Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Thursday, March 29, 2012

Hujafa hujaumbika-13



 Mke wangu akawa keshaondoka kurudi kwao, na nilibakia na wazazi wangu, ambao hawakutaka kabisa kunielewa, na hawakuamini kile kilichotokea na walitaka kujua kwanini imetokea vile, ...kila sababu niliyowapa haikuwatosheleza, na mwishowe wakanishauri kuwa nifike huko kijijini nikaombe msamaha yaishe, lakini mimi niliwaambia waziwazi, kuwa sihitaji kumuomba msamaha mtu yoyote , kwasababu yeye mwenyewe anajua kosa lake, nikasema bila aibu

‘Yeye ndiye alinisukuma hadi nikafikia huko,....nimejaribu weee....hapana ,sasa nimempata mtu angalau, hata kama hamtakubali hayo, ....basi ndio hivyo na iwe hivyo....’ nikajitetea hivyo.

‘Mwanangu unakumbuka wakati unataka kumuoa huyu binti, nilikuambia wazi,...kwanza hakulelewa katika mazingira mema, kama ulivyokuwa kumuona, anahitaji muda kujifunza kila kitu unachokihitaji, na hatuelewi hizo sababu zako zina msingi gani...hazina mshiko....ni aibu tupu kamawakisikiawazee kule kijijini...kwa ufupo wewe ndiye uliyeshindwa majukumu..’akasema baba.

‘Mwanangu tulikuambia na kujaribu kuzuia ndoa yako, hatukupenda kabisa mtoto wa watu aje kuumia tena...unakumbuka, tulikuambia hakikisha kweli unamuhitaji, kwani yule binti kaumia sana katika maisha yake, hatukupenda kabisa aishie kwenye maisha maisha ya taabu  tena...mimi nilibeba hiyo dhamana toka kwa mrehemu mama yeke, na hapa nilipo nashika nafasi yake kama mama yake...tafadhali mrudie ukamuombe msamaha...’akasema mama..

‘Kwani mimi nilimfukuza, kila kitu anapata, chakula nyumba hiyo hapo , alikuwa anapata,...aje, sijamfukuz amimi, lakini inavyoonekana anajitia kiburi, unaona alivyofanya katimukia huko kwao, sijui kwenu au sijui kaenda wapi, au kwa mwanaume mwingine. Ili alipize kisasi...sijui...yeye mwenyewe atalikoroga,...sina uvumilivu mimi,...kwa mtizamo huo  aspoangalia mimi nitaoa mke mwingine...’nikasema bila kujali..

‘Umechanganyikiwa mwanangu na nani huyo mke mwingine ndiye huyo uliyekuwa ukizini naye...?’ akasema mama kwa hasira.

‘Kwani tofauti ipo wapi mama...mimi huyo naye nampenda,na anajua nini ninachokitaka....mama unajua katika msiah haya ya ndoa nimejifunza mengi,mimi sikuwa natakiwa nikurupuke kuoa, ilitakiwa nifanye uchunguzi wangu mwenyewe,...nifanye majaribio kwanza, mwisho wa siku ningelijua yupi ananifaa...’nikasema bila aibu na mama akaniangalia kwa chuki.

‘Usinichefue wewe mtoto, unafikiri wanawake ni watu wa kufanyiwa majaribio, ina maana huyo binti hafai...hapana, kuna kitu hapo....’akasema mama kwa hasira.

‘Mama sio kwamba huyo mke wangu hafai,lakini tabia zetu zimekwua tofauti, hisa na mapendeleo yangu yawe vipi, ...mama samhani kusema kuwa, yule amekaa kishamba shamba sana, na mimi naishi mjini....unaoana alitakiwa kujifunza hivyo....lakini mengine hataki mimi nifanyeje....’nikasema.

‘Haya kamahutaki kwenda kumuomba mwenzako msammaha, sisi itabidi tukafanye hivyo, maana taratibu na mila zetu, tendo ulilofanya ni baya na faini yake ni kubwa, na inategemea huyo bintii atakusamehe au la...kwasababu ushahidi kila kitu kimeoenekana wazi....’akasema baba.

‘Sikilizeni wazazi wangu, kama mnataka kufanya hivyo, mimi siwakatazi, na mwambieni huyo mke wangu, yupo huru kurudi hapa, mimi sijamfukuza....kama hataki basi, sina jinsi....’nikasema na baadaye wazazi wangu wakaondoka.

                                 *********

Nilibakia ndani na kujiona mpweke, nikawaza mengi, na kun amuda akili inanijia na kujialaumu, lakini sijui kwanini, mawazo tu yalipokwenda kwa huyu kimwana, akili ikaruka na  bila kupoteza muda nikakurupuka mbio mbio nikamwendea huyo kimwana,...

