Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Monday, May 28, 2012

Hujafa hujaumbika-42



Niliambiwa kuwa nahitajika kwenda kumuoma mgonjwa kwani keshazindukana na anahitaji kuniona mimi, nikajiandaa kwa haraka, na moja kwa moja nikachujuliwa kwenye gari , hadi huko hospitalini, na tulipofika tulikuta walinzi, yule dereva aliyenichukua akajitambusliha na kuonyesha ushahidi wa maandishi kuwa kweli ni yeye, ilikuwa ni utaratibu, lakini wanamjau kuwa ni mmoja wa dereva wao, tukaruhusiwa kupita baada ya mimi kukaguliwa mwili mzima kuwa sina silaha yoyote.

Nikaingizwa kwenye chumba cha maalumu cha wagonjwa mahututi, na pale nikamuona mgonjwa akiwa kalala mipira yote inayohitajika ikiwa imewekwa mwilini mwake, nikasogea na kusimama mbele yake, alikuwa kafumba macho, baadaye akayafumbua na kuniangalia, …kwanza aliniangalia kwa makini, halafu kama anatoa mshangao, akasema;

‘Sasa hivi sitaki kuongea na wewe, bado najisikia vibaya, ngoja nipumzike kidogo, nitakuona baadaye…usiondoke mbali…’akafumba macho na mimi nikabakia nimeshangaa, maana niliambiwa kuwa huyo mgonjwa anataka kuongea na mimi, lakini yeye mwenyewe anasema bado hajisikii vyema.

Nilisimama pale kwa muda mara akaja askari na kuniuliza kuwa mgonjwa kasema nini, nikamwambia, mgonjwa kazungumza kwa sauti ya shida akasema anajisikia bado anajiskia vibaya, anahitaji kupumzika kidogo, ataongea na mimi baadaye, kwahiyo nisubiri,nisiende mbali….

Basi yule mlinzi akaniambia nikakae pembeni, kuna sehemu wanapokaa madakitari, nikaambiwa nikae hapo nisubiri, ni chumba kidogo,ila unaweza kuona kule kitandani.

Nilikaa pale kwa muda mrefu hadi usingizi ukanipitia, na mara nikazindukana, ….sijui ilikuwaje ,ila nilipofumbua macho, niliangalia moja kwa moja  kule kwenye kitanda alipolala mgonjwa, nikaona daktari kamuinamai mgonjwa,…akawa kama anamwangalia , akasimama na  kuchunguza ile mipra iliyokwenda hadi kwenye mashine, akasogea hadi kwenyemipira mmojawapo akaukata na mkasi…

Nikashangaa, …akasoge kwa nyuma na kusubiri kidogo,  akamwangalia mgonjwa, ambaye alikuwa kama anatingishwa, akasoegea pembeni na mara akasogelea ile mashine ambyo mwanzoni kwa umbali ule ilikuwa ikionyesha ile mistari ya kupanda na kushuka sasa ikawa imenyooka, na ikawa inapiga kelele, akasogea mbali na akageuka akawa anakuja pale nilipokuwa nimekaa, moyo ukaanza kunidunda,…

Alikuja hadi pale nilipokaa, kwa jinsi nilivyokuwa nimekaa pembeni, hakuniona kwa haraka, alichofanya ni kuvua ile miwani yake, akawa kama anaipangusa na kitambaa, halafu akageuka,  akaniona, alishituka, lakini akajifanya kama vile hajashituka, aliniangalia kwa muda bila kusema kitu.Mimi kwa kiherehere change nikamuuliza;

‘Docta vipi,mbona umeukata ule mpira wa mgonjwa huoni kuwa ndiyo inayomsadiai kupumua…?’ nikamuuliza.

