Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Friday, April 27, 2012

Hujafa hujaumbika-28



Nikiwa nimeshika ile picha mkononi, niliinua kichwa na kumwangalia Yule wakili mwanadada, ambaye alikuwa kipita na gari,…. akanikuta nikiwa nimekaa kwenye jiwe, na hapo nimeishikilia ile picha. Tulisalimiana na akaniuliza habari za maisha yangu tukaongea kidogo na akanialika kwenye chakula cha mchana, nikashukuru kwa ofa hiyo.

Tulipomaliza kula, akaniuliza hiyopicha nimepata wapi, na  hapo nikamhadithia kisa cha huyo mwanamama chotara wa kizungu mweney nywele nyingi, na kisa hicho kikamvutia sana, na alikuwa anataka kuondoka, lakini nikaona ana hamu kusikia mengi kuhusu huyo chotara wa kizungu.

Nilipomaliza kumhadithia yaliyonikuta, akaingalia ile picha ambayo kwa muda huo nilikuwa nimeiweka mezani ,akaniangalia kwa makini halafu akasema;

‘Sasa mbona umebakia na hiyo, ina umuhimu gani tena, maana kama umesemahuyo mwanamama akikuona anakimbia, na hiyo picha umesema haifanani kabisa na yeye, unanini na hiyo picha,maana unavyoiangalia ni kama vile unamfahamu huyo aliyepo kwenye hiyo picha.. au umependa hiyo picha maana kweli mweney hiyo picha anaonekana ni mrembo….hebu niambie kulikoni…?’
.
‘Kiukweli namfahamu sana mwenye hii picha, …na inanikumbusha mbali sana, mbali kulko maelezo,,cha kujiuliza ni je huyu mwanamama kaipataje hii picha, au ana uhusiana gani na huyo binti, mwenye hii picha, maana sijawahi kumuona huyu mwanamama huko kijijini, ….hapo sijaelewa…’nikasema.

‘Huenda ndio hawo mawakala wa kutafuta mabinti na kuwarubuni kwa matajiri….’akasema huyo wakili.

‘Inawezekana,…. maana haiji akilini awe na picha yake,na sizani kama huyu binti yupo hapa nchini, na nionavyo mimi labda atakuwa keshaolewa au yupo nchi za nje, kaolewa na wazungu,…kwani ni kipindi kirefu…nakumbuka siku anapiga hii picha nilikuwepo, alinipa kopi moja,….kopi yangu nilikuwa sibanduki nayo , lakini ilikuja kupotea.

‘Kama ni hivyo mbona ni muda mrefu sana….hatakuwa hivyo anavyoonekana, isije ikawa ni binti wa huyo mwenye hiyo picha….maana mimi ninavyo hata kama huyu mwanamama ni wakala, hawezi akatafuta huyo binti, kwasababau hatafaa kwa hiyo kazi,najua wao wanatafuta mabinti wadogowadogo..sijuii unanipata hapo…?’ akasema huyo wakili.

‘Na kweli,labda kuna jambo….na ndio maana nawaza sana, na nitafanya kila njia nikutane tena na huyo mwanamama, hasa kwa jili ya hii picha sio vinginenvyo….’nikasema

‘Natamani nisikie kisa chako na huyo mwenye hiyo picha, mmh,….sijui kama nina muda,…naona maisha yako yanavisa vingi na vingi ni vya kusikitisha, una damu gani wewe …?’akasema huyo wakili huku akicheka na kusubiri asikie nini nitasema, nami hapo hapo,kwanza nikaangalia juu na kutabasamu, halafu kumbukumbu zangu za utotoni zikanijia na kuaanza kumhadithia huyu wakili kisa changu na huyo anayeonekana katika hiyo picha;

***********

‘Hawa watoto wanapendana sana,….utafikiri ni ndugu, wakiwa wakubwa  kama wataoana natumaifamilia yaoitakuwa na raha, …..’akasema mama mmoja.

‘Nikuambia ukweli mama Nanhii,ni nadra sana kwa watoto wanakuwa hivi kuja kuoana, maana mwanaume anachelewa sana kukua na kuanza maisha, mpaka ahangaike ajiweke sawa, binti atakuwa kesahakuwa mkubwa, na wakiacahaan kidogo tu,kunatokea mabadiliko, na hata wasijuane tena,…..’akasema mama mwingine waliyekuwa naye,na kauli kama hizo tulishazisikia sana.

‘Hivi kweli tukiwa wakubwa si tutaoana..?’ nikamuuliza mwenzangu.

‘Kwani kuoana ni nini,mimi naona raha tukiwa hivi hivi milele..sijui nitaishije kama tutatengana tusionane tena…kweli tukiwa wakubwa, uahidi kuwa hutaniacha, utanioa mimi...’akasema .

‘Naahidi kwa mungu, wewe utakuwa mke wangu,…hata itokee nini, au tuoane sasa hivi kabisa..’nikasema na ikawa kama mzaha, maana tulitafuta vitu tukajiandaa kama bwana ba bibi harusi, na baadaye tukaulizana;

‘Sasa nanai atautufungisha hii ndoa, siunaona wakati wakifunga ndoa kunakuwa na mtu wa kufungisha ndoa, ..?’ tukaulizana.

