Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Wednesday, August 22, 2012

Mbio za sakafuni,huishia ukingoni 6




Mke wangu aliniangalia nikitandika vile vitambaa , akatabasamu na kuchukua baadhi ya vitambaa na kuanza kutandika, na mara mlango ukagongwa, akaingia mtu mmoja, akanisogelea na kuninong’oneza sikioni, haraka niliviweka vile vitambaa kwenye kocho na kuanza kuondoka, nilipofika mlangoi nikakumbuka, nikageuka  na kumwambia mke wangu.

‘Kuna kikao cha dharura  mke wangu, kuhusu hayo maswala yetu…’nikamwambia.

Mke wangu aliniangalia bila kusema kitu, akakaa kweney kocho na kushika shavu, na aliposhika lile shavu nikakumbuka ile siku ya kwanza nilipomuona waakti nahutubia , na isingelikuwa huyo mwenzangu ningelirudi niongee na mke wangu, lakini jamaa alishika mkono na kunivutia nje,akasema;

‘Achana na maswala ya mke, mambo huko sio mzuri, ukiendelea kukaa ndani na mkeo, utabakia hivhi hivyo, siasa sio mchezo, siasa inatakiwa mbinu, kuongea na kuwa mjanja,….’akaniambia.

‘Sawa lakini nijuavyo mimi siasa na uongozi huanzia nyumbani,…kama nizpoiweka familia yangu vyema, nina uhakika hata huo uongozi hautakuwa na maana kwangu…’nikasema.

‘Sikiliza,mimi mambo haya nimeyaanza siku nyingi, ukiwa katika kampeni, unakuwa kama upo vitani, unatakwia usahau kabisa familia, ….familia itakuja kukuona wa maana hapo ukiitwa muheshimiwa, sasa hivi haioni nini unachokifanya,….sikiliza, sasa hivi kuna mambo muhimu yakufuatilia, kwanza tunahitaji wadhamini, kwasababu tunahitaji pesa,…’akasema.

‘Tunahitaji pesa, na ili tupate pesa tunahitajika kupata wadhamini, lakini hata hawo wadhamini, wanategemea nguvu yako kwanza, je umajiuandaaje, maana tusije tukaadhirika…’akasema jamaa yangu huyo akizidi kunitonesha, maana haijapita mwezi tangu nilipouza shamba langu kubwa na nyumba, kwa ajili ya kuweza kufanikisha kupitihwa jina langu, sasa jina limepita, lakini…..

‘Hela yako hiyo itarudi, ukiingia kwenye bungeni, mambo yatanyooka…wewe ni kiongozi, uwaziri kwako upon je nje…’akanipa moyo, na tukawa kimiya kwa muda huku gari likiwa kwenye foleni tukielekea sehemu ya kikao maalumu kwa ajili ya kujiandaa kwa uchaguzi….

Wakati tumetulia mawazo yangu yalikwenda mbali, yakikumbuka siku ile ya ushindi, siku ambayo kwangu niliiona kuwa ni yaushindi wa maisha yangu, …lakini sikujua kuwa kuna mengine yanakuja mbele, ambayo yana hitaji juhudi za ziada,…..mara sauti za siku ile zikatanda amsikioni mwangu…

******

‘Nataka nikutoroshe, ….siwezi kukubali uolewe na huyo jamaa, nimekuja leo na kundi langu, hiyo harusi kesho haifungiki….’nikasema kwa sauti ya kuwewesa, maana humo niliingia kwa ufichohakuna anayejua ujio wangu na kundi langu, ….watu nje walikuwa kwenye pilika pilika za maandalizi ya hiyo harusi.
‘Mimi sielewi, …’akaanza kusema yule binti.

Nilimuangalia kwa makini na kwajinsi alivyokonda kwa siku chache ungelimuonea huruma, ilionyesha wazi kabida kuwa hayupo tayari na  hiyo ndoa, lakini angelifanyaje, ….wazazi wake, walikuwa wakali kupita kiasi na wameshachukua pesa nyingi toka  kwa rafiki yangu, na wameanzishiwamiradi ya biashara,…..

