Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Monday, June 25, 2012

Hujafa hujaumbika-57 Hitimisho-15



Kilikuwa kipindi cha mapumziko, tukawa tunapata chakula cha mchana,na chakula hicho tulipatia hapo hapo, kuna mgahawa upo kwa nje ya hiyo mahakama. Mimi na wakili mwanadada tulikuwa tumekaa pamoja,mbali kidogo na wenzetu, tukawa tunaongea pole pole,

‘Nimekuona…’akaanza kwa utani.

‘Umeniona, kwa vipi?’ nikamuuliza.

‘Mhh,maana macho yako yalikuwa hayabanduki kwa Yule mwanadada, rafiki ya mke wa wakili wetu mkuu, inaonekana mmh….’akasema wakili mwnadada.

‘Unajua ni kwa vile tulikuwa tumekaa huku tumeangaliana,….’nikajitetea.

‘Hata kama mumekaa huku mumeangaliana, lakini macho yenu yalikuwa yakiongea mengi. Mbona wengine walikaa hivyo hivyo, lakini sikuona dalili kama zenu. Unajua yeye tabasamu lilikuwa halimuishi usoni kila kikutupia macho, kweli ni mrembo, au sio, lakini hata  hivyo mara nyingi, alionekana yupo mbali pengine kwa kukuwaza wewe….’akasema wakili mwanadada, huku akifungua gazeti, ….

Nikageuza kichwa kumwangali kule alipokaa huyu mwanadada rafiki wa mke wa wakili mkuu, walikuwa wamekaa pamoja na rafiki yake wakiongea, ilionekana wazi wameivana, na wakati namtupia jicho, kumbe na yeye alikuwa kageuka kuniangalia, macho yetu yakakutana tena, kwa haraka nikageuka kumwangalia wakili mwanadada,ambaye alikuwa akisoma gazeti.

‘Hakuna la maana kwenye gazeti, ni mambo yao ya kila  siku, ufisadi, ufisadi….’akasema na kuliweka gazeti pembeni, akaniangalia, na kunikuta nikigeuka haraka kutoka kumwangalia Yule mwanadada, nay eye akageuka kumwangalia, akasema huku akitabasamu….

‘Mhh, tuendelee sema…unaona kitu hicho, kimetulia….’akasema huku akinangalia machoni, yale macho yake ya kawaida, sio yale ya mahakamani.

‘Wewe unasema alikwua na mawazo akiniawaza mimi,kwanini awe na mawazo ya kuniwaza mimi wakati hanijui,…sizani kama tunajuana…..Labda alikuwa akimuwaza mtu wake, lakini kwa vile tulipata bahati ya kukaa sehemu ambayo tunaangaliana ndio maana ikawa hivyo, kwani Yule ni nani…hasa, ndio ni rafiki ya mke wa wakili, lakini unamjaueje?’ nikauliza.

‘Una uhakika kuwa kweli humjui…..?’ akaniuliza huku akiniangalia kwa makini, na kabla sijamjibu akasema;

‘Mimi namjua kama unavyomjua wewe…..’akasema.

‘Hapana wewe unamjua zaidi yangu…na kwanini nisema simjui kama namjua kiuwkeli, ….ila hisa zangu zinanituma kama vile nimewahi kukutana na sura kama hiyo….hebu niambie ni nani na anakaa wapi?’nikauliza

‘Hiyo itakuwa shutukizo kwako wenzetu wanasema ni `surprise’ kama kweli humjui…., usiwe na papara, kila kitu kitawekwa wazi,….cha muhimu ni kuhakisha kuwa kesi hii inafikia kikomo, naona hata hakimu amefurahishwa na utaratibu huu, maana watu wanakuwa huru kujielezea …’akasema wakili mwanadada akionyesha kuwa na furaha kubwa.