‘Mungu anatosha,…mungu ndiye atatufungisha hii ndoa na ndiye shahidi wetu. …’nikasema na kweli tukakaa vyema na kuanza kusema yale maneno tuliyosikia wakisema wakati wanafungisha ndoa, na toka siku ile tukawa tunaitana mke na mume.

 Ulikuwa ni utoto, maana tulipoanza kusoma, akili zileza kitoto zikawa zinapotea,lakini kukweli ndani ya nfasi zetu,tulikuwa tumejenga upendo wa dhati, tulikuwa karibu na hata tukienda na tukirudi tunakuwa pamoja.
Nilipofika darasa la saba, ndipo nikaanza kuwa na utundu kutokana na vile vitabu nilivyokuwa nikisoma kwa 

Mjomba, na hapo ndipo nikawa na akili ya kujua kuwa kuna mahusiano ya mume na mke,kutokana na hivyo vitabu, lakini sikuwa na akili ya kikubwa kihivyo, ni utundu tu. Utundu wangu ulikuwa kwa wasichana wengine, sio kwa huyu binti,….’nikasema huku nikiwa nimeshika ile picha mkononi.

‘Binti huyu nilimuheshimu sana, licha ya kuwa moyoni nilimpenda, lakini kwa viletulikuwa pamoja muda mwingi ikawa namuona kama dada yangu zaidi. Hata yeye aliniona kama kaka yake, maana alija kwetu anauliza kaka Msomali yupo wapi,…na hata mimi nikienda kwao naulizia kama dada, sio mke au mume, kama tulivyoahidiana tukiwa watoto.

Urafiki wangu na huyo binti ulianza kuingia sura mpya,pale mini nilipoanza masomo ya sekondari,na kutokana na vile vitabu nilivyosoma vya mapenzi, nikawa naanza kuvutika zaidi, na kwa vile sekondari ilikuwa ni  ya bweni, basi nilikiwa shuleni kila mara namuandikia barua huyo binti, na sasa tunaitana wapenzi, …kaka mpenzi na dada mpenzi.

 Nakumbuka nilikuwa na boksi zima laa barua nilizoandikiana na huyu binti,  na kwakweli alikuwa akijua kuandika barua za kimapenzi, hata kipindi nilipokuw mkubwa, na nikiwa nikizipitia, nilitambua kuwa huyu binti atakuwa na kipaji Fulani cha mambo hayo, kama sio uandishi basi akisomea fani zinazoendana na mambo haya atafanaikiwa sana.

‘Huyu kweli akiwa mpenzi wangu sitakuwa na shida, nitampenda sana….kwasababu anajua kupenda…’nilikuwa nikisema hivyo.

Mambo yakaanza kubadilika pale walipohama na kwenda kuishi Kenya, akawa ansomeahuko, lakini mara kwa mara walikuwa wakija likizo, na mimi nnikiwa likizo, tunakutana, na huwa tunaongea sana,….hutaamini nikiwakaribu naye, siwezi kumchezea, au kumfanyia chochote, tunaheshimiana kama kaka na dada, ila tunaongeza kimoyoni `mpenzi’….nilikuwa naogopakumuuzi,au kumfanyao jambo litakalo mkasirisha.

‘Hivi unakumbuak wakati tukiwa wadogo,unaikumbukaile ndoa yetu ya kitoto…’akaniuliza huyu binti, na mimi nikacheka sana,na kucheka kule alikutafsiri vibaya,maana nilimuona akikunya uso kwa hasira, akaniangalia kwa makini halafu akauliza;

‘Ina maana wewe umeshabadili ile ahadi yetu…?’ akaniuliza

‘Ule ulikuwa utoto, hivi unaweza kukubali kuwa wewe ni mke wangu?’ nikamuuliza.

‘Ndio ulikuwa utoto, lakini ndio ulikuwa mwanzo wa maisha ya kikubwa….nakuuliza ina maana wewe yale hayapo tena moyoni mwako, unakumbuka barua tulizokuwa , unakumbuka kila mara nilikuwa nakikuuliza kuhusu ahadi yetu…?’ akaniuliza.

‘Nakumbuka sana,…lakini mengi ni ya utoto, au sio, na sio kwamba nasema sikupendi, nakupedna sana,na kama ningelikuwa na uwezo ningelikuambia tufunge ndoa , lakini sisi bado wadogo, bado tunasoma,… na sipendi wewe nikuharibie maisha yako, kwa mambo ya kimpanzi, wewe nakuheshimu sana, nitaumia sana nikifanya jambo litakalokuumiza baadaye….’nikasema hivyo, lakini nakumbuka tika siku ile nilimuona akiniangalia kwa jicho la hasira .

 Hata kipindi kimoja tulikutana na maongei yetu yakafikia huko huko, aliniambia wazi kuwa, kama nitakuwa nimevunja ahadi yetu hatanisamehe hadi kufa kwake. Niliwaza sana kuhusu huo usemi,lakini ndio utoto, bado tulikuwa vijana na sikujua kuwa mwenzangu alikuwa kadhamiria kweli,  ….na kipindi kile ndio damu ilikuwa ikichemka, utundu wangu kwa wasichana wengine ulikuwa mkubwa sana, hadi kesi zinaletwa nyumbani kuhusu huo utundu….