Hakusema kitu, akageuka kutaka  na kunitizama, huku akiwa kava miwani, akasema ;

‘Mgonjwa alishapona, hahitaji ile mipira anampa shida….na hayakuhusu wewe,….’akaondoka hadi mlangoni, alipofika pale mlangoni, akaataka kamakurudi, lakini alihisi kuna matu anakuja, akageuka nakuondoka kwa haraka.Mimi bila kupoteza muda nikaenda pale alipolala mgonjwa nikamwangalia, nilikuta katulia kimiya, huku macho yamemtoka..

Nikarudi pale nilipokuwa nimekaa, nikaona sehemu ya simu ya kuita dakitari nikapiga haraka, na mara dakitari akaja ;

‘Mbona kaja dakitari hapa na kukata ule mpira kwa mgonjwa,….?’ Nikauliza.

‘Eti nini….!, dakitari, dakitari gani huyo….?’ Yule dakitari akashangaa, akaenda pale alipo yule mgonjwa, na kuangalia, akakuta ule mpira kweli umekatwa, akachukua simu yake na kupiga namba,mara wakaja watu wanne, wakachunguza na baadaye , wakamfunua yule mgonjwa….

Yule dakitari wa mwanzo akaongea na mwenzake, na yule mwenzake akaja pale nilipo na kuniambia nitoke mle ndani niende nje, maana wapo kazini,….nikasita , kwani nilitaka kujua nini kinaendelea, lakini yule dakitari akawa kanishika mkono na kunivutia nje,… nikatoka, na nilipofika mlangoni nikageuka kuangalia kule kitandani, nikashangaa, na kabla sijaweza kuangalia vyema,… yule daktari akafunga mlango haraka, nikabakia pale mlangoni, nikiwaza, ni kweli nilivyoona au nimacho yangu tu, yanajenga hisia.

*******
Nilipotoka pale hospitalini, sikurudishwa kule kwenye mahabusu, nilipelekwa nyumbani kwa Mkuu, waliniambia wanafanya hivyo kwa ajili ya usalama wangu. Nilipouliza ni nani anataka kunizuru, wakasema hawataniambia hilo kwa sasa.

Nikafika kwa Mkuu, nilikuta ulinzi mkali, nikaonyeshwa chumba ambacho natakiwa nikae, kama mahabusu, nilijiona huru kidogo, ingawaje niliitwa mahabusu, nikaonyeshwa kazi ambazo natakiwa kufanya kila siku, kuhudumia bustani na kazi ndogo ndogo za hapa na pale.

Kesho yake nilichukuliwa na kwenda kule hospitalini, nikaambiwa kuna gwaride la utambusho , natakiwa kumtambua huyo docta niliyemuona akiukata ule mpira kwa yule mgonjwa.

‘Ukimuona utaweza kumkumbuka…?’ akaniuliza askari mpelelezi.

‘Ninaweza maana alivua miwani nikamuona vyema usoni…’nikasema.

‘Hakikisha kuwa unamkumbuka vyema, ni muhimu sana…’akasema huyo mpelelezi,

Basi gwaride hilo la utambulisho , likafanyika, lakini sikuweza kumtambua huyo dakitari, hakuwepo kabisa, na wakasema zoezo hilo limekamilika, nikaambiwa nirudi huko nilipokuwa. Zikapita siku mbili, na ya tatu, wakaniambia kuwa nimekubaliwa kupewa dhamana, lakini sitakiwi kusaafiri au kwenda mbali ya hili jiji. Nikashukuru sana angalau nipo huru, licha ya kuwa nipo kwenye uchunguzi .

 Siku hiyo nikiwa nyumbani kwangu wakanijia wageni , alikuwepo mkuu, mwanadada mpelelezi na mkuu, walisema kuwa walikuja kwangu kuna mambo wanataka kuyaweka sawa, wanahitaji  kunihoji maana kesi imeshakamilika na kesho yake itakuwa siku ya kuipeleka mahakamani, ninaweza nikahitajika. Nikasema haina shida.

Wakili mwanadada na mkuu, wakakaa kwenye kiti, lakini wakili mkuu, yeye alikuw akasimama, akiangalai nje, kwakupitia drishani,nilimuona kama ana harakaya kutaka kuondoka, kinyume na wenzake, wakisema kuwa hawahitaji muda wangu mwingi ni maswali machache ya hapa na pale.

