Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Tuesday, January 31, 2012

Akufaaye kwa dhiki ndiye rafiki wa kweli-77 hitimisho-21




‘Doctor Rose…mmh, tunafurahi sana kukutana na wewe kwani nyie madaktari ni watu muhimu sana, na ni watu tunaowahitaji sana kule kwetu, mimi ni muwakilishi wa nchi yangu hapa India, na kukutana na wewe ni kama nimekutana na ndugu yangu,…’akanyosha mkono kumsalimia Rose na Rose akaupokea mkono wa shangazi na akatambulishwa kwa wengine na kusalimiana nao.

Yule jamaa aliyeonekana kama msemaje mkuu akaendelea kuongea na kusema `Kwani tukiwa huku nchi za nje tukikutana watu wa nchi moja ni sawa na kukutana wanandugu mliozaliwa na baba na mama mmoja au sio…’yule jamaa alianzia mbali, na hakujua kuwa kwa kufanya hivyo, alikuwa akimkera Rose, Kwa Rose alijua ni maongezi madogo tu, lakini alivyoona lile jopo la watu akajua hapo kuna muda mrefu utatumika nay eye hakuhitaji muda mwingi alikuwa na hamu ya kukaa na mgonjwa, amuone kwa macho yake akifunua macho amtizame, …..

Alipowaza hilo, akakumbuka jinzi alipoonana na huyo mgonjwa kwa mara ya kwanza, ilikuwa hivyo hivyo akiwa kazimia, alipofunua macho wakaangaliana , kuna hisia zilijijenga tangu siku hiyo, hisia ambazo kwakwe yeye aliziona kama chanzo cha mabadiliko katika maisha yake. Lakini alipoundua kuwa huyo alikuwa ni mume wa ndugu yake, aliona kama ndoto yake imepotea kabisa, ….hata hivyo mazungumzo aliyosikia kwa huyo mgonjwa yamemchanganya kichwa. Na hilo alilitaka kulijua haraka iwezekanavyo, sasa anaitwa tena huku na hawa watu, wangelijua kuwa hawana umuhimu kwake…..

‘Sasa Rose, Dakita Rose, kuna jambo muhimu sana tumekuitia hapa, sisi ni watu wa usalama, kazi yetu kubwa ni jukumu mlilotupa….’ Yule mtu akaawa anaongea lakini kwa Maua mawazo yalikuwa mbali, hata hivyo alijitahidi kumsikiliza.

‘Na tunafanya hili tukijali kodi zenu ambazo zinatoka kwenye mishahara yenu, lakini hata hivyo, hili jukumu ni letu sote,mimi na wewe, siwezi kufanya hii kazi kama sitapata msaada wako wewe na raia wema wengine, …bila msaada toka kwa raia wema, katu hatutaweza kufanikiwa katika kazi zetu…’akatulai kidogo na kumwangalia Rose kwa makini. Rose akajitahidi kumwangalia machoni, lakini baadaye akaangalia chini.

‘Docta Rose, hili nataka ulielewe kwa makini…’akasema na kuwageukiwa wenzake ambao walitingisha kichwa kumkubalia.

‘Unaona….’akasema na kumeukia yule dakitari mwingine aliyekuja na Rose na kumeukia Rose tena. Sisi watu wa serikalini, tunajivunia hasa tukifika nchi za wenzetu tukawakuta watu kama nyie,….tuna bahati sana, ndani ya nchi ya India tuna madakitari wetu mabingwa, wanafanya kazi kubwa sana….’akatabasamu na kuwaangalia wenzake huku akiendeela kuongea kwa kusema;

'Kwanini hawa watu wetu wasingelifanyai kazi hizo ndani ya nchi zetu, kwanini wewe Rose, usingelisomea ndani ya nchi yako , kweli hatuna vyuo vinavyotoa hayo masomo….?’ Akawa kama anamuuliza Rose, lakini hakuwa anamwangalia yeye akasema;

`Inafikia hatua watu wetu wanakimbilia nchi za nje…wanatafuta nini, elimiu, maslahi bora au kuna jambo jingine….ndio huenda ni maslahi duni, lakini sizani kuwa ni hilo tu peke yake…’akaeuka na kuwaangalia wenzake.