‘Vipi mambo yameendaje, mke yupo nyumbani....maana wanawake wa kijijini wavumilivu hata uwatendeeje, hawabanduki, nakumbuka mama yangu alikuwa akiishii na baba, baba alikuwa mlevi kupindukia, akirudi anafanya maajabu, anampiga mama....lakini mama anakubali tu, na hata kumfulia matapishi,au awakati mwingine kwasababu ya ulevi, anapitiwa na haja...aah, mimi siwezi kabisa..’akasema kimwana.
‘Ina maana na mimi nikiwa hivyo utanikimbia.....?’ nikamuuliza.

‘Ikizidi sana ...., kulewa sio mbaya, hata mimi nakunwa, lakini sio ulewe na mipombe yako iwe kero,...iwe mipombe ya kupigana, .... uje unipige....hapana, tutapigana, mimi hilo ulijue wazi,....siwzi kuw amtumwa, kama nikupendana tupendane,kama tunageuza mapenzi uwanja wa ngumi, tutazichapa...ehe,,haya niambie imekuwaje..?’ akasema huyo kimwana.

Nikamuelezea ilivyokuwa na jinsi nilivyopagawa nikamuelezea kila kitu,....sijui akili yangu muda ule ilikuwaje,sikuwa hivyo kabla....nilikuwa kama mjinga fulani.

‘Sasa unajua mimi name nimetafakari sana kuhus maisha yangu, ....nimejiuiza nitaishi hivi mpaka lini,umri unakwenda, na msiha ndiyo hayo yanabadilika, nahitaji na mimi kutulia na kuwa na watoto wangu, kwa mtaji huo, name nasema hivi...kama unanipedna kweli, tufunge ndoa, na ndo aiwe ya haraka iwezekanavyo...’akasema huyo kimwana.

‘Eti nini...?’ nikashituka.

‘Eti nini..nikuulize unanipenda au hunipendi....?’ akauliza.

‘Hiyo umenishitukizia, nifunge ndoaa na wewe..hapana, sio kwa sasa, unajua ndoa lakini wewe, ukiingia kwenye ndoa, kuna masharti yake, na wewe sizani kama unaweza kutulia kwenye ndoa....tusubiri kwanza kidogo, kwanza sijaachana na mke wangu...mambo hayajakuwa shwari....’nikamwambia.

‘Sikiliza mimi sio Malaya, kama watu wanavyonisema, siwezi kukaa na wewe tu, huku najua mimi sio mke wako, kwahiyo amua moja, tufunge ndoa, au uishie zako...’aaksema kwa nyodo.

‘Sijasema sitaki kufunga ndoa na wewe, lakini ni mapema sana,....huoni hali ilivyo, mke yule tumesigishana, hatujakaa na kuamua kuachana na mara nafunga ndoa na wewe...kwanza yule ni rafiki yako mtaangaliaan vipi...’nikajaribu kujijitetea.

‘Umenisikia, lakini....kama hutaki ndoa, basi ishia,... umenikuta na maisha yangu, ....na kama walivyonikuta wengine na nilipowagusia ndoa wakaukata na wewe unaweza ukaukata vile vile, mimi sio jamvi la wageni na mimi nahitaji mume nitulie...nilee watoto wangu, hayo ndio maamuzi yangu...kwaheri nenda kafikiria ukija hapa uje na jibu,....’akasimamia kwenye msimamo huo na akasoegeela mlango akaufungua na kunionyeshea niondoke.

***********

Mtu mzima niliwaza sana,nikanywa mapaka nikapitiliza, nakumbuka siku hiyo nilijikuta nimelala kibarazani mwanyumba yangu nikiwa bwiii...na kesho yake natakiwa kazini.  Nilifika kazini nikasingizia naumwa, na kwenda kwenye barm huko nakiutwika kisawasawa...

Nilipofika kwa kimwana akanifukuza akiwa na msimamo huo huko wakutaka ndoa,na hakutaka kabisa kunifungulia na alinitishia kuwa nikiendelea kukaa hapo nje ya nyumba yake ataniitia watu kuwa mimi ni mwizi.

Ikawa kila nikienda kwake, ananitolea nje, na siku moja nikakuta mlango umefungwa kabisa, hayupo , hapo moyo ukaanza kuniuma,...wivu ukanijaa moyoni,  ikabidi nihangaike kumtafuta, na nilipompata akasema anajiandaa na safari ya kwenda kijijini kuna jamaa kaahidi kumuona, na yeye anachotaka sasa ni ndoa, ...

‘Muda wa kuolewa umefika, sitaki kuipoteza hii bahati....wewe umeshaoa unajua utamu wa ndoa, mimi je...kwahiyo toka leo tusijuane, mimi ni mchumba wa mtu...’akasema  looh, nikamzaba kibao, na yeye akanirudishia cha nguvu, nikabaki nimeduwaa....