‘Kesi zingekuwa hivi, mbona mtu usingekuwa na wasi wasi kusema madhambi yake, maana hapa unakuwa kama unatubu dhambi zako na kuelezea kiukweli kile ulichokifanya,….’nikasema.

‘Tatizo ni udhaifi wetu wa kibinadamu, mwanadamu alivyo, ukimpa mwanya wa kujitetea na kuweza kuficha makucha yake, atakana hata lile alilolifanya makusudi,anaweza akasema kabisa sijanywa supu wakati mdomo una mabaki ya mafuta ya supu na harufu tele, akadai na mafuta ya losheni. Lakini hatua kwa hatua kama ikizoeleka watu kusema ukweli, kungekuwa hakuna shida….’akatulia na kuniangalia na mimi nilitaka kugeuka kumwangalia Yule mwanadada,lakini nikajizuia

‘Unazani kuwa yote waliyoongea mle ndani ni ukweli, sio kwamba wengine wametungia ili kuficha ukweli….kweli unamwamini huyo Sokoti, ..?’ nikauliza.

‘Karibu kila kitu ninakijua…nilishafanya uchunguzi wa kina,….ila kiuhakika bado kuna utata, hasa ni nani alifyatua risasi iliyomuua Kimwana…kuwahoji hapa ni kutaka kupata uhakika, kama kuna mtu ataongea uwongo, nitambana kwa maswali, maana nina ushahidi wa kutosha, …hilo usijali, mambo yote waliyoongea pale yanaonekana niya u kweli, na ukweli ni nani alifatua hiyo risasi utadhihiri humo humo….’akasema wakili mwanadada.

‘Hapo ndipo unaponichanganya, kama sikosei mwanzoni ulisema unamjau ni nani aliyemuua Kimwana,sasa unasema huna uhakika,….kwahiyo hujui kiuhakika kuwa ni nani hasa alimuua Kimwana, inavyoonyesa bado kuna utata…?’ nikauliza.

‘Wewe subiri, kwa vile mambo yote yapo mbele ya mahakama, utamsikia mwenyewe akijitambulisha,...pale hauna atakaye jificha, ….’akatulia na kuangalia saa yake, halafu akaniangalia an kuniuliza swali;

‘Kwani wewe unazani ni nani anaweza akawa muuaji wa Kimwana?’akaniuliza swali.

‘Mpaka hapo ilipofikia sio rahisi kubashiri, maana kila unayemzania mwisho wa maelezo yake anakana kuwa yeye sio muuaji….mwanzoni wa maelezo ya Sokoti,nilijua kabisa yeye ndiye muuaji,…lakini kakana kabisa kuwa sio yeye, labda kama kuna maswali ya kumbana, mapaka akiri kuwa yeye ndiye muuaji,….hata hivyo, maelezo yake yanaonyesha kabisa kuwa yeye hakushika hiyo bunduki na kumuua Kimwana, sasa sijui ni nani kwakweli…’nikasema huku nikiwaza

‘Usijali ukweli utadhihiri,….kwa wakili kama mimi hadi hapo ningeliweza kubashiri kuwa ni nani,licha ya ushahidi nilio nao, ambao mwisho wa siku kama muuajai atakana nitauweka hadharani,lakini siomahalai pake….’akatulia na kuangalai saa yake.

‘Naona muda tayari tusogee mahakamani….’akasema na mimi kabla ya kuinuka nikaangalia kule walipokuwa mke wa wakili na rafiki yake,nikawaonana wao wakiinuka kuondoka,….na hapo nikapata mwanya wa kumwangalia Yule mwanadada, rafiki wa mke wa wakili akiwa kasimama, na maumbile yake, kwakeli kila kitu kwake kilikuwa kizuri. Kweli nilikiri moyoni kuwa nimempenda Yule mwanadada.

Tulipoingia kwenye kile chumba mambo yaliendelea kama kawaida na Sokoti alimalizia maelezo yake, na muheshimiwa hakimu akauliza kama kuna swali la kumuuliza, wakili mwanadada akasema kwasasa hakuna swali, maswali yatakuja baadaye.