‘Kuna jambo kubwa sana ambalo tunatakiwa mimi na wewe na raia yoyote wa nchi yetu tusaidieani, na hili hatutasaidiwa na watu wengine hatutasaidiwa na India au Marekani au Ulaya, kwanza tunatakiwa kujisaidia wenyewe. ….’akatulia kidogo na kukohoa kama vile anarizika na kile anachokionea kuwa kaongea jambo ambalo ni muhimu sana.

‘Sikatai kusaidiwa n hilo hata Marekani au Ulaya wanasaidiwa, lakini tutaweza kusaidiwa endapo na sisi wenyewe tumejisaidia, na hili ni muhimu sana kwako wewe, na vizazi vijavyo…na hili ndilo tulilokuitia hapa, kuwa bila wewe, bila raia wema ndani ya nchi yetu hatuweza kufanikiwa kwa lolote lile, tutaishia kukimbilia kwa wenzetu na mwisho wa siku tutasutwa, tutachekwa , na hata kusimangwa na wenzetu,…’akaonyesha uso wa huzuni na kuwageukiwa wenzake huku akisema;

‘Hamjasikia watu wanapigwa vita na raia wa nchi wanapoishi, vijana wao hawana ajira wanaona raia wageni wanakwenda kufanya kazi katika nchi zao…..kwanini …’akamgeukia Rose na kumkazia macho. Rose akaangalia saa na kubetua mdomo, na alipoona huyo mtu anamwangalia yeye akamkazia macho na yeye kujifanya anamsikiliza kwa makini.

‘Najua wewe kama mtaalamu utaona nakupotezea muda, wewe kwako sasa hivi unafikiria wagonjwa, hapo ulipo unamfikiria mgonjwa wako, lakini na hili ninalotaka kukuambia hapa ni muhimu sana, lakini huenda hutaweza kulielewa kwa hivi sasa na kama nisipokupa mifano hai hutaweza kulielewa kabisa, na ndio maana nakuanzia mbali kwa mifani hai…’akawageukiwa wenzake na kusema;

‘Unajua siasa ni muhimu, ili kuzijenga nyoyo za hawa vijana, hawaelewi hilo , wao wamekongwa na tekinolojia, na nyenzo za kuwarahishia maisha, matokea yake wanapupika, kunakosekana hekima,…siasa ni hekima, hekima ya kumjenga mtu awe na subira , hekima za kujenga uzalendo, bila uazalendo hamtaweza kuzijenga nchi zenu….’akasema yule mtu. Wenzake wakatikisha vichwa kumkubalia na kama isingelikuwa ni hospitalini wangelimpigia makofi.

‘Sasa Rose, jambo kubwa ambalo wengi wanashindwa kulielewa na ambalo sasa ni donda ndugu katika nchi zetu za Afrika. Na watu wetu wanashindwa kuelewa kuwa hata hawo wenzetu wanapenda hiyo hali iwepo, wakiuma na kupuliza, ili wauze silaha, ili wapate ajira, ili wataalamu kama nyie mkimbilie kwao,…donda ndugu hili tunalisababisha wenyewe, ….kwasababu hatutaki kuelewa, hatuna muda wa kusubiri wakati wa shida, hatuna hekima, mioyo yetu imegubikwa na chuki za kibinafsi…tunachotaka ni tiba, badala ya kinga…, na bora ya kinga kuliko tiba, au sio docta…’akasema na kumgeukia Rose huku akwia akmkazia macho.

‘Saamhani, lakini…’Rose akaanza kulalamika.

‘Najau , najua Rose, unaona nakupotezea muda wako, lakini haya ninayokuambia hapa sio yako tu, hayataishai hapa kwako wewe tu, ni kwa ajili yako na wengine, ipo siku ujumbe huu ninaoutoa hivi leo utawafikia wenzako kuwa nilikuwambia hili, …unajua donda ndugu hilo ni gonjwa gani…?’ akamgeukia Rose na kumwangalia kwa makini.

‘Mmmm, wewe ni docta, huenda unafikiria nini nakizungumzia, gonjwa hili halihitaji mavyombo yenu, lakini cha muhimu ni kujua gonjwa hili ni gonjwa gani, ni kinyume cha amani. Ugonjwa wa kutokuwa na amani katika nchi unachangia kwa kiasi kikubwa sana kurudisha mendeleo yetu nyuma, badala kufikiri kutengeneza miuno mbinu, mnafikiria kununua silaha, kujenga maghala, kukodisha maaskari, na mambo mengi ambayo kama amani ingelikwepo, …tusingeliwaza hayo…’akasema na kuwageukiwa wenzake.