‘Wewe unanipiga kibao mimi,...koma, kama ulivyokoma ziwa la mama..ko... kampige mkeo...toka humu ndani kwangu, sitaki hata kukuona....’akanifukuza kabisa, ikabidi nitoke pale nikiwa nimenywea, nikafika kwangu na kesho yake nilipofika kazini, nikakuta barua ya kusimamishwa kazi....

‘Huu sasa mkosi...’nikasema na kwenda kumuona mkurugenzi ambaye aliniambi waziwazi kuwa wamenivumilia sana, na wamenionya sana, sasa imefikia kikomo;

‘Unasikia ndugu yetu, wewe umeamua kuishi maisha yako unayotaka, ...maisha ambayo hayaendani na maadili ya kazi, unakuja umelewa, kazini hukai, una madeni mengi,uanitia kampuni hasara ....sisi tumechoka kukubeba, kwahiyo hiyo ndio zawadi yako, na ukiangalia hapo, madeni yako ni makubwa hata kuliko mafao yako, lakini kampuni imeamua kukusamehe madeni yaliyozidi, .tutakachofanya ni kukata madeni yetu kutokana na kiwango cha pesa ya mafao yako,...na hutakuwa na chochote kutoka kwetu, zaidi ya .....barua hii....’akasema mkurugenzi.

‘Eti nini, hapo niatawapeleka mahakaamni, sikubali, mnataka mkate kila kitu, nitaishije mimi....’nikalalamika.

‘Sawa wewe nenda huko mahakamani siunadai haki yako bwana, kama ipo tutakulipa, ....kwaheri bwana, tunakutakia maisha mema, kwakweli tumejitahidi vya kutosha, ....nenda kastarehe na kimwana wako...lakini kumbuka kuwa starehe ni gharama......’akasema huyo mkurugenzi na kweli nikafukuzwa na walinzi nikaishia zangu mitaani....

Nilipofika nyumbani kwangu nikamkuta yule kimwana kajaa tele, akanipokea kwa bashasha, utafikiri sio yule aliyenifukuza kwake, na aliponiona nilivyonywea akajua kuan jambo;

‘Vipi mpenzi mbona unakuwa kama umemwagiwa maji....?’ akauliza.

‘Sasa mzee mzima nimeumbuka,kazi sina....’nikasema.

‘Kazi huna, wewe mwanaume bwana, kwani kazi ipo moja hapa duniani, nikuambie ukweli, mimi nilifukuzwa kazi siku nyingi sana, lakini naishi, natesa raha....hapa sin akazi, lakini sijawahi kulala njaa, ni akili kichwani...bongo hapa, wewe tesa maisha, ukiyapatia ....maisha yenyewe mafupi, unataka kuyawahisha kabla ya  siku zake....sikiliza utanioa au hunioi?’akasema bila kujali  matatizo yangu.

‘Sasa wewe umeshasikia kuwa sina kazi....bado unataka tuoane,  tutaishije?’ nikamuuliza.

‘Kwani mimi naishi hivi nina kazi, kwani hawo waliopo mitaani wakihangaika wana kazi zakuajiriwa hebu jiulizei wanaishije...tutajua jinsi ya kuishi wewe usijali kabisa..hayo maisha ya mbeleni niachie mimi, ilimradi usiniingilie,....mimi nitakulipa fadhila zako, ili ujue kweli nakupenda, unafikiri,...hebu jiulize kwanini nisiwang’ang’anie vipoba wanaojigonga kwangu, nakuja kwako, kwasababu nimezimia kwako, ....wewe namimi tunaendana....unasemaje mpenzi...’akasema

‘Sawa kama upo tayari kuishi na mimi hata bila kazi, hapo najua kweli unanipenda....sasa unataka tuoane vipi..harusi au juu kwa juu...maana pesa sina?’ nikauliza.

‘Eti nini, Juu kwa juu, watu watajuaje kuwa na mimi nimeolewa....acha hiyo, ngoja nikuonyeshe njia, tutayarishe kadi, nitawapelekea marafiki zangu na wewe wapelekee rafiki zako, siulishawahi kuwachangia,.... sasa ....sasa ni wakati wao kulipa deni...hilo litafanyika tu....’akasema baadaye tukakubaliaan hilo.

Kweli mambo yalijipanga, baadhi ya marafiki zangu wakanichangia na pesa ikapatikana  yakutosha harusi ikafanyika, bilakujali kuwa nina mke mwingine kijijini, ndoa ikafungwa, ...na kimwana nikawa naishi naye ndani, siku , miezi ikapita,....

                                ************

Siku moja nikapokea ugeni, walikuwa mjomba na mke wangu wa kwanza, na baadaye akaja baba na mama, walikuja kwa mabasi tofauti, na wakanikuta nipo ndani na kimwana, akawakaribisha vizuri tu, ...

‘Huyu ndiye nani ...?’ akauliza mjomba.

‘Ni mke wake...’akajibi kimwana

‘Hujaulizwa wewe binti...’akasema mama.