 Walipokuja safari nyingine,baada ya miaka kadhaa, huyo binti alikuwa sio Yule niliyemjua tena, alikuwa kabadilika kweli, msomi wa nguvu, akili imepevuka, unajua tena wenzetu huko Kenya, Kiingereza ni kama lugha yao ya taifa, kwahiyo huyu binti alikuwa akiongea kiingereza kama mzungu, na alitawaliwa zaidi na maisha na tabia za kizungu, nahali hiyo ilitufanya tuanze kuwa mbali mbali,hasa kutokana na maisha na tabia za familia yetu.

Na hata hivyo sio sisi kama familia yetu tu tuliokuwa tukiwaangalia kwa jicho jingine, lakini hata wavulana wengi, waliogopa kuongea na huyu binti, kwasababu muda mwingi alikuwa akiongea Kiingereza na tukamuona kama ana dharau fulani hivi ,unajua wivu unaweza ukaijengea hoja…Pamoja na hayo huyu binti alijitahidi sana kuwa karibu na mimi, ila mimi nikawa na hisia zilezile za wenzetu, na familia yangu ilianza kunipiga marufu nisewe najuana na huyo binti, eti ataniharibu tabia na kuiga tabia za kigeni.

‘Ataharibiwa kitabia ipi hiyo aliyo nayo ambayo ni nzuri,…. wakati mwenyewe keshaharibika, hivi huoni tabia ya motto wako ilivyo, kila siku kesi za kuwachezea wasichana wa watu,halafu unamkataza kuwa eti siwe karibu na huyo binti,mbona  binti wa watu hana tabia mbovu kama za mwanao….au unamkataza ili asiwe kama mzungu…’akasema mama aliposikia baba akinikanya kuhusu huyu binti.

‘Wewe hayo hayakuhusu, huyu licha ya tabia zake hizo….lakini ni mwanaume,huwezi ukamwambia asiwe na mrafiki wa kike, …ila kuna tabia zingine za kifamilia,huyu binti na familia yao wanaojifanya wazungu wataiweza….haya maswala tunajua sisi tunao-ona mbali,…’akasema baba.

‘Haya,tutaona na huko kuona mbali kwenu..’akakubali mama kwa shingo upande.
Kwa maneno ya baba nikapata kisingizio, sio kwamba nilikuwa napenda iwe hivyo,…moyoni ilikuwa ikiniuma sana, nilikuwa siishi kumuwaza, lakini kila nikikutana naye, nakuwa kama najigonga gonga, nahisi kuna kizuizi fuklani,…..

Yule binti akagundua kuwa nimeanza kujenga umbali kati yangu mimi na yeye na hili hakuweza kuvumilia, siku hiyo akaniita, akasemaakribu ni wataondoka, anaomba tukapige picha ya pamoja,tulipiaga picha, ya pamoja, halafu akapiga picha ya peke yake, ndio akanipa nakala moja na nyingine akabakia nazo mwenyewe.
Tukiwa tunatembea ndio akaniuliza hilo swali nalikumbuka hadi leo, aliniuliza hivi;

‘Hivi kwanini siku hizi nakuona hunipendi kama zamani …unakuwa kama unanikwepa,….niambie ukweli bado nipo moyoni mwako,au ndio umeshakua, nay ale ya utoto hayana thamani tena kwako….?.’siku hiyo akaniuliza.

‘Sio kwamba sikupendi, lakini nakuona kama wewe ni tofauti na mimi sasa, unaonekana umesoma zaidi yangu, upo kama mzungu, na unavyongea kiingereza, wanaume wengi wanakuogopa kuwa utawaabisha…na hata familia yangu inadai kuwa huendani na maadili yetu…..hutaweza kufuatilia mambo yetu ya kimila,ambayo ni muhimu sana kwa wazee wangu….’nikasema

‘Usitafute visingizio, kiingereza ni lugha tu, kama lugha nyingine,haihusiani kabisa na makubaliano yetu, mimi sioni hilo kama ni tatizo, mbonanaongea Kiswahili kama kawaida tu,….kumbuka sana ahadi yetu ya utotoni, mimi kwangu ni kitu muhimu sana, ….kwasaabbu nakupenda toka ndani ya moyo wangu, sio kuhusu mambo mengine ya nje….’akasema na kuniangalia akionyesha uso wa huzuni.

‘Hata mimi nakupnda hivyo hivyo….ila, mambo ya familia…..’nikasema

‘Kuhusu familia yenu ,kwani utaishi na wao milele, wao wana maisha yao, na njua kabisa ipo siku utaachana nao,utakuwa na familia yako, unatakiwa uaanze kulielewa hilo, pia mambo mangapi ya kifamilia unayokwenda kinyume nayo…yapo mengi, lakini huo ni utaratibu wako,…..mimi ninawasiwasi na wewe,nahisi umepata mwinginemoyoni mwako….’akasema na kuonyesha kuona aiabu Fulani.