‘Mwaanngu unaona sasa mimi ni mzee, nguvu za kupambana na maisha zimepungua na hali yangu ya kuumwa, inanafanya nisihangaike tena, hapa sana sana namtegemea mama yako,…lakini kama umjuavyo mama yako, ubinfasi umemzidi, nakuwa kama sio mume ndani ya nyuma….’hiyo ilikuwa kauli ya baba wa binti wakati ananismulia kwanini kaamua kukubali kuolewa.

‘Baba nakuelewa, lakini huyo mume sio chaguo langu, nilishampaat mtu ambaye ndiye chaguo langu…’akajitetea binti.

‘Binti yangu skiliza kwanza haya ninayotaka kukuambia, najua hilo, ulishaniambia, lakini uangalai na mimi misha yangu, huyu mchumba wako keshaniwekea mradi ambao utaniingizia pesa, sitakuwa nahangaika tena, ….na juzi tu nimepata tenda ambayo itaniwezesha kusimama kwa miguu yangu, na mimi nitaitwa baba tena, nitaitwa mume tena, na pia itaniwezesha kuendelea na matibabu yangu bila kuwa omba omba….sasa nakuomba, mwanangu,…ni kwa ajili ya afya yangu, ….’akasema baba yake.

Binti alimwangalai baba yake akiwa kitandani, …alikuwa kakonda, ….na kwa kipindi kile mama hakuwa karibu naye sana, kwa sababu ya pilika pilika za kibiashara, mama alikuwa ndiye akihangaika kwa ajili ya familia, baba ni mgonjwa hajiwezi.

‘Sikiliza mwanagu, nakupenda sana, ….na napenda furaha yako, napenda na wewe uishi maisha mazuri, na nina uhakika ukimpata huyo mume hutapata shida, pesa anazo, ….ana ajira yenye uhakika, na sasa kafungua kampuni yake, sasa unataka nini, unataka ukaishie kwenye maisha ya dhiki, na huyo ….’akasema huku akikunja uso kwa maumivu.

‘Baba sijui nifanyeje miye …maana nilishaahidiana na mhumba wangu ninayempenda, yeye kanisaidia sana toka zamani, kumteleekza sasa hivi ni dhambi kubwa sana ambayo sitaweza kuivumilia,…baba yeye atakusaidia tu….’akasema binti.

‘Atanisaidia tu, lini…na hali unavyoiona,…au unataka nife, ndio uone kuwa naumwa, hali unaiona, na mtu kajitolea kuniasaidia, ..mwanagu hii ni kwa ajili ya afya yangu, na pia ni kwa ajili ya bibi yako kule kijijini, kwa ajili ya kuniokoa na huu umasikini ulionikumba,kwaajili ya kunifanya na mimi nionekane mume tena…’akasema kwa uchungu huku machozi yakimtoka.

‘Baba …..’binti akataka kusema neno na mara baba yake akagugumia kwa maumivu, na hali ikawa mbaya,….docta alipoitwa, akasema kuwa hali kama hiyo itakuwa ikitokea mara kwa mara, mapaka hapo matibabu ya maana yatakapopatikana, akasema baba anahitajika upasuaji wa haraka,…lakini ni vyemamatibabu hayo, yakafanyika India ambapo kuna uhakika zaidi,….na hivyo basi inahitajika pesanyingi tu…..

‘Hizo pesa tutaizpatia wapi…!’akalalamika mama akionyesha kukata tamaa.

‘Mama msiwe na shaka,mimi nimeshawaambia,kuwa…..kwa vile mimi ni mkwe wenu mtarajiwa, nitajitolea kila kitu, hilo swala la matibabu ya baba, niachieni mimi, nitahakikisha waiki hii anasafiri kwenda India kwa matibabu…baada ya ndoa yetu’akasema rafiki yangu, mimi hayo nilikuwa siyajui,alikuja kunisimulia huyu binti, dakika hizo za mwisho, akiwa tayari keshaandaliwa kama bibi harusi mtarajiwa.

