Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Tuesday, July 24, 2012

Hujafa hujaumbika-73 hitimisho 31



Usemi huu hujafa hujaumbika nimetokea kuupenda sana, nikiimanisha jinsi gani mtu unavyoweza kukutana na mambo mengi ya ajabu ambayo hukutegemea kukutana nayo. Kila hatua unakutana na jambo la kushangaza, ulitarajia iwe hivi lakini unakuta inakuja kuwa tofauti kabisa, na kubakia kushangaa.. . 

Hii inaonyesha kuwa sisi ni binadamu tu,yapo mengi ya ajabu, na huwezi kuyamaliza, kuyamaliza kwako labda ile siku unawekwa kaburini…’alisema rafiki yangu huyu, siku anaendelea kunimalizia kisa hiki, nikatulia kumsikiliza.

Huyu wakili mwanadada, ninawea kumuita kuwa ni jembe, ni wale wanawake wenye akili ya ziada, dada huyu hana papara katika kazi yake, anakuwa makini na kinachomsaidia sana ni kuwa yupo karibu sana na watu wa aina zote, hajali kuwa huyo mtu yupoje,….

Hebu turejee kidogo kule hospitalini tuone nini kinaendelea maana kule tuliacha wagonjwa, na mimi ilibidi niache shughuli zangu niwe nawatembelea wagonjwa, maana sasa hawo wagonjwa wameshakuwa jamaa zangu.

Ukumbuke tulishaelewana na yule mchumba wangu wa utotoni, lakini kukutana kwetu ilikuwa ni nadra sana kwani yeye ni mtu wa kazini, na akitoka kazini anakuwa kwake na mara nyingi anahitaji mudawakupumzika. 
Na mimi sikupenda kwenda kwake kumsumbua, kwani kila nilipofika kwake,nilimkuta akiwa kachoka kweli…huwa namuonea huruma naondoka zangu nakumuacha apumzike!

Hata hivyo alishaniambia kuwa mimi na yeye tutakuwa pamoja pale tu tutakapofunga ndoa na ndoa yetu ilitakiwa ikafanyike huko kijijini,nami sikumkatalia, kama alivyoesema yeye mwenyewe inabidi tupeane muda wakutafakari na kujipima je tupo tayari kuishi pamoja kama mke na mume, maana ndoa sio kitu cha kukurupuka tu, ….

‘Ndio Msomali, naona kiukweli mambo yetu yameisha na mimi nipo tayari kuwa na wewe,lakini mengi yamepita kati yetu, siwezi nikajua undani wako kwa sasa, halikadhalika wewe huwezi ukajua undani wangu kwa sasa, cha muhimu ni kupeana muda, kila mtu atafakari kwa makini, na mwisho wa siku tuje kuambiana ukweli, kwamba je tupo tayari kuishi kama mke na mume…’aliniambia.

‘Lakini mimi nimeshakuambia kuwa nipo tayari kuishi na wewe kama mke wangu. Mimi kwasasa nahitaji kuwa na mke,na mke ambaye nilikuwa nikimuwaza muda wote ni wewe…’nikamwambia.

‘Kauli ni rahisi sana kuitoa mdomoni, lakini ukweli wa mtu ni nafsi yake, na muda ndio unaweka mambo hadharani, ni vyema tukayafanya haya mambo kama watu wenye hekima, sio kwamba sikupendi, mimi nakupenda sana, lakini tuwe makini sana na kitu kinachoitwa ndoa,….’akaniambia na kuanza kunitia wasiwasi maana sikutegemea tena kama itakuwa hivyo.

‘Kwani kuna tatizo gani?’ nikauliza

‘Hakuna tatizo,… wewe chukua muda wako jitahidi sana kila upatapo nafasi, jaribu kutafiti, na kujisomea nini kuhusu ndoa, nini kuhusu mwenzako katika ndoa, nini kuhusu maisha na mahusiano katika ndoa,…ukimaliza kujifunza, jiulize mwenyewe  nafsini mwako kuwa je upo tayari kuishi na mwenzako…..’akaniambia.

‘Mimi nipo tayari….sina wasiwasi na hilo….’nikasema kwa haraka.

‘Bado hujawa tayari, kama ungelikuwa tayari, usingelimuacha yule binti watu wa kijijini, yule ni mke kweli kweli, alihitaji msaada kidogo tu, alihitaji kuelimishwa mambo mengine ambayo kwake yalikuwa ni mapya, lakini wewe ulimchukua na kuja kumtelekeza, unajua nini kilimsibu moyoni mwake,…?’ akaniuliza.