‘Umeanza kutekwa na maneno ya kusikia ….hapa mitaani waananisingizia mambo mengi, lakini hata hivyo, ni kawaida,mvulana lazima uchukue mazoezi, ili nikikuoa wewe niswe na taabu ya masisha, kama unaniona nipo na wasichana wengine, ni kupteza muda tu,lakini moyo wangu upo kwako….’nikaaema

‘Hivi maneno gani hayo unayoyaongea, una akili kweli, hivi na mimi nikifanya hivyo utajsikiaje ukiniona, sitapasuka kwa wivu na hasira,….nikuambia kitu, …ni vyema ukajenga hisia za kumfikiria mwenzako,kuwa je nikifanay hili mwenzangu atajifikiriaje, na je kama ningelifanyiwa mimi nitasikiaje, huo ndio upendo wa kweli, kuthaminiana, ….lakini wewe unajifikiria mwenyewe, hunijali mimi hisia zangu….’akasema na mimi nikabaki akukuna kichwa,nilikuwa na tabia mtu akiniambia kitu kamasina jibu la kumpa, najikuna kichwa.

‘Kwahiyo wewe unasemaje…nianze utundu kama ninavyowafanyia wasichana wengine…mimi sipendi kukuharibu, nataka tukioana ndio tuanze mapenzi ….au wewe unaonaje…?’ nikasema nikiwanamwangalia na yeye akacheka kwa dharau, na kicheko chake cha dharau kilikuwa sikipendi,na wavulana wengi walikuwa wakiliongela hilo.

‘Unajua mambo hayo mnayofanya nyie…., kwa umri huo, sio wakati wake kabisa,mimi ninachoongelea hapa ni urafiki wa kweli, ambao hatima yake ni kuwa mke na mume, sio mapenzi ya kimwili,….bado muda wake…’akasema na kuniangalia kwa makini.

‘Hivi wewe siunaishi maisha ya kizungu….mimi najua wazungu …kwa mambo hayo ndio wenyewe, mmmh…’nikajiuma uma, na sikusema kitu, ila yeye akasema;

‘Unajua nyie wavulana mnajidanganya sana mkikutana, mna tabia mbaya sana,… nimeshasikia tabia yako…ya kuwaharibu wasichana wa familia zawatu wengine,…na hivi mnafikiri wazungu wao sio wastaarabu,….ndio wapo waliharibika kama nyie, lakini wengine wanajiheshimu, kujiheshimu ni ubinadamu wa kila mtu, awe mzungu au mwafrika…..’akasema na kuniangalia machoni.

‘Hapo hujaniambia kitu…..’nikasema.

‘Tatizo ni kwa vile mnachukulia mapicha mnayoangalia, au hawo wanaorudi huku wakiwa wamechanganyikiwa ndio mnachukulia kuwa wote wapo hivyo….wenzenu kwanza elimu, na mengine yanafuata baadaye, lakini nyie, mnayachanganya mapema,kwanza starehe,elimu itakua yenyewe, hutafika namna hiyo…’akasema.

‘Usinidanganye, usione kwa vile na kuheshimu ukafikiri sijui maisha ya kizungu,….lakini ipo siku..’nikasema.

‘Wewe, usione na mimi nakuangalia unavyofanya ukafikiri sitaweza kumtafuta Yule atakayenipenda, …huko wananibembeleza lakini sikubali kwa ajili yako,……kwa ajili ya kukupenda, kwa ajili ya ahdi yetu…lakini mwenzangu naona hata hunifikrii kabisa…’akasema.

‘Usinidanganye, ….najua huko Kenya unao wengi tu, hasa wazungu…ukirudi huku unajifanya huna mtu….lakini yote hayo ya nini, nimeshakuambi kuwa wewe niye tegemeo la moyini mwangu, hwo wengine wanakuwa wakupotezea muda,….’nikasema.

‘Hiyo kauli,…..kama ungelijiua nisivyoipenda,….hebu nikuulize hivi dada yako akifanyiwa hivyo utafurahi, ninavyokujua usingekubali kamwe….kama hupendi, kwanini sasa unawafanyia watoto wa wenzenu, ….nakukanya kuhusu hiyo tabia,sio nzuri….. ukumbuke tulivyoahidiana tulivyokuwa wadogo kuwa tutapendana….lakini hatutaharibiana hadi tukiwa wakubwa, hadi tukifunga ndoa, yale yalikuwa na maana sana, ina maana ahadi yetu ilikuwa ya uwongo….?’akasema kwa masikitiko.

‘Sio kwamba sikupendi,..na ahadi yetu ipo moyoni….na, na…ndio maana wewe nakuheshimu sana, siwezi kukufanyia mambo ninayowafanyiwa wasichana wengine…’ nikasema na yeye akainuka na kuniangalia kwa hasira na kusema

‘Mimi kauli yako hiyo siipendi,….kwanini hujali hisia za wenzako, …eti mambo ninayowafanyia wasichana wengine, ina maana una wasichana wengine unawafanyia …nini sijui, unao sio…..?’ akaniangalia kwa hasira,…..