Aliyeanza kuniuliza maswali ni mwanadada wakili, akaniuliza , naweza kumuelezaje yule docta aliyefika siku ile kule hospitalini. Nikawaelezea jinsi anavyoonekana, na niliwatizama wote kuangalia kuwa nani mwenye umbile sawa nay eye, sikuweza kumlinganisha na yoyote, ila nikaona kama anakaribiana na …, nikasema.

‘Umbo lake linakaribiana sawa kidogo kama huyo wakili wenu mkuu…’nikasema na yule wakili mkuu akageuza kichwa na kuniangalia mra moja, halafu akawa akageukia huko alipokuwa akiangalia, na baadaye akauliza swali bila ya kuniangalai aaksema.

‘Una uhakika na hilo…maana ni muhimu sana kwetu…?’akaniuliza huyo wakili mkuu.

‘Nimesema kiumbile wanakaribiana, sina uhakika zaidi ya hilo…’nikasema.

Waliniuliza maswali mengine, na baadaye waliporizika wakaondoka, na siku inayofuata akaja wakili mwanadada, na tukawa tunaongea mambo mengi, baadaye akaniuliza swali ambala waliniuliza jana yake.
‘Una uhakika ukimuona huyo docta hata leo unaweza kumkumbuka vyema..?’ akauliza.

‘Kwanini nisimkumbuke, sura yake haijanitoka, lakini kuna jambo nataka nikuulize kwanza’nikasema.

‘Uliza….unataka kuuliza kuhusu nini, uliza tu,…?’ akasema na kuniangalia kwamashaka huku akijaribu kutoa tabasamu,licha ya kuonekana kukerwa, hakuwa na uso wa furaha, nikajua labdani kwasababu ya kazi nyingi.

‘Mna uhakika kweli kuwa yule mgonjwa kafariki ?’ nikauliza,na yeye akawa kama kashituka na kuniangalai bila kunjibu kwa muda akasema;

‘Kama mgonjwa alikuwa akipumulia mshine, na ile mashine ikaondolewa mipira kabla hajazindukana anaweza akapona…wewe mweyewe unakiri kuwa ulipoingia ulimkuta kakodoa macho kuonyesha kuwa uhai haukuwepo….hukumgusa,kuhakikisha ?’ akaniuliza.

‘Sikumgusa, na kweli kama mtu alikuwa akipumulia mashine,ikiondolewa, sizani kama anaweza kupona, na kweli nilipofika pale niliona ile mishale ya kuonyesha uhai ilikuwa imesimama, na hata mgonjwa  mwenyewe alionyesha kabisa kafariki, maana alikuwa katoa macho….lakini…’nikasema.

‘Lakini nini tena….usihisi vitu kama hivyo, unachotakiwa ni kusema ulichokiona,sio kuhisi,…..nikuulize swali,kwanini unamashaka, na kwanini ukaniuliza hilo swali?’akauliza wakili mwanadada, nikawaza kwa muda, nikashindwa la kuongea, maana hisia zangu siku ile zilinisuta, nilikuwa na uhakika kabisa, kuwa yule mgonjwa alikuwa kafariki, ingwaje sikumgusa, lakini wakati natoka pale mlamngoni niligeuka nakaona kama yule mgonjwa alikuwa kaka kitandani akiongea na wale madakitari, …huenda ni hisia zangu tu,…sikusema kitu tena.

‘Una mshaka gani..?’akaniuliza tena wakili mwanadada.

‘Hapana, maana hisia zangu zinanituma kama huyo mgonjwa,……hapana, unajau mimi ninakuw ana mahisia ya ajabu,huenda ni kuchanganyikwia tu, ila natamani nimuone huyo…hayo maiti kwa kwanza ili nihakikishe mwenyewe…..’nikasema.

