Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Wednesday, April 11, 2012

Hujafa hujaumbika-20



Nilifanya kama nilivyambiwa, baada ya chakula., na kinywaji kidogo, yule mama akasema;
`Mimi lengo langu ni kumkomoa mume wangu, yeye kila siku anajirusha na visichana vya mitaani, leo ni zamu yangu...na mimi..mmh, mbona hiki kinywaji kinakuwa ..nasikia kulewa...ooh...'mara akadondokla kwenye meza.

 Mimi hapo sio kazi yangu, nilitakiwa kwenda chumba maalumu, huko nisubiri, na kweli nilipofika huko, nikatulia kidogo mara watu wawili wakaja wakiwa wanamsaidia yule mama kutembea, .....

'Oh, afadhali nimekukuta....mpenzi, nilijua umenikimbia, nasikia ovyo....mmh, najisikiaje sijui...'akasema na mimi nikamsaidia hadi kitandani.

'Usijali tupo pamoja...'nikamwambia na kuanza kufanya kama nilivyoagizwa...na nikamweka kitandani na kumchojoa nguo zote....nikajifanya kama vile tupo kazini, ....lakini haikuwa hivyo ni geresha, tu...nikamaliza na kuchuku anguo zangu...

'Usiniache mpenzi....'akasema.

'Nakuja usijali...', nikamdanganya na mara nikasikia kama anakoroma, nikageuka kumuangalia, ...nikakuta mdmo upo wazi, na macho yamemtoka ...nikamsogelea, na nilipomgusa, mara akawa kama anatuingishwa, na mara akatulia kimiya...

Nikaharakisha kutoka, nikafungua mlango na kutoka nje, lakini sikuwa na amani nikarudi tena, nikajaribu kumtikisa, lakini alikuwa kimiya...nikagua sehemu ya shingo ya mapigo ya moyo..kimiya...mwili ukaanza kuniishia nguvu, ina maana nimeua..lakini sio mimi...sio mimi, na mara nikasikia kama watu wanongea kwa nje...mwili ukafa ganzi, leo nimepatikana.....

            ***********


 Kazi naitaka, na ili nipate hiyo kazi inabidi nikubaliane na masharti ambayo nilitakiwa niyafuate, nilitakiwa nikaonane na mama mmoja wa mheshimiwa, na kila kitu kilishapangwa nilichotakiwa nikufika hapo kwa ajili ya chakula cha usiku na mengine yatafuta baadaye...lakini.

Lakini nimeshachoka na hiyo hali, nataka kuachana nayo, na ili niachane nayo inabidi nikubaliane na utaratibu uliopangwa na kikao maalumu nilichokutana na wale akina mama baada ya mkutano waohuo ambao ulikuwa ukizungumzia mambp ya kina mama,na humo ndani ndio likachomekwa hilo swala na kupambana na hicho kikundi haramu.

‘Ole wako ukitusaliti...unamjau yule jamaa aliyekuwa akiitwa nani..na yule mpelelezi,na yule ....wote sasa haivi hawapo duniani, na wengine wamepooza miili yao hawana kauli tena, na ni sababu ya kujifanya wajuaji...’akasema mke wangu.

‘Mliwafanya ninin...?’ nikauliza.

‘Hata mimi sijui, ila habari ndio hizo, ikitokea hapo,mimi tena sina usemi, nitaomboleza siku mbili tatu, nitakusahau nitapata mwingine...’akasema huku akijifanya kusikitika.
‘Lakini haya yote mnafikiri mtashinda,....kuna ubaya una mwisho wake, ipo siku mtanaswa na sijui itakuwaje siku hiyo...’nikasema.
‘Hiyo usijali, ipo siku,...hayo nimeyasikia miaka kumi iliyopita...kwa jinsi ilivyo ukipya hata mwaka mmoja tu wa kutumia,inatosha, sasa, fikiri hali hiyo imekuwa hivyo hivyo, sasa miaka kumi,hakuna cha kukamatwa au kushukiwa, ...wenzako wamejipanga kitaalamu, kukitokea hivi wanajua jinsi ganii ya kujihami...kwasababu hata mwanzo hatukuwa tunafanya hivi, leo tunatumia vyombo va kitaalamu...’akasema mke wangu.

‘Sawa, yangu macho..mimi nina imani kuwa ngoma ikilia sana,hatimaye hupasuka...na mwisho wa ubaya ni fedhaha, bora ujihami sasa hivi kabla ya fedhaha...’nikamshauri mke wangu.

