Hii ni blog maalum kwa kumbukumbu za kimaisha, na matukio yenye mafunzo ndani yake, ndio maana nikaiita 'diary'(shajara). Pia tunakaribisha mijadala yenye kuelimisha

Na kwa kuifanya iweze kuvutia zaidi tunaandika matukio hayo kwa mfumo wa visa, hadithi au tamithilya..

Wewe ukiwa mdau muhimu, unaweza kuchangia na wenzako kwa kutoa hoja (comments). Pia unaweza kutoa maneno ya hekima, utaalamu, au dukuduku lako (kilio chako)kwa jamii ili kuweza kukidhi mahitajio yetu.

MUHIMI, SOMA , CHANGIA, NA TOA kisa chako, au lolote lenye mafunzo ili tuliweke hewani.

TUPO PAMOJA DAIMA


Tushirikiane, Tusaidiane, Tupendane, Tuvumiliane, Tusaidiane, Tusameheane.

Kwa visa motomoto tunapatikana pia kwenye mitandao ya kijamii ya: Facebook, na Twitter, bofya hapa upate visa zaidi;

https://www.facebook.com/emu.three, na kwa ajili ya kuitangaza hii blog, ingia hapa:

https://www.facebook.com/diaryyangu/

`u-like' na pia unaweza kutwitter hapa;

https://twitter.com/emuthree



Sunday, January 15, 2012

Akufaaye kwa dhiki ndiye rafiki wa kweli-74 hitimisho 18



‘Docta nakuomba tafadhali usiviondoe kwanza hivyo vifaa...subiri subiri tafadhali..’akasema Rose huku akimsogela yule docta aliyekuwa akihangaika, kuondoa vile vifaa na kuanza kuviweka sawa, kitendo kile kimlishanagza yule Docta msaidizi na kubakia kumwangalia kwa muda kabla hajasema kitu.

Yule Docta in a bosi hakujua afanyeje kwa tukio lile la haraka, kwani alishapewa amri na bosi wake kuondoa vifaa hivyo mwilini mwa mgonjwa kwani uahi wa huyo mgonjwa ulikuwa haupo tena, akageuka haraka kumwangalia bosi wake ambaye naye alikuwa kashikwa na butwaa, ....

‘Nimeshapewa amri niondoe hivi vifaa na bosi wangu, sasa kwanini unaniingilia nisiviondoe, wewe huoni kuwa hakuna uhai tena hapa ...docta keshaona hilo na kuizinisha, na kila kitu kimeonyesha wazi, wewe unataka kufanya nini zaidi,....!’akasema yule dakitari msaidizi.

Wakati huo docta muhusika alikuwa kama kachanganyikiwa , maana hakutarajia kabisa ile hali kama hiyo itatokea hivyo, kila kitu kilienda sawa, na dalili zote za kupona mgonjwa zilionekana...hakujua tatizo hilo limetokeaje, ...alijuta kwanini alichukua muda kidogo kuja kuona nini kinaendele, hata hivyo hakutarajia tatizo lolote..., alishindwa kabisa kuamini kuwa kazi yake aliyoifanya kwa ufundi mkubwa haikuzaa matunda!

Wakati anawaza haya, alikuwa akitembea mwendo wa taratibu kutoka nje, na huku akisema kimoyomoyo, siku za mgonjwa zilishafika, hakuna jinsi ngoja nikawape taarifa wanandugu...akawa anaondoka huku akisita sita na wakati anafika mlangoni, ndipo akakutana na hawo mabinti wakija mbio mbio, wakampita bila hata kusema neno, na kukimbilia pale alipolazwa huyo mgonjwa, ambaye kwa sasa docta alishamuita maiti....

Alisimama ghafla na baadaye akageuka kuwaangali kwa masikitiko,... na pale aliposikia sauti ya Rose ikisema kuwa wasiondoe yale mashine, akashikwa na butwaam kwanza, akijiuliza kwanini huyu binti anasema hivyo, ndio ni docta, lakini hastahili kuingilia mambo yasiyomuhusu akasubiri aone nini anachotaka kufanya, kwani yeye alishajitoshekeza kabisa kuwa mgonjwa hana uhai tena, kila kitu kilishaonyesha dhahiri kuwa yule mgonjwa alishakata roho, kumwekea mashine ile ni kupoteza muda tu.