Hakimu akauliza ni nani anayefuata, wakili mwanadada akamwangalia  Yule mwanadada,nesi. Yule mwanadada nesi akakaunja uso, …..na wakili mwanadada akageuka kumwangalia muheshimiwa hakimu, akasema;

‘Naona sasa tumsikia mke wa wakili wetu mkuu….’ Alisema wakili mwadada,na hakimu akaangalia saa yake, na akamuita wakili mwanadada, mkuu wa kituo, wakateta kwa muda ,halafu akasema;

‘Niliwaita hawa wawili kwasababu ndio walioniletea huu utaratibu, nimefurahia sana, lakini hata hivyo ninahitajika kwenye kesi nyingine, dakika tano zijazo, na niliona labda baada ya hiyo kesi tukutane tena, lakini nimeongea na wenzengu wameona tuiahirishe hadi Kesho asubuhi ambapo nitakuwa na  muda wa kutosha.

Ninachowaomba ni kuwa sote tuhakikishe tumehudhuria, mimi nawaamini kwasababu nyie wote ni waajiriwa, na mumeaminika, nia na lengo letu ni kuhakikisha kuwa tunalitatua hili tatizo, tunajisafisha, na tutaona kama kuna hatua nyingine,… lakini hilo litategemea na nyie wenyewe mtakavyokuwa wakweli mbele yangu.

‘Kwa maana hiyo tutakutaka kesho asubuhi, saa tatu….’akasema na kuondoka.

*********

Kesho yake tukafika, na tulipofika tukakutana nje kusalimiana, na baadaye tukaongozana kuelekea ndani. Mimi kama kawaida nilikuwa na wakili mwanadada, alikuwa ndiye mtu wangu wa karibu kuliko wengine waliokuwepo.

Wenzangu wakatangulia kuondoka na sisi tukafuata nyuma yao, nilimuona yule mwanadada kaamua kuwa mwafrika kweli, kasuka kiafrika, na kuvalia nguo nyeusi, sikujua ana maana kuvaa hivyo, maana kila mtu anahulka yake katika mavazi yake, huenda ndivyo alivyoona inapendeza kwake, na kweli elipendeza.

Tukaingia hadi sehemu ya mapokezi, pale kulikuwa na viti, wengine alikaa, lakini yule mwanadada rafiki wa wakili, akasimama nyuma ya kiti na kuwa kama kajiegemeza huku kaweka mkono kidevuni, na walionekana walikuwa wakiongea jambo Fulani la kufurahisha, na wakati tunakuja muelekeo huo waliokuwa wapo wapo, tukawa tunangaliana huku bado akiwa na lile tabasamu mdomoni, sijui alifanya hivyo makusi ili aniangalie au ilitokea hivyo tu…ila moyo wangu ulizidi kuvutika kwake

Macho yetu yalipokutana na yeye, akazidisha lile tabasamu,… huenda ilitokea hivyo kwasababu alikuw akiongea na mwenzake kwani hata mwenzake alikuwa akitabasamu hivyo hivyo, na hapo nikahisi jambo ambalo sikuwa na uhakika nalo, ….akili ikawa inanicheza na kusema haiwezekani, …sio yeye,mbona kabadilika hivyo, haiwezekani….

Na mara akaja askari na kutuambia kuwa  tumebadilishiwa chumba, maana kile tulichokuwa tukikitumia kinatumiwa na watu wengine, kwahiyo sisi tukaambiwa tuingie kwenye ukumbi wa mahakama kwani kwa muda huo ulikuwa hautumiki. Ilitisha kidogo kuingizwa sehemu hiyo, kwani ilikuwa kama kweli mtu anahukumiwa.