Kauli yangu hiyo ilikuwa ikimvunja sana moyo,na akawa kaninunia na yeye akaanza kujenga umbali fukani na mimi, ingawaje kila mara nikikutana naye nilimgundua akiwa akiniangalia kwa jicho la kujiiba,na nikikutanisha macho yangu na yake huangalai pembeni kwa haraka, hakutaka macho yetu yakutane.

 Na mimi hapo nikaona ni bora nisijitese kwa ajili yake, nikawa sijifichi tena kuwa na wasichana wengine, na akitokea akinikuta nikiwa nao,nilimuona kabisa akikunja uso wa hasira, na nilijua kabisa namuumiza moyo wake,lakini nikawa najifanya sijali,ila sikupenda kumuumiza, kwanii mara nyingi nilikuwa nikijitahidi asionione , lakini wasichana wa pale kijijini walikuwa wanataka kama kumkomoa vile, wakamuona wanajionyesha kuwa mimi na mpenzi wao.

Nakumbuka safari moja,ambayo nilimuumiza sana huyo binti, ni siku moja alipokuja nyumbani, akiwa na malengo ya kuniaga kuwa wanaondoka, akaniifumania na msichana mmoja, tukiwa  chumbani kwangu, kitandani,…maana kule kijijini nilikuwa nimepewa chumba changu cha uwani, ….sitasahu siku hiyo.

Alifungua mlango, sikujua kwa waakti huo, maana nilikuwa mbali,nilipogeuzakichwa change na kumuona akiwa kasimama mlangoni,nilishikwa na aibu ya mwaka, nikumbuka niliziba macho kama afanyavyo mtoto mdogo, aili sionekane, wakati unaonekana….na yule msichana tuliyekuwa naye mlendani akawa ananishikilia, na mimi nikawa namsukumambli na mimi…..

‘Hivi kwanini wewe unanifanyai hivyo….?’ Akasema akiwa analia ….niliondoa mikono machonii na kumwangalia kwamasikitiko, niliumia sana moyo wangu sikuu ile, sikutarajia kuwa angelikuja. Na hapo hapohapo akageuka na kuondoka.

Toka siku ile hatukuonana tena, liondoka kurudi Kenya,na huko walikaa sana, na hata walipokuja mara moja, hakuweza kuja kuniona, nilipata ujumbe tu, kuwa walikuja, na ujumbe huo ulisema kuwa yeye bado anatunza ileahadi yetu, na kama nimeamua kuivunja, …ipo siku nitajuta…ilikuwa karatasi ambayo hakuwa na maneno mengi kinyume na alivyokuwa akiniandikia zamani, mwishoni aliandika na hivi;

‘Ulinichonifanyia sitakisahau maishani , lakini ipo siku utajuta na utanikumbuka…..

 Kimiya kikatawala

*******

‘Kauli hiyo,….,huenda ndio inanitafuna hadi leo….’nikasema,na kutulia kidogo , halafu nikayarudia yale maneno kwa sauti ya taratibu nikayasema tena;

 ‘Ulinichonifanyia sitakisahau maishani , lakini ipo siku utajuta na utanikumbuka…..’ na kweli najuta na namkumbuka sana huyo binti. Wakali akaniangalia kwa makini, na baadaye akatabasamu, hakusema kitu kwa muda natumai huyu wakili alikuwa akiwaza yake,au alikuwa akiwaza yale niliyomwambia, na baadaye akasema;

‘Pole sana, inaonyesha huyo binti alikupenda sana,lakini wewe ulikuwa kinyume chake….na ndivyo mlivyo wanaume wengi, mkipendwa hamjali, huwa hamjali hisia za wenzenu, sijui kwanini..’akasema nafikiri na yeye kuna mambo yalitokea katika maisha yake, …sikumuuliza, nikafuta uso wangu na kusema;

‘Hiyo ndio habari ya huyu mwenye picha hii,….’nikaiangalia kwa makini, na kusema tena;

‘Sasa sijui kwanini ilifika kwenye huo mkoba wa huyu mwanamama mwenye manywele mengi anayenikimbia kama akaona jinamizi, mama sikumbuki kabisa kumuona huyu mwanamama huko kijijini, ni sura ngeni kabisa, tena aonekana kabisa ni mchanganyiko wa damu za wazungu na kiafrika…Yule ni chotara…’nikasema.

Yule mwanadada wakili aliniangalia machoni kwa makini, halafu akasema; ‘Siku hizi kuna madawa yanabadili sura za watu,ukimeza vidonge, unabadilika kabisa na kuwa mweupe,…lakini weupe huo sio mnzuri, ngozi inakuwa ya namna namna….Sijui kwa huyo mwanamama unavyosema ana sura kama ya chotara wa kiafrika na mzungu,kama ningelimuona karibu ningelijua kuwa ni rangi ya asili au ndio hawo wanaomeza madawa…’

‘Sina uhakika na hilo, na wala hilo halinisumbui kichwa changu, …..maana nilimuona mara moja, na nywele zilikuwa zimefunka sana usoni mwake, na mara ya pili nilimuona kwa mbali, akiwa uso wazi kidogo, ,lakini nywela kaziachia na kufunika sehemu kubwa ya uso, nafikiri ndio mtindo wake huo….lakini anaonekana kabisa kama ni mweupe kama mzungu…’nikamwambia wakili huyo

Wakili huyo alitabasamu na kutaka kuondoka, nilimshukuru ka chakula hicho alichoninunulia name nikamwambia kuwa naahidi kuwa safari nyingine na mimi nitamnunulia chakula….akasema nisijali sana, nakabla hajaondoka akaniulizia kama nimeshapata taarifa yoyote kuhusu alipo mke wangu au Yule mama Docta.