‘Sikilizeni, mimi nina uzoefu mkubwa na huyo mgonjwa, sio mara ya kwanza kutokea hivi,nawombeni msubiri kidogo,..hata hivyo nina wasiwasi na jambo moja...’akasema Rose na kusogelea ile mashine ya kusaidia kupumulia na akawa anaichunguza kwa makini, na wakati anafanya hivyo, Maua akamsogela yule mgonjwa na kumshika mkono wake huku akiomba kwa dhati... akisema kimoyomoyo.;

‘Oh, Mhuja, wewe ndiye uliyekuwa mume wangu wa dhati, niliyekupenda kwa dhati, licha ya yote yaliyotokea, lakini moyo wangu hautakusahau kamwe, nakuomba ewe mola, mjalie apone, mjalie ayashinde haya mauti, ili aje nimsimulie kwanini niliamua kuchukua uamuzi ule mgumu wa kufunga ndoa na rafiki yake...oh, mola wangu, nakuomba kwa dhati yako umsaidie huyu mgonjwa apone, kwani nina hisia kuwa bado umri wake wa kuishi upo....oh..ewe mola..’akaendelea kuomba na ni wakati ule docta alipoondoa kile kitu kama kichuma na ndio wakati huo machozi ya Maua yalikuwa yametua kwenye mkono wa mgonjwa, mara...


********

Wakati Maua anaendelea kuomba huku kamshikilia mkono mgonjwa wao, Rose alikuwa na kazi kubwa ya kuchunguza ile mipira iliyokwenda mwilini kwa mgonjwa na mara alipofika sehemu akashituka, aliona kitu kama kichuma kidogo sana, mara nyingi kinatumika kubania karatasi, ilikuwa sio rahisi kukiona kwani kilibandikwa kwa chini na sehemu iliyojificha, ni karibu kabisa na pale mpira huo ulipoanzia,...

Rose akasogeza mkono, lakini akasita, hakujua ni kwanini kichuma kile kiwepo hapo, na kabla hajakivuta akageuka kumwangalia Docta.

‘Unataka kufanya nini...’akasema yule docta huku akimsogelea Rose, kwani alishaona kuna haja ya kuingilia kati, kwani mtu akifikiwa na hali kama hiyo, hata kama ni docta anaweza akapagawa, asiamini ukweli ulivyo.

‘Vipi umeona nini, huyu kama mashine inavyoonyesha hana uhai, hebu angalia mwenyewe kule kwenye mtiririko wa mapigo ya moyo...hakuna uhai kabisa..kila juhudi tumefanya hata kumzindua kwa kumsukuma kwenye mapafu, kifuani, haikusaidia kitu...’akasema yule Docta, huku akimwangalia Rose na macho yake yakafuatilia kule anapoangalia Rose!

Docta macho yake yakatua pale..., naye akakiona kile kichuma, ambacho hakuwahi kukiona kabla, akasogea karibu kuhakiki macho yake, na hapo hapo akasogeza mkono na kukitoa....kilikuwa kimeweka kitaalamu, na rangi yake ilikuwa sawa sawa na mpira, kiasi kwamba usingeliweza kukigundua kwa haraka, kilikuwa kimakata kabisa mawasiliano.

‘Hiki kichuma kakiweka nani hapa, ...unajua hii,....,haiwezekani, ...kuna mtu kakibandika hapa ,....hebu niambieni mlipokuwa humu ndani aliingia docta yoyote, ulisema umeota, au ni kweli aliingia mtu...?’ akauliza yule docta huku akihangaika kuurekebisha ule mpira, hakuwa na haraka ya kuchunguza zaidi kwani ilijua haitasaidia kitu, maji yameshamwagika hayazoeleki..

‘Kwanza hakikisha kile kitu kipo sawa, tutayazungumza hayo baadaye.....’akasema Rose huku akiangalia ule mpira.

‘Haitasaidia kitu, kama ni makosa hayo yameshafanyika, iliyobakia ni kufanya uchunguzi, lakini sioni itamsaidiaje mgonjwa....huyu sasa ni marehemu, wewe ni docta bwana, ...’akasema yule Docta.