‘Amani haipotei tu kwa kupigana, amani pia hupotea kama nafsi hazijatulia….maisha magumu, maadui ujinga na maradhi, umasikini uliokithiri….vyote hivyo ni chanzo cha kuvurugika kwa amani…’akatulia na kuwaangalia wenzake kwa makini, halafu aaksema;

‘Kuna tatizo la uongozi, hasa atika nchi zetu, tatizo hili ni la kubeza nguvu kazi, serikali nguvu kazi yake ni raia wake, kama raia wana njaa, raia ni wagonjwa, raia hawapati huduma muhimu, unafanya nini kwenye hayo madaraka, achia ngazi, umeshindwa…kwasababu mtu ni kama gari, gari kama halina mafuta haliwezi kwenda, mtu bil achakula ataweza kufanay akzi kweli, hawezi, ndivyo ilivyo katika serkali, katika mashirika yetu, makampuni,kama hawatawajali wafanyakaz wao, wakawa na afya wasitarajie miujiza…’akawageukia wenzake kulia na kushoto.

‘Usione watu wanaingai misituni, wao sio wajinga, ….hilo inabidi viongozi wakae watafakari, kwanini, tuskimbiulie kusema wanaofanya hivyo wana uchu wa madaraka, hapana, tuangalie chanzo ni nini, utagundua hilo, kuwa hakuna amani katika mioyo ya watu,…ukiangalia kwa makini utagundua kuwa ni njaa, maradhi na haki isiyo sawa,…hakuna kingine….chunguzeni hilo, nawaambia….’akasema na kutulia tena halafu akamgeukia Rose na kusema;

‘Nazungumza hili kwasababu nyie watendaji ndio mihimili muhimu , ni watendaji lakini mtakuwa na madaraka maofisini mwenu, uwe dakitari, lakini kutakuwa na dakitari kiongozi, ..walimu, lakini kutakuwa na walimu viongozi, nakadhalika, kama kiongozi unatakiwa ueelwe hilo, kuwa unaowaongoza, sio watumwa, ni watu , na watu kama wewe, ….kama unatembeela gari na wao wanahitaji pia, kama unakual vizuri na wao wanahitaji kula vizuri, ….na kama watoto wako wanasoma shule za kimataifa,kwanini usiwasaidie na wafanyakazi wako, watoto wao wakasoma angalau shule za kati na kati na kati….ubinafasi unaanzia hapo, umimi, na kujenga matabaka…’akaonyeshea kwa mikono .

‘Kwahiyo viongoz wanatakiwa walielewe hilo, na wewe raia mwema , mtaalamu uwajibike katika sehemu yako ili hayo yasiwepo, kwa kufanya hivyo utakuwa umeijenga amani…na ili kufanikiwa hilo, tunatakiwa tuwe kitu kimoja, tuwe raia wema, tuwe wazalendo, ili hapa kukiharibika, tuwe pamoja kupajenga , kwani nalawa yetu ni moja, …kukiwa na matundu tutazama sote…hilo ni muhimu kulijua, sio kwa vile wewe ni kiongozi au raia wa kawaida hutohusika,…hapana.’akasema na kwa msisitizo huku akimwangalia yule docta mwingine, ambaye alikuwa akipitia majalada mbali mbali na kuyatengeansiha katika mafungu mawili.

Yule jamaa alipomuona yule docta mwingine hamuangalii akamgeukia Rose na kusema;

‘Sasa Rose, amani hujengwa na mimi na wewe, bila wewe kazi yangu haitaweza kukamilika, nakuomba tushirikiane kwa hili, hapa namkabidhi mwenzangu mtaalamu wa mambo hayo aendelee,… samahani kwa kukupooteze muda wako, muda wenu, ila mimi ni mtu wa usalama, lakini katika kitengo cha siasa na utawala bora, ndio maana nikawa muongeaji sana, lakini ni kwa manufaa yako, …ngoja mwenzangu akuhoji halafu kama una swali, utaniuliza, hasa kwanini nikakuambia haya yote…’akawa aanongea kwa haraka kama vile anataka kuondoka kuwahi jambo fulani, lakini badala ya kuondoka akamgeukia mwenzake na kuinama kidogo kama kumkaribisha.