Mimi nikawaangalia kwa makini halafu nikamwangalia mke wangu wa kwanza, niakasema kwa utaratibu;
‘Hivi ni haki mke kuondoka kwa mumewe ikapita zaidi ya miezi mitatu...aah,ishafika sita?’nikauliza huku nikiangalia kalenda ukutani.

‘Je wewe kwanini ulimruhusu akaondoka, ...na ukumbuek huyu mke, ulimchukua kwa wazazi wake, na ukaahidi kuishi naye ikiwemo ulinzi na usalama wake, je alivyoondoka,ulijitahidi kumtafuta,je ulijuaje anaishi vipi huko alipo....?’ akauliza baba.

‘Najua alikwenda wapi, ndio maana sikumtafuta na mlipoondoka hapa niliwapa maagizo kuwa arudi, hakurudi, ina maana alionyesha kiburi, na....maisha yangu siwezi kuishi bila mke, na ndio maana nikaamua kuoa mke mwingine, kama huyu yupo tayari kuishi nami tena, anakaribishwa, isitoshe, huyu mke wangu mpya walikuwa marafiki sana....mimi sijali...’nikasema.

‘Wewe nani aishi na...’akataka kuongea kimwana wangu, lakini mke wangu wa kwanza akaanza kuongea kwa huzuni. Kwanza aliziba macho yake kwamikono, nafikiri alikuwa akificha machozi, akawa ananiangali kwa jicho moja kupitia kwamkono aliyofunika machoni, na baadaye akaondoa na kuaniangalia moja kwa moja , sikuja ana maana gani.

‘Mama na baba na mjomba, nyie ni wazazi wangu, na ninawaheshimu sana, ..hali ilivyo sizani kwamba kuna ndoa tena hapa, mimi nimekulia maisha ya shida, nimeteseka sana, na nilijua kuolewa ndio mkombozi wangu, lakini naona ni kama kuruka mkojo na kukanyaga kinyesi....’akasemamke wangu wa kwanza kwa huzuni.

‘Wazazi wangu, labda ndivyo mungu alivyonipangia kuwa maisha yangu yawe hivyo...namshukuru sana mungu, ...mwenzangu naye ana hulka na maisha yake ambayo labda nimeshindwa kuyafikia, ...je nikiishi naye hapa yatakuwa yamefikia huko, kwasababu mimi ni yule yule, na tabia zangu ni zile zile...unafikiri itakuwaje ....sio kugeuka mfanyakazi na mtumwa wa nyumba hii...hapana nisingelipenda kuwa hivyo tena.....’akasema mkewangu huku machozi yakimtoka.

‘Mwanangu tulia, huondoki hapa, wewe ni mke halali wa mtoto wetu, tumekuozesha kwa sheria zote,...’ ...akasema mama halafu aaknigeukia na kusema ;

‘Hebu tuambia huyu unayedai kuwa ni mke wako mpya ulimoa kwa sheria gani, nani mzazi wako aliyeshuhudia hiyo ndoa,....huo ni uhuni wenu mumechukuana tu mitaani na kujifanya mumeoana, haipo hiyo...hatuitambui hiyo ndoa kma kweli ipo...’akasema mama.

‘Ndoa zipo za namna nyingi, kuna ya kimlia ya dini na ya bomani,....sasa mama unatakaje,sio lazima nioe kwa seheria za kimlia...mimi na huyu tumeoana bomani, na ndoa inakubalika, na vyeti vyetu vipo, na huyu mke ....maana nashindwa hata kumuita mke, kaondoka kwangu miezi mitatu,...ooh sita sasa....sna inaweza ikawa zaidi kaka huko, nitamuaminije, huenda...alikuwa kwa bwana’ke....’nikasema kwa hasira.

‘Niombe tafdhali....niombe radhi kabisa, mimi sio Malaya kama huyo hawara yako....mimi nimakulia kwenye maadili, siwezi kuuzalilisha mwili wangu kwa wanaume bila ndoa...hilo nakuthibitishia na mungu wangu ni shahidi...kwahiyo kama umeamua kumuoa huyo hawara yako, sawa, mimi naondoka, ila nataka talaka yangu...’akasema mke wangu wa kwanza.

‘Hilo tu, talaka yako ipo tayari nilishaitayarisha, nilikuw anasubiri tu hizi porojo ziishe nikukabidhi, kingine unahitaji nini, sidhani kuwa kuna maliyoyote tulichuma pamoja, sijachuma na wewe hata kitu kimoja....ulikuwa mfanyakazi tu wa ndani...na kuhsu mtoto, mimi nitatoa matunzo yote, atasoma, ukitaka kukaa naye sawa, kama hutaki nitakaa naye mwenyewe hakuna shida...’nikasema.

