Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Thursday, January 26, 2012

Akufaaye kwa dhiki ndiye rafiki wa kweli-76 hitimisho-20




‘Hivi kweli huyo docta Adam mumeshindwa kumkamata, anaweza kutupotea kirahisi hivi, na mbona hospitali yake inafanya kazi, inaendeshwa na nani, maana naona ipo inafanya kazi kama kawaida, lazima kuna mtu yupo pale ambaye anawasiliana naye, hatujafanya uchunguzi wa kutosha…’akasema mkuu wa polisi.

‘Mkuu uchunguzi wa kutosha umfanyika, na kumbukumbu zinaonyesha kuwa , Docta Adam, alishaondolewa kwenye uongozi wa juu wa hiyo hosptali, na alishawekwa mtu mwingine, kwahiyo kutoweka kwake kumetokea baadaye, na wao wanahisi hakupenda kuondolewa, ndio maana baadaye aliandika barua ya kuacha kazi, lakini wadhamini wa hospitali hiyo wakakata….’akaongea askari wa kitengo cha upelelezi

‘Walipokataa ndipo akaondoka, au ilikuwaje mpaka akatoweka kwenye hiyo hosptali…?’ akauliza mkuu wa kituo.

‘Kutoweka imetokea akiwa likizo, yeye alichofanya ni kuomba likizo yake ya mwaka, alipoidhinishiwa haikujulikana alisafiri kwenda wapi, kwani kwa jinsi inavyoonekena hayupo hapa nchini… na sisi tuliposikia kuwa huko India kuna watu wetu tukafikiria huenda ndiyo yeye, lakini kwa maelezo tuliyoyapata sio yeye kabisa, lakini kwa uhakika tukataka tuwakamate wote wale ambao wapo India kwasababu kwa taarifa tulizopewa, wamekuwa wakijihusisha na ugaidi…’ akasema huyo mpelelezi.

‘Na ugaidi….?’ Akashituka huyo mkuu.

‘Ndivyo walivyotuambia, unajua neno ili ugaidi limekuwa likitumiwa kila mtu anapofanya mambo makubwa nje ya ncho yake , hasa yakihusiana na uvunjaji amani, kuhatarisha maisha ya watu….sasa hawa watu wamesadikiwa kuwa walikuwa nyuma ya mambo hayo, lakini walifuatiliwa kwa karibu sana na wao walipogundua kuwa wanfuatiliwa wakaacha hicho walichokuwa wamepanga..’akasema huyu mpelelezi.

‘Sasa ikawaje, hawo watu wapo wapi maana nimeambiwa hamkumpata hata mtu mmoja hapo uwanja wa ndege imekuwaje?’ akauliza mkuu wao.

‘Ni ajabu kabisa maana picha na kila kitu cha hawo watu tunazo, lakini abiria wote waliotoka kwenye hiyo hakuna hata mtuu mmoja anayefanana na hizo picha, tulishindwa kabisa tumkamate nani, lakini watu wetu wanawashuku baadhi ya abiria waliokuwemo humo na wanafuatiliwa kwa karibu, lazima tutagundua jambo, tunahisi kama watakuwa waliteremka njiani , hawakufika huku moja kwa moja, sijui watakuwa waliteremkia nchi gani, tunajaribu kutafuta mawasiliano sehemu zote ambazo ndege hii ilisimama…’akasema mpelelezi huyo.

‘Vituo vyote hivyo havikuweza kuleta maelezo yoyote ya maana, kwasababu kwa maelezo yako unayotoa hapa umefanya ndege kama gari, na nijuavyo ndege kutoka India haina vituo vingi...au..?'akasema mkuu huyo akiwa anakagua zile taaarifa.

‘Ni kweli hakuna vituo vini na kote huko wametuambia kuwa hakuna mtu kama huyo aliyeteremka kwenye kiwanja chochote, na isitoshe mbona watu kama hawo hawakuonekana kuondoka na ndee hiyo iliyotoka India,…maelezo haya yalituchanganya kidogo, ikabidi tuwasiliane na wenzetu huko India , wao wakasema wana uhakika na hilo, labda kama kuna njia nyingine walitumia, lakini wao wana uhakika abiria hao walipanda hiyo ndege…’akasema mpelelezi huyo.