‘Mimi hawo watu sijawahi kukutana nao, na hata nilipoulizia wapi walipo, hakuna hata mtu mmoja anayejua, ni kama wamepotelea hewani, na hakuna anayejali kujua wapi walipo….’nikasema

‘Inasemekana huyo Docta Mama yupo hapa nchini, na kipindi kile cha kesi alikimbilia Kenya,na huko akawa anafanya yale yale aliyokuwa akiyafanya huku, kule ana kibali, na anatambulika kama docta wa akina mama,… ila hilo kuwa wanamshuku huenda ana biashara nyingine zaidi ya hiyo inyotambulikana….’akasema huyo wakili.

‘Biashara gani hizo…?’ nikauliza.

‘Yeye ana kazi yake yenye kibali inayojulikana kuwa ni mtaalamu  wa ushauri wa ndoa na mahusiano, na pia ni dakitari bingwa wa akina mama, kwa ushauri nasaha,na hata matibabu ya uzazi. Kiujumla ni mtaalamu kweli, huko Kenya anatambulikana sana, …lakini hapa nchini, hatambulikanani kihivyo na pia hapa nchini sio raia, anakuja kwa kibali hicho cha muwekezaji…’akasema huyo wakili.

‘Aaah,kumbe ndio maana hata Kiswahili chake ni cha shida…, na nchi hii itaharibiwa na hawa wawekezaji,tusipoangalia tutakwenda wengi kwa migongoo ya hawa wawekezaji wakigeni…’nikasema

‘Unajua tulishaligundua hilo na mara nyingi tulikuwa tukijaribu kutafuta mwanya wa kumshitaki huyu mwekezaji, hasa tulipogundua kuwa anajihusisha na bishara hiyo haramu ya kuwarubuni akina dada, tukajaribu kulifikisha ngazi zinazostahili, lakini kila vielelezo vilipopatikana, tukakuta tunagonga mwamba, sijui kulikuwa na kikwazo gani,lakini nimegundua haya kupitia kweney hii kesi yako..’akasema.

‘Uligundua nini…?’ nikauliza.

‘Na kipindi cha hiyo kesi yako, ikagundulika kuwa yeye ndiye yupo nyuma ya hayo yote,na alitakuwa ashikwe na kufikishwa mahakamani, sijui alijuaje akawa keshaondoka mapema, na hata kipindi kesi yako ikifanyika alikuwa hayupo hapa nchini….’akasema huyo wakili.

‘Kwanini asishitakiwe huko huko alipo, akakamatwa…?’nikauliza.

‘Sheria zinatubana,na hatuna ushahidi wa moja kwa moja, na utambue kuwa Yule ni mjanja sana, mambo yote hayo alikuwa kiyafanya kwa kupitia watu wengine, yeye anakuwa kama mshauri tu…na hata huyo mwanasheria uliyekuwa akikutetea wewe, hakuwekwa na yeye moja kwa moja, alitumiwa mtu mwingine kabisa, ambaye kwa sasa ni marehemu….

‘Yule mwanamama kafariki….?’ Nikauliza kwa mshangao..

‘Ndio alikufa kwa shinikizo la moyo….na utakuta yeye ndiye alishika kila kitu  kwa hapa nchini, na yule wakili aliyekuwa akikutetea hayupo hapa nchini, aliondoka siku ile ile ya mwisho wa kesi yako, ….alikuwa keshakata tiketi ya kuondoka,…..anakwenda masomoni huko Ulaya, na hata hivyo alitusaidia sana kufichua mambo mengi yaliyokuwa yamejificha.

‘Yule mtu nilikuwa simuamini,ina maana alikuwa akiuma huku na kule….?’ Nikauliza

‘Hayo tuyaache kwa sasa…kuna jingine maana nataka kuondoka…?’ akaniuliza

‘Mhh, ni shukurani tu,ila….mmmh,  nikuulize kitu,…kuna kitu kimoja nakishangaa sana,…mpaka sasa nakuwa na wasiwasi ….sijui kuna nini kimetokea, nashindwa  hata kuamini…’nikasema na kuangalia chini.

‘Kitu gani hicho, niambie ……kama ni kuhusu maisha yako, nitakuasaida lakini sio sasa, ni mpaka mwakani, ambapo kampuni yangu itakuwa tayari kuajiri watu,nimeamua kujiajiri…na wewe nimekuweka katika watu nitakao wachukua, kwa sasa bangaiza hapa na pale ili uweze kuishi, mimi sina la kukusaidia kwa sasa….maana mshahara wangu ni mdogo na una mikono mingi,mara nyingi tunategemea wafadhili ….’akasema huyo mwanamama.