‘Nakuomba uhakikishe kila kitu kipo sawa, niamini nisemavyo,....’akasema Rose huku akikagua kila kitu kama kipo sawa, na Docta yule hakukaidi tena, akafanya lile lilowezekana, ili kumrizisha huyo binti, na mra hali ya hewa ikabadilika, hewa iliyokuwa imezuiwa kuingia mwilini ikaonekana kupita na mara mashine ikaanza kutoa mlio, kila mmoja akageuka kuangalia sehemu ile inayoonyesha mapigo ya moyo, ile misitari iliyokuwa imenyooka , taratibu ikaanza kujipinda...

‘Haiwezekani...’akasema yule docta na huku akihangaika kuweka kila kitu sawasawa, hakuamini...namara wakasikia sauti ya Maua kwa mara ya kwanza, kwani yeye alishazama kwenye kumombea mgonjwa...

‘Rose angalia huku, anatingisha mkono....oh, Rose, ndio nini hii, ina maana kazindukana, oh, ahsante munguee...Rose, angalia huku...’ilikuwa sautI ya Maua akiangalia vidole vya mgonjwa vikicheza cheza,....Rose alitaabsamu kidogo, hakusema kitu, aliendeela kuwajibika na mambo yale anayoyaona yanastahili kwa mgonjwa katika hali kama ile, hakujali kuwa pale yeye ni mgeni tu, alifanya yale anayojua ya kumuokoa mgonjwa anapokuwa katika hali kama hiyo, ...

‘Nakushukuru sana Docta Rose, sitakusahau katika maisha yangu, umefanya kazi nzuri sana...’ alisema yule docta huku akimkumbatia Rose,...na wakati anafanya hivyi, zile hisia zake tangu alipomuona kwa mara ya kwanza zilimjia, ...alitamani sana awe karibu na huyu binti, alitamani amtamkie kuwa anampenda na kumhitaji zaidi ya akzi...lakini cha ajabu hata pale alimpojaribu kumkumbatia Rose , rose yeye hakuinua mikono yake, alikuwa katulia kimiya...

Na alipoona kuwa Rose hakuvutika na lile tendo, akamwamchia haraka na kusema samahani, ...hata hivyo Rose mawazo yake hayakuwepo hapo, yeye akilini alikuwa akimuombea huyo mgonjwa, akiombea miujiza zaidi itokee, mgonjwa azindukane haraka...kwa uzoefu wake, hayo yalitokea, na hutokea hata mara tatu, na akizundukana, anazindukana kiukweli...hakukata tamaa. Na yule docta alimuachia Rose na kumsogelea mgonjwa, huku akionyesha uso wa furaha na kusema;

`Huu ni mujiza mmoja mkubwa sana katika kazi yangu hii ya udakitari, haijawahi kutokea hivi, mgonjwa kufikia hatua hii na ....ooh, hili swala lazima lifanyiwe kazi haraka, lazima huyo docta au sijui ni muumiani gani ashikwe haraka iwezakanavyo...’akasema yule docta huku akimalizia yale mambo muhimu yanayohitajika, na baadaye kila kitu kikawa sawa,na aliporidhika na hilo akachukua kile kichuma na kukiweka kwenye karatasi ya nyepesi ya nailoni, kama ushahidi ...akatoka akiwa na nia ya kukipeleka kwa wana usalama na kuwapa wale akina mama taarifa.

Na aliporudi akakagua ile mashine , na akawa kama ana mashaka Fulani, baadaye ile mashine ikawa inaonyesha kuzima tena, ile mistari ikawa inashuka kuonyesha kuwa mapigo ya moyo yanakwisha, Rose akaanza kuichunguza kwa makini ile mikanda kwa uhakika, moja baada ya mwingine, kuanzia mwilini hadi kwenye mashine, hadi kwenye mtungi wa gesi....sasa akawa hajali kuwa hiyo sio kazi yake kwa sasa, alijiona kama ndio yeye docta mhusika mkuu, na huyo ni mgonjwa wake, akawajibika ipasavyo, na mwenzake hakumsemesha naye akawa anahangaika kuangalia huku na kule, lakini hali iliendelea kuwa mbaya, tena mbaya zaidi....