‘Hapa naona kuna kuchanganyana, nahisi kuna jambo limefanyika, kwasababu haiwezekani watu hawo waonekane upanda hiyo ndege na ghafla wayeyuke…fanyeni uchunguzi wa kina hakikisheni abiria wote waliopanda hamo mumewafauatilia kwa karibu, hilo mumelifanya?’ akauliza mkuu.

‘Hilo tumelifanya na ndio maana watu wetu wametawanyika kila sehemu kufuatilia nyendo za abiria ambao walitoka India, ni kazi ngumu kidogo, maana wapo wengi, lakini shabaha yetu imewalenga wanaume na wale ambao wanasifa zinazokaribiana na hawo watu tunaowatafuta…’akasema huyo mpelelezi.

‘Safi, sasa hata hivyo hakuna mtu mwingine ambaye anaweza kutusaidia kwa hili, yaani mtu ambaye alikuwa karibu sana na huyo dakitari…?’ akauliza mkuu huyo.

‘Kuna watu wawili, kwanza mkuu, tulikuomba umuombe Inspekta yule wa ncho jirani aje kutoa msada, kwani swala hili ndiye tangia awali alikuwa nalo, anaweza akatupa msaada mkubwa, ….’akasema huyo mpelelezi,

‘Hilo tumeshalifanya, lakini ukumbuke kuwa yule sio raia wan nchi hii, kwahiyo kibali chake mpaka kikubaliwe ni maswala makuba ya kiserikali, hata hivyo kwa vile serikali imelipa hili jambo kipa umbele, wakiwa na lengo la kuondoa haya matatizo haraka, basi huenda kwenye wiki hi atakuja…najua ana masaaa mkubwa sana, lakini bado sisi wenyewe hatujashindwa, kwani nimeulizwa, ina maana sisi kazi hiyo imetushindwa….hatujashindwa, ila tunahitaji baaadhi ya maelezo ambayo hayajajitosheleza, au sio, na kuachia huyo hakuna mtu mwingine….’akauliza mkuu wakituo.

‘Kuna binti mmoja ambaye alikuwa akifanya akzi na huyo docta, ingawaje walikosana naye na kuacha kazi inasadikiwa kuwa huyo docta licha kuwa walikuwa wakifanya kazi naye na huyo binti alikuwa msaidizi wake, lakini pia alikuwa mpenzi wake…tunasadiki kuwa huyo binti anaweza akatupa msaada wa kutosha, lakini hapo hapo ndio maana tunamuhitaji huyo Inspekta kutoka ncho ya jirani, kwani unakumuka karibuni alitupigia simu kuwa alikuwa akiwasilina nao…..’akasema huyo mpelelezi.

‘Hapo nimekuelewa, na kweli lazima huyu Insepkta tumuombe aje, na pili lazima huyo binti tuwasiliane naye, ikibidi aitwe, kwasababu ni raia wetu na anaweza kuleta mchango mkubwa, na mna uhakika hana mahusiano na hilo kundi kisirisiri….?’ Akauliza mkuu huyo.

‘Hapana, hayo yote mwanzoni tuliamini hivyo, lakini baada ya uchunguzi wa kina tulithibitisha kuwa hahusiki, na ndio maana kwa ushaurii wa Inspecta, tuliamua tumtumie yeye kama chambo ili tuweze kuwakamata hawo wahusika, kwani walionekana kumfuata fuata sana huyo binti, na unakumbuka jamaa wale wa msituni walioamua kurudi serikalini walivyosema, kuwa huyo binti anawindwa na maadui, sasa hatukujua ni maadui gani, ndio maana tukamtumia yeye kama chambo….na hilo ndilo lililotusaidia kumgundua Docta Adamu, kuwa ana mafungamano na kundi hili la ajabu…kundi ambalo liliamua kuendeleza mapigano ndani ya mji….’akasema huyo mpelelezi.’