Rose akachoka, maana alijua huyo atamaliza kila kitu, kumbe ndio kazi imeanza, akatulia na kumwangalia kwa makini huyo mtu mwingine aliyekaribishwa, hata ukimwangali huyo mtu mwingine alivyojengeka, utakua tu kuwa huyo ni askari….akatulia na kusubiri nini ataulizwa, au ni siasa kama za huyo aliyepita, akasubiri…

‘Shukurani mkuu wangu, hayo ni mambo ya kisiasa, sasa hapa kwangu ni utendaji mtupu, nakuomba Rose uwe huru, na ujisikie kuwa upo na ndugu zako, na lengo letu ni moja, kuleta amani ndani ya nchi yetu, najua wengi mnataka hata kuikimbia nchi yenu kwasababu ya uzaifu huo, sisi tupo bega kwa bega na nyie tumeapa kuilinda nchi yetu, hatutakuwa wasaliti wa nchi yetu , sisi ni wapiganaji kama ulivyo wewe…’akasema huku anafungua jarida lililopo mbele yake.

‘Unajua wewe Rose ni mpiganaji mwenzetu, nafikiri unalijua hilo,….’akatulia kidoo bila kumwangalai Rose, akiwa anaangalai ukurasa ndani ya lile jarida, na kabala Rose hajasema kitu akasema;

‘Rose sasa nitakuuliza maswali machache naomba uyajibu kwa ukweli wa dhati na ukiwa huru na ukijua haya ni kwa ajili ya kulimaliza hilo tatizo ambalo mkuu wetu kaliita donda ndugu, ni tatizo kubwa , lakini ni dogo kama tukishirikiana, …mimi nikiwa an dhima ya dhamana niliyopewa ya kuilinda na kuitetea nci yetu, ….dhima hiyo kakabidhiwa kila mtu, au sio…..? ’akasema huyo mtu mwingine sasa akimwangalai Rose usoni.

Rose alipona kaangaliwa sana usoni, akajua hapo anatakiwa kujibu kitu, akasema kwa sauti ya kuchoka;

‘Sawa Mkuu, nitajibu kama ninavyojua, na kwa kadri ya ufahamu wangu,….’akasema Rose na kugeuka kumwangali yule dakitari ambaye naye alishajichokea kwani hawakuzoe hali ya kukaa na kuongea tu, wamezoea kukimbizana huku na huko kuwahudumia wagonjwa….

‘Rose unamfahamu Docta Adamu..?’ swali lilikuja haraka bila kutegemea kuwa muulizaji angeuliza swali kama hilo mapema hivyo, na liliulizwa kama mahakamani, na kichwani kwa Rose, akawa anawaza mengi, kuhusiana na hilo swali, je huyo docta Adam kakamatwa au amekufa, na vyovyote iwavyo kwanini wamuulize yeye hilo swali….akatulia kidogo halafu akaona haina haja ya kupoteza muda kwa kuuliza swali kwenye swali.

‘Ndio namfahamu….’akasema Rose akijua swali gani litafuta baadaye.

‘Hebu tusaidie ufafanuzi, unamfahamu kivipi,….?’akauliza huyo mtu wa usalama, na kwa vile Rose alishajua kuwa hilo swali litafuata, akaona ajibu kwa sasa kwa ufafanuzi ili kuondoa mlolongo wa maswali mengine baadaye.

‘Namfahamu kwasababu alikuwa bosi wangu katika hospitali niliyokuwa nikifanyia, na kwa nje tulikuwa marafiki wa kawaida, sio urafiki wa kipenzi, hapana, ni marafiki waliozoeana kwasababau ya kuwa pamoja katika shughuli za utendaji na kwahiyo ilifiki ahatua tukawa tunasaidiana katika hili na lile…ndivyo ninavyoweza kusema hivyo…’akasema Rose.