‘Ina maana unataka ukaikague hiyo maiti yake uhakikishe  kuwa kafa,kama unahitaji hivyo ninaweza kukufanyia huo mpango, haina shaka,….’akasema wakili mwanadada.

‘Hapana….  sio hivyo, ..haina haja, kama wewe umethibitisha hilo, haina haja….’nikasema na kutulia kimiya, na baadaye huyo wakili mwanadada akaondoka,na kuniambia niwe mwangalifu katika majibu yangu, na pia niwe mwangalifu kiusalama, nisiondoke ondoke sehemu yoyote bila kutoa taarifa. Nikasema nitafanya hivyo.

 Ilikuwa usiku wa saa sita hivi, nikiwa nimechoka sana,nilipata kibaraua sehemu, na nilifanay hiyo kazi hadi saa kumi, nilipotoka hapo nikaenda sehemu nikapata chakula ambacho nilikichukuliwa kama mla wa siku, na kurudi nyumbani kwangu, sikutaka kutembea sehemu nyingine yoyote maana nilishakanywa kuwa kuna watu wanataka kuniua.

 Ilipofika saa sita za usiku, nikasikia mtu anagonga mlango, nikashituka, kwanza niliogopa kabisa kumfungulia, lakini alipoondelea kugonga, ikabidi nimuulizekuwa yeye ni nani...

‘Mimi ni askari usalama usiwe na wasiwasi….’akasema huyo mtu, nikafungua mlango kwa mashaka.

‘Mbona unaniamusha mudakaam huu ,kuna tatizo …?’ nikamuuliza.

‘Kwasababu ni muhimu sana, na nimetoka kufuatilia mambo fulani kuhusu hii,kesi, na nimeona kabla sijalala niwe na uhakika na jambo moja dogo tu, usijali,na samahani kwa kukusumbua, najua unanikumbuka…’akasema , aliposema `unanikumbuka'  nikamwangalia, sikuwa nimemwangalia vyema mwanzoni,baada ya kusema yeye ni askari usalama,nilishaju labda ni mmoja wa hawo walinzi niliowaona hapo nje.

‘Lakini muda kama huu, jamani…aaah, ni wewe tena, mimi nilijua tumemaliza mchana,…’nikalalamika.

‘Hatuna muda maalumu kwetu, tukihitaji jambo au tukigundua jambo, lazima tulifuatilie, na mimi nimegundua kitu, unajue pale tkupokuja mchana kukuhoji ulinitia mashaka kidogo, angalia yako kwangu ilinitia mashaka, ndio maana nimekuja kukuuliza vyema, nataka kuhitimisha taarifa yangu….’akasema.

‘Sawa lakini nilisema wewe unafanana na huyo docta kimaumbile, sio kabisa kabisa,….’nikasema na muda huo tukawa tumetizamana uso kwa uso, na mwanga toka dirishani ukawa uammulika usoni, na kwamuda huo alikuwa hajavaa miwani, akili yangu ikagundua kitu, sikuwahi kutizamana naye uso kwa uso jana yake,…,laini sasa tulipoangaliana nikakumbuka na mwili ukaanza kunisisimuka,a…..kilichoniponza ni kutokuwa mvumilivu, nikamuuliza swali;

‘Kuna ndugu yako ni docta…?’ nikamuuliza.

‘Kwanini unaniuliza hivyo…?’ akasema.

‘Kwasababu nahisi kama unafanana na yule docta,  nakumbuka kabisa yule docta alipovua ile miwani, mnaonekana kufanana naye kabisa hata sura….’nikasema.

‘Una uhakika na hilo,..? ‘ akaniuliza kwa sauti kali kidogo, halafu akailegeza na kusema

‘Ndilo maana nimekuja kukuona tena, nilitaka kujua kuwa kweli unakumbuka vyema,…usiwe unahisi , uwe na uhakika na hilo uliloliona, ukihisi na kuongea kitu ambacho huna uhakika nacho utaenda jela,..mimi sio docta, na walsinandugu docta, chunga sana mdomo wako,…’akasema na kutabasamu.