‘Kwanini walikuwa wakimtafuta sana huyo binti, hamkuligundua hilo….niliwaagiza mtafute sababu ilikuwaje hamkufanikiwa …?’akauliza mkuu

‘Sababu kubwa iliyoonekana mwanzoni , na natumai waliitumia kama kiini macho , ili ionekane kama ni sababu ya kimapenzi, maana ilivyobainika awali ni kuwa Docta Adamu, alikuwa akimpenda huyo binti, na huyo binti akawa hana mapenzi nay eye, alionekana kumpenda au alikuwa karibu sana na huyo mgonjwa aliyepelekwa India….’ Akasema yule mpelelezi na kutulia kidogo, kumpa nafasi mkuu wake kuoanisha hayo maelezo yake na taarifa iliyopo mezani kwake.

‘Baadaye huyo mgonjwa, ambaye watu walikuja kuamini kuwa ni mume wa huyo binti, kumbe sio mume wake, tulichobaini ni kuwa Docta Adam, alishampenda huyo binti na alipoona huyo binti yupo karibu sana na huyo mgonjwa akajenga wivu, na ndio chanzo cha kutaka kumuondoa huyo mgonjwa duniani, kama unakumbuka ile taarifa yangu ya mwanzo…’akasema huyo mpelelezi.

‘Sizani kama ni mapenzi tu, hilo tuliliwekea ulizo, na niliwaambia mjaribu kufanya uchunguzi kama tunaweza kupata sababu nyingine,….je hilo mlifikia wapi, maana sioni lolote kwenye hii taarifa…?’ akauliza huyo mkuu na kabla hajajibiwa hilo swali akaendelea kuongea kwa kuuliza swali jingine ;

‘Na huyo mgonjwa anaendeleaje, kuna taarifa yoyote toka huko India, …kwani nilipata taarifa nyingine zenye utata kuhusiana na uraia wa huyu mtu, je uchunguzi haujabaini kuwa ni raia wetu au ni raia wa nchi gani?’akauliza mkuu.

‘Mpaka sasa anaonekana ni raia wetu, lakini familia yake haijabainika ni ipi, kitu cha kushanagaza ni kuwa watu wa karibu waliokuja na kwenda kumsaidia huyo mgonjwa ni raia wa nchi jirani, na hii inaweza ikatufungua macho kuhusiana na uraia wa huyu mtu, na hili pia bado linamuhitaji jamaa yetu, tunahitaji msaada wa huyo Inspekta, nahisi atakuwa kagundua jambo ambalo hakuliweka wazi…’akasema mpelelezi.

‘Haya cha muhimu kwa sasa ni kuwasilina na huyo binti, unasema anaitwa jina gani, mmh, Rose au sio.., fanya kila iwezekanavyo tupate maelezo yake, ukumbuke hii ni kazi yako muhimu ukifanikiwa kwa hili utaoana matunda yake, mimi nitawasilina na huyo Inspekta kwa simu, na ninafanya mpango wa kumuomba aje huku kumalizia kazi yake…ingawaje hatujashindwa kwa hili, lakini yeye ni mtu muhimu sana kwetu…sawa tutawasilina baadaye, hakikisha sasa hivi unawasilina na huyo binti nani vile vile…

‘Ndio mkuu, nitawasilina na huyo binti anayeitwa Docta Rose.

*********

Rose hakuamini kuwa mtu aliyempenda ndio siku zake zimefika, akamsogelea na kumshika shingoni, akaondoa mkono haraka, ilikuwa kama mtu aliyeshika kaa la moto, akageuka kumwangalia Maua ambeya likuwa kamshikilia mkono huku akiwa kafumba macho, ikiashiria kuwa bado yeye alikuwa kwenye kuomba, na utafikiri hajasikia docta alichosema;

‘Sasa mumeamini, mashine yote inaonyesha kuwa uhai haupo,m safari nashukuru kuwa mpo na siono umuhimu wa kusubiri tena, lakini kama huamini docta Rose, nakuachia muda wa kufanya miujiza yako tena, kwani umesema ilishatokea mara nyingi ukiwa naye, mimi inabidi nitoke kidogo, kwani nina mgonjwa mwingine….’akasema na kuanza kuondoka.