‘Sikia we mtu, kama umeanza mambo hayo, kama unataka kusaliti, tafadhali ...narudia tena, kama kuna mpango kama huo,acha mara moja, utajuta...’akasema na kutoka nje, baadaye akarudi na kuniambia nijiandae ili nikawahi huo mpango nilioandaliwa.

‘Kumbuka huo mpango ni mahususii ya kupata pesa kwa ajili ya akzi yako,kama unahitaji hiyo kazi fanya kaam nilivyokuagiza, lakini kama huhiataji na huna haja ya maisha yako ya baadaye fanya kinyuem chake, na ..narudia tena, usije ukalogwa ukaenda kinyuma na makubaliano,ukisaliti, mimi sitakuangalia mara mbili...wenyewe watajua nini cha kukufanya, utaiona sura yangu ya pili, ....na ndio itakuw kwaheri...’akasema

Nilitaka kumwambia usinitishe lakini nikatulia kimiya huku nikitafakari, maana huko kwa akina mama nako nilishapewa majukumu na nikaahidi kwa maandishi, kuwa nitafanya kama tulivyopanga na ili kufanikiwa hilo inabidi kuwe na usiri mkubwa  ukizingatia kuwa kundi hilo lina mtandao mkubwa...

‘Hawa watu wanatumia mitandao, na wana wataalamu wa hali ya juu , wana watu wao huko nje, hapa ni kama katawi tu, na walichofanya ni kupandikiza watu kile sehemu muhimu, kiasi kwamba kila jambo klinalotokea sehemu husika haraka taarifa hizo huwafikia kwenye ofisi yao kuu...’akasema dada mmoja ambaye ni mtaalmu wa mitandao.
‘Kama ni hivyo tutawezaje kuwashinda, maana  hata huenda kuna mtu wao, ....’akauliza mama mmoja.

‘Ukiwa kwenye mapambano angalia ushindi kwanza, ...hata kama unajua kuwa wewe ni mzaifu, usijali, hata kama unajua kuwa mwenzako ana silaha kubwa kubwa,...wewe weka nia ya ushindi, hiyo ni hatua kubwa sana ya kumshinda adui yako, pili mtangulize mungu mbele, ukijua kuwa wewe upo kwenye haki, na mara nyingi haki ina nguvu kuzidii batili....’akasema yule mwanadada mtaalamu wa mitandao.

‘Kujipa moyoo ni muhimu sana...’nikasema.

‘Nduu yetu, sisi hapa tumekutana watu waainifu, watu ambao wana uchungu na vizazi vyetu, ...maana ukiwajali watoto sasa, bila kujali kuwa huyu ni wangu, umelijali taifa lako, umewajali na wao katika misha yao ya baadaye,...watuu huwa wanaangalia familia zao tu, bila kujua kuwa watoto wao wataenda kuchanganyika na wenzao, ambao labda ahwana malezi bora, unafikiri nini kitafuta, kama sio na wao kuiga,...kwahiyo ili maadili yapevuke, ni muhimu kuhakikisha watoto wote wanakuwa katika maadili mema.

‘Hiloo ni kweli kabisa...akasema mama mwingine, maana hutaamini, yule mzee pale jirani aliyekuwa akiwafungia watoto wake kwenye geti, wakitoka, wanasindikizwa, na tulikuwa tukipenda walivyokuwa na adabu watoto wa yule baba, tulishangaaa kuona mmoja wa watoto wake ni teja, mla unga....ina maana alikutana na makundi, wakamshawishi akaanza kidgokidogo, wazazi hawajui, mwisho wanakgunduak keshaharibika....

‘Ni kutokana na ubinfasi, kujali familia yako tu ukajiona uanzo, ukajiona uanjua kulea, ukasahau kuwa watoto sio wako tu, hata wa wenzako ni wako, watoto ili waishi vyema, inabidi wakutane na wenzao, wabadilishane mawao,wajifunze changamoto za kimaisha na wewe kama mzazi unatakiwa uwe karibu nao, ili ujue nini wanakihitaji, nini kinachowakwaza, sio kufungia ndani ...haitasaidia...’akasema mama mwingine.

‘Hilo ni moja ya ajenda zetu, tukisimamia kwenye msimamo wetu kuwa sisi ndio walezi, sisi ndio wakulijenga taifa hili, mwanamama akielimika, taifa limelimika, ...kwasababu sisi ndio tuliokaribu sana na watoto wetu, sisi sio tunaowajau watoto wetu vyema, sisi ndio tunaowajua waume zetu vyema, kama humjui mume wako, tutakuashangaa,...’akasema yule mama kungwi.

