui wa muheshimiwa. Ilionyesha dhahiri akiwa kashika bastola akimlenga huyo mwanamke. Wakakamatwa wote, na baada ya kubwa wakakiri na kusema kila jambo.

Mambo hayo yalipogundulikana na kufika kwa adui wa muhehimiwa, aalijaribu kutumia pesa zake kuhonga, lakini haikuwezekana, akazidi kujichimbia kaburi. Na, siri nyingi za huyu adui wa muheshimiwa zikavuja, wengi wa marafiki zake wakamsaliti, kwani walishafikia sehemu  hawaelewani tena, na alipogundua kuwa mmoja wa watu waliokuwa wakimfuatilia ni mke wake, hakuamini, mwili ukaanza kuishiwa nguvu, jasho na moyo kwenda mbio

Katika uchunguzi wa kiserikali iligundulikana kuwa huyo jamaa ana matatizo mengi kazini na uchunguzi ukabaini kuwa utendaji wake mbovu umeiingiza serikali hasara nyingi kwenye kitengo chake, kwa kukwepesha makapuni mengi kutokulipa kodi, kwa masilahi yake binafsi.  Hayo yalipowekwa wazi na ushaidi wa kutosha kutolewa, jamaa akafikishwa mahakamani.

Ikabidi afilisiwe na akaunti zake, ambazo nyingi alizifungulia nchi za nje, zikafungwa, …jamaa kuona hivyo akajaribu kutoroka nchini, lakini akabambwa uwanja wa ndege, akiwa kajbadili sura, kuona maji yamefika shingoni,  shinikizo la damu likapanda, na kiharusi juu. Masikini yale yale yaliyowapata wahasimu wake yakamgeukia na yeye…mbio hadi ICU.

Mwisho.

NB: Imebidi nifanye hivyo, ….kwa kujaribu kukifupisha hiki kisa,ili tuone nini kilitokea kwa jamaa hawa, natumai ujumbe umefika, kama kuna maoni, ushauri, naomba tuambizane, na mungu akipenda tutaanza kisa kingine, …

WAZO LA LEO: Tusipende kutendeana ubaya, kwasababu za kiwivu na chuki binafsi, tujue zamb za ubaya zitalipwa hapahapa duniani, kwani mbio za sakafuni huishiwa wapi? Naombeni mnijibu, hata kwa kimiya kimiya sio mbaya ….


Ni mimi: emu-three

4 comments :

Ammy k said...

JAMANI, KISA HIKI CHA MWISHO M3 UMENIACHA NJIA PANDA, SIJAKIELEWA VIZURI.

emuthree said...

Umekisoma kisa chote toka mwanzo? hebu kisome tena utakielewa vyema, najua nimekifupisha tofauti na utaratibu wangu, lkn sina jinsi. Mambo yapo juu ya uwezo wangu!

EDNA said...

Pamoja sana jirani.

Anonymous said...

Much informative and useful article… I like it personally…
Welcome to my site [url=http://www.about-dogs.zoomshare.com/]www.about-dogs.zoomshare.com[/url].