Rose akatizama mashine na kila kitu kitu kilionyesha kuwa mambo yamekwisha, lakini hakukata tamaa, alipomshika shingo na kuona ujoto wa uhai upo, akaingiwa na ujasiri , akijua hiyo siyo mara ya kwanza kupambana na huyo mgonjwa,….akamsogelea na kuweka shavu karaibu kabisa na mdomo, ….akainua kichwa na haraka, na kwamangalia Maua.

‘Maua mbona siamini….mashine ianyoneyesha vingine, lakini mgonjwa huku anaonekana kabisa….’hakumalizia, akainuka na kushike ile mipira inayotoka mwilini mwa mgonjwa, akashikwa na mshangao, maana ile mipira ilikuwa imeachia kabisa ina maana hakuna mahusiano kati ya mashine na mwili wa mgonjwa….

‘Ohh, mbona hivi, …..’akashangaa, akaivuta ile mipia yote miwili akagindua imeacahia kabisa, akamsogela mgonjwa na safari hii karibu adondoke kwa mshituko, kwani alichoona kilimfanya atoe macho ya kutokuamini….

Maua alikuwa kakodo amacho kumwangalia mgonjwa, naye alikuwa kshikwa mshangao ule ule aliokuwa nao ndugu yake, hakuamini alichokuwa kakiona, na wote wkageuka kuangaliana, na kabla hajawasema kitu wakgeuka kwa pamoja kumwangalia monjwa, wakakuta kinyume na walivyoona mwanzoni.

‘Alikuwa kafumbua macho…nina uhakika huo..;akasema Maua

‘Ndio alikuwa kafumbua macho, sasa nahisi karudi kwenye usingizi, kuna kitu kinanipa wasiwasi, kwanini hii mipira haijaunganishwa na mwili wa mgonjwa, nina uhakika docta aliondoka ikiwa haipo hivyo..’akasema Rose

Rose kabla hajapata jibu akatoka mbio kumwahi docta kwani kulikuwa na dawa zilihitajika na pia hakutaka kabisa docta atoe taarifa yoyote kwa wazazi wao, na alipofika mlangoni akamuona docta anawakaribia wazazi wake, hakutaka kutoa sauti, akamkimbilia na alipomkaribia akamshika mkono , na docta akashituka kuona mtu anamshika mkono na wakati huo alishajiandaa kuongea na ale wazazi ambao walikuwa wameshikwa na butwaa..

‘Docta twende ndani haraka, nataka ukanipe dawa, mgonjwa anahitaji dawa…’akasema Rose.

‘Mgonjwa gani huyo….’akasema Docta kwa mshangao.

‘Wewe twende ndani haraka, hakuna muda wa kuulizana maswali,….wewe unauliza jibu, kwani tulikuwa na wagonjwa wangapi…’akasema Rose huku akimvuta Docta mkono kuelekea ndani. Na yule docta akamfuata huku haamini alichosikia. Akawa anajiuliza ina maana yule mgonjwa kazindukana tena, kweli huyo mgonjwa ana roho saba, ….

Mama na shangazi safari hii hawakukubali wakaamua kuwafuatilia nyuma Rose na Doctor, na bahati nzuri mlinzi alikuwa akijishughulika na mambo mengine kwa vile alikuwa anajua kuwa docta anaonea na hiyo familia, na alipoona wote wanamfuata Docta nyuma, akajua labda wote wameitwa kuingia huko ndani, wakapita mlangoni bila kuzuia na hata alipofika ndani ya ile wodii maalumu wakajikuta wakiwa wameduwaa, na macho yao yote yalikuwa kitandani.