‘Na wewe umeanza tena....’akasema yule mwanadada mtaalamu.

‘Hilo ni kweli binti yangu, nitashangaa nikikuuliza kuwa mume wako ana alama gani mwilini ushindwe kuniamabia...itakuwa ni ajabu kabisa, wewe unatakiwa umjue mume wako, kila sehemu ya kiuongo chake,...nitakuap kisakimoja cha ajali iliyotokea mahali,...watu wengi wakapoteza maisha, na mle kuna baadhi walipona.
‘Sasa watu wakawa wanakuja kutambua maiti zao,na ndugu na jamaa, mama mmoja alipofika akakuta mkono upo karibu na maiti, na akawaambia wenzake  huo ni mkono wa mume wake, mwili hautazamiki ulivyo haribika , wanandugu wakaukusanya vyema ule mwili na kuondoka nao,wakawasilina na hospitali, kua ule mwili hauwezi kulala tena,bora wa uzike siku hiyo hiyo.
Mama mzazi kila akilala anamuota mtoto wake kuwa bado yupo hai, akamuendea mke wa huyo mtoto wake na kumuuliza,;
‘Una uhakika kweli kuwa yule maiti ni mumeo...?’ akauliza.
‘Ndio yeye, huoni mkono wake...uliokuw akaribu naye...’ akasema
‘Mimi sioamini, naona kabala hawajauzika tuombe tukauchunguze vyema ule mwili...’akasema mama.
‘Mama, eti nini, hata mimi sikubali,....unatak niote maisha yangu yote...ile sura itanikaaa kichwani miaka mingi, mimi hilo siwezi ...’akasema mke.
‘Kweli wewe ulikuwa ukimpenda mwanagu vyema...?’ aakmuuliza.
‘Ndio nilikuwa nampenda, lakini sasa ndio keshakufa nifanyeje, hata nikimchunguza vipi hatabadilika..’akasema yule mke.
‘Kamakweli ulikuwa uanmpenda hebu niambie alama gani muhimu katika mwili wake unazozikumbuka...?’ akamuuliza yule mke.
‘Alama gani, mimi sikuwahi kumchunguza , ...mtu mwenyewe kukutana kwetu ni usiku, mchana kila mtu na mihangaiko yake...’akasema mke.
‘Kosa hilo, hii inaonyesha wazi kuwa ulikuwa humoendi mwenzako,...kama ungelikuwa unampenda vyema , ungelijua kila alama kwenye mwili wake...wewe ulikuwa ukijali mali yake tu, na sasa kaondoka, unatarajia nini, ...?’ akaulizwa.
‘Mimi namuomba mungu nisahau, halafu akipatikana mwingine wa kunioa, nitashukuru , ..hata hivyo nitajitahisi kuendeleza miradi yetu, na kama nikiolewa, huyo mume nitamfundisha kama alivyokuwa kifanya mume wangu aliyetangulia mbele za haki...’akasema mke.
‘Kwa mtizamo wako, kuna mtu yoyote unayemtamani ...ili sisi tumchunguze kama anakufaa, maana wewe ni binti yetu,uliolewa kwetu na hatutaki kukutupa....’mama akauliza.
‘Mhh, mama hili tuliache kwanza, ....nitakuambia muda ukifika, yupo, lakini mbona mapema sana...’akasema mke.
‘Unamjua vyema, maana waue wengine ni bora liende, mtoto wangu unasema alikuwa jembe kwa kila eneo, sasa huyo unamjua vyema, usije ukaolewa na garasa...?” akauliza mama.
‘Mama mbona unaniuliza mapema hivi, tupo kweney msiba, tuawazei huu msiba kwanza,mambo mengine baadaye...’akasema mke.
‘Hili ni muhimu sana, maana tukimaliza msiba hapa utaanza kuhangaika, na mimi hilo sitaki, nijibu swali langu , huyo unayemtarajia unamfahamu vyema..?’ akaulzwa.
‘Ndio namfahamu vyema...’akasema.
‘Ana alama gani muhimu mwilini mwake, unazozifahamu..?’ akauliza mama.
‘Sijui....’akasema yule mke.
‘Kwasababu mlikuwa mkijiiba, au sio, lakini mume wako sio mtu wa kujiiba,mna uhuru naye...kwanini umfanye kama huyo wa kujiiba,....ina maana hampendani basi....mwanangu nimekuuliza hayo yote kama mzazi, mimi ndiye niliyewalea watoto wangu toka wakiwa wachanga, kuna alama mwilini kwao zinapotea kabisa wanapokuwa wakubwa, lakini zipo nyingien hazipoteia kabisa...na kuna nyingine zinajitokeza baadaye....mimi namjua mume wangu tangu aliponioa, najua kila sehemu ya mwili wake...kwasababu nampenda, ...kwasababu kuna leo na kesho...’akasema mama.
‘Mama una maana gani, kusema unampenda, ...hizo alama zina umuhimu gani katika kupendana...’akauliza yule mke
‘Mwanangu kupendana ni pamoja na kujaliana, kuwa karibu na kufanya lolote kwa mwenzako ikibidi, kwa mafano mume wako ana ugonjwa ambao hawezi kuvuta makamsi nje, unaweza kuyanyinya kwa mdomo ili kuokoa misha yake? ‘akauliza mama.
‘Mama,unaingea nini....mmh, unataka hata nisikie kutapika..’akasema huyo mke na kutafuta sehemu ya kutema mate.
‘Lakini wewe unaweza ukameza makamsi yako, inatokea hivyo mengine yanamezeka kwa mfano ukiwa na mafua,au sio...makohozi na vitu kama hivyo inatokea ni uchafu ndio lakini ni mambo ya kawaida kibinadamu, sio lengo langu kukukerehesha,ila nataka kukuonyesha umuhimu kati ya mume na mke, kuwa wao ni kitu kimoja ...mwili wa mume wako ni sawa na wa kwako, hebu nikuulize kuna alama gani mgongoni mwako...?’ akauliza tena mama.
‘Sina uhakika kama nazijua vyema...’akasema mke.
‘Ndio maana mojawapo ya kuoana, kuwa wewe peke yako hujakamilika, lazima uwe na mwenzako wa kusaidia kujua pale usipopajua,au kupafikia, kupeana mikono, kujaliana na kushirikiana, kwasababu kuna sehemu zako huwezi kuziona, atakayeziona ni mwenzako, ...’akasem mama.