‘Sawa kabisa umejibu vyema, je katika mazoea yenu, ulimuonaje docta huyo , hakuwa na mambo mengine ya ziada nje ya kazi yake, nakuuliza hili kwa haraka ili tusikupotezee muda, na wewe tujibu kwa ufafanuzi kwa kadri unavyojua, ili tusaidieni kwa hili, ni muhimu sana kwetu, na kwa taifa lako na vizazi vya nchi yetu, sizani kuna mzazi au raia yoyote anayeifurahia hiyo hali, kwanini tusiishi kwa amani, eti Rose….’kabla hajasema zaidi simu ikaita, na jamaa akaipokea na kusema;

‘Saamhani kidogo Rose, huyu mtu ni muhimu sana, ….anahusiaa na hili, ..’akaipokea ile simu na kusikiliza kwa muda, halafu akamgeukia Rose, na kusema;

‘Natumai unamfahamu Inspekta yule wa nchi jirani, anataka kuongea na wewe kidogo….’akamkabidhi Rose ile simu, na Rose kwanza akasita kuipokea, na baadaye aaknyosha mkono na kuipokea kwa mashaka kidogo , halafu akaiweka sikioni kama vile hataki kuisikia hiyo sauti, na kuanza kuisikiliza hakusema halooh, akatuia kusikiliza kwani muongeaji alikuwa keshaanza kuongea jambo….

‘Rose, mimi ni Inspekta, nimekupigia hii simu kupitia hawo jamaa zenu wa usalama, hawo nilikuwa nikifanya kazi nao kwa karibu sana, ni watu wa kuaminika,…natumia neno wa kuaminika, kwani kama unavyoelewa ilifikia hatua hatujui nani umwamini na nani usimwamini, lakini kwa hali ilivyo sasa, mambo yanakwenda vyema, nakuomba sana, wape ushirikiano wako,…’akatulia muongeaji kwenye simu kidogo.

‘Sawa inspekta, lakini, mimi sijui lolote zaidi ya …..’akaanza kujitetea Rose.

‘Hicho hicho kidogo unachokijua, unavyohisi, na ulivyomuona, …. waambie wao ni wataalamu wa ammbo hayo, nakuambia hivyo kwasababu tumegundua kuwa Docta Adam, yupo nyuma ya mambo mengi yaliyotokea hasa kuhusiana na mgonjwa na pia anakuandama sana wewe kwa namana ambayo mwanzoni tulifikiria ni mapenzi …lakini tunahisi ni zaidi ya mapenzi, kwahiyo kwa usalama wa mgonjwa wenu, na usalama wako, na usalaam wa taifa lenu, toa ushirikiana kwa kila watakachokuuliza….sawa Rose…?’ akauliza huyo Inspekta.

‘Sawa, nitatoa …lakini kama nilivyokuambia, sina zaidi ya jinsi watu wanavyofikiria, mipaka yangu ilikuwa kwenye kazi tu….’akasema Rose na kutulia huku akiwajaribu kuwaangalia wale watu waliopo mle ndani, na alipogeuza macho yake pembeni akagundua kuwa kumbe kulikuwa na mashine ya kunasia sauti, ina maana kila wanachokiongea kinanakiliwa kwenye hiyo mashine.

‘Rose nikuambie jambo moja, katika uzoefu wangu, vita uhasama na chuki, kulipiziana visasi havijengi kamwe, nimewashauri wenzangu hawo, kuwa hata wakiwashika hawo watu, wawe na baraza la mariziano, ni vyema hata ujumbe ukamfikia huyoo Docta Adamu, kuwa suluhu, ipo, ajitokeze watu wariziane, kama anataka kujiuna kweney vyama vya siasa, kama ana dukuduku,basi watu wake yaishe, amani ni muhimu sana katika mataifa yetu haya….’akasema muongeaji kweney simu.

‘Nimekuelewa sana Inspekta…..’ akajibu Rose, huku akijiskia vibaya, kwani midume yote iliyokuwemo humo ndani ilishaanza kumchefua…akamkabidhi huyo mtu wa usalama ile simu ambaye aliendela kuongea kidogo na huyo mpigaji simu, halafu akairudisha ile simu kwenye mfuko wake na kumgeukia Rose.