‘Una maana gani kusema hivyo,….kwani,ni…mbona… ?’nikakawa nimeshikwa na kigugumizi, na akawa kama anataka kuondoka akasema;

‘Kwasabbu kesi itaanza kesho na wewe unatakiwa twende ukawaangalia mdakitari wote tena kuhakikisha hilo, ili kama unaweza kumkumbuka huyo dakitari uliyemuona…..inawezekaan siku ile hukuwa makini katika utambuslho ule, ….’akasema huyo wakili.

‘Lakini kazi hiyo nilishaifanya, na sikuweza kumuona docta yoyote anayefanana na huyo niliyemuona…labda kama kuna mwingine kaongezeka..’nikasema.

‘Haina shaka, ….tutaona hapo kesho, tukijaliwa,….hata hivyo naona kuna kitu kinafanyika nyuma ya mgongo wangu, tusubiri hiyo kesho, tutaona mwisho wake….na nakukuanya tena, usiwe unajibu kutokana na hisia zako,…ukijifanya mjanja uanongea saana, utajiponza…..haya lala salama na omba sanamungu wako…..’akasema na kuanza kuondoka na mimi nikaongea kujikosha,hasa palenilipomuona kuwa amekasirika.

‘Mimi ….nilisema kuhisi na kulinganisha tu muheshimiwa, sikuwa na maana mbaya kwako wewe muheshimiwa, nilipewa hicho kibali cha kumuona huyo mgonjwa, tu, mengine yaliyotokea mimi sikujua kuw ayatatokea, na sio kuwa ni wewe niliyekuona…, nafafanisha tu muheshimiwa niwie radhi,kama nimekosea, nitachunga mdomo wangu…’nikasema.

‘Haina shida….’akasema na kuondoka.

Alipoondoka yule wakili nikapokea simu, kutoka kwa wakili mwanadada, akaniuliza kuwa nilitembelewa na nani, nikamwambia, akasema amekuja baada ya kusikia kauli yangu kuwa huyo docta niliyemuona anafanana na huyo wakili, aliamua kuja kuthibitisha kumbukumbu zangu kuwa una uhakika na hilo ulilolisema,….’akasema.

‘Lakini swali mliloniuliza lilitaka nilinganishe na umbile, `anafananaje', ningejibuje bila kulinganisha na kitu ninachokiona,kosa langu hapo lipo wapi…..?’ nikauliza.

‘Ndio maana nahitaji uwe makini katika majibu yako, sema kile ulichokiona usijibu unavyohisi,,…sawa..kama kuna lolote bonyeza simu yako pale nilipokuonyesha,na hakikisha humfungulia  mtu mlango kwa hivi sasa uwe makini, …

‘Lakini nakumbuka mlisema kuwa kuna walinzi wananilinda, nanimeona walinzi hapo nje wakiwana silaha,….’nikasema

‘Ndio wapo walinzi, lakini huwezi jua, ukio na mashaka, tumia akili yako, usiwategemee sana,, ….’akasema na kukata simu.

Sikuweza kupata usingizi, nilihakikisha kuwa nimefunga mlango vyema , kitanda changu kipo eneo la dirishani, hapo ikanitia wasiwasi, nilichofanya ni kuweka mito, mfano wa mtu aliyelala, nikahukua kigodoro kidogo, na kujilaza chini ya meza yangu kubwa, ….hayo niliyafanay kutokana na zile hisia zangu zinavyonijia.

Nilizindukana toka kwenye usingizi, ilikuwa kama saa tisa hivi, nikahisi dirisha likiguswa, na mara nyavu za dirisha zikakatwa, sikusogea pale nilipo, niliinua kichwa kwa mashakanakutizamadirishani ….nikasubiri.