 Wakati wanaongea mara mlango ukagongwa, na mama akasema, kabla hujamfungulia huyo mtu nikuulze swali moja, Je upo tayari kwenda kumchunguza yule maiti kuwa kweli ni mume wakoo au sio?’ akauliza yule mama.
‘Mama mimi siwezi,hilo utanilaumu tu,...sina uwezo huo...keshakufa basi, tumuombee mungu amalze mahali pema peponi...’akasema mke.
‘Basi nenda kamfungulie huyo mgeni...’akasema mama.
‘Unajua nini kilichofuata, ...’yule mama akatuuliza, sisi tuaksema hatujui, tutajuaje wakati yeye ndio msimuliji...akasema ;

‘Ghafla, mshindo wa mtu kuanguka uaksikika pale mlangoni,na mama alipogeuka, alimkuta yule mke wa mwanae kadondoka chini ....na mlangoni kasimama mtoto wake, akiwa kafungwa, hana mkono mmoja....

‘Mwanagu nilijua upo hai...usijali kupoteza mkono mmoja sio mwisho wa maisha, mungu akupe maisha mema, na mkwe mwema...’akasema huyo mama na kutuangalia kwa makini.
‘Ilikuwaje kwa yule mwanamke ....?’ nikauliza.
‘Hilo sio muhimu sana, muhimu ni ujumbe uliopo hapo, kama hujui alama za mume wako, na mume wako hakujui, nyie hampenani, je wewe huzijui alama zako mwilini, achilia mbali zile zisizo onekana,...unazijua, kwanini sasa usimjue mwenzako, wakati mumeambiwa mkioana nyie mnakuwa mwili mmoja.....?’ akauliza na sisi tukaangalia, kila mmoja akijaribu kukumbuka alama za mwenzake. 
Yule mama kila akikaa,anahisi kitu, akasema hata mimi sikubali kuwa yule ni mume wangu, akaomba akaingalai ile maiti vyema,haitazamiki, kila kitu kimehariibika, ...
‘Natumai ujumbe umefika sasa ni kazi.
*********
‘Tunahitaji kupambana na hili tatizo, lakini hatuhitaji kutumia nguvu, ...sisi wanawake silaha yetu sio kushika bunduki, sisi mungu katujalia, tuna silaha ya mdomo, tunaweza kushawishi...kwanza cha muhimu ni kumjua adui yetu mkubwa...’akasema yule mwanadada