Na ile mistari ikanyooka, kuashiria sasa hakuna matumaini tena.....


********


Wakati haya yakiendelea huku nje shangazi na mama walikuwa wakihaha huku na kule, walitamani kuingia kuona nini kinaendelea huko ndani lakini walishindwa, kwani walipojaribu mara ya kwanza walizuiwa na kuambiwa kwasasa hawaruhusiwi kuingia mapaka hapo watakaporuhusiwa, na wakati wanahangaika hivyo, walibahatika kuwaona watoto wao wakiwa ndani na shangazi alishikwa na butwaa kidogo, akasema;

‘Wewe umeona kule ndani, toka lini Maua akajua kazi ya udakitari, nimeona pale akisaidiana na docta kumshughulikia mgonjwa na cha ajabu Rose ndiye kaka pembeni akiwa kamshikilia mgonjwa mkono...’ akasema shanagzi.

‘Una uhakika na hilo, mimi hapa nawachanganya nashindwa hata kuwatofautisha, umejuaje kuwa ni Rose ndiye kaka na Maua ndiye anamshughulikia mgonjwa...?’ akauliza mama.

‘Wewe huoni walivyokuwa mwanzoni, kitambaa cha Rose kimefunika kichwa chote na Maua kajiachia na nywele zinaonekana...hajavaa kama Wahindi wenyewe...’akasema shangazi.

‘Mhh, mimi nahisi hawa watoto walituchezea,ina maana basi huyo tuliyekuwa naye muda wote toka nyumbani alikuwa ni Rose, ...kuna kitu kimefanyika hapa, nah ii ni hatari, inabidi tuwakanye, la sivyo tutkuja kujuta...’akasema mama.

‘Ndio maana tangu mwanzo nilikuwa na shaka, maana Maua namfahamu sana, lakini alipoondoka Rose, sijui ndio Maua, nilipokuwa nikiongea naye baada ya mwenzake kuondoka, niligundua utofauti katika majibu yake...nikahisi kitu, lakini nilidharau nakusema Maua hawezi kujiingiza kwenye hayo mambo , kwanza yeye ni mgeni kabisa katika miji mikubwa kama hii...’akasema shangazi.

‘Tuyaache hayo, sijui huko ndani mambo yanaendeleaje, maana kipndi kimepita, huenda alikuwa hajafa , sisi tulichukulia pupa...’akasema shangazi tena.

‘Hajafa, ile mashine haiongopi, ile mistari kwenye mashine inayoonyesha kwenye runinga, ikiwa ina miinuko miinuko inaonyesha mapigo ya moyo, lakini ikitulia na kunyooka moja kwa moja kama mstari, basi hakuna kitu...mgonjwa keshapoteza mapigo ya moyo na maana yake hana uhai, na unakumbuka yule docta alimwambia mwenzake aandike saa ya mwisho ya uhai wa mgonjwa...unakumbuka, halafu wakatuambia token haraka...’akasema mama.

‘Lakini hawakutuambia moja kwa moja kuwa ameshakata roho...mimi moyo wangu haujakubaliana na hilo, haiwezekani....’akasema shangazi huku akishika kichwa, na kusema; `Hali kama hii haijutakiwa kabisa iwakute wanetu, na hali zao hizi...’akasema shangazi.

‘Na kweli, lakini tutafanyeje...’akasema mama.

‘Hivi niambie unajua nini kuhusu uja uzito wa Rose, maana haijifichi, ni nani baba wa watoto wake, maana siku hizi ni kujizalia tu bila ndoa, umewahi kumuulizia?’ akauliza shangazi.

‘Nimuulizie wapi, kwani hajawahi kuniambia na hali hiyo nimeigundua huku kwa mara ya kwanza, nikuambie mimi na mwanangu tunaweza kukaa hata mwaka hatuonani, hasa nilipogundua yale yaliyokuwa yakitokea nyumbani, niliona njia bora ni kujenga umbali, kwasababu mimi nipo karibu na mume wangu, na kama ikuonana na motto, basii na mume wangu atakuwepo na matokeao yake ni ushirikina usio na maana...’akasema mama.