‘Kwahiyo baba anatakiwa akatibiwe kwa pesa za huyu jamaa, na ni moja ya makubaliano kuwa uolewe na yeye….kwanza….halafu  ndio akatibiwe au sio?’ nikamuuliza.

‘Ndivyo ilivyo, yeye hajasema moja kwa moja hivyo …, ila kasema kuna mipango ya kusafiri, vibali na mambo mengine, ambayo inabidi ayafuatilie, na huku yakifuatiliwa ni vyema ndoa hiyo ifungwe mapema, ili baba ashuhudie., na hata hivyo akasema kuwa weweni mtu mjanja sana, ili mamo waweze kukudhibiti, ni vyema kuwe  na mkataba  wa matidhiano, kati ya familia yangu, na mimi nay eye na familia yake kwa upande mwingine, ili kukuzuia usifanye lolote, amesema ni kwa ajili ya kujilinda kisheria,…’akasema huyo binti.

‘Mkataba!?… ‘Mimi hapo naona kuna jambo limejificha, sina uhakika bado, …’nikasema kwa kushangaa sikujua hayo, nikageuka na kuinama chini, binti akasema;

 ‘Baba anaumwa kweli,anatakiwa akatibiwe, unataka uhakika gani tena, ukumbuke kuwa baba bado hajaondoka, ataondoka kesho kutwa , na inatakiwa ashuhudie kufungishwa kwa ndoa hii, ni moja ya makubaliano katika huo mkataba, na ilibidi nikubali mbele yake kuwa nipo tayari kuolewa na huyo jamaa ili baba akapatiwe hayo matibabu, na kwa ajili ya…ya uhakika kuwa wewe hutaweza kuleta matatizo tena, …’akasemahuyo binti.

 ‘Kwanini mpaka mkataba,…,mimi nilijua alikuwa akimsaidia baba yako kwa nia njema , ina maana pendo lako kwake ni kwa shinikizo, huoni kuwa ndoa yenu itakuwa haina upendo, huoni kuwa hapo kuna kitu katikati kimejificha,,….hamuoni kuwa huyo sio mtu mwenye huruma,….’nikasema kwa hamaki.

‘Mimi najua yote hayo, lakini yeye alidai kuwa wewe ni mtu mjanja sana, unaweza ukanihadaa mimi nikabadili kauli yangu,kwahiyo ili kukubana wewe , inabidi kuwe na mkataka wa kisheria, ndio ukayarishwa huo mkataba na mwanasheria wake, ambao nilitakiwa mimi ,na wazazi wangu kukubaliana nao, ili wewe ukija kwangu usiwe na nguvu tena…’akasema huyo binti.

‘Hiyo sasa kali….lakini nikuulize neno moja,…..je kweli unanipenda mimi?’ nikamuuliza.

‘Hilo sio swali lakuniuliza,nimeshakuambia kuwa mimi nakupenda, nakupenda sana,…lakini angalia hali ya wazazi wangu, ….baba ni mtu muhimu sana katika misha yangu, licha ya mapungufu yake ya kukosana na mama,lakini mara nyingi alikuwa uapnde wangu, pale inapobidi, baba ni mzazi wangu, anahitajika kutibiwa, …kwahiyo inabidi nikubali, kwa ajili yake na kwa ajili ya bibi….nasikitika sana kwa hilo,….’akasema.

‘Mimi sijakubali,…kama kweli unanipenda nataka tufanye jambo…’nikamwambia.

‘Jambi gani hilo?’ akaniuliza akiwa nawasiwasi.