‘Huyu jamaa ametusaidia sana, na hivi tunavyoongea yupo nchini kwetu, anamalizia baadhi ya kazi, na ndio maana akaamua kukupigia, naomba tuendelee na mahojiano yetu, ni maswali machache tu , tukimaliza hapa tutajua nini la kufanya….wewe ongea kile unachokifahamu, hatukulazimishi kwa jambo ambalo unaoana litakukwaza, lakini angalia faida na hasaar yake, …..’akasema yule mkuu na Rose akainamisha kichwa kuashiria kuwa hajisikii vyema, na mwenzake ambaye ni dakitari akaligundua hilo akamsogelea na kumgusa Rose begani…

‘Upo safi, kama hujisikii vyema sema, nakuona kama … sema, tuahirishe kidogo, usiwe na wasiwasi kuhusu mgonjwa, sasa hivi nimepata habari kuwa kazindukana nimemtuma msaidizi wangu akahakikishe mambo yanakwenda vyema, maana siwezi kuondoka hapa bila kuhaikisha kuwa hawa watu hawakusumbui….mgonjwa anaonega na familia yenu, usihofu kwa hilo…’maneno yale yalimuongezea nguvu Rose, akaanza kujisikia vyema, na kumpandisha hamasa Rose na hapo akaanza kuongea kila kitu anachokijua kuhusu dakitari Adam.

*********

‘Hivi mbona Rose amekawia kurudi….?’ Akauliza Maua.

‘Kwani amekwenda wapi…au ndio kaamua kuingilia kazi, maana hawa watu wanaopenda kazi zao, wanaweza wakajitolea popote pale, huenda kweli yupo kwenye kazi ya kuangalia wagonjwa…?’ akauliza shangazi kwa utani.

‘Aaangalie wagonjwa kwani hapa hospitali kwake, yote aliyofanya hapa haikuruhusiwa alitoa kama msaada tu…’akasema Maua.

‘Sasa kama isingelikuwa yeye huoni wenzake walishakata tamaa…’akasema shangazi.

‘Tatizo hapa wana wagonjwa wengi, kwahiyo docta anahitajika kumhudumia huyu na akiona kazi yake kamaliza anataka amfuate mwingine, na hivi vipimo wakati mwingine wasivitegemee sana, mimi inanitia wasiwasi , kama ndio hivyo, watamuua mgonjwa kabla sio siku zake, maana watatoa kila kitu, kumbe bado alihitaji muda….’akasema Maua

‘Hiyo kama ni kutokea ni mara moja kwa bahati…na kama mtu kandikiwa kufa atakufa tu, kama sio siku zake, itatokea kama ilivyotokea hapa….’akasema shangazi.

Mara mama akarudi, alionyesha uso wa wasiwasi kidogo, na alipofika pale waliposimama wenzake, akawa kama anawakwepa wasimuuliza maswali, na kukimbilia kumtizaam monjwa pale alipolala, akainama karibuna uso wa mgonjwa kama kazindukana, alipoinama kumtizama machoni, akainua kichwa haraka na kumgusa wifi yake kwenye bega;

‘Wifi hivi Rose hajarudi anafanya nini wakati wote huko, mimi nahisi kama magonjwa keshazindukana , ukimtizama machoni ingawaje kayafumba, lakini yanaonekana kucheza cheza, hebu tumuuiteni ajae amtizame,….’akasema mama.

‘Si aliitwa kwa hao watu wa usalama, isije ikawa yamegeuka ya usalama na kuwa mengine..naona hata yule dakitari alikuwa akimwangalia Rose kwa jicho la kimahaba, naingiwa na wasiwasi sasa….’akasema shangazi kwa utani.

Mama ambaye ndio alikiuwa karudi huko alikokuwa katoka kusikiliza simu yake baada ya kupigiwa na kuamua kwenda kuipokelea nje ya hiyo wodi maalumu, kwani haparuhusiwi kupokea simu humo ndani akakunja uso kuonyesha hakupendezewa na hayo maneno aliyozungumza wifi yake akasema;

‘Huyo docta kama alimwangalia kwa macho ya mahaba kachelewa, kama ni macho ya mahaba akawatizame manesi wake, mbona nimeona wasichana wengi warembo humu ndani tu, ….nafikiri kuna jambo huko, inabidi tutafiti kuna nini….’akasema mama.

‘Tutatafiti kwa vipi unajua wapi hiyo ofisi ilipo, basi fuatilia….’akasema Maua huku akimwangalia Mgonjwa .

‘Kwanza tuambie hiyo simu uliyokuwa ukiisikiliza ina heri maana ulivyokuja ulionyesha kuwa na wasiwasi sana…?’ akauliza Shangazi.