‘Mtoto wangu nitakaa naye, hawezi kuja kuteseka, kama nilivyoteseka mimi, hilo lisikutie shaka, na kuhusu mali , sihitaji mali yako, unakumbuka uliponitoa, niliweza kuishii maisha magumu kuliko unavyozania, kwahiyo kwangu maisha ni kawaida tu, ninachowatakia ni maisha mema, na nisema kuwa, ....mungu awabariki sana...’akatuli na kuanza kulia.

‘Unalia nini...kama umekubali yaishe basi...’akasema huyo mke mpya.

‘Wew tuli kule, hayakuhsu haya, ...’akasema baba kwa hasira.

‘Yananihusu sana baba, kama hayanihusu, kwanini huyu mwanamke mshamba, alikuwa akinitukana na kuniita hawara, au mliona mimi ni jiti tu, sina mdomo wakuongea...sikilizeni sana wazazi..wa-ngu,mimi nina heshima sana kwa wale wanaotaka heshima yangu, lakini mtu akinikosea,ataikosa heshima yangu, sijali kuwa ni nani, waulizeni wazazi wangu kijijini....’akasema na kutulia kimiya akisikilizia.

‘Kwa hilo tu tunakujau sana, wapo ulipotoka, ndio maana hatutaki uishi na mtoto wetu utatuharibia kizazi, hufai kabisa kuingia kwenye familia yetu, hatukukaribishi kabisa huko...’akasema baba na mjomba ambaye muda mwingi alitulia akasema;

‘Jamani hawa ni watoto wetu, kwa vyovyote iwavyo, na makosa yametokea, na hili ni muhimu tulijue, kuwa kama tutaendeela hivi hatutaweza kulisawazisha hili jambo,...huyu kijana bado anajioa mdogo, na hali niliyoiona hakuna jisni ya kumrudisha nyuma, keshaamua hivyo...labda kuna sababu zake za msingi, lakini hazijafuata utaratibu, na sioni kuwa kuna haja ya kufuata huo utaartibu tena, ...’akatuli amjomba na kuniangalia kwamakini.

‘Kuna usemi usemao, mtoto akililia wembe, mpe, ukimkata atajifunza, sasa wewe umelilia wembe, sawa huo hapo...’akasema na kumwangalia kimwana wangu, sikujlai, ...nikatulia kuskiliza tu, kwakweli akili ilifungwa kabisa, nilimuoa huyo kimwana, ni kila kitu, ...

‘Nakuambia mjomba, mimi maisha niliyapitia, ilifikia mahala niakasema nini natafuta dunia hii, ...starehe zina mwisho wake, na maisha haya yapo, wapo waliishi wafanya makubwa zaidi yetu, wapo wapi....huwezi kufanya lolote likaizidi hii dunia...tunakushauri kama wazazi, kumbuka ulipotoka, kumbuka kuwa maisha ya ndoa sivyo hivyo unavyzania, kuwa natamani hivi , nataka hivi, iwe hivyohivyo mara moja, ....’akasema mjomba name nikampa nafasi maana mjomba namuheshimu hata zaidi ya  baba.

‘Kweli umeonyesha kuwa damu yako inachemka,...na sasa unataka kusihi na wake wawil, hatukukatazi, lakini ujue kuwa maisha ya wake zaidi ya mmoja yana masharti yake....siotu kujiolea...masharti yake ni magumu ndio maana wengi wanashindwa na hata walio-oa, waulize vyema, nini wanachokipata...hukatazwi oa wake upendavyo, laini ukumbuke kuwa na wao ni biandamu,wanstahili zao, uwatendee wema na adilifu, je utaweza hilo...?’ akauliza mjomba.

‘Mzee wangu samahani kwa kuingilia, na huenda tukajadili haya mapaka kesho, wakati swala lipo wazi, kwanza ndio imeshafungwa, mimi ni mke halali, pili kwa kauli ya mume wangu,keshamuacha mke wake wa kwanza,kkwahiyo hapa tuzungumzie ndoa yangu sio ya wake wawili,...'akasema huku akitabasamu kwa dharau.
'Hivi wewe unaongea nini...'akasema mama.


'Ndio mama, huo ndio ukweli, ...ujue kuwa huyo mwenzangu keshaachika, na mimi ndiye mke halali....hukusikia alivyosema mume wangu ...au rudi vyema wasikie...sio nashnikiza iwe hivyo, hapana ila kauli ya mume wangu ndiyo ya msingi...’akasema mke wangu huyo mpya.

‘Nani kakuambia hayo wewe unafikiri ni rahisi hivyo....tulia kwanza wakubwa waongee, na ujifunze kuishi na wakubwa, umeshasema kuwa uheshimiwe na wewe utaheshimu, mbona wewe unakimbilia kuvunja heshima za wakubwa,kweli kwa mtindo huo utasheshimiwa...’akasema mama.

‘Samhani sana mama, nilikuwa naweka wazi, mimi nitafunga mdomow angu mpaka mniruhusu, haya mmmmmh’akasema na kuufumba mdomo wake kwa vidole.