‘Kwani hayo yanakuaje tena hayo….’nikasema kwa kushangaa.

‘Ni muhimu sana kuelewa hilo,….unajua jinsi gani mtu anapata maumivu pale anapoambiwa kuwa mimi na wewe basi….wakati mtu huyo bado unakupenda, na wakati mwingine hujui kabisa kosa lako ni nini….’akaniambia na kunitonesha kidonda.

‘Lakini yote haya yalitokea kwasababu ya Kimwana, natumai kama isingelikwua Kimwana yasingelitokea hayo yaliyotokea….’nikasema.

‘Unaona, nikuambie ukweli, dunia hii Kimwana wapo wengi,  …kauli yako hapo, inaonyesha ukweli fulani,…mwenyewe umejifunga, lakini sio mbaya, kweli kama isingelikuwa Kimwana kukuonyesha yale usiyoyajua yasingelitokea hayo,..je huoni kwamba tukioana sasa hivi,na ukakuta sina hicho ambacho Kimwana alikuwa nacho utajikuta ukijilaumu …na maisha yatakuwa yakubahatisha,…huoni kuwa wewe unachotaka ni mke tu,ilimradi unahitaji mke,….?’ Akaniuliza.

‘Hapanaaa,  sio hivyo,….sio kwamba kwasababu nahitaji mke tu,….nakuhitaji wewe,maana hata nilipokuwa na Kimwana nilikuwa  nakuwaza wewe, wewe ndiye mke ambaye yupo akilini mwangu..nakuomba sana Tausi usiniweke rehani tena, sihitaji kuwa katika majaribio mengine, nimeshawiva na nipo tayari kuwa mume mwema…’nikamwambia.

‘Sawa, kauli yako nimeisikia,lakini msimamo wangu upo palepale, kuwa tupeane muda, …muda wakutafakari,muda wa kujifunza maisha ya ndoa, muda wa kujipima je nina uwezo wa kuishi namwenzangu, na je ni nani huyo mwenzangu…huenda siku kadha unaweza ukakutana na mtu ambaye hukuwahi kukutana naye ukabadili mawazo,….’akaniangalia kwa makini.

‘Hiyo haiwezekani….wewe ndiye kila kitu kwangu nakuhakikishia hilo…’nikamwambia.

‘Rahisi sana kuatamka.., mimi nakushauri kuwa tupeane muda na ifanyie kazi akili yako, ili ijue nini kinachokuja mbele yako, baadaya kuitwa mwanandoa…sio kitu cha mchezo , sio sehemu ya kufanyiana majaribio..ndoa ni jambo takatifu, ….kwahiyo kihitaji kuwa makini …..’akaniambia na hata nilipojaribu kumshawishi hakubadili msimamo wake.

Baadaya mazungumzo hayo nilioanana na wakili mwanadada nakumuomba anisaidie kumshawishi Tausi, maana nahisi kuwa huenda ana mtu mwingine, na anashindwa kuniambia ukweli, na kama kweli yupo mtu mwingine, nitaumia sana.

‘Una uhakika na hilo, kuwa ana mtu mwingine?’akaniuliza

‘Nahisi hivyo tu, maana hili la kuniambia, kila mmoja apate muda wa kutafakari,….nahisi kuna mtu ambaye alishakubaliana naye, na sasa anajaribu kutafuta njia …’nikasema na kukatiza.

‘Sio kweli, mwenzako anajua nini anachokifanya, ujue yule ni dakitari , na ni mwalimu wa wanandoa, anajua jinsi gani watu wanapata taabu katika ndoa zao, kwasababu tu ya kukurupuka kuingia kwenye ndoa, bila kuijua ndoa yenyewe,….ndio maana anajaribu kukuelimishawewe ili uijue ndoa ni nini,kabla hamjaingi akwenye ndoa.Itakuwa ni aibu kwake, muoane na baada ya siku kadhaa muanze kusigishana…fikiria sana na jitahidi kufanya hayo aliyokuelekeza…’akaniambia.

‘Sasa nitajifunza nini kipya katika maswala ya ndoa, ndoa niijuavyo mimi ni kuwa muoane, na mengi mnajifunza mkiwa wawili, nitajuaje wewe unanipenda nini, kama hatupo pamoja, nitajuaje kuhusu wewe kama hatupo pamoja….’nikasema.