’Sijui kama kuna heri au la…, ila nahisi kuna jambo, ….mmh, ndio mume wangu alikuwa akinifahamisha kuwa keshafika, na ameniagiza nimalizie baadhi ya kazi alizokuwa kaziacha, ili zikikamila nirudi na mzigo, maana yeye hatapata muda wa kurudi huku kwa sasa , …na atanipa maelekezo mengine baadaye, kwahiyo nihitajika kuondoka …nasubiri huyu mgonjwa azindukane tu, nikawajaibike, …..yeye hakusema zaidi kuhusu kuwa kuna tatizo huko, ila sauti yake iliashiria kuwa kuna tatizo…’akasema mama.

‘Kwanini usimuulize kuwa kuna tatizo….?’ Akauliza Maua ambaye alionekana kuvutiwa na hayo mazungumzo ya mama yake.

‘Wewe unanioje mimi, unaniona kuwa na akili za kitoto,…’akacheka kwa kebehi halafu akasema;

‘Nilimuuliza ndio, na aunajua nini alichokisema; ‘hakuna tatizo lolote, wewe fanya niliyokuagiza haya ya huku hayakuhusu…’akasema mama na kugeuka pembeni kama vile anaona aibu kuzungumzia mambo ya mume wake.

‘Mama samahani nikuulize swali moja, hivi kweli mna mahusiano mazuri wewe na huyo baba, maana unavyoongea hapo inaashiria kutokuelewana kwa namna fulani, au nimekosea..?’ akauliza Maua
Mama akacheka tena kwa kebehi , halafu akamgeukia Maua na kumtizama machoni, hakupenda kulijibu hilo swali, na pia hakupenda kumvunja binti yake ambaye hakuwahi kulelewa na yeye, na asingeliepnda amuelewe vibaya, akasema;

‘Mambo ya baba na mama ndivyo yalivyo, leo utaona watu wanaongea vyema na utaishia kusema hawa watu wanpendansa sana, kesho inakuwa vinginevyo, lakini mwisho wa siku itaishia kukubali ukweli kuwa hayo ndio maisha ya ndoa…’akatulia kidogo, akijau hapo hajajibu swali la binti yake, akauka kumwangalai wifi yake, kama vile anaomba msaada, lakini kabla hajatulia vyema akasema;

‘Siwezi kusema hakuna maelewano kati yangu na mume wangu, usiwe na wasiwasi na hilo binti yangu, kuna kushuka na kupnda hayo ni ya kawaida. Binti yangu, wewe ndio umeingia kwenye ndoa…najua ulishaisi na mume wa awali, na sasa ndio umempata mwingine, kama nilivyosikia juu juu, utakutana na maisha kama hayo, na kukitokea migongano, usikate tamaa ukiona unajibiwa vibaya, au unaweza hata uisjibiwe ukiuliza swali, usitaharuki, ndivyo maisha ya ndoa yalivyo….’akasema mama na akakatiza waliposikia sauti ya kuhema ya mgonjwa.

Maua haraka haraharaka akamgeukia mgonjwa na kuinama kumtizama usoni, alipotua macho yake usoni mwa mgonjwa akashituka na kupepesa macho yake, kwani alijikuta macho yake yakiangaliana moja kwa moja na macho ya mgonjwa, ….aakhema kwa nguvu, na hakugeuka au kupepesa macho yake, akaendelea kumwangalia mgonjwa, na kwa muda wakawa watizamana,….

Na hali ile ikamkumbusha siku walipokutana kwa mara ya kwanza, siku walipotupiana jicho katika basi la daladala, akatabasamu na mgonjwa naye akajitahidi kutabasamu….na wakati huo huo mama ambaye naye alishaiona ile hali, akakimbilia nje kumuita docta, …..

NB. Kwa leo inatosha, kama nimeacha sehemu tuambizane, maana ndio tunamaliza maliza. Neno la siku ya leo;Amani ya kweli hujengwa toka nyoyoni, kama ulivyo upendo wa kweli . Hata kama hakuna vita vya silaha, lakini kukiwa na vita vya nafsi, amani itakuwa kama kitendawili….Ni hayo tu wenzangu tupo pamoja.

Ni mimi: emu-three

2 comments :

chib said...

Tupo wote

emuthree said...

Tupo pamoja mkuu Chib, angalau umenitoa kimaso maso.