‘Kazi ipo....’akasema baba.

‘Baba msiumie kichwa, mimi haya niachieni mwenyewe kwanza, mimi ni mwanaume, na nawaheshimu na kuwajali sana wazazi wangu, nitakuwa mtomvu wa fadhila kama sitwashukuru kwa yote mliyonifanyia, ...wazazi wangu nyie mumeshatimiza wajibu wenu,nawashukuru sana, ....lakini mimi sio mtoto tena, nimefikia mahala pa mamuzi yangu...’ nikasema huku nwaangali kila mmoja kwa wakati wake.

‘Mimi hapa ni mtu mzima,....namimi kuwa ninachokifanya ni kwa mslahi yangu,....natafuta maisha yangu, na ili nifanikiwe natakiwa nimpate mwenzangu anayekubaliana na matakwa yangu, umerudi kazini, unajihisi , unaburudishwa,hata uchiomvu wote unapotea....si kweli mama, ndivyo wewe unavyomfanyia baba...’nikasema huku namwangali mama kwa aibu kidogo.

‘Sio kwamba binti Yatima alishindwa hayo, kwakweli alijitahidi, ilakuna mambo machache ambayo kwang niliyaona ni muhimu kinaman fulani,..,kweli ana adabu, kweli ana sifa zote za kijijini, kwenu anafaa sana,....lakini niligundua kuwa kwangu itaniwia vigumu,hakubaliani na haendani nitakavyo mimi....hivi wazazi wangu mngelifurahi kuniona natembea mitaani na machangudoa, ...au nivumile tu mpaka nipate vidonda vya tumboni, au .....’nikasema na kucheka halafu nikasema;

‘Kama haiwezekani sawa, lakini kama kuna mbadala, kwanini mtu uumie....kwanini....’kabla sijamaliza kuongea Binti Yatima akanikatiza nami nikatulia kumsikilza nikiwa na hamasa kusikia nini anachotaka kuongea.

‘Wazazi wangu naona kitakachoendelea hapa ni kuzalilishwa tu, kauli hizo sio nzuri, na nisingependa kuingia huko na kulumbana ksuiko na sababu....mimi nimeshakubali, kama alivyosema mwenzangu, kuwa hapa tunaongelea ndoa moja,kuwa yeye keshapata mimi nimeshindwa, ...yote ni heri, karibu sana rafiki yangu na mume huyo wako wote...nawatakia maisha mema,....sina zaidi naomba hiyo talaka yangu,ili kesho na keshakutwa, isije ikawa vinginevyo....na nina... ‘akasema kukatishwa na kilio huku akiziba uso wake kwa mikono miwili, nahisi hakupenda watu wamuone akilia au ndio aibu ya kukaa pamoja na wakwe na kuongea aliyoyaongea..

‘Hivi nani kakuambi umeachika...’akasema baba.

‘Hapana baba mimi sipo kwenye ndoa tena, ndio ni ukweli usiopingika kuwa nilimpenda sana mume wangu, hajui tu, ....nilimpenda tangu siku ile ya mwanzo tuliyokutana naye, nilijua yeye ndiye muokozi wangu na yeye atachukua nafasi ya mama yangu, maana mama yangu alikuwa kipenzi changu,... lakini mungu alimpenda zaidi....lakini kumbe kwa mume huyu nilikuwa kama majaribio ambayo nimeyashindwa na inabidi nikubali ukweli..’akasema huku akifuta machozi.

‘Pole sana....’akasema rafiki yake kwa sauti ya upole, halafu akawa kama kashituka na kuuziba mdomo wake..hakuna aliyemjali kwa muda huo.

‘Hapana hilo kwetu kama wazazi halipo, sisi bado tunakutambua kama mke halali wa mwanetu, kwasababuu taratibu hazijafuatwa,ilitakiwa wewe mtoto wetu, urudi huko kijijini kwa wazee ili tuone tatizo ni nini, na kama inabidi iwe hivyo, basi taratibi zingelifuatwa....’akasema baba.

‘Baba, ukitaka hayo tutaumia wengi...tutaishije hapa...baba , na mama na mjomba kubalini ukweli,najua mnanipenda sana,na nami nawapenda sana,lakini tukubali ukwelil, kuwa kila jambo lina mwisho wake, na ukililazimsiha kuna kuumia hapo , na huenda ukakosa yote, kwani mkamia maji huyanywa...’akasema mke wangu wa kwanza.

‘Hapo umenena mtalaka wangu....na ndio maana nakupenda, ..unajua hali halisi...na nashukuru sana ,na hata hivyo nasikitika, kuwa sikukutendea haki,... lakini hakuna jinsi, inabidi iwe hivyo,...wewe mwenyewe unajua,...tutaishije hivyo...hapana, .... nakuomba uvumilie tu, kwani wapo wengi wanakutafuta kule kijijini, utampata anayekufaa....wewe ni lulu sana kule kijijini...wanakufahamu , wanakupenda na wanaikubali hiyo tabia, hulka, na mienendo yako...sawa eeh..’nikasema huku nakwepa kumwangalia machoni.