‘Samahanini tutatumia humu ndani, lakini sio kwamba kweli mtu anahukumiwa, utaratibu wetu ni ule ule, kama mwanzo….’akasema hakimu. Na kwa kuanza tunamuomba mke wa wakili mkuu apite mbele tuendelee na zoezi letu

Mke wa wakili mkuu akiwa kavalia sare na rafiki yake, na kudhihirisha kweli wanafanana utafikiri mapacha, akainuka haraka na kwenda sehemu ya kizimba, hakimu akasema asiiingie mle ndani yeye akae kwenye kiti kilichokuwa pale mbele..akakaa bila wasiwasi, alionyesha kujiamini, hana wasiwasi…

Kwanza macho yake yalitua kwa mume wake., mume waka akatabasamu na kutikisa kichwa, akionyesha kumpa uhakika kuwa yupo pamoja na yeye kwa lolote atakalosema. Na baadaye akazungusha kichwa na kumwangalia wakili mwanadada, naye akatabasamu na lakini hakutikisa kichwa kama alivyofanya mume wake. Na halafu akamtupia jicho kwa haraka, mwanadada nesi, mwanadada nesi akamwangalia kwa dharau.

Nilishangaa, kama hawa ni ndugu kwanini kuna kamauhasama uliojificha, wanagombea nini,….au ndio kama alivyosema kuwa wakili mkuu walikuwa mchumba wa mwanzo wa huyo nesi, lakini hata kama ni hivyo,mbona mke wa wakili, kama inavyojulikana ndiye aliyemsaidia kutafuta kazi huku Dar.

Nikamwangalia Yule mwanadada,ambaye alikuwa kakunja uso kwa hasira,na mara na yeye akaniangalia, na kwa ajabu kabisa katabasamu. Lile tabasamu,yale macho, yakanifanaya moyo wangu ushituke. Sijui kwanini, nikajikuta kichwa kikihangaika kukumbuka jambo,lakini sikuweza kugundua ni nini.

‘Hebu tueleze kwa kifupi wewe ni nani, na maisha yako na mumeo…..’alianza wakili mwanadada baada ya maelezo ya mwanzo ya utambulisho, ambayo aliulizwa na muhushimwa hakimu.

‘Kama nilivyosema awali, mimi ni mke wa wakili mkuu, na nilizaliwa huko Ulaya, licha ya kuwa makazi yetu ni Kenya, na nawashukuru sana wazazi wangu kuwa baada ya kunizaa ni pacha mwenzangu, tulipelekwa kwa babu babu na bibi, waliokuwa wakiishi Kenya. Babu na bibi wao ni Watanzania ile kwasababu ya biashara, walijiukuta maisha yao wakiwa zaidi Kenya kuliko Tanzania.

‘Pacha mwenzangu yupo Kenya,…nilikuja kuishi huku kwasababu ya mwenzangu, ….’hapo akatulia na kumwangalia mumewe, halafu akaongezea kwa kusema; `nina maana mume wangu…’akatulia na mumewe akatabasamu.

‘Maisha yangu na mume wangu mwanzoni yalikuwa mazuri, lakini nakiri moyoni kuwa jinsi majukumu ya akzi yalivyoongezeka ndivyo mapenzi yetu yalivyoanza kuingia doa. Nilijikuta natumia muda mwingi kazini, na kama mnavyojua kazi zetu, za udakitari, kukutana na watu,kwenda hapa na pale, kuwahudumia wagonjwa walio mahututi, na hata kusaidia katika upasuaji,kuzalisha,..yaanai unarudi nyumbani upo hoi.

‘Ikawa nikirudi nyumbani nimechoka, nab ado majukumu ya nyumbani yanakusubiri, kama ujuavyo, mke ni pamoja na majukumu ya nyumbani, hata kama una mfanyakazi bado unawajibika na mambo yote ya nyumbani. Tofauti na akina baba , na hasa akina baba wengine ambao wakirudi nyumbani , hawagusi kitu, zaidi ya kusubiri kutengewa chakula, maji ya kuoga….’akatulia na kumwangalia mume wake.
Mume wake alionekana kusema kitu mdomoni,lakini hakutoa sauti.