Kwanza nilihisi labda ni wezi, lakini mbona nimeambiwa kuwa kuna walinzi wananilinda kwa nje,nikasubiri…
Mara nikaona kitu kikijitokeza, ni kurunzi ndogo,ikawainamulikapalekitandani, na mara  kikatokeza kitu kingine, ….moja kwa moja nikajua ni sehemu ya mbele ya bastola, ikaelekezwa  pale kitandani,…ambapo nalala, risasa zikafyatuliwa tatu mfululizo,…..tufu-tufu tufu…., lakini hiyo bastola haikutoa sautii, nafikiri walikuwa wameweka kitu cha kuzuia risasi, na baadaye kimiya kikatanda.

Haikupita muda akaja, wakili mwanadada, akagonga mlango na kujitambuslisha, na mimi nikamfungulia, akaniangalia usoni kwa mashaka na kuniuliza nini kimtokea, nikamhadithia akasema anahisi kati ya walinzi kuna ambao sio waaminifu, hajajua ni nani, lakini hilo watalimaza leo hii.

‘Kwa vipi….?’ Nikauliza.

‘Tumeona tukizidi kuvumilia mambo yatazidi kuwa mabaya, na uhai wako utakuwa hatarini, tuna ushahidi wa kutosha kwa sasa, na huyo aliyekuja kwako na kukata nyavu za dirisha alikuwa akifuatiliwa kwa karibu, nashindwa alifikaje na kufanya hivyo, wakati wapo walinzi hapo nje….’akasema wakili mwanadada.

‘Kwani ni nani huyo….?’ Nikauliza huku nikiwaza mengi yaliyotokea, na wakili mwanadada akaniangalia kwa makini, na kabla haongea kitu, mara mlango ukagongwa na aliyeingia alikuwa mkuu, na yeye akanitizama kwa uso wa wasi wasi, akaniuliza.

‘Vipi upo salama….?’ Akauliza.

‘Nalijua mlitajia mtaikuta maiti, au sio,..lakini kama unavyoona mkuu nipo salama…ila mpaka sasa siamini kuwa nipo hai, …hapa nilipo mwili mzima unatetemeka..’nikasema na mkuu akamgeukia wakili mwanadada nakusema;

‘Usituelewe vibaya kabisa, ….’akasema na na bila kuongeza neno akamgeukiwa wakili mwanadada na kusema;

‘Mtu wetu katoweka,…..’akasema.

‘Unasema nini mkuu….toka muda gani, mbona sielewi, mambo mengi yanatendeeka sivyo kinyumena tulivyopanga,….atakuwa kaendawapi huyu mtu?’ Akauliza kwa huku akiwa katoa macho ya kushangaa..

‘Nahisi keshagundua kuwa yupo matatani, …maana kulipopambazuka tu, akawa haonekani, na simu zake zote hazipatikani, na mkewe anasema hajui mumewe aliondoka muda gani, na hajui wapi alipokwenda, maana jana yake walikorofishana, na kila mmoja alilala kivyake,….’akasema mkuu.

‘Ina maana wanalala chumba tofauti….?’akauliza waliki mwanadada.

‘Wana chumba cha akiba, huwa wakikorofishana mmojawapo  anakwenda kulala kwenye hicho chumba chao cha akiba, kwahiyo yeye hakuona ajabu alipoamuka na kumkuta mumewe hayupo, ndivyo wanavyoishi, ….ila kilichomtia mashaka ni kuona kuwa abadhi ya nguo hazipo, na moja ya sanduku la kusafiria halipo, kuonyesha kuwa huyo mtu kaondoka safari….’akasema mkuu.

‘Na huyo mkewe yupo wapi kwa muda huu..?’ akauliza.

‘Kashikiliwa kituoni, tunaona njia peke ya kumnasa huyu mtu ni kumshikilia mkewe…..’akasema mkuu.

‘Hapana msifanye hivyo, muachieni na inatakiwe iwe kama hakuna mtu anayemfuatilia, tutamnasa tu, sizani kama katoka nje ya hili jiji,atakuwa kajificha kwenye moja ya nyumba zake ndogo, wasambaze vijana wako waaminifu….’akasema wakili mwanadads.