‘Sio kuhusu hilo, …ni ….ni….’ nikasita kidogo halafu nikasema;

‘Unajua tangu nitoke jela,  watu wengi wanaonifahamu ….’ Nikatulia tena kidogo na kutingisha kichwa, halafu nikasema;

‘Hii ni ajabu kabisa, hata kumsimulia mtu nashindwa, ….watu wanaonifahamu, nikikutana nao wananikimbia….kabisa, wengine wanatimua vumbi kabisa….kama sijui naonekanaje…’nikamwangalia huyu mwanadada usoni, ili aniangalie vyema, yeye kwanza alionyesha uso wa kujiuliza na baadaye akatabasamu na kuniacha niendelee kuongea.

‘Na ningelisema labda ni kwa huyo mwanamama pekee, lakini sio huyu mwanamama tu peke yake, huyo ninayemzungumzia eehe,…huyo mwenye manywele mengi, ….., hata wengine….wakiniona tu, wakinigundua kuwa ni mimi wanakimbia, hivi nipoje usoni, nimkonda sana..au…. kwanini….unajua inanipa shida sana hiyo hali…huko sio kunyanyapaliwa kwa hali ya juu…au, sijui kwakweli...’nikasema huku nikionyesha uso wa huzuni.

‘Mbona mimi nakufahamu sijakukimbia…huoni kuwa hizo ni hisia zako tu,….kuna jingine labda ambalo hujaniambia…maana hapo sioni kuwa kuna tatizo ni hisia zako tu….’akaniangalia na aliponiona nipo kimiya akasema;

‘Labda ulikuwa na watu wengi unaowadai,wakikuona wanakumbukia deni, na kwasababu hawakutarajia kukutana na wewe, na kwa vile ulikuwa jela, basi wanajua wewe ni mtu hatari, unaweza ukawatolea hasira kwao, au kuna kule kukuona kuwa huna kitu, wanaogopa utawaomba…huo ni utani tu, usije ukaona nakuzarau….’akasema na kucheka.

‘Sio kunizarau,huo ni ukweli usiopingika kuwa kweli sina kitu, nimepigika, nimefulia, nimeanikwa uchi….ndio maana inafikia hadi kuwa omba omba,….lakini sio kwamba napenda iwe hivyo ,ni njaa, ndio maana wanasema aduo yako muombee njaa, njaa sio mchezo jamani…’nikasemahuku nikijaribu kutabasamu.

‘Kwa ujumla….sina uhakika na hilo,ila….kuna tukio sijui kama lina ukweli, kuna watu wamevumisha kuwa kuna ombaomba majini, au masehtani, wao wakikuomba ,ukawaangalia machoni tu, umekwenda na maji,..kwani utawapa kila kitu chako, na mwishowe wanakuchukua na wewe mwenyewe…’akasemahuyo dada akaniangalia machoni.

‘Kukuchukua kukufanyaia nini….’nikasema huku nikiangalia huku na kule kwa uwoga.

‘Kukunyinya damu….wana njaa ya damu za watu….’akasemana aliponiona nikiangalia huku na huku nikionyesha uso  wa uwoga,akasema;

‘Si unaona sasa,binadamu huwa tumejengwana hisia za uwoga, na nyingi tunajijengea wenyewe, unaweza ukawaza na hisia za kumbukumbu Fulani, au hisia tu zinakuja kichwani, ukajikuta mwili unasisimukwa kwa uwoga,…kumbe hakuna kitu….’akasema huku akitabasamu, halafu akaniangalia kwa makini, na aliponiona bado nipo kimiya nikiwa kwenye mawazo au wasiwasi, akasema;

‘Hebu naiomba hiyo picha, ninataka nikaifanyie kazi , kama nilivyokuambia, wafadhili wetu wametupa kazi ya kupambana na madawa ya kulevya,…’akasema.

‘Sasa hii picha inahusianaje na madawa ya kulevya….?’ Nikauliza nikimwangalia kwa mshangao.

‘Wewe umesema kwenye ule mkoba kulikuwa na mfuko wa plastiki, ndani ya huo mfuko kuna vipakti vidogovidogo,vilivyojazwa vitu kama unga unga….au sio, na nakushangaa kidogo, ina maana wewe katika ujanja wako wote hapa mjini, hujawahi kuona madawa ya kulevya?’ akaniuliza.

‘Sijawahi,…kiukweli sijawahi, na kwanini nihangaike kuyajua, wakati situmii , …. nayasikia tu, na kwa muda ule,sikuwa na wazo hilo kabisaaa, ulivyoniambia sasa hivi ndio na mimi najaribu kuwazia hivyo, inawezekana ikawa ni madawa ya kulevya…..nilijaribu kulamba nikizania ni `glucose’, lakini nilitema haraka nilipoona ladha yake sio yenyewe, nikiogopa isije ikawa ni sumu…..’ nikasema huku nikijaribu kukumbuka ladha yake

‘Uivyoelezea inawezekana kabisa hayo ni madawa ya kulevya,…na kwa mtaji huo, huyo mwanamama uliyemuona anaweza akawa mzungu wa unga anayetafutwa sana hapa nchini,tukimpata huyo…kesi imekamilika….na tutakuwa tumepiga hatua kubwa sana,…..kwahiyo ukiwahi kumuona tena,nipigie simu haraka…..unasikia…? akasema akasema kwa sauti aliponiona nimetulia kuonyesha kuwa nipo mbali sana kimawazo

‘Nimesikia…..nakusikia unafikiri,…licha ya kuwa nipo mbali kimawazo,lakini tupo pamoja…..’nikasema huku bado naiangalia ile picha.