‘Je mume wako hakuwa akikusaidia majukumu ya nyumbani,kama vile kuosha vyombo, kufua na hata kupika…?’ akauliza wakili mwanadada, na wakili mkuu akajikuta akicheka, na kutikisa kichwa.

‘Kama unavyoona akitikisa kichwa, yeye anajua kuwa hizosio kazi zake, ni kazi za mwanamke,na mimi sikujali sana kuhusu hayo, nilijua hali halisi yetu sisi Waafrika,licha ya kuwa kwa kiasi kikubwa tulikulia Ulaya tukaona jinsi wenzetu wanavyoishi huko, jinsi baba na mama walivyokuwa wakiishi,lakini bado tulikuwa tunajua milana desturi zetu sisi kama waafrika….’akatulia.

‘Nawashukuru sana baba na mama waliokuja kuliona hilo na kuwa mara kwa mara walikuwa wakiturudisha nyumba ni kuishi na babu na bibi, na pia washukuru sana babu na bibi ambao walijibidisha sana kutufundisha maisha ya mwanamke wa kiafrika, anavyotakiwa awe, hilo lilinisaidia sana vinginevyo, sijui kama ningeliweza kuishi na mwenzangu.

‘Na mwenzako ukiwa na maana gani?’akauliza hakimu.

‘Nikiwa na maana mume wangu….’akasema

‘Uwe muwazi ….endelea…’akasema hakimu.

‘Nakiri kuwa ilifikia mahali maji yakazidi unga, nikawa sitimizi baadhi ya majukumu yanayonihusu, lakini sio kwamba niliamua moja kwamojakuwa sitaki,nilimwambiamwenzangu kuwa nimechoka,au sijisikii, lakini mwenzagu hakupenda kauli hiyo, na alikuwa akinisema sana, na hata ikafikia hatua ya kujibisha na hata kupigana….

‘Yeye alisema nini, ulipomwambia kuwa umechoka, au hujisikii…?’ akauliza wakili mwanadada.

‘Alisema hiyo ni kazi yangu, na mimi kama mke wake ,hataki kusiki kauli hiyo, kwasababuu kanioa, na ukiolewa,yote yanayokustahili kama mwanamke,ni lazima uyatimize,na kama naona kuwa nachoka kazini, niache kazi….’akasema.

‘Kwanini hukuacha kazi..?’ akaulizwa.

‘Jamani,mimi wazazi wangu walipoteza pesanyingi sana kunisomesha, ili niwe dakitari, na hata mimi mwenyewe ni kazi ambayo naipenda, na pia napenda sana kuhudumia wagonjwa,ni kitu ambacho kipo kwenye damu. Udakitari licha ya kuwa ni kazi,lakini ni wito, ukiwa na huowiti, sizani kwamba utajisikai vyema kuona mgonjwa yupo hapo usimuhudumie…..’akatulia.

‘Ilifikia hatua nikawanajiuliza ni nani aliye bora,mume wangu au wagonjwa ninaowahudumia, nikajikuta sipati jibu,ilakukicha,nakumbukakuwa kuna wagonjwa wananisubiri, kuwa akina mama wanahiji kusaidia katika kujifungua, kuna…..hapo akili inahama na mbio nakimbilia hospitalini na kumwavha mume wangu akiwa hana raha,….inaniuma lakini nitafanyaje.

‘Wewe ni muumini wa dini , na unajua nini kuhusu ndoa….?’ Akauliza wakili mwanadada.