‘Hiyo ni hatua baada ya ndoa, kuna mambo mengi unatakwia uyajue kabla yahayo, kwanza ujue kwanini mnatakiwa muoane,kwani ni lazima kuoana, wakati wewe ukihitaji mwanamke unaweza kumpata mitaani, ….hebu jiulize hilo, je mwaname au mwanamke yupoje,ukumbuke watu hutofautiana, je ukimkuta yule ambaye yupo tofauti na wewe utafanyaje…’ akaniambia na kuniangalia kwa makini.

‘Hayo mbona nayaelewa tu…na hata hivyo mbona yeye namjua toka utotoni…’nikasema, na yeye bila kujali maelezo yangu hayo akasema;

‘Je wewe mwenyewe umeshajiweka sawa kuishi na mwenzako, maana usione ni jambo tu lakumchukua mwenzako na kuishi naye kama mke na mume ….eti kwa vile unamjua toka utotoni,….utotoni sio sawa na ukubwani, sio sawa na hali halisi ya mke na mume,…’akaniambia.

‘Mimi nipo tayari,…’nikasema.

‘Nakushauri,jaribu kutulia ,tuliza kichwa chako, ondoa tamaa, tafakari kwanza, ili baadaye msije mkaanza kuhangaika kuwa mtaishije…kuna mambo mengi…ya kujifunza, cha muhimu, kama ingelikuwa mimi ni wewe kwanza ningelimuuliza mwenzangu, maana yeye ni mwalimu….na ni vyema hapa ukaondoa `udume’, weka akili ya kujifunza mbele,mimi kama wewe ningelijishusha na kumuuliza, nifanyeje, au nianze vipi, mchukulie kama mwalimu wako,…’akanishauri.

*************

Basi tulipofika hospitalini, nikawa na wazo moja, la kumuomba tukutane tukitoka hapo, lakini haikuwa rahisi maana mambo mengi yalitokea hapo hospitalini, na baadaye tukatawanyika bila hata ya kupata muda wa kuongea naye.

‘Hali ya nesi sio nzuri…..tumejitahidi sana, lakini sumu yake ilishaharibu sehemu kubwa ya ndani ya mwili, …lakini tumejitahidi tuwezavyo….’akasema docta.

‘Ina maana hatapona?’ nikauliza kwa huzuni.

‘Siwezi kusema hivyo….kupona anaweza akapona,tumejaribu lile liwezakanavyo,iliyobakia ni kumuachia mwenyewe mungu tu..’akasema docta na kuondoka na jinsi alivyoongea na muoenekano wake ulionyesha wazi kabisa kuwa hali ya huyo nesi sio nzuri, hapo kila mmoja aliinama chini akiomba kivyake.

‘Hapa sasa hakuna lakufanya iliyobakia ni kwenda kumuona wakili mkuu, tujue naye anaendeleaje, maana sumu ni hiyo hiyo waliyokunywa wote, ….’akasema wakili mwanadada, na sote tukaondoka kwenda kumuona wakili mkuu, na tulimkuta akiwa kachoka kweli,hata kuongea kwake ilikuwa ni kwa taabu kweli.

‘Nawashukuru sana kwa kunijali, …licha ya mengi yaliyotokea, …’akasema.

‘Yote ni kawaida, binadamu hukutana na mengi, na mwisho wa siku ni kujifunza, na usipojifunza kwa haya, basi wewe ubinadamu wako una kasoro….’akasema mkuu.

‘Aaah,ndio hivyo tena, maana mimi hapa nilipo najiona mwenye mikosi , ….’akasema

‘Kwa vipi?’ akaulizwa.

‘Mwenzangu hataki …’akasema na kuonesha wingu la machozi machoni.

‘Cha muhimu wewe kwasasa ni kutulia, na kuangalia hali yako,kuhusu mwenzako, ni kawaida ni hasira za kawaida, usitarajie kuwa yeye atakukubalia kwa sasa kuwa mambo ni yote ni safi, ….cha muhimu wewe ni kutulia upone, baadaye hayo yatazungumza, mtazungumza na mkihitaji msaada, tupo tutasaidiana na najua mambo yakakwenda vyema…’akasema wakili mwanadada.

‘Unasema tu,kwa vile humjui mke wangu, mimi namjua vyema, huwa akisema neno lake, ninaweza kulipima kuwa hili kalisema kwa kujaribu, lakini kuna jingine akilisema najua kabisa kazamiria, …..nahisi moyo wake haupo tena kwangu…’akasema..

‘Labda wewe mwenyewe unavyoongea umeshaweka hitimisho, inaonyesha kuwa unataka iwe hivyo, maana ni mapema sana kuhukumu hivyo, ….jiulize kama ingelikuwa wewe umetendewa hivyo ungefanyaje,…yeye kama binadamu anahitaji muda wa kutafakari…’akaambiwa.