‘Kwanini mnayaamini sana hayo mambo, hawawezi kufanya kitu, labda mungu mweneywe apende, nina uhakika, ukiwa na moyo thabiti wa kutojali hayo mambo hakuna mtu atakaye kuweza....’akasema shangazi

‘Ni kweli kama hujawahi kukutana na mifano halisi,ukayaona mambo kiuwazi, huwezi amini, ...mpaka sasa najiuliza yule mzee aliyekuwa akikutana na mume wangu ni nani, kwani sikuwahi kumuona kitoka nje,au kukutana naye popote,ingawaje kuna wakati niliwaona wakiongea nje usiku, na wakihisi kuwa kuna mtu anawaangalia hutokea kitu, cha kunifanya nisiendelee kuwaangalia na nikiwaangaliana tena,huyo mzee keshaondoka....’akasema mama.

‘Kwahiyo unaamini kuwa ni mzimu,au ni shetani au ni mtu kweli....?’ akauliza shangazi.

‘Hapo siwezi kusema kuwa ni nani...’ akasema mama akionyesha uso wa kutafakari.

‘Tuachane na hayo,...ni mambo yako na mumeo na tamaa zako za pesa, kama ungeolewa na kaka yangu hayo yote hayangekuwepo, ....sasa nilikuuliza kuhusu Rose, je wewe unahisi mimba ya Rose ni ya nani,...’akauliza shangazi, nia ya mazungumzo hayo ni kupoteza muda, ili waondoe ile hofu iliyowatinga, na alipoona mwenzake anasita kujibu akaongeza kwa kusema, `U-si-iseme kaipatia huku shuleni...?’ akasema shangazi kwa uso wa kutahayari.

‘Mimi sijui, a simjui mwanangu tena, maana alibadilika ghafla hasa baada ya kuondoka hapo nyumbani , kuna kipindi aliniambia niachane na baba yake, nikamuuliza kwa kisa gani, akasema, hamuamini tena huyo baba, ana mambo asiyoyataka, sijui aliwahi kuyaona au vipi, na sikuwahi kumwambia lolote...nilijaribu kumdadisi bilamafanikio, lakini...niliona ni bota tujenge huo umbali kwa manufaa yake...’akasema mama akijaribu kukwepa swali aliloulizwa.

‘Sasa unahsi ujauzito huo ni wa nani, ina maana hakuna mtu ambaye unayemjua, ambaye alikuwa karibu na binti yako, maana sitegemei binti msomi kama yule, alijiachia tu , au ndio kaipata huko huko kwa wazungu, ...hapana shangazi yangu namuona alivyo...kajaa ujasiri na kujiamini, ni lazima ana mtu wake tena wa karibu anayejuana naye, ni lazima tumbane, na ina maana kweli wewe humjui huyo mtu, siamini, ..wewe ni mama gani usiyekuwa karibu na mwanao, hasa binti yako...’akasema na kugeukia mlangoni, pale walipomuona Docta akitoka, wakamsogelea na kumuuliza kujua kuna maendeelao gani.

‘Mhh, bado hatujawa na uhakika kamili, lakini kuna mafanikio kidogo yameonekana, tunajaribu kutizama sababu ya kupoteza fahamu kiasi kile hadi kufikia hatua iliyoonyesha kuwa kakata roho,na kuna jambp amablo tunalifanyiai uchunguzi, tutahitaji ushirikianao wenu baadaye, lakini kwa sasa mvute subira,...tutakuja na jibu muafaka baadaye kidogo...narudi huko kuona maendeleo...’akasema huyo docta na kuondoka.

‘Ana maana gani huyu , nahisi hajafa...’akasema shangazi.

‘Hawa ndivyo walivyo, kama mgonjwa haponi hawawezi kukuambia moja kwa moja, ila kama mgonjwa ni wa kupona wanakuambia moja kwa moja na hata kukupa matumaini, lakini inavyoonyesha hakuna cha matumaini wala nini sijui...sisi tuombe mungu tu, kwasababu niliyaona yale mashine kwa macho yangu mwenyewe, yakionyesha kuwa mgonjwa hana mapigo ya moyo...’akasema mama.