‘Wewe nipe hiyo picha inaweza ikasaidia jambo…siku hizi utaalamu mkubwa,..na hata hivyo….,nahisi kuna kitu ndani yake, …nitakigundua tu, nahisi hivyo,na hisia zangu mara nyingi zinanipeka kwenye ukweli…’akasema.

‘Lakini huyu mwanamama hafanani kabisa na wauza madawa ya kulevya, ….hii sura ya huyu mwanamama,…..mmmh naiona kama sura ngeni sana machoni mwangu….na kwanini alikuwa ndani ya kile kijiwe, na haonyeshi kuwa ana hali ngumu….kile kijiwe ni cha watu waliopigika….uliwahi kuingia mle ? ’nikasema nakumuuliza huku naiangalia ile picha.

‘Hafanani eeh….hahaha, wewe usijali kabisa, wamailiki wakubwa wa hizo biashara,  huwezi  kuwajua kwa sura, ….huwezi kabisa kuwadhania kuwa wanafanya hiyo bishara na wengine hawatumii kabisa, wao wanauza tu…kwasababu wanajua madhara yake….tatizo inakuwa kwa hawa watumiaji,.….hasa vijana wetu, na hasa akina mama ambao ndio nawapigania kwa nguvu zangu zote….’akasema huyo mwanadada wakili.

Nikasita kumpa ile picha,niliona kama ni kitu cha thamani nimekipata baada ya kunipotea, ni kilikuwa ni kitu cha thamani sana kwenye maisha yangu, nikaiangalia kwa mara nyingine na kumkumbuka huyo binti tulivukuwa naye utotoni ikawa inanichezea akilini..sijui sasa yupo wapi natamani nikutane naye angalau mara moja, najua atakuwa keshabadilika sana na huenda keshaolewa ana watoto au yupo huko Ulaya, au …sijui wapi…lakini sijasahau mapenzi yetu ya kitoto…

‘Mbona unasita kunipa hiyo picha….inakukumbusha mbali sana, au sio, nitakurudishia picha yako, nikishamaliza kazi yake, usijali….’akasema na kuichukua mikononi mwangu.

‘Kweli hujafa hujaumbika,…nashindwa kuamini, kuwa kumbukumbu kama hizo zingenijia tena na kunifanya nimuwaze sana huyo binti,…cha ajabu hata kipindi natafuta mke, kila ninayemuona nilikuwa nikilminganisha na yeye, lakini sikumpata, na hata niliyempata, hakunipa kile nilichokuwa nizani ningelipata toka kwa huyo binti….’ Nikasema huku nikiwa bado nipo mballi kimwazao.

‘Unajua …mawazo yangu na yake yalikuwa kitu kimoja, na kilichobakia sasa ni kumbukumbu za barua tulizakuwa tukiandikanana…kumbukumbu hizo bado zipo akilini,i….natamani sana nikutane naye tena..hata kama yupoje….angalau nimuone tu…’nikasema na Yule mwanadada wakili akacheka na kuondoka zake.

NB Najua wengi wana kumbkumbu kama hizi, sijui kwamba kuna waliobahatika na kufanikiwa kuifikia ndoto zao za utotoni, ya kuwa walipendana toka utotoni hadi kuoana, na sasa bado wanaishi kama mke na mume, wapo kweli…kama wapo mungu awabariki sana….

Kisa kinakifikia ukingoni, sina uhakika lini, ...maswali yaliyobakia kichwani, ni je kwanini watu wanamkimbia huyu jamaa, je hiyo picha imefikaje kwa huyo mwanamama,  kwanza huyo mwanamama ni nani...na aliipataje hiyo picha...kuna siri ndani yake,...nikamwangalia msimuliaji anipe jibu, akasema tusubiri sehemu ijayo.....

WAZO LA LEO: Kukosana kwa binadamu ni jambo la kawaida, ni vyema ikitokea sintofahamu kati ya wanandoa, marafiki,majirani, ndugu, na kukatokea kukwaruzana, kwa hapa na pale, jengeni tabia ya kusameheana.

Kama ni wanandoa Kaeni chini na  kuyajadili hayo yalisababisha kukosana au kukwaruzana….ili yasijirudie tena, . huenda yalitokea hivyo ili kuiimarisha ndoa yenu, na hata hivyo tukumbuke kuwa sote ni binadamu hatutaweza kukamilika kwa kila kitu, mkamilifu ni muumba pekee. 


Ni mimi: emu-three

1 comment :

Anonymous said...

Hongera sana, ukituona hatuandiki chochote, sio kwamba hatufurahii kazi yako, wewe ni kiboko, na kama ukiwekwa kwenye mashindano ya KUTAFUTA mtunzi bora wa visa, riwaya na hadithi, utawaacha wengine mbali sana...HONGERA SANA