‘Ndio najua hilo, kuwa mume wako ni seheumu ya mwili wako, najua kuwa kila mmoja anatakiwa amtimizie matakwa mwenzake,bila kukataa, labda uwe na sababu maalumu, na mimi nilikuwa na sababu maalumu, kama mwenzangu angelikuwa na ubinadamu, hebu nikuulize wewe kama wakili, je kuna kesi ipo mbele yako, na mara mume wako akaupigia simu kuwa anakuhitaji, utakatisha hiyo kesi ukamtimizie matakwa yake?’ akauliza.

‘Hapo unazungumza mtu yupo  kazini,lakini wewe ulikuwa ukimkatalia mwenzako wakati upo nyumbani, huhudumii waginjwa, upo huru kufanya yake anayohitaji mume wako. Ukamkatalia kwa sababu ya kuchoka,na kutojisikia, huoni hilo ni kosa,?’ akauliza wakili mwanadada.

‘Ndio ni kosa,….lakini nimeshajieleza kwake kuwa nimechoka na sijisikii anipe muda..sio kwamba nilifanya kiburi na kumkatalia bila sababu…mwili wa binadamu ukichoka hauna jinsi, hata kama utavuta hisia namna gani, utaishia kuwa gogo, na sijui kama mtashibishana,….mimi najua hayo, kwasababu ni dakitari, na pia nimekulia katika mazingira ambayo baba na mama yangu walikuwa wakisaidia watu wenye matatizo ya namna hiyo , na kwahiyo sikuwa nafanya makusudi….’akasema.

‘Hebu nikuulize mara ngapi kwa wiki au kwa mwezi uliweza kuwa na nafasi na mume wako?’ akaulizwa.

‘Kwa wiki ni mara moja au mara mbili…kama unavyojua mimi nafanya kazi sehemu ambayo nahitajika karibu kila siku….’akajitetea.

‘Ina maana kwa wiki nzima au mwenzi mzima, ulikuw hauna nafasi na mume wako, ni mara moja au mara mbili tu?’akauliza wakili mwanadada.

‘Hapana….wakati mwingine zaidi ya mara mbili,..lakini kiuhakika ni mara moja au mara mbili kwa wiki ndipo naweza kusema nakuwa na nafasi na mume wangu…hata hivyo bado una majukumu ya nyumbani,kazi za nyumbani zinakusubiria, minguo imajazana,…..ooh, sijui niseme nini….,lakini mwenzangu yeye alihitaji karibu kila siku…atimiziwe haja yake….’akasema na watu wakacheka.

Na wakili mkuu akatikisa kichwa kama vile kutamba kuwa yeye ni mwanaume halisi…..
Muda umeisha na sehemu hii ni muhimu sana kutokana na kisa chetu. Hebu niwaulize, mke huyu alikuwa na makosa, …..? jibuni hata kimiya kimiya sio mbaya. Tukijaliwa tukutane sehemu ijayo.

WAZO LA LEO:  Kukosoana kupo, na hata kuelekezana, lakini tunapofanya hivyo tusikimbilie kulaumu pale mwenzako anapokosea, maana mara nyingi ni wepesi sana kuona makosa ya mwenzako kuliko kuona makosa yako. Tunasahau kuwa tunaponyosha kidole kimoja kwa mwenzako kuna vidole vitatu vinakuelekea wewe.


Ni mimi: emu-three

3 comments :

Anonymous said...

Mtoto huyoooo, m3 bwana unajua kuturusha roho, unatuwekea oicha za warembo, sasa huyo ndiye nani? Hata hivyo nakuaminia mkuu

Anonymous said...

Hebu nikuulize haya ni ya kweli na kama ni ya kweli, unapata wapi muda wa kuyaandika, maana sio mchezo? ni swali tu!

Anonymous said...

Kusema ukweli huyo mwanamke hana makosa, hayo ni makosa ya mumewe, huwezi kumuachia mwenzio afanye kila kitu achoke hoi kama punda kisha utegemee akuhudumie na wewe. Yeye angekuwa na ubinadamu angelimsaidia mwenzie!