 ‘Ni kweli tujitahidini kulifanikisha hili kwa vitendo...’akasema mama mwingine na baadaye akaongezea kusema;

‘Mimi nawaonea huruma sana hawo wasichana wanaofanya hizo kazi chafu, maana ukiwaona hawo akina dada wanaotumikishwa na hayo machafu ni wasichana wadogo tu, wamechukuliwa na kushawishiwa na kwa vile maisha ni magumu wamekubali....wengine walifaulu kwenda sekondari, lakini kwa vile wazazi wao hawana pesa, basi wakajikuta wakinaswa kwenye huo mtego, wakaahidiwa ajira, na pesa...’akasema mama mwingine.
‘Tatizo ni adui umasikini,na ujinga....na hapo ndipo tunataka kuingiza nguvu zetu, kwanza tuanze kuwaelimisha ubaya wa hayo wanayoyafanya, tukiwa na makongamano, mijadala ya mara kwa mara kwa kuwalenga wahusika, tutafanikiwa na ....makutano yetu ni muda kama huu....hatuna ofisi, na kwa sasa hivi hatuhitaji ofisi...tukiwa na jambo tunaitisha mkutanao, humo ndipo kwenye ofisi, na kama tulivyosema siri ni jambo muhimu....tuwe makini ...wenzetu ni wajanja , lakini hata sisi ni wajanja pia...’akasema yule mwanadada mtaalamu wa mitandao.
Nilikubali kuwa nitashirikiana nao ili kuhakikisha tunakomesha hilo kundi, hatua kwa hatua, na nikapewa mikakati jinsi gani ya kufanya,...waliniambia kuwa wamenichagua mimi kwasababu imegundulika kuwa mimi ni mmojawapo wa watu wanaotumiwa kufanikisha mambo ya hicho kikundi, ingawaje sipendi na sijui undani wake....
‘Wewe kuanzia sasa ukipewa hizo kazi tuwasiliane kwanza, tutajua jinsi ya kufanya…’aliniambii yule dada wa mitandao.

‘Hawa watu wana masikio wanajua kila kitu, mnaniweka kweney hatari kubwa sana…’nikajitetea.

‘Wewe mwanaume bwana, ..upo vitani, ukiogopa tutashindwa, …mimi ni mtaalamu wa mitandao, nimeshajua janja yao…ukija kuniona hakikisha huna simu wala hiyo saa yao…hakikisha hivyo…kwa pamoja tutawashinda, tunachohitaji ni ushahidi wa kitaalamu…’akaniambia

Kwa muda ule nilikubaliana na wale akina mama  kwa haraka sana, bila kufikiria uzito wa jambo lenyewe,nilikubali kutokana ni msongo wa utumwa niliokuwa nikikabiliana nao sikujali hatari ya hawa watu wengine, ambao wanajua kumnyamazisha mtu hata kwa kutumia simu.

Nilijua kabisa kazi hiyo itakuwa imeungwanishwa na hawa watu, sio mke wangu kama alivyoda ....masharti niliyopewa ni kuwa  ili nipate hiyo kazi inabidi nikamilishe hilo jukumu la kukutana na huyo mke wa muheshimiwa, ….nitakiwa nifanye kama nilivyowahi kufanya kazi nyingine, ila huyu anahitaji usiri wa hali ya juu maana ni mke wa muheshimiwa.


‘Kazi hiyo ipo mume wangu, lakini fanya kazi upate kazi…ikiisha hii nitakuambia jambo, kwani hata mimi nimechoka na mambo haya….’akanihakikishie make wangu, ili kuhakikisha hilo nikafanya uchunguzi wangu wa kimiya kimiya kweli nikakuta kazi hiyo ipo, haina shaka, lakini kwa msharti kuwa lazima nimalizane na wakala wangu, huyo wakala kafungwanishwa na mke wangu,  sasa nifanyeje...nikabaki njia panda. 


WAZO LA LEO: Saidia watoto wetu kwa ajili ya kizazi kijacho, usijali kuwa huyo ni mtoto wako au ni wa mwenzako, kwani ukifanya hivyo utakuwa umemjenga mtoto wako njia ya kupita, tukumbuke mtoto wa mwenzio ni wa kwako pia
Ni mimi: emu-three

1 comment :

emuthree said...

Nimeshindwa kuendeleza sehemu ifuatayo leo sababu zipo juu ya uwezo wangu. Nijitahidi tu!