‘Nimekusikia na nashukuru kwa kauli yako hiyo, nami nasema hivi, nakushukuru sana, kwa wema wako na mengi uliyetendea,maana ulinitoa kwenye makucha ya simba, isingelikuwa wewe sijui ningelikuwa wapi, ...nakiri moyoni kuwa wewe ulikuwa kila kitu kwangu,lakini kama nilivyosema awali siwezi kulazimisha hali iilivyo,....’akatulia na kuhema kwa nguvu, baadaye akaendelea kusema;

Mimi nimekubali kushindwa, nisamehe kama nilishindwa kutimiza yale uliyoyataka, najua mwenzangu , ambaye alijifanya ni rafiki yangu, ndio kweli tulisoma anye, na namjua vitimbwi vyake na tabia yake, lakini sikujua kuwa ana malengo hayo, haina shida kabisa...kweli mwenzangu anayaweza hayo, ...lakini tukumbuke kuwa binadamu wote hatulingani,....huyu anajua hili na mwingine hajui, lakini lipo analijua kuliko mwenzake, tunazidiana...’akatulia an kumwangalia rafiki yake.

‘Siongei haya kukubembeelza kuwa nataka turudiane,hapana,....moyo umeshachefuka.... na baada ya hayo, naomba hiyo talaka yangu...niondeoke...’akasema huyo binti akigeuka kuondoka na alipofika mlangoni, mama akamrudisha na kwambia arudi ake, naye bila ajizi akafanya hivyo, akarudi na kukaa kwenye sehemu yake.

‘Mimi bado kauli yangu ni ile ile...ndoa bado ipo, sisi huyu binti unayemuita mkeo hatumtambui, na katu hatutamkaribisha kwenye familia yetu kama mke mwana....kwasababu tumajua , tunakijua kizaizi chake,nini unataka kutuletea katika hii familia....hapana, kama umeamua hivyo, basi jua kuwa sisi hatupo pamoja na wewe....’akasema baba na mama akakubali kwa kichwa.

Na mimi sikusubiri nikaingia ndani na kutoka na karatasi ya talaka, nikawa naisoma kwa sauti kubwa huku natembea kuelekea sehemu yangu niliyokuwa nimekaa awali, na kimwana akawa anatabasamu kwa mbali, na binti Yatima machozi yanamtoka, ...sikujali nikaisoma kwa mbwembe:

Mimi mtoto wa Msomali kwahiari yangu mwenyewe, bila kushurutishwa , nimeamua kumuacha mke wangu,kwa talaka zote .....sababu za msingi, kwanza hatuna mahusiano mema kama mke namume, pili kaondoka nyumbani miezi mitatu bila kuaga, na hakuwahi kunipa taarifa yoyote toka huko alipo,...pamoja na mambo mengine nimeamua kumuacha, yeye sio mke wake tena, na yupo huru kuolewa na yoyote yule....hatudaiani...’Nilipofika hapo nikatupa jicho kumtizama binti Yatima, ambaye alikuwa kafunika uso wake na kitambaa akifuta machozi

 ‘Na kuhusu swala la mtoto yupo huru kuishi na mzazi yoyote kati yetu wawili , na hata hivyo nimekubali  kumhudumia kwa mambo yote muhimu, ....nimemaliza,aukunakipengele nimesahau maana mimi mimisioo mtaalamu kwa mambo haya...’nikasema huku namwangalia mjomba, utafikirii ni jambo la heri lililokubalika, nilipowaona wapo kimiya, nikaweka saini yangu chini, na kumkabidhi binti Yatima ile katarasi, ....

‘Hahaha...kweli wewe mtoto umetushinda, yaani umekaa na huyu binti mkapanga muandike hiyo talaka, eti kuwa hii  ndio talaka, huo ndio utaratibu gani,...lini mlikaa baraza la usuluhishi mkayaongea matatizo yenu, hata ikashndikiana, ...hebu niambie, wapi mlikutana na wazazi mkayaongea matatizo yenu, au kwasababu umeguswa mtima nyongo wako na hawo wanaojua wapi ulipo na kuwazuzua wanaume....sikiliza tutakusubiri kijijini uje ufuate taratibu zote, lakini talaka hii haikubaliki.....’baba akaichukua ile talaka na kuichanachana vipande vipande.