‘Useseme hivyo wifi....ooh, mungu wangu itakuwaje kwa hawa mabinti zetu, na wao wameamua kukaa humo humo ndani, sijuikwanini wamekubaliwa kubakia humo ndani, hivi hawa madakitari hawaoni ni hatari kwao...ooh, sijui tufanyeje, mimi hapa naona miguu yote imeisha nguvu,...’akasema shangazi.

‘Hawa mabinti zetu wapo kwa wataalamu hata likitokea , lakutokea watashughulikiwa haraka na hawo wataalamu wa hii hospitali, hilo lisikutie mashaka, ...mmh,...’akasema na kutulia,

Alimwangalia wifi yake kwa muda na baadaye akaongea peke yake kwa kunong’ona na kusema `Sijui kuhusu huyo mgonjwa, ina maana ndio keshatuaga hivyo, haraka kiasi hiki, hizo gharama tulizojitolea ndio zimepotea hivyo, mmh jamani, kweli maisha hayana thamani, mungu wangu na hawa watoto watawezaje kuvumilia hilo pigo, ooh, mungu wangu wajalie ujasiri wa kuvumilia, mmh, sijui tumuachie mungu...’

Licha ya kuwa mama alijifanya hajali, lakini moyoni kulikuwa hakukaliki, na baadaye liposhindwa kujizuia akasimama na kuangalia juu, na mara akakaa tena, na baadaye akasimama, na hilo miahangaiko ikamafanya shangazi amwangalie kwa mashaka na kabla shangazi hajasema kitu ...simu ya mama ikaita, mama alikuwa kama haisikii, ikaendeela kuita kwa muda , na shangazi akamuuliza kwanini hapokei hiyo simu.

‘Nishajua ni nani ananipigia,....’akasema huku akitamani kuizima ile simu, na vidole vilikuwa vikicheza cheza kwenye ile simu, huku akishindwa kuamua kwa haraka, kuwa aizime au aipokee, baadaye akasema; ’Huyu najua atazidi kunichanganya tu, ....’akaiinua ile simu na kutizama namba na alipogundua ndiyo huyo huyo aliyekuwa akimzania, akaipokea haraka haraka na kusema;

‘Sema mpenzi, kuna habari gani huko...?’ akauliza huku akijitahidi kuficha hisia zake zisitambuliwe kwenye simu.

‘Unasema nini, eti unasafari ya kurudi Uganda, kesho, kuna nini cha haraka hivyo, wakati tulishapanga hadi mwezi ujao..?’ akauliza mama kwa sauti ya kushangaa.

‘Biashara ipi hiyo, kuna biashara nyingine ambayo unaiendesha wewe na mimi siijui,niambie ukweli ,kuna nini kunakusukuma kwenda huko kwa haraka hivyo...?’ akauliza mama kwa hasira.

‘Mgonjwa hatujajua majaliwa yake bado, ...nani kakwambia kuwa haponi,...?’ akauliza kwa hamaki na kujiegemeza ukutani, huku anasikiliza nini mumewe anachoongea.

‘Yaani wewe unafuatilia kwa `remote control’ tu,....au sio,...?’akauliza mama, na akawa anaongea na wakati huo huo mumewe anaongea kitu kwenye simu, kwahiyo wakawa wanaongea kwa pamoja; na alipoona mumewe kanyamaza kumsikiliza akasema `Na atapona tu, mungu ni mkubwa, kama nyie mnasema hatapona nyie na mambi yenu,...kwani sijui nyie mumejiona ni Mungu au nani, lakini mtashangaa akipona...’akasema mama kwa kujipa moyo.

‘Sijasema hivyo kuwa unmuombea vibaya au kuhusika na lolote lile, usijahami kihivyo...’akasemakwa hamaki na kutulia kidogo na alipoona mumewe kanyamaza pia akaongezea kusema ‘Mimi ninachoshangaa ni wewe kusema kuwa haponi, wakati upo huko hujamuona huyo mgonjwa yupoje, hata kama unawasiliana na hawo madakitari, lakini sio cha kukatisha tamaaa kihivyo, sawa,...wewe ndenda safari yako, na nahitaji maelezo ya hiyo biashara, ukumbuke tuwashirika...sawa, nakutakia safari njema, mimi bado nahangaika na mgonjwa, safari njema...ahsante na matumaini yako mema ya kinafiki, kwaheri...’akasema mama na kukata simu kwa hasira.

