Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Friday, January 20, 2012

Siku ya kuf nyani, miti yote huteleza




Unajua siku nyingi nimekuwa nikiwaza kwanini wakwe wanaogopana. Yaani wewe ukioa, basi kukutana na mkweo inakuwa taabu, nikajiuliza hivi mama mkwe au baba mkwe si sawa na mama au baba yako tu? Lakini inakuwa kinyume chake, wanageuka kuwa watu wa kuogopwa kama mtu mwenye ugonjwa wa kuambukiza. Nimesikia kuwa kuna hata wengine wanazidi kiasi, hasa wenzetu wa huko Kusini, nasikia kuna masharti kadhhaa ya kukutana na wakwe, mbona , na wakati nawaza hili nikakutana na tukio moja mbalo linahitaji kutafakari kwa wale wenyewe kuelewa.

Tuwasikilize watoto wetu, tuwe karibu nao, kwani huwezi juanini kinaweza kutokea leo au saa fulani, kwani , siku ya kufa nyani, miti yote huteleza.

Kidsa hiki kimenifundisha mengi, hebu kisome kwa makini,hasa kwawale wanaopenda kuvaa vibukta,na wale wasiopenda kuwasikilza watoto wao.

Yupo jamaa mmoja alikuwa ndani kwake akiwa busy na laptop yake,mara akasikia hodi ikipigwa, kwanza akakunja uso,kwani hakutaka usumbufu, na akaendelea kufanya alichokuwa kifanya, wakati huo pembeni yake alikuwepo mtoto wake...

Mtoto yule mara kwa mara alikuwa akimwangalia baba yake kwa jicho la kujiiba, na mara nyingi akawa kama anamuonyeshea baba yake kwa ishara fulani , ambayo baba yake hakuielewa. Na baba yake akazania ni utundu wa mtoto wake ,kwahiyo akawa hamjali, baadaye akaona ni kero akamfokea na kusema;

'Nimeshakuambia sitaki usumbufu,....huoni nina kazi hapa..nenda kacheze nje…'yule baba akaendelea kuwa busy na laptop yake, siunajua tena siku hizi mambo ni vilaptop, laptop ni kama simu ya mkononi...kama huna kama mimi ulie tu...

Mara huyo mgeni kaingia na yule, mtoto alipogundua kuwa huyo ni mgeni gani, haraka akakimbilia palealipokaa baba yake na kutaka kumnong'oneza kitu sikioni, baba yake akang’aka na akarusha kibao, na kusema `hebu kule mtoto mtukutu wewe, hutaki hata kunielewa...'

Kibao kile kikampata mtoto shavuni, naye kwa hasira akaondoka zake akilia.
Mara yule mgani aliyeingia, akakutana na yule motto akikimbilia nje huku analia, alijaribu kumsemesha, lakini yule motto hakutaka kumsikiliza, akakimbilia nje…Kumbe mgeni yule aliyeingia ni mama mkwe. Mama kwasababu alikuwa na mazungumzo muhimu na baba yule, akaingia na kukaa kwenye kochi, ambalo lilikuwa wazi,mengine yalikuwa na vikorokoro vya yule mtoto, alivyokuwa akichezea, basi, mama yule kwa aibu ikabidi akae mkabala na mkwewe,akijua mazunguzmo yake ni mafupi tu ataondoka zake.

Mama alikaa baada ya kusalimia na jamaa yule, na jamaa yule akarudia kukaa mkao ule ule aliokaa mwanzoni,hakuwa na habari nyingine, , lakini ghafla ,mara akaona mama mkwe akiinuka na kuondoka, akashikwa na mshangao kidogo, hakujali, akazania huenda ni mambo ya ukweni tena, kwasababu mkewe hayupo ndio maana hakutaka kukaa kwa muda mrefu akaendelea kudonoa laptop yake.

Bahati nzuri mkewe akaja, na alipoona mama yake yupo nje kasimama, akasema kwa utani, `mama kwanini unamuogopa mkweo, hamjazoeaan tu, huku mjini mama, kaa ndani uongee naye...siulisema una shida naye mbona umesimamahuku nje…?’ akauliza binti wa huyo mama.

Baadaye mke mtu akampita mama yake na kuingia ndani, lakini wakati anataka kumpita mama yake, mama akamsogeela akitaka kusema jambo,, lakini yule binti alifikiria kwua huenda mama yake aliataka kumpokea, ule mzigo, akaona sio vyema, ngoja auingize ndani kiheshima,…..

'Mama wewe usijali karibu ndani,
'Sikiliza kwanza, ...'akasema mama akitaka kumwambia kitu binti yake, lakini yule mke-mtu akaingia ndani kwa haraka, na kuuweka ule mzigo kwanza, ili baadaye atoke nje ikibidi , na alifikisha ule mzigo, akasogea chumba caha maongezi kuhakikisha kuwa mumewe yupo, au kalala ndani, na abahati akamkuta yupo busy na kilaptop chake.
‘Mbona hukamribishi mama ndani….?’ Akauliza mke mtu.
‘Mbona nimekaribisha….’akasemahuku akiangalia jambo kwenye laptop yake.
Mkewe akatupa jicho, oooh, mungu wangu, ile bukta ….akakumbuka…aakjiuliza ina maana mama alishaingia ndani au bado…aakgeuza macho kuhaikisha kile alichokiona ni kweli au macho yake…akajikuta akiishiwa nguvu, lakini akajipa moyo kuwa huenda mama, alikuwa hajaingia ndani. Jamani hizi bukta sio za kuvaa wakati wote..zingine zinafumuka hata bila kujua..kumbe...

'Mume wangu…hebu inuk hapo haraka…na ukivaa hiyo bukta tena nitakuchapa viboko , sinilishakumbia kuwa bukta hiyo imefumuka....hebu toka kabadili hiyo nguo haraka, …huona mama mkwe yupo nje anataka kuingia...'akasema mkewe
Jamaa alipoinama kujiangalia karibu azimie, aliona aibu ya mwaka,...akaitupa ile laptop pembani na kukimbilia chumbani, huku akisema ;

'Duuh, kumbe ningemsikiliza mtoto wangu nisingeumbuka kiasi hiki, kumbe mtoto wangu alikua akitaka kuniambia jambo...ooh…nimeumbuka mzee mzima, kweli nyani akitaka kufa , miti yote huteleza…siku ikaharibika.

Wenzangu, hata tukiwa ndani kwako...usijiachie sana , wakati mwingine tuangalie na nguo za kuvaa, na pia tupende kuwa karibu sana na watoto wetu, ….

Hebu soma hii toka kwa Da Mija..mdau jirani …inafanana na hiki kisa:

Ni mimi: emu-three

1 comment :

Yasinta Ngonyani said...

Tunazidi kupata madarasa kila siku kuhusu malezi ya watoto, maisha ya ndoa nk. Wengi wanafikiri watoto ni viumbe wasio na akili wenye kusumbua..lakini ni muhimu sana kuwasikiliza. Ahsante kwa kisa.