‘Hilolimeshafanyika, na ….kweli tumamuachia huyo mke wake, alikuwa nahitaji muongee na yeye,anasemani muhimu sana….’akasema mkuu.

‘Sasa kazi imeanza,ni muda wakuwa waangalifu kuliko sikunyingine zote, na ulinzi mkali unahitajika, na tunahitaji watu watu wanaoaminika, …kutoweka kwa huyu jamaa kunatuweka kwenye mashaka makubwa, sijui ana mipango gani, …hapa naingiwa na mashaka kuwa lolote baya linaweza likatokea…’akasema na kumgeukiwa wakili mwanadada na kuendelea kuongea kwa kusema;

‘Nashauri, tumuondoe huyu mtu hapa haraka, ….ni bora aje akakae kwangu…’akasema mkuu na kabala hajaendelea kuongea nikasema kwa haraka;.

‘Hapana mimi siendi popote, ….hisia zangu hazimwamini mtu yoyote tena, naona nitajilinda mwenyewe kuanzia sasa, maana lililotokea usiku wa leo, limenipa fundisho,nitajua wapi pa kwenda na jinsi gani nitajilinda, nahisi sina usalaam tena, nikiwategeema nyie….’nikasema huku nikiwa na mawazo mengi.

‘Usijali upo kwenye ulinzi, yote yanayofanyika yanafuatiliwa kwa karibu….huo ulikuwa mtego…ila…’akasema wakili mwanadada nakumwangalia mkuu, akitaka kusema kitu.

‘Niwaulize kama nisingelikuwa na wazo hilo la kujificha , na kuweka mito kama mtu aliyelala, ningekuwa wapi saa hizi,….kama ni ulinzi wa namna hiyo wa kiniweka mimi kama chambo, sikubali tena, nimechoka na matatizo,…..’nikasema na wakili mwanadada akniangalia akionyesha uso wa kutahayari, akageuka kumwangalia, alitaka kusema kitu, lakini mkuu akawahi nakusema.

‘Mungu yupo pamoja na wewe, tunakubali kuwa kuna kosa limefanyika, na hilo tumeshalisawazisha, mengine ni mambo ya ndani,kama yupo mtu nyuma ya hili tutamshughulikia, na hilo tunalifuatilia kwa karibu….ujue kila kitu hutokea ili iwe ni sababu …na hata kama tungeliweka ulinzi wanamna gani,kama lilipangwa kutokea lingelitokea tu,…hapa tuliweka watu, tukijua hakuna mtu atakayefika kwako, lakini wamefika….nahisi kuna mtu anatusaliti….’akasema mkuu huku akikwepa kuniangalia machoni.

‘Kwamtaji huo, mimi nitajilinda mwenyewe, sihitaji ulinzi wenu tena, kwani nimegundua kuwa kil nikIutegemea ulinzi wenu, nijikuta naingia kwenye matatizo, angalia kama leo, kama nisingejihami mwenyewe, nini ingetokea,,….’nikasema na wote wakaniangalia huku wametahayari usoni.

NB: Tunakuja sasa kwenye hitimisho, ambapo maswali mengi yaliyokuwa ymejificha yatagundulikana, nii nanii huyo yupo yuma ya haya yote, je mgonjwa aliyekufa ni nani, na kwanini hisia za msimuliaji zinasema `hajafa' hayo namengine mengi tutakuja kuyaona. Tupo pamoja

WAZO LA LEO: Tujaribu sana kuchunga ndimi zetu hasa pale tunapohisi jambo bila kuwa na ushahidi nalo, Unaweza ukongea jambo kwa nia njema tu, kumbe ile kauli ikatafsiriwa vibaya,na matokeo yake ikaleta dhahama, kwahiyo ni bora kukaa  kimiya kama huna ushahidi kuliko kuongea kutokana na hisia zako ukazusha mikangano isiyo ya lazima. kama walivyosema wahenga,bora nusu shari kuliko shari kamili. 

Ni mimi: emu-three

1 comment :

Anonymous said...

Kazi nzuri iliyoenda shule