‘Vipi mbona unamjibu mumeo kwa hasira hivyo...?’ akauliza shangazi huku kionyesha uso wa mshangao.

‘We acha tu, huyu tunajuana wenyewe, ukiona tunaongea hivi unaweza ukatufikiria vibaya, lakini muda mchache utashangaa utatukuta tunaongea lugha ya mahaba ya mke na mumewe, ndivyo tulivyo, ila ninachoshangaa ni hii safari ya harakaharaka ...ninashindwa kuelewa....’akasimama na kutemba huku kainama chini akiwaza.

‘Au yanahusiana na yale maeelzo uliyonieleza, kuwa ulimkuta akiongea na ndugu yake ambaye hujamgundua ni nani, huenda kuna jambo limetokea, lakini hayo hayatuhusu kwa sasa, usijiingize kwenye mawazo mengie makubwa , wakati hapa una mzigi usiobebeka wa mawazo...’akasema shangazi.

‘Nina mashaka makubwa, kuna uhusiano wa haya matukio, ...kumbuka binti yetu aliitwa, na hatujajua ni nani alimuita, kumbuka yale maelezo niliyokuambai kuwa nilimfuma mume wangu akiongea na simu na mtu, huyo anayemuita ndugu yake, kumbuka, huyo mtu aliaambiwa aafnye kila njia ili amuoe binti yetu...na kikwazo na huyu mgonjwa, huoni kuna kitu, je huyu mgonjwa kwanini afikie hatua ya kutaka kufa....ghafla ...’akakatisha ghfla, kwani walimuona docta akija kwa haraka, na mwendo wake uliwatia mashaka, ni kama mtu mwenye jambo nzito la kuwaambia,

Mama na shangazi wakawa wanasita kumsogelea,...ilikuwa kama vile wanataka kumkimbia docta kwa kuogopa taarifa mbaya, lakini kwa upande mwingine walikuwa wakihitaji kujua nini kimetokea huko ndani. Wakabakia pale pale wakiwa wamesimama kama wameshikwa na ganzi ya kiwliwili huku macho yao yakiwa yamewatoka kwa woga....yule docta akawasogelea kwa mwendo ule wa harakaharaka, na kuwakabili wale mama wawili na kabla hajasema kitu mara mlango wa ile wodi maalumu ukafunguliwa na Rose akatokea akiwakimbilia....na wote wakageuka kumwangalia.....

NB: Msishangae mkaona kama bado tunazunguka zunguka kwenye sehemu hii,, kuna mambo muhimu sana ambayo yalihitajika kuwekwa wazi ,... kwa wanaofuatilia kisa hiki kwa makini watayagundua hayo, na matokeo yake yataweza kutufikisha pale tulipopatarajia.

Neno muhimu la leo; Wakati wa matatizo, subira ni kitu muhimu sana, kwani mungu yupo na wenye kusubiri, hasa pale wanapokutwa na mitihani ya kimisha, tusikate tamaa...weka subira huku ukitenda haki,.
TUPO PAMOJA .




Ni mimi: emu-three

4 comments :

Yasinta Ngonyani said...

Aiseee! hapa patamu muno...inasisimua, inasikitisha na pia naweza kusema inaogopesha lakini utamu upo. Nina hamu kweli kujua itakuwaje....je huyo mgonjwa atapona kweli?

Anonymous said...

M3 mimi ni mfuatiliaji wa kisa hiki tokea mwanzo na tuko pamoja ila "neno muhimu la leo" limenigusa sana! Eh Mola naomba unijalie moyo wa subira mja wako niko kwenye mapito magumu mno.

Anonymous said...

neno la leo limenigusa sana.thanx emu3

emuthree said...

Tupo pamoja ndugu zanguni msinione kimiya, nahaha huku na kule ili niweke sehemu inayufuata, maana ukipata sehemu mara kuna vizuizi, ukiazima jembe, ukifika home, hakuna umeme, yaani mitihani moja kwa moja, lakini ujumbe wetu unatufundisha tuwe na subira....TUPO PAMOJA