Docta yeye alikuwa mbio mbio akikimbilia kule kitandani alipokuwa kalala mgonjwa, alipofika pale kitandani akamtupia jicho yule mgonjwa halafu akaangalia kitandani, akaangalia ile mipira ambayo ilikuwa imewekwa pembeni ya kitandu kwa mpangilio usio wake, hakujali kwa hilo kwa muda huo, alichokuwa anajali ni hali ya huyo mgonjwa, na alipomuona mgonjwa kakaa na kujiegemeza kwenye bega la Maua akajikuta akisema kwa sauti;

‘Hii ndio miujuza ya mungu, na kweli kama huamini, ukikutana na miujiza kama hii ndipo utagundua kuwa kila mtu hufa kwa siku yake…sasa kwanini umejiondoa hii mipira kwa namna ambayo sivyo inatakiwa iwe hivyo, ni nani kafanya kazi hii?’ akauliza Docta.

Pale kitandani alikuwa kakaa Maua na pembenii yake alijiegemeza yule mtu ambaye wote walijua hayupo dunia, na mkononi Maua alishika gilasi ya maji ambayo ilionyesha ilishatumika, je ni muda gani haya yote yalifanyika, kumuondoa yule mgonjwa ile mipira na Maua kuchuku maji na kumnyishwa mgonjwa, ikawa ni swali la kila mmojawapo, na kabla mshangao wao haujaisha mara wakasikia sauti ya mgonjwa ikisema;

‘Hivi wewe docta mna malengo gani na mimi mlitaka kuniua na hii mipira yenu, au nini…?’ akalalamika mgonjwa.

Docta akamwangalia kwa makini, huku akitabasamu, akageuka kuwaangalia wanafamilia ambao wote walikuwa na sura za furaha isiyomithilika, na bila ya kumgeukia mgonjwa akasema;

‘Tulitaka kukuua au tulikuwa tunakusaidia , hujui kwa muda mrefu ulikuwa ukiishi kwa kutumia msaada wa hii mipira na hewa inayotoka kwenye huo mtungi, …au una maana gani kusema tulitka kukuua..? akauliza docta.

‘Hii mipira yenu ,mliyokuwa mumenitumbukiza mdomoni na puani ilikuwa inaniumiza sana na koo lilikauka na kiu ya maji ilikua haielezeki, kuna muda nilizindukana na kuiondolea mbali hiyo mipira yenu….’akasema huyo mgonjwa.

‘Pole sana, …’ndicho alichoweza kusema docta huku akijaribu kumpima huku na kule kuhakikisha kuwa mambo yapo safi.

‘Sasa unaendeleaje..?’ akauliza docta

‘Sijambo kabisa , najiona kama nimezalwa leo, hakuna maumivu kabisa, mnaweza hata kuniruhusu nirudi nyumbani….,’akasema na kuwafanya wanafamilia wote kucheka kwa furaha.
Mgonjwa akabakia kushangaa, akawatizama wote huku akijiuliza kwanini wanamcheka, na alipoona wote wametulia wakimwangalia, akasema;

‘Hivi hamjaamini kuwa nimepona, mnaniona bado mahututi, au mlishaniandika kwenye kitabu cha marehemu watarajiwa, …sote ni marehemu watarajiwa, au sio. Au ni kweli kama nilivyoota kwenye hizo ndoto nyingi, hata nyingine sizikumbuki vyema, hivi kwanza niwaulize, maana nimemuuliza mhusika mwenyewe hataki kunijibu, sijawa na uhakika kuwa ilikuwa ni ndoto au hayo mambo yametokea kweli, kwanza kabisa nataka kujua kuwa kweli mke wangu kaolewa na …….’ Hapo akageuka kumwangalia Maua halafu akamwangalia Rose.

‘Mbona mambo yanaonekana kama ilikuwa sio ndoto, yupi ni mke wanu kati yenu wawili…?’ akauliza Mgonjwa.

‘Tukuulize wewe, maana unaona halafu usimjue mke wako, bahatisha , ukikosa umemkosa, au tunakutoza faini…?’ akasema Docta akiwa na yeye hana uhakika ni nani kati ya hawo wawili ni mke wa huyo mgonjwa.