‘Hata ukiachana imeshapita hiyo...’nikasema hata bilakufikiria...’na wote wakaniangali huku wananishangaa, hawakuamini kuwa kweli ndiye yule kijana, yule mtoto waliyemtarajia kuwa atashika usukani wa familia kamaalivyo mjomba....wakachoka na hatimaye baba akasimama nakusema;

‘Twendeni zetu....huyu naona kuna lake jambo,...sio bure, .... bila kumkazania huyu tutapoteza mtoto moja kwa moja....’akasema baba na kumgeukia mkewe ambaye alionekana kujawa na huzuni usoni...mama na mtoto bwana,hata awe mkubwa vipi. Na hata mjomba alivyotaka kuongea kitu, akasita na kumfuata baba nyuma, huku kaweka kichwa chini. Mimi mwenyewe kuna muda hisia zilinijia na kutaka kuwaambia wasubiri kidogo, lakini nilipomtizama kimwana, nikayeyuka, nikatabasamu naye akatoa lile tabasamu lake, nikawa hao .....
Mara mlango ukagongwa, tukaangaliana , kwasaabbu ni kwangu nikainuka kufungua mlango, na nje niliona gari ambalo ni la wapiga mnada, nikawaza kuna nini leo hapa, pembeni ya mlango kuna jamaa kashikilia daftari , akaniangali ahalafu akasema;

‘Sisi ni watu wa mnada, hiki hapani kibali toka mahakamani, ...kazi yetu tuliyopewa ni kuwafuatilia wadaiwa sugu, unakumbuka nyumba yako hii ulijenga kwa mkopo...’akawa anaendelea kuongea, lakini sikuweza kumsikia, maana kichwa hapo kilikuwa sio changu,... nilishasahau kuwa hiyo nyumba niliijenga kwa mkopo nadaiwa.....sasa itakuwaje, ...mungu wangu wee....

Je iltakuwaje, na je ilikuwa rahisi hivyo kuwa nimempata kimwana ,ndio kila kitu saafiii...hebu tuone yatakayoajiri...niwaulize kuna yoyote kati yenu aliyewahi kukutwa, au kuwa jamaa yake aliyewahi kukutwa  na majanga kamahaya, je alisaidiwaje?

WAZO LA LEO: Usione watu wapo kimiya, ukazani hawana shida, au matatizo kama yako, ...hapana...kila mtu ana shida au mataizo yake, ila wengine ni rahisi kuyaongea mataizo yao au shida zao na kujiona wao wamezidiwa.

 Ni kweli shida zipo na huenda zikazidiana, na tunatakiwa kusaidiana, na labda wengine wanafikiria kuwa kwa kuongea sana wanaweza kukapata misaada,...inwezekana sikatai, ila isiwe ndio sababu ya kujitangaza kwa kila mtu, kwani kwakufanya hivyo utafukuza baraka, na sio wote wenye nia njema na shida zako. Hili nimejifunza,...sijui wewe,hata hivyo wahenga husema; subira yavuta heri


Ni mimi: emu-three

9 comments :

elisa said...

Mmh inasisimua na kufundisha sana.

emuthree said...

Elisa ulipotelea wapi mpendwa, mpendwa sana, karibu tena, na nashukuru kuwa nami tena...au na wewe uliamua kuwa `kimiya kimiya...'

Kuna mpendwa mwingine naye kaingia mitini...Samira, upo wapi, ...kwa mara ya mwisho kukusikia hapa kijiweni,ulisema unakuja huku bongo,umezamia wapi maana ukifika huku bongo, unachanganywa an maisha, hata kile ulichopangilia kinayeyuka....
Ni matumaini yangu upo na upo salama, na karibu hapa kijiweni kwetu, tunakupenda sana na kukuhitaji kwamawazo yako yeney hekima.

Yasinta Ngonyani said...

Hakika ina sisimua na kufurahisha ...Nimelipenda wazo la leo...Pamoja daima.

samira said...

m3 mzima nipo dear nipo nimerudi na nashukuru kwa kunikumbuka nami nawapenda sana ila life na baadhi ya watu wa tz wamenichanganya sana sana huwezi amini nimemiss miezi miwili mikasa yetu hasa akufaae kwa dhiki tangu nimerudi about 2wk sasa nasoma zilopita vp mzima dear naona kuna mkasa mpya naufatilia japo mda mdogo
nimefurahi sana kunikumbuka nami nipo narejesha akili
love u m3

Precious said...

Wazo la leo lafundisha sana....na kweli mtoto akililia wembe mpe Mtoto wa Msomali ipo siku atamkumbuka Binti Yatima....Tuko pamoja M3 na wadau wote wa blog hii.

emuthree said...

Tupo pamoja dada Yasinta ubarikiwe sana

emuthree said...

Haya ndio maisha yetu mpendwa Samira. Vumbi,jua kudhulumiwa, kuonewa ajira hakuna,maisha ghali.
Huku kufa hatufi lkn cha moto tunakiona

emuthree said...

Precious tupo pamoja,Mungu akupe baraka tele tuzidi kua pamoja

elisa said...

Nipo kabisa miram3,ila mara nyingi nasoma haraka haraka,hata comment nashindwa kuacha ,si unajua majukumu tena ya maisha ,ila tupo pamoja kabisa.