‘Nawaombeni sana, mujaribu kumshawishi,maana yeye ni mke wangu, na nilisha mtendea mabaya ambayo kiukweli yanaumiza, lakini yote hayo tuyaache yapite tugange yajayo, mimi nampenda sana na nimeona kuwa yeye ndiye anayenifaa….’akasema.

Mimi pale nikawa nawazo hivi kwanini inakuwa hivyo, nahisi kama nesi atakuja na kukaa naye pale  karibu huenda akabadili hayo maneno yake, maana ilivyojionyesha toka awali, anampenda sana nesi,….

‘Niwaulize kwanza, nesi anaendeleaje….?’akauliza swali tusilolitegemea toka kwake.

‘Wewe jiangalie kwanza hali yako, yeye anaendelea vyema na matibabu yake…usiwe na wasiwasi nay eye…’akasema  wakili mwanadada.

 Mara simu ya mmoja wawanafamilia ikaita tukiw amle ndani , na yule mwanafamilia kasogea pembeni, akawa anaongea na huyo aliyempigia, na katika kuongea kwake akasema;

‘Docta kasema nesi hali yake sio ya kupona….’ile sauti akasikiwa na wakili mkuu.

Wakili mkuu, alituangalia na mara akageuza macho, na hali ikabadilika ghafla, hata alipoitwa docta, hali haikuwa vyema,…tukataoka pale tukiwa tumechanganyikiwa na watu wakaanza kumlaumu yule jamaa aliyekuwa kiongea na simu, …lakini ndio hivyo tena, hali za watu hawa waili zikawa ni mbaya, na hadi tunaondoka hapo hospitalini hali zao zilikuwa ni za kusikilizia tu….

‘Hali zao sio nzuri, tunajitahidi kufanya kila liwezekanavyo.lakini hali zao zimebadilika na hatukutarajia hili…nawaomba muondoke,mtuachie tufanye kazi, ….’akasema docta, nasi tukaondoka kilammoja akiwa kachanganyikiwa, na kila mmoja akaelekea kwake, huku akiwaza kivyake.

NB Hiki kidogo kilibakia tukaona tukimalizie, kabla hatujahitimisha, ….

WAZO LA LEO:

Tujaribu kuchunga sana kauli zetu, maana kutamka ni rahisi sana,lakini matokeo yake yanaweza yakawa mabaya kwa mwenzako. Ni vyema kabla hajutamka jambo kwa mwenzako hasa mkiwa katika hali ya kufarakana,ukatafakari kwanza.

Katika mwezi huu mtukufu wa Ramadhani, tunatakiwa tuchunge sana ndimi zetu, tujaribu kukwepa kusema mambo yatakayobatilisha swaumu zetu, kama vile matusi, kusengenya,…kusema  uwongo…..utani usio na maana yoyote. Kufunga ni pamoja na matendo yetu.

KUTOKA MAJUMBANI: Siku hizi wezi wanaiba mchana kweupe,…wanakuchunguza nyendo zako,…iwe ni mama wa nyumbani au mfanyakazi, na hata mlinzi, kuwa unatoka saangapi nyumbani au lindoni, na wanachofanya mmoja mwenye simu anakuwa nawe karibu unapotoka hapo nyumbani…., na wenzao wanakwenda nyumbani kwako,….kwahiyo kazi ya yule ambaye yupo nawe ni kuwasiliana na wenzao waliokwenda kwako kuiba….

Wale walikwenda kwako wanavunja mlango kwa pisipisi, na kuchukua vitu huku wakiwa wanawasilina na mwenzo ambaye yupo na wewe…..Tuwe makini majumbani

Ni mimi: emu-three

2 comments :

Anonymous said...

Hiki kitu ulichotuwekea leo hakieleweki mikono imeanzia wapi wa miguu imeishia wapi! yaani hamna connection kabisa na pale ilipoishia, wala haina mwendelezo uliotulia. kweli leo umeamua kutuchosha ndugu! dah

emuthree said...

Oh, Anony,...ina maaa sehemu hii haijaeleweka,hebu wengine ambao hawajaelewa, waniambie ili nijue nini cha kufanya,lakini sehemu hii ina maana yake!
Ukikisoma vyema hiki kipande kwa makini, utajua wapi naelekea,.....

Mwisho wa kisa utakuja kuelewa tu ndugu yangu, vuta subira!