‘Sasa inakuwa kama nilivyoota kwenye hiyo ndoto, na inanitiaa wasiwasi, maana kama kweli mke wangu kaolewa, basi haina haja ya mimi kupona,, nitunduke hayo mapira, nataka kurudi huko nilipokuwa, maana mke wangu nampenda, na sioni sababu ya yeye kuolewa na mtu mwingine, kwani imepita muda gani tangu haya mauza uza yatokee, na mimi nina tatizo gani, hadi….’akapitisha mkono nakushika yale mabandeji aliyofungwa kichwani.

‘Usiyaondoe bado kabisa kuondolewa hayo mabandeji, na naona upumzik kidogo, usijilazimishe kuongea na kukumbuka saana…’akasema Docta.

‘Kukumbuka kupi tena docta, mimi hapa nakumbuka kila kitu, ispokuwa hayo yaliyotokea baada ya hiyo ajali ya meli, nakumbuka wakati naruka toka ndani ya meli hadi kwenye maji, tulipoona meli inazama, niligonga kichwa kwenye machuma ya hiyo meli, na kichwa kiliniuma sana, na tangia hapo, hakikuacha hadi aple nilipopoteza fahamu, na tangu hapo mengine yote yaliyotokea …siyajui vyema, ndio nayaona kama ndoto…’akaeuka kuwaangalia tena Rose na Maua.

‘Kwenye ndoto nakumbuka, kulikuwa na docta, mmmh,…’akawaangalia kwa makini Maua na Rose, halafu akauliza ; `Kitu cha ajabu kwenye hiyo ndoto, nilishangaa kumuona mke wangu akiwa dakitari, wakati sikumbuki yeye kusoema huo udakitari, na sasa …nimegundua kitu , ina maana mke wangu ulikuwa na pacha mwenzako, ….ndio …nimegundua, huyo pacha mwenzako ni dakitari, au sio…anaitwa nani vile….’akageuka kitandani kama anajinyosha,

‘Ndio anaitwa docta Rose,..mmh, nakushukuru sana, kama hiyo sio ndoto , ni kweli, basi wewe ndiye uliyebeba dhamana na masiha yangu nikiwa katika kipindi hicho kigumu, sijui nitakulipa nini, munu mwenyewe ndiye anayejua, kama sio ndoto, basi mungu ndiye ajuaye nini ninachowaza moyoni…kama sio ndoto, hebu niambieni ni nani kati yenu anaitwa Rose..?’ akageuka kuwaangalia kwa makini, lakini wote walibakia kimiya.

‘Kama mnataka nibahatishe kama nilivyobahatisha kweney hiyo ndoto, sitafanya hivyo tena, maana nilikosea, na matokea yake huyo mtabiri aliniambia jambo ambalo sitalisahau maishani,….kama ni kweli, sijui, nitaishije, kama ni kweli, sijui…nitaishije….’akawa aanyarudia yale maneno mpaka wote wakashituka, lakini docta alijua ni kwasababu gani, na akamsogeela mgonjwa na kumshika kichwani na akasema;

‘Sasa anahitaji upumzika, akizindukana tena, muwe na majibu sahihi ya kumjibu, haina haja ya kumtesa kufikiri sana, kwani sasa akili yake ipo safi, ila mengi yaliyotokea kipindi akiwa hana kumbukumbu ndiyo yatakuwa yakimsumbua kidogo, ….kwahiyo msitie shaka, cha muhimu ni kutomshinikiza katika kufikiri sana.Na ni vyema mkampa muda , msimjalie wote kwa pamoja….’akasema docta na kumsogelea Rose.

‘Nashukuru sana Docta Rose , kweli wewe ulibeba dhamana ya huyu mgonjwa, na nina mengi ya kukuuliza, na huenda mojawapo litakuwa hilo alilokuuliza mgonjwa, ni wewe mke wake au ni huyo mwenzake, ..lakini tutaongea baadaye…’akasema Docta na kugeuka kuondoka. Lakini aipofika mebela akaeuka na kusema;

‘Kuna watu wa usalama wanataka kuongea na wewe Docta Rose, kama upo tayari nakuomba ofisini kwangu, ...'akasema yule Docta huku kaweka mikono mfukoni, na kutoa tabasamu, huku akiiniwa nfsi yake ikiwa imezama kweney hisia za kumpenda huyu binti, na akilini aliomba kama ni kumpata mke ampate mke kama huyu.