‘Unajua kutoroshwa,mimi nataka nikutoroshe….leo hii, nimejiandaa kwa hilo…’nikamwambia

‘Hapana,.kumbuka kuwa kuna mkataba wa kisheria, kumbuka kuwa baba yangu anatakiwa akatibiwe, kumbuka nyumba ya bibi, kumbuka miradi ya baba ambayo akirudi ndiyo anaitegemea kuendeleza misha yake..kumbuka, hapana, naomba tukubali matokeo….’akasema binti.

‘Nakuuliza tena, je kweli unanipenda mimi?’ nikamuuliza.

‘Ndio nakupenda,ndio maana, pia sitaki wewe uzurike, ….’akasema na kuziba mdomo.

‘Nitazurika na lipi tenai?’ nikamuuliza.

‘Huyo rafiki yako alisema kama nitafanya kinyume na hayo makubaliano, atakufanyia jambo baya sana, mwenyewe sitaamini,…’akasema huyo binti.

‘Hawezi kunifanya kitu mimi, hivyo ni vitisho tu…’nikasema nikikumbuka jinsi nilivyonusurika kumwagiwa tindika, kumbe ni kipindi ambacho huyo binti alikuwa akionyeshwa moja kwa moja jinsi gani nitafanyiwa kama asipokubaliana na mimi.

‘Hawezi…unasema hawezi, .. , wakati siku hiyo alimtuma mtu wake aje kukumwagia tindikali, na akawa ananionyesha waziwazi kwenye kanda waliyoitegeshea….siwezi kukuona ukifa kwa shida kwa ajili yangu, nakupenda sana na nipo tayari kufanya lolote ili nione wewe huzuriki….’akasema huyo binti akionyesha wasiwasi mkubwa…

‘Hivyo ni vitisho tu…..hawezi kunifanyai hivyo, ndio walikuja watu kunitishia na hiyo tindikali, mimi nilijua ni viabaka tu,na sikujua kuwa ni yeye na watu wake, lakini hilo lipo mikononi mwa polisi, nitahakikisha kuwa anakamatwa…kilichotakiwa ni ushahidi, na wewe ukiwa upande wangu ukatoao huo ushahidi najua atakamatwa…sasa sikiliza muda unakwenda, tuangalie hili nililokuja nalo…

Mara  mlango ukagongwa…na mimi nikajificha nyuma ya mlango, alikuwa shangazi mtu alikuwa kuweka ammbo sawa,alipotoka nikajitokeza kwa yule binti, nikamwambia ajiandae, maana nimeshawasiliana na watu wangu, ….

‘Mbona hunielewi…jamani, …mimi naogoap sana….’akalalamika.

‘Nimekuelewa, lakini tusipofanya huo mpango sasa hivi, haitawezekana tena, kama kweli unanipenda wakati  ndio huu, jiandae,…’nikasema na kujificha pale pembeni ya mlango ulipogongwa tena, na walioingia safari hii,ni watu nisiowajua….nikasikia wakisema;

‘Fanyeni haraka, nimesikia msafara wa bwana harusi upo njiani, kama hataki mbebeni kwa nguvui…’sauti ikasema ikitoke kwa nje, nikashikwa na butwa, na kujiuiza hawa ni akina nani tena ….

NB : Ninajaribu kufupisha , maana hapo kulikuwa na matukio mengi, lakini muda,...

WAZO LA LEO: Pigania penzi lako kwa umpendaye kwa dhati, ukijua kuwa mpende akupendaye!


Ni mimi: emu-three
Enhanced by Zemanta

3 comments :

emuthree said...

Subira upo, tuwasiliane kwenye e-mail!

Subira said...

Nipo, mie huwa sikosi humu hata nitingwe kiasi gani.

Nitakuandikia InshaAllah

Eid Mubarra

Yasinta Ngonyani said...

Kisa kinasisimua,na pia kimenikumbusha familia fulani ambayo haikutaka binti yao aolewe na aliyempenda bali na waliompenda familia ..sijui hapa ni familia ndio wataisha na huyo mume au?...nasubiri muendelezo