Rose akaeuka kuangalia kitandani, baada ya kumuona huyo Docta akimwangalia kwa muda bila kuendelea kusema neno, na kabla hajasema kitu yule docta akageuka kuwaangalia wale wazazi, akiona aibu kuwa huenda wamehisi kitu, akamgeukia tena Rose na kusema;

'Watu wa usalama wapo wanakusubiri...kama hutajali tuongozane ukaonane nao, hakuna jipya, ila ni mambo ya usalama, labda pia wana yo ya kukuuliza....'akasema halafu akawageukia wale akina mama bila kumwangalia Maua ambaye aikuwa bado kamwiinamia mgonjwa, huenda alikuwa kazama kwenye maombi....docta akasema kwa sauti ya utawala, huku akiwa kaangalia upande ambao una viti vya kupumzikia madakitari ;

'Na ndugu zangu wengine tafadhali mkasubiri pale, msimzunguke sana huyo mgonjwa, ningeliwatoa nje, lakini najua jinsi gani mlivyo na hamu ya kumuona mgonjwa wenu, hana matatizo kwa sasa, akizindukana mtaongea naye mpendavyo…’akasema na kuanza kuondoka.

‘Rose watu wa usalama wanakutakai nini…?’ akauliza mama mtu.

‘Sijui, na wala sitaki kujua zaidi, nitajua nikikutana na wao, sina wasiwasi, wasiwasi wangu ulikuwa usalama wa huyu mgonjwa, na ndicho kinachonifanya nisikae mbali nayeye…lakini ngoja nikawaone hawo wanaojiita watu wa usalama, …..nawaomba msiondoke mkamuacha huyu mgonjwa peke yake, nikirudi tuna mengi ya kuongea, hasa...mengi kuhusu monjwa na ndugu yangu….’akasema na kugeuka kumfuata docta.

‘Kweli yapo mengi yakuongea….’akasema shangazi na kumeukia mama mtu, ambaye muda mwingi alikwua kainama, na kabla hajasema kitu simu yake ikaita, akaangalia mpigaji, na kuwageukia wengine , akitaka kuipokea pale , lakini alikumbuka kuwa hawaruhusiwi kupokea simu humo ndani, akaitizama tena ikiendelea kuita, akataka kuikata, hakutaka kuondoka mle ndani, ….akaitizama ile simu ikiendelea kuita…


NB: Sikupenda niishie hapa katika sehemu hii, kwani mambo yapo mengi yakuandika, lakini wakati ukuta. Ama kwa wazo la leo, ni kuwa: Baada ya dhiki tarajia faraja, kwani mchumia juani hulia kivulini, …hangaika na kutafuta maisha, kwani tumeambiwa, fanya kazi, jibidishe na kutafuta maisha kama vile utaishi milele, lakini usisahau kumkumbuka mola wako, na unapomuelekea yeye muombe sana, kama vile ndio saa yako ya mwisho ya kuishi…Tupo pamoja

Ni mimi: emu-three

5 comments :

Pam said...

Nimefarijika saaaana mgonjwa kuzinduka..

Simon Kitururu said...

@M# Nipo ila niko nyuma kidogo sijafika hapa bado na siharibbu mfululizo! Ila nakustua tu kuwa nnipo ukurasani!

Pamoja Sana!

Subira said...

Hii imetosha kwa leo umetuburudisha sana. Vipi mambo yako mengine yanaendeleaje? Kama bado nikupe dozi kubwa na inayofanya kazi fasta. Nijibu hapa halafu hiyo dozi ntakutumia kwa email maana naogopa watu wanaweza kuitumia vibaya.

Subira

emuthree said...

Pam na mkuu tupo pamoja. Subira mambo bado nahitaji sana hiyo dozi

Rachel Siwa said...

Kwanza nampongeza dokta Adam hakugoma,Ndugu wa mimi maneno yako ni ya kweli Mchumia juani........Mungu yu pamoja,Ndimi nduguyo Mpendwa Rachel,Pamoja ndugu wa mimi!!!!!